Friday, 2 January 2026

WANANCHI KIJIJI CHA LAJA WILAYANI KARATU WAISHUKURU TASAF UJENZI SEKONDARI MPYA


Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Karatu

WANANCHI Kijiji cha Laja katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu mkoani Arusha wameishukuru TASAF kukubali Mradi wa kupunguza Umaskini (OPEC) kutekelezwa katika Kiji hicho na kutoa fedha kutekelezwa mradi wa ujenzi wa mpya ya Shule ya Sekondari ambao umesaidia wanafunzi kuondokana na changamoto ya kutembea umbali wa kilometa nane kuisaka elimu.

Wakizungumza wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) Shedrack Mziray aliyekuwa akikagua utekelezaji wa mradi huo,wananchi wa Kijiji hicho wamesema kupitia Mfuko huo wamepata shule hiyo ambayo imeondoa changangamoto wanafunzi waliokuwa wanachaguliwa kujiunga Sekondari kutembea umbali mrefu.

Mkazi wa Kijiji cha Laja Christina Lucas amesema wakati shule haijajengwa katika maeneo hayo wanafunzi walikuwa wanateseka haswa watoto wa kike ambao ndio kundi lililokuwa linaathirika kwasababu wanakutana na adha nyingi.

“Uwepo wa shule hii imepunguza utoro usio wa lazima kwasababu kwa vyovyote vile mtoto akitoka nyumbani kilometa nane njiani anakutana na changamoto nyingi ,mara nyingine wanasindikizwa na bodaboda ambao baadhi yao ni hatari kwa usalama wa wanafunzi Wetu.

“Baada ya kupata mradi huu na shule kujengwa hivi sasa watoto wanakaa katika mabweni hivyo wanakuwa salama na ndio maana mpaka sasa hakuna mwanafunzi ambaye amepata ujauzito kwani wazazi tunafuatilia sana ,watoto wako salama.

Kuhusu TASAF amesema wananchi wa Kijiji cha Laja wanaipongeza na kuishukuru lakini wanatoa ombi la kujengewa majengo ya maabara pamoja na kuongezwa nyumba za walimu kwani zilizopo hazitoshi.

“Tunatamani kama itawezekana basi Rais wetu Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia TASAF atuone tena kwa kutujengea Maktaba,mabweni na nyumba za walimu.Pia namshukuru Rais wangu kwa kuliona hili kwani hii shule hatukutegemea ingejengwa katika maeneo haya.

“Rais wetu ni msikivu ameangalia mpaka huku kwetu ambako tulisahaulika lakini sasa ametujengea shule ya kifahari ambayo pengine ilitakiwa ijengwe hata Karatu ila kwa sasa iko kijijini kwetu.”

Kwa upande wake Andrea Mtupa amesema wanafunzi wanaofaulu kwenda kidato cha kwanza walikuwa wanatembea umbali wa kilometa nane kwenda na kilometa nane wakati wa kurudi kila siku lakini hivi sasa TASAF kupitia mradi wa OPEC wamejengewa shule ya Sekondari ya kisasa.

Awali Ofisa Mtendaji Kijiji cha Laja Daniel Mpigachai amesema mradi wa ujenzi wa shule hiyo umegharimu Sh.774,946,675, ambapo TASAF kupitia OPEC awamu ya Nne walitoa fedha Sh. 659,505,275 na fedha Sh.115,441,400 ni mchango wa jamii ambao umejumuisha mchanga,Kokoto ,mawe,maji na nguvu kazi wakati wa ujenzi.

Kuhusu manufaa ya mradi amesema shule hiyo iliyosajiliwa Novemba 2023 ilianza rasmi mwaka 2024 kwa kupokea wanafunzi 26 wa Kidato cha kwanza, kwa sasa shule ina Jumla ya wanafunzi 63 ambao ni kidato cha kwanza na cha pili na wote wanakaa Bweni.

“Uwepo wa mradi huu umeondoa tatizo la utoro shuleni, wanafunzi kuongeza morali ya kusoma tofauti na awali walipokuwa wanasoma shule ya kata iliyo na umbali wa Zaidi ya kilometa 8 kutoka kijini kwetu, shule imepokea pia watoto wanaotoka viji vya jirani.

Aidha amesema kwa niaba ya Wananchi wa Kijiji cha Laja wanatoa ombi kwa TASAF kama fursa nyingine itajitokeza wanaomba mradi wa ujenzi Majengo mengine yaliyosalia kama Maabara, Maktaba, Nyumba nyingine za walimu na Madarasa.

Wakati huo huo Mkuu wa Shule ya Sekondari Laja Daniel Panga amesema shule hiyo iliyojengwa kisasa mbali kuondoa changamoto wanafunzi kutembea umbali mrefu imeleta hamasa kwa wanafunzi wanaosoma elimu ya msingi wanaamini ipo siku watajiunga na shule hiyo.
Share:

Thursday, 1 January 2026

WAKAZI WA JIJI LA DODOMA WAKISHEREHEKEA MWAKA MPYA 2026 KATIKA ENEO LA NYERERE SQUARE DODOMA LEO



Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Wakazi wa Jiji la Dodoma leo wamejitokeza kwa wingi katika eneo la Nyerere Square kusherehekea kuupokea Mwaka Mpya 2026, huku shamrashamra na furaha zikitawala anga la jiji hilo kuu la Serikali.

Shughuli mbalimbali za burudani, muziki, michezo ya watoto, pamoja na vionjo vya chakula na vinywaji zimetawala katika eneo hilo kuanzia majira ya asubuhi hadi jioni ambapo katika kusherehekea tukio hilo, maeneo ya kandokando ya Nyerere Square yalipambwa kwa taa za rangi jambo lililoashiria kuwa wananchi wanaishi kwa amani.

Jambo hilo limeongeza hamasa kwa wakazi na wageni waliotembelea jiji hilo kwa ajili ya sikukuu.

Baadhi ya wananchi waliozungumza na Malunde Blog wamesema kuwa kuuanza mwaka mpya katika eneo hilo limekuwa tukio la kipekee  kwani linatoa fursa ya kuunganisha jamii, kuimarisha undugu na kutoa matumaini ya safari mpya ya mafanikio.

Sherehe hizo zimeendelea kwa amani na utulivu, huku vyombo vya ulinzi na usalama vikiwa katika uangalizi kuhakikisha kila mkazi anasherehekea katika mazingira salama na rafiki.

Mwaka Mpya 2026 umeanza kwa matumaini mapya kwa wakazi wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla, huku wengi wakitamani mwaka huo kuleta maendeleo, neema na mafanikio katika nyanja mbalimbali za maisha.





Share:

DC NKINDA ACHUKUA HATUA ZA HARAKA KUTATUA KERO YA BARABARA MHONGOLO NA NYASHIMBI, KAHAMA



Na Neema Nkumbi, Kahama

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Frank Nkinda, amechukua hatua za haraka kutatua changamoto ya miundombinu ya barabara katika mitaa na kata mbalimbali za Manispaa ya Kahama, kufuatia kero zilizowasilishwa na vijana wakati wa sherehe za Krismasi walipokutana naye kwa chakula cha pamoja.

Leo Desemba 31, 2025, DC Nkinda ametembelea Mtaa wa Mhongolo ambapo amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoyatoa katika hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Bunge la 13, akiwataka watumishi wa umma kuwahudumia wananchi kwa vitendo na kuwaletea tabasamu wale waliomwamini na kumpa ridhaa ya kuwaongoza.

Akizungumza na waandishi wa habari, Nkinda amesema Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama imefanikiwa kutafuta mtambo wa kuchonga barabara (greda) ili kuanza kushughulikia kero za barabara zilizoharibika katika maeneo mengi kutokana na mvua, akisisitiza kuwa lengo ni kuhakikisha wananchi hawakwami katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, hususan shughuli za kujipatia kipato.

“Ninatoa shukrani zangu kwa Mheshimiwa Rais, kwani Serikali imetutengea fedha kwa ajili ya kumaliza changamoto ya miundombinu ya barabara, Hata hivyo, Ofisi ya Mkuu wa wilaya Kahama imeona ichukue hatua za haraka wakati tukiendelea kusubiri fedha hizo kutufikia,” amesema Nkinda.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Nyashimbi, Kata ya Mhongolo, Emanuel Lutonja, amemshukuru Rais Samia pamoja na DC Nkinda kwa hatua hiyo, akisema ujio wa greda katika mtaa wake umepunguza kwa kiasi kikubwa kero za barabara zilizokuwa na madimbwi makubwa yaliyowaathiri wafanyabiashara, hususan bodaboda, bajaji na wajasiriamali walioko pembezoni mwa barabara.

“Barabara hii ni kiunganishi kikuu kati ya Nyashimbi, Mhongolo hadi mjini, hivyo ukarabati wake utasaidia sana wananchi wa mtaa huu kufanya kazi zao bila wasiwasi,” amesema Lutonja.

Naye Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Mhongolo, Renatus Thomas, amesema jitihada za DC Nkinda zinastahili pongezi, akibainisha kuwa bila uongozi wake barabara hiyo isingetengenezwa kwa wakati hivyo amemuomba DC kuendelea na zoezi hilo kwani barabara nyingi za Mhongolo bado ni mbovu na zina madimbwi makubwa.

Mkazi wa Nyashimbi Sokoni, Japhet Kitima, amesema awali wafanyabiashara walipata changamoto kubwa kuingiza mizigo kwa magari kutokana na ubovu wa barabara, hali iliyosababisha hasara hivyo wanamshukuru DC kwa kuwaletea greda kwani sasa hali imeanza kubadilika.

Kwa upande wake, Zainabu, mkazi wa Mhongolo na mfanyabiashara wa chakula, amesema mashimo na matope yaliyokuwapo barabarani yalikuwa yakisababisha usumbufu mkubwa hasa magari yalipopita, huku mkazi mwingine wa Nyashimbi, Sharifa Ramadhan, ameeleza kuwa maji yaliyotuama barabarani yalikuwa yakirukia madukani mwao na kutoa harufu mbaya, hali iliyosababisha hata bajaji za mizigo kukataa kufika eneo hilo.

Sambamba na ukarabati wa barabara, DC Nkinda amewataka viongozi wa mitaa ya Mhongolo na Nyashimbi kuhakikisha mitaro iliyoziba kwa mchanga inazibuliwa ili kuruhusu maji kupita vizuri, akibainisha kuwa kuziba kwa mitaro ndiko chanzo kikuu cha uharibifu wa barabara nyingi.

Katika ziara hiyo, DC Nkinda ametembelea barabara ya Mhongolo Senta kuelekea KACU pamoja na barabara ya Mhongolo kuelekea Nyashimbi Sokoni, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushughulikia kero za wananchi kwa vitendo na kwa wakati.
Share:

Wednesday, 31 December 2025

MALUNDE 1 BLOG INAKUTAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2026!


 
Share:

WANANCHI FUONI WAJITOKEZA KUPIGA KURA KUCHAGUA MBUNGE WAO

Share:

Tuesday, 30 December 2025

MAKAVAZI YA MUUNGANO: SILAHA MPYA DHIDI YA UPOTOSHAJI NA CHUKI ZINAZOLENGA KUIVUNJA TANZANIA

 Serikali imetangaza kuwa ujenzi wa Makavazi ya Muungano sasa umefika ukingoni, huku ikibainishwa kuwa vituo hivyo vitakuwa "darasa la kudumu" la kukabiliana na mawimbi ya upotoshaji wa historia yanayopandikizwa na baadhi ya wanaharakati na watu wenye nia ovu ya kutaka kuuvunja Muungano wa Tanzania.

Akizungumza Desemba 28, 2025, visiwani Unguja, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, amesema ujenzi huo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inayolenga kuziba mwanya wa kutokuelewa mambo unaotumiwa na maadui wa umoja wa kitaifa.

 Kukabiliana na "Wanaharakati wa Uongo"

Waziri Masauni amefafanua kuwa katika miaka ya hivi karibuni, kumeibuka kundi la watu wanaojiita wanaharakati ambao wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii na majukwaa mengine kupotosha ukweli kuhusu makubaliano ya mwaka 1964. Amesema kutokuwepo kwa kituo kimoja chenye ushahidi wa nyaraka kumesababisha baadhi ya vijana kuyumbishwa na hoja za chuki zinazolenga kuleta mfarakano kati ya Tanganyika na Zanzibar.

"Makavazi haya yatakuwa jibu kwa wale wote wanaotaka kuivunja nchi kwa kutumia historia ya uongo. Kijana akitaka kujua kwanini tulitoka huko na kwanini tuko hapa, hatasikiliza maneno ya mitaani ya watu wenye ajenda zao, bali atakuja makavazi kuona nyaraka, picha, na sauti za waasisi wetu," alisisitiza Mhe. Masauni.

Kuziba Pengo la Maarifa kwa Vijana

Hafla hiyo ya uwekaji jiwe la msingi la jengo la Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Zanzibar, iliyoongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, imetumika kusisitiza kuwa vijana ndio walengwa wakuu. Serikali imebaini kuwa kutokana na kutopata elimu sahihi ya historia mashuleni na kwenye vyanzo rasmi, vijana wengi wamekuwa wepesi kuamini "propaganda" zinazochochea ubaguzi na utengano.

Makavazi kama Kituo cha Elimu na Ushahidi

Mhandisi Masauni amebainisha kuwa makavazi hayo yaliyopo Dodoma, Dar es Salaam (katika Ukumbi wa Karimjee kwa muda), na Zanzibar, hayatakuwa tu majengo ya kuhifadhi vitu vya kale, bali vituo vya kimkakati vitakavyohusisha:

Uhifadhi wa Nyaraka za Asili: Ili kuthibitisha uhalali na faida za Muungano tangu asili yake.

Kumbi za Mikutano na Kusomea: Maeneo ambayo watafiti na wanafunzi wanaweza kuchimba ukweli na kujadiliana kwa msingi wa data, si hisia.

Teknolojia ya Kisasa: Matumizi ya mifumo ya kidijitali kuonyesha safari ya Tanzania ili kuwavutia vijana na kuwapa ukweli usiopingika.

Utekelezaji wa Ahadi ya Rais Dkt. Samia

Waziri Masauni amekumbusha kuwa mradi huu ni kielelezo cha maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa tangu akiwa kwenye kampeni za uchaguzi. Rais aliona mapema hitaji la kulinda amani ya nchi kwa kuimarisha "kinga ya kifikra" kupitia elimu ya historia ya nchi.

Kupitia shamrashamra hizi za miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Serikali imetoa onyo kwa wale wanaotumia ujinga wa historia kama silaha ya kubomoa nchi, ikiahidi kuwa makavazi hayo yatakuwa suluhisho la kudumu la kuunganisha Watanzania kupitia ukweli.

Share:

DC NKINDA AANZA KUTATUA CHANGAMOTO YA BARABARA YA SHUNU–ZONGOMELA, KAHAMA

 


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Frank Nkinda, ameanza utekelezaji wa ahadi yake ya kutatua changamoto ya barabara iliyowasilishwa na mwananchi wa Shunu ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT–Wazalendo wilayani Kahama, Abas Omari, wakati alipokutana na vijana katika sherehe za Krismasi maarufu kama Pilau la Wana.


Katika sherehe hizo, DC Nkinda aliahidi kutembelea eneo husika ili kujionea ukubwa wa tatizo na kuchukua hatua stahiki, Leo, ametimiza ahadi hiyo kwa kutembelea barabara yenye changamoto katika Mtaa wa Hongwa, Kata ya Nyahanga, wilayani Kahama mkoani Shinyanga, inayounganisha eneo la Shunu na eneo la viwanda la Zongomela maarufu Dodoma.


Akiwa katika ziara hiyo, DC Nkinda amejionea adha inayowakabili wananchi wanaoutumia barabara hiyo, hususan wafanyabiashara na wafanyakazi wa viwanda vidogo vidogo zongonela, Kutokana na umuhimu wake kiuchumi, ameagiza mkandarasi anayetekeleza mradi huo Prinax investment limited kuhakikisha anakamilisha ujenzi kwa wakati uliopangwa ili kuondoa kero kwa wananchi na kurahisisha shughuli za uzalishaji na biashara.


Akizungumza kuhusu hatua za utekelezaji wa mradi, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA), mhandisi Juma Masola, ameahidi kumsimamia kwa ukaribu mkandarasi anayetekeleza mradi huo ili kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa, hivyo kuwezesha shughuli za kiuchumi kuendelea bila vikwazo.


Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Nyahanga, Mheshimiwa Josephina Kilimba, amwtaja barabara nyingine korofi zinazohitaji matengenezo ya dharura, ikiwemo barabara ya Vatikani iliyopo Mtaa wa Lugela huku akisisitiza umuhimu wa hatua za haraka ili kuboresha miundombinu na kuongeza ustawi wa wananchi.


Wananchi wa eneo hilo wamepongeza jitihada za Serikali ya Wilaya ya Kahama kwa kuanza kuchukua hatua za vitendo katika kutatua changamoto za barabara, wakieleza matumaini kuwa maboresho hayo yataongeza fursa za kiuchumi na kuboresha maisha yao kwa ujumla.




Share:

Monday, 29 December 2025

Video Mpya : CHIEF MAKER - MWAMBA

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 29,2025



Magazeti
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger