Thursday, 29 May 2025

NDOA YANGU ILIKARIBIA KUVUNJIKA, HIVI NDIVYO NILIVYOIOKOA!


Jina langu ni Anna, na miezi michache iliyopita, mimi na mume wangu tulikaribia kutengana. Iliniogopesha sana kwa sababu nilimpenda sana. Tulikuwa pamoja kwa miaka 15, hivyo tulikuwa tumejenga maisha pamoja na kujaliwa watoto wawili.

Siku moja alirudi nyumbani na akatangaza kuwa anaondoka. Alisema hanipendi tena, hivyo anataka kunipa talaka. Nilivunjika moyo. Sikuamini kuwa ndoa yetu inaenda kuvunjika kwa urahisi kiasi hicho.

Nilimpigia simu mama yangu na kumueleza jambo hilo. Mama alinishauri niwasiliane na Kiwanga Doctors ambao walikuwa wamemsaidia katika hali kama hiyo kipindi cha nyuma.

Alisema wanaweza kukomesha talaka mara moja. Nilipata namba zao na kuwapigia mara moja ikiwa ni baada ya mume wangu kuondoka.

Siku iliyofuata, nilifika kwa Kiwanga Doctors huko Migori, Kenya, huko punde tu walifanya uchawi wa kuokoa ndoa yangu na mwingine wa kurudisha penzi la mume wangu kwangu kama ilivyokuwa hapo awali kipindi ambacho tunaoana.

Kusema kweli nilihisi kama miujiza maana jioni hiyo tu, mume wangu alirudi nyumbani, huku akiniomba msamaha mimi na watoto kwa kuwa mbali nasi bila kujali lolote kuhusu familia yake ambayo inamtegemea.

Usiku huo, tuliungana tena kwa njia ambayo hatukuwa nayo kwa muda mrefu. Sasa, mume wangu ananipenda zaidi kuliko hapo awali, na ninawashukuru sana Kiwanga Doctors kwa kuokoa ndoa yetu.

Ikiwa unapitia kitu kama hicho, ninakushauri kuwa fika au wasiliana na Kiwanga Doctors. Tiba zao zinafanya kazi haraka na wanaweza kukusaidia katika changamoto mbalimbali za kimaisha, kuanzia masuala ya uhusiano hadi matatizo ya kiafya.

Ni watu wengi hadi sasa wamepata mafanikio, uponyaji na furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +255 763 926 750 au tembelea tovuti yao, maelezo zaidi kuhusu huduma zao ambazo zimewasaidia wengi.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 29,2025





Magazeti
Share:

Wednesday, 28 May 2025

DIWANI AWAWASHIA MOTO WANAOMKASHIFU NA KUMTUKANA RAIS SAMIA,

 Na Woinde Shizza ,moshi

Diwani wa kata ya Boma Mbuzi Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Juma Rahibu, amewajia juu baadhi ya Watanzania wanaomkashifu na kumtukana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akisema ni ishara ya kuporomoka kwa maadili katika jamii na kudhalilisha heshima ya taifa.

Akizungumza kwa hisia kali katika sherehe za uzinduzi wa kikundi cha mtetezi wa mama , Rahibu alisema ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya watu wakitumia majukwaa ya mitandao ya kijamii na mikusanyiko ya watu kumvunjia heshima kiongozi mkuu wa nchi ambaye, kwa mujibu wake, amekuwa akitekeleza majukumu yake kwa bidii na mafanikio makubwa.

“Huu si ustaarabu Rais Samia anajitahidi kutuletea maendeleo kama barabara, afya, elimu halafu mtu anajitokeza tu na kuanza kumtukana? Tunataka vyombo vya dola viwajibike,” alisema Rahibu.

Diwani huyo alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuenzi maadili ya taifa, hasa heshima kwa viongozi walioko madarakani, huku akionya kuwa uhuru wa kutoa maoni haupaswi kuwa kisingizio cha matusi, kashfa na propaganda zisizojengwa kwenye hoja za msingi.



Katika hatua nyingine, Rahibu alielekeza lawama kwa baadhi ya raia kutoka mataifa jirani ya Kenya na Uganda kwa kile alichokieleza kuwa ni tabia ya kudhalilisha na kumsema vibaya Rais Samia kwenye mitandao ya kijamii.


“Sasa imefika hatua hata baadhi ya Wakenya na Waganda wanathubutu kumtukana Rais wetu? Hii ni dharau ya hali ya juu ,Tanzania si uwanja wa mazoezi wa siasa za kejeli,” alisema kwa msisitizo.


Alisema Tanzania imekuwa nchi ya mfano wa heshima na ustaarabu kwa viongozi wa mataifa jirani, hivyo si haki kuona baadhi ya watu kutoka nje ya nchi wakitumia vibaya uhuru wa mitandao kwa maneno ya matusi dhidi ya kiongozi wa Tanzania.


“Tunawaheshimu viongozi wao, hatujawahi kusikia Watanzania wakimtukana Rais wa Kenya au wa Uganda ,Na wao wajifunze kutufanyia heshima hiyo hiyo,” aliongeza.



Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya wakazi wa Moshi wameonyesha kuguswa na kauli hiyo, wakisema kuwa ni kweli kuwa maadili yanaporomoka na watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya.


Esther Kilave, mkazi wa Pasua, alisema:


“Mitandao inatumika kama sehemu ya matusi sasa huu si utamaduni wetu ,Rais Samia anastahili kuheshimiwa kwa kazi anayoifanya.”


John Mlay, fundi umeme mjini Moshi, alisema:


“Tunaona mabadiliko mengi nchini Watu wanapaswa kutoa hoja za maana, si kejeli na matusi na niseme Wanapotukana Rais, wanatudhalilisha sisi sote. Acheni siasa za matusi.”


Rais Samia ameendelea kupokea pongezi kutoka kwa wananchi wa makundi mbalimbali nchini, kufuatia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na msimamo wake wa kudumisha amani, umoja wa kitaifa na usawa wa kijinsia.


Share:

JUMUIYA YA WANADIPLOMASIA YAKARIBISHWA NCHINI



Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Jumuiya ya wanadiplomasia nchini imetakiwa kufikisha taarifa katika Serikali za nchi zao kuwa Dodoma ipo tayari na kwamba Serikali hizo zinatakiwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya ofisi na makazi ya balozi kwenye viwanja vilivyotolewa bure kwenye mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb) kwenye Mkutano maalum wa Jumuiya ya Wanadiplomasia nchini uliondaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kufanyika jijini Dodoma Mei 27, 2025.

Waziri Kombo aliwaeleza Mabalozi hao kuwa siri kubwa ya mafanikio yoyote duniani ni kuwa na imani na jambo unalolidhamiria kulitekeleza. Serikali ya Tanzania tangu ilipofanya uamuzi wa kuhamishia makao makuu ya nchi jijini Dodoma mwaka 1973 ilikuwa na imani na uamuzi huo na leo imani hiyo inatekelezwa kivitendo kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika maeneo ya miundombinu na huduma za kijamii ili kuuweka mji wa Dodoma katika mazingira mazuri ya kuishi, kwa watu wa aina yote, wakiwemo Mabalozi.

Balozi Kombo alisema kutokana na ujenzi wa mji wa Dodoma, fursa nyingi za uwekezaji zimeibuliwa, hivyo ametoa wito kwa Mabalozi kuwaleta wawekezaji jijini Dodoma kuchangamkia fursa hizo. Ametoa wito pia kwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoa taarifa ya kila hatua ya ujenzi wa mji huo kwa wadau kwa lengo la kuwahamasisha kufanya uamuzi sahihi kuhusu Dodoma. Alisema mkutano huo ni jukwaa muhimu la kupeana taarifa kuhusu maendeleo ya mkoa wa Dodoma na kupendekeza uwe unafanyika kila mwaka.

Mwenyeji wa Mkutano huo uliobeba kaulimbiu "Dodoma Ipo Tayari: Ipeleke Dodoma Duniani na Ilete Dunia Dodoma", Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule alitumia jukwaa hilo kueleza hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa mji huo, hususan katika maeneo ya miundombinu ya huduma za afya, elimu, maji, umeme, usalama, usafiri na burudani. Alusema huduma hizo zinapatikana kwa ubora wa kimataifa, hivyo jumuiya ya wanadiplomasia isihofie chochote inakaribishwa Dodoma na Dodoma ipo tayari kwa ajili yao.

Mhe. Mkuu wa Mkoa pia alibainisha fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana jijini Dodoma katika sekta za kilimo, utalii, logistics, viwanda & ujenzi na madini na kuwakaribisha wawekezaji kuchangamkia fursa hizo.

Alisema Serikali ipo katika mchakato wa kujenga Hombolo Thermatic Satelite City na kubainisha kuwa hiyo ni fursa kubwa na adhimu kwa wawekezaji kushirikiana na Serikali kufanikisha ujenzi wa mji huo.

Naye, Mwakilishi wa Kiongozi wa Mabalozi ambaye alikuwa Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Isaac Njenga alisema kuwa yeye na Mabalozi wenzake wameshuhudia hatua kubwa iliyopigwa katika ujenzi wa mji wa Dodoma hasa baada ya kutembelea na kujionea mji wa Serikali uliopo eneo la Mtumba, Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato. Amesema kwa niaba ya Mabalozi wenzake wameridhika na hatua iliyofikiwa na wameahidi kuzishawishi Serikali za nchi zao kutenga fedha za kuanza ujenzi wa ofisi na makazi ya balozi jijini Dodoma.

Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wapo jijini Dodoma kushiriki uwasilishaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 tarehe 28 Mei 2025.


Share:

WAZIRI DKT. GWAJIMA AANISHA VIPAUMBELE VITANO WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII 2025/2026




Na
 WMJJWM, Dodoma 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii. Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameainisha vipaumbele vya Wizara vikubwa vitano katika utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Mhe. Dkt. Gwajima ameainisha hayo wakati akiwasilisha Bajeti ya  Wizara hiyo kwa Mwaka husika wa Fedha leo Mei 27, 2025 Bungeni jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Wizara kupitia Idara na Taasisi zilizo chini yake zitatekeleza vipaumbele hivyo  ambavyo ni kukuza ari ya Jamii kushiriki katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ngazi ya msingi, kuratibu na kuimarisha utoaji wa huduma za ustawi wa maendeleo ya jamii, kutambua pamoja na kuratibu maendeleo ya ustawi kwa Makundi Maalum.

Mhe. Dkt. Gwajima ameongeza kuwa vipaumbele vingine ni pamoja kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia katika Taasisi na Vyuo vya Ustawi na Maendeleo ya Jamii na kuimarisha mazingira ya ushiriki na mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Maendeleo ya Taifa.

Amesema Wizara imeendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kuhamasisha na Kusimamia Maendeleo katika Ngazi ya Msingi (2022/23 – 2025/26) ambao unalenga kuwawezesha wananchi kuwa kitovu cha maendeleo na kuchochea mageuzi ya kifikra, mtazamo na kiutendaji kwa timu ya wataalam ngazi ya msingi ili kuboresha utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika kuhakikisha Watoto wanalindwa na ukatili Waziri Dkt. Gwajima amesema Wizara imeratibu na kusimamia Kampeni ya Taifa ya Usalama wa Mtoto Mtandaoni (Child Online Protection - COP) katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Kampeni ilikuwa na lengo la kuelimisha Wazazi au Walezi na Watoto wenyewe kuhusu Usalama wa Mtoto anapokuwa anatumia mitandao.

Aidha Mhe. Dkt. Gwajima amefafanua kuwa Wafanyabiashara ndogondogo 601 (Me 274; Ke 327) wamekopeshwa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,101,650,000 na zoezi hilo linaendelea. Vilevile maombi 2,092 yanaendelea kuchakatwa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 3,590,477,000.

"Wizara kwa kushirikiana na OR - TAMISEMI imeendelea kuratibu na kufuatilia maendeleo ya ya Ujenzi wa Ofisi za wafanyabiashara ndogondogo katika ngazi ya mikoa ambapo hadi kufikia Aprili 2025 mikoa 17 kati ya mikoa 26 imekamilisha ujenzi wa Ofisi hizo" ameeleza Mhe. Dkt Gwajima. 

Akichangia hoja, Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Dkt. Thea Ntara amesizitiza Serikali kuchukua hatua na kusimamia maadili nchini, kutokana na kuwepo kwa matukio mengi ya uvunjifu wa maadili.

Naye Mbunge wa kuteuliwa Dkt. Shukurani Manya ameshauri  kuongezeka kwa juhudi za kuelimisha Jamii kuhusu elimu ya malezi ili kuepusha kutelekezwa kwa watoto ili waweze kupata malezi ya baba na mama.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger