Monday 3 June 2019

Nape Ammwagia Pongezi Waziri Makamba

Mbunge wa Jimbo la Mtama,Nape Nnauye ametoa pongezi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kusimamia suala la katazo la mifuko ya Plastiki.

Katika ukurasa wake wa Twitter leo asubuhi Jumatatu Juni 3, 2019 Nape ameandika ujumbe akisema kazi iliyofanywa na Makamaba ni mfano wa kiongozi na siyo mtawala .

Akiwa ameambatanisha picha yake (Nape) na Makamba wakiwa wamevalia masharti ya rangi ya kijana inayotumiwa na CCM, Nape amendika, “Namna wewe na wenzako mlivyosimamia swala la mifuko ya plastiki ni mfano tosha wa utofauti kati ya kuongoza na kutawala.. Hongera sana!.”

Waziri Makamba ameongoza kampeni hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alilotoa bungeni miezi kadhaa iliyopita akisema kuanzia Juni mosi, 2019, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuingiza, kuuza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za aina yoyote na matumizi yake yatakoma Mei 31, 2019.



Share:

Tangazo la Nafasi za Masomo Kwa Kidato cha Tano Shule ya Sekondari Lake Tanganyika....Changamkia Hii Fursa





Share:

Jeshi la Polisi Kigoma Lafanikiwa Kumkamata kinara wa ubakaji na kujeruhi wanawake

Vyombo vya dola mkoani Kigoma vimefanikiwa kumkamata Hussein Hamis, anayetuhumiwa kuwa kinara wa ubakaji na kujeruhi wanawake nyakati za usiku maarufu kama teleza.

Hamis aliye maarufu kwa jina la Orosho, alikamatwa pamoja na watuhumiwa wengine tisa wakitambuliwa kama teleza, ambao huwaingilia kingono wanawake kwa kuwalazimisha, kuwaibia na kuwajeruhi wakiwa wamejipaka ‘oil’ chafu au mafuta ya mawese ili wanaposhikwa wawe wanateleza.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Mjini, Samson Hanga alisema baada ya kuwapo taarifa hiyo, vyombo vya dola viliendesha  msako mkali kwa kushirikiana na wananchi ili kuwakamata wahalifu.

“Tulitengeneza namna bora ya kuwakamata wahusika, tulifanya kazi ya upigaji kura ya siri tukapata majina, mengine tulipata kupitia vyombo vya dola. Mpaka sasa tumekamata vijana tisa, wapo mahabusu na upelelezi unaendelea,” alisema Hanga.

Alisema katika majina yaliyotajwa na kupigiwa kura, mtuhumiwa mmoja alitajwa na akina mama waliofanyiwa vitendo vya ukatili ambaye ni Hamis.

“Unajua Serikali ina mkono mrefu, macho makubwa, yule kijana alipopata taarifa tunamtafuta alikimbilia kwa mama yake Kijiji cha Kagongo, baadae akakimbilia tena Kijiji cha Kagunga, juzi jioni tukafanikiwa kumkamata wilayani Kasulu na kuletwa hapa kituo cha polisi kwa ajili ya hatua zaidi,” alisema.

Hanga alisema pia wamefanya gwaride la utambuzi kwa waathirika  kuwatambua vijana 10 waliokamatwa.

Alisema msako bado unaendelea na kuonya yeyote anayejihusisha na vitendo hivyo kuacha mara moja kabla vyombo vya dola havijambaini na hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wale wote watakaobainika.
.

Share:

Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) Hashim Rungwe Aripoti Polisi

Mwenyekiti wa Chama cha Umma (Chaumma) Hashim Rungwe ameripoti katika kituo cha polisi Osterbay kuitikia wito wa kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni Mussa Taibu.

Rungwe amefika kituoni hapo saa 4.10 asubuhi ya leo Jumatatu Juni 3, 2019  akiwa amevalia kanzu nyeupe akiongozana na mtu mmoja ambao wote wameingia katika ofisi ya Kamanda Taibu.

Mwenyekiti huyo amefika kituoni hapo baada ya jana Jumapili Eugene Kabendera, kwa niaba ya Sekretarieti ya Ushirikiano wa Vyama nane vya Upinzani kutoa taarifa akisema polisi walifika katika ofisi za Chaumma jijini Dar es Salaam na kueleza Rungwe anatakiwa kuripoti leo Jumatatu Juni 3,2019 katika ofisi za Kamanda Taibu.

Katika mkutano huo, viongozi wa vyama hivyo walitoa tamko la kutoshiriki kwenye uchaguzi wa marudio kwenye kata 32 unaotarajiwa kufanyika  Juni 15, 2019 kwa sababu unasimamiwa na Wakurugenzi Halmashauri za wilaya na Manispaa kinyume na uamuzi wa Mahakama Kuu.


Share:

Kitabu Cha Madini Yapatikanayo Tanzania

Serikali kupitia  Wizara ya Madini chini ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imetoa toleo jipya la kitabu cha Madini yapatikanayo Tanzania kuanzia ngazi ya Mikoa, Wilaya na Kata.
 
Toleo hili la nne linaonesha taarifa nyingi zaidi ambapo maeneo mapya yenye madini yameongezeka zaidi ya 2200.
 
GST inatarajia kuwa kitabu hiki kitaongeza uelewa kwa wananchi na wadau mbalimbali kwa ujumla juu ya rasilimali madini yanayopatikana hapa nchini Tanzania na kuchochea uwekezaji katika sekta ya madini.GST inawakaribisha wadau wa sekta ya madini kujipatia nakala ya kitabu hicho kinachopatikana katika ofisi za GST jijini Dodoma.


Share:

Waziri Mhagama Azindua Baraza La Taifa La Ushauri Kwa Watu Wenye Ulemavu

Na; Mwandishi Wetu
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amezindua rasmi Baraza la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu huku akilitaka baraza hilo kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano ili kuleta tija na mafanikio makubwa kwa Watu wenye Ulemavu nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo alisema kuwa baraza linajukumu kubwa katika kuhakikisha usimamizi wa sekta ya watu wenye ulemavu pamoja na kuishauri Serikali juu ya masuala mbalimbali ya kundi hilo maalumu.

“Mtambue nafasi mliyopewa ni dhamana kubwa katika kuwahudumia watu wenye ulemavu ambao ni takribani asilimia 5 ya watanzania, hivyo ni vyema mkashirikiana na Serikali kubuni mikakati itakayosaidia kutatua changamoto zinazowakabili wenye ulemavu”, alisema Mhagama

Alifafanua kuwa Baraza hilo limeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya Mwaka 2010 na Sheria hiyo imeeleza majukumu ya Baraza ikiwa ni pamoja na kutoa ushauri.

“Ni matumaini yangu mtakuwa washauri wazuri wa masuala ya watu wenye ulemavu kwa kuzingatia usawa kwa wote na si maslahi binafsi,” alisisitiza Mhagama.

Sambamba na hilo alimpongeza Mwenyekiti mpya wa Baraza hilo Dkt. Lukas Kija kwa kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Wajumbe wengine kutokana na uaminifu na uwezo walionao katika kusimamia masuala ya Watu wenye Ulemavu.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha Watu wenye Ulemavu wanapata haki zao za msingi na kwa ajili ya ustawi wao katika Nyanja mbalimbali ikiwemo elimu, afya, uchumi, kuwa na miundombinu rafiki pamoja na nyenzo za kujimudu.

Aidha Waziri Mhagama alitoa rai kwa watendaji wa Baraza hilo kuwa na miongozo yote inayohusu masuala ya Watu wenye Ulemavu itakayo wawezesha kufanikisha utendaji wao wa kazi.

Kwa Upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa amesema kuwa Serikali katika mwaka 2019/2020 itaanza mapitio ya Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010 ili kuwawezesha watu wenye ulemavu kwenda sambamba na mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu Dkt. Lukas Kija alieleza kuwa wapo tayari kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo inayosimamia haki na ustawi wa Watu wenye Ulemavu.

Aliongeza kuwa Baraza hilo lipo tayari kutoa ushauri na hoja zenye tija kwa Serikali juu ya masuala mbalimbali ya Watu wenye Ulemavu.

Pia, Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe alieleza kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu itaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa Baraza hilo na kufanya kazi pamoja katika kutatua changamoto zinazowakabili Watu wenye Ulemavu nchini ikiwemo migogoro na migongano kwa wadau.

Uzinduzi wa Baraza la Taifa la Ushauri kwa Watu wenye Ulemavu umefanyika Juni 2, 2019 jijini Dodoma ambapo Baraza hilo litaongoza kwa kipindi cha miaka mitatu (2019 hadi 2021) likiongozwa na Mwenyekiti Dkt. Lukas Kija. Awali Baraza hilo lilikuwa likiongozwa na Dkt. Edward Bagandanshwa ambalo limemaliza muda wake mwaka 2017.

MWISHO


Share:

Naibu Waziri Kanyasu Awaonya Wananchi Wanaotoa Vitisho Kwa Askari Wanyamapori Wa Vijiji

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amewataka Wananchi waache tabia ya kuwatishia maisha  Askari wanyamapori wa vijiji  (VGS) wakati wanapowakataza wananchi hao kuendesha shughuli za kibinadamu katika maeneo ya mtawanyiko na mapito ya wanyamapori (shoroba)

Kufuatia hali hiyo, Mhe.Kanyasu amemtaka Mkuu wa wilaya ya Namtumbo,  Mhe. Sophia Mfaume afanye uchunguzi kwa kutumia vyombo vyake vya usalama ili kuwabaini Wananchi hao wanaowatishia Askari  wanapotekeleza majukumu yao  na watakaobainika hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Mhe. Kanyasu, ameyasema hayo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya Askari  20 wa  Wanyamapori wa Vijiji  wa kutoka mikoa ya Ruvuma, Mbeya na Singida waliohitimu mafunzo hayo  katika Chuo cha Mafunzo ya Uhifadhi wa Maliasili kwa Jamii cha Likuyu Sekamaganga kilichopo katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma

“leo mmehitimu na tumewaapisha, mmekuwa askari kweli  lakini tambueni kuwa kazi za kiuchumi zinapelekea uharibifu mkubwa sana wa mapito ya wanyama, nendeni mkawaelimishe wananchi wasiendelee kuharibu kwa ustawi wa hifadhi zetu"

Amefafanua kuwa  maeneo ya mtawanyiko na shoroba lazima zilindwe ili kuruhusu wanyamapori waendelee  kuzaliana  na pia kwenda  kupata virutubisho maalum ambayo havipo mbugani.

'' Tunazihitaji hizi shoroba, tulikuwa tumejisahau shoroba nyingi zimekuwa mashamba na makazi na wanyama wamekuwa hawana sehemu ya kupita'' amesema Kanyasu

Amesema shoroba na maeneo ya mtawanyiko zisipokuwepo utalii na Hifadhi vitatoweka.

" Lazima tufike mahali tuamue eneo hili ni kwa ajili ya kilimo na eneo hili kwa ajili ya makazi, haiwezekani maeneo yote tukaanzisha kilimo na makazi ilhali wanyamapori hawana mipaka" Alisisitiza Kanyasu .

Amesema uwepo wa shoroba na maeneo ya mtawanyiko husaidia  kupata kizazi imara cha wanyamapori kwani wakifungiwa sehemu moja huzaliana ndugu na kukosa ubora,ikiwamo kuwa rahisi kushambuliwa na magonjwa.

Katika hatua nyingine, Mhe.Kanyasu amewataka askari hao kufanya kazi kwa uaminifu kwa kujiepusha kuungana na mtandao wa majangili.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Namtumbo, Mhe. Sophia Mfaume amewahakikishia askari hao kuwa wafanye kazi kwa kufuta sheria na wale watakaowakwamisha  katika kutekeleza majukumu yao hatasita kuwachukulia sheria.

Aidha, Amewataka Wananchi wafuate sheria kwa kuheshimu maeneo ya mtawanyiko na shoroba ili Hifadhi ziendelee kuwepo

Kwa upande wake, Mhitimu wa mafunzo hayo Musa Alfred Wakati akisoma risala, Amemueleza Naibu Waziri kuwa mafunzo waliyopewa yatakuwa chachu katika shughuli za uhifadhi nchini.

Naye Mbunge wa viti maalum wa mkoa wa Ruvuma, Jaqueline Msongozi amewataka askari hao wa vijiji watekeleze majukumu yao bila kutishwa na mtu yeyote kwa vile maliasili hizo ni za watanzania wote na wao wanazilinda kwa niaba ya Watanzania.

MWISHO


Share:

Taarifa rasmi ya Tukio la Mama Mjamzito kujijeruhi Kirando - Rukwa

Kuanzia tarehe 30 Mei, 2019 kuna taarifa zilizosambaa na kutolewa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuhusu mama mjamzito anayesemekana kujijeruhi maeneo ya tumboni na kupelekea kutoa mtoto tumboni,tukio lililotokea katika kata ya Kirando Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa. 


Baada ya kupokea taarifa hizo timu ya ufuatiliaji iliyoundwa na wataalam wa Afya kutoka ngazi ya Mkoa na Wilaya husika ikiongozwa na Mganga Mkuu wa Mkoa ilifanya ufuatiliaji wa tukio hilo kwa lengo la kupata uhalisia wake na kubaini mambo yafuatayo:

1. Mhusika katika tukio hili ni Bi Joyce Mweupe Kalinda mwenye umri wa miaka 32 anayeishi katika Kitongoji cha Kalya, Kijiji cha Kamwanda, Kata ya Kirando, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa, umbali wa takribani kilometa moja kutoka Kituo cha  Afya Kirando.

 2.Bi Joyce alipokelewa katika kituo cha Afya Kirando kilichopo katika kata ya kirando Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi majira ya saa 09:30 alfajiri ya tarehe 30 Mei 2019 akiwa amesindikizwa na ndugu zake wawili (Wifi na Shangazi yake) kwa lengo la kujifungua ambapo alipokelewa na kufanyiwa uchunguzi wa awali.

Katika uchunguzi huo ilibainika kuwa mama huyo alikuwa na
ujauzito unaokadiriwa kuwa na miezi tisa, akiwa na dalili za
uchungu katika hali ya kawaida kiafya.

4. Baada ya uchunguzi wa awali kukamilika alipelekwa katika wodi ya wazazi wanaosubiri kujifungua kwa ajili ya kupumzika huku watoa  huduma wakiendelea kutoa huduma kwa wagonjwa wengine.

5. Katika ujauzito huu alikuwa akihudhuria kliniki ya Afya ya Mama na Mtoto katika Kituo cha Afya Kirando ambapo alifanikiwa kufanya mahudhurio matatu na hudhurio la mwisho likiwa ni tarehe 08 Mei, 2019

6. Mnamo saa 10:30 alfajiri wakati watoa huduma wakifuatilia kujua maendeleo yake ndipo walipobaini kuwa Bi Joyce hakuwepo ndani ya wodi na hivyo kuanza kumtafuta katika maeneo mbalimbali ya kituo cha afya na kutoa taarifa kwa mlinzi na uongozi wa kituo cha afya.

7. Wakati juhudi za kumtafuta zikiendelea, majira ya saa 12:30 asubuhi Bi Joyce aliletwa kituoni akiwa amebebwa kwenye godoro na watu watatu (Mojawapo akiwa ni mwenyekiti wa Kijiji cha Kamwanda) huku akivuja damu nyingi.

8. Watoa huduma walimpokea mgonjwa na kumuona akiwa ametapakaa damu, mtoto akiwa nje ya tumbo. Baada ya kumchunguza Bi Joyce alibainika kuwa na jeraha lilililosababishwa na kitu chenye ncha kali tumboni huku sehemu ya utumbo, mfuko wa uzazi, kondo la nyuma na mtoto vikiwa nje na yeye mwenyewe akiwa hajitambui. Baada ya hapo timu ya Kituo cha Afya ikongozwa na Mganga Mfawidhi Dkt. Gideon Msaki iliendelea na huduma za upasuaji wa dharura kwa ajili ya kuokoa Maisha ya Bi Joyce.

Baada ya huduma za upasuaji wa dharura kufanyika timu ya ufuatiliaji iliendelea na ufuatiliaji zaidi wa tukio hili na kubaini ifuatavyo:

1. Bi Joyce alipotoka kituo cha Afya alirudi nyumbani kwake anapoishi yeye,mtoto wake wa kiume aitwaye Linus Sindani anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 12 au 13 na mume wake ambaye siku ya tukio hakuwepo nyumbani. 2. Mara baada ya kurudi nyumbani Bi Joyce alimwagiza mwanaye (Linusi) kwenda kumuita shangazi yake ambaye anaishi maeneo ya jirani na nyumbani kwao. Waliporudi wakiwa na shangazi ndipo walipomkuta Bi Joyce akiwa ameloa damu na hivyo kutoa taarifa kwa majirani na mwenyekiti wa Kijiji kwa ajili ya msaada
zaidi. 

Hitimisho
1. Timu ya ufuatiliaji imejiridhisha kuwa huduma za dharura za upasuaji wa kuokoa Maisha ya Bi Joyce zimefanyika kwa mafanikio makubwa katika kituo cha Afya Kirando na kwamba mama na mtoto ambao kwa sasa wamehamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwa uangalizi zaidi wanaendelea vizuri 

2. Tunatoa pongezi kubwa kwa watumishi wa Kituo cha Afya Kirando kwa juhudi kubwa walizofanya kuokoa Maisha ya Bi Joyce Kalinda. 

3. Tukio hili limeripotiwa katika jeshi la Polisi kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi zaidi.


Share:

Vyama vya Upinzani Vyatangaza Kususia Uchaguzi wa Marudio

Vyama  nane vya upinzani vimesema havitashiriki uchaguzi wa marudio katika kata 32 unaotarajia kufanyika Juni 15, mwaka huu, endapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haitatekeleza agizo la Mahakama la kuwataka wakurugenzi wa halmashauri kutosimamia uchaguzi.

Vyama vilivyosusia ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ACT-Wazalendo, NCCR-Mageuzi,Chauma, UPDP, NLD,CCK na DP.

Wakizungumza kwa niaba ya vyama hivyo nane, viongozi wa vyama vinne vya ACT-Wazalendo, Chauma, UPDP na NLD walisema kitendo cha NEC kuwaruhusu wakurugenzi kuendelea kusimamia uchaguzi huo ni kuidharau mahakama na kwamba hata vyama vyao haviwezi kushiriki kwa kuwa kufanya hivyo ni kushirikiki katika dharau dhidi ya hukumu ya mahakama.

Akisoma tamko la vyama hivyo mbele ya waandishi wa habari jana jijini Dar es Salam, Mwenyekiti wa Taifa wa UPDP, Fahmi Dovutwa, alisema pamoja na kwamba mahakama ilitoa hukumu ya kufuta vifungu vya sheria vinavyowapa wakurugenzi mamlaka ya kusimamia uchaguzi, lakini vyama hivyo vimekuwa vikipokea barua ya mchakato wa uchukuaji na urudishaji wa fomu kutoka kwa wakurugenzi hao.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), ilitangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa marudio katika kata 32, Juni 15, mwaka huu na baada ya tangazo hilo, wakurugenzi wamekuwa wakiviandikia vyama vya siasa juu ya mchakato wa kuchukua na kurudisha fomu na kutia saini kama wasimamizi wa uchaguzi huo,” alisema Dovutwa.

Aliongeza: “Itakumbukwa kuwa Mei 10, mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam ilitoa uamuzi wa kuvifuta vifungu vya sheria ya uchaguzi ambavyo vilikuwa vinawapa mamlaka wakurugenzi wa halmashauri nchini kuwa wasimamizi wa uchaguzi katika maeneo yao. Mara baada ya uamuzi huo wa Mahakama, Mwanasheria Mkuu wa Serikali alisema serikali itawasilisha kusudio lake la kukata rufani kupinga uamuzi huo, lakini mpaka tunavyozungumza hivi, hakuna rufani iliyowasilishwa wala ombi la kisheria la kusitisha utekelezaji wa hukumu hiyo.”

Dovutwa alisema vyama hivyo vinaitaka NEC kupitia mamlaka yake iliyopewa, kuteua wasimamizi wa uchaguzi huo wa marudio mara moja na kama itaendelea na msimamo wake wa kudharau amri ya mahakama, vyama hivyo vitachukua hatua ya kutoshiriki uchaguzi huo na vitawasiliana na wanaharakati waliofungua kesi hiyo kupeleka shauri mahakamani la kukazia hukumu hiyo na kuitaka mahakama iichukulie hatua NEC kwa kudharau amri hiyo ya mahakama.

Pia alisema vitaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika madai ya kuhakikisha wanapata tume huru ya uchaguzi ambayo itakuwa na uwezo kamili na mamlaka ya kuandaa na kusimamia uchaguzi huru na haki ikiwa ni pamoja na kuwa na watendaji na wasimamizi wake wasiofungamana na chama chochote cha siasa.

Vyama hivyo vilitumia nafasi hiyo pia, kuikumbusha NEC kutangaza utaratibu wa kuanza kuandikisha wananchi katika daftari la kudumu la wapigakura katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu June 3




Share:

Sunday 2 June 2019

WACHIMBAJI ZAIDI YA ELFU 10 HATARINI KUPATA MAGONJWA YA MLIPUKO MSALALA KUTOKANA KUJISAIDIA PORINI


 Choo cha maturubai cha wachimbaji.
Akina mama wakitafuta mawe ya dhahabu

Na Salvatory Ntandu - Kahama

Zaidi ya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu 10,000 katika mgodi usiyo rasmi ulipo katika kijiji cha kakola namba tisa katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga wako hatarini kupata magonjwa ya mlipuko kutokana na kujisaindia vichakani.

Hayo yamebainishwa jana na Mwenyekiti wa kijiji hicho Emmanuel Nkenze wakati akizungumza na Waandishi wa Habari waliotembelea mgodi huo, na kusema kuwa tatizo hilo linahidaji kupatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuzuia kuzuka kwa magonjwa ya mlipuko.

Amesema kuwa vyoo vilivyopo kwa sasa ni madundu kumi ambayo yanaonekana ni machache ukilinganisha na idaidi ya wachimbaji wadogo waliopo ambao wanazidi kuongezeka na kila siku hali huku kasi ya uchimbaji wa vyoo ikiwa ni ndogo huku wengi wao hawatambui umuhimu wa kujisaidia katika maeneo salama.

Baadhi ya wachimbali katika Mgodi huo akiwemo Samwel Joseph na Esta Shija wamesema kwa sasa hali sio nzuri katika eneo hilo kwani wachimbaji wengi hawana desturi ya kujisaidia katika vyoo na kuziomba mamlaka husika kulipatia ufumbuzi wa haraka ili kuzuia watu kupata magonjwa kwani idadi ya wachimbaji inazidi kuongezeka.

Wamefafanua kuwa gharama za kujisaidia katika vyoo vilivyopo katika eneo hilo ni kubwa jambo ambalo wao wameshindwa kuimudi kwani zinabadilika badilika mara kwa mara katika vyoo vilivyopo katika maeneo hayo na kusababisha wengi wao kwenda kujisaidia vichakani.

Naye Msimamizi mkuu wa Mgodi huo Husein Makubi Ngh’wananyazala amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa kwa sasa ofisi yake imewekeza nguvu kubwa katika ujenzi wa vyoo ili kukabiliana na Tatizo la uhaba wa matundu ya vyoo ikilinganishwa na idadi kubwa ta wachimbaji.

Hata hivyo amesema kuwa, tatizo la upungufu wa vyoo mgodini umetokana na uongezeko la wachimbaji wadogo ambao wamekuwa wakiongezeka kila siku kutokana na eneo hilo kuwa na wingi wa madini.

Amesema kuwa, ili kuendelea kupamaba na uhaba huo wameanza kuwahamasisha wamilikiwa wa nyumba za kulala wageni zilizojengwa katika eneo hilo,kuhakikisha wanajenga vyoo kabla ya kufungua nyumba yake ali ambayo itapunguza adha ya wachimbaji kujisaidia vichakani.

Akiongea kwa niaba ya wachimbaji wadogo Samweli Joseph alisema kuwa, sababu inayopolekea wachimbaji wadogo kujisadia vichakani,inatokana na gharama ya shilingi 3,00 za kujisaidia katika vyoo viliyopo na kufanya wengi wetu kujisaidia vichakani

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha  amesema kuwa ujenzi wa vyoo katika Mgodi huo unandelea kujengwa kwa haraka ili kuhakikisha Tatizo hilo linakomeshwa mara mmoja.

Share:

Nacte: Tamisemi selection 2019

Nacte Tamisemi selection 2019, Form Five selection, Selection form five 2019/2020 , form five selection 2019/20 first selection form five 2019 pdf tamisemi form five selection 2019 form five second selection 2019/2020 post form five 2019, necta form five selection 2019, www.tamisemi.go.tz form five selection, form 5 selection 2019 pdf download, form five second selection 2019/20

List of students selected to join Form Five, Central Education and Technical Colleges for the 2019 Academy.

The National Council for Technical Education (NACTE) is a corporate body established by the National Council for Technical Education Act, 1997 (Act No. 9 of 1997). The Act provides a legal framework for the Council to coordinate provision of technical education and training and establish an efficient national qualifications system that will ensure that products from technical institutions are of high quality and respond to changing needs as well as technological innovations in the world.

Technical education in this context is defined as “education and training undertaken by students to equip them to play roles requiring higher levels of skills, knowledge and understanding and in which they take responsibility for their areas of specialization”. NACTE is thus, a multidisciplinary and multi-sectoral body empowered to oversee and coordinate the provision of technical education and training in Tanzania.

CLICK HERE TO ACCESS FORM 5 SELECTION 2019

OTHER RELATED ARTICLES

CLICK HERE TO ACCESS FULL PDF FILE- FORM 5 SELECTION 2019

DOWNLOAD >>Form five Joining Instruction 2019/2020

Tamisemi: All girls who passed Form four will Join Form Five or Technical Colleges

[FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection 2019

Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano 2019

NACTE online Application Window for 2019 is now open – apply now

The post Nacte: Tamisemi selection 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WANANCHI WAUA MWIZI ALIYEKUTWA AKIIBA DUKANI HUKU AKIJIHAMI KWA KISU SHINYANGA

Mwanaume, aliyejihami kwa kishu asiyefahamika jina kabila wala makazi yake umri kati ya miaka 28 - 29 ameuawa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi baada ya kukutwa akiiba bidhaa za duka kwenye duka la Bertha John (28), mkazi wa kijiji cha Nyashimbi, kata ya Puni, Tarafa ya Itwangi, wilaya ya Shinyanga.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Richard Abwao tukio hilo limetokea Mei 30,2019 ya saa tano usiku kijiji cha Nyashimbi wilaya ya Shinyanga.

“Chanzo cha tukio hilo ni Marehemu kukutwa na mmiliki wa duka akiiba ambapo alipiga kelele za kuomba msaada na watu walijitokeza kutaka kumkamata marehemu, ndipo marehemu alipochomoa kisu alichokuwa nacho na kumjeruhi kiganja cha mkono wa kulia Thomas Selemani(30)”,ameeleza.

“Kutokana na hali hiyo wananchi hao walichukua uamuzi wa kumuua na kumchoma moto shambani kwa Shigila Kitebbi ( 70), Mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na daktari wa Serikali na kukabidhiwa kwa Viongozi wa Kijiji kwa taratibu za mazishi”,ameongeza Kamanda Abwao.


Amesema juhudi za kuwakamata waliohusika na tukio hilo zinaendelea.

Kadama Malunde - Malunde1 blog
Share:

TBL YAFUTURISHA WAFANYAKAZI WAKE DAR, ARUSHA, MWANZA NA MBEYA



Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL- Dar es Salaam wakishiriki futari iliyoandaliwa na kampuni kwa wafanyakazi wake mwishoni mwa wiki.
Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL-Mbeya wakishiriki futari iliyoandaliwa na kampuni kwa wafanyakazi wake mwishoni mwa wiki
Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL-Mwanza wakishiriki futari iliyoandaliwa na kampuni kwa wafanyakazi wake mwishoni mwa wiki
Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL-Arusha wakishiriki futari iliyoandaliwa na kampuni kwa wafanyakazi wake mwishoni mwa wiki.
Share:

Ngoma Mpya ya Asili : KISIMA - MBINA


Nakualika kutazama video mpya ya Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Majabala 'Kisima The Greatest Singer' kutoka mkoani Simiyu, inaitwa Mbina... Ngoma kali sana mtu wangu,itazame hapa chini

Share:

JAMAA AFURAHIA KUFANYA KAZI NA MAITI ...ADAI HAWASUMBUI KABISA!!

Kwa wengi, maiti huogofya sana na ni wachache pekee ambao huwa na ukakamavu wa kuingia kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti. 


Wengi huteta kuwa huathirika na ndoto mbaya wakati wowote wakikutana na maiti. Lakini 

Basil Enatu ambaye hupenda kufanya kazi na maiti. Ni muhudumu wa hifadhi ya maiti nchini Uganda anasema miili ya waliofariki ndio marafiki wake wakubwa.

 Enatu, mwenye miaka 57, ni baba wa watoto kumi na wawili na amekuwa akifanya kazi kama mhifadhi wa maiti kwa takriban miaka 32 katika hospitali ya Soroti nchini Uganda. 

Akiongea na gazeti la Daily Monitor, mzee Enatu anasema huwa ni raha sana kufanya kazi na maiti kwani hawasumbui. 

“Napenda kufanya kazi na waliofariki kwani maiti hawasumbua,” aliambia Daily Monitor mnamo Juni 1,2019. 

Enatu alisema lake ni kuwaosha na kuwavisha maiti na wakati mwingine madaktari pia humtaka awasaidie kuvikata vipande vya mwili wakati wa upasuaji wakati mwili unafanyiwa uchunguzi. 

 Licha kuipenda kazi yake, mzee alisema ina changamoto kwani wengi hukataa hata kumsalimu wakihofia mikono yake. 

“Nimegundua wakati nilipokuwa nashiriki tembo ya pale mtaani, wenzangu hawakutaka kushiriki pamoja nami. Wauzaji vile vile walikuwa wakiosha chombo nilichokitumia kwa maji moto tofauti na wengine,” Enatu alisema.

 Kisa hicho ni sawia na cha Jane Mumbi aliyekuwa akifanya kazi ya kuhifadhi maiti katika chumba cha City. Mumbi alisema hupata raha sana kuhudumia maiti.
Chanzo - Tuko
Share:

Waziri Mkuu Aushukuru Uongozi Wa Kanisa ......Ni Baada Ya Kutoa Sehemu Ya Eneo Lake Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Shule

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameushukuru uongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi kwa kutoa sehemu ya eneo lake na baadhi ya majengo kwa ajili ya ujenzi wa shule.

Jimbo Katoliki la Lindi limetoa eneo hilo lilipo katika Parokia ya Mnacho wilayani Ruangwa ambalo awali ilikuwa shule ya msingi ya Mnacho sasa imebadilishwa na kuwa sekondari.

Waziri Mkuu ametoa shukurani hizo leo (Jumapili, Juni 2, 2019) alipokwenda kwenye kanisa Katoliki la Theresia wa Mtoto Yesu, Parokia ya Mnacho kuwasalimia waumini.

Amesema lengo la kuibadilisha shule hiyo kuwa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Lucas Malia ni kuwawezesha watoto wa kike wa Wilaya hiyo kusoma katika mazingira mazuri.

Waziri Mkuu ambaye ameambatana na Mkewe Mary amesema shule hiyo ya bweni itawapunguzia vishawishi watoto wa kike, hivyo kuwawezesha kutimiza malengo yao.

Awali, uongozi wa Parokia hiyo uliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuboresha huduma za jamii zikiwemo za afya, elimu pamoja na miundombinu katika wilaya hiyo.

Naye, Mkuu wa wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilwa amewaomba viongozi wa dini washikamane na wahakikishe wanatatua changamoto ya mmomonyoko wa maadili.

Amesema changamoto ya mmomonyoko wa maadiji katika jamii hususani kwa vijana ni kubwa, hivyo ni jukumu lao kuhakikisha kwamba wanawarejesha kwenye maadili bora.

Kadhalika, Waziri Mkuu amekagua ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Lucas Malia na amesema kwamba ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wake.

Shughuli zinazoendelea katika shule hiyo ni pamoja na ujenzi wa mabweni, vyumba vya madarasa, maabara na nyumba nne za walimu ambazo tayari ujenzi wake umekamilika.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger