Sunday 8 November 2015

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBER 8 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Share:

Rais Magufuli: Manunuzi ya Serikali Kuondoka na Watu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY


RAIS John Magufuli, ametoa agizo mahususi katika usimamizi wa manunuzi ya Serikali, ambayo yamekuwa yakitumika vibaya kwa kugeuzwa mwanya wa kuiibia Serikali. 

Ametoa agizo hilo Ikulu jijini Dar es Salaam jana katika kikao chake cha kwanza na watendaji wakuu wa Serikali; wakiwemo makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade. 

Katika kikao hicho, Rais Magufuli ameagiza usimamizi katika suala la manunuzi ambalo limekuwa likitumika vibaya kwa watendaji wabadhirifu kununua vitu vya Serikali kwa bei ya juu kuliko bei halisi iliyopo sokoni. 

“Ikitokea suala hilo likagundulika kwa watu kuongeza bei ya vitu, watendaji watawajibishwa mara moja,” ameonya Rais Magufuli na kusisitiza kwamba kuwajibishwa huko kutahusu yeyote atakayeongeza bei, hata kama bei iliyoongezwa ni ya vitu vya bei ndogo kabisa katika jamii. 

*Mkakati wa Magufuli 

Kauli za Rais Magufuli katika kikao hicho cha jana na cha juzi alipofanya ziara ya kushtukiza ya Wizara ya Fedha, zimedhihirisha mkakati wake wa kuongeza mapato ya Serikali, kwa kuwa katika vikao vyote hivyo, amesisitiza umuhimu wa kukusanya kodi kwa kila mfanyabiashara mkubwa bila woga. 

Mbali na dhamira hiyo ya kuongeza zaidi mapato, agizo la kuchunga manunuzi ya umma, imeonesha dhamira nyingine aliyonayo katika kubana matumizi, kwa kuwa eneo la manunuzi ya umma, ndilo linalochukua asilimia 70 ya matumizi ya Serikali. 

Mbali na eneo hilo kuchukua sehemu hiyo kubwa ya mapato ya Serikali, lakini eneo hilo pia limekuwa likiathiriwa zaidi na vitendo vya rushwa hasa katika utoaji wa zabuni za Serikali. 

Mkakati huo wa Rais Magufuli, umezidi kudhihirisha dhamira yake aliyotangaza wakati wa kampeni, ya kwenda kuziba mianya ya rushwa na uvujaji wa mapato, ili fedha za Serikali zikatekeleze ahadi zake na kutatua kero za Watanzania wa kipato cha chini.
Share:

Saturday 7 November 2015

SERIKALI YA WANAFUNZI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (DARUSO) TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MIKOPO KWA WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Ndugu wanafunzi wa mwaka wa kwanza Chuo kikuu cha Dar es Salaam,wanafunzi wa vyuo vyote nchini na watanzania kwa ujumla, serikali ya wanafunzi chuo kikuu cha Dar es salaam inapenda kuwajulisha kuwa inayo taarifa juu ya sintofahamu nzito kuhusu suala la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu wa mwaka wa kwanza wa masomo 2015/2016 ambapo idadi kubwa ya wanafunzi waliodahiliwa na vyuo mbalimbali nchini wamekosa mkopo. Mfano katika chuo kikuu cha Dar es salaam ni wanafunzi 684 tu waliopata mkopo kati ya wanafunzi zaidi ya 6,000 waliodahiliwa na chuo mwaka wa masomo 2015/2016.

Kutokana na hali hiyo, serikali ya wanafunzi (DARUSO ) kwa umoja wetu kupitia wizara ya mikopo, tuliamua kuungana na kuchukua hatua za kukutana na mamlaka husika ili kuhoji na kushinikiza utolewaji wa haraka wa pesa za mikopo kwa kundi kubwa la wanafunzi wenye sifa waliokosa mkopo katika chuo kikuu cha Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla ambapo kwa mujibu wa bodi ya mikopo (HESLB) ilionesha kuwa waliomba mkopo walifikia idadi ya wanafunzi zaidi ya 70,000 na walioonekana kuwa na sifa za kupata mkopo walikuwa 58000. Lakini katika hali ya kushtua, kushangaza na kusikitisha ni wanafuzi 12,000 pekee ndio waliokuwa wamepatiwa mkopo nchi nzima. Hivyo hatua zifuatazo zilichukuliwa ili kukabiliana na changamoto hii.


Mnamo tarehe 04/11/2014 Serikali ya wanafunzi ikiwakilishwa na kamati maalumu ya viongozi tulifika katika makao makuu ya bodi ya mikopo HESLB na kuzungumza nao kinagaubaga kuhusu uhalisia wa jambo hili na wao wakatupa majibu kuwa walipeleka maombi ya wanafinzi 58000 waliokuwa na sifa za kupata mkopo kwenda wizara ya elimu lakini cha kusikitisha ni kuwa ni wanafunzi 12,000 pekee ndio waliweza kupewa mkopo nchi nzima hivyo kuwalazimu HESLB kutoa mkopo kwa wanafunzi wachache katika kila chuo. Kutokana na majibu haya tulilazimika kuonana na katibu mkuu wa wizara ya elimu ili kujua kulikoni hali hii ikatokea.
Mnamo tarehe 06/11/2015 serikali ya wanafunzi kupitia kamati maalum tumeweza kufika wizara ya elimu na kukutana na kaimu mkurugenzi wa masuala ya elimu ya juu Dr. Mbwambo na kuzungumzia suala hili naye akatupa majibu yaliyokuwa pacha na majibu yaliyotolewa na bodi ya mikopo kuwa kulikuwa na upungufu wa fedha zinazofikia kiasi cha billion 132 ili kuwezesha wanafunzi wote nchini wenye sifa za kupata mkopo waweze kunufaika na mkopo huo, hivyo kutokana na maelezo hayo tulilazimika kuonana na katibu mkuu wa wizara ya elimu ili kuweza kujua ni hatua zipi zimechukuliwa ili kuweza kupata kiasi hicho cha fedha kilichopungua. Lakini tunasikitika kuwa hatukuweza kukutana na katibu mkuu licha ya ukweli kwamba tuliweza kuacha ujumbe wetu kwa katibu wake binafsi. Baada ya hatua hii tuliona ipo sababu pia ya kujua ni nini kinachowakwamisha hazina kutoa pesa hizo.
Hivyo siku hiyo hiyo ya tarehe 06/11/2015 tulifika katika ofisi za hazina na kuzungumza na kamishina wa bajeti nae akatuomba tumpe mda wa kufanya kikao na watendaji wa wizara ya elimu pamoja na bodi ya mikopo na akaahidi kutupa majibu kwa njia ya simu siku hiyohiyo ya tarehe 06/11/2015 mara tuu baada ya kikao.


Hivyo, waziri wa mikopo chuo kikuu cha Dar es salaam MH SHITINDI VENANCE ameweza kupokea simu ya mkononi kutoka kamishina wa bajeti nchini tarehe 06/11/2015 muda wa saa 12:25 jioni na alimpa taarifa kuwa katika kikao cha kamishna na bodi ya mikopo pamoja na wizara ya elimu wameafikiana kutoa fedha ndani ya masaa 48 kwa wanafunzi wote nchini wenye sifa na vigezo vya kupata mkopo lakini majina yao hayakuwamo katika majina yaliyokuwa yametajwa hapo awali.
Hivyo wizara ya mikopo katika selikali ya wanafunzi chuo kikuu cha Dar es salaam(DARUSO) Inapenda kuwatangazia wanafunzi wote wa mwaka wa kwanza katika chuo kikuu cha Dar es salaam na Tanzania kwa ujumla kuwa tutaendelea kusimamia kila hatua mpaka hatua ya mwisho ya mchakato huu pale pesa zenu zitakapo patikana ili muweze kuipata elimu ya chuo kikuu pasi na kikwazo chochote.

IMETOLEWA NA SERIKALI YA WANAFUNZI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (DARUSO)
UNITY IS POWER.
Share:

Magazetini Leo Jumamosi 07/11/2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Share:

NEC Yatangaza Wabunge Viti Maalumu

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeteua wabunge wa Viti Maalumu na kuwasilisha orodha ya wateule hao katika vyama husika vya siasa. 

Vyama ambavyo vimepata nafasi ya kuwa na wabunge hao ni vitatu ambavyo vimekidhi vigezo vya kikatiba na kisheria vya kupata angalau asilimia 5 ya kura zote halali za wabunge. 

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Damian Lubuva, alisema vyama vilivyokidhi vigezo hivyo ni Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi (CUF). 

Hata hivyo Jaji Lubuva alisema, majina ya wabunge wa Viti Maalumu yatapatikana katika vyama husika kwa mujibu wa orodha iliyowasilishwa NEC na kila chama, ili Tume ifanye uteuzi. Alisema kulingana na vigezo vya kupata kura asilimia tano, CCM imepata wabunge 64, Chadema 36 na CUF wabunge 10. 

Kwa uteuzi huo, CCM iliyokuwa na wabunge wa majimbo 182, sasa inakuwa na jumla ya wabunge 246, huku Chadema yenye wabunge wa majimbo 35 ikiwa na jumla ya wabunge 71 na CUF yenye wabunge 39 wa majimbo, ikipata jumla ya wabunge 49. 

ACT na NCCR-Mageuzi wamebakia na mbunge mmoja kila chama. Kwa kufuata aina ya ushirikiano wa vyama vya upinzani chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kambi Rasmi ya Upinzani itakuwa na jumla ya wabunge 121 sawa na asilimia 46.8. 

Katika Bunge la 10, ambalo limemaliza muda wake, kulikuwa na wabunge wa majimbo 254, kati ya hao CCM ilikuwa na wabunge 186, CUF 23, Chadema 24, NCCRMageuzi wanne na UDP mmoja. 

“Kigezo cha kupatikana kwa wabunge wa viti maalumu ni kura zote halali walizopata wabunge wa vyama vyote katika majimbo yaliyofanyika uchaguzi,” alisema Jaji Lubuva. 

Alisema kwa mujibu wa Ibara ya 66(1)(b) na Ibara ya 78 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 vikisomwa pamoja na kifungu cha 86A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343, Tume imepewa mamlaka ya kutangaza viti maalumu vya wabunge wanawake visivyopungua asilimia 30 ya wabunge wote. 

Hata hivyo kwa mujibu wa uamuzi wa Serikali wa mwaka 2010 idadi ya wabunge wa viti maalumu iliongezwa na kufikia asilimia 40 na hivyo katika uchaguzi uliofanyika mwaka huu, idadi ya wabunge wa viti maalumu ni 113. 

“Kutokana na kuwepo majimbo nane ambayo hayakufanya uchaguzi mgawanyo wa viti maalumu kwa sasa ni 110. Viti vitatu vilivyobaki, vitagawanya baada ya uchaguzi kufanyika katika majimbo hayo,” alisema Jaji Lubuva. 

Jaji Lubuva alisema, pia kuna idadi ya wabunge watano ambao wanateuliwa na Baraza la Wawakilishi na hao watapatikana baada ya mchakato wa uchaguzi kukamilika. Alitaja kura halali na zilizopatikana na vyama vyao ni CCM kura 8,333,953, Chadema 4,627,923 na CUF 1, 257,051, ambazo zimetumika kupata wabunge hao wa viti maalumu.
Share:

Polisi Yawahoji Tena Watumishi 38 LHRC

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limekitaka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuwa watulivu na kusubiri jeshi hilo likamilishe upelelezi wake juu ya tuhuma za watumishi wake kukusanya na kusambaza taarifa zisizo sahihi wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni. 

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Kamishna wa Polisi wa Kanda Maalumu Suleiman Kova wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya jana kuwahoji kwa mara ya pili viongozi na wafanyakazi 38 wa kituo hicho wanaotuhumiwa kukusanya na kusambaza taarifa zisizo sahihi kinyume na sheria ya udhibiti wa makosa ya mtandao. 

“Lazima watulie na kuliachia jeshi kuendelea na upelelezi wake na ukikamilika upelelezi basi jalada litapelekwa kwa mwanasheria wa serikali na mpaka kufikia Jumatatu ijayo tutajua hatima ya watuhumiwa pamoja na vielelezo vyao,” alisema Kova. 

Aliongeza kuwa, katika mahojiano ya awali ilibainika kituo hicho kilichopo Mbezi Beach kilipewa kazi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwa waangalizi wa ndani wa uchaguzi na kupewa masharti ya namna ya kutekeleza kazi hiyo ikiwa ni pamoja na kutokutoa maoni na taarifa yoyote kwa vyombo vya habari au umma juu ya mchakato wa uchaguzi wakati wa upigaji kura ukiendelea.

“Kwa sababu hizo sasa tumeendelea kuwahoji ili watoe ufafanuzi kutokana na yale yaliyogundulika na jeshi letu kwamba ni kinyume cha sheria za mtandao pamoja na sheria ya uchaguzi kanuni na maelekezo ya NEC kwa waangalizi wa uchaguzi wa ndani na nje,” alisema Kova. 

Aidha, alisema jeshi hilo kupitia Kitengo cha Sayansi ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai kimegundua kuna makosa ya jinai yaliyotendeka kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii nchini sambamba na hilo pia zipo tuhuma kwamba kituo hicho kilikiuka sheria ya uchaguzi pamoja na maelekezo ya NEC ya mwaka 2015 kuhusu maelekezo na masharti waliyopewa waangalizi wa ndani na nje ambavyo vinazungumzia kuheshimu na kutii sheria za Tanzania. 

Hata hivyo, Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba amelitaka jeshi hilo kuharakisha upelelezi wake kwani vifaa vilivyochukuliwa vina kazi muhimu za taasisi yao na kwamba wanapaswa kutoa taarifa kwa yale waliyoyafanya katika kipindi chote cha uchaguzi.
Share:

HII NDIO LIST YA WABUNGE WA VITI MAAALUMU CCM, CDM, CUF,

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY






Share:

Serikali YASITISHA Matumizi ya Picha Rasmi ya Rais Magufuli

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Serikali inapenda kuzitaarifu ofisi za umma na wananchi kwa ujumla kwamba imesitisha matumizi ya picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Serikali ya Awamu ya Tano, Mhe.Dkt. John Pombe Joseph Magufuli mpaka hapo itakapotangazwa tena.

Awali majira ya saa 6: 00 mchana leo Novemba 6, mwaka huu Serikali ilitangaza kuhusu kuanza rasmi kwa matumizi ya picha ya Rais, ambayo ilikuwa ikiuzwa kwa gharama ya Shilingi Elfu Kumi na Tano tu (15,000/=).

Aidha, Serikali imesema kwamba itazitangazia ofisi hizo na umma wa Watanzania kuhusu kuanza tena kwa matumizi ya picha hiyo hapo baadae.

Imetolewa na
IDARA YA HABARI.
Novemba 6, mwaka 2015
Share:

Friday 6 November 2015

CONTINUE STUDENTS LOAN ALLOCATION SAUT MWANZA 2015-2016

Share:

HAYA HAPA MAJINA AWAMU YA NNE (4TH BATCH) YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA SUA 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Additional of Fourth batch selected students 2015-2016


The following is the additional list of the selected students to join undergraduate degree programmes for the 2015/2016 academic year which starts on the 2nd November, 2015
Share:

HAYA HAPA MAJINA AWAMU YA 5 WALIOCHAGULIWA ST.JOHN UNIVERSITY 2015/2016

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger