Sunday 29 May 2016

Muhongo Aitumbua Kampuni Iliyoingiza Mafuta FEKI Nchini

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
SERIKALI imemsimamisha msambazaji wa mafuta Kampuni ya Sahara Energy Resourses Limited ya Nigeria aliyeingiza mafuta ya ndege (JET A1) yaliyochafuka na kumtaka kusafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta ya kampuni zilizopokea mafuta hayo.

Aidha, imeelezwa pamoja na kutokea kwa tatizo hilo la kuchafuka kwa mafuta hayo nchi haitaingia katika ukosefu wa nishati hiyo muhimu kwa kuwa kuna akiba ya kutosha kwa siku 14 na tayari kampuni ya Puma imeagiza mafuta ambayo yataingia nchini Juni 7, mwaka huu. 
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitoa kauli hiyo jana wakati alipotembea kampuni za mafuta zilizopokea mafuta yaliyochafuka kwa kuchanganyika na petroli jijini Dar es Salaam ili kubaini ukweli wa uhaba wa mafuta ya ndege.

Profesa Muhongo aliiagiza kampuni hiyo ya Sahara Energy Resources Limited ya Nigeria kuhakikisha inasafisha matangi pamoja na mabomba ya mafuta kuanzia leo na kama haitatekeleza hilo itakuwa ni mwisho kufanya kazi nchini. 
“Msafishe haya matenki pamoja na mabomba yote kwa gharama zenu. Haya ni maagizo sisi hatuwezi kuendelea kusubiri, hamuwezi mkasababisha nchi ikawa na uhaba wa mafuta kwa majadiliano yenu ambayo hayana mwisho.

“Usafishaji unatakiwa kuanza kesho, kama hautafanyika kuanzia hiyo kesho, basi Sahara isahau kufanya biashara katika nchi hii. Na sio hilo tu hata tenda (zabuni) alizokuwa amepata nazo tutazifuta,” alisema Profesa Muhongo. 
Alisema kuwa kampuni hiyo haitakiwi kupewa zabuni nyingine hadi hapo uchunguzi utakapokamilika wa kubaini ukweli wa mafuta hayo kuchafuka kwa kuchanganyika na petroli.

Profesa Muhongo alisema hatua walizochukua ya kwanza ni kumsimamisha kujihusisha na zabuni yoyote itakayotangazwa kuanzia sasa lakini pia kutakiwa kusafisha matangi na mabomba hayo. 
Aliongeza kuwa hii ni mara ya pili kwa kampuni hiyo mafuta yake kuwa na tatizo kwani mara ya kwanza mafuta yake yalibainika kuwa machafu akarudishwa nayo.

Awali mwakilishi wa kampuni hiyo ambaye yuko hapa nchini alisema, hawana sehemu ya kuhifadhi mafuta hayo ambayo yamechafuka hivyo wanasubiri meli yao irudi ili waweze kuyaondoa mafuta. 
Hata hivyo, kampuni ya kuhifadhi mafuta nchini ya Tanzania International Petroleum Reserves Limited (TIPER) ilimhakikishia Profesa Muhongo kuwa wana nafasi ya kuhifadhi mafuta yote yaliyochafuka, hatua ambayo waziri huyo aliiagiza kampuni hiyo kuhifadhi mafuta hayo katika matangi ya TIPER badala ya kusubiri meli.

“Hilo linatuchelewesha TIPER wameshakubali wana nafasi ya kuhifadhi hayo mafuta, kwa hiyo yahifadhi hapa ili msafishe hayo matenki, ili mafuta yatakayokuja yakute matenki ni masafi,” alisema. 
Aidha, alisisitiza kuwa taifa haliwezi kuingia kwenye uhaba wa mafuta ya ndege na yapo ya kutosha siku 14 kwani kampuni ya Puma tayari imeshaomba mafuta kutoka katika kampuni za Total na SP ya Rwanda.

Pia meli ya Puma itaingia nchini Juni 7 na meli nyingine itaingia Juni 13. 
Awali akizungumzia hali hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, Michael Mjinja alisema, meli hiyo iliingia nchini Mei 5, mwaka huu na mafuta hayo yalithibitishwa kuwa na ubora na Shirika la Viwango nchini (TBS). 
Alisema baada ya mafuta hayo kushushwa ilibainika kuwa yamechafuliwa hatua iliyowafanya kumuagiza aliyeleta mafuta hayo kuyaondoa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Felix Ngamlagosi alisema, kwa sasa kuna mafuta ya kutosha kwa siku 14 lakini kuna hatua nyingine zinazochukuliwa ili kuhakikisha hakuna uhaba wa mafuta utakaotokea.
 “Hayo yaliyochanganyika kuna hatua zinazochukuliwa ikiwa ni pamoja na kuchukua sampuli za pamoja na sisi ni wasimamizi ili kuhakikisha zinapelekwa maabara na kujua kitu gani kilitokea,” alisema.

Profesa Muhongo alizitembelea kampuni hizo ambazo ni Puma Energy, Gapco Tanzania Ltd, Oilcom, ORXY Energies na TIPER. Meneja wa Huduma za Usafiri wa Anga wa Oilcom, Haruna Magota alimwambia Waziri Muhongo kuwa, mafuta waliyopokea yalikuwa ni lita milioni 8.8 na wao walikuwa na lita milioni 2.6, ambapo mafuta hayo yote yameharibika.

Alisema ukosefu wa mafuta hayo umekuwa ni tatizo kwa wateja wao ambao ni mashirika ya ndege kwani jumla ya lita milioni 10.8 yote yamechafuka. 
Aidha aliongeza kuwa wakaguzi wa meli walishawahi kutoa onyo kwa kampuni hiyo kuwa meli zake hazina viwango vinavyotakiwa vya kubeba nishati hiyo. 
Aidha kampuni za kuagiza mafuta nchini zilitaka kampuni ya Sahara Energy Resources Ltd ya nchini Nigeria kuweka hadharani uthibitisho wa kuhujumiwa kuhusiana na kashfa ya uingizaji mafuta ya ndege machafu hapa nchini inayolikabili shirika hilo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta ya Petroli nchini (TAOMAC) iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari jijini Dar es Salaam juzi, waagizaji hao waliitaka kampuni hiyo kutaja jina la kampuni au mhusika yeyote anayeaminika kuihujumu kampuni hiyo kama ambavyo imenukuliwa na vyombo vya habari nchini ikijitetea kupinga kashfa hiyo.

“Tunawaomba wenzetu hawa wahakikishe wanakabidhi jina la kampuni au mtu yeyote wanayemshuku kuwa anahusika na kashfa inayowakabili kwa Jeshi la Polisi au chombo chochote cha usalama nchini vinginevyo sisi tutaamini kuwa utetezi wao ni uwongo na unalenga kutafuta njia ya kutokea,’’ alisema Mkurugenzi Mtendaji wa TAOMAC, Salum Bisarara kupitia taarifa hiyo.

Sakata la kuingizwa kwa mafuta machafu ya ndege aina ya Jet A1 na hofu ya kukosekana kwa mafuta hayo nchini liliibuliwa na Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017, alisema mafuta hayo yatakosekana kutokana na kampuni moja ya kigeni iliyopewa zabuni kuagiza mafuta hayo, kuingiza mafuta ambayo hayawezi kutumiwa na ndege.
Share:

Serikali yatangaza kuisafisha Sekta ya Elimu na Watumishi wa umma wenye vyeti bandia.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Serikali imetangaza rasmi kuanza kwa kampeni ya kuwashughulikia na kuwaondoa katika utumishi wa umma watumishi wote walioajiriwa katika  sekta hiyo  wakitumia vyeti bandia .

Aidha, imewataka watumishi hao waanze kujitathmini na kuanza kujiondoa wenyewe kabla ya kufikiwa na mabadiliko makubwa ya kusafisha sekta ya elimu na utumishi wa umma yanayokuja nchini.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi Prof.Joyce Ndalichako wakati wa majumuisho ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imejipanga kufanya mabadiliko makubwa katika Sekta ya Elimu nchini ili kuhakikisha kuwa Elimu inayotolewa katika shule, vyuo na taasisi mbalimbali inazalisha wahitimu wenye sifa na ubora kwa maslahi ya Taifa .

Amesema katika kulitimiza hilo Serikali itawachukulia hatua kali za kinidhamu na kisheria watendaji wote walioshiriki na wale wanaoendelea kushiriki kwa namna moja au nyingine kukwamisha maendeleo ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na wale waliohusika katika udahili wa wanafunzi wasio na sifa katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph Songea.

"Serikali ya awamu ya tano imedhamilia kwa dhati kabisa kuboresha kiwango cha elimu yetu kwa kufanya mabadiliko makubwa katika mfumo wa elimu, naomba niwahakikishie kwamba pale panapohitajika kufanyika mabadiliko tutayafanya bila woga" Amesisitiza.

Amesema katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za elimu hapa nchini, serikali imejipanga kubadilisha mfumo wa elimu ambao umekuwa ukilalamikiwa kwa muda mrefu na kwamba mabadiliko hayo yatafanyika kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta hiyo.

" Tunapotaka kufanya mabadiliko kwenye mfumo wetu wa elimu tumekubali kwamba tuna changamoto,  katika changamoto hizi lazima tuwe na mahali pa kuanzia hivyo tunapochukua hatua tunaomba Watanzania mtuunge mkono" Amesisitiza Prof.Ndalichako.

Prof.Ndalichako Amesema lengo la Serikali kupitia Wizara yake ni kuhakikisha sekta ya elimu inaboreshwa hapa nchini kwa kuendelea kutoa wahitimu bora wanaokidhi vigezo na viwango katika soko la ajira.

Amesisitiza kuwa mkakati wa Serikali ni kuanza kuwafuatilia wahitimu wote wasio na viwango ambao wako katika maeneo mbalimbali ya ajira huku akisisitiza kwamba elimu ya Tanzania ni sawa na kiwanda kinahitaji malighafi nzuri ili kitoe bidhaa bora.

Ameeleza kuwa Serikali imejipanga kikamilifu kuvikagua vyuo vyote vinavyotoa elimu ya juu kuona kama vinakidhi sifa na vigezo vya kiutendaji ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wale wote wanaowadanganya wananchi  na kuwapotezea muda vijana wanaowadahili bila kuzingatia sifa.

"Wizara yangu tunaendelea kufanya mawasiliano na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili tuchukue hatua kwa wote walioichezea sekta hii muhimu, tulichofanya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph kinaendelea kwa vyuo vingine"

Kuhusu ujenzi wa maabara amesema kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 12 kwa ajili ya kununulia vifaa vya maabara kwa shule zote 1536 ambazo zimekamilisha ujenzi wa majengo ya maabara kote nchini.

Katika hatua nyingine amesema kuwa Serikali katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 itafanya ukaguzi wa vyuo vyote vya Maendeleo ya Jamii kote nchini ili majengo ya vyuo hivyo yaweze  kutumika kuanzishia vyuo vya Ufundi Stadi VETA katika wilaya na mikoa ili kuwapatia stadi za kazi vijana waweze kujitegemea kwa kujiajiri wenyewe.

Kwa upande wao baadhi ya Wabunge waliopata nafasi ya kuchangia wakati wa Kupitisha Bajeti ya wizara hiyo wameiomba Serikali kuweka mkazo katika usimamizi wa Sekta ya Elimu nchini ili shule, Taasisi na vyuo vya Tanzania vitoe wahitimu wenye ubora kwa maslahi ya Taifa.

Aidha, wameiomba Serikali kupitia Bajeti hiyo itenge fedha za kutosha kwa ajili ya kuimarisha shughuli za ukaguzi wa shule, kuboresha maslahi na kulipa madai ya walimu pamoja na kuziimarisha Mamlaka za Udhibiti wa Elimu ili ziweze kutimiza majukumu yao ipasavyo.
Share:

Basi Jingine la Mwendo kasi Lapata ajali Eneo la Magomeni Usalama

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Basi jingine la mwendo kasi limepata ajali mabaya eneo la Magomeni Usalama. Ni baada ya gari dogo kukatisha kwenye barabara ya magari ya mwendo kasi.

Share:

New AUDIO | Alikiba x Tundaman - School baby[RMX] | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
DOWNLOAD
https://my.notjustok.com/track/download/id/96075
Share:

JWTZ Washusha Abiria Kwenye Magari yao na Bodaboda ili Washiriki Zoezi la Usafi

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

KATIKA hali isiyo ya kawaida, askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Mkoani Mtwara jana walisimamisha vyombo vya usafiri barabarani asubuhi na kushusha abiria waliokuwemo, ili washiriki kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kufanya usafi.

Mwandishi alishuhudia abiria wakishushwa katika magari, pikipiki katika maeneo mbalimbali ya mji wa Mtwara na kutakiwa kushiriki zoezi la usafi.
 
Ufanyaji usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi umekosa mwamko mjini Mtwara tangu kuzinduliwa na Rais Desemba 9, mwaka jana.
 
Bila kujali itikadi za vyama wala cheo cha mtu, JWTZ waliwataka wananchi kupaki vyombo vya usafiri na kufanya usafi ili kukabiliana na milipuko ya magonjwa.
 
Baadhi ya wananchi walioshiriki usafi huo, walipongeza jitihada za JWTZ katika kutilia mkazo zoezi la usafi mkoani humo.
 
Zoezi hilo la usafi liliongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Halima Dendego ambaye alisema litakuwa endelevu mkoni hapo.
Share:

HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU MUHIMBILI MUHAS(UDAKTARI,PHARMACY,NURSING etc)-2016/2017

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
MUHIMBILI UNIVERSITY OF HEALTH AND ALLIED SCIENCES

Applications for Admission into the Undergraduate Degree and Diploma Programmes 2016-2017

Applications are invited from qualified candidates wishing to pursue various Undergraduate degree and Diploma programmes offered by Muhimbili University of Health and Allied Sciences for the academic year 2016/2017. Click here to download the programmes and instruction to Applicants.
Share:

REAL MADRID MABINGWA WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE 2015/2016, WAWACHAPA ATLETICO KWA MATUTA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mshambuliaji wa Real Madrid,Christiano Ronaldo, akimalizia penati ya mwisho ameweza kuwainua mashabikki wa timu yake baada ya kutupia mkwaju wa mwisho kiufundi huku Atletico Madrid,wakikosa penati ya nne na kufanya matokeo kuwa Penati tano kwa 3.
MADRID 1   2  3  4  5
ATLETICO 1  2  3  X -

 Katika Dakika 90 za mchezo huo timu hizo zilitoka sare kwa kufungana bao 1-1, bao la Real Madrid likifungwa na Sergio Ramos katika dakika ya 15 kipindi cha kwanza akimalizia pasi ya kichwa cha utosi ya Bale, bao lililodumu hadi kumalizika kwa dakika 45 za kwanza.

Dakika ya 47, Atletico Madrid, walikosa penati iliyopigwa na Grezmann,baada ya beki wa Madrid, Pepe kumchezea rafu Fernando Tores katika eneo la hatari.

Atletico walisawazisha bao lao katika dakika ya 79, kupitia kwa Carasco, akiunganisha mpira wa krosi kutoka winga ya kulia.
 Tores akijaribu kumtoka beki wa Madrid, Ramos.....
Atletico wakishangilia bao la kusawazisha.
Share:

Music: Mapacha Ft Becka Tittle & Linex – Kipande Flani

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
13181540_502471313269466_2111938126_n 
Wasanii wa hip hop hapa Bongo Mapacha wemaachia wimbo wao mpya unaitwa “Kapande Flani” amewashirikisha Becka Tittle x Linex, Producer Father Beats x NaCh B


>>>>DOWNLOAD HERE<<<<<
Share:

Marlaw Ft. Fundi Samweli - PAMOJA (Official Video) | Download Mp4

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WATCH VIDEO BELOW
 
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MAY 29 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

Saturday 28 May 2016

Breaking news:WANAFUNZI WOTE WA SPECIAL DIPLOMA UDOM WARUDISHWA NYUMBANI,HADI HAPO WATAKAPO TAARIFIWA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
 
Kutokana na tatizo la ufundishaji wa stashahada ya elimu(hisabati,sayansi na teknolojia)chuo kikuu cha udom .serikali kupitia wizara ya elimu sayansi na teknolojia imewarudishwa wanafunzi wote nyumbani.


Soma hapo chini BARUA HIYO

Share:

BREAKING NEWS:WATU WANNE 4 WAMEFARIKI BAADA YA BOTI KUZAMA MDA HUU

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Image result for BREAKING NEWS
Watu 4 wamefariki baada ya boti waliyokuwa wakisafiria ikitokea kigamboni kuzama.

TAARIFA KAMILI ZINAKUJA
Share:

Mkuu wa Mkoa Afumaniwa Akifanya Mapenzi na Mwanae

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkuu wa zamani wa Mkoa wa Kaskazini Pemba na mshauri wa Rais wa Zanzibar kisiwani humo, Dadi Faki Dadi amekamatwa akituhumiwa kufanya mapenzi na mtoto wake wa kambo.

Dadi alikamatwa juzi akidaiwa kukutwa na mtoto huyo wa mkewe wa ndoa mwenye umri wa miaka 21 katika nyumba ya kulala wageni inayoitwa Executive, jirani na makao makuu ya Uhamiaji Zanzibar katika eneo la Kilimani chini na Maisara, mjini Unguja.

Mwanasiasa huyo alijikuta akipigwa pingu na polisi akiwa kifua wazi mbele ya mkewe na wanafamilia na kisha kupelekwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Mwembemadema.
Picha za video zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, zilimwonyesha Dadi akikabiliwa na mashambulizi makali ya maneno kutoka kwa watu waliomkamata, akiwamo mkewe.
“Mwacheni avae nguo kwanza, mpeleke bwana, twende bwana..." ni baadhi ya maneno yanayosikika katika video iliyorekodiwa wakati wa kumtia mbaroni.

Taarifa zilizopatikana miongoni mwa wanafamilia ya kiongozi huyo, zilidai kwamba alikamatwa baada ya kumtilia shaka binti huyo kutokana na mienendo yake ya hivi karibuni na kuamua kumfuatilia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam alithibitisha kumshikilia Dadi kwa muda kabla ya kumwachia kwa dhamana.

“Kijamii alitenda kosa, lakini sisi tunaendelea kufanya uchunguzi, iwapo tutabaini ametenda kosa la kisheria na anaweza kuwa mashtaka tutamkamata ili kumpeleka katika vyombo vya sheria,” alisema Mkadam.

Mmoja wa wanafamilia ambaye aliomba jina lake lisitajwe alisema: “Mwizi siku zake ni arobaini, tulimtega na hatimaye tumemnasa sasa tuone mwisho wake utakuwa nini na kipi kitajiri baadaye.” 

Share:

HAPPY BIRTHDAY DADA ANGU AURELIA (mama kasiga)

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Habari yenu wadau wa blog hii ,
leo nina furaha sana kwani dada angu wa pekee Aurelia (dada ake blogger boy)katimiza miaka kadhaa ya kuzaliwa hapa duniani.

Dada angu Mungu akupe miaka buku,NAKUPENDA SANA.

"NISAIDIENI KUMWISHI HAPPY BIRTHDAY DADA ANGU.
NAMPENDA SANA. "

Share:

MECHI YA FAINALI UEFA LEO MAY 28 2016 REAL MADRID VS ATLETICO

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
  • Real Madrid and Atlético to meet in second Champions League final in three seasons
  • Repeat of 2014 final, when Real Madrid came back to beat Atlético in extra time
  • Madrid also triumphed 1-0 over two legs in last season's quarter-finals
  • Diego Simeone: "Only winning will satisfy me now"
  • Zinédine Zidane says above all Real Madrid must "run: run, run run"
Possible lineupsReal Madrid: Navas; Carvajal, Pepe, Ramos, Marcelo; Casemiro, Kroos, Modrić; Bale, Benzema, Ronaldo.
Out: Varane (hamstring)
Doubtful: none
Atlético: Oblak; Juanfran, Godín, Savić, Filipe Luís; Koke, Gabi, Fernández, Ñíguez; Griezmann, Torres.
Out: none
Doubtful: none
Sergio Ramos: My Magic Moment
Zinédine Zidane, Madrid coach
Ronaldo has been feeling a bit of pain but he's OK. He'll be there 100%. He has a little niggle, but that disappears when you're going to play in a Champions League final.
It's going to be a difficult game for sure, extremely difficult, but we already know this and we're prepared for it. We've had two weeks to prepare and now the players want the ball to start rolling.
I see the players the same as in Lisbon. We're one game away. We're all very happy to be in this final. We're ready for this, and that's the big word: we're ready to play. We've worked hard to achieve this. I'm happy with the work we've carried out. We've suffered a lot, but reaching a final without suffering is impossible. We know how to do that and that's what we'll have to do again, no doubt. In a final it's perfectly normal to have difficulties. If you want to win it, you have to suffer.
©Getty Images
Zinédine Zidane takes training at San Siro
Losing will not be a failure. Failure is in your attitude, or if you don't give your all. It's just a football game. You never know what will happen but I can tell you we're very prepared. [Since 2014] some players have left but the idea of this club is always the same. It's the great story: unity, effort, companionship and, when the time comes to play, quality and leaving everything on the field. We want to repeat that.
When the match begins I'll be a bit more tense [than as a player] but that's usual too – it's part of the coaching job. I like it, I like this kind of pressure. I've experienced it as a player but as a coach it's completely different. Carlo Ancelotti used to tell me that often. He told me before the final in Lisbon: "I hope you experience this some day as head coach." Here we are, so I keep thinking of Carlo.
Above all you have to defend well, first and foremost, especially when you don't have the ball. On top of that, we have our weapons to work well when we're attacking. What we really have to do is run: run, run, run.
Diego Simeone, Atlético coach
The game will be very tense, very even, especially at the beginning. Casemiro enables them to regroup better if they lose the ball. Whoever wins the early battles in midfield will have an advantage – Madrid, with their technical qualities, might try to play more.
The club, the players, the group we've created, is reinventing itself continuously. That's what is most valuable at this club. Everyone works with the idea of improving, growing, and that's life – if you work, work, work, eventually you get what you want.
©Getty Images
Diego Simeone overseeing training
To play a final is absolutely fantastic, to win it is even better. That experience makes you want to continue living these moments. It's not easy; you have to pick yourself up, keep inventing yourself, change the players but not change the commitment, the values, the work. If you keep working, you're insistent, you can achieve things.
We're not really going to change much for this game – neither team will. Madrid haven't changed much [since 2014]; we've changed more but we have the same structure. Casemiro makes Madrid a lot more dangerous on the counterattack – that's how they played in both [semi-final] legs against Manchester City. Many people think that's bad – not me. There could be different situations during the game but it's clear that, if you give Madrid space, they're very dangerous.
I like to have 113 years of history on my back – I like that, I love the pressure. Only winning would satisfy me.
Highlights: See how Real Madrid reached the final
Most recent results
Deportivo La Coruña 0-2 Real Madrid (Ronaldo 7 25)
The Merengues' slim hopes of snatching the title from Barcelona on the last day ultimately came to naught as Luis Suárez led the Catalans to a comfortable win at Granada. Madrid did what they could, and Cristiano Ronaldo's early goal meant that for 15 minutes Zidane's men even topped the provisional table. Ronaldo hit a second soon after – his 35th in the league this term – but Madrid were destined to finish runners-up by a point.
Highlights: See how Atlético reached the final
Atlético Madrid 2-0 Celta Vigo (Torres 51, Griezmann 54)
Atlético, already fated to come third, ended their domestic campaign with a routine victory. Fernando Torres opened the scoring following a fiery, if goalless, opening 45 minutes at the Estadio Vicente Calderón. Antoine Griezmann then overtook Radamel Falcao as the club's top marksman of the Simeone era, with his 44th strike in that frame. The clean sheet meant ever-present Jan Oblak conceded just 18 in the Liga season, equalling Francisco Liaño's Spanish top-flight record.
Form guide (all competitions, most recent first)
Real Madrid: WWWWDW
Atlético Madrid: WLLWWW
Highlights: The sides' 2014 meeting
Reporter's view: Andrew Haslam (@UEFAcomAndrewH)
This is the fourth European Cup final in Milan, and the first in 15 years, but none of the others had such a local flavour. Real Madrid's dramatic defeat of Atlético in Lisbon two years ago was the first European final between teams from the same city and Atlético will not lack for motivation as they seek a first European Cup, while Madrid have the pedigree.
Simeone's side are unbeaten in domestic fixtures against their opponents since that galling 2014 reversal (W5 D3) and, if they can finally translate that form to the continental stage, they could become the 23rd club to lift the trophy.
View from Madrid: Joseph Walker (@UEFAcomJoeW)Simeone and Atlético will attempt to avenge their heartbreak of two years ago as they take on their great city rivals. Atlético will be full of confidence, having lost just once in the last ten meetings between the teams, and knocked out both Barcelona and Bayern München on their way to this final.
Real Madrid, on the other hand, will feel they have the psychological advantage following what happened in Lisbon – and the fact their one victory in the last ten derbies came in last season's UEFA Champions League.
Did you know?
This is the sides' fourth European Cup tie, and Real Madrid have won the previous three: the 1958/59 semi-final, the 2014 final and last term's quarter-final. Find out more in our extensive match background.
Share:

Audio | Songa, Chidy Benz & Nikki Mbishi - Wacha Mchecheto | Mp3 Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Audio | Songa, Chidy Benz & Nikki Mbishi - Wacha Mchecheto | Mp3 Download

- See more at: http://www.johventuretz.com/2016/05/audio-songa-chidy-benz-nikki-mbishi.html#sthash.5mHzZYWE.dpuf

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger