Monday 9 December 2019

LIVE: Sherehe Za Miaka 58 Ya Uhuru Wa Tanzania Bara CCM - Kirumba Jijini Mwanza

Live: Maadhimisho Ya Miaka 58 Ya Uhuru Mwanza


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu December 9






















Share:

Sunday 8 December 2019

Bilionea Ali Mufuruki Afariki Dunia

Mwenyekiti na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Infotech Investment Group ambaye aliwahi pia kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, Ali Mufuruki (60), amefariki  Dunia usiku wa kuamkia leo Disemba 8, 2019  akiwa Afrika Kusini akipatiwa matibabu.

Mufuruki ni kati ya matajiri wakubwa 10 wa Tanzania akiwa ni mmiliki wa Kampuni ya Infotech Investment Group Limited na maduka ya Wolworth.

Oktoba 18, 2019 Mufuruki alijiuzulu nafasi yake ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Vodacom Tanzania ili kupata muda zaidi wa kuendelea na biashara zake.

Mwenyekiti wa sasa wa Ceort, Sanjay Rughan amethibitisha kutokea kwa kifo hicho kilichotokea saa tisa alfajiri katika Hospitali ya Morningside.



Share:

Job Opportunities at Tazama Pipelines Limited

Overview: Tazama Pipelines Limited, an interstate organization owned by the United Republic of Tanzania and the Republic of Zambia and which deals in transportation of crude oil from Dar es Salaam to Ndola, Zambia, wishes to invite applications from suitably qualified candidates to fill the under-mentioned posts below: Vacancy title: Cook  MAIN DUTIES: Undertakes timely the provision of meals… Read More »

The post Job Opportunities at Tazama Pipelines Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Executive Editor Job Opportunity at BBC Media Action

Executive Editor Job Opportunity at BBC Media Action Job Title: Executive Editor Location: Dar es Salaam, Tanzania Special Requirements: Right to work in Tanzania Reports to: Country Director, Tanzania Contract:  Full-time, 24 months with possible extension Salary: Highly competitive within Tanzania, NGO market rates Please do not send certificates or other attachments. Applicants with no separate cover letter will not… Read More »

The post Executive Editor Job Opportunity at BBC Media Action appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Policy Adviser Job Opportunity at BBC Media Action

Job Opportunity at BBC Media Action, Senior Policy Adviser – Gender Equality & Social Inclusion (GESI) Job Title:  Senior Policy Adviser – Gender Equality & Social Inclusion (GESI) Location: Dar es Salaam, Tanzania Special Requirements: Right to work in Tanzania Reports to: Country Director, Tanzania Contract:  Full-time, 24 moinths with possible extension Salary: Highly competitive within Tanzania, NGO market rates Please do not send… Read More »

The post Senior Policy Adviser Job Opportunity at BBC Media Action appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Officer Gender Job Opportunity at BBC Media Action

Project Officer Gender Job Opportunity at BBC Media Action Job Title: Project Officer- Gender Location: Dar es Salaam, Tanzania Special Requirements: Right to work in Tanzania Reports to: Project Manager, Tanzania Contract:  Full-time, 24 months with possible extension Salary: Highly competitive within Tanzania, NGO market rates Please do not send certificates or other attachments. Applicants with no separate cover letter will… Read More »

The post Project Officer Gender Job Opportunity at BBC Media Action appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

48 Data Clerks  Positions  at The USAID Boresha Afya Southern Zone

Data Clerks 48 Positions   VACANCY ANNOUNCEMENT The USAID Boresha Afya Southern Zone is a five-year (1 October 2016 – 30 September 2021) PEPFAR supported program through USAID. Deloitte Consulting Limited implements the program in 42 councils in Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara and Ruvuma with its technical partners Family Health International (FHI360), Engender Health and Management and Development for… Read More »

The post 48 Data Clerks  Positions  at The USAID Boresha Afya Southern Zone appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

9 District Data Officers Job Opportunities at USAID Boresha Afya

District Data Officer 9 Positions VACANCY ANNOUNCEMENT The USAID Boresha Afya Southern Zone is a five-year (1 October 2016 – 30 September 2021) PEPFAR supported program through USAID. Deloitte Consulting Limited implements the program in 42 councils in Iringa, Njombe, Morogoro, Lindi, Mtwara and Ruvuma with its technical partners Family Health International (FHI360), Engender Health and Management and Development… Read More »

The post 9 District Data Officers Job Opportunities at USAID Boresha Afya appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Program Officer, Clinical Services (3 posts) at The Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI)

Program Officer, Clinical Services (3 posts) The Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) is a non-governmental organisation that plays a pivotal role in complementing the Government of Tanzania’s efforts towards the attainment of its development goals. AGPAHI strives to provide quality and integrated HIV/AIDS health services to children and families. AGPAHI supports the provision of high-quality HIV and… Read More »

The post Program Officer, Clinical Services (3 posts) at The Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Program Officer- Pediatrics HIV and AIDS Job Opportunities at AGPAHI

 Program Officer, Pediatrics HIV and AIDS (2) The Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) is a non-governmental organisation that plays a pivotal role in complementing the Government of Tanzania’s efforts towards the attainment of its development goals. AGPAHI strives to provide quality and integrated HIV/AIDS health services to children and families. AGPAHI supports the provision of high-quality HIV… Read More »

The post Program Officer- Pediatrics HIV and AIDS Job Opportunities at AGPAHI appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UDOM: Tentative approval list for the students who requested to be transferred 2019/2020.

UDOM: ANNOUNCEMENT TO STUDENTS WHO APPLIED FOR TRANSFERS (INTER-AND INTERNAL UNIVERSITY TRANSFERS) FOR THE 2019/2020 ACADEMIC YEAR The University of Dodoma (UDOM) would like to inform students who applied for transfers that their tentative approval within the University has been already established pending to the final approval. The following is the tentative approval list for the students who… Read More »

The post UDOM: Tentative approval list for the students who requested to be transferred 2019/2020. appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Jingu Aipeleka Kampeni Ya Makazi Bora Monduli

Na Mwandishi Wetu Arusha
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu amewataka wananchi kuhakikisha wanaboresha makazi yao kutoka makazi ya nyumba za nyasi na tembe kwenda nyumba za tofali na bati.

Aliyasema hayo leo Wilayani Monduli mkoani Arusha alipokuwa akitembelea miradi mbalimbali ya maendeleo iliyoamasishwa na wataalam kutoka Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli kwa kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika miradi ya Maendeleo.

Dkt. Jingu aliwataka wataalam wa Maendeleo ya Jamii nchini kuhakikisha wanakuwa chachu ya mabadiliko na wanawezesha jamii kuwa na mawazo chanya ya kujiletea maendeleo na kubadili changamoto kuwa fursa za kimaendeleo.

"Wataalam wa Maendeleo ya Jamii tuweke nguvu katika kuhakikisha tunabadili jamii zetu kuwa na mawazo chanja hasa ya kujitegemea na kujiletea maendeleo" alisema Dkt. Jingu.

Dkt. Jingu aliongeza kuwa Sekta ya Maendeleo ya Jamii inapaswa kuwa chachu ya maendeleo katika taifa letu hivyo Vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinatakiwa kutoa wataalam wenye weledi na stadi za kubwa za kuleta mabadiliko katika jamii.

"Vyuo vya Maendeleo ya Jamii tutoe wataalam wenye weledi  wa kuhakikisha tunatumia fursa zilizopo katika jamii kutatua changamoto zilizopo" alisema Dkt. Jingu.

Wakati huohuo akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli Dkt. Jingu amewataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kuhakikisha wanatumia stadi watakazopata kubadilisha maisha yao na jamii kwa ujumla.

Dkt. Jingu aliwataka wanafunzi hao kuitumia bahati ya kuwa mmoja ya wanafunzi katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli kwa kuhakikisha wanafanikisha ndoto zao walizozilenga kuzitimiza katika maisha yao kwa kuzingatia masomo na nidhamu.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Monduli Bw. Elibariki Ulomi alimuhakikishia Katibu Mkuu kuwa Chuo hiyo kitahakikisha kinashirikiana na wananchi wa Wilaya ya Monduli katika kutekeleza Kampeni ya Makazi Bora ili kuwawezesha wananchi kuboresha makazi yao na kuhakikisha kinatoa Wataalam wa Maendeelo ya Jamii watakosaidia kuleta mabadiliko katika taifa.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Monduli Bi. Rose Mhina alisema kuwa Halmashauri hiyo imeshaanza kutekeleza kampeni ya Makazi bora kwa kuipeleke ajenda hiyo kwa madiwani na kutoa michoro maalum kwaajili ya ujenzi wa nyumba bora za gharama nafuu.

Aliongeza kuwa Kampeni hiyo ya kuhamaisha ujenzi wamakazi bora itahamasishwa na katika jamii na maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka wilayani maoaka kwemye kata ili kuhakikisha wananchi wanajitoa na kuboresha makazi yao.

Kampeni ya Kuboresha makazi inalenga kuiwezesha jamii ambayo inaishi katika makazi yasiyo bora kuweza kuboresha makazi yao kwa kutumia ramani ziliziotolewa na Halmashauri walizopo zikiwa ni nyumba za gharama nafuu.

MWISHO.


Share:

TRA Yang’ara Tuzo Za NBAA , Yapata Ushindi Wa Jumla

Na Veronica Kazimoto-Dar es Salaam
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeshinda tuzo mbili ikiwemo mshindi wa jumla katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu mwaka 2018 kwa kufuata viwango vya Kimataifa vya Uandaaji wa Hesabu katika Taasisi za Umma yaani mfumo wa IPSASs.

Katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA Bunju jijini Dar es Salaam, TRA imeibuka mshindi wa kwanza katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu kwenye kipengele cha Wakala wa Serikali na mshindi wa jumla kwa taasisi, wakala, kampuni na mashirika mbalimbali ambayo yamefanya vizuri katika kuandaa taarifa za fedha katika shughuli zao za kila siku.

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hizo, Kamishna Mkuu wa TRA Dkt. Edwin Mhede, ameipongeza Idara ya Fedha na idara nyingine ndani ya mamlaka hiyo kwa kufanikisha upatikanaji wa tuzo hizo.

“Nachukua nafasi hii kumshukuru mkuu wa idara anayehusika na Idara ya Fedha pamoja na wakuu wa idara nyingine ndani ya mamlaka maana zote zinatoa mchango mkubwa kuhakikisha idara hii inatoa taarifa sahihi na zenye kuleta mipango sahihi kwa mamlaka na serikali kwa ujumla,” alisema Dkt. Mhede.

Dkt. Mhede alieleza kuwa, taarifa sahihi ni msingi wa mipango kwa kuwa taasisi isiyopanga kushinda ni sawa na taasisi inayopanga kushindwa hivyo suala la uandaaji bora wa taarifa za hesabu ni moja ya ufanisi wa ofisi yoyote hapa ulimwenguni.

Bodi ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu (NBAA) ndio hutoa tuzo hizo kila mwaka ambapo mwaka 2017 TRA iliibuka mshindi wa kwanza tena katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu katika kipengele cha Wakala wa Serikali.

Mwisho.



Share:

Jafo Akerwa Na Utendaji Kazi Wa Watumishi Manispaa Ya Shinyanga

SALVATORY NTANDU
Waziri wa nchi ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo amemwagiza katibu Mkuu wake TAMISEMI kuwahamisha vituo vya kazi Maafisa wawili wa Manispaa ya Shinyanga baada ya kubainika kufanya kazi kwa makundi hali ambayo inaweza kukwamisha shughuli za Umma.

Waziri Jafo amewataja maafisa hao kuwa ni pamoja na Ofisa utumishi wa manispaa ya Shinyanga, Magedi Magezi pamoja na Mweka hazina Paschal Makoye, wahamishwe na  kuwapelekwa katika katika vituo vingine vya kazi.

Jafo ametoa agizo hilo jana baada ya kupokea taarifa ya mkoa wa Shinyanga, kutoka kwa  mkuu wa mkoa wa shinyanga,  Zainab Telack, katika ziara yake ya kikazi ya siku moja iliyoenda sambamba  na ukaguzi wa  ujenzi wa hospitali halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

“Kuna tabia ya watumishi katika manispaa hii wanafanya kazi kwa  makundi na hakuna umoja hasa wakuu wa idara kila mtu ni  mtawala na kusababisha utendaji kazi mbovu nimeamua kuwaondoa ili wakafanya kazi katika sehemu nyingine kuliko kuliko kuwaacha wakiendelea kuwagawa watumishi”alisema Jafo.

Waziri Jafo amesema TAMISEMI itaendelea kufuatilia nyendo za watumisho wote  wa Halmshauri nchini ambao wanafanya kazi kwa mazoea ambao hawaendi na kasi ya Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Pombe Magufuli kwa kuwachukilia hatua za kidhamu ikiwanipamoja ka kuwahamisha katika vituo vya kazi.

“Mimi niko hapa kumsaidia Mh,Rais na siwezi kukubali kuona watumishi wanafanya kazi kwa makundi,nimeshatoa maelekezo kwa wakuu wote wa idara kufanya kazi kwa kushirikiana ili ufanisi wa shughuli za serikali ziweze kufanikiwa na wananchi wapate huduma bora”alisema Jafo.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo, amepongeza ujenzi wa hospitali halmashauri ya wilaya ya Shinyanga baada ya kuyakagua na kuridhika na ujenzi wake na kusema kuwa  Rais Dk John Magufuli amekubali kutoa  Shilingi Milioni 500 ziwezekutumika kuongeza majengo mengine.

Nae  mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack, alibainisha kuwa  kuwa  Serikali ilitoa Shilingi, Bilioni 3 kwaajili ya kujengwa hospitali mbili za wilaya katika mkoani huo, katika Halmashauri za Ushetu na Shinyanga  ambazo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 90.

Mwisho.


Share:

Rais Magufuli Pamoja Na Mkewe Mama Janeth Magufuli Wasali Misa Takatifu Dominika Ya Pili Ya Majilio Katika Kanisa Kuu La Epifania Parokia Ya Bugando Jijini Mwanza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wamejumuika pamoja na waumini wengine wa Kanisa Kuu la Epifania Parokia ya Bugando jijini Mwanza  katika Misa Takatifu ya Dominika ya pili ya Majilio iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza Mhashamu Renatus Nkwande leo tarehe 8/12/2019.



Share:

Kijana Wa Kazi Amuibia Bosi Wake Hati Na Kuikopea

Na. Hassan Mabuye, WIZARA YA ARDHI-Iringa
Mkazi wa Iringa mjini Bi. Lugano Mwadini amejikuta katika deni linalopelekea karibu nyumba yake kupigwa mnada baada kijana wake wa kazi kukopa pesa kiasi cha shilingi 1,000,000 kwa kutumia hati yake ya umiliki wa ardhi ambayo amemuibia.

kadhia hiyo imetokea wakati wa mkutano wa Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi kupitia programu yake ya 'Funguka kwa Waziri' mkoani Iringa alipokuwa akisikiliza na kutatua kero za ardhi kwa wananchi wa mkoa wa Iringa katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo katika Manispaa ya Iringa.

katika mkutano huo Bi. Lugano alimtuhumu Kijana wake wa kazi kwa kumuibia hati na kuenda kukopa kwa Bw. Laurence Panklas ambaye ni askari wa jeshi la polisi mkoani Iringa anayekopesha kwa riba ya 400,000 kila mwezi ambazo kijana huyo hakuweza kuzirudisha kwa wakati jambo lililopelekea kutaka kuuzwa kwa nyumba yake ili kufidia deni hilo.

Bi. Lugano Mwadini aligundua hayo baada ya kupigiwa simu na mkopeshaji huyo kumtaka kwenda kubalisha umiliki wa hati hiyo ili apewe mtu mwingine kwa kuwa hati yake imekopewa na inadaiwa shilingi 1,400,000.

"Mi nilikuwa sipo lakini nikaja kupata taarifa kwa kupigiwa simu kwamba kijana wangu wa kazi ameniibia hati yangu wakati nikiwa katika kazi zangu na amekopea kwa askari mmoja ambaye anakopesha kwa riba ya laki nne kila mwezi, kwa hiyo kijana wangu anadaiwa 1,400,000 na hajalipa hadi sasa" Alisema Bi. Lugano Mwadini.

Waziri Lukuvi alimuagiza Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Iringa Juma Bwire kushughulikia suala hilo, kwanza kwa askali wa jeshi la polisi ambaye anafanya biashara ya pesa na kama ana kibali cha biashara hiyo na analipa kodi, kama halipi basi alipe kodi kwa miamala yote aliyowahi kufanya.

Aidha Waziri Lukuvi aliagiza kukamatwa kwa kijana huyo wa kazi ili alipe deni hilo kwa Bosi wake na kueleza kwanini amefanya uhalifu huo wa kuiba hati ya mtu mwingine.

Katika mkutano huo Waziri Lukuvi aliweza kusikiliza na kutatua migogoro ya wakazi wa mkoani Iringa takribani 200 kwa siku moja ambapo baadhi ya wananchi walieleza kuridhishwa kwa juhudi za waziri lukuvi kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi ya wakazi wa maeneo mbali mbalibila nchini bila kubagua.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger