INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Monday 28 March 2016
Mechi ya Taifa Stars na Chad Yaota Mbawa........Chad Wamejitoa Kwenye Mashindano Kwa Madai Kwamba Hawana Fedha
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Shirikisho la Soka la Chad, limetangaza kuiondoa timu yake ya taifa
katika mechi za kuwania kufuzu Fainali za Afrika zitakazofanyika nchini
Gabon mwakani.
Tanzania na Chad zilikuwa zicheze leo, mechi ya
marudiano ya kuwania kufuzu fainali hizo. Katika mchezo wa kwanza, Stars
iliifunga Chad bao 1-0, mchezo uliofanyika kwenye mji wa N’Djamena.
Mtandao
wa Twitter wa Shirikisho la Soka Afrika, CAF ulithibitisha jana kupokea
taarifa ya Chad na tayari limetangaza adhabu ya kuisimamisha nchi hiyo.
“Shirikisho la Soka la Chad limeondolewa kushiriki mashindano
yajayo ya Afcon na linatakiwa kulipa faini ya Dola 20,000,” ilisema
taarifa hiyo ya CAF kwa kifupi.
Kujitoa kwa Chad kumevuruga
msimamo wa Kundi G la michuano hiyo kwani kwa mujibu wa Kanuni za
Mashindano ya CAF, Ibara ya 58 inasema: “Ikiwa timu itajitoa kwenye
mashindano hatua za awa li za makundi, matokeo yote yatafutwa (pointi,
mabao ya kufunga na kufungwa).
Ibara ya 59 ya kanuni hizo za mashindano inasema Kamati ya Maandalizi itatoa adhabu kali kulingana na uzito wa timu kujitoa.
Kwa hatua hiyo, Misri iliyoshinda mabao 5-1, Nigeria 2-0 na Tanzania 1-0 zitakuwa zimepoteza matokeo hayo.
Kwa mujibu wa kanuni, Misri sasa itakuwa na pointi nne ikifuatiwa na Nigeria pointi mbili na Tanzania itabakia na pointi moja.
Michezo
itakayobakia ni ya Misri kuifunga Tanzania 3-0 na sare ya 1-1 dhidi ya
Nigeria wakati Taifa Stars inabakiwa na pointi moja ya suluhu na
Nigeria. Nigeria itabakia na pointi mbili za Tanzania na Misri kabla ya
mchezo wao wa kesho kwenye mji wa Alexandria.
Mratibu wa timu ya
Taifa, Msafiri Ahmed Mgoyi alikiri kuziona taarifa za Chad kutocheza
mchezo na kusema: “Tumezipata taarifa hizo lakini bado tunaendelea
kujiandaa kama kawaida mpaka pale tutakapopata taarifa rasmi kutoka TFF
ambao wanapokea maelekezo kutoka Caf.”
Rais wa Shirikisho la
Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi alisema jana kupitia ukurasa wake wa
Twitter kuwa iwapo Chad itashindwa kucheza mchezo, uamuzi wa mwisho
utatolewa na chombo husika kinachosimamia mashindano hayo.
“Hadi
sasa timu ya Chad haijatua nchini kwa ajili ya mechi ya kesho. TFF
itatoa taarifa kamili leo usiku (jana) baada ya kikao cha maandalizi ya
mchezo. Kwa mujibu wa kanuni za CAF Kamati ya Maandalizi ya mashindano
ya Caf ndiyo inatoa uamuzi,” alisema Malinzi.
Kocha Msaidizi wa
Taifa Stars, Hemed Morocco alisema jana kuwa benchi la ufundi na
wachezaji kama ilivyo kwa watu wengine nao wamezipata taarifa hizo
ingawa haziwezi kuathiri saikolojia yao kwa namna yoyote ile.
“Sisi
kwa upande wetu tunafahamu mechi ipo kama kawaida kwani hatujapewa
taarifa yoyote kutoka kwa TFF, hivyo kama ni kweli au la haiwezi
kuvuruga mipango na maandalizi yetu kama timu, ingawa ufafanuzi zaidi
tunausubiri,” alisema Morocco.
Wakati hali hiyo ikitokea,
mashabiki wa soka walikwishaanza kukata tiketi za mchezo kati ya
Sh25,000 ikiwa ni kiingilio cha juu na Sh5,000.
Makonda Aingilia kati Vurugu za makanisani.....Asema Muumini Atakayekimbilia Polisi Kulishitaki Kanisa Atamuweka Rumande
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema mkoa wake hauko
salama kama watu wanavyodhani kwa sababu silaha nyingi zinamilikiwa
kiholela na mafunzo ya matumizi ya silaha hizo hutolewa hata kwa watoto.
Makonda alisema hayo jana wakati wa ibada ya Pasaka
iliyofanyika katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano na kuwataka
wakazi wa Dar es Salaam kujitokeza kuhakiki silaha zao na kusalimisha
zile zinazomilikiwa kinyume cha sheria.
Alisisitiza kwamba
ifikapo Julai Mosi, operesheni maalumu ya kukamata silaha zinazomilikiwa
kinyume cha sheria itaanza na yeye mwenyewe ndiye atakayeiongoza.
“Tumegundua
kwamba kwenye bonde la mto unaotenganisha Mkoa wa Dar es Salaam na
Pwani, kuna mafunzo yanatolewa kwa watoto. Wazazi wanadhani watoto wao
wamekwenda shule kumbe wamechukuliwa huko.Hatuwezi kukubali hali hiyo iendelee."Alisema
Mkuu
huyo wa mkoa aliwataka waumini waendelee kumuombea ili afanye kazi yake
vizuri kwa kutenda haki pia aliwataka pia wamwombee Rais Magufuli kwa
sababu kazi anayoifanya ni kubwa.
Alisema
Rais anapotumbua jipu moja,ndani yake kuna kundi la watu wanaoathirika
na hatua aliyoichukua hivyo, alisema watu wa aina hiyo hawawezi
kumpenda kwa sababu amevunja mtandao wa masilahi yao.
“Ninaomba
kanisa pamoja na viongozi wote wa dini mnisaidie katika kuhimiza suala
la ulinzi na usalama ili amani yetu iendelee kudumu. Ninaomba
tushirikiane katika hilo, Dar es Salaam haiko salama kama mnavyodhani,
mengine siwezi kusema kwa sababu sijaruhusiwa na Rais,” alisema.
Migogoro kanisani
Akizungumzia migogoro makanisani, Makonda alisema
hataki kusikia kiongozi yeyote wa dini anakimbilia polisi au mahakamani
kutaka suluhisho la matatizo yao ya ndani na kuwa atamweka ndani
atakayejaribu kufanya hivyo.
Alisema ni aibu kubwa kwa kanisa
kukimbilia kwenye vyombo vya dola badala ya polisi na Serikali
kukimbilia kanisani kuomba ushauri. Alisema kanisa ndicho chombo cha
usuluhishi wa matatizo mbalimbali ya jamii.
“Serikali inahitaji
msaada wa kanisa na viongozi wa dini ili iweze kufanya kazi vizuri.
Sitaki kusikia polisi wanakwenda kanisani (kukamata watu) katika mkoa
wangu na wale wanaotoa taarifa kutaka polisi nitawaweka ndani,” alisema
Makonda ambaye kabla ya kuwa mkuu wa mkoa, alikuwa mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni.
Askofu Mokiwa
Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana,
Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa alibainisha mambo mbalimbali
aliyoyaita majipu ambayo yanafanya kanisa hilo lisiendelee katika
kufundisha waumini wake yaliyo mema.
Mokiwa alitaja mambo hayo
kuwa ni pamoja na mashindano ya kimadhehebu. Alisema madhehebu
mbalimbali yanashindanishwa kupima kanisa lipi ni kubwa, lina waumini
wangapi, linamilikiwa na nani na nguvu yake ni ipi.
Jambo
jingine alisema ni maaskofu wenyewe kupigana vita. Alisema sasa ni
kawaida kwa askofu mmoja kumchimba mwingine, askofu mmoja kupanga
mapinduzi dhidi ya mwingine na baadhi ya maaskofu kutukanana waziwazi.
20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya
Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa
akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zubeir Mwombeji alisema tukio hilo lilitokea
Machi 24 saa 3.00 usiku maeneo ya Shule ya Msingi Mfaranyaki, karibu na
Kituo Kikuu cha Polisi Songea Mjini.
Mwombeji alimtaja mwanajeshi
huyo aliyejeruhiwa kwa kushambuliwa na waendesha bodaboda kuwa ni Luten
Samweli Nginila (32), ambaye amelazwa Hospitali ya Rufani Mkoa.
Alisema
Luteni Nginila alijeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili na kupoteza
fahamu baada ya kushambuliwa na waendesha bodaboda, ambao walivunja kwa
mawe vioo vya gari alilokuwa akiendesha.
Aliendelea kuwa chanzo
cha tukio hilo, inadaiwa kutokea ajali maeneo ya majengo ambako askari
huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Nissan XTRAIL akitokea Bar ya
Ramour .
Alisema alipofika eneo la majengo, Bahati Mbero
alikatisha ghafla barabarani hivyo askari huyo kushindwa kumudu gari na
kusababisha ajali.
Kufuatia hali hiyo, waendesha bodaboda
waliokuwa karibu walikusanyika kwa lengo la kumshambulia, hali
iliyomlazimu kuwasha gari kukimbia ili kuokoa maisha.
Hata
hivyo, bodaboda hao walimkimbiza na alipofika Shule ya Msingi Mfaranyaki
tairi la gari lake lilichomoka, hivyo walimzingira na kumshushia kipigo
wakiwamo abiria watatu aliokuwa nao.
Mwombeji aliwataja
waliokuwamo ndani ya gari hilo kuwa ni Kaumbya Kateka (24) mkazi wa
Majengo, Joyce Edson (24) mkazi wa Mpambalyoto na Jackline Mwita (22)
mwanafunzi wa Chuo cha Uuguzi Peramiho. Alisema katika vurugu hizo
baadhi ya vitu vilipotea ambavyo ni mali ya askari huyo.
Vitu vilivyopotea ni simu mbili za mkononi, pochi ambayo ilikuwa imehifadhi vitambulisho mbalimbali na Sh120,00.
Alisema wanaendelea kuwabaini wengine waliohusika, taratibu za kuwafikisha mahakamani zitafuata.
Sunday 27 March 2016
Ajali ya Lori Yaua watu 7 na Kujeruhi 10
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
WATU
saba wamekufa na wengine 10 k u j e r u h i w a baada ya gari
walilokuwa wanasafiri nalo aina ya Mitsubishi Fuso kupasuka tairi la
mbele na kugonga kingo za barabara katika barabara kuu ya
Igunga-Singida.
Wengi wao walikuwa wafanyabiashara ya samaki waliokuwa wakitokea Igunga kwenda kijiji cha Loya wilayani Uyui, Tabora.
Kutokea
kwa ajali na vifo hivyo kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa
Tabora, Khamis Selemani Issah aliyesema ilitokea majira ya saa tatu
usiku katika kijiji cha Nanga, kata ya Nanga wilaya ya Igunga.
Alisema
lori hilo lenye namba za usajili T 124 ACS lilibeba abiria wengi
kinyume na sheria za usafirishaji wa abiria na kuongeza kuwa hatua kali
zitachukuliwa kwa watakaobanika kubeba abiria katika magari ya mizigo.
Mara
baada ya ajali hiyo, dereva wake aliyetajwa kuwa ni Joseph Masali
alitoweka eneo la tukio na jeshi la polisi linamtafuta aweze kujibu
tuhumu zinazomkabili kuhusiana na ajali hiyo.
Kamanda
huyo aliendelea kusema ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa dereva
kutokana na mwendo kasi pamoja na pia kwa kuvunja sheria ya kubeba
abiria kwa gari la mizigo.
Mganga
Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Abdallah Ombeni alipokea
majeruhi 11 na miili 6 katika hospital hiyo huku majeruhi mmoja
alisafirishwa katika Hospital ya Rufaa ya Nkinga kwa matibabu zaidi
kutokana na hali yake kuwa mbaya, hata hivyo alifariki dunia akiwa
njiani.
Amewataja
waliokufa kuwa ni Masesa Sagalali, Omar Rajabu, Shaaban Ibrahim,
Sagalali Maige, Selestine Lipande, Juma Iddi na mwingine aliyetambulika
kwa jina mmoja la James. Juma Hassan, mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo
alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.
Mama Aporwa Kitoto Kichanga Bugando
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
MTOTO wa siku moja ameibwa katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.
Akizungumzia uporaji huo jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amesema aliyepora mtoto huyo aliingia ndani ya wodi ya wazazi ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa amejifunga ushungi.
“Alipoingia wodini alikuta mama wa mtoto amesinzia akiwa peke yake wodini, ndipo akamuiba mtoto wake wa kike mwenye umri wa siku moja na kuondoka naye kwenda kusikojulikana,” alisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kuhoji wauguzi, walinzi na wazazi waliokuwa wamelazwa wodini hapo.
Katika hatua nyingine, Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la Polisi mkoani humo, litaanza kufanya uhakiki wa silaha kuanzia Aprili mosi hadi Juni 30 mwaka huu, katika ofisi za makamanda wa Polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.
Amesema uhakiki wa silaha ni wa kitaifa na utahusu wamiliki binafsi, kampuni binafsi na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zinazomiliki silaha.
“Lengo ni kupata kumbukumbu ya uhalali wa umiliki wa silaha. Watu wote wanaomiliki silaha watii agizo hili bila kulazimishwa, ili tufanikishe uhakiki kwa wakati na tuimarishe usalama katika mkoa wetu,” alisema.
Aliwataka watu wanaomiliki silaha isivyo halali, kusalimisha silaha hizo wenyewe kwenye ofisi za Serikali na kwa wakuu wa Polisi wa wilaya (OCD) kabla ya muda wa uhakiki wa silaha kumalizika.
“Baada ya hapo tutafanya msako kabambe wa watu waliokaidi kuhakiki silaha zao,” alisema.
MTOTO wa siku moja ameibwa katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.
Akizungumzia uporaji huo jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amesema aliyepora mtoto huyo aliingia ndani ya wodi ya wazazi ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa amejifunga ushungi.
“Alipoingia wodini alikuta mama wa mtoto amesinzia akiwa peke yake wodini, ndipo akamuiba mtoto wake wa kike mwenye umri wa siku moja na kuondoka naye kwenda kusikojulikana,” alisema.
Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kuhoji wauguzi, walinzi na wazazi waliokuwa wamelazwa wodini hapo.
Katika hatua nyingine, Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la Polisi mkoani humo, litaanza kufanya uhakiki wa silaha kuanzia Aprili mosi hadi Juni 30 mwaka huu, katika ofisi za makamanda wa Polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.
Amesema uhakiki wa silaha ni wa kitaifa na utahusu wamiliki binafsi, kampuni binafsi na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zinazomiliki silaha.
“Lengo ni kupata kumbukumbu ya uhalali wa umiliki wa silaha. Watu wote wanaomiliki silaha watii agizo hili bila kulazimishwa, ili tufanikishe uhakiki kwa wakati na tuimarishe usalama katika mkoa wetu,” alisema.
Aliwataka watu wanaomiliki silaha isivyo halali, kusalimisha silaha hizo wenyewe kwenye ofisi za Serikali na kwa wakuu wa Polisi wa wilaya (OCD) kabla ya muda wa uhakiki wa silaha kumalizika.
“Baada ya hapo tutafanya msako kabambe wa watu waliokaidi kuhakiki silaha zao,” alisema.
Saturday 26 March 2016
NACTE;HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA NA KOZI MBALIMBALI ZITOLEWAZO NA VYUO VILIVYO CHINI YA NACTE 2016/2017
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
PUBLIC NOTICE - MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS FOR ACADEMIC YEAR 2016/17
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
(NACTE)
PUBLIC NOTICE
MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS
The
National Council for Technical Education (NACTE), would like to inform
the Public and other Education stakeholders on the minimum entry
requirements to join Basic Technician Certificate (NTA Level 4), which
will eventually lead to Ordinary Diploma (NTA Level 6) for successful
Candidates.
An
applicant should possess secondary certificate from National
Examinations Council of Tanzania (NECTA) with a minimum of four passes
(Four D’s) excluding religious subjects. Holders of foreign certificates
should submit to NECTA for equivalence of their awards to Tanzania
awards system to enable them to Apply.
It should be noted that, the entire process of admission is done via Central Admission System (CAS). For more information about registration status for Institutions and programmes/ courses offered, kindly visit our website at www.nacte.go.tz.
ISSUED BY;
THE OFFICE OF EXECUTIVE SECRETARY
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
24th March, 2016
Majambazi Waua Watu Wawili na Kujeruhi Saba Jijini Mwanza
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Watu
wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku
Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa
likitoa huduma mbalimbali za kifedha.
Kamanda
wa Polisi Mkoani Mwanza, Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo
lilitokea jana majira ya saa mbili usiku katika eneo la Bugarika Sokoni,
baada ya watu watatu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliokuwa na
bunduki aina ya SMG kuvamia katika duka la mfanyabiashara na mkazi wa
eneo hilo aitwae Daniel Marwa (30).
Kamanda
Kamugisha amewataja waliouawa kuwa ni Julius Wankaba (30) ambae ni
dereva bodaboda, pamoja na mfanyabiashara mmoja mwenye duka katika eneo
hilo aliefahamika kwa jina la Mama Yuni (35).
Amewataja
waliojeruhiwa kuwa ni Magesa Mungari (38), Simioni Charles (26) ambao
wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando huku wengine wakiwa ni Mwita
Ryoba (30), Frank Willium (19), Saumu Said (20), Masumbuko Kanduru (38)
pamoja na Emmanuel Francis ambao wanapata matibabu katika Hospital ya
Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure.
Baadhi
ya Mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo mmiliki wa duka lililovamiwa,
wanasema majambazi hao walipofika eneo la tukio walianza kufyatua risasi
ovyo ili kuwatawanya wananchi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo
wakiangalia taarifa ya habari na wengine wakinywa kahawa, na hivyo
kusababisha wananchi kutawanyika jambo lililosababisha vifo na majeruhi
hao.
Katika
tukio hilo, Majambazi hao walifanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha
Shilingi Milioni Mbili, Vocha za simu za mitandao mbalimbali
zinazokadiliwa kuwa za shilingi Laki Nane pamoja na simu sita za wateja.
Kamanda
Kamugisha amesema Jeshi la polisi Mkoani Mwanza limeanzisha msako mkali
ili kuwakamata waliohusika na tukio hilo, huku likiahidi zawadi ya
fedha kiasi cha shilingi Milioni Moja kwa yeyote atakaesaidia kufanikiwa
kukamatwa kwa watuhumiwa hao.
Wakati
huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linaendelea kumsaka mtu
aliehusika na wizi wa mtoto mwenye umri wa siku moja katika Hospitali ya
Wilaya ya Magu, ambapo tukio hilo limetokea Machi 23 mwaka huu, majira
ya saa nane mchana baada ya mtu mmoja asiefahamika mwenye jinsia ya
kike, kufika katika wodi ya wazazi na kumuiba mtoto huyo wakati mama
yake amelala.
Aidha
katika katika kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, Jeshi hilo limepiga
marufuku watoto kwenda kuogelea katika fukweni (Beach) pamoja na uwepo
wa disko toto Jijini Mwanza.