Wednesday 18 November 2015
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO AWAMU YA NNE 2015/2016-BATCH 4
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita, Bodi ilitoa orodha ya Awamu ya Tatu iliyokuwa na waombaji 6,915 waliopangiwa mikopo. Kati ya waombaji hao waliopangiwa mikopo, waombaji 4,642 ni walikua ni wale wanaojiunga na shahada ya kwanza katika vyuo mbalimbali nchini na waombaji 2,273 ni wanafunzi wanaojiunga na Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Kwa msingi huo, Bodi inapenda kuufahamisha umma kuwa hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 48,469 wa mwaka wa kwanza. Katika awamu ya kwanza, Bodi ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282; Awamu ya Pili wanafunzi 28,554; Awamu ya Tatu wanafunzi 6,915 na Awamu hii ya Nne wanafunzi 718 wamepangiwa mikopo.
Majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo kutoka katika awamu zote tatu yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb.go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili.
Mwisho.
AWAMU YA NNE YA WANAFUNZI WALIOPANGIWA MIKOPO
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuwafahamisha waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 kuwa imetoa orodha ya AWAMU YA NNE yenye jumla ya waombaji wa mwaka wa kwanza 718 waliopangiwa mikopo.Itakumbukwa kuwa wiki iliyopita, Bodi ilitoa orodha ya Awamu ya Tatu iliyokuwa na waombaji 6,915 waliopangiwa mikopo. Kati ya waombaji hao waliopangiwa mikopo, waombaji 4,642 ni walikua ni wale wanaojiunga na shahada ya kwanza katika vyuo mbalimbali nchini na waombaji 2,273 ni wanafunzi wanaojiunga na Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Kwa msingi huo, Bodi inapenda kuufahamisha umma kuwa hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 48,469 wa mwaka wa kwanza. Katika awamu ya kwanza, Bodi ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282; Awamu ya Pili wanafunzi 28,554; Awamu ya Tatu wanafunzi 6,915 na Awamu hii ya Nne wanafunzi 718 wamepangiwa mikopo.
Majina yote ya waombaji waliofanikiwa kupangiwa mikopo kutoka katika awamu zote tatu yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb.go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). Aidha, orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili.
Mwisho.
Tuesday 17 November 2015
NDUGAI ASHINDA USPIKA KWA KURA 264 SAWA NA 70% YA KURA ZOTE
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mbunge
wa Kongwa (CCM) Job Ndugai ashinda kiti vcha Uspika kwa kura 264 sawa
na kura asilimia 70 huku mpinzani wake kupitia Chadema Goodluck Ole
Medeye akipata kura 109 huku wagombea wengine wakipata kura 0.
NDUGAI anakuwa Spika wa Bunge la 11 la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Monday 16 November 2015
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwataarifu wote waliochaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) baada ya Mfumo wa CAS kuonyesha kuwa umechaguliwa kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma, utaratibu ni kusubiri UDOM na vyombo vyake vya ndani kuthibitisha majina hayo. Waliodahiliwa wanatakiwa kwenda chuoni baada ya kupata joining instructions na wito kutoka Chuo husika.
TAARIFA KWA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAHADA ZA UALIMU ELIMUMSINGI NA ELIMU YA SEKONDARI KUPITIA MFUMO WA UDAHILI WA PAMOJA (CAS) KATIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA (UDOM)
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwataarifu wote waliochaguliwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) baada ya Mfumo wa CAS kuonyesha kuwa umechaguliwa kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma, utaratibu ni kusubiri UDOM na vyombo vyake vya ndani kuthibitisha majina hayo. Waliodahiliwa wanatakiwa kwenda chuoni baada ya kupata joining instructions na wito kutoka Chuo husika.
Kumekuwapo na wanafunzi waliosafiri kwenda kuripoti chuoni kabla ya
taratibu hizi kukamilika na hivyo kusababisha usumbufu kwao wenyewe na
kwa taasisi za NACTE na UDOM. Majina ya wanaotakiwa kwenda kuripoti na
tarehe za kuripoti mara zote hutolewa na chuo husika. Kwa kuwa majina
yamekwenda vyuoni kwa makundi (batches) sio makundi yote yamepitishwa na
katika mchakato wa ndani ya vyuo.
Baraza (NACTE) hutoa uchaguzi wake ili kuondoa usumbufu kwa wanafunzi kuangalia tovuti za vyuo mbalimbali kusaka majina yao. Iwapo kwa sababu zozote UDOM itashindwa kuwapokea baadhi ya waliochaguliwa, Baraza litawapa nafasi katika vyuo vingine. Ikumbukwe kuwa kuna vyuo vingi ambavyo havijapata wanafunzi wa kutosha.
Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
15 Novemba 2015
Baraza (NACTE) hutoa uchaguzi wake ili kuondoa usumbufu kwa wanafunzi kuangalia tovuti za vyuo mbalimbali kusaka majina yao. Iwapo kwa sababu zozote UDOM itashindwa kuwapokea baadhi ya waliochaguliwa, Baraza litawapa nafasi katika vyuo vingine. Ikumbukwe kuwa kuna vyuo vingi ambavyo havijapata wanafunzi wa kutosha.
Imetolewa na:
Katibu Mtendaji
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)
15 Novemba 2015
Students Fear Impending Dropout Due to Lack of Loans
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Scores
of university students will be forced to drop out because of
prolonged delay of loans to cover tuition and other expenses.
The development comes in the wake of last week’s announcement by
the High Education Students’ Loan Board (HESLB) that it issued loans to
over 40,000 students out of 50,830 applications received in 2015/16
academic year.
However, the payment only covered new students but skipped all together the majority of continuing students.
In separate interviews, a cross-section of students from different
universities blamed the loans facility of being “too selective” and
giving little consideration to continuing students.
Charles Alphonce, a second year student at Mzumbe University, told
The Guardian that he had all the required qualifications to secure a
loan yet he had being left out.
“This is the third time I am applying for a loan and I have never got any luck,” he lamented.
“I can’t understand what’s wrong with my applications,” he said
with the sad acknowledgment that, “...should I fail to get the loan this
time around I will have to postpone my classes.”
Alphonce who comes from a poor family background said he has been
struggling to raise funds for his studies but due to increasing costs he
may be forced to drop out.
Another student from the University of Science and Technology
(MUST) Mbeya Campus, Samuel Hosea shared a similar experience and
appealed to the board to treat all eligible loan applicants fairly
without bias.
Hosea also called upon the board to give special consideration to
students from outside the campus regions who have to go out of pocket to
survive while waiting for the loans that may not come at all.
Chairman of the Ministers of Loans in High Education in Tanzania,
Shitindi Venance, said the gravity of the problem is such that only 400
students of 6,000 eligible students at the University of Dar es Salaam
received their loans in their first year.
Expressing profound dismay over the exclusion of continuing
students, Venance said numerous continuing students have not being
considered for the loan and remain in dilemma.
“The government should be transparent in issuing of loans because
the money is not given to the students as an offer but as a loan which
will later be repaid,” he said.
He challenged the 30, 000/- fees charged for every application made
by students and asked the loan facility to reconsider the amount to
accommodate more applications.
HESLB Assistant Director of Communication, Education and
Information, Cosmas Mwaisoba said the continuing students who applied
for loans for the first time will be treated as are the first year
applicants.
Students who have received loans so far are 40,836 students and the loan amount is pegged at 155.2bn/-.
Opposition says no to working with new govt
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Former Chadema presidential candidate Edward Lowassa speaks to journalists in Dar es Salaam yesterday. (Photo: Mpoki Bukuku)
The Coalition of People’s Constitution (Ukawa) said
yesterday said it will not co-operate with the fifth-phase government
under President John Magufuli, citing “electoral fraud”.
The decision by Ukawa comes ten days after Magufuli was sworn-in
the United Republic of Tanzania President following a 58.45 per cent
victory against Chadema’s Edward Lowassa who garnered 39.97 per cent.
Addressing a press conference in Dar es Salaam yesterday Lowassa
explained the coalition had sufficient evidence to prove how last
month’s General Election was marred by vote rigging.
Lowassa who was supported by parties forming the Coalition of
People’s Constitution (Ukawa) objected the presidential results which
were announced by National Electoral Commission, Chairman Justice (rtd)
Damian Lubuva.
The former prime minister, vowed to unmask what transpired during
the tallying process anytime from now after getting enough evidence.
His statement follows a secret meeting held last Saturday in Dar es
Salaam between Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD national leaders and the
Zanzibar presidential candidate on CUF ticket Seif Sharif Hamad.
Lowassa maintained to keep a low-profile on the revelations about the ruling party’s presidential candidate victory.
He further explained the coalition was simply buying time to reveal
what happened at the “backstage” of the presidential polls tallying
exercise.
“We cannot at the moment reveal what had transpired,” and the coalition will not cooperate with the fifth phase government.
Lowassa was saddened by the country’s Constitution which bars
individuals or institution to challenge the presidential elections
results before the courts of law.
“We are asking Tanzanian to keep on protesting the General Election
results because there were rigged. No one should demonstrate as leaders
were looking for other appropriate actions,” he said.
Referring to the Zanzibar general elections, Ukawa demanded the
Zanzibar Electoral Commission (ZEC) to declare Civic United Front (CUF)
presidential candidate, Maalim Seif Sharif Hamad the winner of the
elections.
He said: “How is it possible for one pot to cook legal and illegal
things at the same time? If ZEC claims the election results were illegal
then the Union results were also not legal because they all came from
the same pot.”
Ukawa despite protesting the presidential results said that they
would still take part during the National Assembly proceedings scheduled
for tomorrow.
However Lowassa also called for a new constitution that would ensure free and fair elections in the country.
“The new constitution will ensure the country has independent
election commission which is responsible to the public, without new
constitution the country will continue be under the ruling Chama cha
Mapinduzi dictatorship.”
Meanwhile Ukawa has called on the government to take immediate
action over the mysterious death of former Chadema candidate for Busanda
constituency in Geita Region in the recent parliamentary elections,
Alfonce Mawazo.
NCCR-Mageuzi National chairman, James Mbatia strongly condemned the
killing, calling the authority to identify culprits behind the death of
Chadema’s Geita regional chairman.
Lowassa Ataja Sababu 4 Kumpinga Magufuli.....Zifahamu Hapa
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa, ameeleza sababu za kutokubaliana na
ushindi uliomuweka madarakani mpinzani wake kupitia CCM, Dk. John
Magufuli katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Aliyekuwa mgombea urais wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) chini ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),
Edward Lowassa (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana juu ya hali ya kisiasa nchini. Wengine ni
Kaimu Mwenyekiti wa Cuf, Twaha Taslima (wa kwanza kushoto), Makamu
Mwenyekiti wa Chadema, Prof. Abdallah Safari (wa pili kushoto) na
Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia (wa kwanza kulia). PICHA: MPOKI
BUKUKU
Aidha, amewataka Watanzania kutoyakubali matokeo hayo na kuyapinga
kwa nguvu zao zote bila ya kuandamana na kufanya fujo na kwamba umoja
huo hautashirikiana na serikali ya Dk. Magufuli kwa madai haikuingia
madarakani kihalali.
Lowassa alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa jijini
Dar es Salaam jana juu ya hali ya kisiasa nchini na mustakabali wa
Zanzibar baada ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa visiwa hivyo.
ATAJA SABABU ZA KUPINGA
Lowassa alisema yeye na wenzake ndani ya Ukawa hawaukubali na
ushindi alioupata Dk. Magufuli kwani wana ushahidi wa kutosha juu ya
namna Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kilivyopora ushindi
wake (Lowassa) kwa kuyakachakua matokeo.
Hata hivyo, Lowassa hakuwa tayari kuuweka wazi ushahidi, akisema atafanya hivyo wakati muafaka ukifikaa ambao pia hakuutaja.
Alitaja sababu nyingine za kutokukubali na ushindi wa Dk. Magufuli
kuwa ni, matumizi makubwa ya vyombo vya dola wakati wa uchaguzi.
Alisema wakati wa uchaguzi huo serikali ilitumia nguvu kubwa na
vitisho vya askari wenye silaha za kivita ikiwamo kutumia magari yenye
maji ya kuwasha yaliyonunuliwa kwa mabilioni ya fedha, ambayo yalikuwa
yanarandaranda mitaani, ili matokeo aliyodai ya wizi huo wa kura
yakubalike.
Sababu nyingine aliyoitoa Lowassa ni hatua ya serikali kupinga
maandamano ya Ukawa na kuvitisha vyombo vya habari kufanya kazi zake kwa
uhuru.
Nyingine alisema ni hatua ya serikali kupiga marufuku mikutano ya
kisiasa iliyopangwa kufanywa na viongozi wa Ukawa na kuwanyima viongozi
hao fursa ya kuwashukuru wananchi kwa kuwapigia kura baada ya uchaguzi.
“Wanatumia gharama zote hizo huku bei ya vitu mbalimbali hasa
vyakula inapanda kwa kasi kubwa, kama CCM inadai imeshinda kwa nini wana
hofu kubwa mpaka kuhujumu uhuru wa vyombo vya habari, kupiga marufuku
mikutano ya kisiasa na kunyima viongozi wa Ukawa hata fursa ya
kuwashukuru wananchi kwa kutuunga mkono katika safari yetu ya kuleta
mabadiliko, hii ni aibu kwa taifa letu,” alisema Lowassa na kuongeza:
“Tuna ushahidi wa kutosha jinsi matokeo ya uchaguzi wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano yalivyochakachuliwa na kiasi cha kura zilizoibwa,
wakati muafaka tutaweka bayana ushahidi huo ili Watanzania wajue kwa
nini Ukawa inasema kwa dhati kwamba haitambui matokeo yaliyotangazwa na
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) na kwa nini haitashirikiana na serikali
ya sasa ambayo ni batili kisheria.”
Lowassa alisema endapo Katiba ingekuwa inaruhusu matokeo ya urais
kupingwa mahakamani wangefanya hivyo, lakini kwa kuwa hairuhusu
wataendelea kutoitambua serikali hiyo, huku akiwataka wananchi kukataa
matokeo hayo katika hali ya utulivu wakati Ukawa ikiendelea na harakati
nyingine za kisiasa katika nyanja mbalimbali ili kutekeleza azma yao ya
kuleta mabadiliko ya kweli nchini.
ZANZIBAR
Aidha, Lowassa alisema Ukawa unamuunga mkono mgombea urais wa
Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi(Cuf), Maalim Self Sharif Hamad, kama
mshindi wa uchaguzi mkuu visiwani humo na kuitaka Tume ya Uchaguzi
Zanzibar (Zec) imtangaze mara moja.
Alisema kinyume na Tanzania Bara ambako uchaguzi uligubikwa na
mizengwe, uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa wazi na wa amani, huku vyama
vyote vya siasa na hata waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa walisema
uchaguzi huo ulifanyika kwa amani, lakini wanashangaa Zec kufuta
uchaguzi huo.
Alisema uamuzi huo wa Zec unalaaniwa vikali na Ukawa na kwamba
uamuzi wa kutaka uchaguzi huo urudiwe hawakubaliani nao kwa kile
alichosema hizo ni mbinu mpya ambazo zimepangwa kuhujumu uchaguzi huo
na una lengo la kuhatarisha amani na utulivu visiwani humo.
“Wakuu wa Ukawa walikataa dhana kuwa uchaguzi uleule unaodaiwa
kufutwa kwa kuwa ulikuwa na mizengwe, ulizaa matokeo halali ya wabunge
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ya urais wa Jamhuri,
lakini ni batili kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Rais wa
Zanzibar, dhana hii haina mantiki yeyote bali ni ubabe wa kisiasa,”
alisema Lowassa na kuongeza:
“Haiwezekani chungu kimoja kikapika halali na haramu kwa pamoja.
Kigezo cha Zec kuwa uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa batili, basi matokeo
yake yote ikiwa ni pamoja na yale ya urais wa Jamhuri pia ni batili. Hii
ina maana kuwa hata ushindi unaodaiwa wa Dk. Magufuli, mbali ya kuwa ni
matokeo haramu ya wizi kwa kura za Tanzania Bara, pia ni batili
kisheria kwani hana ridhaa ya watu wa pande zote mbili za Muungano.”
KATIBA MPYA
Lowassa alisema bado wataendelea kupigania kuandikwa kwa Katiba
mpya ambayo watahakikisha inazingatia maoni na matakwa ya Watanzania.
Alisema pasipo Katiba hiyo, matatizo mengi yanayojitokeza hivi sasa
hayatapatiwa ufumbuzi ikiwamo kuwa na tume huru ya uchaguzi na
serikali inayowajibika, huku akisisitiza kuwa katika mazingira ya sasa
na chini ya Katiba inayotumika sasa, Tanzania haitakuwa na demokrasia na
itaendelea kuwa nchi inayotawaliwa kwa mizengwe na udikiteta .
AELEZA HATMA YAKE
Lowassa alisema hatarudi nyuma wala kustaafu siasa, bali ataendelea
kuimarika katika nyanja hiyo kwa kuwa mstari wa mbele kupigania Ukawa
na mabadiliko.
MBATIA
Kwa upande wake, Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, James Mbatia, alisema
vurugu zinazoendelea hivi sasa na mauaji ya Watanzania katika matukio
tofauti na matumizi ya mabavu, itafika mahali Watanzania watakosa
uvumilifu na endapo machafuko yakitokea Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,
Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete pamoja na
Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva, wote watafikishwa katika mahakama
za kimataifa.
Mbatia alidai Kikwete atawajibika pamoja na mambo mengine kwa
kutumia nguvu kubwa kununua vifaa vya kivita vyenye thamani ya Sh.
bilioni 409 katika uchaguzi wa mwaka huu, huku akimtaja Jaji Lubuva
kwamba atawajibika kwa kukiuka sheria za uchaguzi kwa kuibeba CCM na
Mkapa atawajibika kwa kusababisha mauaji katika uchaguzi Mkuu 2001,
Zanzibar.
Akizungumzia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa
Geita, Alphonce Mawazo, aliyeuawa juzi kwa kukatwa mapanga na watu
wasiojulikana, Mbatia alihusisha kifo chake na mauaji mengine ambayo
yamekuwa yakihusishwa na chuki za kisiasa.
Lowassa aliungana na Mbatia kulaani mauaji hayo na kulitaka Jeshi
la Polisi kufanya uchunguzi wa haraka ili kubaini waliohusika na
kuwachukulia hatua.
MALALAMIKO VITI MAALUM
Akizungumzia malalamiko kutoka maeneo mbalimbali nchini kuhusu
mgawanyo wa viti maalum kwenye nafasi ya ubunge ndani ya Chadema, Makamu
Mwenyekiti wa chama hicho, Prof. Abdallah Safari, alisema Chadema
imepokea malalamiko mengi kuhusiana na mgawanyo wa wabunge wa vitihivyo
na kwamba kinayafanyia kazi na yale ya msingi yatafanyiwa uamuzi na
yasiyo ya msingi yataachwa.
Naye Kaimu Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (Cuf), Twaha Taslima,
alisema masuala ya wabunge wa viti maalum yanazungumzwa ndani ya chama
na si katika vyombo vya habari.
Katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu, Nec ilimtangaza Dk. Magufuli wa CCM
kuwa mshindi wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano kwa kupata
asilimia 58.46 ya kura halali zilizopigwa, huku Lowassa akipata
asilimia 39.97.
CHANZO:
NIPASHE
CHADEMA Watangaza hali hatari,Ni mauaji ya MAWAZO sasa vijana wote waagizwa kuelekea mwanza
INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Na Exaud Msaka Habari
Baraza la vijana la chama
cha Demkocrasia na maendeleo chadema
BAVICHA wametoa siku tatu kwa jeshi la polisi nchini kumwachia Mwenyekiti wa
baraza hilo PATROBAS KATAMBI aliyekamatwa jana mkaoni mwanza pamoja na
kuwakamata wahusika wote waliohusika na kifo cha Mwenyekiti cha CHADEMA mkoani
GEITA Bwana ALPHONCE MAWAZO huku wakisema kuwa kama hayo hayatafanyika
watalazimika kulipa kisasi.
Akizungumjza na
wanahabari mchana wa leo jijini Dar es salaam katibu wa uenezi wa baraza hilo
Taifa Bwana EDWARD SIMBEYE amesema kuwa kwa sasa vijana na wanachama wa chadema
wamechoka na mauaji ya viongozi wa chama
hicho huku kukiwa hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wahusika hivyo sasa wameamua
kuhakikisha kuwa wanajilinda wenyewe ikiwa ni pamoja na kuwatafuta wahusika wa
tukio la Geita na kuwakamata kama polisi watakuwa wameshindwa kufanya hivyo kwa
muda muafaka..
Akizungumzia tukio la
jana mkoani mwanza amesema kuwa wakati jana mwili wa marehemu MAWAZO ukiwasili
katika hospitali ya BUGANDO kwa ajili ya kuhifadhiwa na kufanyiwa uchunguzi
zaidi Polisi walipanga njama za kuutorosha mwili wa marehemu kwa ajili ya
kwenda kuuzika kimya kimya jambo ambalo amesema wanachama na viongozi wa
CHADEMA walishtuka na kuamua kulinda mwili huo na ndipo ilipotokea vurugu
iliyopelekea kiongozi wa vijana taifa kukamatwa na polisi bila sababu yoyote ya
msingi.
Amesema kuwa
inashangaza kuona jeshi la polisi likiwa
katika mstari wambele kuhangaika juu ya mwili wa Marehemu ALPHONCE MAWAZO
wakati iko wazi kuwa wakati anauawa na wananchi polisi walikuwepo eneo la tukio
na kushindwa kutoa hata msaada wa gari kwa ajili ya kumpeleka hospitalini
lakini jana polisi walipata gari la kuja kumtorosha katika hospitali hiyo jambo
ambalo amesema limekuwa likifanywa na polisi kila mara yanapotokea matukio ya
mauaji kana haya.
Kiongozi huyo amesema
ni lazima jeshi la polisi sasa waeleze ukweli kama sio wao na serikali ya CCM
wanaohusika na mauaji ya viongozi wa chadema Basi waweke wazi ni nani hasa
anayefanya unyama huo juu ya Democrasia ya Tanzania.
Aidha katika hatua
nyingine vijana hao wametangaza rasmi kuwa baada ya siku tatu na polisi
kushindwa kuwaachia huru viongozi wao na kuwakamata wauaji wa MAWAZO
wamewaagiza vijana wote wa Tanzania kukusanyika kwa wingi mkaoni mwanza kwa
ajili ya kushinikiza kuwaachia viongozi wao pamoja na kulinda mwili wa marehemu
ALPHONCE MAWAZO ambao umelazwa katika hospitali ya Bugando mkoani mwanza.
Marehemu ALPHONCE
MAWAZO aliuawa na wananchi mkoani GEITA baada ya kushambuliwa na wananchi
waliokuwa na sialaha za jadi ambao hadi sasa hakuna taarifa rasmi inayoeleza
hali halisi ya mauaji hayo.