Wednesday 29 May 2019

RAIS MAGUFULI ATAKA JUMUIYA ZA KIMATAIFA KUONDOA VIKWAZO DHIDI YA ZIMBABWE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amempongeza Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Emmerson Mnangagwa kwa hatua madhubuti za kufanya mageuzi ya kiuchumi katika nchi hiyo na ametoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kuondoa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Zimbabwe.


Rais Magufuli amesema hayo wakati akitoa hotuba katika Dhifa ya Kitaifa iliyoandaliwa na Rais Mnangagwa kwa heshima yake na kufanyika Ikulu Jijini Harare.

Rais Magufuli amesema katika kipindi kifupi cha tangu Rais Mnangagwa aingie madarakani hali ya uchumi imeanza kuimarika ambapo kwa sasa uchumi wa Zimbabwe unakua kwa wastani wa asilimia 3.5, mwaka ujao unatarajiwa kukua kwa wastani wa asilimia 4.2 na mwaka unaofuata kuongeza hadi wastani wa asilimi 4.4.

Kufuatia hali hiyo ameisihi Jumuiya ya Kimataifa kuondoa vikwazo mbalimbali vilivyowekwa dhidi ya Zimbabwe kwa kuwa vikwazo hivyo vinawaumiza wananchi wa Zimbabwe wakiwemo watoto na wanawake.

Katika hotuba hiyo, Rais Magufuli kwa mara nyingine amewapa pole Rais na wananchi wote wa Zimbabwe kwa kupoteza watu takribani 400 waliofariki dunia katika mafuriko yaliyosababishwa na Kimbunga Idai kilichoikumba Zimbabwe Machi 2019. Amesema Watanzania wanaungana na ndugu zao Wazimbabwe katika majonzi ya kuondokewa na jamaa zao na wanawaombea kwa Mwenyezi Mungu aziweke roho zao mahali pema peponi, Amina.

Kuhusu uhusiano wa Tanzania na Zimbabwe ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Mzee Robert Mugabe, Rais Magufuli amesema Tanzania inatambua na inathamini uhusiano huu wa kihistoria na kidugu na amebainisha kuwa jukumu lililopo sasa ni kuelekeza nguvu nyingi zaidi katika uhusiano na ushirikiano wa kiuchumi utakaoziwezesha Tanzania na Zimbabwe kuongeza biashara na uwekezaji.

Rais Magufuli amebainisha kuwa katika mazungumzo yake ya faragha na Rais Mnangagwa leo mchana wamekubaliana kusimamia ipasavyo makubaliano yaliyopo katika Kamati ya Pamoja ya Kudumu (Joint Permanent Commission – JPC) kwa manufaa ya nchi zote mbili.

“Rais Mnangagwa ujio wangu hapa Zimbabwe ni kuthibitisha kuwa urafiki wetu bado upo imara na sisi Tanzania tumejipanga kuuimarisha zaidi, tunataka tufanye biashara zaidi na nyinyi ndugu zetu wa Zimbabwe ili tukuze uchumi wa nchi zetu na kuongeza kipato cha wananchi wetu” amesisitiza Rais Magufuli.

Kwa upande wake, Rais Mnangagwa amemshukuru Rais Magufuli kwa kukubali mwaliko wake, na amemthibitishia kuwa yeye na wananchi wa Zimbabwe wanatambua kuwa Watanzania ni ndugu zao waliojitolea kwa dhati katika ukombozi wao wakiongozwa na dhamira ya dhati ya Hayati Mwl. Nyerere.

Amemshukuru Rais Magufuli kwa kuwa kiongozi wa kwanza katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kutoa msaada wa chakula, dawa na vifaa vya kujihifadhi wakati Zimbabwe alipokumbwa na mafuriko yaliyosababishwa na Kimbunga Idai mwezi Machi 2019.

Rais Mnangagwa amesema msaada huo uliwagusa Wazimbabwe wengi na kuwakumbusha umuhimu wa kuchukua tahadhari dhidi ya majanga na mabadiliko ya tabia nchi.

Amesisitiza kuwa daima Zimbabwe itabaki kuwa rafiki na ndugu wa kweli wa Tanzania na hivyo amemhakikishia Rais Magufuli kuwa nchi hiyo ipo tayari kukuza zaidi ushirikiano wa kiuchumi kwa kuongeza biashara na uwekezaji pamoja na kushirikiana katika usafiri wa anga.

Amemshukuru Rais Magufuli kwa kumpa mbinu mbalimbali za kiuongozi ikiwemo kuondoa watumishi hewa ambao wamekuwa mzigo mkubwa kwa Serikali na ameahidi kudumisha ushirikiano kati ya chama chake ZANU-PF na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Share:

Bodi ya Ligi Kuu (TPLB): STAND UNITED IMESHUKA DARAJA...KAGERA SUGAR IMEBAKI

Utata uliojitokeza wa timu ipi itaungana na African Lyon kushuka daraja baada ya msimu kumalizika, umehitimishwa rasmi leo baada ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) kutangaza rasmi kuwa Stand United ya Shinyanga imetereka daraja baada ya kumaliza nafasi ya 19 kwenye msimamo wa ligi.

Sintofahamu hiyo iliibuka baada ya msimamo wa mwisho wa ligi uliotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuonyesha kuwa Kagera Sugar ndio inapaswa kushuka daraja ikizidiwa idadi ya mabao ya kufunga na Stand United.

Msimamo huo ulionyesha kuwa timu hizo zote zina idadi sawa ya pointi ambazo ni 44, huku kigezo cha pili cha kuamua mshindi baina yao ambacho ni kutazama utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa pia wakiwa sawa kwa maana ya timu zote mbili kuwa na mabao -11.

Kwa mujibu wa msimamo huo uliotolewa na TFF, Stand iliwekwa juu ya Kagera Sugar kwa kutazama kigezo cha tatu ambacho ni uwingi wa mabao ya kufunga ambapo wao walikuwa na mabao 38 huku Kagera wakiwa nayo 33.

Hata hivyo msimamo huo wa ligi uliotolewa na TFF ulionekana kuwa na makosa kwani kwa mujibu wa matokeo halisi ya timu hizo, Kagera walimaliza wakiwa na utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa -10 huku Stand United wakiwa na -12 na ndio walipaswa kushuka.

Akizungumza jijini leo, Mtendaji Mkuu wa TPLB, Boniface Wambura alisema baada ya bodi na TFF kupitia upya takwimu za ligi, Stand United ndio timu itakayoshuka daraja.

Na Charles Abel - Mwanaspoti
Share:

SERIKALI YATOA TAMKO KWA WATU WENYE VITAMBI TANZANIA


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema uwepo wa vitambi ni mojawapo ya dalili za mtu ananyemelewa na magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza na kuwataka watu wenye vitambi kuzingatia suala la mlo bora.

Naibu Waziri Ulega ametoa kauli hiyo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali kwa niaba ya Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto ambapo amesema si dalili nzuri.

Akizungumza kwenye kikao hicho Naibu Waziri Ulega amesema kuwa "kitambi ni dalili mojawapo ya uzito kupita kiasi hii si dalili njema, hupelekea magonjwa yasiyoambukiza"

Aidha Naibu Waziri Ulega amesema kuwa "katika kupambana na kitambi nikujikinga kupunguza chakula cha wanga, sukari, chumvi, mafuta kwenye chakula, kunywa maji lita 1 na nusu na kupunguza unywaji wa pombe uliopitiliza"

Kwa sasa Bunge linaendelea Bungeni jijini Dodoma ambapo Mawaziri mbalimbali wameendelea kuwasilisha makadirio yao ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/2020
Share:

MUFTI WA TANZANIA ASHIRIKI FUTARI ILIYOANDALIWA NA KIBADA GARDENS KIGAMBONI,ATOA NENO KWA WAGENI WAALIKWA

   Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally na Mh. Ali Davutoglu, Balozi wa Uturuki nchini Tanzania pamoja na baadhi ya wageni wakibadilishana mawazo kabla ya kufuturu.
     Muda wa Kufuturu (Iftar)
Maulid Kitenge (MC) akifurahia jambo pamoja na Mufti, Sheikh Abubakar Zubeir.
Mufti akitoa mawaidha kwa watu mbalimbali waliofika Kibada Gardens kwa ajili ya Iftar maalum  iliyoandaliwa siku hiyo,Mufti amewataka Waislamu waendelee kumcha Mungu na kuendelea kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu,na kwa si kwa wakati huu tu wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani,lakini pia wakati wote.
Sheikh wa msikiti wa Kibada akikabidhiwa baadhi ya vitu kwa ajili ya Futari kwa wakazi wa Kibada.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mr. Ali Davutoglu akipeana mkono na Sheikh wa wilaya ya Kigamboni, Mr. Sharrif Hassan wakati wa Iftar iliyoandaliwa na Kibada Gardens Dar es Salaam. Pili kushoto ni Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir bin Ally
    Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir bin Ally akitoa maneno ya hekima kwa baadhi ya watu waliofika katika Iftar maalum iliyoandaliwa na Kibada Gardens, Kigamboni Dar es salaam.
    Mufti wa Tanzania pamoja na baadhi ya masheikh wa bakwata wakiwasili Kibada Gardens kwa ajili ya Iftar iliyoandaliwa maalum katika mfungo wa Ramadhan unaoendelea.
1.      Kibada Gardens imeandaa Iftar maalum ambayo ilihudhuriwa na Mh. Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally na Mh.  Ali Davutoglu, Balozi wa Uturuki nchini Tanzania.
Share:

Simbachawene Aitaka Serikali Ipunguze Gharama za Umeme

Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene (CCM), amesema gharama za uzalishaji wa umeme kwa sasa ziko juu, hivyo Serikali inatakiwa kuliangalia jambo hilo wakati ikielekea katika uchumi wa kati.

Kauli hiyo ameitoa bungeni leo Jumatano Mei 28, wakati akichangia mjadala wa Wizara ya Nishati kwa mwaka 2019/20.

Aidha, mbunge huyo ambaye amewahi kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, amesema umeme utakuwa na tija kama utaenda katika huduma za kijamii na shughuli za uzalishaji.


Share:

Makonda atangaza vita na Wamachinga wasio na vitambulisho Dar

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema kuanzia June 3 mwaka 2019 ni marufuku kwa Wamachinga wote wasio na vitambulisho kufanya biashara katika maeneo yote jijini Dar.

Ametoa kauli hiyo leo Jumatano Mei 29, 2019 katika mkutano wake na waandishi wa habari kuhusu mwitikio wa wafanyabiashara kuchukua vitambulisho hivyo vilivyotolewa na Rais John Magufuli kwa wakuu wote wa Mikoa nchini.

Makonda amesema Jiji hilo lilipatiwa vitambulisho 175,000 lakini wapo ambao hawajachukua hadi sasa.

Amesema kuwa atafanya msako mkali kuwatafuta wamachinga wote wasio na vitambulisho hivyo


Share:

Serikali Kuajiri Watumishi Wapya 44,800 kwa kipindi cha 2019/20

Watumishi 44,800 wataajiriwa katika taasisi za Serikali kwa kipindi cha 2019/20

Hayo yameelezwa na naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Dk Mary Mwanjelwa jana Jumanne Mei 28, 2019. na kubainisha kuwa ajira hizo zitawalenga Watanzania wenye sifa.

Dk Mwanjelwa alisema kuwa si Serikali pekee ndio inayotakiwa kutoa ajira, hata watu binafsi wanaweza kutoa ajira kwa vijana.

Naibu Waziri huyo alikuwa akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Aida Khenan aliyehoji kama kuna utaratibu wowote wa kuajiri watu waliohitimu vyuo na kukidhi vigezo vya kuajiriwa.

Katika swali la nyongeza mbunge huyo amehoji kwa nini Serikali inaendelea kuweka vigezo vya uzoefu kazini wakati inajua hakuna vijana wenye uzoefu.

Katika majibu yake, Dk Mwanjelwa alisema duniani kote Serikali si mwajiri pekee, akitolea mfano waajiri wengine ambao ni sekta binafsi, mashirika, asasi za kiraia na maeneo mengine.

Kuhusu uzoefu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama alisema wameondoa uzoefu badala yake Serikali imeanzisha kozi maalum kwa wahitimu ambazo husaidia kuwapa ujuzi.


Share:

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH ....Anauwezo wa wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Mohamedi Buruhani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Mohamedi Buruhani  Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036



Share:

WAANDISHI WA HABARI IRINGA WAMKALIA KOONI MKUU WA MKOA...WAMTAKA AOMBE RADHI

Waandishi wa Habari Mkoa wa Iringa wamempa siku saba mkuu wa Mkoa huo, Ally Hapi kuwaomba radhi baada ya kuwataka nao kuwa na vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo.

Hapi alitoa kauli hiyo juzi Jumatatu Mei 27, 2019 wakati akizungumza na watendaji wa Serikali kuhusu ugawaji wa vitambulisho vya wafanyabiashara.

Aliwataja waandishi wa habari kama wafanyabiashara na vibarua wasio rasmi, huku akianisha makundi 53 yanayostahili kupata vitambulisho hivyo.

“Wafanyabiashara ni wengi kuna wapiga debe, wauza nyanya, mchicha, wachoma mahindi na hata waandishi wa habari na wapiga picha wote wanatakiwa kuwa na vitambulisho ili kuchangia kodi kutokana na kazi wanazofanya,” amesema Hapi.

Akizungumza jana  Jumanne Mei 28, 2019 mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Iringa, Frank Leornald amesema kauli ya Hapi inadhalilisha taaluma ya habari.

Leornald amesema waandishi wa habari mkoani humo wamefanya majadiliano na kuazimia mambo sita watakayoyawasilisha katika ofisi ya mkuu huyo wa Mkoa, na kutaka majibu ya haraka.

“Tumesikitishwa kuwekwa katika kundi moja linalolinganisha taaluma ya habari na wafanyabiashara. Katika maazimio hayo sita tumemuomba Hapi kutoa tafsiri rasmi anayoijua yeye kuhusu waandishi rasmi na wasio rasmi.”

“Tunaamini taaluma ya habari ni kama taaluma nyingine za sheria, udaktari na ualimu hivyo kuingiza wanahabari katika kundi la wafanyabiashara wanaotakiwa kuwa na hivyo vitambulisho ni kuidhalilisha taaluma yetu,” amesema Leornald.

Amebainisha kuwa Hapi anapaswa kuomba radhi kutokana na kauli yake hiyo.

“Mengine tutayatolea uamuzi baada ya Hapi kujibu barua yetu tuliyomuandikia,” amesema Leornald.
Share:

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Yapendekeza TANESCO Igawanywe

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imependekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kugawanywa na kuwa mashirika mawili ili kuepuka hasara.

Hayo yameelezwa  jana Jumanne Mei 28, 2019 na msemaji wa kambi hiyo wa Wizara ya Nishati, John Mnyika wakati akiwasilisha  maoni ya wapinzani bungeni.

Alisema kwa kipindi kirefu Tanesco inajiendesha kwa hasara, akitolea mfano kwamba  tangu utawala wa  Serikali ya Awamu ya Nne ilikuwa ikipata hasara ya Sh124 bilioni.

Alibainisha kuwa  takwimu zinaonyesha baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia madarakani, shirika hilo linapata hasara kubwa zaidi, kwamba  hadi  2017 ilipata hasara ya Sh346 bilioni sawa na ongezeko la Sh122 bilioni.


Share:

Mbwana Samatta Akutana Na Kufanya Mazungumzo Na Msemaji Mkuu Wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi

SERIKALI imesema itaendelea kumsaidia kwa hali na mali Nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, anayechezea Klabu ya Genk ya Nchini Ubelgiji Mbwana Samatta ili kuhakikisha kuwa anafungua milango ya uwekezaji na kuiweka juu ramani ya Soka la Tanzania katika anga la kimataifa.
 
Akizungumza jana Jumanne (Mei 28, 2019) Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam na Nahodha huyo waTaifa Stars, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema Samatta ameonyesha njia iliyoshindwa kufikiwa na wachezaji wengi wa miaka ya nyuma waliojaribu kucheza Soka la kulipwa katika vilabu mbalimbali vya Nchi za Nje hususani Bara la Ulaya.
 
Dkt. Abbasi alisema Serikali ilimteua Sammatta kuwa Balozi wake wa Utalii kutokana na sifa kubwa zilizoletwa na mchezaji huyo nje ya mipaka ya Tanzania kwa kuwa Serikali ina Imani naye kubwa katika kufungua milango ya fursa za uwekezaji hususani katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano hapa nchini. 
 
“Mbwana Samatta ameonyesha njia ambayo ilikuwa ndoto iliyoshindwa kutimizwa na wachezaji wengi wa zamani, hatua hii aliyofikia ni kubwa na imetokana na sifa kubwa ya nidhamu na kipaji cha mchezo huu hili ni funzo kwa wachezaji wetu chipukizi” alisema Dkt. Abbasi.
 
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema kwa sasa yapo mambo makubwa na mazuri hususani vivutio vya sekta ya utalii, hivyo kupitia nafasi yake ya Ubalozi Serikali itatoa msaada wowote unaohitajiwa na mchezaji huyo ili kuhakikisha kuwa vivutio vya Tanzania vinabainishwa na hivyo kutangaza mambo mazuri ya Tanzania.
 
Aidha Dkt. Abbasi alisema Ofisi yake imeandaa mikakati mbalimbali ya mawasiliano ya kitaifa katika kuisema nchi katika maeneo mbalimbali hivyo kumtaka mchezaji huyo kutumia majukwaa hayo kwa ajili ya kuona namna bora ya kutumia fursa hizo ili kuitangaza Tanzania nje ya mipaka yake.
 
Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alimtaka mchezaji huyo kuwasiliana naye iwapo kutakuwepo na changamoto yoyote anayoweza kuipata katika kutekeleza majukumu yake ya nafasi ya Ubalozi kwani kwa sasa Serikali ya Awamu ya Tano imefungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua katika kuwaletea maendeleo wananchi wake.
 
Kwa upande wake, Nahodha huyo wa Taifa Stars, Mbwana Samatta alisema akiwa nchini Ubelgiji tayari amefanya juhudi kubwa katika kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini, ambapo mwanzoni mwa mwezi ujao madaktari 5 wa timu hiyo wanatarajia kuja nchini kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali ya utalii nchini.
 
Samatta alisema raia wengi wa kigeni wana shauku ya kutembelea Tanzania kutokana kusikia na kuona uzuri wa vivutio mbalimbali vya utalii ikiwemo Wanyama, hivyo akiwa Balozi wa Utalii afanya kila liwezekanalo  kukaa karibu na viongozi na wachezaji wa klabu yake ya KRC Genk kuwaeleza uzuri wa Tanzania ili na wao waonesha nia ya kuitembelea Tanzania.
 
“Wachezaji wengi hususani wale wa kiafrika waliopo nje hususani Bara la Ulaya wanaipenda sana Tanzania, na hi inatokana na sifa tuliyonayo, na hivyo kwa kutumia nafasi yangu ya Ubalozi nitaendelea kushawishi waitembelee Tanzania” alisema Samatta.
 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Samatta Tours, Hamis Waziri aliishukuru Serikali kutokana na jitihada mbalimbali inazofanya kwa ajili ya kuhamasisha sekta ya utalii nchini na kusema taasisi hiyo itakuwa tayari kutangaza matukio mbalimbali kwa ajili ya kulitangaza jina la Tanzania.


Share:

Waziri Mkuu Ataka Watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu Waongeze Kasi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu waongeze kasi ili utendaji kazi Serikalini uweze kufikia hatua nzuri.

“Ninawashukuru watumishi wote kwa ushirikiano mnaotupatia mimi pamoja na mawaziri wenzangu, makatibu wakuu wote watatu, wakurugenzi mbalimbali na wakuu wa vitengo. Tunatakiwa tuongeze kasi ili tufikie hatua nzuri ya utendaji kazi Serikalini,” alisema.

Alitoa kauli hiyo jana usiku (Jumanne, Mei 28, 2019) alipokutana na viongozi na watumishi wa ofisi yake na kufuturu nao pamoja kwenye makazi yake jijini Dodoma.

Alisema utendaji kazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu ni mgumu kwa sababu unahusika na usimamizi wa shughuli za Serikali nzima na watendaji wote wa Serikali. “Sekta yetu ni ngumu kwa sababu sisi ni wasimamizi wa Serikali na watendaji wote wa Serikali. Tuna wajibu wa kuwaunganisha watendaji wa wizara zote serikalini,” alisema.

“Sisi sote ni watumishi wa umma, kwa hiyo mchango wenu una maana kubwa na unachangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya Serikali nzima. Ninawapongeza kwa utumishi mwema na wenye uadilifu,” alisema Waziri Mkuu.

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa kufuturu pamoja, Waziri Mkuu alisema mwezi wa Ramadhan ni muhimu kwa Waislamu wote kwa sababu ni kipindi ambacho wanakamilisha nguzo kuu muhimu ya uislamu.

“Tukio la Ramadhan linatoa ujumbe mzito kwetu, ni wakati ambao tunatubu kwa maovu tuliyoyatenda. Wakati huu, inasisitizwa tuweze kushikamana, tujenge tabia ya umoja na pia tuweze kuvumiliana,” alisisitiza.

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na watumishi hao, Waziri wa Nchi (OWM-SBAU), Bi. Jenista Mhagama alisema uamuzi wake wa kuwaalika watumishi na kufuturu nao ni dalili njema kuwa anathamini kazi zinazofanywa na watumishi walio chini yake.

“Ni viongozi wachache sana wanaowakumbuka watumishi walio chini yao. Tunakushukuru kwa kututhamini na tunaahidi kukupa ushirikiano wa dhati unaoenda sambamba na utendaji kazi uliotukuka,” alisema.

Akitoa shukrani kwa mwaliko huo, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Waziri Mkuu na Bunge, Bibi Maimuna Tarishi alisema anatoa shukrani kwa niaba ya watumishi wote na kuahidi kufanya kazi kwa bidii.

“Tunaahidi kuongeza juhudi zaidi kwenye kazi zetu ili tuweze kuwa watu wa kupigiwa mfano na wengine,” alisema.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Waziri aagiza mkandarasi kuwekwa korokoroni saa 24

Na Amiri kilagalila-Njombe
Waziri wa maji Prof. Makame Mbarawa ameagiza jeshi la polisi kumshikilia kwa saa 24 Mkandarasi wa kampuni ya Water and Earth Works Ltd (BWE ) Emmanuel Mzena anayesimamia mradi wa maji bwawani mjini Makambako mkoani Njombe kutokana na kushindwa kutekeleza mradi huo kwa wakati.

Waziri Mbarawa alifikia uamuzi huo jana mjini Makambako wakati alipotembelea mradi huo.

“Nataka kesho watu wako waje kwenye site na wewe utakaa ndani leo mpaka kesho kwa masaa 24, kama watu wako hawata kuja tutakuingiza tena hivyo hivyo mpaka utaleta wafanya kazi ujinga sitaki kuusikia, na ninyi makandarasi mpaka muwekwe ndani ndio mfanye kazi,wananchi wote hawa watoto wadogo wanaharisha ninyi mmepewa pesa za serikali hamfanyi kazi mnajifanya mnajua sheria kumbe nyie ndio wezi wa serikali”alisema Mbarawa 

Aidha waziri huyo amemtaka mkurugenzi wa mamlaka ya maji mjini makambako kusimamia mradi huo kwa kuhakikisha tanki la maji la mradi huo linajazwa maji na akishindwa naye atawekwa ndani.

Awali akizungumza kuhusiana na mradi huo kushindwa kukamilika kwa wakati na kushindwa kuendelea na kazi katika mradi huo mkandarasi huyo Emmanuel Mzena amesema wameshindwa kuendelea na kazi  kutokana na malipo yao kucheleweshwa.

“Ni kwamba tumesimama kwasababu tulifanya kazi lakini tumechelewa kulipwa na certificate ya mwisho tulilipwa mwezi wa 9,lakini mkataba unasema mkandarasi akiwa anaendelea na kazi anaendelea kulipwa”alisema Mzena

Huseni Nyemba ni mkurugenzi wa mamlaka ya maji mjini makambako amesema kuwa kutokana na agizo la waziri tatizo hilo linafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo licha ya kuwa mradi huo unasimamiwa na mamlaka ya maji safi na usafi wa wa mazingira Iringa (ILUWASA).

“Huu mradi ulikuwa kiu yetu lakini wananchi wanatakiwa waelewe mradi ule walioingia mkataba ni mamlaka ya maji mkoa wa Iringa na wenyewe ndio wapo kisheria na kiutaratibu wa kimkataba sisi mamlaka ya maji Makambako  ni kama wanufaikaji baada ya mradi kukamilika ,nashkuru leo waziri alipotoa maagizo ni kama ametupatia ufunguo”alisema Mkurugenzi

Mradi wa huo wa maji Bwawani ulianza mwaka 2017 na ulitakiwa kukamilika mwezi wa sita mwaka 2018 lakini mpaka sasa haujakamilika.


Share:

NACTE Yasitisha Udahili Kozi Ya Hudumu Ya Afya Ngazi Ya Jamii Kwa Mwaka Wa Masomo 2019/2020

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE)limetangaza kusitisha udahili wa wanafunzi wapya wa program ya Huduma ya Afya Ngazi ya Jamii(Community Health) kwa mwaka wa masomo 2019/2020 hadi hapo itakapotangaza tena.

Akizungumza mbele ya wanahabari Jijini Dodoma  janas Mkurugenzi wa uzingativu, ufuatiliaji na Tathmini wa NACTE Jofrey Oleke, amesema maombi ya udahili kwa waombaji wapya wa Astashahada na Stashahada kwa mwaka wa masomo 2019/2020, umesitishwa hadi hapo baraza litakapotangaza maamuzi mengine.

Kufutwa kwa udahili huo kumetokana na maelekezo yaliyotolewa na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kwamba kwa mwaka huu wa masomo hakutakuwa na kozi hizo.

Kuhusu kusitishwa kwa udahili, amesema baraza limepokea maagizo kutoka wizara ya afya ambao ndio wanaosimamia kozi zote za afya, kuwa katika mwaka huu wa masoma hakutakuwa na udahili katika ngazi hiyo afya ya jamii nasi tunatekeleza.

“Baraza linavitaarifu vyuo na umma kwamba udahili wa wanafunzi katika programu ya Huduma ya afya Ngazi ya Jamii umesitishwa hadi hapo itakapotangazwa tena”,amesema.

Pia baraza limetangaza kufunguliwa kwa udahili mpya kwa ngazi za Astashahada na stashahada kwa kozi zote isipokuwa kwa kozi za ualimu na utaendelea mpaka tarehe 2 mwezi wa tisa mwaka huu kwa vyuo vyote vinavyotoa mafunzo katika ngazi hizo.

Amefafanua kuwa kwa waombaji wa programu za Afya katika vyuo vya Serikali watatakiwa ama kuomba moja kwa moja kupitia vyuoni ambapo vyuo vitasawasajili kupitia baraza la chuo au wanaweza kuomba kupitia tovuti ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (www.nacte.go.tz) kubonyeza kwenye ‘apply online'(SAVS).

Kuhusu waombaji wa programu za Afya kwenye vyuo visivyo vya Serikali na waombaji wa programu nyingine zote wanatakiwa kuomba moja kwa moja kwenye vyuo husika.

“Hivyo vyuo vitapokea maombi na kufanya uchaguzi wa wanafunzi wenye sifa na kisha wawasilishe NACTE majina ya waliochaguliwa kwa ajili ya uhakiki kabla ya kuyatangaza, vyuo vinaelekezwa kuzingatia utaratibu wa udahili kama ulivyotolewa na baraza katika mwaka wa masomo 2019/2020,”amesema.

Amewataka wahitimu wote wa Elimu ya Sekondari na vyuo wenye sifa za kujiunga na kozi za Astashahada na Stashahada, kufanya maombi kwa umakini ili kuweza kupata nafasi ya kujiunga programu wanazozipenda na ambazo wanatimiza vigezo/sifa za kujiunga nazo kwa mwaka 2019/2020.

Pia baraza limewashauri waombaji na wazazi kuhakikisha kuwa wanaomba kwenye vyuo vinavyokidhi ubora ambavyo vimeorodheshwa kwenye kitabu cha mwongozo wa udahili kwa mwaka wa masomo mwaka 2019/2020 .


Share:

Taarifa Kuhusu Ushiriki Wa Tanzania Kwenye Mkutano Wa 109 Wa Baraza La Mawaziri Wa Nchi Za Afrika, Karibbean, Na Pasifiki (ACP)

Ndugu Waandishi wa Habari,
1. Nilipata heshima ya kuongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Mkutano wa 109 wa Baraza la Mawaziri wa nchi za Afrika, Karibiani, na Pasifiki (ACP) uliofanyika Brussels, Ubelgiji kuanzia tarahe 20 hadi 22 Mei 2019. Mkutano huu, ulifuatiwa na Mkutano wa 44 wa pamoja wa Mawaziri wa nchi za ACP na wenzetu wa Umoja wa Ulaya (EU) ambao ulifanyika mnamo tarehe 23 na 24 Mei 2019.

2. Katika mkutano huu, upande wa Tanzania niliongozana na Watendaji Waandamizi kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Fedha na Mipango, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Pia, Watalaam kutoka Ofisi ya Ubalozi wetu wa Tanzania Brussels, walishiriki mikutano hii.

3. Aidha, katika mikutano yote miwili, majadiliano yetu yalijikita katika maeneo makuu matatu. Mosi, ni kupitia na kutathimini utekelezaji wa makubaliano na mipango mbalimbali tuliyonayo ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Pili, kuainisha, kujadili, na kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ushirikiano ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Tatu, kutoa muongozo juu ya mustakabali wa ushirikiano tunaotarajia uwepo ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU katika kipindi kijacho.

 4. Kwa upande wa agenda ya kwanza, tulipitia utekelezaji wa makubaliano ya programu mbalimbali ndani ya nchi za ACP na baina ya nchi za ACP na EU. Programu hizo ni pamoja na zile zinazohusu masuala ya ubia wa kimaendeleo, biashara, masoko, kilimo, elimu, maendeleo ya sekta binafsi, teknolojia, mifumo ya kodi, uhifadhi wa mazingira, hifadhi ya bahari, na masuala mengine yanayofanana na hayo. Kwa ujumla tulikubaliana kuwa programu hizi ni muhimu katika kuchochea kasi ya maendeleo ya nchi zetu na zikaendelea kutekelezwa kwa kasi inayostahili, mgawanyo ulio sawa na kwa kuzingatia mahitaji ya nchi husika.

5. Kwa mfano, katika eneo la kilimo, Tanzania ilitoa hoja ambayo baada ya majadiliano ya kina ilikubalika kuongeza mazao ya korosho, pamba, na kahawa katika orodha ya mazao yaliyopo katika mpango wa mwaka 2019 wa utekelezaji wa programu ya ACP ya kuendeleza mnyororo wa thamani katika mazao ya kilimo. Mpango huu unafadhiliwa na EU na umetengewa kiasi cha Euro milioni 125. Katika zao la korosho, nchi wanachama wa ACP iliisifu na kuipongeza Tanzania kwa uamuzi wa kishujaa uliochukuliwa na Serikali chini ya uongozi thabiti wa Mhe. Rais Magufuli kwa kuzuia mwendelezo wa mdororo wa bei ya korosho na hatua za makusudi zinazoendelea katika kuongeza mnyororo wa thamani wa zao hilo.

6. Katika kuimarisha sekta binafsi, ujumbe wa Tanzania uliuomba Umoja wa Ulaya kupitia mkakati wa kusaidia sekta binafsi (ACP Private Sector Development Strategy), kuangalia uwezekano wa kuja na mfumo rafiki kwa nchi za ACP, na Tanzania ikiwemo, ambao utawezesha sekta binafsi ya nchi hizo kunufaika. Katika mkutadha huo, ujumbe wa Tanzania uliiomba Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB), inayosimamia mpango huo, kuanza majadiliano na serikali na kukubaliana namna ya kusaidia sekta binafsi katika utoaji wa mikopo nafuu ya maendeleo (development finance) kwa ajili ya kuchochea uzalishaji na 3 kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Umoja wa Ulaya kupitia mpango wake wa kuwezesha ufanikishaji wa utekelezaji miradi ya kibiashara na sekta binafsi imetenga kiasi cha Euro bilioni 1.1 kwa kipindi cha mwaka 2014 hadi 2020.

7. Wakati wa mkutano huu, ujumbe wa Tanzania ulieleza kwa kina hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano katika kujenga uchumi wa viwanda kwa lengo la kufikia uchumi wa kati. Miongoni mwa hatua tulizozieleza ni pamoja na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama vile ujenzi wa reli ya kisasa (SGR), mradi wa uzalishaji wa umeme wa mto Rufiji, ununuzi wa ndege na kufufuliwa kwa ATCL, ujenzi wa barabara, kupanuliwa kwa bandari, viwanja vya ndege na miradi mingine. Tulitumia nafasi hiyo kuzihakikishia nchi za ACP na Umoja wa Ulaya juu ya uwepo wa mazingira rafiki ya uwekezaji na biashara nchini Tanzania na kuwajulisha kuwa Serikali kupitia mwongozo wa BLUEPRINT inatekeleza mikakati ya kuboresha zaidi mazingira ya uwekezaji na biashara. Hatimaye, tuliwaomba wadau wetu wa maendeleo ndani ya ACP na Umoja wa Ulaya kuunga mkono juhudi hizi madhubuti za Serikali na kuhimiza raia wa nchi zao kuja kuwekeza nchini.

8. Katika agenda ya kujadili changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ushirikiano wetu, tulibainisha na kujadiliana na wenzetu wa Umoja wa Ulaya juu ya changamoto hizo na umuhimu wa kupata ufumbuzi wake. Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na kasi ndogo ya utekelezaji wa baadhi ya programu za maendeleo, kiwango kidogo cha biashara baina ya nchi za ACP, kuendelea kuibuka kwa vikwazo vipya vya biashara visivyo vya kiforodha kwa bidhaa za ACP katika soko la Ulaya, sintofahamu inayoendelea baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya katika kusainiwa na kutekelezwa kwa Mikataba ya Ubia wa Kiuchumi (Economic Partnership Agreements – EPAs), na kuwepo kwa vikwazo kwa baadhi ya nchi wanachamaa wa ACP na kuwepo kwa maamuzi 4 yasiyozingatia misingi ya uhuru wa nchi (sovereignty), usawa (equal partnership), na kuheshimiana. Nchi za ACP, ikiwemo Tanzania, zilisisitiza changamoto hizi zipatiwe ufumbuzi haraka kwa kila upande unaohusika na tulikubaliana kuwa katika ushirikiano wetu ni muhimu kila upande ukaheshimu kanuni za ushirikiano, sheria na tamaduni za nchi husika. Kwenye hili, Tanzania ikiungwa mkono na nchi nyingine za ACP haja na umuhimu wa kuzingatia na kuheshimu matakwa ya Ibara ya 12 ya mkataba wa ubia wa sasa unaojulikana kama Cotonou Partnership Agreement. Ibara hiyo inazuia upande wowote kuchukua uamuzi wenye madhara kwa upande mwingine bila kuingia kwenye mashauriano ya kina na upande huo.

9. Katika majadiliano yetu, juu ya mstakabali wa ubia mpya baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya baada ya ubia wa sasa kufikia ukomo wake ifikapo tarehe 29 Februari 2020, tulipokea taarifa ya majadiliano yanayoendelea. Tulisisitiza mambo makuu matatu. Kwanza, mkataba wa ubia mpya uzingatie zaidi kuziinua nchi za ACP kiuchumi, maendeleo, na biashara. Pili, tulisisitiza umuhimu wa mkataba wa ubia mpya kutohusianishwa moja kwa moja na mikataba mingine ambayo majadiliano yake bado yanaendelea baina ya nchi za ACP na Umoja wa Ulaya ikiwemo mkataba wa EPA na mikataba mingine. Tatu, kwa kuzingatia kuwa tunahitahi majadiliano ya kina na yanayozingatia maslahi mapana ya nchi za ACP, ikiwemo Tanzania, tulitoa fursa kwa majadiliano haya kuendelea hata ikibidi kwa muda wa nyongeza ili kuwezesha zoezi hilo muhimu la majadiliano kwa mstakabali wa ushirikiano wetu na EU kwa miaka mingine ijayo kukamilika kwa ufanisi unaostahiki.

10.Katika hatua ya kuimarisha zaidi ushirikiano na nchi mbalimbali katika ngazi ya kitaifa, kikanda, na kimataifa, hususan kwenye masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, tulipata pia fursa ya kuonana na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa nchi 5 zingine zilizoshiriki mkutano huo. Viongozi tulioonana nao na kufanya mazungumzo ni pamoja na kiongozi wa ujumbe wa Ethiopia, Eswatini, Chadi, Zambia, Equatorial Guinea, Commoro, na Namibia. Pia, tulipata nafasi ya kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi ya Romania na Umoja wa Ulaya. Mazungumzo haya kwa ujumla yametupa uelewa wa pamoja baina ya nchi yetu na nchi hizo kwenye agenda mbalimbali za kitaifa, kikanda, na kimataifa na pia kuimarisha zaidi ushirikiano wenye maslahi baina ya Tanzania na nchi hizo.

11.Ndugu Waandishi wa Habari, kwa ujumla ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huu ulikuwa muhimu na wenye manufaa. Ujumbe wa Tanzania ulitoa mchango mkubwa na kwa hakika hoja nyingi za Tanzania zilikubaliwa na kuwa sehemu ya maamuzi na maazimio ya mkutano. Tutaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa maamuzi na maazimio hayo.

 Asanteni kwa kunisikiliza. NAIBU WAZIRI, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI 28 MEI 2019, DODOMA


Share:

Serikali ya Poland Yaonyesha Nia ya kuisaidia Sekta ya Afya Nchini

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameishukuru Serikali ya Poland kwa kuonyesha nia ya dhati ya kuisadia Tanzania katika Sekta ya Afya Nchini ili kuboresha na kupunguza changamoto katika Sekta hiyo.

Mhe. Jafo ameyasema hayo wakati wa kikao na wadau wa maendeleo katika Sekta ya Afya kutoka Poland cha kujadili masuala mbalimbali yanayouhusiana na Afya na jinsi Nchi hiyo inavyoweza kusaidia kuimarisha na kuboresha Sekta ya Afya nchini.

Mhe. Jafo ameishukuru Serikali ya Poland kwa ushirikiano wanatoa katika Miradi mbalimbali ya maendeleo na kutambua umuhimu wa sekta ya afya nchini kwa kuwa bila kuimarisha Sekta ya afya hakutakuwa na maendeleo na kushindwa kufikia uchumi wa kati.

“Sekta ya afya ni muhimu kwa jamii, jamii isipokuwa na afya bora hakutakuwa na maendeleo, hivyo ni vyema Serikali ikajikita kuwekeza katika Sekta ya afya kwa kuhakikisha inajenga miundombinu bora, uwepo wa vifaa na vifaa tiba ili kuboresha huduma za afya nchini” Amesema Mhe. Jafo

Amesema kuwa hatuwezi kufikia uchumi wa kati endapo watu wetu hawatakuwa na afya bora, ili watu wafanyekazi kwa bidi waweze kuzalisha na kulipa kodi inavyotakiwa wanatakiwa kuwa na afya bora hivyo tunawakaribisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya kuwekeza katika Sekta hiyo.

Mhe. Jafo amendelea kuishukuru Serikali ya Poland kwa kuonyesha nia ya kuisaidia Serikali mkopo wenye gharama nafuu utakaosaidia kuimarisha na kuboresha sekta ya Afya nchini lengo likiwa ni kupunguza changamoto mbalimbali katika sekta hiyo.

Ameiomba Serikali ya Poland kujikita zaidi katika kusaidia kwenye kuimarisha huduma za msingi hasa ujenzi wa Vituo vya afya na upatikanaji wa vifaa na vifaa tiba kwa kuwa ndipo kwenye changamoto kubwa katika suala zima la utoaji wa huduma na itasaidia kupunguza vifo kwa jamii
Mhe. Jafo amefafanua kuwa katika eneo la Sekta ya Afya Serikali itapata fursa ya kusaidiwa ujenzi wa Vituo vya afya, ambavyo vitakuwa vya mfano kwa kuwa na vifaa vyake na kuwa na nyumba zaidi ya nne za madaktari na hivyo kupunguza changamoto zilizopo.

Mhe. Jafo amelishukuru shirika la Light For Africa kwa kuunganisha nchi ya Poland na Tanzania ambao wameonyesha nia ya dhati katika kusaidia masuala ya Sekta ya Afya nchini jambo ambalo litasaidia kuleta maendeleo kwa jamii

Aidha Wadau hao watatembelea, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Hospitali ya Mirembe, Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Hospitali ya Amana na Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe kwa lengo la kuangalia ni namna Tanzania inavyotoa huduma za afya na kuangalia maeneo ambayo wanaweza kusaidia katika kutumia fursa walizonazo.


Share:

Mazungumzo ya kibiashara kati ya Marekani na China yavunjika

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Lu Kang amesema kuwa, mazungumzo ya kibiashara kati ya Washington na Beijing yamevunjika.

Kang ameyasema hayo katika kikao na waandishi wa habari mjini Beijing ambapo ameongeza kwamba siasa za kimabavu na mashinikizo yasiyo ya kimantiki ya Marekani dhidi ya China, ndio sababu ya kuvunjika kwa mazungumzo hayo. 

Amesisitiza kwamba, mazungumzo ya kibiashara ya nchi mbili yatafikia natija pale tu maslahi ya pande hizo yatakapozingatiwa sambamba na kuwepo hali ya kuheshimiana kati ya Washington na Beijing. 

Ameongeza kwamba daima China imekuwa ikisisitizia udharura wa kutatuliwa tofauti zote za nchi mbalimbali kupitia njia ya mazungumzo chanya, lakini katika safari yake nchini Japan Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa nchi yake haipo tayari kufikiwa makubaliano ya kibiashara na Beijing.
 
Hivi karibuni, Marekani ilizipandishia ushuru wa forodha wa asilimia 10, yaani sawa na kiasi cha Dola bilioni 200 bidhaa za China zinazoingizwa nchini Marekani kama ambavyo pia ilitangaza kuwa inafikiria kupandisha ushuru mwingine wa asilimia 25 sawa na kiasi cha Dola bilioni 325 bidhaa za nchi hiyo ya Asia. 

Kufuatia hatua hiyo, serikali ya China nayo ilizipandishia bidhaa za Marekani ushuru wa dola bilioni 60, sawa na asilimia 10 hadi 25. 

Mgogoro wa kibiashara kati ya China na Marekani ulianza tangu mwezi Machi mwaka jana.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger