Friday 6 May 2016

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MAY TAREHE 6.5.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
20160506_044234
20160506_044247
20160506_044259
20160506_044313
20160506_044330
20160506_044342
20160506_044352
20160506_044402
20160506_044414
20160506_044423
20160506_044436
20160506_044452
20160506_044503
20160506_044514
20160506_044528
20160506_044545
20160506_044601
20160506_044613
20160506_044625
20160506_044635
20160506_044647
20160506_044656
20160506_044714
20160506_044724
20160506_044736
20160506_044748
20160506_044759
20160506_044810
20160506_044822
20160506_044834
20160506_044851
20160506_044900
Share:

Thursday 5 May 2016

ASHA ROSE MIGIRO ATEULIWA KUWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Asha-Rose Migiro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza.

Dkt. Asha-Rose Migiro anakwenda kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kalaghe ambaye amerudishwa nyumbani.

Dkt. Asha-Rose Migiro ataapishwa kesho Alhamisi tarehe 05 Mei, 2016 katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
04 Mei, 2016
-------------------------------

Mapito ya Dk. Migiro
Dk. Migiro alizaliwa tarehe 9 Julai  1956 katika Wilaya ya Songea, Ruvuma. Alisoma Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, Dar es Salaam mwaka 1963 hadi mwaka 1966.

Dk. Migiro alihamia Shule ya Msingi Korogwe, Tanga ambapo aliendela na elimu ya msingi mwaka 1967–1969.

Baadaye akajiunga kidato cha kwanza mpaka cha nne katika Shule ya Sekondari Weruweru, Kilimanjaro mwaka 1970 hadi 1973 na Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Korogwe mwaka 1974 -1975.

Dk. Migiro alikuwa mmoja wa wasichana waliofaulu vizuri Korogwe Sekondari na alipojiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1977, alichukua masomo ya sheria na kuhitimu Shahada yake (LLB) mwaka 1980.

Baadaye aliajiriwa UDSM kufundisha masomo ya sheria kama Mhadhiri Msaidizi. Alifanya kazi hiyo kwa miaka miwili kabla ya kuendelea tena na masomo ya juu ya sheria mwaka 1982–1984 hapohapo UDSM na kutunukiwa shahada ya uzamili (LLM).

Kati ya mwaka 1985–1988, alifundisha UDSM. Mwaka 1988 alikwenda Chuo Kikuu cha Konstanz, Ujerumani ambako alisoma na kutunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika masuala ya Sheria mwaka 1992.

Dk. Migiro alirejea Tanzania akiwa Mhadhiri Mwandamizi na aliendelea kufundisha katika Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hadi mwaka 2000 alipoingia kwenye siasa.

Akiwa UDSM kati ya mwaka 1992 – 1994 Dk. Migiro alikuwa Mkuu wa Idara ya Sheria za Katiba na Utawala.

Kati ya mwaka 1994 – 1997 aliongoza Idara ya Sheria za Makosa ya Jinai (Idara zote zipo katika Kitivo cha Sheria UDSM).

Dk Migiro ni mzungumzaji mzuri katika lugha ya Kiingereza, Kifaransa na Kijerumani. Ni mke wa Profesa Cleophas Migiro na wana watoto wawili wa kike.

Dk Migiro alianza na siasa za kujijenga akitokea katika taaluma. Mwaka 2000, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa alimteua kuwa waziri kwenye Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.

Alitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2005 bila kubadilishwa akisimamia mambo mengi ya kisera na kimiundombinu, bila kusahau utekelezaji na upiganiaji wa haki za wanawake na watoto.

Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alimteua kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje, Januari 2006 na kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kushikilia wadhifa huo. Katika kipindi cha mwaka mmoja tu, alifanya kazi nyingi za kimataifa zilizomweka katika anga nyingine kisiasa.

Januari 5, 2007, aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu (UN) mpaka 2012 alipomaliza muda wake. Januari mwaka 2013, Dk Migiro aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Desemba 2013 aliteuliwa kuwa mbunge katika Bunge la Tanzania.

Januari 2014 aliteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba, nafasi ambayo alidumu nayo mpaka Rais Kikwete alipomaliza muda wake mwaka jana.
Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MAY TAREHE 5.5.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Wednesday 4 May 2016

Mpya: Serikali Kutoa Ajira 71,456

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Serikali inakusudia Kuajili wafanyakazi wapya 71,456, katika mwaka mpya wa fedha 2016/2017 kwa la kujaza nafasi zilizo wazi, huku wilaya ya mbulu ikitengewa nafasi 466.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na utawala bora, Angela Kairuki, aliliambia bunge jana kuwa, maombi ya nafasi za ajira kwa kawaida hufanyika kwa uwazi kupitia bajeti ya seriksli, ambayo huidhinishwa na bunge.
Angela alikuwa akijibu swali la Zacharia Isaya (Mbulu-CCM), Aliyetaka kujua ni lini serikali itajaza nafasi za ajira zilizo wazi katika maeneo mbalimbali nchini kwa ngazi za wizara, mikoa, wilaya na vijiji.
Alisema ajira hizo hufanywa na baada ya waajiri kuwasilisha maombi yao serikalini na kidhinishwa kwa kuzingatia ukomo wa bajeti ya mishahara serikalini.
Waziri alisema kwa halmashauri ya mbulu, katika mwaka wa fedha unaomalizika, ilitengewa kuajiri watendaji wa vijiji (VEO) Kumi na watendaji wa kata (WEO) sita.
Hata hivyo, Waziri alisisitiza kwamba pamoja na nafasi hizo, serikali itajaza nafasi zilizo wazi kila mwaka, kutokana na bajeti itakavyoruhusu na kuzingatia vipaumbele.
Aidha katika kuzingatia kupanda kwa gharama za maisha, Waziri alisema serikali imekuwa ikipandisha kima cha chini cha mshahara kulingana na uwezo wa bajeti, hususani mapato ya ndani.
Kutokana na hatua hiyo, Angela alisema Tanzania ni moja ya nchi za afrika, ambazo kwa sasa hulipa kima cha chini cha mshahara sawa na asilimia 80 ya kiwango cha gharama za maisha (Minimum Living Wage).
Waziri huyo alisema,  serikali itaendelea kuboresha mishahara ya watumishi wake wa umma kulingana na uwezo wa Kiuchumi.
Chanzo: Gazeti la Uhuru
Share:

Wanafunzi 1,500 Vyuo Vikuu Wanolewa

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel, imedhamini kongamano la ajira kwa vijana wa chuo kikuu, lenye lengo la kuwaweka pamoja waajiri na waajiriwa watarajiwa, kuwapatia fursa zitakazowasaidia katika kuendesha shughuli za kiuchumi.

Share:

Scholarships for Masters Programmes tenable in the Republic of Korea - 2016/2017

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MAY TAREHE 4.5.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger