Tuesday 31 December 2019

Rais Uhuru Kenyatta asema wakili Miguna yuko huru kurejea Kenya

Rais Uhuru Kenyatta amesema wakili aliyetimuliwa  nchini Kenya  Miguna Miguna yuko huru kurejea Kenya kwani ni haki yake Kikatiba.

Kiongozi  huyo wa taifa alisema Miguna ataruhusiwa kurejea nchini lakini atumie uhuru wake wa kujieleza kueneza amani na umoja miongoni mwa Wakenya.

Akizungumza katika hafla ya mazishi ya mwanasiasa mkongwe Charles Rubia katika Kaunti ya Murang’a mnamo Jumatatu, Desemba 30, Uhuru alisema serikali yake itatoa uhuru kwa Wakenya wote kama ilivyopiganiwa na viongozi waliotangulia.

“Hakuna mtu ambaye amezuiwa kusema yale anayotaka kusema. Ata nasikia kuna wengine wanataka kupanda ndege warudi..waendelee..hio ni uhuru wao," alisema kiongozi huyo wa chama cha Jubilee.

Wakili Miguna anatazamiwa kuingia nchini Jumanne 7, Januari 2020.

Wakili huyo alitangaza kuwa atarejea nyumbani kupitia ukurasa zake za utandawazi siku ya Alhamisi, Desemba 19.

“Narejea nyumbani. Haki ya kuzaliwa, Haki ya Katiba na amri ya korti. Mabadiliko kwa ushawishi. Nitawasili: Jumanne, Januari 7, 2020 mwendo wa saa tatu na dakika 25 usiku kupitia ndege ya Lufthansa LH 590,” aliandika Miguna kwenye Twitter.

Wakili huyo alitimuliwa Kenya  kwa mara ya kwanza Februari 2018 baada ya kumuapisha kiongozi wa ODM Raila Odinga kama rais wa watu mnamo Jumanne, Januari 30 katika bustani ya Uhuru.

Mnamo Machi 2018, juhudi zake za kuingia nchini ziliambulia patupu huku serikali ikisema kwamba aliasi uraia wake wa Kenya ili kuwa raia wa Canada.


Share:

Urusi na Ukraine zafikia makubaliano ya kupitisha gesi kuelekea Ulaya Magharibi

Urusi na Ukraine zimesaini makubaliano ya upitishaji wa gesi ambayo yanaweza kuathiri eneo kubwa la Ulaya Magharibi. 

Kampuni ya gesi inayomilikiwa na serikali ya Urusi, Gazprom, na ile ya nishati ya Ukraine, Naftogaz, zilifikia makubaliano jioni ya jana, baada ya wapatanishi kutumia siku kadhaa kupitia vipengele vya makubaliano hayo, kwa mujibu wa Rais Volo-dy-myr Zelensky wa Ukraine.

 Mkuu wa kampuni ya Gazprom ya Urusi, Alexej Miller, pia amethibitisha kufikiwa makubaliano hayo, kwa mujibu wa shirika la habari la Urusi. 

Mkataba wa awali baina ya pande hizo mbili ulikuwa unamaliza muda wake leo baada ya kutumika kwa miaka kumi, ambapo mkataba huu mpya ni wa miaka mitano. 

Mataifa mengi ya Muungano wa Ulaya yanalitegemea bomba la gesi la Urusi linalopitia Ukraine. 

Hata hivyo, kwa miaka kadhaa mzozo baina ya nchi hizo mbili umekuwa ukiathiri makubaliano hayo ambayo yanaipatia Ukraine mabilioni ya euro.


Share:

Katibu Mkuu CCM Awataka Vijana Kuwa Wabunifu

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally amewaleza vijana umuhimu wa kuwa na maarifa kwani ukiwa na shahada pekee sio pesa, ila maarifa yako ndio hutengeneza pesa, hivyo vijana ni lazima wawe wabunifu, bila kuchapa kazi maisha yataendelea kubana.

Dkt. Bashiru amesema, yeye ni Katibu Mkuu wa CCM kwa sasa, lakini hakuna magulio asiyoyafahamu wilayani Bukoba, kwa kuwa alipokuwa anasoma na baada ya kuhitimu masomo yake, kazi kubwa aliyokuwa akiifanya bila uwoga ni uchuuzi kwenye magulio kazi ambazo vijana wengi wakiwa na shahada kichwani hawawezi kuzifanya.

Dkt. Bashiru ameyasema hayo, Desemba 29, 2019 alipokuwa akitoa salamu za Chama wilayani Muleba kata ya Mayondwe katika shughuli ya dua iliyojumuisha maombi mbalimbali pamoja na kuiombea amani nchi yetu.

“Vijana bila kuchapa kazi maisha yatabana, na vyuma vitabana kwelikweli, mimi ni Katibu Mkuu kwa sasa hakuna magulio nisiyoyafahamu hapa Bukoba na Muleba kwa kiasi, wakati nasoma na baada ya kuhitimu masomo kazi kubwa niliyoifanya kwa muda mrefu ni uchuuzi kwenye magulio kazi ambayo vijana wengi wakiwa na shahada kichwani hawapendi kuzifanya.’’ Bashiru ameeleza

Ameongeza kuwa, ukiwa na elimu ya shahada kichwani hiyo sio pesa, ila maarifa yako ndio yatatengeneza pesa akimtolea mfano Bw. Jafari Swalehe waliosoma naye darasa moja shule ya msingi Katerero na kuishia darasa la saba mkazi wa Bukoba vijijini ambaye kwa sasa ni mkulima mkubwa wa mbogamboga na matunda wilayani hapo.

Wakati huo huo, Dkt. Bashiru ameeleza wazi kuwa, CCM inajukumu la kutunga Sera wezeshi ili kundi kubwa la vijana waweze kupata mazingira mazuri ya fursa mbalimbali zikiwemo biashara, kilimo na viwanda, ambalo wameendelea kulifanya na katika Sera na Ilani ijayo suala hili litapewa uzito wa pekee ili kuwezesha kundi kubwa la vijana kupata na kumudu fursa za kimaendeleo.

Aidha, Dkt. Bashiru katika salamu hizo amehimiza upendo miongoni mwa wanafamilia na jamii kwa ujumla, ambapo ameeleza kuwa, maisha yetu ya upendo na undugu hutegemea maisha yetu ya kila siku, maisha ya upendo hutengenezwa katika ndoa, shule, siasa, biashara na maeneo mengine. Unayempenda huwezi kumfitini na utapenda afanikiwe, na vitabu vya dini zote vinahimiza upendo, hata CCM inahimiza upendo, kukemea chuki na fitina.

Awali kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu, Shekhe Nuran Amri, akitoa neno la ukaribisho, amesisitiza kuwa, utofauti mkubwa wa binadamu na wanyama ni akili, binadamu tumepewa uwezo wa kutambua kibaya na kizuri, amani na fujo, chuki na upendo, hivyo hatuna budi kuitunza amani yetu, na kuwaombea viongozi wetu wakiongozwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli ili wazidi na waendelee kuwa na upendo na uwajibikaji wa haki kama ilivyo sasa.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na waumini wa dini zote viongozi mbalimbali wakiongozwa na Kaimu Shekhe wa Wilaya ya Muleba Bw. Hashim Haruna na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Ndg. Athuman Kahara.

Katibu Mkuu yupo Bukoba Mkoani Kagera kwa mapumziko ya siku kumi ambapo anatarajiwa kumaliza mapumziko hayo mwanzoni mwa mwezi Januari, 2020.


Share:

Mama Mzazi wa Erick Kabendera Afariki Dunia

Mama mzazi wa Mwandishi Erick Kabendera, Verdiana Mjwahuzi amefariki Dunia leo Jumanne Dec 31, 2019 katika Hospitali ya Amana Da es Salaam  alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Bi. Verdiana alionekana hadharani mara ya mwisho  Disemba 13 Mwaka huu akiomba mwanae aachiwe huru kwakuwa anamtegemea kwa matibabu.

Erick ambaye kwa sasa yuko rumande katika gereza la Segerea, Dar es Salaam, alikamatwa Julai 2019 kwa makosa ya utakatishaji fedha, kukwepa kodi na kushiriki katika genge la uhalifu.


Share:

Mwalimu Mbaroni Kwa Tuhuma za Kulawiti Watoto Wadogo

Mkuu wa Wilaya wa Iringa Mjini, Richard Kasesela amesema polisi wilayani humo inamshikilia mkazi wa Semtema, Anord Mlay ambaye ni mwalimu kwa tuhuma za kulawiti watoto wadogo 24

Imeelezwa kuwa wengi wa watoto hao ni wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika eneo hilo.

Taarifa zinaeleza kuwa watoto hao wanadaiwa kulawitiwa katika kipindi cha miaka mitatu na na mtuhumiwa huyo.

Akizungumza na wananchi wa mtaa huo, Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alieleza akushtushwa na ukubwa tatizo hilo na kuamua kuchukua hatua ikiwamo kuunda kamati ya watu 10 kwa ajili ya kufuatilia na kubaini watoto ambao wamefanyiwa ukatili huo.

Kasesela alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa na michezo ya kompyuta, na kwamba alikuwa akiwarubuni watoto kwa zawadi ndogo ndogo zikiwamo fedha.

Kasesela alifafanua zaidi kuwa Mlay pia alikuwa akiwatishia watoto kuwatoa uhai ikiwa wangeruhusu mtu mwingine kujua suala hilo.

Alisema alieleza kuwa uchunguzi dhidi ya mtuhuhiwa huyo ukikamilika, atapelekwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Kasesela, Mlay ni mwalimu ambaye alihitumu katika Chuo Kikuu cha Iringa, na anamiliki kituo chake cha kuchezesha michezo ya kompyuta kwa watoto wadogo katika mtaa wa Semtema ‘A’.

Kasesela  pia aliwataka wazazi na walezi katika Manispaa ya Iringa kuwa makini na watoto wao wanaocheza michezo katika vituo vya watoto maarufu pamoja na kuwataka kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kuwafichua wanaojihusisha na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne Disemba 31























Share:

Monday 30 December 2019

Fursa Ya Ufadhili Kwa Watanzania : | Scholarships Tenable In The People’s Republic Of China For The Academic Year 2020/2021

    1.0Call for Application

The General Public is hereby informed that the Chinese Government is offering undergraduate and postgraduate fully-funded scholarships for Tanzanian citizens in various domains for the academic year 2020/2021.

    1.1Eligibility

Applicants should meet the following requirements:
  1.     Be a citizen of the United Republic of Tanzania;
  2.     Must have completed high school (‘A’ level) and below 25 years if applying for a Bachelor degree program;
  3.     Must have a Bachelor’s degree and below 35 years if applying for a Master’s degree program;
  4.     Must have a Master’s degree and under the age of 40 if applying for a Doctoral degree program; and
  5.     Must be in good health.
    2.0Application Documents
  1.         A completed application form of the Chinese Government Scholarship filled either in Chinese or English;
  2.         Certified copies of Certificate for Secondary Education Examination (CSEE), Advance Certificate for Secondary Education Examination (ACSEE), Diploma, Bachelor or Master’s degree. Documents in languages other than Chinese or English must have attachments of certified Chinese or English translations;
  3.         Academic transcripts in languages other than Chinese or English must have attachments of certified Chinese or English translations;
  4.         A study plan or research proposal in Chinese or English with a minimum of 200 words for undergraduate applicants and 800 words for postgraduate applicants;
  5. Two recommendation letters for applicants applying for postgraduate programs written in either Chinese or English from professors or associate professors;
  6.  Certified copies of birth certificates.
  7.  Applicants under the age of 18 should submit the valid documents of their legal guardians in China; and
  8.  Applicants planning to stay in China for more than 6 months must submit a photocopy of the Foreign Physical Examination form completed in English (the original copy should be kept by the applicant). This form can be downloaded from:
The physical examination must cover all the items listed in the Foreign Physical Examination Form. Incomplete records without the Physicians signature, official stamp of the hospital or passport size photograph of the applicant are invalid. Please select the appropriate time to take a physical examination as the results are only valid for only 6 months.

    3.0Documents required for submission

<<INGIA HAPA KUZIPAKUA>>

Issued by:
Permanent Secretary,
Ministry of Education, Science and Technology,


Share:

Rwanda Education Board-REB Results 2019-2020

REB TVET National Examinations Results 2019/20, Rwanda Education Board REB Results 2019: www.reb.rw result 2019 by National Examinations Results – The Rwanda National Examinations Council (RNEC) is responsible for the overall administration, regulation, and supervision of national examinations and accreditation in primary and secondary school in Rwanda. Kureba Amanota y’Ikizami cya Leta yasohowe na Rwanda Education Board (REB)… Read More »

The post Rwanda Education Board-REB Results 2019-2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Latoa Ufafanuzi Kukamatwa kwa Dereva wa Katibu Mkuu CHADEMA Na Afisa Habari

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP.Muliro Jumanne amekanusha taarifa zilizokuwa zinasambaa katika mitandao ya kijamii zikieleza kuwa kuna wanachama wa chadema wametekwa jijini hapa.

Muliro amesema hakuna utekaji uliotokea bali wanachama hao walikamatwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.

Akizungumza na Waandishi wa Habari,  ACP Muliro Muliro amesema siku ya Desemba 29, Mwaka huu Majira ya 15:00 Mtaa wa Mahina Kata ya Mahina wilayani Nyamagana kulipatikana taarifa toka kwa raia wema kuwa kumeonekana watu wawili waliohisiwa kuwa siyo watu wema wakiwa karibu na Hoteli ya Paradise na kuingia nyumba jirani iliyokuwa karibu na hoteli hiyo.

Kamanda Muliro, amesema baada ya kupatikana taarifa hizo jeshi la polisi  lilifanya ufuatiliaji wa haraka na kufika eneo hilo na kuwakamata watu hao wawili, ambao katika mahojiano ya awali walikataa kutoa utambulisho wao kuwa wamefika maeneo hayo kufanya shughuli gani.

"Walichukuliwa na kupelekwa kituo cha polisi kati na kutoa ushirikiano kwa askari pia kutaja majina yao kuwa ni Abdukarimu Muro (31), mchaga Afisa Habari Katibu Mkuu CHADEMA Mkazi wa Kinondoni B, Dar es Salaam na Said Haidani (30), Dereva wa Katibu Mkuu CHADEMA, Mkazi wa Mbezi Kimara Dar es Salaam wameambatana na Katibu Mkuu CHADEMA, Mh. John Mnyika na polisi waliwaachia baada ya kujiridhisha hawakuwa wahalifu waliachiwa huru," amesema ACP Muliro.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limetoa onyo kwa kwa watu wasiokuwa na taarifa rasmi na wenye tabia za kuzusha mambo hasa ya watu wanapokamatwa wao husema kuwa wametekwa na hivyo kuzusha taharuki kwa jamii kwani matendo hayo ni makosa na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao watakapobainika.


Share:

Iran yalaani mashambulizi ya Marekani Iraq na Syria

Iran imelaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani nchini Iraq na Syria dhidi ya wanamgambo wa Kataib Hezbollah wanaoungwa mkono na Iran.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq, Abbas Mousavi amesema wanalaani vikali uchokozi wa Marekani katika ardhi ya Iraq na vikosi vya Iraq na wanauona kama mfano wa wazi wa ugaidi. 

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper alisema jana vikosi vyake vilifanya mashambulizi yaliyowalenga wanamgambo wa Iraq wanaoungwa mkono na Iran, wakiwalaumu kwa shambulizi la roketi lililomuua mkandarasi wa Kimarekeni. 

Esper amesema Marekani imeyashambulia maeneo  matatu ya magharibi mwa Iraq na mawili mashariki mwa Syria, ikiwemo maghala ya silaha na kambi zinazodhibitiwa na wanamgambo. 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo amesema mashambulizi hayo ni ujumbe kwamba Marekani haitovumilia vitendo vyovyote vya Iran ambavyo vinahatarisha maisha ya Wamarekani.


Share:

MOE-SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE PEOPLE’S REPUBLIC OF CHINA FOR THE ACADEMIC YEAR 2020/2021

MOE-SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE PEOPLE’S REPUBLIC OF CHINA FOR THE ACADEMIC YEAR 2020/2021 1.0Call for Application The General Public is hereby informed that the Chinese Government is offering undergraduate and postgraduate fully-funded scholarships for Tanzanian citizens in various domains for the academic year 2020/2021. 1.1Eligibility Applicants should meet the following requirements: Be a citizen of the United Republic… Read More »

The post MOE-SCHOLARSHIPS TENABLE IN THE PEOPLE’S REPUBLIC OF CHINA FOR THE ACADEMIC YEAR 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Korea Kaskazini yaitaka Marekani kubadili mwelekeo wa mazungumzo ya nyuklia

Wakati muda wa mwisho wa mazungumzo na Marekani juu ya mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini ukiwadia, kiongozi wa taifa hilo, Kim Jong Un, ameitisha mkutano wa dharura wa maafisa wakuu wa kijeshi na kidiplomasia.

Kwenye taarifa yake ya leo, shirika rasmi la habari la Korea Kaskazini (KCNA) limesema kiongozi huyo alizungumza kwenye mkutano maalum wa Chama cha Wafanyakazi wa Korea, akielezea matatizo yanayoikumba sekta ya viwanda na wakati huo huo akiwapangia majukumu wasaidizi wake kurekebisha matatizo hayo.

Kim alitaka pawepo na matayarisho ya haraka ya kisera juu ya masuala ya kiusalama, silaha na kile alichosema kuwa ni ulinzi wa uhuru wa Korea Kaskazini.

Kauli hizi zimetafsiriwa na mahasimu wake wa Korea Kusini na Marekani kwamba ni dalili zisizo njema kuelekea muda wa mwisho aliokuwa ameuweka wa tarehe 31 Disemba 2019, ambapo alitaka utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani uwe umeshalainisha msimamo wake kwenye mazungumzo ya mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Kuna wasiwasi kwamba huenda kwenye hotuba yake ya mkesha wa mwaka mpya, Kim akaamuru kusitishwa kwa mazungumzo hayo na badala yake kurejea kwenye majaribio ya makombora ya masafa marefu, ambayo aliyasitisha tangu mwaka 2017.

Korea Kaskazini inaitaka Marekani kuacha kuiwekea vikwazo mara moja, ikiwa inataka kuyaokowa mazugumzo  hayo.


Credit:DW


Share:

QA Software Engineer at NALA

What is NALA? NALA is building the future of digital payments and banking in Africa. Customers use our app to pay 7x faster all without using the internet and across multiple accounts. We’re a small team based in Tanzania with a few people working in remote cities across the globe. We recently completed Y-Combinator.  Find us on TechCrunch,… Read More »

The post QA Software Engineer at NALA appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jobs at World Vision Tanzania-December 2019

Driver -Itilima & Karatu at World Vision Tanzania Purpose of the position: To drive WVT vehicles so as to facilitate staff/visitor movements as assigned by Senior Transport Officer and keep the vehicle clean and in good working condition Communicate World Vision’s Christian ethos and demonstrate a quality of spiritual life that is an example to others. To keep… Read More »

The post Jobs at World Vision Tanzania-December 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Hotel Operation & Quality Assurance Manager Job Opportunity at Hatari Lodge

Hotel Operation & Quality Assurance Manager The African Embassy, Hatari LodgeArusha, Tanzania Hotel Operations Manager (f/m/x) to lead the Hatari Operation in Tanzania Currently consists of a luxurious lodge and a tented camp operation. The position is ideally suited for individual applicants although couples will also be considered. The ideal candidates will have a strong knowledge of international… Read More »

The post Hotel Operation & Quality Assurance Manager Job Opportunity at Hatari Lodge appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Local Content Specialist Job Opportunity at African Underground Mining Services

Local Content Specialist Job Opportunity at African Underground Mining Services, Deadline 6 January 2020

The post Local Content Specialist Job Opportunity at African Underground Mining Services appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Assistant Manager – Concurrent Audit Job Opportunity

Job title: Assistant Manager – Concurrent Audit Job type: Permanent Emp type: Full-time Job ID: 32213 Job Description Responsibilities • Ensuring compliance with laid down systems, procedures and policies and highlighting any unacceptable exceptions and ensuring completeness of collection. • Providing value adding recommendations to key processes which enhance efficiency. • Represent Internal Audit in projects intended to… Read More »

The post Assistant Manager – Concurrent Audit Job Opportunity appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger