Sunday 4 December 2016

New AUDIO | Bob Junior - Chuku Chuku | Download

Share:

31bn/- to support construction of Arusha regional referral hospital

Regional Administrative Secretary of Arusha Adoh Mapunda
 The Tanzania Investment Bank (TIB) has agreed to provide 31bn/- to finance construction of the Arusha Regional referral hospital which will be erected at the current premises of Mount Meru Regional Hospital.
 
Speaking to reporters at the start of the week, Arusha Regional Commissioner Felix Ntibenda, said the money is a loan and all procedures to secure it have been completed.
 
“Very soon a pact will be signed between the bank officials and the Regional Administration Secretary (RAS) for the construction to start,” the RC said.
 
Ntibenda said the authorities continue to improve buildings and health service delivery at the hospital ahead of construction of the referral hospital. He cited among other improvements,  introduction of an MSD pharmaceutical depot that is at 95per cent completion and is already preparing to open soon.
 
“It will make access to medical services more affordable and spare the public the high prices at  the private stores,” he said.
 
Regional Administrative  Secretary of Arusha Adoh Mapunda placed the loan signing sometime next week at which point, the bank will announce a tender to find a contractor to build the hospital.
 
He congratulated stakeholders who have contributed to the ongoing renovation at the regional hospital while the regional engineer, Edward Mwabomba, noted that the hospital was built back in 1915 and is considerably depleted.
 
“The hospital was built as barracks to treat casualties of the First World War...the plan is to now build new buildings and demolish the old ones,” he said.
 
He said the new building will consist of eight sites including staff quarters, training, recreation and other amneties like parking lots.
“These buildings will reduce the burden of patients especially women during delivery and reduce deaths during childbirth,” he said noting that the main section will be a five storey building.
 
 On his part, doctor in charge at the hospital Dr Jacklin Urio said the 500-bed hospital serves 1.6 million people a year and that population growth is overwhelming the facility.
 
He said the new referral hospital will have 600 beds, 50 beds will be for intensive care (ICU), the third floor will be for VIPs including national leaders and internationals.
Share:

Additional Admission, transfer from other institution and change of programme 2016/2017

MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCESThis is to inform you that Tanzania Commission for Universities (TCU) has responded to various requests for admission, transfer from other institutions and change programme of study at MUhimbili University of Health and Allied Sciences for academic year 2016/2017 as shown on the link . Click here to view the list.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DEC 4 2016

Share:

Rais Magufuli na Mkewe wachangia Sh. Mil 5 Matibabu ya Mtoto Haidari Bonge anayeotwa na nyama kichwani

Share:

Waziri Mkuu Akabidhi Pikipiki 200 Kwa Vijana wa Arusha ,Asema Watumishi wa Umma Watakaobainika Kula Fedha Za Miradi Watatimuliwa

Share:

Tanesco yatimiza agizo la Rais Magufuli la Kumpatia Umeme Bakhressa


SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limetimiza agizo la Rais
Share:

Serikali Yakanusha Katibu Mkuu, Ofisi Ya Rais-utumishi Kujiuzulu



Share:

RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI ATEUA MABALOZI WAPYA

rej1
Share:

Saturday 3 December 2016

SERIKALI KUAJIRI WALIMU WAPYA MWAKA WA FEDHA 2016/17



Baada ya serikali kusitisha utoaji wa ajira mpya ili kupisha zoezi la uhakiki wa watumishi wa umma nchi nzima.Imepanga kutoa ajira mpya kwa waalimu 35,000 katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.

Hayo yamesemwa Disemba 2, 2016 na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Suleiman Jaffo katika kikao cha maelekezo ya utendaji kazi kwa watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Jaffo amesema watakao ajiriwa ni wale waliohitimu kozi za ualimu mwaka jana na waliohitimu mwaka huu.

Kuhusu kikao cha maelekezo kwa watumishi wa umma, amewaagiza Wakurugenzi wa Idara wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Manispaa ya Ilala kuwapangia malengo ya kazi wakuu wao wa idara ili kupima utendaji kazi wao.

“Kila Mkurugenzi hakikisha mnakaa na wakuu wa idara muwekeane malengo ni nini cha kufanya katika mwaka wa fedha husika, wapo watakao tekeleza malengo hayo na wapo wasiotekeleza na kwamba hapo utajua utendaji kazi wao,” amesema na kuongeza.

“Wakuu wa idara pia wakae na watumishi wa chini ili kufanikisha utekelezaji wa malengo hayo. Tunataka utendaji kazi wa watumishi ujibu matatizo na kero za wananchi.”

Aidha, Jaffo amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa kujiamini ili kuboresha utendaji kazi wao.

“Wafanyakazi wafanye kazi kwa kujiamini na kutumia elimu zao na wasio waadilifu wawe waadilifu ili kuepusha migogoro wasifike ofisini na kuwaza kutumbuliwa,” amesema.

Kuhusu madeni ya watumishi wa serikali, amesema TAMISEMI imemaliza kuhakiki madeni ya watumishi hao na kwamba hivi karibuni watalipwa fedha zao.

Share:

KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO JUMAMOSI TAREHE 3.12.2016

TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE HABARI ZA MICHEZO LEO..


TANO BORA ZA MASWAYETU BLOG KWENYE KATUNI ZA LEO..


KUMI BORA ZA MASWAYETU BLOG KURASA ZA NDANI MAGAZETINI LEO


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Barrow ambwaga Jammeh urais Gambia


Gambia Präsidentschaftswahl Adama Barrow (Getty Images/AFP/M. Longari)
Tume ya Uchaguzi nchini Gambia imemtangaza mgombea wa upinzani, Adama Barrow, kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika Jumapili na kuna taarifa kuwa tayari Rais Yahya Jameh amekubali kushindwa.
"Ni jambo la kipekee kwamba mtu ambaye ametawala nchi hii kwa kipingi kirefu kama hiki amekubali kushindwa," mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Alieu Momar, aliwaambia waandishi wa habari muda mchache kabla ya kutaja rasmi matokeo ya uchaguzi huo mjini Banjul hivi leo (Ijumaa, Novemba 2).
Tume hiyo ya uchaguzi inasema Barrow amepata asilima 45.5 ya kura, huku Jammeh akipata asilimia 36.7.
Jammeh, ambaye mara moja alikuwa amesema kuwa angelitawala kwa miaka bilioni moja Mungu akipenda, alikuwa akijaribu kuwania wadhifa huo kwa mara ya tano kupitia chama chake cha  Alliance for Patriotic Reorientation and Construction (APRC).
Televisheni ya taifa ya Gambia ililiambia shirika la habari la AFP kwamba Jammeh angelitoa taarifa yake baadaye kumpongeza Barrow. 
Barrow, mwenye umri wa miaka 51, alikuwa ni mfanyabiashara asiyejuilikana sana lakini akateuliwa na muungano wa upinzani kupambana na Jammeh aliyekaa madarakani kwa miaka 22, akijikuta kuwa ana ufuasi mkubwa uliokuwa haukutazamiwa.
Barrow kuongoza serikali ya mpito
Ikiwa kweli Rais Jammeh atatangaza kushindwa, Barrow anatazamiwa kuhudumu muhula wa miaka mitano akiongoza serikali ya mpito kuelekea mageuzi rasmi ya kidemokrasia kwenye koloni hilo dogo la zamani la Uingereza, maarufu kwa fukwe zake.
Meneja wa kampeni wa Jammeh, Yankuba Colley, alisema hakuwa akijuwa chochote kuhusiana na tangazo la mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, lakini alikuwa na hakika kuwa kama raia wa Gambia wameamua rais huyo aondoke, basi ataondoka.
"Ikiwa watu wa Gambia wametoa hukumu yao, yeye ni muumini mzuri," aliliambia shirika la habari la AFP, akiongeza kuwa: "Ni matokeo mabaya lakini mtu ninayemjuwa mimi atakubali vyovyote yatakavyokuwa."
Timu ya Barrow ilithibitisha tangazo la Tume ya Uchaguzi. 
Uchaguzi huo wa Alhamis ulikumbwa na kuzimwa kwa huduma za Intaneti, hatua iliyosababisha lawama kali kutoka makundi ya haki za binaadamu na Marekani. 
Lakini matokeo ya awali asubuhi ya Ijumaa yalikuwa mazuri kwa Barrow, baada ya kuutwaa mji mkuu, Banjul, ambao awali ulikuwa ngome madhubuti kwa Jammeh.
Barrow alishinda takribani asilimia 50 ya kura kwenye majimbo matatu ya Banjul kwa mujibu wa tume ya uchaguzi, ikilinganishwa na asilimia 43 za Jammeh.
Vikosi vya usalama vilimiminwa kwa wingi mitaani, kukiwa na wasiwasi kwamba huenda Jammeh asingekubali matokeo ya kura hiyo.
Hadi nyakati za alfajiri, wanajeshi, polisi na maafisa wa vyombo vyengine vya usalama walionekana kwenye vizuizi vya barabarani, huku raia wakisalia majumbani mwao kufuatilia matokeo.
Share:

RC SINGIDA AWAAGA VIJANA WAHADZABE 43 WANAOENDA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JESHI


rcc
Share:

Magazeti ya Leo Jumamosi ya Disemba 3 2016

Share:

Friday 2 December 2016

Mahakama Yawaachia Huru Wafuasi wa CHADEMA Waliokuwa Wakikusanya na Kusambaza Matokeo ya Uchaguzi Mkuu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia huru wanachama watano wa Chadema pamoja na watu wengine watatu wasio raia wa Tanzania waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhalifu wa kimtandao.

Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage aliwaachia huru washtakiwa hao jana chini ya Kifungu cha 91(1) cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kusema hana nia ya kuendeleza mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.

Waliachiwa huru, baada ya Wakili wa Serikali, Elia Athanas kuomba kufutwa kesi hiyo chini ya kifungu hicho na Mahakama kuridhia.

Kesi hiyo, imefutwa ikiwa katika hatua ya kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka baada ya kukamilisha upelelezi wao na washtakiwa hao kusomewa maelezo ya awali.

Katika kesi hiyo, washtakiwa hao walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Oktoba 27, 2015 na kusomewa mashtaka ya makosa ya uhalifu wa kimtandao, wakidaiwa kukusanya na kusambaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Washtakiwa hao ni Mashinda Edwin Mtei, Julius Mwita, Fredrick Eddie Fussi, Meshack Carlos Mlawa na Anisa Nicholaus Rulanyaga.

Mbali na wanachama hao wa Chadema, washtakiwa wengine ambao ni raia wa kigeni ni Julius Mwonga Matei (Kenya), Jose Mavinga Nimi ambaye kwa sasa ni marehemu (Angola) na Kim Hyunwook (Korea) kwa pamoja wanadaiwa kutenda makosa hayo kinyume cha Kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Uhalifu wa Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Kwa pamoja, walidaiwa kuwa kati ya Oktoba 25 na 26, 2015 kwenye maeneo tofauti ndani ya Jiji la Dar es Salaam, walichapisha matokeo ya uchaguzi wa urais wa mwaka 2015 yasiyo sahihi na ambayo hayakuthibitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kwa lengo la kuipotosha jamii.

Walidaiwa kuwa siku hiyo ya tukio, walichapisha na kusambaza matokeo hayo kupitia mfumo wa uratibu wa uchaguzi uitwao ‘M4C Election Results Management’ na kupitia mitandao mingine ya kijamii, kama vile Facebook na Twitter.

Washtakiwa Matei, Mavinga na Hyunwook wanadaiwa kujihusisha na ajira nchini bila ya kuwa na kibali, kinyume cha Sheria ya Uhamiaji. Wanadaiwa kuwa Oktoba 26, 2015 katika Hoteli ya King D, iliyoko wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, wageni hao walijihusisha katika ajira ya kukusanya na kusambaza matokeo ya uchaguzi wa urais nchini kwa Chadema bila kibali.

Pia wageni hao walidaiwa kujihusisha na shughuli za biashara nchini kwa niaba ya Wanama Saccos, bila ya kuwa na kibali kinyume cha Sheria ya Uhamiaji.
Share:

Serikali yapiga marufuku uchapaji holela wa vitabu vya kujifunzia



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepiga marufuku uchapaji holela wa vitabu vya kufundishia na kujifunzia kwa wachapaji binafsi na badala yake uchapaji huo utasimamiwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TEA) ili kuthibiti ubora.

Amesema mbali na kudhibiti wa ubora pia uamuzi huo unalenga kuwa na kitabu kimoja kwa kila somo kwa kila mwanzfunzi kwa nchi nzima ili kuweka uwiano mzuri katika ufundishaji na upimaji wa wanafunzi .

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Desemba 2, 2016) wakati akizungumza na walimu wa halmashauri ya Jiji la Arusha na wilaya ya Arusha kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) akiwa katika siku ya kwanza ya ziara ya kikazi mkoani Arusha.

Ziara hiyo inalenga kukagua utelelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM,Utendaji wa Serikali, kusikiliza na kujionea kero zinazowakabili wananchi wa Mkoa huo kwa kushirikiana na viongozi wa Mkoa ili kuweza kuzitafutia suluhisho.

Amesema kipindi cha nyuma vitabu vilikuwa vinachapwa na watu mbalimbali hivyo kusababisha malalamiko makubwa kutokana na vitabu hivyo kuwa na makosa mengi. “Sasa vitabu vikibainika kuwa na makosa tutaibana Taasisi ya Elimu Tanzania,”.

Aidha, amesema Serkali itahakikisha kila mtoto anakuwa na kitabu chake ili kuwawezesha kusoma vizuri na kuwa na uelewa wa kutosha ikiwa ni pamoja na kuwarahisishia walimu katika ufundishaji.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu madeni ya walimu, ambapo amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kutenga fedha katika mapato yao kwa ajili ya kulipa madai ya watumishi mbalimbali katika maeneo yao wakiwemo walimu.

Awali Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Jiji na wilaya ya Arusha na kumuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Arusha kumchunguza Ofisa Utumishi wa wilaya ya Arusha, Bi. Imelda Isosi kufuatia tuhuma za rushwa, ufisadi, unyanyasaji kwa watumishi zilizotolewa dhidi yake.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo baada watumishi hao kupewa fursa ya kumuuliza maswali ambapo mhudumu wa Chumba cha kuhifadhia maiti wa Hospitali ya Ortumet Wilayani Arusha, Bw. Bernard Mtei kudai kwamba halmashauri ya wilaya ya Arusha inanuka ufisadi na rushwa hususan katika sekta ya afya.

Baada ya kutoa madai hayo Bw. Mtei alimkabidhi Waziri Mkuu nyaraka mbalimbali zenye uthibitisho wa madai hayo, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo amuhakikishia Waziri Mkuu kwamba watafanya uchunguzi wa kina dhidi ya tuhuma hizo na zikithibitika wahusika watachukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria

Wakati huo huo Waziri Mkuu ameitaka Idara ya Uhamiaji kudhibiti wahamiaji haramu kwa kuanza kufanya misako katika nyumba za kulala wageni ili kuwabaini wageni wanaoingia nchini bila ya kibali kwani ni chanzo cha kuingiza silaha haramu nchini.

Amesema inashangaza kuona silaha za aina nyingi katika maeneo mbalimbali ambazo Tanzania hakuna ambazo zinadaiwa kuingia nchini kupitia maeneo ya mpakani. “Hivyo ni lazima Idara ya Uhamiaji ihakikishe wanadhibiti uingiaji wa wahamiaji kwenye mipaka mbalimbali nchini,”.

Waziri Mkuu amesema Serikali haizuii wageni kutoka mataifa mengine kuingia nchini ila ni lazima udhibiti wa wageni hao ufanyike ikiwa ni pamoja na kujiridhisha sababu za kuja nchini na muda watakao kuwepo.

Hata hivyo aliwasihi watumishi wa idara mbalimbali za Serikali kuhakikisha wanafanya kazi kwa nidhamu, weledi, uadilifu na kuwatumikia wananchi wanaohitaji huduma mbalimbali hata kama wamekosea kuuliza katika maeneo yao.

Amesema “baadhi ya wananchi hawana uelewa juu ya wapi wapeleke malalamiko yao lakini kwa kuwa wewe ni mtumishi wa umma unapaswa kumsikiliza na kumwelekeza aende wapi badala ya kumtolea maneno yasiyofaa,
Share:

Rais Magufuli Aridhia Ombi la Kustisha Mkataba na Kustaafu la Jenerali wa Magereza John Minja

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger