Sunday 14 May 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 14 2017

Share:

TCRA yawatahadharisha watumiaji wa kompyuta juu ya shambulio la Kirusi Kiitwacho WANNACRY kwenye kompyuta

Shambulizi la kihalifu mitandaoni lililotendeka kupitia vifaa vinavyoaminika kuibwa kutoka kitengo cha ujasusi nchini Marekani NSA limeathiri mashirika tofauti duniani.

Kampuni ya kulinda uhalifu wa mitandao Avast, imesema kuwa imeona kesi 75,000 za programu zinazotumika kufanya uhalifu mtandaoni inayojulikana kama 'WannaCry' duniani.

Kuna ripoti za maambukizi katika mataifa 99 ikiwemo Urusi.
Kati ya mashirika yalioathirika zaidi ni shirika la huduma za afya nchini Uingereza na Uskochi.

Programu hiyo ilisambaa kwa kasi siku ya Ijumaa ambapo ilitaka malipo ya dola 300 ili kufungua faili ilizokuwa imeziteka nyara katika kompyuta.Siku nzima, mataifa ya Ulaya yaliripoti maambukizi hayo.
==> Hii ni Tahadhari Iliyotolewa  na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA  kuhusu Kirusi hicho



Advertisement
==
Share:

Wednesday 10 May 2017

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UDAHILI WA WANAFUNZI WA ASTASHAHADA NA STASHADA KATIKA PROGRAMU MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2017/2018


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UDAHILI WA WANAFUNZI WA ASTASHAHADA NA STASHADA KATIKA PROGRAMU MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2017/2018

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ni chombo kilichoanzishwa kwa sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, Sura 129, ili kusimamia na kuratibu utoaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini. Sheria hii inazitaka Taasisi zote zinazotoa elimu ya ufundi kusajiliwa kabla ya kuanza kuendesha mafunzo yoyote. Baraza pia huidhinisha mitaala kabla haijaanza kutumika. Hivyo taasisi zote haziruhusiwi kuanza kutoa mafunzo yoyote bila kibali maalumu kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Baraza linapenda kuwataarifu wadau wa sekta ya Mafunzo ya Ufundi na Umma kwa ujumla kuwa udahili na uchaguzi wa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya Astashahada na Stashahada mbalimbali yanayotolewa na vyuo vyote hapa nchini, utafanyika moja kwa moja vyuoni, isipokuwa kozi za afya na ualimu zinazotolewa na  vyuo vya Serikali tu. Hivyo maombi yote ya nafasi za masomo yatumwe kwenye chuo husika.

Udahili wa kozi za Afya na Ualimu katika vyuo vya Serikali  utaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; na Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia kwa kushirikiana na Baraza (NACTE). Hivyo maombi ya Udahili kwa kozi za Afya na Ualimu kwa vyuo vya serikali tu yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz) au kupitia vyuo husika vya Afya na Ualimu ambavyo vitashughulikia maombi hayo na kufanya udahili kwa njia ya mtandao kupitia ‘Institutional Panel’ zao.

Aidha vyuo vyote vitatangaza au kuwafahamisha moja kwa moja waombaji majina ya watakaochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali; na wale wa kozi za Afya na Ualimu watatangazwa na Wizara husika na kupitia tovuti ya NACTE.

Baraza linapenda pia kuwafahamisha kuwa Vyuo vitaanza kupokea maombi ya udahili wa wanafunzi kuanzia tarehe 15 Mei, 2017 hadi tarehe 20 Agosti, 2017. Majina ya waliochaguliwa yatatangazwa tarehe 14 Septemba, 2017. Masomo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe 25 Septemba, 2017.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE: 10/05/2017
Share:

ADMISSION OF STUDENTS FOR VARIOUS CERTIFICATE AND DIPLOMA PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2017/2018

THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION

(NACTE)
PUBLIC NOTICE

ADMISSION OF STUDENTS FOR VARIOUS CERTIFICATE AND DIPLOMA PROGRAMMES FOR ACADEMIC YEAR 2017/2018

The National Council for Technical Education (NACTE) is a statutory body established under the National Council for Technical Education Act, Cap. 129, to oversee and coordinate the provision of technical education and training in Tanzania.  Under the establishing Act, in order to attain and maintain the status of a training provider, all institutions are required to be registered, accredited and have their curricula approved by the Council. Institutions are not allowed to admit students and start offering any programme without the approval of the Council.

The Council wishes to inform all technical education stakeholders and the general public that, admission and selection of students for various Certificate and Diploma Programmes offered by Technical Institutions, Universities and their constituent Colleges shall be conducted by Technical Institutions and Universities themselves.

Kindly be informed that, all applications for admissions should be submitted to respective technical Institutions or Universities except for public institutions offering health & allied sciences; and teacher education courses.

Admission into public institutions offering health & allied sciences, and teacher education courses shall be coordinated by the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly & Children; and Ministry of Education, Science & Technology respectively in collaboration with NACTE. In that respect, all applications for admission into Certificate and Diploma programmes for health & allied sciences; and teacher education programmes delivered by public health & allied sciences schools, and public Teacher Training Colleges should be made online via NACTE website (www.nacte.go.tz) or through the respective schools and colleges that will submit received applications for admission through their respective Institutional Panel.

The Council wishes also to inform that, publication of selected students will be made by the respective Technical Institutions or Universities and selected students for health & allied sciences and teacher education programmes will be made public through NACTE website and respective Ministry’s websites.

The Council further wishes to inform that, applications for admission will be received as described above from 15th May, 2017 to 20th August, 2017. Publication of selected students for various Certificate and Diploma programmes will be made on 14th September, 2017. Studies for academic year 2017/2018 will commence from 25th September, 2017.

Issued by:
OFFICE OF THE EXECUTIVE SECRETARY
NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION (NACTE)
DATED: 10TH MAY, 2017
Share:

NACTE : Udahili na uchaguzi 2017/18 wa Astashahada na Stashahada kutafanyika moja kwa moja vyuoni

Baraza linapenda kuwataarifu wadau wa sekta ya Mafunzo ya Ufundi na Umma kwa ujumla kuwa udahili na uchaguzi wa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya Astashahada na Stashahada mbalimbali yanayotolewa na vyuo vyote hapa nchini, utafanyika moja kwa moja vyuoni, isipokuwa kozi za afya na ualimu zinazotolewa na vyuo vya Serikali tu. Hivyo maombi yote ya nafasi za masomo yatumwe kwenye chuo husika.

Udahili wa kozi za Afya na Ualimu katika vyuo vya Serikali utaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; na Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia kwa kushirikiana na Baraza (NACTE). Hivyo maombi ya Udahili kwa kozi za Afya na Ualimu kwa vyuo vya serikali tu yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz) au kupitia vyuo husika vya Afya na Ualimu ambavyo vitashughulikia maombi hayo na kufanya udahili kwa njia ya mtandao kupitia ‘Institutional Panel’ zao.

==========

upload_2017-5-10_20-35-15.png
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UDAHILI WA WANAFUNZI WA ASTASHAHADA NA STASHADA KATIKA PROGRAMU MBALIMBALI KWA MWAKA WA MASOMO 2017/2018

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) ni chombo kilichoanzishwa kwa sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, Sura 129, ili kusimamia na kuratibu utoaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi nchini. Sheria hii inazitaka Taasisi zote zinazotoa elimu ya ufundi kusajiliwa kabla ya kuanza kuendesha mafunzo yoyote. Baraza pia huidhinisha mitaala kabla haijaanza kutumika. Hivyo taasisi zote haziruhusiwi kuanza kutoa mafunzo yoyote bila kibali maalumu kutoka Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).

Baraza linapenda kuwataarifu wadau wa sekta ya Mafunzo ya Ufundi na Umma kwa ujumla kuwa udahili na uchaguzi wa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya Astashahada na Stashahada mbalimbali yanayotolewa na vyuo vyote hapa nchini, utafanyika moja kwa moja vyuoni, isipokuwa kozi za afya na ualimu zinazotolewa na vyuo vya Serikali tu. Hivyo maombi yote ya nafasi za masomo yatumwe kwenye chuo husika.

Udahili wa kozi za Afya na Ualimu katika vyuo vya Serikali utaratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; na Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia kwa kushirikiana na Baraza (NACTE). Hivyo maombi ya Udahili kwa kozi za Afya na Ualimu kwa vyuo vya serikali tu yatumwe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya NACTE (www.nacte.go.tz) au kupitia vyuo husika vya Afya na Ualimu ambavyo vitashughulikia maombi hayo na kufanya udahili kwa njia ya mtandao kupitia ‘Institutional Panel’ zao.

Aidha vyuo vyote vitatangaza au kuwafahamisha moja kwa moja waombaji majina ya watakaochaguliwa kujiunga na kozi mbalimbali; na wale wa kozi za Afya na Ualimu watatangazwa na Wizara husika na kupitia tovuti ya NACTE.

Baraza linapenda pia kuwafahamisha kuwa Vyuo vitaanza kupokea maombi ya udahili wa wanafunzi kuanzia tarehe 15 Mei, 2017 hadi tarehe 20 Agosti, 2017. Majina ya waliochaguliwa yatatangazwa tarehe 14 Septemba, 2017. Masomo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 yanatarajiwa kuanza rasmi tarehe 25 Septemba, 2017.

IMETOLEWA NA:

OFISI YA KATIBU MTENDAJI

BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)

TAREHE: 10/05/2017
Share:

Sunday 7 May 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY TAREHE 7.5.2017


Share:

Barua ya Bodi ya Ligi kuhusu sakata la alama tatu kati ya Kagera Sugar na Simba SC.

Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewajibu rasmi Simba SC juu ya sakata lao la kupokwa pointi tatu za mezani walizopewa baada ya rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar wakidai kumcheza mchezaji Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.
 
Kwa mujibu wa barua kutoka katika Bodi ya Ligi zimesema kuwa Fakhi hakuwa na kadi tatu za njano wakati akicheza mchezo dhidi ya Simba uliofanyikia uwanja wa Kaitaba, Bukoba Aprili 2 mwaka huu.

"TFF ambayo ndiyo yenye dhamana ya usimamizi wa mpira nchini na ambayo ndiyo iliyokaimu madaraka kwa TPLB kuendesha ligi kuu iliitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambayo ilichunguza kwa undani sakata hili na baada ya uchunguzi wao ambao walihoji watu mbalimbali, walituandikia kutujulisha kuwa wamebaini mchezaji Mohamed Fakhi anayelalamikiwa na Simba hakuwa na kadi 3 siku ya mchezo wa Kagera Sugara dhidi ya Simba hivyo alikuwa halali kucheza mchezo huo". Ilisema barua hiyo
Share:

Saturday 6 May 2017

Habari Mbaya: Wanafunzi 20 wahofiwa kufa katika ajali ya basi Karatu

Wanafunzi zaidi ya 20 wanahofiwa kupoteza maisha katika ajali ya basi iliyotokea wilayani Karatu leo asubuhi.
Habari zinaarifu kuwa , basi hilo limeanguka kabla ya kuingia karatu mjini na kuua watoto wengi .
Inaarifiwa kuwa Wanafunzi hao  ni wa shule inayoitwa Lucky Vicent ya Arusha ambao walikua wanaenda karatu kufanya mitihani ya mashindano na shule za karatu.
Share:

Update: Wanafunzi Waliofariki Katika Ajali Leo Wafika 32

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema wanafunzi 31 na walimu wao wamefariki katika ajali iliyotokea wilayani Karatu, ulipo mto Mlera.

Mkumbo amesema wanafunzi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni wa shule ya mchepuo wa Kiingereza, iitwayo Luck Vicent ya mjini Arusha.

Kati ya wale waliofariki 28 walikuwa wanafunzi huku watatu wakiwa ni dereva na walimu wao

Ripoti zinasema kuwa basi hilo liliteleza na kukosa mwelekeo ,likatoka katika barabara na kuanguka katika mto katika eneo la Marera eneo la Rhotia, kilomita chache kabla ya karatu katika barabara ya Arusha
Share:

Lowassa awalilia wanafunzi Waliofariki katika Ajali........Maiti 32 zapelekwa mochwari katika Hospitali ya Lutheran Karatu.

Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa ametuma salamu za rambi rambi kutokana na tukio la watu 32 kufariki dunia katika ajali ya basi.

Waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Karatu, ni wanafunzi 29, walimu wawili, pamoja na dereva wa gari hilo.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo, ni ajali mbaya ambayo inaifanya siku hii kuwa mbaya katika historia ya nchi yetu,”alisema

Miongoni mwa wanafunzi waliofariki ni pamoja na wanaume 11 na wasichana 18.

Kadhalika maiti 32 zikiwamo za walimu wawili, dereva mmoja na wanafunzi 29 zimepokelewa sasa hivi katika Hospitali ya Lutheran Karatu.

Share:

Friday 5 May 2017

TANZANIA YAPOKEA TUZO UMEME VIJIJINI

 Displaying MOJA.JPG
TANZANIA YAPOKEA TUZO UMEME VIJIJINI
Jitihada za Wizara ya Nishati na Madini za kuhakikisha umeme unafika na kusambaa maeneo ya vijijini zimetambuliwa kimataifa hali iliyopelekea Serikali kupokea Tuzo ya Uwezeshaji wa Mazingira Bora ya Upatikanaji wa Umeme Vijijini kwa Nchi zinazoendelea.

Serikali imetunukiwa Tuzo hiyo mwezi Machi, 22 na Taasisi ya Kimataifa ya Alliance for Rural Electrification yenye Makao Makuu yake nchini Ubelgiji ambayo ilipokelewa na Meneja Miradi wa Kampuni ya Umeme ya Ensol, Prosper Magali kwa niaba ya Serikali katika hafla ya utoaji tuzo iliyofanyika Lisbon, Ureno. Magali pia ni Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya Nishati Jadidifu (TAREA).
Share:

Sunday 30 April 2017

TETESI:WAHITIMU WA SUA ELIMU YAO HATIHATI BAADA YA WALIMU WAO WENGI KUWA NA "VYETI FEKI"

 Image result for sua tanzania
Baada ya Rais Kupokea ripoti ya watumishi wa serikali wenye vyeti Feki,Wasiwasi umetokea kwa wanafunzi na wahitimu waliosoma Chuo kikuu Sua kutokana na kufundishwa na walimu ambao majina yao yametajwa kama ni watumishi wenye vyeti feki.
Share:

MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE APRIL 30,2017

Share:

Saturday 29 April 2017

AJIRA ZA MADAKTARI APRIL 2017


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF HEALTH, COMMUNITY DEVELOPMENT,
GENDER, ELDERLY AND CHILDREN

ANNOUNCEMENTS:

The Ministry of Health in Tanzania has announced the list of employed Medical Doctors and Health Specialists (April 2017) and their working stations.

Click HERE to read the announcement

Click HERE to download the list

Source: Ministry of Health Official Website
Share:

BREAKING NEWS:HII HAPA ORODHA YA MAJINA YA WAFANYAKAZI WENYE VYETI FEKI MIKOA YOTE TANZANIA

Habari zenu,

Kama kawaida yetu MASWAYETU BLOG ni kukupa kitu roho inapenda,tumekuweke hapo chini orodha yenye majina ya watumishi wenye vyeti feki TANZANIA.


WAFANYAKAZI WA HALMASHAURI WENYE VYETI FEKI 

<<BONYEZA HAPA>>

KWA WAFANYAKAZI WA TAASI ZA SERIKALI MFANO,UDSM 
Share:

AUDIO | Sholo mwamba - Namba moja(Usije Mjini) | Download

Share:

Saturday 22 April 2017

SERIKALI KUMWAGA AJIRA 52,436




SERIKALI inakusudia kuajiri watumishi wapya 52,436 katika mwaka ujao wa fedha.

Ajira hizo mpya ni tofauti na zile za madaktari 258 na wataalamu wa afya 11 waliotangazwa kuajiriwa Jumatano wiki hii baada ya kupeleka maombi na kukidhi vigezo kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ajili ya kwenda kufanya kazi nchini Kenya.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger