Friday 6 November 2015

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO SAUT 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
logo
Share:

TCU YATOA TANGAZO KWA WANAFUNZI WANAOTAKA KUHAMA VYUO VIKUU 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Tanzania Commission for Universities Form six students’ transfer procedures for 2015-2016 academic year 1. Introduction After the release of names of students selected for admission into various higher education institutions in the 2015/2016 academic year, TCU has been receiving enquiries from a large number of applicants seeking to transfer from one institution to another. For this reason, TCU hereby announces the transfer procedures for the academic year 2015/2016.


 2. Things to observe

 Students selected for this academic year and wishing to transfer from one institution to another should apply through the Central Admission System (CAS). These students should also observe that: (a) A non-refundable transfer fee of Tshs 30,000/- will be required, (b) Transfers will depend on the applicants’ possession of relevant admission qualifications and availability of admission slots in the programme that one wishes to transfer to, (c) Transfers will be on merit basis and those applying for transfer will compete for available slots in the programmes of their choice, and (d) The names of successfully transferred students will be posted on the TCU website and these students will be notified through their mobile numbers. 

3. How to pay transfer fee 

Transfer fee shall be paid through M-Pesa, Tigo-Pesa and Max-Malipo. Click here to view payment procedures... 4. How to transfer (a) Applicants should first login into Central Admission System. (b) Click on View Possible Transfer Programmes. Then a list of programmes with available slots will open. Please note that for each programme the following information will be displayed: - Programme name, - Institution, - Cut-off points for the respective programme, - Number of vacant slots, - “View Details” link, - “Check Eligibility” link. (c) If the applicant wishes to proceed with the transfer then one should pay a nonrefundable transfer fee of Tsh. 30,000/= through the prescribed payment method. (d) Having paid for the transfer, the applicant should click on “Apply for Transfer”, then a form will open where the payment identification or voucher number can be entered. (e) Having entered the payment identification number, the applicant should click the “Select Transfer Programme” link then choose a programme that one wishes to transfer to. 5. Deadline for transfers The deadline for transfers is 2nd December 2015. Transfers done after this date will not be processed by the system. 6. Other transfers Please note that those wishing to transfer from one programme to another in the same institutions should consult their respective institutions for procedures. Also note that students with diploma qualifications should consult NACTE for their transfer procedures. Issued by Executive Secretary, Tanzania Commission for Universities (TCU), 4 th November 2015.
Share:

Kikwete Aaga Kwa Kusamehe Wafungwa 4,160

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

RAIS mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 4,160 katika kuaga na kukabidhi madaraka ya Serikali kwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli.

Dk Magufuli aliapishwa jana kuwa Rais wa Tano wa Tanzania katika sherehe zilizofana kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam huku Kikwete akimaliza miaka yake 10 ya kuongoza nchi kama ilivyoelekezwa na Katiba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe kwa vyombo vya habari jana Dar es Salaam, kati ya wafungwa hao, wafungwa 867 wataachiwa huru na wafungwa 3,293 watapunguziwa vifungo vyao na kubaki gerezani wakitumikia sehemu ya vifungo vyao vilivyobaki.

“Ni mategemeo ya Serikali kwamba wafungwa watakaoachiwa huru watarejea katika jamii kushirikiana na wananchi wenzao katika ujenzi wa Taifa na watajiepusha na utendaji makosa ili wasirejee tena gerezani,” alisema Chikawe katika taarifa hiyo.

Chikawe aliwataja walionufaika na msamaha huo kuwa ni wafungwa wote wapunguziwe moja ya sita ya vifungo vyao zaidi ya punguzo la kawaida linalotolewa chini ya Kifungu cha 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58 isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika ibara ya 1 (i-xix).

Aliwataja wengine kuwa ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama Ukimwi, kifua kikuu, saratani ambao wako kwenye hatua ya mwisho ambao watathibitishwa na waganga chini ya Mganga mkuu wa mkoa au wilaya.

Pia wazee wenye umri zaidi ya miaka 70, wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani na walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya na walemavu wa mwili na akili na ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga.

Kwa mujibu wa Chikawe, msamaha hautawahusu wafungwa wenye adhabu za kunyongwa, waliohukumiwa kunyongwa na adhabu hiyo baadaye kubadilishwa kuwa kifungo cha maishaau kifungo gerezani.

Wengine ni wafungwa waliotumikia kifungo kwa makosa ya usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya, makosa yanayohusu uombaji, upokeaji na utoaji rushwa, unyang’anyi na kujaribu kutenda makosa hayo, kubaka, kulawiti au kujaribu kutenda makosa hayo.

Aidha, makosa mengine ambayo vifungo vyake haviko kwenye msamaha huo ni makosa ya kuwapa mimba wanafunzi, wizi wa magari, pikipiki au kujaribu kutenda makosa hayo, matumizi mabaya ya madaraka, waliowahi kupunguziwa vifungo na Rais.

“Wengine ni waliopatikana na hatia kwa kuwazuia watoto kupata masomo, utekaji watoto, usafirishaji binadamu, ukatili dhidi ya albino, usafirishaji nyara za Serikali na ujangili,”ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Mengine ni wanaotumikia vifungo kwa makosa ya wizi na ubadhirifu wa fedha za Serikali, kutoroka au kujaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi halali na wafungwa wanaotumikia vifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole Sheria Namba 25 ya Mwaka 1994 ya Sheria ya Huduma kwa Jamii Namba 6 ya Mwaka 2002
Share:

Thursday 5 November 2015

5th Batch of Selected Students to join with Bachelor Degree at SJUT 2015/2016

Share:

ANGALIA ADA KAMILI KWA WANAFUNZI MLIOCHAGULIWA MBEYA UNIVERSITY MUST 2015/2016

Share:

HAYA HAPA MAJINA 3RD BATCH WALIOCHAGULIWA MZUMBE UNIVERSITY 2015/2016

Share:

DOWNLOAD HAPA JOINING INSTRUCTIONS NA NAMES OF DIPLOMA STUDENTS SELECTED KCMC 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
kcmuco banner

Selected Candidates for Diploma

Admission Offer / joining instructions for 2015
Share:

ANGALIA HAPA ADA KWA WANAFUNZI WA DUCE 2015/2016

Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOVEMBA 5 2015

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Share:

Jukwaa la Wahariri Walaani Tukio la Kuzomewa Dk Reginald Mengi na Wafuasi wa CCM

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
JUKWAA la Wahariri (TEF), limelaani kitendo cha kuzomewa na kudhalilishwa kwa waandishi wa habari wa ITV, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Dar es Salaam, Oktoba 30 mwaka huu.

Akizungunza na waandishi wa habari Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena amesema kuwa kitendo hicho si cha kukaliwa kimya kutokana na kukwaza utendaji wa kazi na kudhalilisha utu wa waandishi hao mbele ya jamii.

Meena amesema kuwa waandishi na wafanyakazi wa kituo hicho walikuwa katika ofisi hizo za CCM, wakirusha na kuandika habari za tukio la mapokezi ya Dk. John Magufuli baada ya kukabidhiwa hati ya ushindi wa urais na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika hafla iliyofanyika siku hiyo katika ukumbi wa Diamond Jublee.

“Kuzomewa kwa waandishi hao katika ofisi za CCM ni muendelezo wa kile kilichoanzia Diamond Jubilee ambapo wafuasi wa Chama cha Mapinduzi CCM, walionekana wakiwazomea wafanyakazi wa ITV na baadaye kumzonga Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk Reginald Mengi ambaye ni mmliki wa kituo hicho,” amesema Meena.

Ametoa onyo kwa kuwataka wafuasi hao waache vitendo hivyo, akisema kuwa utafiti mdogo waliofanywa na Jukwaa hilo kuhusu vitendo hivyo vinatokana na wafuasi hao kuchukizwa na jinsi kituo hicho kilivyoripoti, matukio ya kampeni na kuwapa fulsa wagombea wa vyama vingine vya siasa.

Amesema kuwa kituo hicho ni miongoni mwa vyombo vya habari vilivyofanya kazi zake kwa weredi wakati wa kampeni za wagombea wa vyama vyote nchi nzima ambapo Dk. Magufuli na Mgombea Mwenza, Samia Suluhu walikuwa na wandishi wa kituo hicho miongoni mwao ni Emmanuel Buhohera na Halfan Liundi ambapo umma wa watanzania ulipata kufahamu kinachoendelea katika mikutano yao ya kampeni.

Meena ameongeza kuwa hilo sio tukio la kwanza kufanywa na chama hicho kwani wakati wa kampeni za mgombea urais kilimfukuza katika msafara wa Dk. Magufuli mkoani Mbeya, mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Peter Elias kwa madai ya kutofurahishwa na habari aliyoandika kuhusu mgombea wao.

Amesema kuwa matuko hayo siyo ya kiungwana na hayatakubalika katika jamii ya watu wastaarabu. Ikiwa waandishi wa habari au vyombo vya habari vinafanya makosa zipo njia za kisheria za kushughulikia makosa hayo pamoja na kufanya mazungumzo kupitia taasisi za waandishi wa habari.

“Tunachukua fulsa hii kuvitaka vyama vya siasa kama taasisi viongozi, wanachama na wapenzi wake kuacha mara moja vitendo vya kuwashambulia waandishi wa habari kwa sababu zozote zile. Tusingependa ifike hatua kutangaza kwamba matukio ya chama fulani ni hatari kwa waandishi wa habari,” amesema Meena.

Kadhalika tunachukua fursa hii kuvitaka vyama vya siasa na watu binafsi wanaoandaa mikutano inayowahusisha waandishi wa habari kuhakikisha kuwa waandishi wanakuwa salama wanapo hudhuria kwenye mikutano yao na kuchukua hatua ya kukemea.

“Tunasikitika kwa ukimya wa chama hicho ulionyesha kufurahishwa kwa tukio hilo kutokana na kutotoa kauli yoyote,” amesema Meena.
Share:

New AUDIO | Baba Jonii Ft. Dolafosalamitido - AEIOU | Download/Listen

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
https://mkito.com/song/aeiou-ft-dolafosalamitido/17102/bwi-1-33483
Share:

BEN POL AKIMBILIA SAUZ KUPAKUA MZIGO MPYA

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Mkali wa R&B Bongo, Ben Pol.
KACHAA mkali wa R&B Bongo, Ben Pol muda wowote kuanzia sasa anatarajia kuelekea nchini Afrika Kusini ‘Sauz’ kwenda ku-shoot video zake mbili mpya.Ben ameliambia Championi Jumatano kuwa akiwa ‘bondeni’ atatengeneza video mbili za nyimbo zake hizo mpya.
Moja inaitwa Ningefanyaje, aliyoimba na mwanadada mrembo wa Kenya, Avril na nyingine amempa shavu msanii mahiri wa Kenya, Nameless.Aidha, ameongeza kuwa Kampuni ya Gorilla Films chini ya Director, Justin Campos, aliyetengeneza video kali ya Nusu Nusu ya Joh Makini ndiye atakayefanya naye kazi hiyo kwa muda wa wiki moja na nusu.

“Muda wowote tangu sasa nitaenda Sauz ku-shoot video zangu mbili na kampuni ya Gorilla Films, kila kitu kimekaa sawa na tutatumia muda kama wa wiki na nusu hivi kukamilisha kila kitu. Nameless nishaongea naye na nitakutana naye hukohuko kumaliza kazi,” alisema Ben Pol.
Share:

Maalim Seif akutana na JK

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayemaliza muda wake Dkt. Jakaya Kikwete. Mazungumzo hayo yaliyochukua muda wa dakika 50 yalifanyika Ikulu ya Rais Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:24 asubuhi na kumaliza saa 5:14. (Picha na Salmin Said, OMKR)

Share:

Masanja Mkandamizaji Achukua Form za Kugombea Ubunge Ludewa na Ktangaza nia Kuchukua Nafasi ya Marehemu Filikunjombe

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Masanja Mkandamizaji
MSANII maarufu na mwigizaji Emmanuel Mgaya maarufu kwa jina la (Masanja mkandamizaji) ameahidi kuvaa viatu vya Deo H. Filikunjombe kwa kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo la Ludewa na kusema ana uwezo mkubwa na kasi kama ya marehemu Filikunjombe ambaye alikuwa rafiki yake.

Ameyasema hayo alipokuja kuchukua fomu ya kugombea kupata ridhaa ya Chama cha Mapinduzi,jumla ya watu tisa akiwemo mdogo wa marehemu Fillipo Filikunjombe ambaye ni mwanasheria wa TCRA wamechukua fomu ili kuweza kuomba ridhaa
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO RUAHA UNIVERSITY-RUCU 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY

Students Eligible for loan (2015/2016) 
<<Download Here>>
Share:

Wednesday 4 November 2015

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA UDSM 8TH BATCH 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Tokeo la picha la UDSM
The following additional applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2015/2016 academic year. The selected applicants should report at the Mwl. J.K. Nyerere Mlimani Campus for the orientation week which  will end on Saturday 7th November 2015.  Applicants selected for admission into Dar es Salaam University College of Education (DUCE) and Mkwawa University College of Education (MUCE) should report directly to the college's campuses in Chang'ombe and Iringa respectively on the same dates. Joining instructions and admission letters should be collected at the University campuses where one is admitted. Joining instructions  and other important information can also be downloaded from the University website at www.udsm.ac.tz  (go to the Undergraduate Section).
Click Here to View the selected  applicants.
Share:

FIFTH AND FOURTH BATCH -STUDENTS SELECTED MWENGE UNIVERSITY 2015/2016

INNOCENT-THE BLOGGER-BOY
Research and Publication image

SELECTED APPLICANT FOR ACADEMIC YEAR 2015/2016 FIFTH BATCH

SELECTED APPLICANT FOR ACADEMIC YEAR 2015/2016 FOURTH BATCH

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger