Monday 28 March 2016

Mechi ya Taifa Stars na Chad Yaota Mbawa........Chad Wamejitoa Kwenye Mashindano Kwa Madai Kwamba Hawana Fedha

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Shirikisho la Soka la Chad, limetangaza kuiondoa timu yake ya taifa katika mechi za kuwania kufuzu Fainali za Afrika zitakazofanyika nchini Gabon mwakani.

Tanzania na Chad zilikuwa zicheze leo, mechi ya marudiano ya kuwania kufuzu fainali hizo. Katika mchezo wa kwanza, Stars iliifunga Chad bao 1-0, mchezo uliofanyika kwenye mji wa N’Djamena.

Mtandao wa Twitter wa Shirikisho la Soka Afrika, CAF ulithibitisha jana kupokea taarifa ya Chad na tayari limetangaza adhabu ya kuisimamisha nchi hiyo.

“Shirikisho la Soka la Chad limeondolewa kushiriki mashindano yajayo ya Afcon na linatakiwa kulipa faini ya Dola 20,000,” ilisema taarifa hiyo ya CAF kwa kifupi.

Kujitoa kwa Chad kumevuruga msimamo wa Kundi G la michuano hiyo kwani kwa mujibu wa Kanuni za Mashindano ya CAF, Ibara ya 58 inasema: “Ikiwa timu itajitoa kwenye mashindano hatua za awa li za makundi, matokeo yote yatafutwa (pointi, mabao ya kufunga na kufungwa).

Ibara ya 59 ya kanuni hizo za mashindano inasema Kamati ya Maandalizi itatoa adhabu kali kulingana na uzito wa timu kujitoa.

Kwa hatua hiyo, Misri iliyoshinda mabao 5-1, Nigeria 2-0 na Tanzania 1-0 zitakuwa zimepoteza matokeo hayo.

Kwa mujibu wa kanuni, Misri sasa itakuwa na pointi nne ikifuatiwa na Nigeria pointi mbili na Tanzania itabakia na pointi moja.

Michezo itakayobakia ni ya Misri kuifunga Tanzania 3-0 na sare ya 1-1 dhidi ya Nigeria wakati Taifa Stars inabakiwa na pointi moja ya suluhu na Nigeria. Nigeria itabakia na pointi mbili za Tanzania na Misri kabla ya mchezo wao wa kesho kwenye mji wa Alexandria.

Mratibu wa timu ya Taifa, Msafiri Ahmed Mgoyi alikiri kuziona taarifa za Chad kutocheza mchezo na kusema: “Tumezipata taarifa hizo lakini bado tunaendelea kujiandaa kama kawaida mpaka pale tutakapopata taarifa rasmi kutoka TFF ambao wanapokea maelekezo kutoka Caf.”

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi alisema jana kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa iwapo Chad itashindwa kucheza mchezo, uamuzi wa mwisho utatolewa na chombo husika kinachosimamia mashindano hayo.

“Hadi sasa timu ya Chad haijatua nchini kwa ajili ya mechi ya kesho. TFF itatoa taarifa kamili leo usiku (jana) baada ya kikao cha maandalizi ya mchezo. Kwa mujibu wa kanuni za CAF Kamati ya Maandalizi ya mashindano ya Caf ndiyo inatoa uamuzi,” alisema Malinzi.

Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Hemed Morocco alisema jana kuwa benchi la ufundi na wachezaji kama ilivyo kwa watu wengine nao wamezipata taarifa hizo ingawa haziwezi kuathiri saikolojia yao kwa namna yoyote ile.

“Sisi kwa upande wetu tunafahamu mechi ipo kama kawaida kwani hatujapewa taarifa yoyote kutoka kwa TFF, hivyo kama ni kweli au la haiwezi kuvuruga mipango na maandalizi yetu kama timu, ingawa ufafanuzi zaidi tunausubiri,” alisema Morocco.

Wakati hali hiyo ikitokea, mashabiki wa soka walikwishaanza kukata tiketi za mchezo kati ya Sh25,000 ikiwa ni kiingilio cha juu na Sh5,000.
Share:

Makonda Aingilia kati Vurugu za makanisani.....Asema Muumini Atakayekimbilia Polisi Kulishitaki Kanisa Atamuweka Rumande

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema mkoa wake hauko salama kama watu wanavyodhani kwa sababu silaha nyingi zinamilikiwa kiholela na mafunzo ya matumizi ya silaha hizo hutolewa hata kwa watoto.

Makonda alisema hayo jana wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano na kuwataka wakazi wa Dar es Salaam kujitokeza kuhakiki silaha zao na kusalimisha zile zinazomilikiwa kinyume cha sheria.

Alisisitiza kwamba ifikapo Julai Mosi, operesheni maalumu ya kukamata silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria itaanza na yeye mwenyewe ndiye atakayeiongoza.

“Tumegundua kwamba kwenye bonde la mto unaotenganisha Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani, kuna mafunzo yanatolewa kwa watoto. Wazazi wanadhani watoto wao wamekwenda shule  kumbe wamechukuliwa huko.Hatuwezi kukubali hali hiyo iendelee."Alisema
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka waumini waendelee kumuombea ili afanye kazi yake vizuri kwa kutenda  haki pia aliwataka pia wamwombee Rais Magufuli  kwa sababu kazi anayoifanya ni kubwa.
Alisema Rais anapotumbua jipu moja,ndani yake kuna kundi la watu wanaoathirika na hatua aliyoichukua hivyo, alisema watu wa aina hiyo hawawezi kumpenda kwa sababu amevunja mtandao wa masilahi yao.

“Ninaomba kanisa pamoja na viongozi wote wa dini mnisaidie katika kuhimiza suala la ulinzi na usalama ili amani yetu iendelee kudumu. Ninaomba tushirikiane katika hilo, Dar es Salaam haiko salama kama mnavyodhani, mengine siwezi kusema kwa sababu sijaruhusiwa na Rais,” alisema. 
Migogoro kanisani 
Akizungumzia migogoro makanisani, Makonda alisema hataki kusikia kiongozi yeyote wa dini anakimbilia polisi au mahakamani kutaka suluhisho la matatizo yao ya ndani na kuwa atamweka ndani atakayejaribu kufanya hivyo.

Alisema ni aibu kubwa kwa kanisa kukimbilia kwenye vyombo vya dola badala ya polisi na Serikali kukimbilia kanisani kuomba ushauri. Alisema kanisa ndicho chombo cha usuluhishi wa matatizo mbalimbali ya jamii.

“Serikali inahitaji msaada wa kanisa na viongozi wa dini ili iweze kufanya kazi vizuri. Sitaki kusikia polisi wanakwenda kanisani (kukamata watu) katika mkoa wangu na wale wanaotoa taarifa kutaka polisi nitawaweka ndani,” alisema Makonda ambaye kabla ya kuwa mkuu wa mkoa, alikuwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.
 Askofu Mokiwa 
Awali, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa alibainisha mambo mbalimbali aliyoyaita majipu ambayo yanafanya kanisa hilo lisiendelee katika kufundisha waumini wake yaliyo mema.

Mokiwa alitaja mambo hayo kuwa ni pamoja na mashindano ya kimadhehebu. Alisema madhehebu mbalimbali yanashindanishwa kupima kanisa lipi ni kubwa, lina waumini wangapi, linamilikiwa na nani na nguvu yake ni ipi.

Jambo jingine alisema ni maaskofu wenyewe kupigana vita. Alisema sasa ni kawaida kwa askofu mmoja kumchimba mwingine, askofu mmoja kupanga mapinduzi dhidi ya mwingine na baadhi ya maaskofu kutukanana waziwazi.
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MARCH 28 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zubeir Mwombeji alisema tukio hilo lilitokea Machi 24 saa 3.00 usiku maeneo ya Shule ya Msingi Mfaranyaki, karibu na Kituo Kikuu cha Polisi Songea Mjini.

Mwombeji alimtaja mwanajeshi huyo aliyejeruhiwa kwa kushambuliwa na waendesha bodaboda kuwa ni Luten Samweli Nginila (32), ambaye amelazwa Hospitali ya Rufani Mkoa.

Alisema Luteni Nginila alijeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili na kupoteza fahamu baada ya kushambuliwa na waendesha bodaboda, ambao walivunja kwa mawe vioo vya gari alilokuwa akiendesha.

Aliendelea kuwa chanzo cha tukio hilo, inadaiwa kutokea ajali maeneo ya majengo ambako askari huyo alikuwa akiendesha gari aina ya Nissan XTRAIL akitokea Bar ya Ramour .

Alisema alipofika eneo la majengo, Bahati Mbero alikatisha ghafla barabarani hivyo askari huyo kushindwa kumudu gari na kusababisha ajali.

Kufuatia hali hiyo, waendesha bodaboda waliokuwa karibu walikusanyika kwa lengo la kumshambulia, hali iliyomlazimu kuwasha gari kukimbia ili kuokoa maisha.

Hata hivyo, bodaboda hao walimkimbiza na alipofika Shule ya Msingi Mfaranyaki tairi la gari lake lilichomoka, hivyo walimzingira na kumshushia kipigo wakiwamo abiria watatu aliokuwa nao.

Mwombeji aliwataja waliokuwamo ndani ya gari hilo kuwa ni Kaumbya Kateka (24) mkazi wa Majengo, Joyce Edson (24) mkazi wa Mpambalyoto na Jackline Mwita (22) mwanafunzi wa Chuo cha Uuguzi Peramiho. Alisema katika vurugu hizo baadhi ya vitu vilipotea ambavyo ni mali ya askari huyo.

Vitu vilivyopotea ni simu mbili za mkononi, pochi ambayo ilikuwa imehifadhi vitambulisho mbalimbali na Sh120,00.

Alisema wanaendelea kuwabaini wengine waliohusika, taratibu za kuwafikisha mahakamani zitafuata.
Share:

New AUDIO | Alice Kella & Vanessa Mdee, Ruby, Maua Sama, Ibrah - Awena Remix | Download

Share:

Sunday 27 March 2016

Ajali ya Lori Yaua watu 7 na Kujeruhi 10

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

WATU saba wamekufa na wengine 10  k u j e r u h i w a baada ya gari walilokuwa wanasafiri nalo aina ya Mitsubishi Fuso kupasuka tairi la mbele na kugonga kingo za barabara katika barabara kuu ya Igunga-Singida.

Wengi wao walikuwa wafanyabiashara ya samaki waliokuwa wakitokea Igunga kwenda kijiji cha Loya wilayani Uyui, Tabora.

Kutokea kwa ajali na vifo hivyo kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora, Khamis Selemani Issah aliyesema ilitokea majira ya saa tatu usiku katika kijiji cha Nanga, kata ya Nanga wilaya ya Igunga.

Alisema lori hilo lenye namba za usajili T 124 ACS lilibeba abiria wengi kinyume na sheria za usafirishaji wa abiria na kuongeza kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa watakaobanika kubeba abiria katika magari ya mizigo.

Mara baada ya ajali hiyo, dereva wake aliyetajwa kuwa ni Joseph Masali alitoweka eneo la tukio na jeshi la polisi linamtafuta aweze kujibu tuhumu zinazomkabili kuhusiana na ajali hiyo.

Kamanda huyo aliendelea kusema ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa dereva kutokana na mwendo kasi pamoja na pia kwa kuvunja sheria ya kubeba abiria kwa gari la mizigo.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Abdallah Ombeni alipokea majeruhi 11 na miili 6 katika hospital hiyo huku majeruhi mmoja alisafirishwa katika Hospital ya Rufaa ya Nkinga kwa matibabu zaidi kutokana na hali yake kuwa mbaya, hata hivyo alifariki dunia akiwa njiani.

Amewataja waliokufa kuwa ni Masesa Sagalali, Omar Rajabu, Shaaban Ibrahim, Sagalali Maige, Selestine Lipande, Juma Iddi na mwingine aliyetambulika kwa jina mmoja la James. Juma Hassan, mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi.
Share:

Mama Aporwa Kitoto Kichanga Bugando

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha

MTOTO wa siku moja ameibwa katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.

Akizungumzia uporaji huo jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha, amesema aliyepora mtoto huyo aliingia ndani ya wodi ya wazazi ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa amejifunga ushungi.

“Alipoingia wodini alikuta mama wa mtoto amesinzia akiwa peke yake wodini, ndipo akamuiba mtoto wake wa kike mwenye umri wa siku moja na kuondoka naye kwenda kusikojulikana,” alisema.

Kwa mujibu wa Kamanda Kamugisha, Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kuhoji wauguzi, walinzi na wazazi waliokuwa wamelazwa wodini hapo.

Katika hatua nyingine, Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la Polisi mkoani humo, litaanza kufanya uhakiki wa silaha kuanzia Aprili mosi hadi Juni 30 mwaka huu, katika ofisi za makamanda wa Polisi wa wilaya zote za Mkoa wa Mwanza.

Amesema uhakiki wa silaha ni wa kitaifa na utahusu wamiliki binafsi, kampuni binafsi na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za kiserikali zinazomiliki silaha.

“Lengo ni kupata kumbukumbu ya uhalali wa umiliki wa silaha. Watu wote wanaomiliki silaha watii agizo hili bila kulazimishwa, ili tufanikishe uhakiki kwa wakati na tuimarishe usalama katika mkoa wetu,” alisema.

Aliwataka watu wanaomiliki silaha isivyo halali, kusalimisha silaha hizo wenyewe kwenye ofisi za Serikali na kwa wakuu wa Polisi wa wilaya (OCD) kabla ya muda wa uhakiki wa silaha kumalizika.

“Baada ya hapo tutafanya msako kabambe wa watu waliokaidi kuhakiki silaha zao,” alisema.
Share:

Magazeti Ya Leo Jumapili Ya March 27, 2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Share:

Saturday 26 March 2016

New AUDIO | Yemia Alade Ft. Sauti Sol - Africa | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/9tsxwhj0qdq8/Yemia_Alade_ft_Sauti_Sol_-_Africa.mp3?d=1
Share:

NACTE;HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA NA KOZI MBALIMBALI ZITOLEWAZO NA VYUO VILIVYO CHINI YA NACTE 2016/2017

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

PUBLIC NOTICE - MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS FOR ACADEMIC YEAR 2016/17

 
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
(NACTE)
PUBLIC NOTICE
MINIMUM ENTRY REQUIREMENTS

The National Council for Technical Education (NACTE), would like to inform the Public and other Education stakeholders on the minimum entry requirements to join Basic Technician Certificate (NTA Level 4), which will eventually lead to Ordinary Diploma (NTA Level 6) for successful Candidates.
An applicant should possess secondary certificate from National Examinations Council of Tanzania (NECTA) with a minimum of four passes (Four D’s) excluding religious subjects. Holders of foreign certificates should submit to NECTA for equivalence of their awards to Tanzania awards system to enable them to Apply.
It should be noted that, the entire process of admission is done via Central Admission System (CAS). For more information about registration status for Institutions and programmes/ courses offered, kindly visit our website at www.nacte.go.tz.

ISSUED BY;
THE OFFICE OF EXECUTIVE SECRETARY
THE NATIONAL COUNCIL FOR TECHNICAL EDUCATION
24th March, 2016
Share:

Majambazi Waua Watu Wawili na Kujeruhi Saba Jijini Mwanza

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Watu wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa likitoa huduma mbalimbali za kifedha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Justus Kamugisha, amesema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa mbili usiku katika eneo la Bugarika Sokoni, baada ya watu watatu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliokuwa na bunduki aina ya SMG kuvamia katika duka la mfanyabiashara na mkazi wa eneo hilo aitwae Daniel Marwa (30).

Kamanda Kamugisha amewataja waliouawa kuwa ni Julius Wankaba (30) ambae ni dereva bodaboda, pamoja na mfanyabiashara mmoja mwenye duka katika eneo hilo aliefahamika kwa jina la Mama Yuni (35).

Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Magesa Mungari (38), Simioni Charles (26) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa Bugando huku wengine wakiwa ni Mwita Ryoba (30), Frank Willium (19), Saumu Said (20), Masumbuko Kanduru (38) pamoja na Emmanuel Francis ambao wanapata matibabu katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure.

Baadhi ya Mashuhuda wa tukio hilo, akiwemo mmiliki wa duka lililovamiwa, wanasema majambazi hao walipofika eneo la tukio walianza kufyatua risasi ovyo ili kuwatawanya wananchi waliokuwa wamekusanyika katika eneo hilo wakiangalia taarifa ya habari na wengine wakinywa kahawa,  na hivyo kusababisha wananchi kutawanyika jambo lililosababisha vifo na majeruhi hao.

Katika tukio hilo, Majambazi hao walifanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni Mbili, Vocha za simu za mitandao mbalimbali zinazokadiliwa kuwa za shilingi Laki Nane pamoja na simu sita za wateja.

Kamanda Kamugisha amesema Jeshi la polisi Mkoani Mwanza limeanzisha msako mkali ili kuwakamata waliohusika na tukio hilo, huku likiahidi zawadi ya fedha kiasi cha shilingi Milioni Moja kwa yeyote atakaesaidia kufanikiwa kukamatwa kwa watuhumiwa hao.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza linaendelea kumsaka mtu aliehusika na wizi wa mtoto mwenye umri wa siku moja katika Hospitali ya Wilaya ya Magu, ambapo tukio hilo limetokea Machi 23 mwaka huu, majira ya saa nane mchana baada ya mtu mmoja asiefahamika mwenye jinsia ya kike, kufika katika wodi ya wazazi na kumuiba mtoto huyo wakati mama yake amelala.

Aidha katika katika kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, Jeshi hilo limepiga marufuku watoto kwenda kuogelea katika fukweni (Beach) pamoja na uwepo wa disko toto Jijini Mwanza.
Share:

New AUDIO | Shery Zuu Ft. Msaga Sumu - Babu Uyo | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
http://old.hulkshare.com/dl/xe5p61m1hn28/Shery_Zuu_Ft_Msaga_Sumu_-_Babu_Uyo.mp3?d=1
Share:

NAFASI ZA MASOMO BUGANDO UNIVERSITY 2016/2017 NGAZI ZA YA DIPLOMA NA POSTGRADUATE,HIZI NDIO SIFA ZA KUJIUNGA BUGANDO

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Application and Medical Forms Downloads 



MODE OF APPLICATION FOR UNDERGRADUATE PROGRAMMES

Applicants with the appropriate “A” Levels passes (Direct Entrants) and Diploma Holders (Equivalent qualification) seeking admission at CUHAS into the Bachelor of Medical Lab Sciences (Code CU001), Bachelor of Science in Nursing Education (Code CU002), the Bachelor of Pharmacy (Code CU003), Doctor of Medicine (Code CU004) and Bachelor of Science in Nursing (CU005) are required to apply through the CENTRAL ADMISSION SYSTEM with the Tanzania Commission for Universities (TCU) using the guidelines provided by TCU as detailed in pages 35,36,37.

    Undergraduate Courses:


  • DOCTOR OF MEDICINE (MD) – 5 YEARS
  • Direct Entrants (Form Six)
    Holders of Principal pass at “C” grade or higher in Chemistry, Biology or Physics, provided that the other two passes are not below “D” at ADVANCED level. Preference will be given to applicants with "C" grade or higher in Chemistry or Biology in that order.Consideration will also be given to applicants with Principal passes at C grade on higher in Chemistry and a ‘D’ grade or higher in Biology or Physics. [C, D (5 points from 2 subjects)]

    Equivalent Qualifications
    Holders of B. Sc. Degrees from recognized institutions, majoring in BIOLOGY or CHEMISTRY. Holders of a Diploma in Clinical Medicine with principal passes at any level in Chemistry, Biology or Physics, in the ADVANCED certificate examinations.

  • BACHELOR OF MEDICAL LAB SCIENCE BMLS) – 3 YEARS
  • Direct Entrants (Form Six)
    Direct Entrants (Form Six) Holders of three Principal passes in Biology, Chemistry or Physics/Geography; provided 2 principal passes are at D level or higher [D,D,E(minimum 5 points from three subjects)] Consideration will also be given to applicants with two principal passes in Physics, Chemistry or Biology provided that one of them is at C grade or higher [C,E (4 points from 2 subjects)]

    Equivalent Qualifications
    Holder of an appropriate Diploma/Advanced Diploma with three Principal passes at any grade in Physics, Chemistry and Biology at “A” level. Appropriate Diploma/Advanced Diploma with at least three credit passes at any grade in Physics, Chemistry, Biology, Mathematics and English at “O” level and has passed Diploma/Advanced Diploma with an average of B grade or above. Preference will be given to students who have attempted “A” level.

  • BACELOR OF PHARMACY (B.PHARM) -
  • Direct Entrants (Form Six)
    Principal pass at C grade or higher in Chemistry, Biology or Physics provided that the other two subjects are NOT below D at (“A”) level. Preference will be given to applicants with “C” grade or above in CHEMISTRY or BIOLOGY in that order. Consideration will also be given to applicants with Principal passes at C grade on higher in Chemistry and a ‘D’ grade higher in Biology or Physics [C, D (5 points from 2 subjects)].

    Equivalent Qualifications
    A Diploma in Pharmacy from a recognized and accredited Institution with passes at a minimum of “B” grade in all Diploma subjects with three principal passes at E grade in Physics/Geography and Chemistry and Biology at “A” Level provided a minimum pass of C in Biology and D in Chemistry was obtained at “O” Level.

  • BACHELOR OF SCIENCE IN NURSING EDUCATION
  • Direct Entrants (Form Six)
    Holder of form-six certificate with THREE Advanced level passes in Physics, Chemistry and Biology; at least TWO passes are at “D” or higher.

    Equivalent Qualifications (3 Year Programme)
    Holder of Diploma in nursing with at least THREE credits in the following subjects: Biology, Chemistry, Physics, Mathematics and English. They should have a working experience of at least 2 years. Preference will be given for those who have attempted “A” Level.

    Equivalent Qualifications (2 Year Conversion Programme)
    Holder of Advanced Diploma in Nursing Education with at least THREE credits in the following subjects of “O” Level secondary certificate: Biology, Chemistry, Physics, Mathematics and English.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger