Thursday 24 November 2016
BONGO MOVIE SHINYANGA NA SWAHILI ARTS WAMEKULETEA TAMTHILIA YA VAISI VESA -TAZAMA HAPA SEHEMU YA KWANZA 'WIVU'
Tamthilia ya Vaisi Vesa- sehemu ya kwanza Wivu,itazame chini ya maelezo yote hapo chini
Amani
Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo
Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016 wakiendelea na kazi
Amani Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016
Kundi la
sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha na Bongo Movie
Shinyanga wameamua kuja upya kwa kuunganisha asasi zao na kufanya kazi
kwa pamoja ili kuhakikisha wanaiwakilisha vyema Shinyanga na
kuitambulisha tasnia ya filamu mkoa wa Shinyanga.
Wakizungumza
na Malunde1 blog,wamesema sasa wameamua kuja kwa ujio mpya ambao
utakuwa bandika bandua kwa kazi zenye ubora na mafunzo na wameanza kwa
tamthiliya ya Vaisa Vesa.
Hatua
hiyo imekuja baada ya mwongozaji wa filamu nchini Amani Masuka
anayeongoza kundi la sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha
na mmliki wa Eden Media Creation,kumaliza tofauti zilizojitokeza
mwanzoni mwa mwaka 2015 na Bongo Movie Shinyanga inayosimamiwa na
Ibrahim Songoro ambaye pia anamiliki Songoro Media Production.
Pamoja na
mikakati kibao waliyonayo itakayoanza mwezi Desemba 05 mwaka
huu,magwiji hao wa sanaa ya uigizaji na uongozaji wa filamu wameahidi
kuja na mkakati utakaotengeneza wasanii wapya na kujenga misingi imara
ya kiwanda cha filamu mkoa wa Shinyanga.
Tayari
wameanza na tamthilia fupi inayojulikana kwa jina la 'Vaisi Vesa'
itakayokuwa inarushwa kwa njia ya mitandao ya kijamii kama vile
youtube,instagram,whatsapp n.k.
Wahusika wakuu katika tamthilia hiyo ni Ibrahim Songoro na Miss Grace,mwongozaji ni Masuka A.J na mpiga picha ni David Skerah.
Mwandishi
na mwongozaji wa tamthilia ya Vaisi Vesa,Amani Masuka amesema filamu
hiyo imejaa visa mbalimbali vinavyotokea katika maisha ya binadamu
vinavyotokana na watu wawili kupishana kauli.
“Tamthilia
ya Vaisi Vesa itakuwa inatoa visa vifupi ambavyo wahusika huwa
wanatofautiana kauli ‘kauli tata’,itakuwa inahusisha watu
wawili”,anaeleza Masuka.
Amesema
sehemu ya kwanza ya tamthiliya hii inaitwa “Wivu”,ambapo utata umeibuka
kutokana na kauli ya “Ugonjwa usiokuwa na tiba”,ambapo mhusika mkuu
Ibrahim Songoro anatafsiri ugonjwa usio na tiba kuwa ni Ukimwi ilhali
binti aliyekuwa anamshawishi awe mpenzi wake akimaanisha ugonjwa usio na
tiba kuwa ni wivu.
“Hapo
tunaona unafiki wa Songoro anayewakilisha wanaume walaghai akibadilika
ghafla na kumshtumu binti huyo kuwa ni muuaji aliyekusudia kumwambukiza
virusi vya Ukimwi”,anaeleza Masuka.
“Binti
anajitahidi kumwelewesha Songoro kuwa alimaanisha wivu,ndipo Songoro
anarudi kinafiki na kuanza kujichekesha,hapa tunapata ujumbe kuwa siyo
kila neno unaloambiwa unatakiwa kuliamini(wanawake),lakini pia kabla ya
kuchukua maamuzi unapaswa kufikiria sana kabla ya kutoa uamuzi ulio
sahihi (wanaume)”,ameongeza Masuka.
Akizungumzia
tamthilia hiyo, mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga Ibrahim Songoro
“Songoro Gaddafi” amesema tamthiliya ya Vaisi Vesa imelenga
kuielimisha,kuiburudisha na kuikosoa jamii katika masuala mbalimbali.
Kwa
taarifa zaidi kuhusu tamthilia ya Vaisi Vesa na mambo mengine ya sanaa
ya uigizaji wasiliana na Ibrahim Songoro kwa simu namba 0767831036 na
Amani Masuka simu namba 0767856192.
Tumia dakika zako chache kutazama Tamthilia ya Vaisi Vesa hapa chini katika sehemu yake ya kwanza inayoitwa “Wivu”.
Wednesday 23 November 2016
TAARIFA KWA UMMA: KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
TAARIFA KWA UMMA
KUONGEZWA
KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA
(CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA
UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
FINAL LIST OF GRADUANTS SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE 2015/2016
Taarifa ya Sherehe za Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo.
Uongozi wa
Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo unayo furaha kuwafahamisha wahitimu
wote, wanajumuiya wote wa Chuo na umma kwa ujumla, kuwa sherehe ya Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo, itafanyika Ijumaa tarehe 25 Novemba, 2016 katika Kampasi ya Solomon Mahlangu “Nelson Mandela Freedom Square” Mazimbu, kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Sherehe hiyo itatanguliwa na sherehe ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri sana katika masomo yao “Prize awarding Ceremony” hapo alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa baraza la Chuo yaani “Council Chamber” uliopo kampasi kuu, kuanzia saa 2:30 hadi saa 4:30 asubuhi.
Aidha, mkutano wa majalisi ya wanataaluma wa SUA yaani “Annual general meeting of SUA convocation” utafanyika siku hiyo ya Alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 “Multipurpose hall” kampasi kuu, kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.
Wahitimu ˝Graduands˝ wanakumbushwa kushiriki katika mazoezi ˝Rehearsal˝ yatakayofanyika 25 Novemba, 2016 kuanzia saa 2.00 hadi saa 3.00 asubuhi, “Nelson Mandela Freedom Square”, kampasi ya solomon mahlangu, mazimbu.
Wote Mnakaribishwa.
Imetolewa Na:
Kitengo Cha Mawasiliano Na Masoko, SUA
Kitengo Cha Mawasiliano Na Masoko, SUA
>>KUONA MAJINA YA WAHITIMU BONYEZA HAPA<<
Tuesday 22 November 2016
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUFUNGWA RASMI KWA ZOEZI LA UDAHILI KWA WAOMBAJI WA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA) KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
TAARIFA KWA UMMA
Wakili wa Serikali Amuomba Radhi Hakimu kwa Kushindwa Kumkamata Tundu Lissu
Wakili wa Serikali, Patrick Mwita amemuomba radhi Hakimu Mkazi Mkuu wa
Kisutu kwa kushindwa kutekeleza amri ya kumkamata mbunge wa Singida
Mashariki (Chadema), Tundu Lissu anayekabiliwa na kesi ya uchochezi
pamoja na wahariri wa gazeti la Mawio.
Wakili Mwita alifanya
hivyo jana baada ya hakimu huyo, Thomas Simba kumuhoji sababu za
kushindwa kutekeleza amri hiyo wakati hati ya kumkamata ilitolewa
Novemba 3, 2016 na wakili huyo kuisaini. “Kwa nini hamkumkamata” Si
mlikuwa na wajibu wa kumkamata? Mnamuogopa?” alihoji hakimu huyo.
Hata
hivyo, pamoja na kuomba radhi hiyo mahakama imechukua hati ya kusafiria
ya Lissu ili kudhibiti safari zake nje ya nchi kwa kuwa amekuwa
akisafiri bila kuitaarifu mahakama.
Katika kesi hiyo, Lissu na
watu wengine watatu wameshtakiwa kwa makosa matano ya uchocheza kutokana
na habari iliyochapishwa na gazeti la Mawio kuhusu hali ya kisiasa
Zanzibar.
Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 28, 2016 na washtakiwa wote wapo nje kwa dhamana.
Kabla ya uamuzi huo, Wakili Mwita alisema jana ilikuwa siku ya kesi hiyo kutajwa na kwamba upelelezi unakaribia kukamilika.
Kuhusu
madai ya kudharau mahakama Wakili Peter Kibatala anayemwakilisha Lissu
aliiambia mahakama kuwa mteja wake yupo mahakamani, hivyo ametii amri ya
mahakama na kwamba jukumu la dhamana ni kuhakikisha mshtakiwa anakuwapo
mahakamani wakati wa kesi yake na kwamba uwepo wake ni kutii masharti
ya dhamana.
Hata hivyo, Wakili Mwita alidai kuwa kitendo cha
Lissu kutofika mahakamani mara mbili mfululizo ni kama kuonyesha dharau
kwa mahakama hiyo.
Mwita alidai kuwa Lissu ni mwanataaluma wa
sheria na anafahamu taratibu za kufuatwa kama hafiki mahakamani na
kwamba mdhamini si mbadala wa mshtakiwa mahakamani.
“Alipaswa
kuandika barua kuitaarifu mahakama hii kama wakili kuwa ana kesi ya
uchaguzi anayoiendesha Bunda na kuambatanisha na samansi ama orodha ya
kesi. Tunaomba mahakama iheshimiwe na jukumu la kumfutia dhamana ama
kutokumfutia dhamana Lissu bado lipo mikononi mwako mheshimiwa,”
alieleza wakili huyo wa Serikali.
Akizungumzia hoja hizo, Hakimu
Simba alisema Lissu ni wakili maarufu, msomi na anajua taratibu zote za
mahakama, lakini wadhamini wake wanababaika, hivyo alimtaka aeleze
sababu za kwenda Ujerumani bila kutoa taarifa mahakamani.
Lissu
alijibu kuwa hakuwa na nia ya kuidharau mahakama, wala kuikimbia kesi
inayomkabili bali alikwenda Ujerumani katika mazingira ya dharura.
Hakimu
Simba alimwambia mahakama inafahamu kesi za uchaguzi na maelekezo yake,
hivyo ikamuuliza sababu za kutotoa taarifa wakati alipokwenda
kushughulikia kesi ya Bunda
“Nilipopata taarifa ya kwenda kuiendesha
kesi hiyo ilikuwa ni siku moja baada ya kutoka nchini Ujerumani na
kwamba niliandika barua ya kuitaarifu mahakama na nilituma iletwe
mahakamani kupitia wasaidizi wangu,”alisema Lissu.
Lakini
Hakimu Simba alisema: “Hakuna barua iliyotufikia. Usituingize katika
migogoro kutokana na nafasi yako katika jamii ya mwanasheria.
Hatukuogopi labda upande wa mashtaka ndio wamekuogopa.
“Tunataka
kufuata mfumo, hatutakuogopa na wala hatutakuonea. Hapa naona upande wa
mashtaka wanapiga blaa blaa, tuelewane tunaichukua hati yako ya
kusafiria ili ukitaka kusafiri tujue.”