Monday 2 September 2019

RADI YAUA NG'OMBE 22 KIGOMA

Na Rhoda Ezekiel - Malunde1 blog Kigoma
Ng'ombe  22 wenye thamani ya shilingi milioni 12 ,wamekufa baada ya kupigwa na radi iliyoambatana na mvua na upepo mkali katika kijiji cha  Kaziramihunda  kata ya Gwanumpu wilayani Kakonko mkoani Kigoma.


Wakizungumzia tukio hilo wamiliki wa ng'ombe hao,akiwemo Abdu Kasungu,wamesema tukio hilo limetokea Septemba 1,2019 majira ya saa kumi na moja jioni wakati vijana waliokuwa wametoka kuwanywesha  maji ng'ombe katika Kijiji cha Msenga lakini wakiwa njiani ulitokea upepo mkali ulioambatana na radi na kuwapiga ng'ombe 22 ambao walikufa papo hapo.

Kasungu amesema kati ya ng'ombe 20 alizokuwanazo amepoteza ng'ombe 16  na kwamba anashukuru Mungu kwa kuwa watu waliokuwa wakiwachunga walibaki salama kwa kuwa imetokea ni bahati mbaya hawana budi kulipokea hilo.

Naye Filbert Chibedese aliyepoteza ng'ombe sita amesema tukio hilo limewasikitisha kwa kuwa litawarudisha nyuma sana kiuchumi lakini hawana namna kwa kuwa ni majanga ya kiasili yanayojitokeza bila kutarajia.

Akizungumza na wananchi hao wakati alipofika katika eneo la tukio, Mkuu wa Wilaya ya Kakonko,Kanali Hosea Ndagala amesema tukio hilo ni kama matukio mengine halikutegemea litojee hivyo watu wanatakiwa kuwa wavumilivu na kujua kuwa mambo hayo ni mpango wa mwenyezi Mungu na kutoa pole kwa wote walioingia hasara katika kupoteza ng'ombe hao.

"Nitoe pole kwa wote mliondokewa na mifugo hii, ni kweli inaumiza sana na ni hasara kubwa mmeipata, jambo kubwa ni kumshukuru Mungu kwa kuwaponya watu waliokuwa wanawachunga ng'ombe hao, kikubwa ni uvumilivu msikate tamaa muendelee kupambana haya mambo yanatokea hatuna sababu ya kukata tamaa katika utafutaji poleni sana", amesema Kanali Ndagala.

Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akizungumza na wananchi waliojitokeza katika tukio la ng'ombe kupigwa radi.Picha zote na Rhoda Ezekiel - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akiangalia ng'ombe waliokufa kwa kupigwa radi.
Share:

RAIS MAGUFULI AWAPA RUNGU WATENDAJI WA KATA KUWATWANGA MAWAZIRI,WAKURUGENZI, MA RC WANAOFANYA MAMBO YA HOVYO


Rais wa Tanzania, John Magufuli amewataka watendaji wa kata nchini kutoa taarifa kuhusu wakurugenzi, mawaziri na wakuu wa mikoa wanaofanya matendo yanayokiuka misingi ya utawala bora.


Ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Septemba 2, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam alipokutana na watendaji hao kutoka mikoa yote nchini.

Amebainisha kuwa mtendaji wa kata ndio bosi wa eneo lake, “Hata kama kuna kiongozi wa nafasi gani yuko chini yako na anapoonekana kuenenda visivyo unapaswa kumwajibisha au kutoa taarifa kwa mamlaka yake.”

“Katika kata kuna mkurugenzi wa halmashauri, RC (mkuu wa Mkoa), waziri au nani, wewe (mtendaji kata) ndio msimamizi, kama wewe upo katika kata na ambayo kuna waziri, RC, mkurugenzi sijui nani wewe ndiyo msimamizi,” amesema Magufuli.

Ameongeza, “Usiogope kumlima (barua) na kumwandikia maoni, hata kama anakuzidi cheo kwamba katika kata hii namwona mtumishi huyu anakwenda kinyume na maadili. Na ukimwona ni mkubwa sana, piga nakala hapa kwangu, lazima watu tujifunze kuogopana.”

Huku akizungumza zaidi kwa mifano amesema, “Kila siku anapigana (kiongozi) baa katika kata yako kwa sababu ni mkubwa unaacha kumripoti, chalaza kalamu na ndio maana watendaji kata wana kalamu na saini zao.”

Huku akiwataka kutokubali kudharaulika katika maeneo yao, Magufuli amesema, “Hapa (Ikulu) ni kwenu na mimi ni mpangaji tu hapa na mnaoamua nani aende Ikulu ni nyinyi na wananchi.”
Via Mwananchi

Share:

Angalia Picha : RAIS MAGUFULI AKIZUNGUMZA NA WATENDAJI WA KATA ZOTE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Watendaji wa Kata zote za mikoa ya Tanzania Bara Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Share:

MWAKYEMBE AFURAHISHWA UANZISHWAJI WA SHULE YA MICHEZO 'KAHAMA UNITED SPOTS ACADEMY'

Na Salvatory Ntandu 
Waziri wa Habari Sanaa na Utamaduni, Dkt. Harrison Mwakyembe ameupongeza uongozi wa (Kahama United Sports Academy) kwa kuanzisha shule maalumu ya michezo yenye lengo la kuinua na kukuza vipaji vya mipira wa miguu hapa nchini.

Pongezi hizo amezitoa jana wilayani Kahama mkoani Shinyanga katika hafla maalum ya uzinduzi wa shule hiyo na kusema kuwa endapo kila mkoa hapa nchini utaanzisha shule za michezo Tanzania itakuwa na hazina kubwa ya vijana wenye vipaji maalumu vya michezo tofauti tofauti ambayo iwasadia kupata ajira.

Amefafanua kuwa Michezo kwa sasa ni ajira hivyo kuwepo kwa shule hizo kutatoa fursa kwa wachezaji kuajiriwa na vilabu mbalimbali vinavyoshiriki mashindano ya ndani ya nchi na kimataifa kutokana na kupata maarifa sahihi katika shule hizo.

Waziri Mwakyembe amesema serikali itaendelea kuwaunga mkono wadau wote wa michezo watakaokuwa tayari kuanzisha shule za michezo ili kuhamasisha vijana kupenda kushiriki katika michezi mbalimbali na kuwawezesha kutojiunga na makundi hatarishi katika jamii.

Aidha Mwakyembe amekubali kuwachukua wachezaji wawili wa shule hiyo ambao ni pamoja na Delphinius Dikson,Raphael Kevin na Peter Nzogoya na kuwapeleka kufanyiwa majaribio katika timu ya taifa ya vijana ya Serengeti.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Usaji wa shule hiyo,Hamis Mgeja ameiomba serikali kuziwezesha shule hizo kwa kuzipa vifaa vya michezo vya kisasa ili kuendana na soka la ushindani hapa nchini.
Waziri wa Habari Sanaa na Utamaduni, Dkt. Harrison Mwakyembe akikata keki wakati wa uzinduzi wa shule ya  Kahama United Sports Academy
Mwenyekiti wa bodi ya Usaji wa shule ya  Kahama United Sports Academy, Hamis Mgeja akizungumza wakati wa uzinduzi wa shule hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Kahama,Anamringi Macha akizungumza wakati wa uzinduzi wa shule ya  Kahama United Sports Academy
Share:

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAWAPA MAFUNZO KAMATI YA BUNGE


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene amesema mchakato wa Mkataba Minataka kuhusu Zebaki unaenda hatua kwa hatua ili kuwaandaa watu kuweza kupokea mabadiliko.

Mhe. Simbachawene amesema hayo jana Septemba mosi, 2019 wakati wa semina kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira ya Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki na Uwajibikaji kisheria na fidia kwa madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya bioteknolojia iliyofanyika Jijini Dodoma.

Alisema Serikali iliridhia Mkataba wa Minamata ili kulinda afya ya binadamu na mazingira dhidi ya madhara yanayotokana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na Zebaki. 

"Umoja wa Mataifa ulikaa na kuona kwa fundisho lililotokea Minamata huko Japan hivyo madhara hayo yasiendelee kutokea duniani pamoja na hayo lakini bado zebaki ina kazi ya kufanya unapotaka kuwatoa watu kutoka utamaduni mwingine mabadiliko yanakuwepo. 

"Pengine mnaweza kusema kwanini zebaki isipigwe marufuku mara moja mambo yanayobadilika yanafanywa polepole si kwa haraka na hatimaye watu wataelewa tu," alisema.

Awali aakiwasilisha mada hiyo, Mhandisi wa Viwanda kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo imeandaa semina hiyo Julius Enock alisema madhara yanayotokana na zebaki ni kuathiri mfumo wa neva za fahamu.

Katika kuathiri kwa mfumo huko inasababisha kusikia, kuongea, kuona, kumeng’enya, kumeza chakula, kutembea kuathiriwa pamoja na ukakamavu wa mwili. 

Aidha madhara mengine aliyotaja Enock ni kuathiri viungo muhimu vya mwili ambayo ni moyo, mapafu, ini, figo na hata mimba.


Share:

Mahakama kuamua leo kuhusu Hatima ya Mrithi wa Ubunge Jimbo la Tundu Lissu

Hatima ya kuapishwa kwa mbunge mteule wa Jimbo la Singida Mashariki, Miraji Mtaturu (CCM), itajulikana leo baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuamua iwapo itatoa zuio la kuapishwa kwa mbunge huyo ama la.

Katika maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na kaka wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Tundu Lissu, Alute Mungwai Lissu, pamoja na mambo mengine, ameiomba Mahakama hiyo itoe zuio la kuapishwa kwa mbunge huyo mpya na ruhusa ya kumshtaki Spika wa Bunge, Job Ndugai, kwa kumvua ubunge pasipo sababu za msingi.

Awali Mahakama hiyo ilitupilia mbali mapingamizi yaliyowekwa na upande wa Jamhuri uliotaka kesi hiyo isisikilizwe mahakamani hapo, kutokana na walichodai ni mapungufu ya kisheria ya maombi hayo, hivyo kutaka yasisikilizwe.

Jaji wa Mahakama Kuu, Sirilius Matupa, aliyatupa mapingamizi hayo baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri haukuwa na hoja za msingi za kuizuia kesi hiyo isisikilizwe mahakamani hapo, hivyo kukubaliana na hoja za Wakili wa Lissu, Peter Kibatala.


Share:

LIVE: Rais Magufuli Azungumza Na Watendaji Wa Kata Zote Tanzania Bara Ikulu Dar es Salaam

LIVE: Rais  Magufuli Azungumza Na Watendaji Wa Kata Zote Tanzania Bara  Ikulu Dar es Salaam


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 2,2019






































































Share:

Sunday 1 September 2019

WAANDISHI WA HABARI WATAMBULISHA KUNDI LA 'STRONG DADAZ JOURNALIST' ...DC MAHUNDI ATIA NENO


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya,Mhandisi MaryPrisa Mahundi akiwa katika picha ya pamoja na kikundi cha Strong Dadaz Journalist

Na Esther Macha,Chunya
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya,Mhandisi MaryPrisa Mahundi amewataka wanawake kuendelea kujituma kufanya kazi ili kuongeza thamani yao katika maisha badala ya kutegemea kuolewa.

Akizungumza  na waandishi wa habari wanawake waliomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kutambulisha kikundi chao kinachojulikana Strong Dadaz Journalist kilichopo Mkoani Mbeya.

Mhandisi Mahundi aliwataka wanapofanya kazi pia kazi wajitahidi kumtanguliza mungu wakati wanafanya kazi zao za kila siku ili waweze kufanikiwa katika shughuli zao.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa pia wajiongozee dhamani pamoja na kusaidiana wenyewe kwa wenyewe ili kufikia malengo waliyojiwekea ikiwa ni pamoja na kupendana.

“Siri ya Mwanamke ni kujishughulisha katika maisha msikate tama wanawake wenzangu kitendo cha nyie kuamua kuwa na umoja wenu ni faraja tosha kwenu”alisema Mkuu huyo wa Wilaya.

Aidha Mhandisi Mahundi alitoa kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya kusaidia kikundi hicho cha Strong Dadaz Journalist ili kiweze kusajili Online Tv ambayo kikundi hicho kimedhamiria kufungua ili kuboresha huduma za kihabari kwa wanawake katika kurahisisha upatikanaji wa habari kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bomba Fm Radio ,Fredy Herbert aliahidi kuchangia kikundi hicho sh.100,000/= katika kusaidia kukamilisha usajili wa Online tv.

“Mhe. mimi nitakuwa na waandishi hawa pindi watakapohitaji msaada wa jambo lolote nitakuwa nao karibu katika kuwasaidia ",alisema Mkurugenzi huyo.

Share:

BASI LA MWENDOKASI LATEKETEA NA MOTO KIMARA JIJINI DAR ES SALAAM


Basi la usafiri wa haraka (Mwendokasi) la kampuni ya UDART la limeshika moto na kuteketea eneo la Kimara, jijini Dar es Salaam usiku huu.

Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika na pia hakuna taarifa kuhusu majeruhi ama vifo kwenye moto huo.
Share:

JISAJILI KUSHIRIKI MKUTANO WA KIBIASHA NA MAONESHO KATI YA TANZANIA NA UGANDA SEPT 6-7, 2019 JIJINI DAR ES SALAAM



• Sisi ni Zaidi ya Ujirani

• Sisi ni ndugu wa Damu

Tanzania na Uganda katika meza moja ili kukuza na kujenga Uchumi imara na madhubuti!

#TZUGBusinessForum19

#SisiNiTanzaniaMpyA+ ya Wazalendo, Waadilifu, Waaminifu, Wachapa Kazi!
Share:

PAPA FRANCIS AKWAMA KWENYE LIFTI DAKIKA 25 BAADA YA UMEME KUKATIKA AKIWAHI KANISANI

Papa Francis ameomba radhi kwa kuchelewa misa katika kanisa la Mt. Petro na kusema kuwa alikwama kwenye lifti akiwa anaelekea kanisani.

Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 82 alikwama kwenye lifti kwa dakia 25 mara baada ya umeme kukatika na kuweza kutoka kabla ya kikosi cha wazima moto hakijawasili.

"Ninapaswa kuomba radhi kwa kuchelewa," Papa huyo aliawaeleza waumini wake huku akitabasamu.

Na kuwataka waumini wote kuwapongeza wazima moto kwa kazi kubwa waliofanya .

Papa akiwahutubia umati wa watu kusema "kumekuwa na itilafu ya umeme hivyo lifti ilisimama".

"Namshukuru Mungu na kikosi cha zima moto kilifika kwa wakati"

Televisheni inayorusha matangazo ya moja kwa moja ya sala hiyo walihisi papa huyo amechelewa kufika katika misa kutokana na sababu za kiafya, shirika la habari la AFP limeripoti.

Papa huyo alitangaza pia kuwa mwezi ujao, atatangaza makadinari 10 wapya wa kanisa katoliki.
Chanzo - BBC
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger