Monday 4 July 2016
Sunday 3 July 2016
OMMY DIMPOZI NA WYNE ROONEY KATIKA PICHA YA PAMOJA
Picha ambayo imepigwa na Dimpoz ni picha ya video ambayo wanaonekana wanazungumza kitu lakini sauti ya video hiyo imezimwa (mute) so wakati tunasubiri Ommy Dimpoz mwenyewe atuambie walichokuwa wanazungumza ninayo hiyo video mtu wangu ambayo Ommy Dimpoz kapost kwenye akaunti yake ya Instagram.
Kwenye post zake Ommy Dimpoz ameonekana akila raha sehemu mbalimbali za Ibiza,mahali ambako mastaa wengi wa Dunian hutembelea kwa ajili ya mapumziko.
Video: Barnaba (Official Video) – Chozi La Afrika | Mp4 Download
Hii ni video mpya ya Barnaba ambayo iko chini ya Binti Foundation, Wimbo unaitwa Chozi La Africa, Tazama na kuipakua hapa chini
New Video: Jacky Chant Feat Yamoto Band - Wabaya | Download MP4
New Video: Jacky Chant Feat Yamoto Band - Wabaya | Download MP4
Baada Ya Kuitema Malaika Band Ya Christian Bella.. Jacky Chant
Kawashirikisha Yamoto Band Kwenye Hii Ngoma Yake Mpya WABAYA.. Itazame
na Kupakua Hapa..
WATCH FROM YOUTUBE
VIDEO:MKUU WA MOA WA DAR ES SALAAM PAUL MAKONDA,APIGA MARUFUKU VITU VITATU JIJINI DAR,VISOME HAPA
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amepiga marufuku vitu vitatu kutoonekana katika mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumza kwenye kongamano la Dini lililofanyika katika uwanja wa Taifa alisema..’Kwanza
kwa watumiaji wa biashara ya Sheesha katika maeneo ya Bar, Clubs na
sehemu zingine kuanzia leo ni marufuku katika maeneo hayo’- Paul Makonda
‘Pili
ni marufuku kwa wavutaji wa Sigara kwenye sehemu za wazi kwani
wataalamu wanasema ule moshi unamuathiri yule asiyetumia hiyo Sigara
kuliko yule anayetumia Sigara’– Paul Makonda
‘Tatu
ni marufuku kwa ushoga kwenye mkoa wangu wa Dar es Salaam na mashoga
wote walio kwenye instagram na Facebook watakamatwa na wale wote wanao
wa follow mashoga kwenye mitandao ya kijamii basi watakuwa na hatia ile
kama ya mashoga‘- Paul Makonda
VIDEO
VIDEO
KANUSHO KUHUSU JOHN MNYIKA KUNENA MAZITO KUHUSU LOWASSA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA KWA UMMA
Ipo hoja nyepesi mno iliyopikwa na Vijana wa Lumumba juu ya Mbunge wa Kibamba na Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika kuwa alimkataa Lowassa
Hoja hiyo ni ya kupuuzwa kwa kuwa haina ukweli wowote ule, na nitalishangaa Jeshi la Polisi kuendelea kukaa kimya,na kumuacha aliepotosha Umma kwa kiwango kikubwa kiasi hicho,jambo ambalo limempa Usumbufu mkubwa Naibu Katibu mkuu kwa chama na Wananchi wake katika jimbo lake.
Nataka kuona nguvu ya Cyber Crime kama kweli sheria hiyo ni dhahiri ni msumeno au huwa inakata upande mmoja tu!.Mnyika ni Kiongozi mkubwa na katika Taasisi kubwa sana nchini CHADEMA,hapaswi kunenewa uongo kwa nia ya kuupotosha Umma naliomba jeshi la Polisi liingie kazini Mara moja kutimiza majukumu yake.
Imetolewa July 03
Edward Simbeye
Katibu Mwenezi BAVICHA Taifa
Ipo hoja nyepesi mno iliyopikwa na Vijana wa Lumumba juu ya Mbunge wa Kibamba na Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika kuwa alimkataa Lowassa
Hoja hiyo ni ya kupuuzwa kwa kuwa haina ukweli wowote ule, na nitalishangaa Jeshi la Polisi kuendelea kukaa kimya,na kumuacha aliepotosha Umma kwa kiwango kikubwa kiasi hicho,jambo ambalo limempa Usumbufu mkubwa Naibu Katibu mkuu kwa chama na Wananchi wake katika jimbo lake.
Nataka kuona nguvu ya Cyber Crime kama kweli sheria hiyo ni dhahiri ni msumeno au huwa inakata upande mmoja tu!.Mnyika ni Kiongozi mkubwa na katika Taasisi kubwa sana nchini CHADEMA,hapaswi kunenewa uongo kwa nia ya kuupotosha Umma naliomba jeshi la Polisi liingie kazini Mara moja kutimiza majukumu yake.
Imetolewa July 03
Edward Simbeye
Katibu Mwenezi BAVICHA Taifa
BREAKING NEWS:ALIEKUWA MBUNGE WA KILINDI "BEATRICE SHELUKINDO" AFARIKI DUNIA
Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Kilindi mkoani Tanga, ndugu Beatrice Shelukindo amefariki dunia Leo jioni jijini Arusha alikokuwa akijiuguza.
Mwili umehifadhiwa kwenye Hospitali ya Mount Meru.
Innalillah waina illaih rajiun
BODI YA MIKOPO YAKANUSHA KWAMBA TAARIFA ILIYOSAMBAA KWAMBA HAINA PESA
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
TAARIFA KWA UMMA
KUKANUSHA TAARIFA KWAMBA BODI HAINA FEDHA
Bodi ya Mikopo ya
Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kukanusha taarifa za upotoshaji zinazoenezwa
kwa sasa kwamba haina fedha.
Si kweli kwamba
Bodihaina fedha, ila ni kweli kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa kufikisha
fedha za wanafunzi vyuoni kutokana na zoezi la kuhakiki wanafunzi wanaonufaika
na mikopo linaloendelea vyuoni hivi sasa.
Hata hivyo,
maandalizi ya malipo hayo yameshafanyika na ‘pay sheets’ zimeshapelekwa vyuoni
tayari kwa wanafunzi wanaonufaika na mikopo kusaini.
Bodi inatarajia
wakati wowote wiki ijayo baada ya zoezi la uhakiki kukamilika; itapeleka fedha
hizo vyuoni.
IMETOLEWA
NA:
KITENGO
CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO
BODI
YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
TAREHE
2 JULAI 2016
Breaking News:GARI AINA YA NOAH YAPATA AJALI WILAYANI MASWA-MKOA WA SIMIYU
Gari aina ya NOAH imepata ajali maeneo ya zanzui wilayani MASWA mkoani SIMIYU,Hakuna mtu aliepoteza maisha.
(Picha zote na Samweli Mwanga)