Monday 20 February 2017
Sunday 19 February 2017
HII HAPA REPORT YA WANASAYANSI KUHUSU KUWEPO KWA BARA LA NANE DUNIANI
Wanasayansi wafahamisha kuwa bara la 8 lawezekana kuwa lipo chini ya bahari ya Pasifiki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika jarida la Marekani la 'Geological Society of America' ni kwamba bara hilo limepewa jina la Zealandia .
Bara hilo lililokubalika na wanasayansi linasemekana kupatikana katika upande wa Kusini Magharibi mwa bahari ya Pasifiki.
Liko na ukubwa wa kilomita milioni 5 za mraba sawa na thuluthi ya ardhi ya bara la Australia .
Wanasayansi wamesema kuwa bara hilo limefinikwa na maji ya bahari .
Zijue Namba Maalum za Magari ya Viongozi, Serikali na Taasisi za Umma kwa Ujumla..!!!
Ukiona mtaani gari zimeandikwa ktk plate number kama ifuatavyo usiumize kichwa jua ni hivi:
1. Ngao-Rais, makamu wa rais na waziri mkuu
2. S-Spika wa bunge
3. JM- Jaji mkuu
4. JR- Jaji wa mahakama ya rufaa
5. JK- Jaji Kiongozi
6. J- Jaji wa mahakama kuu
7. XXXX-Mkuu wa majeshi(CDF)
8. CAG-Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali
9. CS- Katibu mkuu kiongozi
10. W mwanzoni inaashiria waziri kisha kifupi cha wizara yake hufuata
11. NW-Naibu waziri
12. DFP-Donor's Fund project
13. ST-Serikali ya Tanzania kisha herufi nyingine hufuata
14. SMZ-Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
15. PT-Police of Tanzania
16. SM-Serikali za mitaa
17. CD- Magari ya ubalozini
18. SU-Shirika la umma.
19. gari za jeshi pia zina namba zake ambazo zina vifupi vya JW
20. MT-Magereza Tanzania
21. CGP-Commissioner General of Prison(Mkuu wa Magereza)
22. Gari nyingine za umma zina namba zaidi ya moja kwa kazi maalum
NYONGEZA:
Gari za biashara zina plate number nyeupe na zile za matumizi binafsi plate number ya njano.
MUGABE ANAWEZA KUPIGIWA KURA HATA AKIWA MAITI...
Mke
wa Rais mkongwe wa Zimbabwe, Robert Mugabe, amesema kuwa mumewe ni
mashuhuri sana hivi kwamba anaweza kupigiwa kura hata akiwa maiti.
Bwana Mugabe, ambaye atakuwa na umri wa miaka 93 mnamo Jumanne,
ametangaza mara kadhaa kuwa atagombea kiti cha Urais katika uchaguzi
mkuu wa mwaka ujao.
Grace Mugabe ana miaka 40 mchanga kwa mumewe.
Aliambia mkutano wa chama tawala cha ZANU-PF kuwa hata mumewe akifariki,
bado jina lake litawekwa kwenye karatasi za kupiga kura.
Alisema watu wa Zimbabwe wanampenda rais wao sana, hivi kwamba wangempigia kura hata akiwa maiti.
Bi Mugabe amekuwa mkosoaji mkuu wa wakosoaji wa mumewe na kwa wale walio na tamaa ya kumrithi.
Inadhaniwa kuwa alikuwa mstari wa mbele wa kumwachisha kazi aliyekuwa makamu wa rais, Joice Mujuru mwaka 2014.
Bwana Mugabe, ambaye siku hizi haonekani sana hadharani, ametawala Zimbabwe tangu taifa hilo kuwa huru miaka 37 iliyopita.
Via>>BBC
MAELFU WAJITOKEZA KUMZIKA MCHEZAJI BONNY MWANDANJI
Maelfu
ya wakazi wa mkoa wa Mbeya wamejitokeza katika mazishi ya mchezaji wa
zamani Geoffrey Bonny Mwandanji aliyefariki dunia juzi na kuzikwa katika
makaburi ya kanisa Katoliki Makandana wilayani Rungwe.
Akizungumza wakati wa mazishi baba mzazi wa marehemu,Bonifasi Mashamba
alisema amepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mwanae na kuongeza kuwa
aliishi na watu vizuri jambo lililochangia watu wengi kujitokeza
kumuuguza ikiwa ni pamoja na misaada mbali mbali.
Naye Mjomba wa marehemu, Innocent
Sigonda alisema marehemu alikuwa akisumbuliwa na kansa ya mapafu pamoja
sukari ilikuwa ikishuka mara kwa mara.
Mwenyekiti wa tawi la Yanga mkoa wa Mbeya Lusajo Kifamba alisema
marehemu alikuwa mwanachama wao hivyo uongozi unasikitika kumpoteza
mwanachama wake ambaye alikuwa akitoa msaada wa kiufundi kila
alipotakiwa.
Naye mwakilishi wa uongozi wa yanga makao makuu Shadrack Nsajigwa
alisema marehemu aliishi naye kama ndugu kwani walisaidiana na kupeana
ushauri.
Alisema marehemu alikuwa na kipaji cha mpira pia alikuwa anajituma hivyo alikuwa mfano wa kuigwa kwa vijana waliopo.
Aliongeza kuwa wachezaji wa zamani ni hazina kwa taifa hivyo ni vyema wakatunzwa na kuthaminiwa.
Aidha alitoa wito kwa wachezaji wengine kujipanga kimaisha ili baada ya
kustafu wasisubiri kuomba misaada pindi wapatapo matatizo.
Alisema in vyema pia kuanzisha vyama vya kuwasaidia kama wachezaji wastaafu.
AMIRI JESHI MKUU RAIS DKT MAGUFULI ATUNUKU KAMISHENI KWA MAAFISA WAPYA WA JWTZ IKULU DAR
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akikagua gwaride wakati wa
sherehe za Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la
Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini
Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli akitunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi
la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu
jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli akiweka saini katika hati ya Kamisheni muda mfupi kabla
ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania
na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es
salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli akiweka saini katika hati ya Kamisheni muda mfupi kabla
ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Tanzania
na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es
salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri
Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe
Magufuli akiwasili Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la
Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya
Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Kikundi cha ngoma cha JWTZ kikitumbuiza kwa ngoma ya Chaso ya Pemba
wakati Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt
John Pombe Magufuli alipotunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa Jeshi la
Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika viwanja vya
Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John
Pombe Magufuli, Makamu wa rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe
Kassim Majaliwa, Waziri wa ulinzi nja Jeshi la Kujenga taifa Dkt Hussein
Mwinyi, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Juma Kijazi na viongozi wengine
katika picha ya pamoja baada ya Kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya wa
Jeshi la Ulinzi la Tanzania na kadhaa kutoka nchi marafiki katika
viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam Jumamosi Februari 18, 2017.PICHA
NA IKULU
Saturday 18 February 2017
Mwanamke asimulia alivyobakwa na askari Msumbiji
Wakati Serikali ikiahidi kufanya
uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika kutimua
Watanzania nchini Msumbiji, mwanamke mmoja amesema alibakwa na askari
watatu kabla ya kuwekwa mahabausu ambako alikaa siku tatu bila kula.
Mwanamke huyo, aliyejitambulisha kwa jina la Halima (si jina lake
halisi) ni mmoja kati ya zaidi ya Watanzania 180 ambao wamekuwa
wakitimuliwa nchini Msumbiji tangu mwanzoni mwa wiki na wengi wakidai
wana hati halali za kuishi nchi hiyo jirani na wengine kulalamikia
vitendo vya ukiukwaji haki wakati wa utekelezaji wa operesheni hiyo.
Tayari Serikali imesema kuwa itafanya uchunguzi wa madai hayo, ambayo
yanaweza kuharibu uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Msumbiji.
Halima anasema
walianza kufukuzwa usiku wa Jumamosi ya Februari 11, muda ambao askari
hao waliutumia kumfanyia kitendo hicho.
Halima anasema kuwa alisikia
watu wakivunja geti la nyumba waliyokuwa wakiishi na kudhania ni
majambazi, kumbe walikuwa ni askari ambao waliwalazimisha kutoa nyaraka
zao zote za kuishi Msumbiji pamoja na pesa.
“Niliwasikia wakivunja geti
nikamwambia mume wangu watakuwa ni majambazi kumbe askari, mume wangu
akajificha chini ya uvungu, lakini wakamtoa na baadaye kututoa ndani na
kuanza kutupiga.”
Anasema baada ya kipigo walilazimishwa kuzoa mali
zao kutoka ndani na zikawekwa kwenye gari la polisi na kisha kuwafunga
mikono na baadaye kuwapeleka mahabusu.
“Cha kushangaza tulibebeshwa vitu
wenyewe kuweka kwenye gari pasipo kuelezwa sababu baada ya hapo askari
akanivuta nyuma ya nyumba na kuniingilia kimwili. Nikajua ni mmoja,
lakini waliendelea hadi wakafikia watatu,” alisema.
“Ninaona aibu
walinibaka kwa njia ya kawaida tofauti na taarifa za wengine wanaosema
tulibakwa kinyume na maumbile, si kweli. Nawaomba waelewe hatukubakwa
kinyume na maumbile kama wanavyosema ilikuwa kawaida.”
Hata hivyo
anaeleza baada ya hapo waliwekwa mahabusu kwa siku tatu pasipo kula,
hali iliyowalazimu kunywa maji yaliyokuwa yamewekwa chooni.
“Tulikaa
mahabusu siku tatu, hamna kula wala kunywa, chooni tulienda kwa mtutu
tukalazimika kunywa maji ya chooni kwa sababu hakukuwa na jinsi na njaa
ilizidi. Kwa hiyo inabidi useme unakwenda chooni ili ukanywe maji,”
alisema Halima.
Kutokana na hali hiyo, Halima anashangazwa na kauli ya
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Susan Kolimba kwamba waliorudishwa
hawakuwa na nyaraka huku kaimu balozi wa Tanzania nchini Msumbiji
akiwatangazia wengine kuondoka ndani ya siku tano.
“Kweli mtu utathubutu
vipi kuishi nchi ya watu bila kibali? Hata kaimu balozi na yeye
anatukana, kwamba hatujaingia na documents (nyaraka)? Ilibidi atutetee
lakini katukana. Mungu atatulipia,” alisema.
Mwanamke mwingine
aliyewekwa mahabusu kabla ya kurudishwa nchini, Mary Makundi anasema
askari wa kiume walimwambia awape fedha na alipowajibu kuwa hana,
walimpekua na kuzikuta.
Anasema walizichukua fedha hizo pamoja na simu
kabla ya kumpiga na kutaka kumbaka.
“Walivunja mlango wakanikuta.
Wakaniambia niwape nyaraka zangu. Nikawapa nikijua wanazikagua tu na
kuniacha, lakini cha kushangaza walizichana mbele yangu na kunitaka
niwape pesa na simu. Nikawaambia sina wakanipiga na kunikagua hadi
sehemu za siri na kuchukua pesa na simu,” alisema Mary.
“Baada ya hapo
walinipiga kwanza kabla ya kunifunga mkono. Askari mmoja akataka
kunibaka, nikamwambia kuwa hata kama hawatutaki nchini kwao, hawawezi
kuniingilia bila kinga.
“Nilipoona hali imekuwa mbaya, nilisema wacha
nigombane nife kwa silaha, lakini si kubakwa.”
Mtanzania mwingine
Mohamedi Said ni mmoja wa wafanyabiashara walioambiwa waondoke pasipo
kuchukua chochote na anadai kuacha mali zake zote pamoja na nyumba
aliyojenga.
“Polisi walikuja ghafla wakatuambia wageni wote tunatakiwa
tuondoke. Hapa nina vibali vyote mpaka leseni ya biashara, lakini
imebidi niondoke kwa sababu ya usalama wangu,” alisema Said.
“Hakuna
anayejua sababu mpaka sasa. Nimekuja nyumbani kufuatilia haki yangu kwa
sababu mpaka kibali cha kujengea ninacho.
“Mpaka sasa amekuja kaimu
balozi kutoka ubalozi wa Tanzania na amesema kwa ripoti aliyopewa
ametupa siku tano tuondoke. Hatujui kwanini siku tano. Utahamishaje vitu
kwa siku tano au kumtafuta mnunuzi wa nyumba kwa siku tano kwa sababu
imenibidi niache duka kubwa na gari,” alisema Said.
Akizungumzia tukio
hilo, mwenyekiti wa Kijiji cha Kilambo kilichopo mpakani na Msumbiji,
Mohamed Mkama alisema wananchi wa kijiji chake wamekuwa wakishirikiana
na wanakijiji wa vijiji jirani vya Msumbiji, lakini tukio hilo
limewashangaza.
Amesema mara nyingi wamekuwa wakitembeleana na hata
wengine kutoka upande wa Msumbiji kuja kutibiwa Tanzania kutokana na
ujirani mwema uliopo.
“Kijiji changu kina vitongoji vitano ambavyo
tumekuwa tukishirikiana na kijiji cha upande wa pili kwa muda mrefu na
wengine wana vitambulisho vya uraia mwema, lakini tunashangaa kwanini
wanarudishwa pasipo kuelezwa sababu,” alisema Mkama.
Ofisa uhamiaji Mkoa
wa Mtwara, Rose Mhagama alisema idadi ya Watanzania waliorudi na
kusajiliwa katika mpaka wa Kilambo ni watu 221 hadi kufikia jana mchana.
Thursday 16 February 2017
NECTA yasitisha mtihani wa udahili kwa kidato cha kwanza Jambo Blog 10
BARAZA la Mitihani la Tanzania (NECTA) limesitisha mpango wa kuwafanyia mtihani wa udahili wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika shule za sekondari za serikali uliokuwa ufanyike Februari 28, mwaka huu.
Naibu Katibu Mtendaji wa Necta, Athumani Salumu alisema hayo juzi kwenye kikao cha wadau wa sekta ya elimu Mkoa wa Morogoro alipokuwa akihitimisha mada yake kwa wajumbe wa kikao hicho kilichoongozwa na mkuu wa mkoa huo, Dk Stephen Kebwe.
Salumu alisema mpango wa kuwafanyia mtihani wa udahili wanafunzi hao ulitokana na matakwa yaliyowasilishwa Necta na baadhi ya wakuu wa shule za serikali wakipendekeza kupitia maofisa elimu wa mikoa na wilaya kuwa wanafunzi wa kidato cha kwanza waliochaguliwa na kupangiwa shule zao wengi hawana sifa na uwezo wa kumudu masomo.
Naibu Katibu Mtendaji wa Necta alisema wakuu wa shule walikuwa wakiomba kupata idhini ya kuwafanyia mtihani wanafunzi ili kubaini uwezo wao na kwamba baraza liliwasiliana na maofisa elimu mkoa na wilaya likiwataka kuwasilisha orodha ya idadi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza waliopangiwa kwenye shule ya zao.
Alisema baada ya kufahamika idadi ya wanafunzi hao, baraza ndilo litatunga maswali ya mitihani yenye kuzingatia mfumo na vigezo maalumu na kutumiwa wakuu wa shule hizo ili kuusimamia kwa lengo la kuweka uzani sawa wa mtihani huo.
Alisema moja ya masharti ni kwamba mtihani huo ulitakiwa ufanyike kwa wanafunzi wa kidato hicho kwa shule zote za serikali siku moja na kwa muda uliopangwa.
Hata hivyo, alisema baada ya kuwatumia masharti hayo, wakuu wa shule hizo walishindwa kuwasilisha orodha ya wanafunzi kwa maofisa elimu wa mikoa na wilaya ili itumwe Necta na kutokana na mazingira hayo, baraza limeamua kusitisha kuwadahili wanafunzi wa kidato cha kwanza na kuitaka mamlaka inayosimamia elimu kuendelea na utaratibu wao wa kawaida.
“Necta imewasiliana na wahusika kwa barua rasmi ya kusitisha mtihani huo ambao ulipangwa ufanyike Februari 28, mwaka huu na wanafunzi wote waliopangiwa kidato cha kwanza shule mbalimbali za serikali zikiwemo za bweni, waendelee na masomo kama yalivyopangwa,” alieleza Naibu Katibu Mtendaji wa Necta.
Novemba mwaka jana, serikali ilitangaza kuwa wanafunzi 526,653 sawa na asilimia 94.8 ya waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka jana, wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule za sekondari za serikali katika awamu ya kwanza huku 28,638 wakishindwa kupangiwa shule katika awamu ya kwanza.
Kati ya wanafunzi hao, wasichana ni 268,052 sawa na asilimia 94.5 ya wasichana waliofaulu na wavulana ni 258,601 sawa na asilimia 95.2 ya wavulana waliofaulu.
Chanzo: Habari Leo
Wednesday 15 February 2017
NECTA: ADVANCED CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION MAY 2017
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Ref. ACSEE 2017
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL
ADVANCED CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION MAY 2017
Monday 13 February 2017
Zitto Kabwe Amtaka Rais Magufuli Avunje Bunge
Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amemshauri Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli kulivunja Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania endapo analiona ni kikwazo kwake.
Ushauri huo ameutoa jana ikiwa ni saa chache baada ya Rais Magufuli kukosoa uamuzi wa Bunge kumuita Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kujieleza mbele ya Kamati ya Bunge, kutokana na kilichodaiwa na wabunge kuwa ni kauli ya kulidhalilisha Bunge.
Katika hotuba yake aliyoitoa jana wakati wa kuapishwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rais Magufuli aliwataka viongozi wengine kumuunga mkono mtu anayejitokeza kupiga vita dawa za kulevya badala ya kumdhalilisha.
"Tunapomuona mtu anajitokeza kupambana na haya madawa ya kulevya, badala ya kumdhalilisha tumuombee na kumtia moyo, hawa wanaweza hata kubadilisha maneno uliyoyazungumza wakabadilisha wakatengeneza kwenye clip wakatupa, na wakajitokeza wengine wakasema wameingilia mamlaka yao, wakati wao wanaingilia mamlaka ya kuwaita wengine, hii ni vita". Alisema Magufuli
Baada ya kauli hiyo ya Rais, Zitto kupitia ukurasa wake wa Facebook ameonesha kushangazwa na kile alichodai kuwa Rais hakujua kuwa sheria ya kuundwa kwa mamlaka hiyo, ilitungwa, na kwamba anashangaa kuona Rais hakuwa akijua kuwa alipaswa kumteua Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo
Ujumbe wa Zitto unasema
"Wabunge walitoa Hoja Binafsi kuhusu Madawa ya kulevya ( Esther Bulaya na Faustine Ndugulile ) na kufuatia hoja hiyo Serikali ikaleta Muswada bungeni na Bunge likatunga Sheria ya Kupambana na Madawa ya kulevya mwaka 2015.
"Serikali mpya ikaingia madarakani mwezi Novemba 2015. February 2017 Ndio Kamishna Mkuu anateuliwa tena baada ya wabunge kuhoji na kushinikiza kupitia Kamati husika na pia mbunge Esther Bulaya aliyetoa Hoja Binafsi katika Bunge la Kumi.
"Rais anasema hakuwa anajua kuwa sheria hiyo ipo. Lakini Rais anapogawa Wizara huwa anatoa instruments na Hizo instruments hutaja kila sheria kwa kila Waziri. Ilikuwaje Rais akasahau sheria hii nyeti kama alikuwa na nia ya dhati ya Kupambana na Madawa ya kulevya?
Rais anaona Bunge kikwazo kwa sababu Bunge linamwongoza afuate sheria. Lakini Kama anaona Bunge linamkera turudi kwenye uchaguzi tu, alivunje".
Yusuf Manji Alivyochukuliwa na Gari la Wagonjwa Polisi na Kisha Kupelekwa Hospital
Mfanyabiashara maarufu na Mwenyekiti wa Club ya soka ya Yanga Yusuph Manji amekua akishikiliwa na Polisi kituo cha kati Dar es salaam toka Alhamisi ya February 9 2017 baada ya kwenda kuhojiwa kutokana na kutajwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kwenye orodha ya watu 65 kwenye sakata la dawa za kulevya.
Jana jioni Mfanyabiashara huyo alichukuliwa na gari la kubebea Wagonjwa lenye namba za usajili za DFP na alionekana akitembea na kuingia kwenye gari hilo (Land Cruise Nyeupe) yeye mwenyewe bila kubebwa au kusaidiwa huku gari lake aina ya Range Rover likitangulia mbele na watu wengine.
Baada ya gari hilo kumchukua msafara huo ulikwenda moja kwa moja kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Muhimbili Dar es salaam ambako watu mbalimbali wanaosumbuliwa na moyo hupata matibabu.