Saturday 7 January 2017

Picha 8: Muonekano wa sasa wa Jennifer na Patrick walioibuliwa na marehemu Steven Kanumba

Watu wengi watawakumbuka Jennifer na Patrick kwa jinsi walivyoweza kutikisa tansia ya filamu Tanzania kipindi cha nyuma walipoibuliwa na marehemu Steven Kanumba.

Watoto hawa wawili walicheza kwa ustadi mkubwa katika filamu za Uncle JJ na This is It zote za marehemu Kanumba.

Kwa sasa Hanifa Daud ‘Jennifer’ na Othman Njaidi ‘Patrick’ si watoto tena. Wawili hawa hawajaonekana sana kwenye filamu baada ya Steven Kanumba aliyewatoa kufariki.

Jennifer ambaye amehitimu kidato cha nne mwaka jana mara ya mwisho alionekana kwenye filamu ya Zena na Betina ya Salma Jabu a.k.a Nisha mwaka 2014. Kwa upande wake Patrick, yeye alisema kuwa hana shauku ya kuigiza tena kama ilivyokuwa awali.
Credit: Bongo5
Share:

Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya January tarehe 7.1.2017




Share:

Vigogo Wengine Kutumbuliwa TANESCO,Lengo ni kuimarisha utendaji wa Shirika Hilo

Siku moja baada ya vigogo watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kushushwa vyeo, uongozi wa shirika hilo umesema utaendelea na fagio hilo kama njia ya kuongeza ufanisi kwenye utendaji.

Vigogo hao wa ngazi za juu ambao ni wakurugenzi, wamehamishiwa Chuo cha Mafunzo cha Tanesco (TSS) kwa madai kuwa shirika linaboresha ufanisi wake.

Walioshushwa vyeo ni pamoja na Declan Mhaiki aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia usambazaji wa umeme.

Wengine ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji na Huduma kwa Mteja, Mhandisi Sophia Mgonja na Naibu Mkurugenzi Mtendaji Uzalishaji Umeme, Nazir Kachwamba.

Wakati hao wakipitiwa na panga hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu, Watson Mwakyusa, aliamua kuandika barua kuacha kazi mwenyewe.

Juzi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Dk. Tito Mwinuka, alisema jana wangetoa taarifa kuhusu hamisha hamisha hiyo.

Jana mchana Idara ya Kitengo cha Mahusiano cha Shirika hilo, kilitoa taarifa na kusema kuwa wataendelea na hatua mbalimbali za mabadiliko ya uongozi kwa lengo la kuongeza ufanisi zaidi wa kiutendaji.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa mabadiliko yanayoendelea ndani ya Tanesco yatawekwa wazi wakati mwafaka kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za shirika kupitia vyombo vya habari.

Kitengo hicho kilieleza kuwa kwa sasa bado wanaendelea na panga pangua na endapo watakamilisha watatoa taarifa kwa umma.

“Tunaomba vyombo vya habari vitoe fursa kwa mamlaka husika kuendelea kukamilisha zoezi hili muhimu kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla na taarifa rasmi itatolewa baada ya zoezi kukamilika,’’ ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Januari Mosi, mwaka huu, Rais Dk. John Magufuli alimteua Dk. Mwinuka kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, baada ya kumng’oa aliyekuwa mkurugenzi wa shirika hilo, Mhandisi Felchesmi Mramba.

Mramba alitenguliwa uteuzi wake siku mbili baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), kutangaza kuridhia ombi la Tanesco la kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 8.5 kutoka 18 waliyoomba.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Mwinuka alikuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Akiwa mjini Bukoba kwenye ibada ya Mwaka Mpya, Rais Magufuli alisema amekerwa na kusikitishwa na vitendo vya baadhi ya watumishi wa umma kujitokeza hadharani na kutangaza au kuzungumzia mambo ya kitaifa kama uamuzi wa Serikali bila kushirikisha viongozi wao wa ngazi za juu.

Kutokana na hali hiyo, alisema watendaji hao ni miongoni mwa majipu yanayostahili kutumbuliwa.
Share:

Waziri Nchemba: Hatutamhukumu mtu kwa kazi anayoifanya, tutamhukumu kwa kosa analolifanya

Ikiwa imepita siku moja tangu waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba kusema kuwa watakaofanya unyama wa kuua au kuchinja watu au wanyama kwa mapanga na sime wataona chamoto, bado kauli hiyo imekaidiwa kwa baadhi ya watu wanaosadikika kuwa ni wa jamii ya kifugaji baada ya kumjeruhia kichwani kwa sime Rajabu Ayub (36) mkazi wa kijiji cha Mbigiri wilayani kilosa, akiwa shambani kwake na kumsababishia maumivu.

Polisi mkoani Morogoro mpaka sasa inawashikilia watu 24 kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo. Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza nguvu zaidi ya dola iongozwe katika maeneo hayo mpaka mhusika wa tukio hilo atakapopatikana.

Hili ni tukio la pili tangu Waziri Mwigulu awepo mkoani Morogoro la kwanza likiwa la Fabiano Bago mkazi wa kolelo wilaya ya Morogoro ambaye alijeruhiwa maeneo ya kichwani kwa sime na watu wa jamii ya kifugaji mara baada ya kumuona akiongea na simu wakidhani anawataarifu polisi na Fabian alifariki dunia kutokana na majeraha aliyopata
Share:

Marekani kumsaka mtoto wa Osama Bin Laden Aliyeapa Kulipa Kisasi

Marekani imesema kuwa imemuorodhesha mtoto  wa mwisho wa Osama Bin Laden, Hamza, katika orodha ya magaidi wanaosakwa na taifa hilo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema kuwa Hamza Bin Laden ameanza kushiriki katika maswala ya kundi la al Qaeda, kundi la jihad lililofadhiliwa na babake.

Hamza amesema kuwa atalipiza kisasi mauaji ya babake yaliotekelezwa na kikosi maalum cha Marekani kwa kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wamarekani.

Hamza amepigwa marufuku  kufanya biashara na raia wa Marekani huku mali zake zikizuiliwa pia.

Mamake Hamza ni Khairiah Sabar, mmoja wa wake za Osama aliyekamatwa wakati wa shambulio la wanajeshi wa Marekani kwenye maficho ya Osama mjini Abbotabad nchini Pakistan mwaka 2011.

Mkuu wa kitengo cha usalama cha kundi la al-Qaeda Ibrahim al-Banna pia ameongezwa katika orodha hiyo .

Marekani imetoa kitita cha dola milioni 5 kwa mtu yeyote atakayemkamata al-Banna.

Hamza bin Laden alitambuliwa kuwa mmoja wa viongozi wa al-Qaeda mwaka 2015 na baadaye akaapa kulipiza kisasi mauaji ya babake mwezi Julai mwaka uliopita.
 
Katika ujumbe wa sauti wa dakika 21 wenye kichwa "We Are All Osama," (Sote ni Osama), na uliochapishwa katika mitandao, aliapa lazima angelipiza kisasi mauaji ya babake mwaka 2011 nchini Pakistan.

''Tutaendelea kuwasaka na kuwapiga popote pale mtakapokuwa mmejificha ati nyuma ya pazia za usalama kwa maovu mnayoyaendeleza ,Palestina, Afghanistan, Syria, Iraq, Yemen, Somalia na kote kwenye ardhi ya waislamu mnayokalia,'' shirika la habari la Reuters lilimnukuu.

''Na kwa wale wanaodhania kuwa tutakuwa tukilipiza kisasi mauaji ya Osama ole wenu, kwanini sisi tutakuwa tukilinda dini ya kiislamu'' alisema Hamza.

Hamza, kulingana na wachanganuzi, alitambulishwa na kiongozi wa kidini wa kundi la al-Qaeda Ayman al-Zawahiri katika ujumbe huo uliolenga kuwavutia vijana ambao kwa sasa wamejiunga kwa wingi na kundi la Islamic state.

Hamza sasa anaungana na nduguye wa kambo, Saad, kuwa miongoni mwa watu wa jamii ya Osama walioorodheshwa kuwa magaidi.

Chanzo: BBC
Share:

Serikali yapiga marufuku ununuzi wa sare za jeshi la zima moto na uhamiaji toka taasisi binafsi

Naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mhandisi Hamad Yusuph Masaun amepiga marufuku ununuzi wa sare za jeshi la zima moto na uhamiaji kwa taasisi binafsi na badala yake ameagiza sare hizo zizalishwe katika viwanda vya jeshi la magereza nchini.

Mhandisi Masauni ameyasema hayo baada ya kutembelea kiwanda cha jeshi la magereza kilichopo Ukonga kinachoendeshwa kwa nguvu kazi ya wafungwa ikiwa ni ufuatiliaji, utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania la kulitaka jeshi hilo liwasimamie wafungwa katika uzalishaji wa sare.

“Kuanzia leo uhamiaji,zima moto wote washone nguo, kama ambavyo magereza wanashona katika kile kiwanda, kwamba dhamira ya mheshimiwa rais ya kutoa maelekezo ambayo yamefuatilia utendaji kazi wake nimeridhika, kwamba ni marufuku kama alivyosema mheshimiwa rais kwa askari Magereza na askari wote wa vyombo vya usalama nchini kununua uniform kwa raia, jeshi la magereza linatengeza furniture zenye ubora wa hali ya juu,” alisema Mhandisi Masauni.
Share:

Lowassa Atajwa Kusababisha Deni la Milioni 1

Jina la waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa limetajwa na mkaazi mmoja wa Mbeya mbele ya Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla kuwa sababu ya deni la shilingi milioni moja kutokana na mapenzi ya wafuasi wake.

Mkaazi huyo wa kata ya Ruanda Nzovwe aliyejitambulisha kwa jina la Amos Mwakyambiki alidai kuwa wafuasi wa Chadema waliharibu paa la nyumba yake walipopanda kwa lengo la kufuatilia mkutano wa Lowassa wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana, na kwamba chama hicho kilimuahidi kumlipa fidia ya shilingi milioni moja lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa.

Alimueleza mkuu wa mkoa huo kuwa kutokana na uharibifu huo mkubwa uliofanyika, wapangaji wake waliamua kuhama nyumba yake hivyo kukosa kipato.

“Naomba Serikali ya Mkoa inisaidie kuzungumza na meya (wa Chadema) ili niweze kulipwa stahiki zangu kwani sasa sijui hatma yangu. Kuku niliokuwa nauza kwa ajili ya kupata nauli kwenda ofisi za jiji wamekwisha,” Mkaazi huyo anakaririwa.

Kutokana na madai hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alimuagiza Mkuu wa Wilaya kufuatilia suala hilo huku akitahadharisha wananchi kuhusu matumizi ya nyumba zao wakati wa kampeni.

“Lakini na nyie wananchi msikubali nyumba zenu zibadilishwe kuwa viwanja vya siasa,” alisema Makalla.

Akizungumzia taarifa hizo, Mkuu wa Idara ya Habari ya Chadema, Tumaini Makele alisema kuwa chama hicho kitafuatilia kuona ni nani aliyetoa ahadi hiyo kwa mwananchi huyo na ilikuwa katika mazingira gani ili walifanyie kazi ipasavyo.
Share:

Friday 6 January 2017

MAJINA YA WALIOPATA MKOPO SUA AWAMU YA 10 NA 11 2016/2017

Share:

Magazetini Leo Ijumaa Januari 6, 2017


https://mpaper.s3-us-west-2.amazonaws.com/mpaper_1483644803_586e9f839540f/mpaper_1483644803_586e9f839540f.jpg
Share:

Watu 11 wapoteza maisha katika ajali ya barabarani Kisumu


media
Ajali za barabarani zimekithiri, Watu 11 wapoteza maisha katika ajali ya barabarani Kisumu, nchini Kenya.
Watu 11 wamepoteza baada ya kutokea kwa ajali ya barabara katika Kaunti ya Kisumu Magharibi mwa Kenya. Ajali za barabarni zimekithiri katika nchi za Afrika hasa afrika ya Mashariki
Kamishena wa Kaunti ya Kisumu, Mohammed Maalim amesema chanzo cha ajali hiyo ilikuwa ni mwendo wa kasi wa gari la abiria maarufu kama Matatu ambalo pia lilikuwa limejaa kupita kiasi.
Ripoti zinasema kuwa, gari hilo la abiria lilikuwa linatoka katika mji wa Sirare karibu na mpaka wa Tanzania kwenda mjini Kisumu likiwa na idadi kubwa ya abiria.
Inaarifiwa kuwa gari hilo liliondoka barabarani na kuanguka shimoni katika eneo la Nyakatch, asubuhi ya leo.
Serikali ya Kaunti hiyo inasema inachunguza ni kwanini gari hilo lilikuwa na abiria wengi.
Ajali nyingine kama hii ilitokea jijini Kampala nchini Uganda Jumatano wiki hii na kusababisha vifo vya watu 14
Share:

Ajinyonga kwa kunyimwa na mkewe samaki mbichi




MKAZI mmoja wa kijiji cha Kalundi kilichopo kata ya Kipande wilayani Nkasi, Vedast Kazumba (51) amejiua kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa kuwa alighadhabika, baada ya mkewe kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, George Kyando alithibitisha tukio hilo.

Alisema ni la usiku wa mkesha wa Mwaka Mpya na kwamba Kazumba alifikia uamuzi huo mgumu kwa kujinyonga akitumia kamba ya katani .

Alieleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na polisi kuhusu tukio hilo na uchunguzi wake unaendelea . Habari kutoka kijijini humo, zinaeleza kuwa chanzo cha Kazumba kujinyonga ni kukasirishwa na kitendo cha mkewe, Antoniata Mwisua kumnyima kitoweo cha samaki mbichi.

“Mke wa marehemu aitwae Antoniata alimwandalia mumewe huyo chakula cha usiku, kitoweo chake kikiwa ni samaki mbichi alimkomba samaki huyo kisha akamwomba amwongezee kitoweo kingine cha samaki, lakini mkewe alimweleza kuwa kitoweo hicho kimekwisha. Ndipo mumewe alipokasirika akidai kuwa mkewe amemnyika kwa makusudi kitoweo hicho ndipo alipochukua hatua ya kuzira kula“ alieleza mmoja wa mashuhuda kwa masharti ya kutoandikwa gazetini.

Akizungumzia mkasa huo , Mwenyekiti wa Kijiji cha Kalundi , John Kalasa alidai kuwa marehemu wakati wa uhai wake alikuwa ni mtu mwenye kujawa na ghadhabu ambapo mara kadhaa alisikika akitishia kujinyonga.
Share:

Amuua mkewe kwa nyundo Kisa Wivu wa Mapenzi


Mwanamke mmoja mkazi wa Mikumi wilayani Keya, Mbeya aliyefahamika kwa jina la HILDA SIGARA  amefariki dunia akiwa anapelekwa Hospitali kwa matibabu baada ya kupigwa nyundo kichwani na mume wake aitwaye REBSON TWEVE umri kati ya miaka 30 – 35

Kamanda wa polisi mkoani humo DCP Dhahiri Kidavashari amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 05.01.2017 majira ya saa 12:00 asubuhi ambapo imedaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi kwani inasadikiwa mtuhumiwa alikuwa akimtuhumu marehemu kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine.

Amesema katika eneo la tukio kumekutwa nyundo moja, kisu kimoja na fimbo ya muanzi ambavyo vinasadikiwa kutumika katika tukio hilo.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya Kyela ukisubiri kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu na upelelezi unaendelea huku mtuhumiwa akiwa ametoroka mara baada ya tukio na juhudi za kumtafuta zinaendelea.

Aidha, katika matukio mengine kamanda huyo amesema kuwa jeshi la polisi limepokea taarifa za kujinyonga kwa watu wawili ambao miili yao imekutwa ndani ya nyumba zao katika maeneo tofauti.

Watu hao ni pamoja EDWARD PETER  mfanyabiashara na Mkazi wa Majengo na aliyekutwa amekufa chumbani kwake huku mwili wake ukiwa hauna majeraha yoyote, na mwingine ni ROBERT MWAISENYE Mkazi wa Mbugani wilayani Chunya ambaye alikuwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya manila akiwa ndani ya nyumba yake
Share:

Marekani: Ilikuwa ajabu Urusi kuingilia uchaguzi wa 2016



Urusi inalalamikiwa kudukua taarifa za uchaguzi wa Marekani 2016
Image captionUrusi inalalamikiwa kudukua taarifa za uchaguzi wa Marekani 2016
Mkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper, kitendo cha Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani mwaka uliopita kilikuwa cha ajabu kushuhudia katika utendaji kazi wake.
Akizungumza katika Baraza la senate Nchini Marekani, Clapper amesema udukuzi huo wa barua pepe za chama cha Democratic kuelekea uchaguzi uliofanyika mwezi Novemba ulisimamiwa na Raisi wa Urusi Vladimir Putin, na kuongeza kuwa atatoa taarifa kamili kwa umma wiki ijayo.
Mkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper
Mkurugenzi wa usalama wa Marekani James Clapper
Clapper amesema kuwa ifikapo ijumaa atatoa mchanganuo wa tafiti zake kwa Rais mteule wa Marekani Donald Trump aliyewahi kulaani na kutilia shaka ushiriki wa Moscow.
Urusi pia imekanusha madai ya kuhusika katika udukuzi huo.BBC
Share:

5,219 wafa ajali za barabarani



AJALI za barabarani katika mkoa wa Dar es Salaam, zimeongezeka kutoka 3,710 kwa kipindi cha Januari hadi Desemba mwaka 2015 hadi kufikia ajali 5,219 kwa kipindi kama hicho mwaka jana.
Hilo ni ongezeko la ajali 2,009 ambazo ni sawa na asilimia 36.5. Aidha kuna ongezeko la vifo 9 ambapo kwa kipindi kama hicho mwaka 2015 vilitokea vifo 316 ikilinganishwa na vifo 325 vilivyotokea mwaka jana ambavyo ni sawa na ongezeko la asilimia 2.7.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya usalama barabarani kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Desemba 2016, ikilinganishwa na Januari hadi Desemba mwaka 2015.
“Pia kuna ongezeko la watu 654 waliojeruhiwa kwani Januari hadi Desembwa mwaka 2016 walijeruhiwa watu 4,066 ukilinganisha na watu 3,412 waliojeruhiwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2015 sawa na asilimia 16” alisema.
Alisema kwa upande wa makosa yaliyokamatwa, kuna ongezeko la makosa 382,207 kwani katika kipindi kama hicho mwaka jana yalikamatwa makosa 769,170 yaliyoiingizia serikali maduhuli ya Sh 23,065,020,000 ikilinganishwa na makosa 386,963 yaliyoiingizia serikali maduhuli ya Sh 11,608,700,000 kwa mwaka 2015, ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 49.6.
Takwimu za ajali za pikipiki, zimeonesha kuna upungufu wa ajali 168. Kwa kipindi kama hicho mwaka jana zilitokea ajali za pikipiki1036 ikilinganishwa na ajali 1,204 zilizotokea mwaka 2015 ambazo ni sawa na asilimia 13.9.
Sirro alisema kwa upande wa vifo vilivyotokana na ajali za pikipiki vimepungua kwa idadi ya watu nane kwani Januari hadi Desemba mwaka jana watu 80 walifariki kutokana na ajali za pikipiki ikilinganishwa na watu 88 waliofariki mwaka 2015 sawa na upungufu wa asilimia tisa.
Pia alisema majeruhi wa ajali za pikipiki nao wamepungua watu 225 kwani Januari hadi Desemba 2016 walijeruhi watu 904 ikilinganishwa na watu 1,129 waliojeruhiwa mwaka 2015 ambao ni sawa na asilimia 20.
Share:

Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Humprey Polepole atangaza neema kwa Wanafunzi waliokosa mikopo


 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM, Humprey Polepole amewatangazia neema wanafunzi wa elimu ya juu waliokosa mikopo, akiwataka wamtafute ili awaoneshe cha kufanya

Polepole ambaye alikuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni cha EATV  aliuzwa na baadhi ya watu kuhusu tatizo lililopo la mikopo ya elimu ya juu, ambapo aliwajibu kuwa serikali imekwishatoa maelekezo kwamba haiwezi kumkopesha kila mtu na kwamba inatoa mikopo kwa vigezo vilivyowekwa.

Kuhusu watu wasioweza kujigharamia elimu hiyo na wamekosa mikopo, amewashauri kuahirisha masomo yao, ili wafanye kazi ambazo zitawasaidia kupata pesa na ndani ya mwaka mmoja ana uhakika watakuwa wamepata pesa zinazohitajika na kuendelea na masomo yao.

Polepole alitaja baadhi ya shughuli ambazo angewashauri wazifanye kuwa ni pamoja na kilimo huku akitolea mfano baadhi ya watu aliowashauri wajiingize kwenye kilimo cha matikiti na wakaufanyia kazi ushauri huo, ambapo baada ya muda wameona matunda yake.

"Waliokosa mikopo vyuo vikuu wanitafute, nitawaonesha cha kufanya, na wawe tayari kuahirisha masomo mwaka mmoja"

Akizungumzia uamuzi wa serikali kusimamisha ajira, Polepole amesema serikali haiwezi kuendelea kuajiri wakati inafanya kazi ya kuondoa wafanyakazi hewa ambao wanalitia hasara taifa na kuwataka watanzania waendelee kuwa watulivu na kumuunga mkono Rais Magufuli, ili amalize mchwa wote serikali na kisha ajira zitatoka.

"Nawaambia vijana wakati unasubiri ajira usibweteke kwani mtu anayebweteka akipata kazi ataharibu kazi yetu"

Kuhusu serikali kuajiri walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati pekee, Polepole amesema uamuzi huo ni sahihi kwa kuwa taifa lina uhaba mkubwa wa walimu wa Sayansi na Hisabati kuliko walimu wa masomo ya sanaa.

"Tunao utimilifu wa walimu wa sanaa, tunao upungufu wa walimu wa Sayansi"
Share:

Thursday 5 January 2017

Waziri Mkuu aonya ujenzi holela Manispaa Kigamboni

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger