Monday 2 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARY TAREHE 2.1.2017

Share:

LOWASA APONGEZA USHINDI WA TRUMP

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, amewapongeza raia wa Marekani kwa kumchagua Donald Trump kuwa rais mpya wa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa Lowassa, Trump atakuwa rais mwenye kufanya uamuzi mgumu kwa kuwa ni shupavu na ana uwezo.

Trump ambaye ni Rais Mteule wa Marekani, alichaguliwa kuwa Rais mpya wa Marekani baada ya kumshinda mpinzani wake, Hillary Clinton, mwishoni mwa mwaka jana.

Lowassa aliyasema hayo jana katika misa maalumu ya shukrani ya mwaka mpya 2017 iliyoshirikisha madhehebu mawili ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Monduli na Kanisa Katoliki, wilayani Monduli, Mkoa wa Arusha.

Ibada hiyo, ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo wa Serikali na wa vyama vya siasa, wakiwamo Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye pia ni Katibu wa Chadema, Mkoa wa Arusha.

“Wamarekani hawakufanya makosa kumchagua Trump kwani anaonekana kuwa na uwezo mkubwa wa kuongoza Taifa hilo tajiri duniani ambalo linategemewa na mataifa mengine.

“Dunia imebadilika, amechaguliwa rais mmoja huko Marekani ambaye ni mwamba kweli kweli.

“Hatuwezi kumtabiri mambo yake yatakavyokuwa, lakini inabidi kila mtu afanye kazi kwa bidii na kwa maarifa kwa sababu huyo hakubali upuuzi wowote,”alisema Lowassa.

Lowassa ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Monduli kwa miaka 20, aliwataka wananchi kufanya kazi kwa bidii na kuacha kulalamika kwani hiyo ndiyo njia iliyo sahihi ya kuweza kuondokana na umasikini.

“Mwaka jana, tarehe kama hii, tulimuaga Mbunge Julius Kalanga na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli, Isack Joseph, nikawaambia nawatakia heri wachape kazi vizuri, naona wamefanya vizuri au siyo?alihoji Lowassa.

Akizungumzia upande wake, Lowassa alisema hivi sasa anafanya siasa za kimataifa tofauti na siasa alizokuwa akifanya kipindi kilichopita.

“Mimi sitaki kusema sana maana watasema napiga siasa. Siku hizi napiga siasa za kimataifa, naomba niwatakie heri ya mwaka mpya na kila mtakachoshika, Mungu akibariki kiwe dhahabu,”alisema
Share:

Tulia: Tanzania mpya inawezekana

Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson amesema kuwa Tanzania mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 iwapo inawezekana  iwapo kila mmoja wetu atafanya kazi kwa bidii ili kuliletea taifa maendeleo.

Ameyasema hayo wakati wa ibaada maalum  ya mkesha wa kitaifa wa mwaka mpya uliofanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam, Dk. Tulia amewataka watanzania kuwa na ushirikiano wa pamoja ili kufikia maendeleo.

“Tanzania mpya na nchi mpya yenye matokeo chanya kwa mwaka 2017 inawezekana hivyo tushirikiane kwa pamoja na kila mmoja akifanya kazi kwa bidii, lazima maendeleo yatapatikana tu”amesema Dk. Tulia.

Aidha, amewataka watanzania kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali ili waweze kupata maendeleo kwa haraka zaidi.
Share:

Sunday 1 January 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARY TAREHE 1.1.2017

Share:

MWANAFUNZI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MFANYABIASHARA TARIME



MFANYABIASHARA Robert Mwikwabe, maarufu kama Ndugu, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga risasi ya kichwani na kusababishia kifo papo hapo mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya sekondari Sirari, Masaite Mrimi(17).
Kutokana na tukio hilo, Mwikwabe ambaye pia ni mmliki Hoteli katika mji mdogo wa Sirari wilayani Tarime mkoani Mara, alinusurika kuteketezwa yeye na familia yake Hali hiyo ilitokea baada ya wananchi kuamua kuchoma moto lori la mfanyabiashara huyo na kwenda nyumbani kutaka kuchoma hoteli.
Mashuhuda walisema tukio hilo ni la juzi mchana, jirani na nyumba anayoishi mwanafunzi huyo, eneo la stendi mpya ya mabasi na malori ya Ngerengere.
Walisema mfanyabiashara huyo alifika akiwa na lori lake likiwa na mawe na alisimama na kutaka kuchukua pumba za mchele, zilizomwagwa na malori yanayosafirisha ng’ombe kwenda nchini Kenya.
Eneo hilo ni jirani na nyumbani kwao marehemu, ambako kulitokea mzozo kati ya Robert na wazazi wa mwanafunzi huyo. Kufuatia mzozo huo, mwanafunzi huyo aliyekuwa na panga mkononi, alimtishia kumkata Robert, ambaye alichomoa silaha yake aina ya bastola na kumpiga risasi kichwani na kumsababisha kifo.
Baada ya tukio hilo, familia ya marehemu na wananchi walianza kumfukuza Robert aliyeacha lori lake likiwa na mawe na kukimbilia lori lake lingine la jirani. Kisha alikimbilia Kituo cha Polisi Sirari, kuokoa maisha yake.
Umati mkubwa wa watu kutoka vijiji vya Ngerengere na Sirari, walikwenda nyumbani kwa mfanyabiashara huyo kwa lengo la kutaka kuchoma moto hoteli na nyumba.
Lakini, polisi na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga walifanya juhudi kubwa kuwazuia wananchi hasa vijana, kuacha kuteketeza mali za mfanyabiashara huyo yakiwemo magari, ambayo sasa yamehifadhiwa kituo cha polisi kwa ajili ya usalama.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Tarime-Rorya, Andrew Satta alithibitisha kutokea kwa kifo cha mwanafunzi huyo na kwamba maiti imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya Tarime.
Share:

ATUMBUKIA GHAFLA KWENYE CHEMBA YA MAJI TAKA YENYE UREFU WA FUTI 12 DAR


Mkazi wa Temeke Mikoroshoni, Miradji Sanyero, jana alipatwa na mkasa wa kutumbukia katika ‘chemba’ ya kupitishia maji taka yenye urefu zaidi ya futi 12, iliyopo eneo la Bakhresa, Tazara, Barabara ya Mandela jijini Dar es Salaam.
Alipatwa na mkasa huo akiwa katika harakati ya kujitafutia maisha, ambapo ghafla alitumbukia katika chemba hiyo iliyokaa vibaya katika mlango mkuu unaotumiwa na magari makubwa wa ofisi za Bakhresa.
Akijojiwa, akiwa mahututi, alisema “Nilikuwa napita jirani huku nikichukua tahadhari nisigongwe na magari yanayoingia na kutoka katika ofisi hizo, ndipo nikajikuta ghafla nimetumbukia ndani ya chemba hii na kuumia kidole cha mkono wa kulia, miguuni na mbavu ambazo sasa zinauma sasa”.
Wafanyabiashara wadogo (machinga) wa eneo hilo, walisema chemba hiyo ni hatari na watu kadhaa wametumbukia katika kipindi cha hivi karibuni. Walidai huyo alikuwa mtu wa tatu.
“Tunaomba Tanroads wafike eneo hili, waone kisha wazibe chemba hii. Kama hawatafanya hivyo, kuna hatari ya kupoteza maisha hasa watoto wadogo ambao uwezo wao wa kuhimili vishindo ni mdogo sana” alisema machinga mmoja, Ali Tematema.
Gazeti hili lilishuhudia baadaye trafiki wakishirikiana na wananchi, wakimsaidia Sanyero kwenda kupanda bajaji kwenda Polisi kuchukua Fomu Namba 3 ili aende hospitali kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Chanzo-Habarileo
Share:

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MWANDISHI WA HABARI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA AGIZO LA DC KAHAMA


 


TAARIFA KWA UMMA

UONGOZI wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Shinyanga (SPC),na baadhi ya waandishi wa habari wilayani Kahama,wamekutana na mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu ili kupata muafaka wa tatizo la kukamatwa na kufikishwa mahakamani mwandishi wa habari wa kujitegemea Paul Kayanda.

Kikao hicho cha usuluhishi kilichofanyika leo Jumamosi Desemba 31,2016 katika ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo,kimehudhuriwa pia na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya Kahama. 


Kayanda alikamatwa jana Desemba 30,2016 na kufikishwa mahakamani kwa agizo la Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akimtuhumu kuandika habari za kumdhalilisha na kuzisambaza kwenye barua pepe mbalimbali za vyombo vya habari.


Katika kikao ,Uongozi wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga ,ulimuomba mkuu wa wilaya Nkurlu kutaka kufahamu kilichomsukuma kuchukua maamuzi hayo,na nini ushauri wake juu ya suala hilo lakini pia kumsikiliza mwandishi Paul Kayanda.


Baada ya kusikiliza pande zote mbili,kikao kilibaini kuwepo kwa mapungufu katika habari iliyoandikwa na Kayanda kuhusu habari ya laptop mbili zilizoibiwa nyumbani kwa mkuu huyo wa wilaya.

Mkuu huyo wa wilaya alikiri kuwepo kwa tukio la wizi nyumbani kwake lakini mwandishi huyo aliandika habari kwa kuingilia uhuru binafsi wa kiongozi huyo akielezea watu wanaoingia na kutoka nyumbani kwake lakini maisha anayoishi na kijana wake.


Kwa kuangalia maslahi mapana ya umma kutokana na kutegemeana katika kusukuma maendeleo ya jamii baina ya uongozi wa serikali na waandishi wa habari ,kikao kimemtaka Kayanda kumwomba radhi mkuu huyo wa wilaya kwa kuingilia uhuru wake binafsi na kuuhusisha na habari ya wizi wa laptop badala ya kujikita kwenye tukio la wizi wa laptop pekee.


Kikao pia kimebaini kuwa pamoja na mapungufu ya mwandishi, ni ukweli ulio wazi kuwa mkuu huyo wa wilaya aliibiwa kompyuta mpakato (lap top) mbili nyumbani kwake na kuagiza vijana watatu wakamatwe kwa mahojiano polisi akiwemo mmoja anayeishi nyumbani kwake japo ameelezea kuwa hakujua walishikiliwa kwa siku ngapi.


Mkuu huyo wa wilaya pia alieleza kukerwa na ujumbe mfupi wa maandishi kwa njia simu ya mkononi (sms) alizodai kutumiwa na Kayanda kwa kutumia simu nyingine (tofauti na anayotumia) zenye lugha ya kumtuhumu na kumdhalilisha.

Hata hivyo kikao hakikuona kuwepo kwa ushahidi wa moja kwa moja kuthibitisha kama ni za mwandishi huyo kweli au la huku kikao kikiomba sms hizo zifuatiliwe ili wamiliki wa namba hizo wajulikane .


Baada ya kujadiliana kwa kina katika kikao hicho kilichodumu kwa muda wa saa mbili,Kayanda amemwomba mkuu wa wilaya msamaha kwa mapungufu yaliyojitokeza katika habari hiyo aliyoiandika, na mkuu wa wilaya ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kahama amekubali kumsamehe mwandishi huyo akiahidi kufuata taratibu zingine kuondoa kesi mahakamani na kutaka kusafishwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ilikoandikwa habari hiyo.


Nkurlu amesema anatambua kazi nzuri inayofanywa na waandishi wa habari wilaya ya Kahama na mkoa wa Shinyanga kwa ujumla katika kuandika habari zinazohusu serikali na akaomba kudumishwa kwa ushirikiano uliopo baina ya viongozi wa serikali na waandishi wa habari ili kusaidia kuharakisha maendeleo ya wananchi huku akiwasisitiza waandishi wa habari kuzingatia weledi katika kazi zao.

Aidha Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga imewasisitiza waandishi wa habari kuzingatia weledi na kufuata maadili katika kutekeleza majukumu yao ili kuepuka migongano isiyokuwa na tija kwa umma.

Pia tunawashauri wadau wote wa habari pindi inapotokea kuingia katika mgogoro wowote ama na waandishi wa habari au chombo cha habari si vyema kwenda mahakamani moja kwa moja bali wawasiliane na viongozi wa klabu za waandishi wa habari katika mkoa husika ili kusuluhishana na kuwekana sawa.

Imetolewa na 

Kadama Malunde

MWENYEKITI –SPC

Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu,waandishi wa habari na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kahama wakiwa katika kikao cha usuluhishi
Waandishi wa habari wakiwa katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kahama
Kikao kinaendelea
Waandishi wa habari wakiondoka katika ofisi ya mkuu wa wilaya baada ya kikao kumalizika

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala, Ushauri n.k.?Basi Wasiliana Nasi Simu/WhatsApp 0757478 553 ,0625 918 527

Malunde1 blog Ipo Play Store…Download HAPA ,Uwe unapata habari kwa urahisi zaidi
 Bofya Hapa
Share:

Soma habari hizi pia:

TAFUTA HABARI HAPA

Harusi- Itendele Mchenya

HABARI KALI ZAIDI 2016

Kali ya Mwaka: NYOKA WA MAAJABU AFA NA MTU WAKE,ALIKUWA AMEMBEBA KWENYE NGUO YAKE

NB-Siyo nyoka aliyeuawa DUNIANI kuna mambo, ndivyo unaweza kusema kutokana na mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis K...

Tazama Video Hapa

 Bofya Hapa

Ngoma ya Asili:MANJU MATEMBA IGOMWASHU -BENI

HABARI KALI MWEZI HUU

UNGANA NASI HAPA

MAKTABA YETU

Instal Malunde1 blog kwenye simu yako

 Bofya Hapa

Translate This Blog

Powered by Google TranslateTranslate
Share:

Saturday 31 December 2016

MAGAZETI YA LEO TZ NA NJE,DEC 31 2016

Share:

Basi la National Express lapata ajali Singida....Wawili Wafariki, 26 Wajeruhiwa

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 26 kujeruhiwa kwenye ajali iliyohusisha basi la kampuni ya National Express T.662 DEF, baada ya kuacha barabara na kupinduka zaidi ya mara tatu katika eneo la kijiji cha Tumuli, wilaya ya Mkalama mkoani Singida.

Waliofariki ni dereva wa basi hilo Athumani Idd (47) mkazi wa Mabibo jijini Dares Salaam na mwalimu wa shule ya msingi Malunga aliyefahamika kwa jina moja la Janet (anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 29).

Habari zilizopatikana jana eneo la tukio, zimedai kuwa katika siku za hivi karibuni mwalimu Janet alimpeleka mama yake jijini Dar es salaam kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Imedaiwa kuwa baada ya kufika Dar es Salaam, aligundua kuwa amesahau kuchukua kadi ya bima ya afya, na hivyo akalazimika kurudi Iramba.

Jana asubuhi Janet alichelewa basi la National Express katika kituo cha Kyengenge na kuamua kukodi bodaboda kulifukuzia basi hilo na kufanikiwa kulikuta kituo cha Malunga. Baada kupanda basi hilo, dakika chake baadae, basi hilo lilipata ajali na kulaliwa na basi kichwani.

Watu hao wamefariki dunia papo hapo na miili yao ipo katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida. Basi hilo lilikuwa linatokea New Kiomboi, likielekea jijini Dar.

Akizungumza kwenye eneo la tukio, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida , ACP Debora Daudi Magiligimba, alisema ajali hiyo imetokea Desemba, 30 saa 12.45 asubuhi katika eneo la kijiji cha Tumuli.

Alisema ajali hiyo pia imesababisha majeruhi 26 ambao wamelazwa katika hosipitali ya mkoa kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Kamanda Magiligimba alisema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa ajali hiyo kwa kiwango kikubwa imesababishwa na mwendo kasi na uzembe.

“Eneo hili ilipotokea ajali hii kuna mteremko na kona kali. Kutokana na mwendo kasi, dereva alishindwa kulimudu na hivyo kuacha barabara na kuingia kwenye korogo la mto, na kuruka juu kisha kupinduka mara tatu,” alisema.

Kwa upande wake mganga mkuu mkoa wa Singida, Dk. John Mwombeki, alikiri kupokea miili ya watu wawili waliofariki dunia kwenye ajali ya basi la National Express, pamoja na majeruhi 26.

“Kati ya majeruhi hawa, mmoja dada Joyce tumempa rufaa kwenda hospitali ya taifa Muhimbili kutokana na sehemu yake ya mwili ya chini kutokufanya kazi. Majeruhi 10 wao tunaendelea kuwafanyia uchunguzi” alisema Dk. Mwombeki.

Mmoja wa majeruhi hao mfanyakazi wa shirika la TBC jijini Dar es Salaam, Victor Elia, alisema pamoja na kupoteza kila kitu, anamshukuru Mungu kwa kupona kufa kwenye ajali hiyo mbaya.

“Kilichonisaidia ni kufunga mkanda … abiria wenzangu wote ambao hawakufunga mikanda ndio walioumia zaidi wakiwemo waliopoteza maisha. Ajali hii kwa vyovyote imechangiwa na mwendo kasi,” alisema Victor ambaye ni mtayarishaji na mtangazaji wa TBC.

Kondakta wa basi hiyo, Nicolaus Apolinari (23) mkazi wa jijini Dar es Salaam, alisema ajali hiyo imechangiwa na utelezi uliosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha katika eneo hilo.
Share:

Kamanda Sirro Katoa Tathmini ya Uhalifu Dar kwa Mwaka Mmzima wa 2016

KIKOSI cha Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imekamata jumla ya watuhumiwa 13,626 na kuwafikishwa mahakamani kwa tuhuma mbalimbali, ikiwemo dawa za kulevya na ujambazi wa kutumia silaha kwa kipindi cha mwaka mmoja wa 2016.

Aidha, hali ya uhalifu wa kutumia silaha katika jiji la Dar es Salaam umepungua, ukilinganisha na mwaka uliopita wa 2015 na matukio yanayoongezeka kwa wingi ni ya ubakaji na ulawiti.

Akitoa tathmini ya mwaka mmoja, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema jana kuwa matukio ya unyang’anyi wa kutumia silaha yamepungua kutoka 204 mwaka jana hadi 127 mwaka huu.

Idadi hiyo ni pungufu ya matukio 77, sawa na asilimia 37.7 huku matukio ya kutumia nguvu yamepungua kutoka 1,181 mwaka jana hadi 874 sawa na asilimia 26.

Kamishna Sirro alifafanua kuwa matukio ya mauaji, yamepungua kwa asilimia 11 ukilinganisha na mwaka jana, ambapo kulikuwa na jumla ya matukio 327 wakati kwa mwaka huu ni matukio 291 pungufu ya matukio 36.

Alisema matukio ya ubakaji, yameongezeka kutoka 972 mwaka jana hadi 1030 mwaka huu, sawa na asilimia sita wakati matukio ya ulawiti yameongezeka kutoka 310 mwaka jana hadi 383 mwaka huu sawa na asilimia 23.5.

‘’Kwa matukio ya ubakaji yaliyoongezeka ni 58 na ulawiti matukio yaliyoongezeka ni 73. Lakini wizi wa watoto umepungua kutoka 26 mwaka jana hadi matukio 19 mwaka huu sawa na asilimia 27,’’ aliongeza.

Kwa mujibu wa Sirro, matukio ya uvunjaji yamepungua kwa asilimia 5.7 ambapo kwa mwaka jana kulikuwa na matukio 5,677 na mwaka huu matukio 5,355 sawa na upungufu wa matukio 322.

Kwa upande wa wizi wa magari, umepungua kwa asilimia 18.1 kutoka matukio 392 hadi 321 mwaka huu huku wizi wa pikipiki ukipungua kutoka pikipiki 2,644 mwaka jana hadi 2,191 ambapo matukio 453 yamepungua sawa na asilimia 17.1.

Wizi wa mifugo umepungua kutoka 197 mwaka jana hadi 163 mwaka huu sawa na asilimia 17.3 ikiwa ni pungufu ya matukio 34.

“Sababu za kuongezeka au kupungua kwa matukio hayo kumetokana na juhudi za polisi wa kuzuia na kupambana na uhalifu kwa kufanya doria pamoja na misako mbalimbali iliyosaidia kukamatwa kwa wahalifu wa makosa mbalimbali pamoja na raia wema ambao wametoa taarifa za siri ili kugundua makosa hayo,’’ alieleza Sirro.

Akielezea watuhumiwa hao, Sirro alisema kuwa kati yao 52 walikutwa na silaha za kivita 67 na risasi 1,076, na watuhumiwa 126 walikutwa na dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 75 na gramu 254.

Pia alisema kuwa watuhumiwa 7,625 walikutwa na bangi kilo 2,843 na gramu 78 huku watuhumiwa 269 walikutwa na cocaine kilo tatu na gramu 255 na heroine kilo moja na gramu 654.

‘’Watuhumiwa 5,627 walikutwa na pombe haramu ya gongo lita 8,547 na mitambo 34 na tuliwafikisha mahakamani. Pia tumekamata wahamiaji haramu 105 kutoka mataifa mbalimbali ambao hawana kibali cha kuingia na kuishi nchini,’’ alisema Sirro.

Katika hatua nyingine, Sirro alisema kuwa jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu wanne wakiwa na gari moja aina ya Noah lenye namba za usajili T 188 CZN rangi nyeupe ambalo liliibwa mkoani Kilimanjaro.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Erasto Edward (36), mkazi wa Kawawa Moshi, Wilson Kapori (37) mkazi wa Njia Panda Himo mkoani Kilimanjaro, Hussein Issah (32) mkazi wa Chanika na David Marwa mkazi wa Pugu Kajiungeni.

Watuhumiwa hao walikamatwa Desemba 21 mwaka huu, saa 5 asubuhi katika misako maeneo ya Tabata Bima. Watuhumiwa walitumia ufunguo bandia kuiba gari hiyo.
Share:

Friday 30 December 2016

UTAFITI: Mwanamke Huota Tofauti Na Mwanaume

Wanasema mwanamke na mwanaume ni tofauti kwenye baadhi ya mambo, kimaumbile. Lakini, sio yale mambo yenye kuonekana peke yake, kwani imebainika sasa ni kwamba, tofauti huenda hadi kwenye usingizi. Ni kwamba mwanamke na mwanaume huota tofauti.

Kwa hiyo, hata wakiwa usingizini, mwanamke na mwanaume wanaendelea na tofauti zao.
Dk. Mark Blagrove, ambaye ni mtaalamu wa saikolojia, anasema kwamba, yeye pamoja na mwenzake wamefanya utafiti kwa watu zaidi ya 100,000 na kubaini kwamba, kuna tofauti kati ya mwanamke na mwanaume hasa linapokuja suala la kuota ndoto.

Utafiti uliofanywa na Blagrove na wenzake umehusisha watu wa dunia nzima, sio ulaya na marekani peke yake.

Hivyo, ni utafiti ambao unazungumzia jambo linalohusu dunia nzima, siyo upande fulani tu wa dunia.

Katika utafiti huo, wamegundua kwamba, wanandoa ambao wamelala kitanda kimoja, ubavu kwa ubavu, wanakuwa na ndoto tofauti kabisa, ingawa wanaweza wakawa wanaota wakati mmoja.

Ndoto za wanawake zinaonekana wazi zinahusu kazi, zimejaa hisia sana ndani yake na huchukua muda mrefu zaidi.

Mwanamke anaweza kusimulia kuhusu ndoto yake, ukadhani imechukua saa kadhaa kuota kwa jinsi ilivyo ndefu. Huwa wanaota ndoto moja kwa muda mrefu zaidi.

Ndoto za wanawake zimejengwa kwenye msingi wa nyumbani na kuhusisha watu wengi na hasa wa familia zaidi, kuliko watu wa nje ya familia.

Kwa upande wa ndoto za wanaume, kuota wageni ni jambo la kawaida sana kwao. Wageni, ina maana watu ambao hawawafahamu. Ndoto za wanaume zimejengwa kwenye msingi wa maeneo ya barabara, magari na vurugu.

Hauwezi kupita muda mrefu kabla mwanaume hajaota kuhusu gari, barabara au vurugu za aina fulani.

Huhusisha pia tendo la ndoa na wanawake wasiowajua, mara nyingi.
Ndoto za wanaume pia zimejengwa pia kwenye mazingira ya kazi, na kuhusiana na hofu za kipato na hofu za kupoteza kazi au kufilisika. Zimejaa masuala ya kazi au shughuli.

Mwanasaikolojia aliyeandika pia vitabu kadhaa kuhusu ndoto, Veronica Tonay, anasema, utafiti huu unathibitisha tafiti za siku nyingi ambazo zilikuwa zinadai kwamba, wanawake huota tofauti na wanaume.

Hivi sasa, inaweza kusemwa kwamba, suala hilo halina utata tena. Inaonyesha pia kwamba, zaidi ya nusu ya watu wote wanapata ndoto mbaya angalau mara moja kwa wiki.

Kuna wengine ambao ndoto mbaya ni sehemu ya maisha yao ya kindoto,yaani karibu kila siku zinawatokea.

Inaelezwa kwamba, kazi anayofanya mtu inaweza kuchangia kwenye kuwa kwake na ndoto za jinamizi au ndoto mbaya.

Kwa mfano, wauguzi wahasibu na watumishi kwenye vyombo vinavyohusiana na mawasiliano, ndiyo ambao hukumbwa sana na ndoto hizi mbaya.

Soma; Ili ufanikiwe zaidi, unahitaji kuishi na watu hawa.
Kukimbizwa, meno kudondoka, kuanguka, kutegewa au kuwekewa kizuizi, ni miongoni mwa mada zinazootwa sana, hasa na wale wanaoota majinamizi.

Wanasaikolojia wanasema, ndoto zinahusiana na shughuli ambazo hatujazimaliza kwenye mpangilio wetu wa kazi wa siku au kujaribu kufanya kile ambacho tulishindwa kukifanya tukiwa macho.

Kwa mfano, kuota kupata fedha, jambo ambalo katika hali ya kawaida, limekuwa gumu kwetu.
Watafiti hapo wanazidi kuchambua ndoto kwa kusema kwamba, ndoto zinazohusu mambo mabaya ndizo ambazo zinaotwa zaidi kuliko zile zinazohusu mambo mazuri.

Hata wale watu wenye furaha maishani, wanaonekana kuota ndoto zenye mada zisizopendeza kuliko mada zenye kupendeza.

Ingawa wataalamu wa ndoto wanasema, kila ndoto ina maana kutegemea na mtu aliyeota, utafiti huu unaonyesha kwamba, pamoja na kuwa hilo ni kweli, kuna mambo ambayo mtu mmoja akiyaota , maana yake ni ile ile kwa mtu mwingine yeyote.

Kwa mfano, kuanguka, kwenye ndoto ina maana ya mtu kukosa uhakika wa usalama.
Kukimbizwa au kufukuzwa, bila kujali ni nani anaota, inaweza kuwa na maana ya kukimbia matatizo.

Ndoto ya kupoteza au kung’oka meno inahusiana na mtu kujali namna anavoonekana au sura.
Ndoto ya mtu kukimbia, lakini lakini akajikuta bado yupo pale pale, yaani hasogei, ina maana au inahusiana na mtu kuwa na kazi nyingi kumzidi uwezo.

Ndoto ya mtu kuwa uchi, ina maana kwamba, mhusika ana matamanio ya kuwasiliana na mwingine au wengine.

Kile ktiendo cha kuvua nguo ndotoni kina maana ya mtu kuondoa vikwazo vinavomkabili kwenye maisha ake.

Pamoja na kwamba, lengo la utafiti huu lilikuwa ni kuona kama mwanamke na mwanaume wanaota tofauti, bado umezaa masuala mengine muhimu ynayohusiana na ndoto. Moja ya hili lilozaliwa ni maana ya ndoto, ambazo hazibadiliki, bila kujali ni nani ameziota.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger