Friday 13 January 2017

RAIS MAGUFULI APIGILIA MSUMARI KWA WAPIGA DILI NCHINI

Rais John Magufuli ameendelea kupigilia msumari kwa watanzania na viongozi wasiopenda kujishughulisha na kuwajibika na kutegemea zaidi fedha za bure za umma.

Amehakikishia kuwa hali zao zitaendelea kuwa mbaya, isipokuwa kwa wale watakaowajibika na kujishughulisha.

Amesema wale wote wanaolalamika kuwa hawana fedha mfukoni kwa hivi sasa, walizokuwa nazo hazikuwa zao, ndio maana wanalalamika.

Katika hotuba zake mwaka jana katika sehemu mbalimbali nchini, Rais alisema wanaolalamika hawana hela mfukoni ni ‘wapiga dili’.

Rais alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano, itahakikisha inamaliza hali mbaya iliyokuwa inalikumba taifa la watanzania, ambapo watu wachache ndio waliokuwa wakinufaika na fedha za umma huku wananchi wengi wakiendelea kuumia na umasikini.

Alisema hayo mkoani Shinyanga jana wakati akizungumza na wananchi kuhusu maendeleo ya mkoa huo na kumbukumbu ya maadhimisho ya Miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 
“Nimejitoa sadaka kwa ajili ya nchi hii, mimi sikuwa na urais ila mmenipa nyie, sasa nawaahidi mimi na serikali yangu tutawatetea kwa nguvu zote dhidi ya mafisadi.

"Nasikia kuna watu wanalalamika kuwa eti fedha hamna, kwani zilikuwa zinauzwa sokoni?" alihoji. 
Alisema watu wote wanaolalamika kuwa fedha zimepotea mitaani, ni wale waliokuwa wamezoea kupata fedha za bure bila kuzitolea jasho.

Aliwahakikishia kuwa wataendelea hivyo hivyo kutaabika, huku wale waliokuwa wakijishughulisha wakineemeka. Alisema fedha zilizotumiwa na mafisadi kipindi cha nyuma ni nyingi mno, kwani kila serikali ikitenga na kutoa fedha za maendeleo, zimekuwa zikiishia mikononi mwa mafisadi.

“Watu walikuwa wanajipatia tu fedha bila kuzitolea jasho, unakuta mtu anaenda nje kila siku, wapo waliofikia kufanyia mikutano ya taasisi zao za ndani nje ya nchi, mfano pale Muhimbili (hospitali ya taifa) nilipoenda nilikuta akinamama wanajifungulia chini huku fedha zipo lakini zimetengwa kwa ajili ya starehe,” alifafanua.

Alisema wakati serikali yake inaingia madarakani ilikuta nchi ina hali mbaya hali iliyoilazimu asafishe kila kona ya idara, ndipo walipopatikana watumishi hewa zaidi ya 18,000, wanafunzi hewa 65,000, mikopo ya elimu ya juu hewa yenye thamani ya Sh bilioni 3.5.

Alisema hata fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), zinazotolewa kwa kaya maskini, zilitolewa kwa kaya hewa 55,000.

Rais alisema ni wakati sasa Watanzania na serikali kwa ujumla wakashirikiana kuijenga Tanzania mpya, itakayomkomboa kila mwananchi akiwemo masikini, kwani kutokana na utajiri ambao Tanzania inayo, imekuwa ikichekwa kwa kuendelea kuwa masikini.

Utumbuaji majipu
Alisema pamoja na kwamba wapo baadhi ya watu wanachukizwa na hatua ya utumbuaji majipu kwa watumishi wasiowajibika, serikali yake itaendelea kuwatumbua watumishi na viongozi wanaokwenda kinyume na maadili yao.

“Ni bora nichukiwe na watu wachache kuliko kupendwa na wengi huku mambo yakienda mrama. Wale wote wanaodai mtindo wangu wa kutumbua ni mbaya hawa ndio majipu. Kabla ya utumbuaji watanzania walikuwa wanaishi maisha ya ajabu, na kusisitiza kuwa alikuwa mtumishi wa serikali kwa kipindi cha miaka 10 anajua anachoongea,” alisisitiza.

Aliomba Watanzania wamuombee ili aweze kuendeleza jitihada zake za kupambana na mafisadi kwani serikali yake ya awamu ya tano imejipanga kuendelea kuongoza kwa ukali kwa faida ya watanzania wote wakiwemo wanyonge na masikini.

“Lengo langu ni kuhakikisha wale wote waliokuwa wakila na kuchekelea kipindi cha nyuma wakati wenzao wanataabika, sasa waishi kama mashetani na wale waliotaabika waishi kama wafalme,” alisema.

Hatua za maendeleo
Dk Magufuli alisema kutokana na kutambua adha wanayoipata watanzania kutokana na huduma mbovu, serikali yake imejitahidi kupambana na kuboresha maendeleo mengi ikiwemo sekta za elimu, miundombinu usafiri na afya.

Alitolea mfano namna serikali hiyo ilivyofanikiwa kukusanya mapato kwa kubana maeneo yote yenye ubadhirifu na kufanikiwa kuongeza mapato kutoka Sh bilioni 31 hadi Sh trilioni moja, hali iliyosaidia serikali hiyo kununua ndege sita, mbili zikiwa tayari zimewasili.

Pia alisema serikali imefanikisha kusimamia elimu bure kwa kutenga kiasi cha Sh bilioni 18.77 kila mwezi, zinazokwenda moja kwa moja shuleni kwa ajili ya kuwezesha wanafunzi kusokma bure katika shule za msingi na sekondari.

Alisema pia serikali yake kwa kipindi kifupi, imefanikiwa kuongeza bajeti ya afya na kufikia Sh trilioni 1.99 na kati ya fedha hizo bajeti ununuzi wa dawa imeongezeka kutoka Sh bilioni 31 hadi Sh bilioni 250.

Mikakati
Aidha, kiongozi huyo alisema serikali yake imejipanga kuendelea kuwaletea maendeleo wananchi, ambapo pamoja na kununua meli mbili katika Ziwa Victoria na Tanganyika, pia imeanza mchakato wa kujenga reli ya kisasa ambayo imetengewa jumla ya Sh trilioni moja katika bajeti ya mwaka 2016/17.

Alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali za kutosha ikiwemo bahari, mito, maziwa, madini kama vile dhahabu na wanyama, lakini bado imeendelea kuwa na umasikini.

Alisema kutokana na hali hiyo, serikali yake imejipanga kuijenga Tanzania mpya ikiwemo viwanda ili kuweza kutimiza lengo la kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye kipato cha kati.

“Hapa Shinyanga kuna mwekezaji ambaye ana takribani miaka 10 sasa tangu nikiwa waziri wa mifugo na uvuvi na baadaye ujenzi, hajaendeleza kiwanda cha nyama, naagiza uongozi wa mkoa wawekezaji kama hawa waondolewe wapewe wengine tusonge mbele,” alisisitiza.

Pamoja na mwekezaji huyo, pia alipotembelea mgodi wa Maganzo alipatiwa taarifa za kuwepo kwa migogoro ya ardhi na kuwataka mawaziri wa ardhi na mazingira, kushughulikia suala hilo haraka iwezekanavyo.

Maji
Akizungumzia kero ya maji iliyowasilishwa mbele yake na Mbunge wa Shinyanga Mjini, Steven Masele, Dk Magufuli alibainisha kuwa atamtuma Waziri wa Maji kufuatilia bei inayotozwa kwa wakazi hao, ili kuwaondolea mzigo wa kutozwa bei kubwa ya maji.

Hata hivyo, Rais huyo aliweka wazi kuwa endapo atabaini bei inayotozwa kwa wakazi hao, haiendani na bei zinazotozwa katika miji mingine, atahakikisha ama anaipunguza au kuiongeza ili iendane na miji mingine.

Mapinduzi
Pamoja na hayo, Dk Magufuli alizungumzia maadhimisho ya siku ya mapinduzi ya Zanzibar na kubainisha kuwa kuanzia sasa serikali itakuwa inaadhimisha sikukuu za kitaifa katika mikoa mbalimbali ili kila mtanzania afaidike na sherehe hizo.

Alisema yeye na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein walipanga kila mmoja aadhimishe sherehe hizo katika maeneo tofauti, ambapo Dk Shein alikuwa visiwani Zanzibar yeye akiwa Shinyanga.

“Watu wamezoea wakisikia sherehe za kitaifa basi viongozi ni kulundikana sehemu moja. Sasa hili hatutolifanya, hizi ni sherehe za kitaifa kila mtanzania ana haki ya kuziadhimisha akiwa na viongozi wa kitaifa” alisema.
Share:

RAIS DKT SHEIN APANDISHA MSHAHARA KWA ASILIMIA 100%

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ametangaza neema mpya kwa wafanyakazi visiwani humo baada ya kuwakikishia kupandisha kima cha chini cha mshahara kuanzia mwaka huu (2017).

Dkt. Shein ametoa hakikisho hilo jana wakati akiwaongoza watanzania kuadhimisha Miaka 53 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar katika sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Amani visiwani humo.

Alisema kuanzia mwaka huu kima cha chini cha mshahara kitaongezeka kutoka Tsh. 150,000 hadi Tsh. 300,000 ikiwa ni ongezeko la asilimia 100.

Dkt. Shein alitoa tathmini yake ya mwaka mmoja tangu achanguliwe tena kuiongoza Zanzibar, ambapo alisema mwaka 2016 umekuwa ni wa mafanikio makubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu, kilimo, viwanda, huduma za jamii ikiwemo afya na huduma za maji, miundombinu n.k.

Akihutubia kwenye uwanja wa Amani Dkt. Shein alisema, serikali yake itaendelea kudumisha na kuenzi umoja na mshikamano ambao uliasisiwa na viongozi wa mapinduzi hayo.

Alisema, mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kukuza pato la taifa hadi kufikia 6.6% licha ya kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka 5.7% katika mwaka 2015 hadi kufikia 6.7% mwaka 2016.

Pia Dkt. Shein alieleza utekelezaji wa sera ya kulipa pensheni kwa wazee, ambapo amesema hadi mwezi Desemba mwaka 2016, jumla ya shilingi bilioni 4.3 zimetumika kuwalipa wazee 25,259 waliosajiliwa kiasi cha shilingi 20,000 kila mwezi, zoezi ambalo litaendelea kutekelezwa.

Katika hatua nyingine, Dkt Shein alitangaza rasmi kuwa matangazo yote ya TV yatahama kutoka mfumo wa 'Analogue' na kuhamia mfumo wa 'kidigitali' kuanzia mwezi April mwaka huu.
Share:

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARY TAREHE 13.1.2017

Share:

Thursday 12 January 2017

AUDIO | Chege Ft. Nandy - Kelele Za Chura | Download

Share:

Wednesday 11 January 2017

Watu 10 Watiwa Mbaroni Kwa Kumchapa Mwanamke Viboko 30 Rorya

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya mkoani Mara, linawashikilia watu 10 kwa udhalilishaji wa kumchapa viboko mwanamke hadharani.

Watu hao ni wa kijiji cha Kinesi tarafa ya Suba wilayani Rorya. Miongoni mwa watu hao, wamo viongozi watano wa baraza la mila liitwalo Irienyi ndogo la kabila la Wasimbiti.

Watu hao wanatuhumiwa kumchapa viboko zaidi ya 30 hadharani mwanamke huyo, kitendo kilichomdhalilisha mbele ya jamii.

Mapema wiki hii, baadhi ya video ilisambaa katika mitandao ya kijamii, ikimuonesha mwanamke akichapwa viboko na wanaume kwa zamu huku akilia mbele ya hadhara na sauti za wanaume zilisikika zikishabikia kitendo hicho.

Kamanda wa Polisi Tarime/ Rorya, Andrew Satta alisema kuwa tukio hilo ni la Desemba 23 mwaka jana mchana katika kitongoji cha Migutu kijiji cha Kinesi tarafa hiyo ya Suba wilayani Rorya katika maeneo ya Mastooni, ambako kulikuwa na mkutano wa Ritongo wa mila.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 38, mkazi wa kijiji hicho (jina limehifadhiwa) aliitwa na kufuatwa na vijana na kupelekwa katika mkutano huo wa mila, uliohudhuriwa na mamia ya wakazi wa kijiji hicho. Ilidaiwa kuwa mwanamke huyo alimtuhumu mama yake mzazi wa umri wa miaka 55 kuwa ni mchawi.

Kwamba hamtambui na kumkana kuwa si mama yake mzazi; huku akidai kuwa mama huyo anataka kumuua kwa uchawi. 
Kamanda Satta alisema katika mkutano huo wa baraza la mila la Irienyi, vijana sita waliamriwa kumchapa kila mmoja viboko vitano makalioni mwanamke huyo, hali iliyomsababishia majeraha, kumuathiri, kumdhalilisha na kumshushia utu wake kwa jamii.

“Tumewakamata mwenyekiti wa baraza hilo, viongozi wenzake wanne na vijana sita walioshiriki kumkamata na kuadhibu kwa kumlaza chini, kumchapa viboko na kumsababishia madhara makubwa mwilini na kumdhalilisha,” alisema Kamanda. Alisema watuhumiwa hao wanahojiwa na jeshi hilo linaendelea kuwasaka wengine waliohusika.
****

Share:

NUH MZIWANDA AKANA KUTOKA KIMAPENZI NA SHILOLE MKONI MWANZA

Msanii Nuh Mziwanda ambaye bado anafanya vyema na wimbo wake 'Jike shupa' amekanusha tetesi za yeye kuwa pamoja na mpenzi wake wa zamani Shilole jijini Mwanza siku mbili hizi.

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo, Nuh Mziwanda anasema ni kweli alimuona Shilole Mwanza kwenye club ambayo yeye alikuwa anafanya show na aliambiwa kuwa yupo pale lakini hakukutana naye wala ku-kiss na yeye kama ambavyo watu wanadai kuwa waliwaona wakali hao wakiwa pamoja na waki kiss.

"Mimi nimekuja Mwanza kwenye show zangu nimekutana naye tu Club hivyo mimi siwezi kumkataza mtu kuingia sehemu hivyo hilo ni jambo la kawaida, mimi mwenyewe niliambiwa yupo humu so sikujali maana mimi nilienda kufanya kazi na yeye alikwenda kufanya kazi kimpango wake. Kwa hiyo hayo maneno mengine yanayoongeleka mimi mwenyewe siyajui mimi nimekuja Mwanza kutafuta pesa" alisema Nuh Mziwanda

Mbali na hilo Nuh Mziwanda anasema kwa yeye saizi ni mume wa mtu hivyo hawezi kufanya mambo ya ajabu ajabu kama hayo kwa kuwa yeye anajiheshimu na kuheshimu ndoa yake

"Mimi nimeoa najiheshimu siwezi kufanya vitu ambavyo si vya maadili au ambavyo sitakiwi kuvifanya kilichonileta Mwanza ni kufanya show na kufanya makubaliano na kusaini mkataba wa show yangu nyingine itakayofanyika Dar es Salaam" alisema Nuh Mziwanda
Share:

RAIS MAGUFULI KATIKA ZIARA YAKE LEO MKOANI SIMIYU

Rais  John Magufuli leo anatarajia kufanya ziara ya siku mbili katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga na atazungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais.

Katika ziara hiyo Rais Magufuli anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya rufaa ya mkoa iliyopo mtaa wa Nyaumata na kufungua barabara ya Bariadi kwenda Lamadi ya urefu wa kilometa 50.3.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka alisema kwa siku hizo mbili atafanya shughuli hizo na baadaye atazungumza na wananchi lengo kufahamu matatizo yao.

Alisema mkutano huo utafanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Somanda.

Mtaka alisema kuwa Rais Magufuli kwa siku ya kwanza atazungumza na wananchi wa mkoa wa Simiyu lilipowekwa jiwe la ufunguzi wa barabara hiyo, siku ya pili atatembelea kiwanda cha kutengeneza chaki kilichopo Maswa na baadaye ataweka jiwe la msingi katika barabara ya Mwigumbi-Maswa.Pia atazungumza na wananchi wilayani Maswa.

Aidha aliwataka wananchi mkoani hapa kujitokeza kwa wingi kumlaki na kumsikiliza Rais Magufuli ambaye hajawahi kufika mkoani humo tangu achaguliwe kuwa Rais.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainabu Telack, amesema Rais Magufuli anatarajia kufanya ziara ya siku moja mkoani kwake kesho na atazungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara na kusikiliza kero zao.

Telack alisema kuwa ujio wa rais mkoani hapa ni kusherehekea siku ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo kitaifa zinafanyika kisiwani humo.

“Rais anatarajia kuwasili mkoani kwetu kwa ziara ya siku moja kwa lengo la kuzungumza na wananchi na siku hiyo itakuwa ni siku ya sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar hivyo atazisherekea akiwa mkoani hapa,” alisema.
Share:

MBWANA SAMATA KUENDELEA KUSHINDANIA NAMBA YAKE GENK

Siku 14 zimepita toka mshambuliaji wa KRC Genk Nikolaos Karelis ambaye alikuwa anashindania namba na mtanzania Mbwana Samatta atangazwe kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi 8 hadi 9 kufuatia jeraha la goti la kushoto alilolipata wakati wa mchezo dhidi ya KAA Gent dakika ya 51 December 27.

January 10 2017 KRC Genk imetangaza kukamilisha usajili wa mshambuliaji Jose Naranjo kutokea Celta Vigo ya Hispania, hiyo itakuwa ni changamoto mpya kwa Mbwana Samatta kuendelea kupambania namba ya kucheza na Naranjo katika kipindi ambacho Karelis atakuwa nje.

Jose Naranjo amejiunga na KRC Genk ya Ubelgiji akitokea Celta Vigo ya Hispania kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu, Naranjo mwenye umri wa miaka 22 amewahi kuichezea Villarreal kwa mkopo mwaka 2014 akitokea Recreativo.
Share:

UTAPELI GAZETI LA LETE RAHA WASHUTUKIWA,MMILIKI ATUPWA SELO

Idara ya Habari (MAELEZO) imebaini nyaraka za kughushi zilizowasilishwa na Mmiliki wa Kampuni ya FUKANI, Joseph Sheka wakati alipoziwasilisha kwa ajili ya kusajili gazeti la LETE MAMBO.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa MAELEZO, Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa mtuhumiwa huyo aliwasilisha nyaraka mbalimbali akidai kuwa ni za Mamlaka ya Mapato (TRA) ambazo uchunguzi wa awali umebaini kuwa mihuri na sahihi za baadhi ya maafisa wa Mamlaka hiyo zilizotumiwa ni za kughushi.

“Ni vyema jamii ikafahamu kuwa huu siyo wakati wa kujaribu kuishi kwa njia zisizo halali, kila mwananchi anapaswa kufuata taratibu zinatohitajika pindi anapotaka kupatiwa huduma katika maeneo mbalimbali ya ofisi za Umma."

Dkt. Abbasi alitoa rai kwa ofisi mbalimbali za Umma kuwa makini na nyaraka zinazowasilishwa na wateja wao kwani zinaweza kuwa na malengo mbalimbali ya kuiingiza Serikali katika matatizo hivyo kuitia hasara.

Mbali na hayo Dkt abbasi alisisitiza kuwa wale wanaohisi waliwasilisha nyaraka zao na kuona kwamba zina utata kuja kuzirekebisha na watakaobainika kuwa walighushi nyaraka hizo sheria itafuata mkondo wake.

Kwa sasa Idara ya Habari imemkabidhi mtuhumiwa katika Kituo cha Polisi cha Kati jijini dar es salaam kwa mahojiano zaidi.
Share:

SIMBA YATINGA FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI KWA KUICHAPA YANGA PENATI 4-2

Yanga imeendelea kusulubiwa kwenye mashindano ya Mapinduzi Cup baada ya kujikuta ikichezea kichapo kutoka kwa Simba kwenye mchezo wa nusu fainali ya pili kwa mikwaju ya penati 4-2 kufatia dakika 90 kumalizika bila timu hizo kufungana.

Baada kichapo cha 4-0 kutoka kwa Azam FC, Yanga imeondoshwa kwenye michuano hiyo na kuziacha Simba na Azam zikutane kwenye mchezo wa fainali ambao utachezwa siku ya Ijumaa January 13, 2017 ikiwa ni siku moja baada ya kilele cha Mapinduzi ya Zanzibar.

Golikipa wa Simba Daniel Agyei ndio alikuwa shujaa kwa upande wa Simba hususan kwenye changamoto ya mikwaju ya penati. Agyei ameokoa penati mbili za Deogratius Munishi na Mwinyi Haji huku yeye akifunga penati yake baada ya Mkude kufunga ya kwanza.

Wachezaji wa Simba waliofunga penati: Jonas Mkude, Daniel Agyei, Mzamiru Yassin na Javier Boukungu

Method Manjale ni mchezaji pekee wa Simba aliyekosa penati ambayo iliokolewa na golikipa wa Yanga Deogratius Munishi.

Simon Msuva na Thaban Kamusoko ndio wachezaji pekee wa Yanga waliofunga penati zao huku Deogratius Minish ‘Dida’ na Mwinyi Haji penati zao zilitua kwenye mikono ya golikipa wa Simba Daniel Agyei.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATNO JANUARY TAREHE 11.1.2017




Share:

MOKIWA AKATAA KUJIUZULU NGOMA BADO NZITO

Hali  ya amani ndani ya Kanisa la Anglikana nchini, bado si nzuri baada ya Askofu wa Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk Valentino Mokiwa aliyevuliwa uaskofu kutoa msimamo wake na kudai kuwa yeye ni msafi, na ndio Askofu wa Dar es Salaam, hang’oki hata kwa dawa, na amewasamehe wanaompinga.

Askofu Mokiwa aliyasema hayo kwenye Kanisa la Anglikana Ilala jana, alipozungumza na waandishi wa habari. Alisema licha ya kusemwa mambo magumu, lakini yeye kama Askofu, kazi yake ni kuwaombea waliomkosea na hana matatizo nao, kwani amekwisha wasamehe.

Askofu Mokiwa pia alienda mbali zaidi kwa kudai kuwa Dayosisi ya Anglikana Dar es Salaam haina mgogoro, bali viongozi watano wa dayosisi hiyo ndio wanatengeneza mgogoro huo kwa maslahi binafsi, wakitumia Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Andrea la Magomeni kama njia ya kupitishia migogoro yao.

“Siogopi kusema baba askofu kapotoka katika hili, ameshauriwa vibaya na washauri wake wa kisheria,”alisema Askofu Dk Mokiwa ambaye alimtaja Profesa Palamagamba Kabudi kuwa mshauri wa kisheria wa askofu mkuu.

Kauli hiyo ya Mokiwa imekuja siku chache baada ya kuvuliwa uaskofu, kwa kile kilichoelezwa mashtaka 10 yaliyofunguliwa na walei 32 wa Kanisa hilo Dayosisi ya Dar es Salaam, yakiwemo ya ufisadi wa mali za kanisa, ndio sababu ya Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Dk Jacob Chimeledya kumvua uaskofu.

Hata hivyo, Dk Mokiwa amegomea uamuzi huo, kwa maelezo kuwa mwajiri wake ni Sinodi ya Dar es Saalam, ambayo ndiyo yenye uamuzi wa kumfuta kazi na si askofu mkuu; au askofu mwingine yeyote wa kanisa hilo Tanzania.

Uamuzi wa kumvua uaskofu, ulichukuliwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Askofu Chimeledya baada ya Askofu Mokiwa kugoma kujiuzulu, kama ilivyoshauriwa na Nyumba ya Maaskofu, ambayo ilimkuta na hatia ya kufuja mali za kanisa hilo na kukiuka maadili ya kichungaji, ambayo yalibainishwa kwenye ripoti ya uchunguzi iliyoundwa na kiongozi mkuu wa kanisa hilo nchini.

Akizungumzia suala hilo, Mokiwa alisema, “Alikuja na maaskari zaidi ya 12 ambao wamevaa sare, na wengine ambao hawakuvaa sare sijawajui idadi yake, askofu mkuu alidai amekuja kuleta mrejesho wa halmashauri kuu, na matokeo yake akaishia kusema ameniondoa kwenye huduma ya uaskofu.
"Nimesema siondoki, na nimeona wanasema wataweka kila kitu hadharani, nawambia hivi, mimi ni msafi na sina uchafu sehemu yoyote ile, wawe huru na amani kuanika madudu yangu kama yapo, waweke tu hadharani wala siogopi.

“Ninavyo vyombo  halali kwenye Dayosisi hii ambayo hakutaka kukutana navyo ambavyo ni Halmashauri ya Kudumu, hakuwahi kutaka kuwasiliana na sisi, sisi tulitaka kuwasiliana na yeye, angejibu mawasiliano yetu ya kujenga mahusiano na kutekeleza yaliyoamuliwa, hukutaka kutekeleza leo unakuja na hoja ya kuniaondoa. 
“Halmashauri ya Kudumu inamwambia hatujawahi kumpelekea mgogoro sisi kama Dayosisi ya Dar es Salaam, waswahili wanasema ‘jipu linamsumbua mwenye mwili wake’, hujawahi kupelekewa neno lolote la machafuko, ni nani aliyekwambia Dayosisi ya Dar es Salaam ina migogoro?
 “Askofu anafanya kazi na sisi, askofu ana vyombo vya kutawala, hana mamlaka ya kujiamulia mambo yake mwenyewe, ukisema Dar es Salaam kuna machafuko wewe Askofu Mkuu tunajua unasimama na watu na makundi katika Dayosisi hii. 
“ Yeye ni askofu kama mimi, yeye yupo Mpwapwa, tuna taratibu zetu kama za bendera ukiingia mahali unashusha bendera kidogo, kwa nini Askofu Mkuu afanye kazi na watu ambao sio sehemu ya mamlaka ya Dayosisi ya Dar es Salaam.

“Halmashauri Kuu inamwambia kwa kuwa amekuja na tamko lake bila ya kuwashirikisha, wamemwambia Dar es Salama kuna askofu mmoja tu ni Mokiwa. 
“Yeye kama Askofu Mkuu hakupaswa kucheza nje ya Nyumba ya Maaskofu, mimi pia naingia kwenye Nyumba ya Maaskofu, kuchomoka na kufanya kazi nje ya taratibu, hii sio sawa.

"Askofu Mkuu ana timu yake ya maofisa ambao wamemshauri vibaya, na yote yaliyonukuliwa yote yamekosewa katika kusimamia taasisi, kila taasisi ina uhuru wa kurekebisha pale palipoharibika pasipo kuingiliwa.

“Dayosisi ya Dar es Salaam haina mgogoro na mimi ndio Askofu wake, mgogoro uliopo ni wa kutengeneza, katika timu yake kuna watu wenye ‘interest maalum’ ambao ni Profesa Palamagamba Kabudi, yeye ndio mshauri mkuu wa askofu lakini amekuwa akimpotosha, askofu akikosea na yule ni mwanasheria aliyebobea na ndiye anayeingiza kanisa kwenye migogoro iliyobobea.

“Tumewahi kuandikiwa barua na serikali Kanisa letu ndio vinara wa migogoro, wamekuwa wakitengeneza mgogoro kati ya waumini na maaskofu wasielewane, wakubwa waingie kushika hatamu za uongozi hapa. 
“Nina kibali cha kuzungumzia Dayosisi ya Victoria Nyanza Mwanza, uongozi wa kanisa umeingia pia na kufanya kazi na makundi, kando ya taratibu, kugombanisha askofu na watu wanaowangoza na kusababisha maumivu makubwa, lakini nasema bila kufuata taratibu yeye akiwa kiongozi mkuu, ni hatari sana kiongozi anayeacha kuongoza kwa taratibu na kufuata matakwa yake mwenyewe. "
Ataja majipu 5 ndani ya Kanisa 
Askofu Mokiwa alisema kuwa ndani ya Kanisa hilo, kuna majipu ambayo yamekuwa kiini cha migogoro kila kukicha na kuchafua taswira nzima ya kanisa hilo.

“Askofu Mkuu anashauriwa na Mwanasheria (Profesa Kabudi) anayeheshimiwa na watu wengi, aliyezalisha wanasheria wengi zaidi katika nchi hii lakini halitendei haki kanisa, halisaiidi kusimama sawa sawa, kuliokoa kanisa na mvurugiko, haonekani mara zote kwa kuwa amejificha nyuma ya taratibu hizo.

“Mwingine ni askofu Oscar Mnung’a, Makamu Askofu Mkuu, huyu anakuja kufanya kazi na makundi Dar ili aje kuwa askofu mkuu, alikuwa padri wangu na ni askofu wa Newala, naamini watu wa Mpwapwa na Newala wanawafahamu, kuwa ndio viongozi wao ndio chanzo cha maumivu kwenye kanisa hili.

“Mwingine ni Johnson Chinyong’ole ni Katibu Mkuu, Padri wa Dayosisi ya Morogoro, moyoni mwake anaamini mimi ndiye niliyebana asiwe askofu mkuu, nataka kusema Kanisa Anglikana ni Kanisa kubwa nchi hii, alipaswi kuonekana na dalili yoyote ya migogoro, lina uwezo wa kufanya mambo yake ndani bila ya kuvuana nguo kama ilivyo sasa tena bila ya sababu za msingi.

“Askofu mkuu anafanya kazi na Kanisa la Andrea Mtakatifu Magomeni, kule kuna mtu anaitwa John Mhina, yule alikuwa Padri katika dayosisi yangu na tulimuondolea haki za sakramenti na huduma za kichungaji mikononi mwake, tulifanya hivyo kwa sababu ya kukiuka jambo moja tu la utii. 
“Tulifanya uhamisho katika Dayosisi ya Dar akagoma, akatengeneza tuhuma kwa taasisi moja kubwa ambayo naiheshimu, na sitaki kukosea ikavurugikiwa kwa sababu ya maneno ya kinywa changu, taasisi hiyo sina uchafu nao, na sina uchafu popote.

“Sababu ya Mhina kumuondoa ni kwamba haifai, mtu ni kuhani wa Mungu halafu anaenda kukopa benki na kukimbia vielelezo ninavyo, benki alizokopa ni BOA, Akiba Commercial Bank na Tanzania Investment ambayo iliwahi kumtoa mpaka picha zake.

“Mwingine ni Paul Mtweve alikuwa mkuu wa idara ya Uinjilisti, naye nilimuondoa kwa sababu za kiuaminifu, kulikuwa na Saccos ambayo alijikopesha na sasa imefungwa, wamechafua taswira nzima ya Dar es Salaam na ndio wamekuwa wakitumika na askofu mkuu, ndio wamekuwa vinara wa kutengeneza mashaka. Kuthibitisha kuwa wanafanya kazi na Askofu mkuu, uhamisho wa Mhina, alipopinga kuhama, askofu Mkuu ‘alisapoti’, kwangu mimi kwa Dar es Salama sio tena Askofu, mwaka jana sikukuu ya Matende alisema amehamina Mpwapwa sasa sijui amebaki huko au vipi maana hapa sijamuona.

“Nilisali Ubungo siku ya Krismasi, e-mail zilinaswa ambazo zilikuwa zikisambazwa kwa wanangu wa Magomeni ambao hawakusali Krismasi kwa sababu walipewa taarifa kupinduliwa kwangu, hivyo walijua kutakuwa na mapinduzi. 
“Taasisi za dini hazipaswi kufanya kama hivi ni aibu, waumini wakimbilie wapi wakati wanaamini Kanisa ndio mahali salama. 
“Waumini watulie, kwa jimbo la Dar es Salaam hawatatusikia katika migogoro yoyote, bado nina imani na waumini wa Dayosisi hii, tushikane pamoja, kuifanya kazi ya Mungu. 
“Tuna shule, vituo vya watoto yatima, nataka ninaofanya nao kazi bila njaa, na wale wanaocheza nje ya zizi, warudi kundini nitawakaribisha,” alisema.

Mokiwa alifunguliwa mashtaka 10 Machi 2015 ambayo ni kuizuia dayosisi ya Dar es Salaam, kupeleka michango pasipo maelekezo ya Sinodi ya Dayosisi ya Dar es Salaam, kuhamasisha dayosisi kujitoa katika udhamini wa Kanisa la Anglikana Tanzania (KAT) kwa lengo la kuifarakanisha dayosisi na Jimbo, kinyume na katiba ya dayosisi.

Mashitaka mengine ni kufuja mali za kanisa na kuingia mikataba kiholela yenye viashiria vya rushwa katika eneo la kanisa la Mtoni Buza na miradi mingine, kushindwa kutatua migogoro inayohusu uwekezaji na maadili baina ya dayosisi na mitaa ya Magomeni ambao kuna mgogoro na Benki ya DCB, kanisa la Kurasini na mengine.

Askofu huyo pia anadaiwa kushindwa kutatua migogoro baina ya mapadiri na waumini na kutunza mali za kanisa katika mtaa wa Watakatifu wote Temeke na kutelekeza nyumba ya askofu iliyopo Oysterbay ambako imegeuzwa kuwa yadi ya kuuza magari. 
Pia alilalamikiwa kushitakiwa mahakamani na Marehemu Christopher Mtikila na watu wengine watatu kwa kosa la kuwatishia silaha ya moto na kuwapapasa maungoni mwao bila ridhaa yao kinyume na maadili ya kikanisa.

Askofu Mokiwa pia analalamikiwa kuanzisha taasisi ya MEA Foundation iliyomwezesha kupokea fedha nyingi za wafadhili kwa ajili ya maendeleo ya dayosisi, lakini fedha zimefujwa na hesabu za chombo hazikuwahi kukaguliwa. 
Tuhuma zingine ni kurejea kwa mchakato wa mapitio ya katiba mpya na kuvuruga mchakato wa awali wa maandalizi ya katiba mpya ya dayosisi kwa kutumia fedha za dayosisi na kutekelezwa askofu msaidizi dayososi ya Katanga Kalemi .

Hata hivyo akijibu tuhuma hizo Mokiwa alisema; Nyumba ya Maskofu Oysterbay 
“Ile nyumba haijatekelezwa bali vigae vilikuwa vinaanguka, nina kijana wangu ambae ana matatizo mpaka sasa ni mkubwa lakini hasemi vizuri kuna siku nilimkuta anacheza na nyoka, paa linavuja mvua zikinyesha, ndio niliamua kuhama na sasa naishi nyumbani kwangu Mbezi Luisi. 
“Kuna fedha Sh milioni 60 ambazo zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa nyumba hiyo ikikamilika nitarudi kukaa.

“Silverhok iliyopo Upanga, nyumba haikuwa kwenye hali nzuri jengo halikua salama, ndio maana tuliwahamisha na jengo halijatekelezwa kwani tunataka kulifanya la kisasa kama majengo mengine yanayozunguka eneo lile la Mindu. 
"Fedha za DCB Kuna watu wanaeneza nimekuwa nikilipwa Shilingi bilioni 6 na DCB, huku ndani mimi nimewahi kuunda chombo ambacho kinahusisha DCB Magomeni, wa wawakilishi wa dayosisi, lakini Magomeni wenyewe ndio wanakimbia vikao, DCB ndio waliojenga na ndio wanaolipa Kanisa Dayosisi ya Anglikana.

“Kama ni vita yenye maslahi, fanyeni uchunguzi mjue anayepokea fedha kutoka DCB ni nani, mtapa ukweli kuwa ni Magomeni wenyewe, inashangaza wao ndio wanakula na kushiba lakini ndio wamekuwa wakipiga kelele na kupotosha watu.

“Kwa mikono yangu niliwaidhinishia Sh milioni 200 za ujenzi wa Kanisa lakini mpaka leo halijajengwa, mabati yapo pale yamesimama kama kaburi, hakuna kilichofanyika na hela zimeliwa, waseme yote kwa ukweli na sio kuweka siasa. "
Share:

Tuesday 10 January 2017

VIDEO | Snura - Shindu | Watch/Download


Share:

MAPENZI YAZIDI KUCHUKUA ROHO ZA WATU JIJINI MBEYA

Katika kile kinachoweza kuelezwa kuwa ni ubaya wa mapenzi, kijana mmoja mkazi wa Mbalizi Mbeya amefariki dunia kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi baada ya baba wa mpenzi wake kumvamia kijana huyo na kumshambulia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya DCP Dhahiri Kidavashari amesema kuwa mnamo tarehe 07.01.2017 majira ya saa 03:00 asubuhi katika Kijiji cha Dimbwe kilichopo Kata ya Ulembo, Wilaya ya Kipolilsi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la VARENCY POSTA mkazi wa kijiji cha Dimbwe alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika kituo cha afya Ilembo baada ya kuchomwa kitu chenye ncha kali kichwani na mtu aliyefahamika kwa jina la MISIS EDWARD mkazi wa Dimbwe.

Inadaiwa kuwa chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa mapenzi kutokana na binti wa mtuhumiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na marehemu.

Inadaiwa kuwa mtuhumiwa kabla ya kutenda kosa hilo alimvizia njiani marehemu akiwa anatoka kuangalia mpira na kisha kumchoma kitu chenye ncha kali hali iliyosababisha kutokwa damu nyingi na kupelekea kifo chake akiwa anapatiwa matibabu.

Kidavashari amesema mtuhumiwa amekamatwa na mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa ndugu kwa taratibu za mazishi.

Katika matukio mengine, Kamanda Kidavashari ametoa taarifa nyingine za mauaji ambapo watu wawili wanaosadikiwa kuwa majambazi waliuawa na wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi baada ya kuvamia eneo la wachimbaji wadogo wa dhahabu wakiwa na silaha aina ya Short gun iliyotengenezwa kienyeji kwa lengo la kufanya unyang’anyi na ndipo walizidiwa nguvu na wananchi hao.

Pia amesema mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la NURU ROMAN MWANG’OLELA Mkazi wa Ubaruku Wilaya ya Mbarali na mwenyeji wa Bujela Kisale Wilaya ya Kyela aliuawa kwa kupigwa mawe sehemu mbalimbali za mwili wake na kundi la watu waliojichukulia sheria mkononi kwa tuhuma za wizi.
Share:

Dr. Shein Akerwa na Kauli za Maalim Seif.......Asisitiza Yeye Ndo Rais Halali wa Zanzibar

Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amewataka wananchi visiwani humo kuacha kusikiliza maneno ya propaganda kutoka kwa wapinzani kwa kuwa katu hakuna Rais mwingine atakayeongoza Zanzibar wakati yeye yupo madarakani.

Amesema kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wakipita mitaani na kujinadi kwa wananchi kuwa huenda wakawa marais wakati wowote, huku wakimkataa yeye kuwa si Rais halali wa Zanzibar.

Shein alisema hayo jana baada ya kuzindua soko na ofisi ya Baraza la Mji la Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, ikiwa ni sehemu ya sherehe za miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ingawa Dk Shein hakutaja jina, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ndiye ambaye amekuwa akitoa kauli za namna hiyo na juzi akihutubia mkutano wa kampeni alisema, “Hata wafanye kitu gani mwaka huu msumari umewaganda na hivi karibuni Wazanzibari watafurahia mambo yao mazuri.” 
Alisema mipango imara ya kuhakikisha kuwa mambo hayo yanakaa sawa inakwenda vizuri na wakati wowote matunda hayo yataonekana.

Maalim Seif aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015, aliwataka wananchi na wanachama wa CUF wakae mkao wa kula.

“Sidhani kama nitashindwa ila ikiwa nitaona dalili za kushindwa nawaahidi kuwa nitawaambieni hadharani ili mchukue uamuzi ninyi wenyewe ya kudai haki yenu katika uchaguzi uliopita,” alisema Maalim.

Maalim Seif alifafanua kuwa ni jambo la kushangaza kuona kuwa Dk Shein analazimisha wananchi kumtaja ndani ya misikiti, huku akihoji kama yeye (Dk Shein) ni Rais kwa nini alazimishe kutajwa?

Lakini, jana Dk Shein aliwataka wananchi kuacha kusikiliza na kufuata kasumba hizo za wanasiasa kwa kuwa Serikali tayari imeshaundwa na yeye ni Rais halali wa Zanzibar.

Alisema anashangazwa kuona kuna watu wa aina hiyo wa kuwadanganya wananchi huku wakifikiri kuna watu wa nje wenye uwezo wa kuingilia mambo ya Zanzibar.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger