Thursday 28 April 2016

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRIL TAREHE 28.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Share:

Wednesday 27 April 2016

MECHI YA LEO UEFA ATLETICO VS BAYERN MUNICH SAA 21:45 USIKU

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

...
Share:

MASTER SCHOLARSHIP NCHINI IRAN 2016/2017

Share:

Mwanafunzi Amkaanga kortini polisi anayedaiwa kumbaka katika kibanda cha ulinzi cha benki.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mwanafunzi wa kidato cha tatu, juzi alimkaanga askari polisi anayedaiwa kumbaka kwa kuieleza Mahakama jinsi alivyotendewa kitendo hicho katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Akitoa ushahidi mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Misungwi, Ruth Mkisi, shahidi huyo alidai siku ya tukio askari huyo, Raphael Sixstus (30), alimuita alipokuwa akipita karibu na Benki ya CRDB Tawi la Misungwi, alipoitikia wito ghafla alivutiwa ndani ya kibanda hicho na kumbaka.

“Wakati akinitendea kitendo hicho, alikuwa akinitishia kisu huku akiniambia nikipiga kelele ataniua, niliogopa nikaa kimya ingawa niliumia na kutokwa damu nyingi sana,” alidai shahidi huyo.

Akiongozwa na Mwendasha Mashtaka wa Polisi, Doreth Mgenyi, mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16 alidai kabla ya kumbaka, mshtakiwa huyo alimvua nguo zote za ndani.

Awali, Mwendesha mashtaka alipokuwa akimsomea makosa mshtakiwa huyo alidai kuwa Novemba 20, mwaka jana, akiwa eneo la lindo katika Benki ya CRBD Tawi la Misungwi, alimbaka mwanafunzi huyo saa 1.00 usiku wakati akitoka mashine kusaga unga katika maeneo ya Bomani.

Hakimu Mkisi aliahirisha kesi hiyo hadi leo itakapoendelea kusikilizwa kwa upande wa mashtaka kuita mashahidi wengine. Mshtakiwa yuko nje kwa dhamana.
Share:

Tahadhari ya Mvua kubwa na Upepo mkali f kuanzia tarehe 26-04-2016 Hadi 29-04- 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetahadharisha uwepo wa mvua kubwa na upepo mkali unaozidi kasi ya kilomita 40 kwa saa iliyotarajiwa kuanza jana hadi keshokutwa.

Sambamba na upepo huo, taarifa hiyo ya TMA imesema mvua za zaidi ya milimita 50 zinatarajiwa kunyesha huku bahari ikitarajiwa kuwa na mawimbi makubwa yanayozidi mita 2.0 

Taarifa hiyo imeelezwa kuwa hali hiyo imesababishwa na mgandamizo mdogo wa hewa katika Pwani ya Tanzania unaotakana na kimbunga cha Fantala.

Maeneo yaliyotajwa na TMA kwamba yataathiriwa na hali hiyo ni mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mtwara, Unguja na Pemba na kwamba mvua hizo pia zinatarajiwa kusambaa hadi katika maeneo ya mikoa ya Kilimanjaro na Mashariki mwa Manyara.

Ofisa Habari wa TMA, Monica Mutoni aliwataka wakazi wa maeneo hayo na watumiaji wa bahari kuchukua hatua stahiki ili kuepuka uwezekano wa kupata madhara yanayoweza kujitokeza.

“Mvua hizi ni kama zile zilizonyesha wiki iliyopita. Wajibu wetu ni kutoa taarifa pale tunapoona kiwango cha juu cha mvua na upepo ili watu wachukue tahadhari. Kwa watumiaji wa bahari umakini uzidi kuongezeka kwani mawimbi yatakuwa makubwa na upepo wa bahari utakuwa kilomita 30 kwa saa,” alisema Mutoni.
Share:

Ripoti ya CAG Yawaweka Kikaangoni Vigogo wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD)

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Ripoti iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad imezichanganya Hospitali ya Taifa Muhimbili na Bohari ya Dawa (MSD), huku Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akihitaji maelezo ya kina kuhusu mkanganyiko huo. 
 
Ummy ameitaka MSD kuandika maelezo ya kina kwa maandishi, kuhusu vifaa vya Sh2 bilioni ambavyo viko njiani kwenda Muhimbili kwa miaka minne sasa, kabla wizara yake haijatoa tamko rasmi. 
 
Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu  jana alisema bohari haina mzigo wowote ulio njiani kuelekea Muhimbili bali imekuwa ikisambaza dawa zake nchi nzima. 
 
Bwanakunu alisema tatizo lililojitokeza ni mfumo wa kompyuta ambao unaonyesha mzigo upo njiani, hivyo muamala katika kompyuta unavyoshindwa kukamilika, mzigo lazima uonekane upo njiani. 
 
“Mwaka 2012 tulibadilisha mfumo wa kompyuta kutoka wa awali mpaka tunaotumia sasa, hivyo kuna miamala ilihitaji kubadilishwa, mwaka huu tulifanya zoezi la kukamilisha baadhi na si kwa Muhimbili pekee kwa mfano kuna mzigo unatoka MSD Ubungo kwenda Muleba ukifika kule mtu anashindwa kuingiza kwenye mfumo kwamba umepokelewa,” alisema Bwanakunu. 
 
Alifafanua kwamba majibu ya MSD kwa CAG yalieleza kuwa walitengeneza timu ya uchunguzi na baadhi ya watu walichukuliwa hatua, “nimeshachukua hatua za haraka baada ya kupata hiyo ripoti, tangu mwanzoni mwa mwaka huu wale ambao hawakujaza hiyo miamala tulishawachukulia hatua, hakuna mali iliyopotea MSD.” 
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba kuna ripoti ya Muhimbili ambayo inaonyesha katika vitabu kwamba kuna mzigo ambao Muhimbili iliununua kutoka MSD, lakini haujafika, lakini Bwanakunu alipoulizwa alisema hakuna vitabu vinavyoonyesha kuwa Muhimbili inadai vifaa tiba na dawa MSD. 
 
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru alisema kwa taarifa alizonazo mpaka sasa CAG alifanya ukaguzi katika vitabu vya MSD na si wao na alipouliza vifaa viko wapi alijibiwa kuwa vinakwenda MNH. 
 
Alisema kuwa Watanzania wawe na subira na kwamba watapewa majibu kesho (leo), baada ya Muhimbili kupekua kwa kina vitabu vya mwaka 2012, ili kujiridhisha iwapo vifaa vilipokelewa au havikuwahi kununuliwa Muhimbili. 
 
“Hiyo ripoti tumeiona leo Jumanne. Hayo mambo yametokea mwaka 2012 huwezi kuwa na jibu la kila kitu, kesho tunataka tukapitie hiyo ripoti kwa sababu ni ukaguzi wa MSD, tukaangalie vitabu hivyo vifaa vilifika?” Alisema Museru. 
 
Naye Waziri Ummy Mwalimu alisema katika ripoti hiyo kuna hoja mbili ambazo ni MSD na TFDA, huku akifafanua kwamba amezungumza na Mkurugenzi wa MSD lakini hajaridhika na majibu na kumtaka aandike maelezo ya kina. 
 
“Nimetaka maelezo ya maandishi kutoka kwa MSD na TFDA kuhusu ripoti ya CAG tumekubaliana na Katibu Mkuu walete maandishi ndiyo tutatoa msimamo rasmi wa wizara, kwa upande wa MSD ndiyo maana tuliweka pembeni wale wakurugenzi wanne sababu ya changamoto hii ambayo CAG amekutana nayo,” alisema Ummy.
Share:

Rais Magufuli Aivunja Bodi ya TCRA na Kumsimamisha Kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka Hiyo Dr Ally Yahaya Simba

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameivunja Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Dkt. Ally Yahaya Simba kutokana na kutosimamia ipasavyo Mkataba wa utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa mawasiliano ya simu (TTMS), na kusababisha nchi kupoteza mapato ya takriban shilingi bilioni 400 kwa mwaka.

Rais Magufuli amechukua hatua hiyo leo tarehe 26 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya kufanya kikao cha kazi kati yake na viongozi na wataalamu kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Wizara ya fedha na Mipango na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU).

Tarehe 22 Machi, 2013 Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) iliingia mkataba na kampuni ya SGS juu ya uwekaji, uendeshaji na uhamishaji wa mapato ya simu ambapo kampuni hiyo ilipaswa kutekeleza vipengele vitano lakini mpaka sasa kampuni ya SGS haijaanza kutekeleza kipengele kidogo kinachohusiana na uthibiti wa mapato ya simu za ndani (Offnet), hali ambayo imesababisha serikali kukosa mapato yanayokadiriwa kuwa shilingi bilioni 400 kwa mwaka.

Pamoja na kuivunja bodi ya TCRA inayoongozwa na Profesa Haji Semboja na Kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Ally Yahaya Simba, Rais Magufuli pia amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa Mnyaa kumteua Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo mara moja.

Aidha, Rais Magufuli amewataka Waziri Prof. Mbarawa, Katibu Mkuu na Naibu Katibu katika wizara hiyo kuchukua hatua mara moja ili mfumo wa ukusanyaji wa mapato ya simu kwa simu za ndani (Offnet) uanze kufanya kazi, na nchi ipate mapato yanayostahili kukusanywa.

“Waziri hakikisha unachukua hatua mara moja, nataka tukusanye mapato yote ya serikali yanayostahili na sitasita kuchukua hatua  dhidi ya yoyote atakayekwamisha jambo hili” Amesisitiza Rais Magufuli.

Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Aprili, 2016
Share:

Picha: Rais Mstaafu Benjamini Mkapa Akutana na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Rais Mstaafu wa Tanzania Benjamini Mkapa akiwa na Mwenyeji wake Uhuru Kenyatta katika State House ya Kenya baada ya kukutana na kufanya mazungumzo
Share:

Rais Magufuli Asamehe Wafungwa 3,551

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,551, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Projest Rwegasira ilisema wafungwa 580 wataachiwa huru, huku wengine 2,971 watapunguziwa moja ya sita ya vifungo vyao.

Alisema rais ametoa msamaha huo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aliwataja watakaonufaika na msamaha huo kuwa ni wafungwa wenye ugonjwa wa ukimwi, kifua kikuu na saratani ambao wapo kwenye hatua za mwisho. Wengine ni wazee wenye umri wa miaka 70 na kuendelea, wajawazito na wale waliongia na watoto gerezani.

Wafungwa wengine watakaonufaika na msamaha huo ni wenye ulemavu wa akili ambao wamethibishwa na jopo la waganga kuwa wana tatizo hilo.

Katibu mkuu wa wizara hiyo alisema msamaha huo hautawagusa wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa au kifungo cha maisha jela.

Pia, wafungwa wanaotumikia kifungo kwa makosa ya usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya, upokeaji na utoaji rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, unyang’anyi kwa kutumia silaha na kubaka ni miongoni mwa waliokosa msamaha huo.

Wengine ambao hawataguswa na msamaha huo ni wale wanaotumikia vifungo kwa makosa ya kupatikana na  silaha, wizi wa magari na pikipiki, kuwapa mimba wanafunzi na ubadhirifu wa fedha za Serikali.

Wafungwa wengine watakaoendelea kubaki magerezani ni wale waliohukumiwa kutokana na usafirishaji wa nyara za Serikali na ujangili, utekaji wa watoto, biashara ya binadamu, kukutwa na viungo vya binadamu na waliojaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi.

Katika maadhimisho ya Uhuru yaliyofanyika Desemba 9, 2015, Rais Magufuli aliwasamehe wafungwa 2,336, kati ya hao 117 waliachiwa huru huku 2,219 wakipunguziwa moja ya sita ya vifungo vyao.

Kwa idadi hiyo mpaka sasa wafungwa 5,887 wamenufaika na msamaha wa Rais Magufuli tangu aingie madarakani baada ya kushinda katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, 2015.
Share:

Mke wa Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki ,Mama Lucy Kibaki Afariki Dunia

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mke wa Rais mstaafu  wa    Kenya, mama Lucy Kibaki amefariki dunia . Lucy alifariki katika hospitali ya Bupa Cromwell mjini London alikokuwa amelazwa.

Alisafrishwa hadi mjini Landon wiki moja iliopita kwa matibabu.

Akithibitisha kifo chake rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa kenya imesikitishwa na kifo cha mama Lucy mke wa aliyekuwa rais wa Kenya Mwai Kibaki.

Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari Uhuru amesema bi Lucy amekuwa mgonjwa kwa kipindi cha mwezi mmoja .

Amesema kuwa Kenya imempoteza mwanamke aliyechangia mengi katika maendeleo ya taifa la Kenya hususan katika vita dhidi ya ugonjwa wa ukimwi.

Rais ametuma risala za rambi rambi kwa mtangulizi wake Mwai Kibaki pamoja na familia yake.
Chanzo:BBC
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL TAREHE 27.4.2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
20160427_053527
20160427_053542
20160427_043807
20160427_043852
20160427_043905
20160427_053622
20160427_053635
20160427_043914
20160427_043929
20160427_043939
20160427_044001
20160427_044011
20160427_044020
20160427_044030
20160427_044044
20160427_044055
20160427_044106
20160427_044117
20160427_044135
20160427_044145
20160427_044158
20160427_044206
20160427_044225
20160427_053650
20160427_053700
20160427_053759
20160427_053810
20160427_044235
20160427_044256
20160427_044304
20160427_044348
20160427_044405
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger