Wednesday 27 July 2016

New AUDIO | Prof J Ft. Sholo Mwamba - Kazi Kazi | Download

Share:

NAFASI ZA KAZI CHUO KIKUU SUA -Title: Vice Chancellor

Employment Opportunity - Job Title: Vice Chancellor

Image result for suanet.ac.tz

The term of office of the current Vice Chancellor will come to an end on 5th October, 2016 and the University hereby invites competent and qualified candidates to apply for the following position:-
Read More Information>> Employment Opportunity - Job Title: Vice Chancellor
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE INTERVIEW CHUO CHA SUA JULY 2016

Call for Interview July 2016

Image result for suanet.ac.tz 

Below is a list of candidates applied for various positions in the IFPHTM/PREDICT/VISHA Projects based at Sokoine University of Agriculture
Read More: >> Call for Interview
Share:

Nay Wa Mitego Afungiwa na BASATA....... Atozwa Faini Ya Tsh. Milioni 1


Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limemfungia kwa kipindi kisichojulikana Msanii wa muziki wa kizazi kipya Emmanuel Elibariki maarufu kwa jina la Nay wa Mitego hadi hapo litakapojiridhisha kwamba ametekeleza maagizo yote aliyopewa na Baraza sambamba na yeye kubadilika katika kubuni kazi zenye maadili na zisizo dhalilisha watu wa kada mbalimbali.

Maagizo aliyopewa Msanii Nay ni pamoja na kulipa faini (adhabu) ya kiasi cha Shilingi milioni 1, kufanya marekebisho ya mashairi ya wimbo wake wa ‘Pale Kati’, kufuata sheria, kanuni na taratibu za urasmishaji sekta ya Sanaa kwa maana ya kusajiliwa na BASATA na kuhakikisha wimbo wake umefuata taratibu zote.

Aidha, Msanii Nay ameagizwa kuwaomba radhi watanzania kwa kutoa kazi ya muziki yenye kuvunja maadili na kudhalilisha watu wa kada mbalimbali hususan wanawake.

Maamuzi haya yamefanyika kwa mujibu wa kifungu cha 4(2) cha sheria nambari 23 ya mwaka 1984, ikisomwa pamoja na kifungu cha 30(1)(2) na waraka wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wa tarehe 16/7/2009 ambayo kwa sasa inafahamika kama Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Adhabu hizi zimetolewa kufuatia BASATA kufanya kikao cha pamoja na Msanii huyu jana siku ya Jumanne tarehe 26/07/2016 kwenye Ukumbi wa Baraza na yeye kukiri makosa na kuahidi kubadilika.

Makosa aliyosomewa na yeye kuyakiri kwa maandishi ni pamoja na;
1. Kujihusisha na shughuli za Sanaa pasipo kusajiliwa na BASATA.
2. Kutoa wimbo wa “Pale Kati” na kuupakia katika mitandao ya kijamii bila kuuleta kufanyiwa uhakiki wa maudhui yake.

3. Maudhui ya wimbo wa ‘Pale Kati’ kwa sehemu kubwa hayafai kwa matumizi ya wazi na ni kinyume cha sheria za nchi na maadili ya mtanzania.
 
Ikumbukwe kwamba mnamo tarehe 16/07/2016 BASATA lilitoa taarifa kwa umma ya kuufungia wimbo wa Pale Kati kufuatia kubeba maudhui yenye uvunjifu mkubwa wa maadili na kupambwa na picha dhalilishi kwa wanawake.

Aidha, tarehe 12/02/2016 BASATA liliufungia wimbo wa Shika Adabu Yako wa Msanii huyuhuyu kwa makosa yanayofanana na haya. Hivyo adhabu hii imetolewa ili kumpa muda wa kujifunza, kujitathimi na kujirekebisha kama kweli ana nia ya kuendelea kufanya kazi ya muziki 
 
SANAA NI KAZI TUIKUZE, TUILINDE NA KUITHAMINI
Godfrey L. Mngereza
KATIBU MTENDAJI, BASATA.
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WADAIWA SUGU BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU FIRST BATCH 2016

Share:

HII HAPA TAARIFA KUHUSU MAJINA YA WADAIWA SUGU BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU 2016-FIRST BATCH

FIRST BATCH OF LOAN BENEFICIARIES WHO HAVE NOT STARTED TO REPAY THEIR LOANS

 Image result for heslb.go.tz

 

The Higher Education Students’ Loans Board (HESLB), hereby notifies all loan beneficiaries who are not servicing their loans and whose names appear herein that they have breached a contract as per the HESLB Act. No. 9 of 2004 (as amended) Section 19 (1).
These Loan Defaulters are further notified that according to HESLB Act No. 9 0f 2004 the Board, intends to take the following steps: -

(i) Shall be liable to legal action as per Section 19 (a) (1) of the HESLB Act.
(ii) Shall be subjected to additional monthly Penalty of 5% p.a. on the outstanding loans, over and above the 5% that was levied earlier.
(iii) Shall have his/her outstanding loan loaded with the cost of tracing that will be charged after being traced by the Board.
(iv) Shall be blacklisted and his/her information shall be submitted to the Credit Reference Bureaux, following which they shall be barred from access to credit facilities from all Financial Institutions.
(v) Shall be barred from securing Government scholarships or admission for Postgraduate studies in any Higher Learning Institution within and outside the country.
(vi) Their details shall be submitted to the Ministry of Home Affairs, Department of Immigration and all Embassies where they will be denied approval for travelling abroad.

All Loan Beneficiaries whose names have been published in the newspapers and on this website of the Board through http://olas.heslb.go.tz are required to repay their due loans immediately to avoid facing the above listed measures.  Loans statements and other details of their due loans can be accessed by visiting HESLB Offices or writing to:
Acting Executive Director,
Higher Education Students’ Loans Board,
P.O. Box 76068
Dar es Salaam
Email: info@heslb.go.tz
Share:

Official VIDEO | Raymond - Natafuta kiki [Guitar Version] | Watch/Download


Share:

MPYA:APPLICATION ZA DIPLOMA KWENDA DIGRII KUANZA RASMI TAREHE 31.7.2016

tcu bannerHabari zenu,
wale wote ambao wanasubiria kuomba vyuo vikuu kupitia Diploma,taarifa iliyopo ni kwamba application zitaanza rasmi tarehe 31.7.2016.
Pia kitabu au nacte guide book 2016/2017 itapatikana mpya siku si nyingi.
Tafadhali endelea kusubiri.
Share:

Denouncement of the fabricated rumours on the suspension of Admission into some University Institutions

Share:

Sunday 24 July 2016

JINSI YA KUOMBA KOZI MBALIMBALI ZA CHETI &DIPLOMA THROUGH NACTE 2016/2017

The System allows you to apply for Admission into Further and Higher Education for academic year 2016/2017.
Available Application Categories:-

  • - Admission into Certificate/Diploma and Higher Diploma
    • Administration, Business, Law, Planning, Social Work, Community Development, Tourism and related Programmes :- Deadline 05/08/2016
    • Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences :- Deadline 05/08/2016
    • Health and Allied Sciences (Including Community Health, Health Records etc) :- Deadline 05/08/2016
    • Teacher Education :- Deadline 05/08/2016

IMPORTANT NOTES:
You are advised to select your most preferred category according to prior qualifications that you hold, because your selection depends on your choices and qualifications.
To proceed with the this application you must have the following
  • 1. Valid and Working Email Address
  • 2. Valid Phone Number
  • 3. Payment Mpesa Confirmation Code
Read Guide Book:
To know exactly requirement of programmes you wish to apply, it is highly recommended to carefully read admission guidebook. Click here to download.

APPLICATION FEE (Non refundable): Application fee for this academic year are as in following categories:-
  • - For Certificate/Diploma And Higher Diploma in
    • Administration, Business, Law, Planning, Social Work, Community Development, Tourism and related Programmes alone :- TShs 20,000/=
    • Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences alone :- TShs 20,000/=
    • Health and Allied Sciences (Including Community Health, Health Records etc) alone :- TShs 30,000/=
    • Teacher Education alone :- TShs 20,000/=
    • NOTE: For More than one professional area e.g Teacher Education and Agriculture, Livestock, Engineering, ICT and other related Sciences professional areas shall be TShs 30,000/=
Which shall be paid through M-PESA or Airtel Money using the following menu:- Note: Payment Instructions: Please follow the steps below to pay through M-Pesa or Airtel Money:
Payment Instructions Using Vodacom Mpesa: Malekezo ya Jinsi ya kulipia kwa Vodacom Mpesa:
  • 1. Dial *150*00#
  • 2. Select 4. Payments
  • 3. Select 4. Enter business number
  • 4. Enter the business number (607070)
  • 5. Enter reference No. (1234)
  • 6. Enter Amount (e.g 50,000/=)
  • 7. Enter PIN
  • 8. Press 1 to Confirm:
  • 1. Piga *150*00#
  • 2. Chagua 4. LIPA kwa M-Pesa
  • 3. Chagua 4. Weka namba ya kampuni
  • 4. Tafadhali weka namba ya kampuni No. (607070
  • 5. Weka namba ya kumbukumbu ya malipo No. (1234)
  • 6. Weka kiasi (e.g.50,000/=)
  • 7. Weka namba ya siri.
  • 8. Bonyeza 1 kuthibitisha:
After confirmation you will receive a message from Vodacom (e.g. "BA54KP432 Confirmed. Tshs. 50,000 sent to business NACTE for account 1234 on 14/4/14 at 2:33 PM New M-Pesa balance is Tsh 200").
*Use the confirmation code at the beginning of the message to enter on payment details text box (BA54KP432).

Baada ya kutuma utapokeo ujumbe kutoka vodacom (Mfano "CB02AK669 Imethibitishwa. Tsh. 20,000 imetumwa kwa NACTE kwenye akaunti namba 1234 tarehe 29/3/16 saa 12:38 PM salio lako la M-PESA ni Tsh. 200").
*Tumia Uthibitisho wa malipo mwanzoni mwa ujumbe mfupi ulutumwa kutoka vodacom kuingiza kwenye kiboxi cha uthibitisho wa malipo (CB02AK669).

Payment Instructions Using Airtel Money: Malekezo ya Jinsi ya kulipia kwa Airtel Money:
  • 1. Dial *150*60#
  • 2. Select 5. Make Payments
  • 3. Select 3. Enter business Name
  • 4. Enter the business Name (607070)
  • 5. Enter Amount (e.g 50,000/=)
  • 6. Enter the reference Number. (1234)
  • 7. Enter PIN to confirm Paying 607070
    TShs 50000 with reference number 1234
  • 1. Piga *150*60#
  • 2. Chagua 5. Lipia Bili
  • 3. Chagua 3. Weka Jina la Kampuni
  • 4. Tafadhali Andika Jina La Biashara. (607070
  • 5. Ingiza Kiasi cha Pesa (e.g.50,000/=)
  • 6. Ingiza Namba ya kumbukumbu. (1234)
  • 7. Ingiza namba ya siri kulipia 607070,
    Tshs 50000 kumbukumbu rejea namba 1234.
You will receive a message from Airtel (e.g. " Txn Id: MP160506.0908.A07884 You have paid 50000.00Tshs to NACTE: Your available Airtel Money balance 200.00Tshs.").
*Use the Txn Id: (MP160506.0908.A07884,) to enter on payment details text box.

Baada ya kutuma utapokeo ujumbe kutoka Airtel (Mfano "Kitambulisho rejea: MP160506.0908.A07884, Umelipa 50000.00Tshs Kwenda NACTE.Salio lako jipya ni 200.00TShs.").
*Tumia Kitambulisho rejea: wa malipo (MP160506.0908.A07884) mwanzoni mwa ujumbe mfupi ulutumwa kutoka Airtel kuingiza kwenye kiboxi cha uthibitisho wa malipo.

NB: All applicants are advised to keep in safe place their confirmation number from Vodacom M-PESA payment or Txn Id from Airtel Money for future reference. Applicants are advised to read carefully the admission requirements of each programme they anticipate to apply in the guidebook before finalizing the application process in order to avoid problems that may arise due to failure to follow appropriate instructions.

REGISTRATION: To apply for mentioned category you must be registered to CAS follow the below link to proceed.


  • If this is your first time click here to start your application.
  • If you are already registered please click here
Share:

TCU YAFUNGIA VYUO KUDAHILI 2016/2017


TCU YAFUNGIA VYUO VINGINE KUDAHILI.
BAADA ya wiki jana kutangaza orodha ya vyuo ambavyo havitaruhusiwa kudahili Wanafunzi Kwa Mwaka wa Masomo 2016/17

 katika vyuo vya;
 (IMTU,KAMPALA,UDOM,SUZA,SFCHAS)-MEDICINE ,BAGAMOYO UNIVERSITY NA ST.JOSEPH 

KUNA TETESI KWAMBA KUNA VYUO VINGINE VIMEFUNGIWA....... (ninafuatilia kuhusu vyuo vingine kufungiwa ni kweli au la)

PLEASE WAIT!!!!!!!
Share:

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 1 & 2




Mtunzi:Eddazaria G.Msulwa
Ni siku ya jumamosi kama kawaida wanafunzi wote wa shule tunayosoma tunakwenda viwanjani kucheza michezo mbali mbali kama mpira wa miguu na michezo mingine ambayo wanacheza wasichana waliopo katika shule yetu ambayo niya bweni yenye mchanganyiko wa wasichana na wavulana kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita na nishule ya mtu binafsi(PRIVET SCHOOL) iliyopo katoka mkoni Arusha.
Kama kawaida yangu ya kuwa shabiki wa timu ya darasa langu la kidato cha tano ninachosoma ninaendelea kutazama mechi tunayocheza na kidato cha tatu hadi wakati huu tumeshafungwa goli mbili kwa moja huku dakika zikiwa zinakimbia kuelekea ukingoni huku mashabiki wa kike wa kidato cha tano wakiendelea kuwapa moyo wachezaji wetu waliopo uwanjani

“Oya Eddy mcheki yule manzi pale”
“Yupi?”
“Yule aliyevaa sweta jeupe”
“Ana nini?”
“Cheki alivyo bomba majamaa kibao wamemtokea wamepigwa chini”
“Yupo kombi gani?”
“HKL”
“Ndio maana angekuwa huku tulipo sisi wala asingekuwa mzuri”

“Hembu acha pumba zako Eddy”
“Kweli John unadhani angekuwa science unadhani angekuwa hivi wewe si unawaona wakina Matha walivyo kauzu class hadi kuwatongoza mtu unashindwa”

Tukajikuta tukikatisha mazungumzo baada ya mchezaji wetu mmoja kufunga bao la kukomboa jambo lililoturudishia furaha hata ya kuwepo uwanjani.

Kabla hata ya dakika mbili mbele mchezaji wetu yule yule akafunga bao jingine kupitia mpira wa kona uliopigwa na akaudumbukiza nyavuni kwa kichwa na kuamsha shangwe za wanafunzi wote wa kidato cha tano na kuwafanya mashabiki baadhi kuingia uwanjani huku wakishangilia kwa furaha kwani tayari dakika zilisha kwisha.

Mimi na rafiki yangu John tukabaki nje ya uwanja huku sura zetu zikiwa na furaha kupita maelezo

“Wee dada jamaa anakuita hapa”.John alimuita yule msichana tuliyekuwa tunamjadili dakika kadhaa zilizopita.

Akatuangalia kwa dharau yeye na rafiki zake kisha wakaongea maneno ya kunong’onezana na kuanza kucheka kicheko kilichotufanya tuwe kimya kama tumemwagiwa maji ya baridi.

Safari ya kurudi shuleni ikaanza kwani kiwanja chetu cha mpira kipo eneo la nje ya eneo la shule.Tukiwa tumeongozana na kundi la wasichana wa kidato chetu wakiimba nyimbo za ushindi mimi na John tukawa na kazi ya kumfwatilia yule msichana ambaye kusema la ukweli amejaliwa uzuri unaweza kusema alipewa siku yake ya pekee katika uumbwaji wake

Tukafika hadi kwenye duka la shule ambapo yule msichana alikwenda na rafiki yake ambaye kidogo naye anavutia japo si sana.Kutokana hatukuwa na lengo la kufika katika duka hilo kwa aibu tukajikuta tukinunua mifuko miwili ya pipi za Big boom

“Claudia ile hela siioni” Yule msichana alizungumza huku akiwa anajipapasa papasa kwenye mifuko ya sketi yake huku akionekana kuwa na wasiwasi wa hali ya juu kwani tayari walishakunywa soda pamoja na kula keki za watu

“Hebu tazama vizuri”
“Kweli si unaona mifuko yote haina hela jamani sijui imeangukia wapi”

Nikawatazama kwa huruma kisha nikatoa waleet yangu mfukoni iliyotuna kwa wingi wa pesa nikamuuliza muuza duka ni kiasi gani cha pesa anachowadai akaniambia nikawalipia na chenchi iliyobaki nikamwambia muuza duka awapatie.

Tukaanza kuondoka kabla hatujafika mbali Claudia akatuita na tukasimama wakaja katika lile eneo tulilosimama huku rafiki yake ambaye ndio aliyetufanya twende pale dukani kwa kumfatilia akaawa analia

“Samahani kaka zangu tunawashukuru”

“Haina shida vitu vya kawaida,Eddy twende zetu”

“Ngojeni kwanza”

Claudia alizungumza huku akimshika John beda aliyeanza kugeuka na kutaka kuanza kuondoka katika eneo tulilo kuwepo

“Mbona huyo mwenzako analia”

 “Amepoteza pokety money yake ndio kwanza ametoka kuipokea leo mchana kwenye basi”

“Mmmm poleni”

John alizungumza kwa maringo na kuanza kuondoka ikanilazimu mimi kubaki kwani roho ya huruma ilianza kunitawala huku wakati wote nikimtazama yule msichna ambaye bado sikulitambua jina lake

“Amepoteza sh ngapi?”

“Eti Salome umepoteza shii ngapi?”

“Elfu themanini na tano”

Nikakaa kimya kama dakika mbili nikifikiria nini nifanye,nikajikuta nikiitoa wallet yangu mfukoni na kuesabu noti tisa za elfu kumi kumi kisha na kuzitoa na kumpa Salome taratibu akazipokea huku akiwa haamini tukio linalo tendeka kwa wakati huo.

“Zitakusaidia saidia siku mbili tatu”

“Asante sana kaka yangu”

“Powa ukiwa na shida utakuja darasa la PCB ndio ninaposoma”

Nikawapa na mfuko wa pipi nilio nunua kisha nikaondoka huku moyoni mwangu nikijifariji kuwa tayari nimesha fanikiwa katika hatua ya kwanza ya kumpata mtoto mzuri.

Tukafika bwenini tukaoga kujiandaa na sikukuu ya wanafunzi ambayo hufanyika kila mwisho wa mwenzi wakati wa usiku katika ukumbi wa shule.

Sikukuu hii hutoa fursa ya wanafunzi kuonyesha vipaji vyao mbali mbali.Tukapitia katika cantin ya shule na tukanunua chakula kisha tukaelekea kwenye ukumbi uliojaa wanafunzi kuanzia kidato cha kwanza ahadi cha sita

Shughuli zikaanza huku wanafunzi mbali mbali wakionyesha vipaji vyao huku wakishangiliwa na wanaofanya vibaya huzomewa.Ukumbi ukakaa kimya huku tukiwasubiria washiriki wa shindano la umiss wa shule kupita mbele yetu huku majaji wakiwa ni waalimu wetu wa michezo pamoja na wanafunzi baadhi.

Wakaanza kuingia mmoja mmoja huku wakiwa wamependeza,nikajikuta ninanyanyuka kwa furaha huku nikipiga makofi hii ni baada ya kumuona Salome akiwa katika msururu huo wa mamisi waliochanganyika vidato mbali mbali.

Wakajipanga mbele ya majaji na kuanza kuulizwa maswali mmoja baada ya mwingine kwa lugha ya kingereza.Ikafika zamu ya Salome kuulizwa swali wanafunzi wote wakakaa kimya kumsikiliza atakacho kijibu

“SALOME CAN YOU TELL US WHAT IS LOVE?”(Salome unaweza kutuambia upendo ni nini?)

“Love is force of nature however much we may want to,we can not command,demand or disapper love,any more than we can and in adition love cannot  be bought,sold or trade.You cannot make some one to love you.Thanks”(Upendo ni hali ya msukumo wa kihalisia kwa jinsi tunavyo hitaji.Hatuwezi kulazimisha,kukomalia au kutawanya upendo kwa kadri tunavyoweza na kwa kuongezea Upendo hauwezi kununuliwa kuuzwa au kubadilishana.Hauwezi kumfaya mtu kukupenda wewe.Asante”)

Ukumbi mzima ukapiga makofi kasoro mimi kwani nikajikuta sentensi ya mwisho ya Salome ikijirudia rudia akilini mwangu “YOU CAN CANNOT MAKE SOMEONE TO LOVE YOU”(Huwezi kumfanya mtu kukupenda).Wakatoka ukumbini kwa wimbo walio ingilia kupisha mambo mengine kuendelea huku tukisubiri matokeo kutoka kwa majaji wetu.

Muda wa matokea ukawadia huku washiriki waote wakisimama mbele yatu.Jaji mmoja akaanza kutangaza nafasi kuanzia ya tatu na ya pili huku nafasi ya kwanza akimkabidhi mgeni rasmi ambaye ni mmiliki wa shule kuitangaza huku wakiwa wamebakia washiriki wanne.Tukakaa kimya kusubiria ni nani atakaye nyakua taji kwa mwaka huo

“NA MSHINDI WETU NI……………………..SALOME ALEX EDWARD”

Ukumbi mzima ukanyanyuka na kuanza kupiga makofi ikiwemo mimi huku John akinisukuma sukuma kila wakati huku akinionyeshe jinsi Salome alivyopendeza na kuzidi kuvutia kwenye macho ya wengi.Akaanza kuvalishwa vitu wanavyo valishwa mamisi pale wanapashinda huku akikabithiwa uwa kubwa na mgaeni rasmi.

Muongoza shindano MC akamuomba Salome amchague mtu wa kwenda kucheza naye mziki kwa dakika tano.Salome akachukua kipaza sauti na sote tukakaa kimya kumsikiliza ni nani atapata bahati hiyo ya kuitwa mbele ya ukumbi huo.Salome akatizama tizama na macho yake akaelekea sehemu tuliyokaa sisi.Akanyoosha kidole chake watu wote wakaangalia tulipo sisi

“Eddy hichi kidole ni chako”.John alizungumza huku akinisukuma sukuma kwa kutumia bega lake.Nikanyanyuka kidogo ila Salome akatingisha kidole chake kwamba si mimi ni jamaa aliyekaa kiti cha nyuma yetu ambaye ni kaka mkuu wetu.

Jamaa akanyanyuka kwa furaha huku wezake nyuma wakimtuma akamchezee Salome hadi alainike.Mimi na John tukabaki kama watu wasio amini huku mimi roho ikianza kuniuma kupita maelezo na kumfanya John kuachia msunyo mkali adi watu wa pembeni yetu wakamtazama na kuanza kucheka

“Mademu wengine bwana was**e kama nini” John alizungumza huku akiendelea kutoa misunyo.Jamaa kama alivyoagizwa na wezake akawa anazidi kumshika shika Salome mwili wake huku wanafunzi wakishangilia kwa furaha na kuzidi kunifanya niichukie sikukuu hiyo

“John twende zetu tukalale” Tukanyanyuka kwenye viti vyetu kutokana na mlango wa kutokea upo mbele tukalazimika kupita mbele ya ukumbi huku macho yangu yaliyojaa hasira yakimtazama Salome ambaye naye alinitazama kwa sekunde kadhaa kisha akayapeleka macho yake sehemu nyingine.Tukashuka kwenye ngazi za ghorofa lenye ukumbi wa shule.Kabla hatujafika chini mwanafunzi mmoja akatuita.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger