Wednesday, 28 May 2025

DIWANI AWAWASHIA MOTO WANAOMKASHIFU NA KUMTUKANA RAIS SAMIA,

 Na Woinde Shizza ,moshi

Diwani wa kata ya Boma Mbuzi Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Juma Rahibu, amewajia juu baadhi ya Watanzania wanaomkashifu na kumtukana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akisema ni ishara ya kuporomoka kwa maadili katika jamii na kudhalilisha heshima ya taifa.

Akizungumza kwa hisia kali katika sherehe za uzinduzi wa kikundi cha mtetezi wa mama , Rahibu alisema ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya watu wakitumia majukwaa ya mitandao ya kijamii na mikusanyiko ya watu kumvunjia heshima kiongozi mkuu wa nchi ambaye, kwa mujibu wake, amekuwa akitekeleza majukumu yake kwa bidii na mafanikio makubwa.

“Huu si ustaarabu Rais Samia anajitahidi kutuletea maendeleo kama barabara, afya, elimu halafu mtu anajitokeza tu na kuanza kumtukana? Tunataka vyombo vya dola viwajibike,” alisema Rahibu.

Diwani huyo alisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuenzi maadili ya taifa, hasa heshima kwa viongozi walioko madarakani, huku akionya kuwa uhuru wa kutoa maoni haupaswi kuwa kisingizio cha matusi, kashfa na propaganda zisizojengwa kwenye hoja za msingi.



Katika hatua nyingine, Rahibu alielekeza lawama kwa baadhi ya raia kutoka mataifa jirani ya Kenya na Uganda kwa kile alichokieleza kuwa ni tabia ya kudhalilisha na kumsema vibaya Rais Samia kwenye mitandao ya kijamii.


“Sasa imefika hatua hata baadhi ya Wakenya na Waganda wanathubutu kumtukana Rais wetu? Hii ni dharau ya hali ya juu ,Tanzania si uwanja wa mazoezi wa siasa za kejeli,” alisema kwa msisitizo.


Alisema Tanzania imekuwa nchi ya mfano wa heshima na ustaarabu kwa viongozi wa mataifa jirani, hivyo si haki kuona baadhi ya watu kutoka nje ya nchi wakitumia vibaya uhuru wa mitandao kwa maneno ya matusi dhidi ya kiongozi wa Tanzania.


“Tunawaheshimu viongozi wao, hatujawahi kusikia Watanzania wakimtukana Rais wa Kenya au wa Uganda ,Na wao wajifunze kutufanyia heshima hiyo hiyo,” aliongeza.



Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya wakazi wa Moshi wameonyesha kuguswa na kauli hiyo, wakisema kuwa ni kweli kuwa maadili yanaporomoka na watu kutumia mitandao ya kijamii vibaya.


Esther Kilave, mkazi wa Pasua, alisema:


“Mitandao inatumika kama sehemu ya matusi sasa huu si utamaduni wetu ,Rais Samia anastahili kuheshimiwa kwa kazi anayoifanya.”


John Mlay, fundi umeme mjini Moshi, alisema:


“Tunaona mabadiliko mengi nchini Watu wanapaswa kutoa hoja za maana, si kejeli na matusi na niseme Wanapotukana Rais, wanatudhalilisha sisi sote. Acheni siasa za matusi.”


Rais Samia ameendelea kupokea pongezi kutoka kwa wananchi wa makundi mbalimbali nchini, kufuatia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na msimamo wake wa kudumisha amani, umoja wa kitaifa na usawa wa kijinsia.


Share:

JUMUIYA YA WANADIPLOMASIA YAKARIBISHWA NCHINI



Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Jumuiya ya wanadiplomasia nchini imetakiwa kufikisha taarifa katika Serikali za nchi zao kuwa Dodoma ipo tayari na kwamba Serikali hizo zinatakiwa kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya ofisi na makazi ya balozi kwenye viwanja vilivyotolewa bure kwenye mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb) kwenye Mkutano maalum wa Jumuiya ya Wanadiplomasia nchini uliondaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kufanyika jijini Dodoma Mei 27, 2025.

Waziri Kombo aliwaeleza Mabalozi hao kuwa siri kubwa ya mafanikio yoyote duniani ni kuwa na imani na jambo unalolidhamiria kulitekeleza. Serikali ya Tanzania tangu ilipofanya uamuzi wa kuhamishia makao makuu ya nchi jijini Dodoma mwaka 1973 ilikuwa na imani na uamuzi huo na leo imani hiyo inatekelezwa kivitendo kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika maeneo ya miundombinu na huduma za kijamii ili kuuweka mji wa Dodoma katika mazingira mazuri ya kuishi, kwa watu wa aina yote, wakiwemo Mabalozi.

Balozi Kombo alisema kutokana na ujenzi wa mji wa Dodoma, fursa nyingi za uwekezaji zimeibuliwa, hivyo ametoa wito kwa Mabalozi kuwaleta wawekezaji jijini Dodoma kuchangamkia fursa hizo. Ametoa wito pia kwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kutoa taarifa ya kila hatua ya ujenzi wa mji huo kwa wadau kwa lengo la kuwahamasisha kufanya uamuzi sahihi kuhusu Dodoma. Alisema mkutano huo ni jukwaa muhimu la kupeana taarifa kuhusu maendeleo ya mkoa wa Dodoma na kupendekeza uwe unafanyika kila mwaka.

Mwenyeji wa Mkutano huo uliobeba kaulimbiu "Dodoma Ipo Tayari: Ipeleke Dodoma Duniani na Ilete Dunia Dodoma", Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule alitumia jukwaa hilo kueleza hatua mbalimbali zilizofikiwa katika ujenzi wa mji huo, hususan katika maeneo ya miundombinu ya huduma za afya, elimu, maji, umeme, usalama, usafiri na burudani. Alusema huduma hizo zinapatikana kwa ubora wa kimataifa, hivyo jumuiya ya wanadiplomasia isihofie chochote inakaribishwa Dodoma na Dodoma ipo tayari kwa ajili yao.

Mhe. Mkuu wa Mkoa pia alibainisha fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana jijini Dodoma katika sekta za kilimo, utalii, logistics, viwanda & ujenzi na madini na kuwakaribisha wawekezaji kuchangamkia fursa hizo.

Alisema Serikali ipo katika mchakato wa kujenga Hombolo Thermatic Satelite City na kubainisha kuwa hiyo ni fursa kubwa na adhimu kwa wawekezaji kushirikiana na Serikali kufanikisha ujenzi wa mji huo.

Naye, Mwakilishi wa Kiongozi wa Mabalozi ambaye alikuwa Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Isaac Njenga alisema kuwa yeye na Mabalozi wenzake wameshuhudia hatua kubwa iliyopigwa katika ujenzi wa mji wa Dodoma hasa baada ya kutembelea na kujionea mji wa Serikali uliopo eneo la Mtumba, Hospitali ya Rufaa ya Benjamin Mkapa na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato. Amesema kwa niaba ya Mabalozi wenzake wameridhika na hatua iliyofikiwa na wameahidi kuzishawishi Serikali za nchi zao kutenga fedha za kuanza ujenzi wa ofisi na makazi ya balozi jijini Dodoma.

Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa wapo jijini Dodoma kushiriki uwasilishaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 tarehe 28 Mei 2025.


Share:

WAZIRI DKT. GWAJIMA AANISHA VIPAUMBELE VITANO WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII 2025/2026




Na
 WMJJWM, Dodoma 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii. Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameainisha vipaumbele vya Wizara vikubwa vitano katika utekelezaji wa Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Mhe. Dkt. Gwajima ameainisha hayo wakati akiwasilisha Bajeti ya  Wizara hiyo kwa Mwaka husika wa Fedha leo Mei 27, 2025 Bungeni jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Wizara kupitia Idara na Taasisi zilizo chini yake zitatekeleza vipaumbele hivyo  ambavyo ni kukuza ari ya Jamii kushiriki katika kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa ngazi ya msingi, kuratibu na kuimarisha utoaji wa huduma za ustawi wa maendeleo ya jamii, kutambua pamoja na kuratibu maendeleo ya ustawi kwa Makundi Maalum.

Mhe. Dkt. Gwajima ameongeza kuwa vipaumbele vingine ni pamoja kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia katika Taasisi na Vyuo vya Ustawi na Maendeleo ya Jamii na kuimarisha mazingira ya ushiriki na mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika Maendeleo ya Taifa.

Amesema Wizara imeendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Kuhamasisha na Kusimamia Maendeleo katika Ngazi ya Msingi (2022/23 – 2025/26) ambao unalenga kuwawezesha wananchi kuwa kitovu cha maendeleo na kuchochea mageuzi ya kifikra, mtazamo na kiutendaji kwa timu ya wataalam ngazi ya msingi ili kuboresha utendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika kuhakikisha Watoto wanalindwa na ukatili Waziri Dkt. Gwajima amesema Wizara imeratibu na kusimamia Kampeni ya Taifa ya Usalama wa Mtoto Mtandaoni (Child Online Protection - COP) katika Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Kampeni ilikuwa na lengo la kuelimisha Wazazi au Walezi na Watoto wenyewe kuhusu Usalama wa Mtoto anapokuwa anatumia mitandao.

Aidha Mhe. Dkt. Gwajima amefafanua kuwa Wafanyabiashara ndogondogo 601 (Me 274; Ke 327) wamekopeshwa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1,101,650,000 na zoezi hilo linaendelea. Vilevile maombi 2,092 yanaendelea kuchakatwa yenye thamani ya Shilingi Bilioni 3,590,477,000.

"Wizara kwa kushirikiana na OR - TAMISEMI imeendelea kuratibu na kufuatilia maendeleo ya ya Ujenzi wa Ofisi za wafanyabiashara ndogondogo katika ngazi ya mikoa ambapo hadi kufikia Aprili 2025 mikoa 17 kati ya mikoa 26 imekamilisha ujenzi wa Ofisi hizo" ameeleza Mhe. Dkt Gwajima. 

Akichangia hoja, Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Dkt. Thea Ntara amesizitiza Serikali kuchukua hatua na kusimamia maadili nchini, kutokana na kuwepo kwa matukio mengi ya uvunjifu wa maadili.

Naye Mbunge wa kuteuliwa Dkt. Shukurani Manya ameshauri  kuongezeka kwa juhudi za kuelimisha Jamii kuhusu elimu ya malezi ili kuepusha kutelekezwa kwa watoto ili waweze kupata malezi ya baba na mama.

Share:

MWENYEKITI WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE KAHAMA AWAKARIBISHA WANANCHI KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI

  

Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Wilaya ya Kahama aliebeba shajala akiwakaribisha wananchi wote wa Manispaa ya Kahama na viunga vyake kushiriki katika mkutano mkubwa wa injili utakaoanza kesho, tarehe 28 Mei 2025, na kudumu kwa siku tano.


NA NEEMA NKUMBI - KAHAMA


Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Wilaya ya Kahama amewakaribisha wananchi wote wa Manispaa ya Kahama na viunga vyake kushiriki katika mkutano mkubwa wa injili utakaoanza kesho, tarehe 28 Mei 2025, na kudumu kwa siku tano.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 27, 2025, Mwenyekiti huyo amesema maandalizi yote yamekamilika na tayari wageni waalikwa kwa ajili ya mkutano huo wamewasili.

Mkutano huo utaanza kesho asubuhi kwa semina ya Neno la Mungu itakayofanyika kuanzia saa 1:00 asubuhi katika kanisa la Shalom Temple na  baada ya semina hiyo, shughuli za mkutano wa injili zitaendelea katika Uwanja wa Magufuli uliopo eneo la Majengo, Manispaa ya Kahama.

“Nawakaribisha watu wa dini zote na rika zote kushiriki nasi katika mkutano huu wa kiroho, Tuanze na semina ya Neno la Mungu saa 1:00 asubuhi katika kanisa la Shalom Temple, kisha tuhamie katika viwanja vya Magufuli kuendelea na mkutano wa injili,” amesema Mwenyekiti huyo.

Mkutano huo unatarajiwa kuwaleta pamoja maelfu ya wakazi wa Kahama na wageni kutoka maeneo mbalimbali, kwa ajili ya kushiriki ibada, maombi, na mafundisho ya Neno la Mungu.


Mwisho.
Share:

Tuesday, 27 May 2025

ALIYENIFUKUZA KISA NILIKATAA KULALA NAYE, AKUMBWA NA MAZITO!


Naitwa Judithi kutokea Mwanza, miezi sita iliyopita, nilianza safari ya mabadiliko maishani kwa kuhama kutoka kwenye kazi yangu ya zamani na kwenda nyingine ambayo nilikuwa na matumaini makubwa nayo.

Uamuzi huu ulitokana na hamu ya kupata changamoto mpya ili kuwa na ukuaji katika kazi yangu katika maeneno mbalimbali hasa upande wa kiuchumi.

Licha ya kuwa mdogo, kupata nafasi kama mfanyakazi wa kitengo cha mawasiliano katika hoteli ya kifahari ya nyota tano, ilikuwa hatua kubwa kwangu hasa upande wa kupata uhuru wa kifedha.

Hata hivyo, msisimko wangu wa awali ulibadilika na kuwa mfadhaiko nilipojikuta nikikabiliana na mambo yasiyokubalika kutoka kwa Meneja wa hoteli ili ambayo nilikuwa naifanyia kazi.

Wiki mbili tu baada ya majukumu yangu mapya, Meneja alianza kutembelea ofisi yangu mara kwa mara kwa madai ya mazungumzo ya kawaida ambayo yanalenga kuboresha kazi lakini akavuka mstari kwa kunigusa sehemu ambayo sio sawa.

Nikiwa nimeshtuka na kuchukizwa, nilikataa kitendo chake kwa ajili ya usalama wa kazi. Hata hivyo, kukataa kwangu kulinigharimu maana alipanga mipango ya kulipiza kisasi.

Meneja alibuni mashtaka ya uongo na kushawishi nifukuzwe kazi. Licha ya juhudi na majaribio yangu ya kujitetea, nilijikuta nimefukuzwa kazi kwa madai ya matumizi mabaya ya ofisi.

Nikiwa nimekata tamaa, nilimweleza rafiki yangu mkasa huo, mara moja alinielekeza kwa Kiwanga Doctors, wataalamu wa tiba asilia ambao wamesaidia watu wengi ukanda wa Afrika Mashariki.

Kutokana sikuwa na chochote cha kupoteza, nilifika kwa Kiwanga Doctors ili kupata suluhisho la shida yangu. Kupitia uganga na uchawi wao, walifanya mambo ambayo yalimtesa Meneja hadi akakubali kosa lake na kuomba nirudishwe kazini.

Kama walivyosema, ndani ya saa 24, Meneja huyo alisalimu amri kutokana na kusumbuliwa na misukosuko isiyoelezeka na magonjwa katika familia yake.

Hivyo basi niliweka masharti ya maridhiano ili aweze kuondokana na shida hizo, moja ya masharti ni pamoja na kujiuzulu, jambo ambalo alitekeleza kwa muda muafaka na punde tu niliweza kurejeshwa kazi tena katika nafasi yangu ile ile ya mwanzo.

Ni watu wengi hadi sasa wamepata mafanikio, uponyaji na furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +255 763 926 750 au tembelea tovuti yao, maelezo zaidi kuhusu huduma zao ambazo zimewasaidia wengi.
Share:

SERIKALI YAMWAGA MILIONI 815 KUBORESHA HUDUMA YA MAJI KWA VIJIJI VINNE MTWARA



Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Mkoani Mtwara Mhandisi Hamis Mashindike aliyeshika fimbo,akimuonyesha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi miundombinu ya mradi wa maji Dihimba uliofanyiwa ukarabati mkubwa ili kuboresha hduma ya majisafi na salama kwa Wananchi wa Vijiji vinne vya Dihimba,Mpondomo, Kinyamu na Ndumbwe.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi,akiangalia kisima cha maji katika kilichofanyiwa ukarabati mkubwa kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji kwa Wananchi wa Vijiji vya Ndumbwe,Dihimba,Mpondomo na Kinyamu Wilayani Mtwara,kushoto Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mtwara Hamis Mashindike na kulia Mkuu wa Wilaya
Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mtwara Hamis Mashindike aliyeshika fimbo akitoa maelekezo kwa kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Ismail Ali Ussi wakati alipokwenda kukagua kisima cha maji kilichokarabatiwa na kuboreshwa kwaajili ya huduma ya wananchi wa vijiji vinne wilayani humo


Na Regina Ndumbaro-Mtwara 

Serikali kupitia Wizara ya Maji imetoa Shilingi 815,453,185 kwa ajili ya kukarabati Mradi wa Maji wa Dihimba unaohudumia wakazi zaidi ya 7,489 katika vijiji vya Dihimba, Mpondomo, Kinyamu na Ndumbwe, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara. 

Mradi huu ni hatua muhimu katika kuboresha huduma ya majisafi na salama kwa wananchi waliokuwa wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji kwa muda mrefu.

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mtwara, Mhandisi Hamis Mashindike, amesema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi 694,271,895 zilitumika kumlipa mkandarasi na Shilingi 121,181,200 zilinunulia mabomba kupitia RUWASA Makao Makuu. 

Ukarabati huo ulianza Januari 2024 na unatarajiwa kukamilika Juni 2025 baada ya kuchelewa kutokana na changamoto kama mvua nyingi na ucheleweshaji wa malipo. 

Mradi huu unatekelezwa na wakandarasi M/S Zonghi Plumbing & General Supplies na M/S Seba Construction, ambapo hadi sasa umekamilika kwa asilimia 75.

Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa tenki la lita 100,000 katika kijiji cha Mpondomo, ukarabati wa matenki mawili ya lita 200,000 katika Ndumbwe, ujenzi wa vituo 17 vya kuchotea maji, nyumba ya muhudumu, ofisi ya Jumuiya ya Watumia Maji (CBWSO), pamoja na ulazaji wa bomba wa zaidi ya kilometa 24. 

Utekelezaji wa mradi umeongeza upatikanaji wa huduma ya maji kutoka asilimia 37.04 hadi 93.47 kwa mwaka 2025.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ismail Ali Ussi, alipata fursa ya kutembelea na kukagua miundombinu ya mradi huo huku akielezwa mafanikio yaliyopatikana. 

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Patrick Sawala, ameeleza kuwa mradi huo ulioanzishwa mwaka 1989 haujawahi kufanyiwa ukarabati mkubwa na sasa umeleta ahueni kubwa kwa wananchi, ambao awali walilazimika kutembea umbali mrefu kufuata maji.

Mwananchi wa Kijiji cha Dihimba, Mwanahawa Rashid, ameeleza kuwa kabla ya ukarabati huo walilazimika kutembea hadi vijiji vya jirani kwa ajili ya maji.

 Ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kusikiliza kilio cha wananchi na RUWASA kwa usimamizi mzuri wa mradi huo ambao sasa umewapunguzia adha kubwa ya upatikanaji wa maji safi na salama.
Share:

TAKUKURU YADHIBITI UBADHIRIFU WA MILIONI 92 ZA WAKULIMA WA TUMBAKU USHETU, SHINYANGA

 

Na Kadama Malunde – Malunde 1 Blog

 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga imefanikiwa kudhibiti ubadhirifu wa kiasi cha shilingi milioni 92.16 zilizotengwa kwa ajili ya kuwafidia wakulima wa tumbaku wa Chama cha Msingi cha Ushirika (AMCOS) Ibambala, kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Ushetu mkoani humo.

Taarifa hiyo imetolewa leo Mei 27, 2025 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Shinyanga.

Kwa mujibu wa Kessy, fedha hizo zilitolewa kwa wakulima waliopata hasara kutokana na mafuriko yaliyoathiri uzalishaji wa tumbaku katika msimu wa kilimo wa mwaka 2023/2024, lakini hazikufika kwa walengwa kama ilivyokusudiwa.

“TAKUKURU ilibaini kuwa shilingi milioni 11.62 zilichukuliwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho kwa matumizi yao binafsi, akiwemo Katibu Meneja Bw. Charles Alex Shiyengo na Mwenyekiti Bi. Faida Paulo Deda,” amesema Kessy.

Aidha, TAKUKURU imebaini kuwa kiasi kikubwa cha fedha—shilingi milioni 151.53—kiligawiwa kwa watu wasiostahili, wakiwemo ndugu wa viongozi hao. Miongoni mwa waliopokea fedha hizo ni Bi. Lucy Masanja Dglibata, mke wa Katibu Meneja, ambaye alipokea shilingi milioni 34.58, pamoja na Bw. Charles Charles Masanja aliyelipwa shilingi milioni 5.58.

Hatua za awali za kurejesha fedha hizo zimeanza kuchukuliwa huku wahusika wakikabiliwa na hatua za kisheria.

Katika kipindi cha Januari hadi Machi 2025, TAKUKURU Shinyanga pia imepokea jumla ya taarifa 57 za tuhuma za rushwa, ambapo 52 zilifanyiwa uchunguzi na 13 kati yake zimefikishwa mahakamani.

Kwa upande wa elimu kwa umma, taasisi hiyo imeendesha mikutano ya hadhara 61, semina 30, na vipindi vya redio na runinga 13 kupitia programu yao ya Takukuru Rafiki, lengo likiwa ni kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa.

Kessy amewahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na TAKUKURU kwa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa njia ya simu ya bure 113 au kupitia tovuti yao ya www.pccb.go.tz.


Share:

Monday, 26 May 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 27,2025





Share:

SERIKALI ,WANAZUONI KUJADILI PPP, UCHUMI NA DIRA 2050

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia (PPPC), David Kafulila, na Mwenyekiti wa REDET, Prof. Rwekaza Mukandala.

Mei 26, 2025

Na Mwandishi Wetu _ Dar es Salaam

Serikali inatarajiwa kukabiliana na hoja za wanazuoni na sekta binafsi kesho kuhusu dhana ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP), mwenendo wa uchumi chini ya Awamu ya 6 na mwelekeo wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia (PPPC) David Kafulila, mjadala huo wa wazi utafanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Kituo cha PPPC kitafanya kongamano kwa kushirikiana na Taasisi ya Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia (REDET)  ambayo iko chini ya UDSM.

Mada kuu ya kongamano ni: Dola, Masoko na Uhamasishaji wa Mitaji: Nafasi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi Kufikia Malengo ya Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050.

Kafulila atafanya wasilisho kuhusu Dhana ya PPP na Nafasi yake Kuelekea Dira ya Taifa 2050 na Mwenyekiti wa REDET, Prof. Rwekaza Mukandala, ataongoza kongamano kama moderator.

Kongamano litafanyika katika Ukumbi wa Maktaba Mpya, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumanne tarehe 27 Mei 2025 kuanzia saa 3:00 asubuhi mpaka saa 6:00 mchana.

Maafisa waandamizi wa serikali, wakuu wa makampuni ya sekta binafsi, wanazuoni na wawakilishi wa kada nyingine mbalimbali wanatarajiwa kushiriki kwenye mjadala wa wazi utakaorushwa mubashara na vituo kadhaa vya televisheni.

"Wananchi wote wanakaribishwa kuhudhuria kongamano hili la wazi ili waweze kushiriki kwenye mjadala kuhusu dhana ya PPP na nafasi yake kwenye kutekeleza Dira ya Taifa 2050," Kafulila amesema.

"Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP) una nafasi kubwa kwenye mwelekeo mpya wa uchumi na maendeleo ya Tanzania."

Kituo cha PPPC kinasimamia jumla ya miradi 84 ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi ambayo iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Miradi hiyo ipo kwenye sekta za usafirishaji, nishati, miundombinu na maeneo mengine.

Baadhi ya miradi hiyo ni Barabara ya waendao haraka (Express way) ya Kibaha–Chalinze -Morogoro (205km), na ile ya Isongole-Tunduma (210km) ambazo zikijengwa njia nne za barabara (epxress way), zinaweza kugharimu karibu dola za Marekani Bilioni 1.6.

Mradi wa barabara kwa ajili ya kupunguza foleni katikati ya Jiji la Dar es Salaam (Outer ring roads) nao ni miongoni mwa miradi ya kutekelezwa kwa ubia wa PPP.

Share:

MWENGE WA UHURU WAZINDUA VISIMA TANDAHIMBA, WANANCHI WAPATA MAJI YA BOMBA KWA MARA YA KWANZA TANGU UHURU

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi,akikagua miundombinu ya mradi wa Kisima cha maji katika Kijiji cha Mivanga Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara kabla ya kuzindua mradi huo.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi,akizindua mradi wa Kisima cha Maji katika Kijiji cha Mivanga Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara,kulia Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Mtwara Mhandisi Primy Damasi

Meneja wa RUWASA Wilaya ya Tandahimba Mkoani Mtwara Falaura Kikusa,akimuonyesha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2025 Ismail Ali Ussi ,mchoro wa mradi wa Kisima cha maji uliotekelezwa katika Kijiji cha Mivanga.

Na Regina Ndumbaro-Tandahimba 

Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 umeweka historia katika Kijiji cha Mivanga, Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara baada ya kuzindua mradi wa uchimbaji wa visima vya maji, hatua iliyowapatia wakazi wa kijiji hicho huduma ya maji ya bomba kwa mara ya kwanza tangu Tanzania ipate Uhuru. 

Uzinduzi huo umefanywa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussi, ambaye alikagua na kuzindua rasmi kisima hicho akiwa ameongozana na viongozi wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA).

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Tandahimba, Falaura Kikusa, amesema jumla ya Shilingi 452,500,000 zimetengwa kwa ajili ya kuchimba visima vitano katika vijiji vya Mivanga, Lyenje, Dinduma, Mchangani na Michenjele. 

Mradi huo ni sehemu ya programu ya uchimbaji wa visima 900 kote nchini, unaotekelezwa kwa kutumia wataalam wa ndani (force account), kwa kipindi cha miezi sita tangu Mei 2024, na unatarajiwa kukamilika Juni 2025 baada ya kuchelewa kutokana na changamoto mbalimbali.

Kwa mujibu wa Kikusa, hadi sasa ujenzi wa miundombinu ya maji na usimikaji wa matanki ya kuhifadhi maji yenye ujazo wa lita 10,000 umekamilika katika vijiji viwili, huku usimikaji wa pampu na mfumo wa nishati ya jua ukifanyika katika vijiji vinne. 

Kisima cha Mivanga pekee kinazalisha lita 372,000 za maji kwa siku. 

Fedha za utekelezaji zinatokana na program ya Lipa kwa Matokeo, Mfuko wa Taifa wa Maji pamoja na michango ya wadau mbalimbali wa maendeleo.

Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, Katani Ahmed, ameishukuru serikali kwa kutatua tatizo la muda mrefu la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, akisema kuwa mradi huo umepunguza changamoto kubwa iliyokuwa ikikwamisha shughuli za maendeleo vijijini. 

Kwa upande wake, Ismail Ali Ussi amewataka wananchi kushirikiana na serikali kulinda miundombinu ya miradi hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuleta tija kwa jamii.

Asha Seleman, mkazi wa Kijiji cha Mivanga, amesema kabla ya mradi huo walilazimika kununua ndoo moja ya maji kwa Shilingi 1,000, jambo ambalo liliongeza gharama za maisha. 

Amesema sasa wameondokana na adha hiyo, na wana matumaini makubwa kuwa huduma hiyo itaboresha maisha yao kiuchumi na kiafya.

Share:

MAPEPELE AWANOA MAAFISA HABARI WA TAMISEMI, AWATAKA WAWE WAZALENDO


Na Mwandishi Wetu, OR- TAMISEMI

Mkuu wa Kitengo Cha Mawasilino Serikali na Msemaji Mkuu wa Wizara ya TAMISEMI, John Mapepele ametoa wito kwa Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri zote nchini kutanguliza uzalendo na weledi wakati wa utoaji wa taarifa ili habari hizo ziwe na tija kwa taifa.

Mapepele ametoa wito huo mwisho wa juma wakati akiwasilisha maada kuhusu Mawasilino ya Kimkakati ya Kutangaza Nafanikio ya Sekta za Afya, Elimu na Miundombinu chini ya TAMISEMI kwa Maafisa Habari zaidi ya 200 wa Mikoa na Halmashauri zote nchini jijini Dodoma kwenye kikao kazi cha siku mbili kwa MaafisaHabari hao kilichoratibiwa na Wizara hiyo.
Kikao kazi hicho kilichofunguliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.Mohamed Omary Mchengerwa na kufungwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa kimejadili pamoja na mambo mengine, mikakati mbalimbali ya kutangaza mafanikio ya Serikali, pia kuwajengea uwezo Maafisa Habari hao kwa mada mbalimbali za kitaaluma hususan matumuzi ya mifumo ya kidigitali kwenye utoaji wa taarifa na kuja na maazimio kadhaa ya kuboresha utendaji kazi.

Aidha, Mapepele amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa katika mikoa na Halmashauri zote nchini ambayo haijatangazwa ipasavyo na Maafisa Habari katika maeneo hayo na kuwataka kuwa wabunifu wa kutoa taarifa hizo

"Ndugu zangu Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanya mapinduzi makubwa kwenye sekta ya miundombinu ambapo tumeshuhudia mabarabara, madaraja, vituo vya mabasi na masoko yakitengenezwa kila uchao, ukiachia mbali madarasa, zahanati, vituo vya afya na vifaa tiba kwenye kila kona hivyo ni wajibu wetu sisi Maafisa Habari wa Halmashauri na Mikoa kuwa wazalendo na kuisemea Serikali yetu ili wananchi waweze kujua na kutumia huduma hizi kikamilifu". Amefafanua Mapepele

Akifungua kikao kazi hicho Mhe. Mchengerwa amewataka Maafisa Habari wote wa TAMISEMI kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi kwa wakati za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo yao ya kazi. 

"Mmebeba dhamana kubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi hivyo msiache watanzania walishwe habari potofu". Amesisitiza Mhe. waziri Mchengerwa

Akifunga kikao kazi hicho, Katibu Mkuu Msigwa ameipongeza Wizara ya TAMISEMI kwa kuratibu kikao kazi hiki ambapo ameshauri kiwe kinafanyika kila mwaka ili kufanya tathmini wa utendaji wa kazi na kujadiliana masuala mbalimbali ya utendaji wa kazi wa kundi hili kubwa la Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri nchini katika kutoa taarifa za miradi ya maendeleo.



Share:

Sunday, 25 May 2025

TAASISI YA UDOPRESA YAZINDULIWA UDOM




Kamati ya Uzinduzi wa UDOPRESA ikikabidhi zawadi ya Picha kwa Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph katika Hafla ya Uzinduzi wa Taasisi hiyo.

.......

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu cha Dodoma, Bi. Rose Joseph katika Ukumbi wa LT2 (CHSS) UDOM amefanya Uzinduzi wa Taasisi ya Wanafunzi wanaosomea Uandishi wa Habari na Uhusiano wa Umma Chuo Kikuu cha Dodoma - The University of Dodoma Public Relations Students Association (UDOPRESA) yenye jumla ya wanachama 250.

Taasisi hiyo imeanzishwa kwa dhamira kuu ya kuwaunganisha wanafunzi wanaosoma Taaluma ya Uhusiano na Umma na Uandishi wa Habari wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Kuimarisha Taaluma, Kushirikiana katika Tafiti na Mafunzo na kuwa chachu ya Maendeleo ya Taaluma hiyo Nchini.

Akizungumza wakati wa Hafla ya Uzinduzi; Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Chuo Kikuu cha Dodoma Bi. Rose Joseph ameahidi kuwapa ushirikiano wowote watakaohitaji huku akiwaasa kutumia Taasisi hiyo katika kulinda taswira ya Chuo na kuwataka watangulize uzalendo kwa Taifa mbele, kulinda na kuheshimu fani hiyo; pamoja na kuzingatia Sheria, Taratibu na Miongozo yote ya maafisa Uhusiano na Habari.

"Hili ni Jukwaa muhimu sana ambalo si tu kwamba linawaleta pamoja wanafunzi wanaosomea Uhusiano wa Umma UDOM, lakini naamini ni jukwaa zuri la kuwanoa, kuwaweka tayari kwa ajili ya kwenda kulitumikia Taifa, kutetea Tasnia na kwenda kuwa waandishi bora na maafisa bora wa umma" Aliongeza Bi. Rose.

Kwa Upande wake; Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari, Dkt. Deograsia Ndunguru amewapongeza Wanachama wote wa UDOPRESA huku akisisitiza kuwa Taasisi hiyo itawasaidia kuongeza ujuzi, Maarifa hasa katika kuwajenga kuwa maafisa Uhusiano Bora wa baadae.

Naye; Mlezi wa Taasisi hiyo Dkt. Mary Kafyome, amesema ulikuwa ni mchakato mkubwa kufanikisha jambo hilo huku akitoa pongezi kwa wote walihusika kufanikisha tukio hilo na ametoa wito kwa wanafunzi wanaobaki kuendeleza taasisi hiyo.

"UHUSIANO BORA, JAMII BORA!"
Mgeni Rasmi kwenye Hafla ya uzinduzi wa chama cha UDOPRESA, Bi. Rose Joseph akihutubia wakati wa uzinduzi.
Mlezi wa Taasisi ya UDOPRESA Dkt. Mary Kafyome akitoa neno la Shukurani wakati wa Uzinduzi wa Hafla ya UDOPRESA
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Masoko Chuo kikuu cha Dodoma Bi. Rose Joseph akikata keki kama ishara ya Uzinduzi wa Taasisi ya UDOPRESA kutoka kulia kwake ni Mkuu wa Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari Dkt. Deograsia Ndunguru, akifuatiwa na Mlezi wa UDOPRESA Dkt. Mary Kafyome na Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa UDOPRESA Bw. Swerd Mwakage akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Huduma za Wanafunzi UDOM Bw. Gabriel Elia.
Mkuu wa Idara ya Sanaa na Taaluma za Habari Chuo Kikuu cha Dodoma Dkt. Deograsia Ndunguru akitoa neno wakati kwa Washiriki wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Wanachama wa UDOPRESA wakiwa katika hali ya furaha wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph akikabidhi Cheti cha Uongozi Bora kwa Mwenyekiti wa UDOPRESA Bw.Swerd Mwakage wakati wa Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Kamati ya Uzinduzi wa UDOPRESA ikikabidhi zawadi ya Picha kwa Mgeni Rasmi Bi. Rose Joseph katika Hafla ya Uzinduzi wa Taasisi hiyo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger