Thursday 24 November 2016

Official VIDEO ,Download Darassa Ft. Ben Pol – Muziki

vlcsnap-2016-11-23-16h23m16s238
Share:

New AUDIO | Darassa Ft. Ben Pol – Muziki | Download


15056726_1788955811344767_5399682663202160640_n
Share:

BONGO MOVIE SHINYANGA NA SWAHILI ARTS WAMEKULETEA TAMTHILIA YA VAISI VESA -TAZAMA HAPA SEHEMU YA KWANZA 'WIVU'



Tamthilia ya Vaisi Vesa- sehemu ya kwanza Wivu,itazame chini ya maelezo yote hapo chini

Amani Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016 wakiendelea na kazi 

Amani Masuka(kushoto) na Ibrahim Songoro(kulia) wakiwa katika ofisi ya Bongo Movie Shinyanga Jumatano,Novemba 23,2016
Kundi la sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha na Bongo Movie Shinyanga wameamua kuja upya kwa kuunganisha asasi zao na kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha wanaiwakilisha vyema Shinyanga na kuitambulisha tasnia ya filamu mkoa wa Shinyanga. 
Wakizungumza na Malunde1 blog,wamesema sasa wameamua kuja kwa ujio mpya ambao utakuwa bandika bandua kwa kazi zenye ubora na mafunzo na wameanza kwa tamthiliya ya Vaisa Vesa. 
Hatua hiyo imekuja baada ya mwongozaji wa filamu nchini Amani Masuka anayeongoza kundi la sanaa ya uigizaji la Swahili Arts la jijini Arusha na mmliki wa Eden Media Creation,kumaliza tofauti zilizojitokeza mwanzoni mwa mwaka 2015 na Bongo Movie Shinyanga inayosimamiwa na Ibrahim Songoro ambaye pia anamiliki Songoro Media Production. 
Pamoja na mikakati kibao waliyonayo itakayoanza mwezi Desemba 05 mwaka huu,magwiji hao wa sanaa ya uigizaji na uongozaji wa filamu wameahidi kuja na mkakati utakaotengeneza wasanii wapya na kujenga misingi imara ya kiwanda cha filamu mkoa wa Shinyanga. 
Tayari wameanza na tamthilia fupi inayojulikana kwa jina la 'Vaisi Vesa' itakayokuwa inarushwa kwa njia ya mitandao ya kijamii kama vile youtube,instagram,whatsapp n.k. 
Wahusika wakuu katika tamthilia hiyo ni Ibrahim Songoro na Miss Grace,mwongozaji ni Masuka A.J na mpiga picha ni David Skerah. 
Mwandishi na mwongozaji wa tamthilia ya Vaisi Vesa,Amani Masuka amesema filamu hiyo imejaa visa mbalimbali vinavyotokea katika maisha ya binadamu vinavyotokana na watu wawili kupishana kauli. 
“Tamthilia ya Vaisi Vesa itakuwa inatoa visa vifupi ambavyo wahusika huwa wanatofautiana kauli ‘kauli tata’,itakuwa inahusisha watu wawili”,anaeleza Masuka. 
Amesema sehemu ya kwanza ya tamthiliya hii inaitwa “Wivu”,ambapo utata umeibuka kutokana na kauli ya “Ugonjwa usiokuwa na tiba”,ambapo mhusika mkuu Ibrahim Songoro anatafsiri ugonjwa usio na tiba kuwa ni Ukimwi ilhali binti aliyekuwa anamshawishi awe mpenzi wake akimaanisha ugonjwa usio na tiba kuwa ni wivu. 
“Hapo tunaona unafiki wa Songoro anayewakilisha wanaume walaghai akibadilika ghafla na kumshtumu binti huyo kuwa ni muuaji aliyekusudia kumwambukiza virusi vya Ukimwi”,anaeleza Masuka. 
“Binti anajitahidi kumwelewesha Songoro kuwa alimaanisha wivu,ndipo Songoro anarudi kinafiki na kuanza kujichekesha,hapa tunapata ujumbe kuwa siyo kila neno unaloambiwa unatakiwa kuliamini(wanawake),lakini pia kabla ya kuchukua maamuzi unapaswa kufikiria sana kabla ya kutoa uamuzi ulio sahihi (wanaume)”,ameongeza Masuka.
Akizungumzia tamthilia hiyo, mwenyekiti wa Bongo Movie Shinyanga Ibrahim Songoro “Songoro Gaddafi” amesema tamthiliya ya Vaisi Vesa imelenga kuielimisha,kuiburudisha na kuikosoa jamii katika masuala mbalimbali.
Kwa taarifa zaidi kuhusu tamthilia ya Vaisi Vesa na mambo mengine ya sanaa ya uigizaji wasiliana na Ibrahim Songoro kwa simu namba 0767831036 na Amani Masuka simu namba 0767856192.
Tumia dakika zako chache kutazama Tamthilia ya Vaisi Vesa hapa chini katika sehemu yake ya kwanza inayoitwa “Wivu”.

Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOV 24 2016


X

1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

Magazeti ya Leo Alhamisi tarehe 24.11.2016


Share:

Wednesday 23 November 2016

TAARIFA KWA UMMA: KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
TAARIFA KWA UMMA

KUONGEZWA KWA MUDA WA KUFANYA MAOMBI YA UHAMISHO KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) CHA UALIMU ELIMU YA MSINGI NA AWALI NA STASHAHADA (DIPLOMA) YA UALIMU ELIMU YA SEKONDARI KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
Share:

FINAL LIST OF GRADUANTS SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE 2015/2016

Taarifa ya Sherehe za Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo.

Uongozi  wa Chuo Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo unayo furaha kuwafahamisha wahitimu wote, wanajumuiya wote wa Chuo na umma kwa ujumla, kuwa sherehe ya Mahafali ya 32 ya Chuo Kikuu Cha Sokoine Cha Kilimo, itafanyika Ijumaa tarehe 25 Novemba, 2016  katika  Kampasi ya Solomon Mahlangu “Nelson Mandela Freedom Square” Mazimbu, kuanzia saa 4:00 asubuhi.
Sherehe hiyo itatanguliwa na sherehe ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri sana katika masomo yao “Prize awarding Ceremony” hapo alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa baraza la Chuo yaani “Council Chamber” uliopo kampasi kuu, kuanzia saa 2:30 hadi saa 4:30 asubuhi.
Aidha, mkutano wa majalisi ya wanataaluma wa SUA yaani “Annual general meeting of SUA convocation” utafanyika siku hiyo ya Alhamisi tarehe 24 Novemba, 2016 “Multipurpose hall” kampasi kuu, kuanzia saa 5:00 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.
Wahitimu ˝Graduands˝ wanakumbushwa kushiriki katika mazoezi ˝Rehearsal˝ yatakayofanyika 25 Novemba, 2016 kuanzia saa 2.00 hadi saa 3.00 asubuhi, “Nelson Mandela Freedom Square”, kampasi ya solomon mahlangu, mazimbu.
Wote Mnakaribishwa.
Imetolewa Na:
Kitengo Cha Mawasiliano Na Masoko, SUA

>>KUONA MAJINA YA WAHITIMU BONYEZA HAPA<<
Share:

New AUDIO | Stamina Ft. Mr BLUE – Nitampigia | Download

stamina-ft-mr-blue-nitampigiadjmwanga1bdownloadlogo
Share:

New Video: Rich Mavoko ft Diamond – Kokoro


Share:

Magazeti ya Leo Jumatano tarehe 23.11.2016


Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI ZA MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOV 23 2016

Share:

Tuesday 22 November 2016

New AUDIO | Rich Mavoko Ft. Diamond Platnumz – KOKORO | Download


15048071_948415888595585_7603261663579471872_ndjmwanga1bdownloadlogo
Share:

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUFUNGWA RASMI KWA ZOEZI LA UDAHILI KWA WAOMBAJI WA KOZI ZA ASTASHAHADA (CHETI) NA STASHAHADA (DIPLOMA) KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017


 
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI


TAARIFA KWA UMMA


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu Wadau na Umma kwa ujumla kuwa zoezi la kupokea maombi ya kujiunga na masomo kwa kozi za Astashahada (Cheti) na Stashahada (Diploma) kwa mwaka wa masomo 2016/2017 litafungwa rasmi tarehe 21 Novemba 2016.
Share:

Wakili wa Serikali Amuomba Radhi Hakimu kwa Kushindwa Kumkamata Tundu Lissu


Wakili wa Serikali, Patrick Mwita amemuomba radhi Hakimu Mkazi Mkuu wa Kisutu kwa kushindwa kutekeleza amri ya kumkamata mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu anayekabiliwa na kesi ya uchochezi pamoja na wahariri wa gazeti la Mawio.

Wakili Mwita alifanya hivyo jana baada ya hakimu huyo, Thomas Simba kumuhoji sababu za kushindwa kutekeleza amri hiyo wakati hati ya kumkamata ilitolewa Novemba 3, 2016 na wakili huyo kuisaini. “Kwa nini hamkumkamata” Si mlikuwa na wajibu wa kumkamata? Mnamuogopa?” alihoji hakimu huyo.

Hata hivyo, pamoja na kuomba radhi hiyo mahakama imechukua hati ya kusafiria ya Lissu ili kudhibiti safari zake nje ya nchi kwa kuwa amekuwa akisafiri bila kuitaarifu mahakama.

Katika kesi hiyo, Lissu na watu wengine watatu wameshtakiwa kwa makosa matano ya uchocheza kutokana na habari iliyochapishwa na gazeti la Mawio kuhusu hali ya kisiasa Zanzibar.

Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 28, 2016 na washtakiwa wote wapo nje kwa dhamana.

Kabla ya uamuzi huo, Wakili Mwita alisema jana ilikuwa siku ya kesi hiyo kutajwa na kwamba upelelezi unakaribia kukamilika.

Kuhusu madai ya kudharau mahakama Wakili Peter Kibatala anayemwakilisha Lissu aliiambia mahakama kuwa mteja wake yupo mahakamani, hivyo ametii amri ya mahakama na kwamba jukumu la dhamana ni kuhakikisha mshtakiwa anakuwapo mahakamani wakati wa kesi yake na kwamba uwepo wake ni kutii masharti ya dhamana.

Hata hivyo, Wakili Mwita alidai kuwa kitendo cha Lissu kutofika mahakamani mara mbili mfululizo ni kama kuonyesha dharau kwa mahakama hiyo.

Mwita alidai kuwa Lissu ni mwanataaluma wa sheria na anafahamu taratibu za kufuatwa kama hafiki mahakamani na kwamba mdhamini si mbadala wa mshtakiwa mahakamani.

“Alipaswa kuandika barua kuitaarifu mahakama hii kama wakili kuwa ana kesi ya uchaguzi anayoiendesha Bunda na kuambatanisha na samansi ama orodha ya kesi. Tunaomba mahakama iheshimiwe na jukumu la kumfutia dhamana ama kutokumfutia dhamana Lissu bado lipo mikononi mwako mheshimiwa,” alieleza wakili huyo wa Serikali.

Akizungumzia hoja hizo, Hakimu Simba alisema Lissu ni wakili maarufu, msomi na anajua taratibu zote za mahakama, lakini wadhamini wake wanababaika, hivyo alimtaka aeleze sababu za kwenda Ujerumani bila kutoa taarifa mahakamani.

Lissu alijibu kuwa hakuwa na nia ya kuidharau mahakama, wala kuikimbia kesi inayomkabili bali alikwenda Ujerumani katika mazingira ya dharura.

Hakimu Simba alimwambia mahakama inafahamu kesi za uchaguzi na maelekezo yake, hivyo ikamuuliza sababu za kutotoa taarifa wakati alipokwenda kushughulikia kesi ya Bunda 
“Nilipopata taarifa ya kwenda kuiendesha kesi hiyo ilikuwa ni siku moja baada ya kutoka nchini Ujerumani na kwamba niliandika barua ya kuitaarifu mahakama na nilituma iletwe mahakamani kupitia wasaidizi wangu,”alisema Lissu.

Lakini Hakimu Simba alisema: “Hakuna barua iliyotufikia. Usituingize katika migogoro kutokana na nafasi yako katika jamii ya mwanasheria. Hatukuogopi labda upande wa mashtaka ndio wamekuogopa.

“Tunataka kufuata mfumo, hatutakuogopa na wala hatutakuonea. Hapa naona upande wa mashtaka wanapiga blaa blaa, tuelewane tunaichukua hati yako ya kusafiria ili ukitaka kusafiri tujue.”
Share:

Picha: Waziri Mkuu atembea kwa miguu toka nyumbani hadi ofisini kwake, Dodoma

Share:

Waliohamishiwa UDOM kutoka St Joseph kurudia mwaka

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger