Saturday 26 March 2016

Kificho Ang’oka Uspika

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


Pandu Ameir Kificho
ALIYEKUWA Spika wa Baraza la Wawakilishi kwa zaidi ya miaka 20 sasa, Pandu Ameir Kificho, ameng’olewa katika nafasi hiyo baada ya kushindwa katika kura za kuwania awamu nyingine ya uongozi wa baraza hilo.

Badala yake wajumbe wateule wa Baraza la Wawakilishi, wamemchagua Zubeir Ali Maulid, kuwa Spika mteule wa baraza hilo, baada ya kupata kura 55 na kumuacha kwa mbali Kificho aliyeambulia kura 11 katika uchaguzi uliofanyika jana katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar.

Aidha katika uchaguzi huo ambao wawakilishi 72 walipiga kura, Janeth Nora Sekihola ambaye ni hakimu mstaafu akipata kura 4 wakati kura mbili ziliharibika.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangushwa katika uchaguzi huo, Kificho alisema amekubali kushindwa na yupo tayari kutoa ushirikiano akitakiwa kufanya hivyo.

“Hiyo ndiyo demokrasia, nimekubali kushindwa na nipo tayari kutoa ushirikiano mkubwa nikitakiwa kufanya hivyo kwa sababu ni ukweli kwamba ninao uzoefu mkubwa katika nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka 20,” alisema.

Naye Spika mteule wa baraza hilo, Maulid alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya kuleta maendeleo na mabadiliko makubwa katika chombo hicho ambacho ni moja ya mihimili ya dola katika utekelezaji wa majukumu yake.

Amesema atatumia uzoefu alioupata kufanya kazi katika taasisi za kutunga sheria, kwa ajili ya kuleta mabadiliko hayo kwa kuhakikisha kwamba Baraza la Wawakilishi linafanya kazi inayotakiwa ya kuisimamia Serikali kwa mujibu wa Katiba.

“Nimekuwa Mwakilishi Shauri Moyo na Waziri mwaka 2000, pia nimekuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa miaka miwili na nusu kwa hivyo uwezo wa kufanya kazi katika mabunge ya Jumuiya ya Madola ninao mkubwa,” alisema.

Aliwaomba wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wateule kumpa kila aina ya ushirikiano utakaomwezesha kutekeleza na kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, kwani chombo hicho ni moja ya mihimili ya dola.

Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliozungumza na gazeti hili, wamesema kwamba mabadiliko hayo ni ishara na ujumbe tosha kwa Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kwamba wawakilishi wanataka mabadiliko makubwa kwa Serikali kwa ajili ya kuwatumikia wananchi.

“Mabadiliko makubwa tuliyoyafanya sisi wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa kumchagua Zubeir Ali Maulidi kuwa Spika mteule mpya, ni dalili tosha kwamba sasa tunataka mabadiliko makubwa ndani ya Serikali kwa kuwa na viongozi watakaowatumikia wananchi moja kwa moja,” alisema Rashid Ali Juma mwakilishi mteule wa jimbo la Amani.

Kificho ameweka historia kuwa Spika wa Kwanza katika Baraza la Wawakilishi la mfumo wa vyama vingi kuanzia mwaka 1995, ambapo kabla ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo, alikuwa mwakilishi wa Jimbo la Makunduchi kuanzia 1988.

Zubeir Ali Maulid mwaka 2000 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Shauri Moyo kwa tiketi ya CCM na kuteuliwa kuwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, chini ya Serikali ya Rais mstaafu Amani Abeid Karume, ambapo alidumu katika wadhifa huo kwa miaka mitatu.

Mwaka 2005, Zubeir alichaguliwa kuwa Mbunge wa Kwamtipura kwa tiketi ya CCM ambapo akiwa bungeni katika kipindi cha miaka miwili na nusu, alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na kuongoza vikao mbali mbali kwa kusaidiana na spika na naibu spika.

Katika hatua nyingine, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein, amemteua Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Uteuzi huo ndio wa kwanza kufanyika, tangu Rais Shein alipokula kiapo cha kuongoza Zanzibar kwa miaka mitano ijayo Alhamisi ya wiki hii.
Share:

Viongozi wa Dini Wakumbusha Kutenda Haki

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY



Askofu Msaidizi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa.

WAKATI Rais John Magufuli, Baraza la Mawaziri na viongozi wengine wakiombewa ili kufanya kazi vizuri katika ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika jana, viongozi mbalimbali wamekumbushwa kutimiza wajibu wao wa kuwatumikia wananchi kwa haki bila kushinikizwa.

Akihubiri katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Maxmillian Maria Kolbe, Mwenge jijini Dar es Salaam, Askofu Msaidizi, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa, alisema ni vyema viongozi katika jamii wakumbuke wamepewa dhamana ya kuangalia wengine na kuongoza kwa haki na kuacha tabia ya ubinafsi na maamuzi ya kushinikizwa.

“Sisi tuliopewa dhamana tuamue kwa haki na kamwe tusiamue kwa shinikizo, kwa sababu ni heri kufa shahidi kuliko kuangamiza damu za watu wasio na hatia,” alisema Askofu Nzigilwa katika Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kitaifa kanisani hapo.

Aliwataka waumini kutumia Ibada ya Ijumaa Kuu kuwa kiele- lezo cha upendo kwa wengine na kamwe usaliti usiwepo kwa kuwa ni jambo baya lin- aloleta uharibifu. Alisema usaliti uliofanywa na Yuda Iskariote wa kumbusu Yesu Kristo, ni jambo gumu linalotakiwa kuepukwa na wanadamu kwa sababu ni sumu inayoua.

“Matendo ya unafiki na usaliti ni mabaya, kwa sababu mtu au watu wanaofanya huyafanya dhidi ya wengine huku mkichekeana, lakini kwa ndani unamuua, tafadhali tusiwe na sura mbili, kama ni ndiyo iwe ndiyo na sio iwe sio,” alisema Askofu Nzigilwa.

Naye Askofu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk Valentino Mokiwa, amewataka Watanzania hasa waumini wa dini ya Kikristo kuachana na dhambi na kuishi katika uadilifu unaompendeza Mungu.

Akizungumza baada ya misa ya Ijumaa Kuu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano, Askofu Mokiwa alisema, kuna kila haja ya watu kubadilika na kuachana na maisha ya dhambi kwa kuwa hayampendezi Mungu.

Naye Padre Nicholaus Masamba wa katika Kanisa Kuu Katoliki la Mtakatifu Joseph, aliwataka Watanzania kutekeleza wajibu wao katika mambo mbalimbali ili kuhakikisha familia zinakua na maadili mazuri.

“Wazazi wanatakiwa kuhakikisha watoto wanalelewa katika malezi bora ili kuendana na tafakari ya Yesu iliyosema yametia wakati anakata roho baada ya kutimiza wajibu wake,” alisema.

Katika Kanisa la Kiinjili la Kiletheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Azania Front, Mchungaji wa kanisa hilo, Charles Mzinga, aliwataka Wakristo kumtegemea Mungu katika kila jambo wanalopitia na kulifanya kwa kuwa ndio nguzo muhimu katika maisha ya binadamu.

Alisema ibada hiyo inawakumbusha mateso na kifo cha Yesu hivyo kila mmoja anapaswa kumpokea na kumtegea katika maisha yake.

Magufuli aombewa

Katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kipawa Kigango cha Stakishari, Mlezi na Mhadhiri wa Seminari Kuu ya Mtakatifu Karoli Lwanga, Segerea, Padre Peter Msafiri, aliwataka Wakristo kuombea Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli.

Aliwataka pia kuwaombea mawaziri, makatibu wakuu na wakuu wote wa vitengo serikalini, ili Mungu awaongeze kwenye utendaji kazi wao.

Wakati katika Kigango cha Stakishari wakifanya sala maalumu ya kumuombea Rais Magufuli na Serikali yake, Rais Magufuli pamoja na mke wake, Janeth Magufuli, walishiriki ibada ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Dar es Salaam.

Katika ibada hiyo, mbali na Rais Magufuli na mke wake, viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na mke wa Waziri Mkuu, mawaziri na wabunge.

Mkoani Morogoro, Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Telesphor Mkude juzi katika ibada ya Alhamisi Kuu, aliwaasa waumini kuonesha dhamira ya kujishusha na kuhudumia wadogo.

Mkude alisema Yesu Kristu anataka unyenyekevu huo katika jumuiya, katika familia na jamii nzima kwa ujumla ambapo alisema kuwa wanapaswa kutoa sadaka ya kuhudumiana.

Uchaguzi Zanzibar

Nako huko Dodoma Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Dodoma, Mchungaji Samwel Mshana ameshauri vyama ambavyo havikushiriki uchaguzi wa Zanzibar kuingizwa katika serikali ya Umoja wa Kitaifa, kwani nao wana nafasi kubwa ya kujenga uchumi amani na ustawi wa Zanzibar.

Katika mahubiri yake pia aliwakumbusha waumini kuiona Pasaka hiyo kama sehemu ya kujihoji kwenye matendo wanayoyafanya kama kuna mahusiano yoyote na Mungu badala ya kuichukulia kuwa ni sikukuu kama zingine.

Naye Askofu mstaafu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tabora, Francis Ntiruka alishauri serikali ya Unguja kuachana na siasa na badala yake iwatumikie wananchi. Askofu huyo aidha amemtaka Rais wa Zanzibar kujali na kuwatimizia mahitaji wananchi wote kama alivyoahidi bila kujali kama kuna vyama ambavyo vilisusia uchaguzi huo.

Aidha amewataka Wakristo kuhakikisha wanaitumia Pasaka kwa kutenda mema na kuonesha upendo kwa vitendo huku wakijiepusha matendo yasiyofaa kama vile ulevi uasherati wizi ikiwemo na matumizi ya madawa ya kulevya.

Imeandikwa na Ikunda Erick, Regina Kumba, Theopista Nsanzugwanko na Katuma Masamba Dar, Agnes Haule, Morogoro na Sifa Lubasi, Dodoma.
Share:

Magazeti Ya Leo Jumamosi ya March 26,2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

























Share:

Friday 25 March 2016

download Jose Chameleone Ft. Bob Junior - BAKI NAE | Download

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

DOWNLOAD via HULKSHARE
http://old.hulkshare.com/dl/6yy4h4yd4bk0/Jose_Chameleone_Ft._Bob_Junior_-_BAKI_NAE.mp3?d=1
Share:

Harry Redknapp aiongoza Jordan kushinda goli 8 – 0, Australia nayo yapiga 7 – 0

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Kocha wa zamani wa Tottenham, Harry Redknapp ameiongoza timu ya taifa ya Jordan ambayo ndiyo anayoifundisha kwa sasa, kupata ushindi wa goli 8 – 0 dhidi ya timu ya taifa ya Bangladesh.

Katika mchezo huo wa kutafuta nafasi ya kufuzu kombe la Dunia 2018 Urusi, magoli ya Jordan yalifungwa na Hamza Aldaradreh aliyefunga magoli matatu dk. 23, 29 na 40, Abdallah Deeb dk. 29, Yusef Al Rawashdeh dk. 32, Baha Faisal dk. 62, Atiqur Rahman Meshu dk. 71, Yousef Al Naber dk. 81, Karim Rezaul dk. 83 na Ahmed Samir dk. 90.

Mchezo mwingine ulikuwa kati ya Australia na Tajikistan ambapo Australia imeibuka na ushindi wa goli saba kwa bila.

Baada ya matokeo hayo, Australia inaongoza kundi B ikiwa na alama 18 huku nafasi ya pili ikishikwa na Jordan iliyo na alama 16 na nafasi ya mwisho ikikamatiliwa na Bangladesh iliyo na alama moja. 
Share:

Watumishi hewa 169 wagundulika Kigoma.....Mkuu wa Mkoa awataka wakurugenzi kubainisha kiasi walicholipwa mwaka mzima.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali Emanuel Maganga amewataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wote waliopo katika halmashauri zote kutaja kiasi cha fedha kilichotumika kuwalipa mishahara watumishi hewa 169 kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Akiongea na waandishi wa habari, Brigedia Jenerali Emanuel Maganga alisema kuwa agizo hilo ni kufuatia agizo la Mheshimwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli la kufanya uhakiki wa watumishi katika halmashauri zote ili kuwabaini watumishi hewa wanaolipwa mishahara kinyume na utaratibu za utumishi.

Alisema katika hao watumishi hewa 169 waliowabainika wapo ambao walishafukuzwa kazi, wapo ambao wameshafariki na wengine hawana sifa za kuwa watumishi wa umma.

Mhe. Maganga alisema kuwa suala la kuwa na wafanyakazi hewa ni wizi ambao hauwezi kuvumilika na wizi wa kuibia wanyonge hauwezi kuvumilika.

"Hakuna anayeweza kuvumilia wizi wa waziwazi kiasi hiki unaofanywa na baadhi ya watumishi wasiowaaminifu, wale wote watakaobainika wajiandae kwani hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao"Alisema Maganga.

Alisema kuwa fedha walizokuwa wakilipwa watumishi hao hewa kwaajili ya mishahara zinatakiwa kurudi zote, pia wakurugenzi wawafute watumishi hao hewa kwenye orodha ya malipo.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa sasa hivi katika serekali hii ya awamu ya tano hakuna kufanya kazi kwa mazoea.

Alizitaja halmashauri zenye watumishi hewa kuwa ni halmashauri ya kasulu watumishi 78,halmashauri ya Kigoma 23,Manispaa ya Kigoma Ujiji 29,halmashauri ya Buhigwe 11,Uvinza 19,kibondo 5,ofisi ya Mkuu wa Mkoa 4 na halmashauri ya Kakonko hakuna mtumishi hewa.
Share:

Marekani, Ulaya Wasusia Kuapishwa Dk. Shein

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.
Mabalozi kutoka Marekani na Nchi za Umoja wa Ulaya, wameendelea kuonyesha msimamo wao wa kutoridhishwa na uchaguzi wa marudio Zanzibar baada ya jana kususia mwaliko wa kushiriki sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein.
 
Wanadiplomaasia hao walipewa mwaliko rasmi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), lakini waliiambia kuwa hawatashiriki sherehe hizo.
 
Mkurugenzi wa Mambo ya Nje Zanzibar, Silima Kombo Haji, aliliambia Nipashe kuwa serikali ilitoa mwaliko rasmi kwa Mabalozi wote wa nchi za Afrika na Ulaya kuhudhuria sherehe hizo, lakini Mabalozi wa Umoja wa Ulaya na Marekani walijibu kuwa hawatahudhuria bila kutoa sababu zozote.
 
“Tumewaalika na mialiko imewafikia na kutujibu kuwa hawatahudhuria. Hatukuwa na sababu ya kuwang’ang’ania," alisema Haji.
 
Hata hivyo, alisema licha ya Mabalozi wa Marekani na Umoja wa Ulaya kutohudhuria sherehe hizo, Mabalozi wa nchi nyingine walioalikwa walihudhuria sherehe hizo na wengine kutuma wawakilishi wao.
 
Aliwataja Mabalozi wa nchi waliohudhuria sherehe hizo ambao wengi ni kutoka nchi za Afrika kuwa ni Balozi wa Cuba, Zimbabwe, DRC, Indonesia, Iran, Kenya, Kuwait, Malawi, Msumbiji na Oman.
 
Wengine ni Palestina, Ruwanda, Algeria, Angola, Burundi, China, Japan, Libia, Pakistan, Umoja wa Nchi za Kiarabu, India, Uganda, Uturuki, Urusi na Mratibu Mkaazi wa UN.
 
Nipashe lilipomuuliza Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Roeland van de Geer, endapo walipata mwaliko huo na sababu za kutohudhuria sherehe hizo, alisema ushirika wao usingeakisi dhamira ya tamko lililotolewa na Balozi mbalimbali nchini  Machi 21, mwaka huu.
 
Tamko hilo lilitolewa na Mabalozi na Wawakilishi wa nchi za Ubelgiji, Canada, Denmark, Umoja wa Ulaya, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Hispania, Sweden, Switzerland,  Uingereza na Marekani.
 
“Tumesikitishwa na uamuzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) wa kuendesha marudio ya uchaguzi uliofanyika 25 Oktoba 2015, bila kuwapo makubaliano ya pamoja baina ya pande kinzani na ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa visiwani humo uliotokana na majadilino baina ya pande husika. 
 
“Ili uwe wa kuaminika na kukubalika ni lazima mchakato wa uchaguzi uwe jumuishi na unaowakilisha kwa dhati matakwa ya watu,” lilisema tamko lao la awali na kuongeza:
 
“Tunarejea wito wetu kwa Serikali ya Tanzania kuonyesha na kuchukua uongozi katika suala la Zanzibar na kujielekeza katika kupatikana kwa ufumbuzi wa mgogoro huu kwa kupitia mazungumzo baina ya pande husika kwa lengo la kudumisha amani na umoja."
 
Mabalozi wamekuwa na msuguano na Serikali ya Zanzibar kwa kupinga kitendo cha Tume ya Uchaguzi Zanzibar (Zec) kufuta uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana kwa kile wanachodai kuwa haukuwa na kasoro yoyote na kwamba ulikuwa huru na haki.
 
Mwenyekiti wa Zec, Jecha Salim Jecha, Oktoba 28, mwaka jana, alifuta uchaguzi mkuu kwa madai kuwa haukuwa huru na haki, lakini waangalizi wa kimataifa wakisema kuwa ulikuwa huru na haki.
 
Wanadiplomasia hao hawakufurahishwa na kitendo cha Mwenyekiti huyo wa Zec kufuta uchaguzi, hivyo kutounga mkono uamuzi wa Zec kurudia uchaguzi ambao ulifanyika Machi 20, mwaka huu na Dk. Shein kushinda kwa kura 299,982 sawa na asilimia 91.4.
Share:

Leo ni Ijumaa Kuu… Wakristo Duniani kote wanaadhimisha mateso na kifo cha Yesu Kristo

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

ljumaa Kuu ni siku ya mwaka ambayo wafuasi wengi wa Yesu Kristo wanaadhimisha kifo chake msalabani ambacho kilitokea nje ya kuta za mji wa Yerusalemu siku ya Ijumaa.

Kadiri ya Mtume Yohane kesho yake ilikuwa Sabato na pia Pasaka, jambo lisilotokea kwa kawaida. Kwa sababu hiyo wataalamu mbalimbali wanakadiria ilikuwa tarehe 7 Aprili 30.

Ijumaa kuu ni sehemu ya Juma Kuu linaloanza kwa adhimisho la Yesu kuingia mji huo akishangiliwa kama mfalme wa Wayahudi (yaaniMasiya au Kristo). Adhimisho hilo linafanyika mwanzoni mwa wiki, yaani Jumapili ya matawi.

Ijumaa kuu ni pia sehemu ya siku tatu kuu za Pasaka zinazoadhimisha mateso na kifo chake, kulala kaburini, na hatimaye kufufuka kwa utukufu

Siku tatu kuu za Pasaka ndizo kiini cha mwaka wa Kanisa.

Zinamuadhimisha Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka, yaani siku ya kwanza (Alhamisi kuu jioni hadi Ijumaa kuu jioni) inaadhimisha mateso yake kuanzia karamu ya mwisho hadi kifo cha msalaba; siku ya pili (Ijumaa kuu jioni hadi Jumamosi kuu jioni) inaadhimisha maiti yake kubaki kaburini na roho yake kushukia kuzimu; siku ya tatu (kuanzia Jumamosi kuu jioni hadi Jumapili ya Pasaka jioni) inaadhimisha ufufuko wake mtukufu.

Siku hizo tatu ni kama bawaba kati ya Kwaresima na kipindi cha Pasaka
Share:

Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 25,2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
















Share:

Thursday 24 March 2016

New Music Video: Vanessa Mdee – Niroge.

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
vanessa 1
Baada ya Never Ever ambayo ilifanya vizuri katika soka la muziki ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee ameachia nyimbo mpya ambayo ina jina la ‘Niroge’.
 
Share:

Scholarship Opportunity for a PhD Programme under the Project in the Field of Hydrology and Water Resources Engineering

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

 

Scholarship Opportunity for a PhD Programme under the Project in the Field of Hydrology and Water Resources Engineering

Please click ><HERE>> for more information
Share:

Google Is Working On YouTube Connect, Aiming To Beat Periscope At Its Own Game

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


VentureBeat is claiming to have wind of a new app by YouTube, named 'Connect.' The app will reportedly be used for live-streaming, in much the same way as Periscope and Facebook. According to VentureBeat's sources, Connect has many of the same features as those two apps, including a 'news feed' to see which of your subscriptions are streaming or have shared video, and chat among users.

This marks the fourth YouTube spin-off app, following Gaming, Music, and Kids. It's interesting to note that Connect will introduce a social element to the internet's go-to video service. While YouTube does have a subscription feed updated with videos from creators you subscribe to, it's a poor rendition of a true news feed à la Facebook. You, of course, log into the app with your Google account and can then immediately begin streaming your life in all its glory. Simples.

Videos will be watchable in-app, and VentureBeat says that these videos will also be 'storable,' meaning others can watch them later. Currently, Periscope only offers the ability to watch replays 24 hours after the broadcast; after that they disappear. Facebook Live replays will stay on Facebook until the uploader chooses to delete them. However, Connect does not have the ability to share to social networks other than YouTube yet; VentureBeat does not say if this feature will be added when the app launches.

The publication closes the rumor by saying that a release before or at I/O seems likely, which is probably a reasonable assumption.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger