Sunday, 1 March 2026

PROF. JANABI AZINDUA WODI YA WATOTO NJITI HOSPITALI YA WILAYA YA KWIMBA, MWANZA

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Prof. Mohamed Janabi amezindua wodi ya kwanza na ya kisasa nchini kwa ajili ya watoto njiti, iliyojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Prof. Janabi amefanya uzinduzi huo jumamosi Februari 28, 2028 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus ambapo ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 2.125 ikijumuisha jengo, vifaa tiba na mbili nyumba za watumishi.

Prof. Janabi ametumia fursa hiyo kuipongeza taasisi ya Doris Mollel (Doris Mollel Foundation- DMF) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Keep a Child Alive (KCA) na Shirika la JHPIEGO  kwa kufanikisha mradi huo utakaosaidia kuzuia vifo vya wazazi na watoto hasa wanaozaliwa kabla ya wakati ama chini ya uzito.

"Kila mwaka Kanda ya Afrika inapoteza watoto milioni hivyo WHO tutaendelea kuunga mkono jitihada hizi ili kuhakikisha hakuna mtoto ama mzazi anapoteza maisha" amesema Prof. Janabi huku pia akiipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada inazoendelea kuchukua kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuboresha huduma za afya.

Mkurugenzi wa DMF, Doris Mollel amesema wazo la ujenzi wa wodi hiyo lilianza mwaka 2021 taasisi hiyo ilipoenesha kampeni ya kuchangia vifaa tiba kwa ajili ya wodi za watoto njiti nchini ambapo Wilaya ya Kwimba ilibainika kuwa kwenye uhitaji wa wodi na hivyo kuanza mchangato wa kutafuta fedha zilizofanikisha kukamilisha mradi huo.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la JHPIEGO Tanzania, Alice Christensen amesema kukamilika kwa wodi hiyo kutatoa mfano kote nchini namna wodi za watoto njiti zinavyopaswa kuwa hatua itakayosaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua ambapo shirika hilo limechangia zaidi ya shilingi milioni 200 kwenye utekelezaji wa mradi huo.

Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa Kwimba akiwemo Modesta Malashi, Vumilia Ally na Mariam Lucas wamesema wodi hiyo itawaondolea adha ya kubanana kwenye wodi ya pamoja iliyokuwepo awali hospitalini hapo huku pia wakilazimika kusafiri umbali mrefu hadi Bugando inapotokea changamoto ya kujifungua.
Na George Binagi, Mwanza
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (wa tano) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati (watoto njiti) katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (mwenye kofia) akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (mwenye kofia) akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Viongozi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza ambayo imegharibu shilingi bilioni 2.125 ikijumuisha jengo, vifaa na nyumba za watumishi. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus kwenye hafla ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Naibu Waziri wa Afya, Florence Samizi akizungumza uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Elikana Balandya akizungumza kwenye hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda.
Mkurugenzi Shirika la JHPIEGO Tanzania, Alice Christensen akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation (DMF), Doris Mollel akizungumza kuhusu ujenzi wa wodi ya watoto njiti katika hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza na kutoa shukurani kwa wadau wote ikiwemo Shirika la JHPIEGO kwa kusaidia ujenzi wa wodi hiyo.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika- Prof. Mohamed Janabi, Viongozi wa Serikali na wadau wa maendeleo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Viongozi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akimpongeza mmoja wa akina mama katika wodi mpya ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Baadhi ya wazazi katika wodi ya watoto njiti iliyopo Hospitali ya Wilaya Kwimba mkoani Mwanza wakifurahia mazungumzo na viongozi wakati wa uzinduzi wa wodi hiyo.
Mwonekano wa miongoni mwa nyumba za watumishi zilizojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Kikundi cha Sungusungu Wilaya ya Kwimba kikitoa burudani ya asili wakati wa uzinduzi wa wodi ya watoto njiti iliyojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MACHI MOSI 2026


Magazeti
 
Share:

SHIRECU YAANDIKA HISTORIA MPYA YA USHIRIKA, MKUTANO MKUU WAPITISHA BAJETI ZAIDI YA SH BILIONI 2.8

 

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU

Meneja  wa Chama cha Ushirika SHIRECU Alphonce Makasi  akisoma  rasimu  ya  bajeti  kwenye mkutano Mkuu wa 31 

                   Chama Kikuu Cha Ushirika Mkoani Shinyanga (SHIRECU)  kimepitisha rasimu ya  bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 2.8  kwa mwaka wa fedha 2026/2027 huku ikijizatiti kuanza  kukopesheka  kwenye taasisi za kifedha.

Bajeti hiyo limepitishwa leo  April 28, 2026   baada ya Meneja  wa chama cha ushirika Shirecu Alphonce Makasi  kuwasomea  taarifa na rasimu  ya  bajeti  kwenye mkutano Mkuu wa 31  uliowakutanisha  wajumbe  202 kati ya wajumbe 214  waliokuwa wakitakiwa kuhudhuria kwenye mkutano huo.

Akisoma taarifa hiyo Meneja Makasi amesema wajumbe wakiridhia kupitishwa kwa bajeti zaidi ya shilingi bilioni 2.8  na kukopa kwenye taasisi za kifedha wataweza kutimiza adhima ya mipango ya kuendeleza biashara ya ununuzi wa mazao.

Pia mazao hayo yatakuwa Mchanganyiko,uanzishwaji na kufufua kiwanda kipya cha kukamua mafuta ya alizeti na kuendeleza duka la pembejeo.

“Awali taasisi za kifedha zilikataa kabisa kutukopesha kutokana na kuwepo kwa vikwazo vya deni kutoka benki ya Uwekezaji ya (TIB) lakini sasa tumeanza kuonyesha uaminifu wa kulipa na kupata ruhusa ya kuendelea kukopesheka kwenye taasisi za kifedha zozote nchini”amesema Makasi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Shirecu Naomi Chaba amesema  kuna vyama vya ushirika (Amco’s) 107 na wanachama 7413, ambapo mpango ulioanza mwaka 2025 hadi  Februari  2026  wamefanikiwa kununua mazao Mchanganyiko kama choroko na dengu,kugawa kompyuta mpakato 50 nakutoa mafunzo

"Pia ,tumefanikiwa kukarabati shule ya sekondari Buluba  na kusomesha wanafunzi 28  wa kidato cha tano kwa awamu,  kwa gharama ya shilingi Milioni 45."    pia  Chama kinatarajia kujenga kiwanda cha dengu kufanya biashara ya pamba ukarabati wa magala ,  amesema Chaba

Naye  Mrajis msaidizi  wa Ushirika mkoa wa Shinyanga Ibrahim  Kakozi amesema taasisi za kifedha   sasa zikae sawa kuwakopesha shirecu  huku akiwataka wajumbe waeleze yale ambayo wanataka yatekelezwe na yakikwama waihoji bodi  nakutoa ushauri zaidi nini kifanyike ili kuboresha zaidi.

"Niombe kila Amcos iripoti kila tatizo lililopo ili chama kiweze kufuatilia na kujua tatizo nini, kwani mkileta kwa barua itakuwa ni rahisi kufuatiliwa kwa haraka zaidi"amesema Kakozi.

        Mwakilishi wa COASCO Rodrick Kilemile 
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Lucy Mayenga akizungumza kwenye mkutano wa SHIRECU

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU
Wajumbe wa mkutano wa SHIRECU

Mkutano unaendelea

Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU




Share:

Saturday, 28 February 2026

BARRICK YAPONGEZWA KWA KUWEKA MIUNDOMBINU YA KITUO CHA MICHEZO BUZWAGI

 
Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi akitoa maelezo kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake walipotembelea kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na ujumbe wake wakitembelea maeneo mbalimbali ya kituo cha michezo cha Buzwagi.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa shirikisho hilo Wallace Karia na Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi.

**


Mgodi wa Barrick Buzwagi ambao uko katika mchakato wa kufungwa kwa kushirikiana na Serikali umepongezwa kwa kuweka miundombinu ya kituo cha michezo ambacho kitasaidia kukuza mchezo wa soka na michezo mingineyo nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia, alipoongoza wajumbe wa Mkutano Mkuu wa taifa wa shirikisho hilo kutembelea eneo hilo ambapo amesema miundombinu iliyopo inaridhisha.

Amesema miundombinu hiyo kuanzia nyumba za malazi kwa wanamichezo, viwanja vya michezo, usalama, pamoja na mazingira yake kwa ujumla ipo katika hali nzuri na inakidhi mahitaji ya kuanzishwa kwa kituo hicho.

“Natoa shukrani kwa kampuni ya Barrick na Serikali kwa kukubali ombi la kuanzishwa kituo cha michezo katika eneo la mgodi uliofungwa, tunafurahi kuona kituo kiko katika hali nzuri na kina viwango vikubwa kwa ajili ya kuhudumia wanamichezo, hii ni fursa muhimu kwa maendeleo ya michezo yetu”, amesema.

Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Taifa ya TFF, Azan Mufti, amesema kutengwa kwa eneo hilo kwa ajili ya wanamichezo kunadhihirisha ushirikiano mzuri uliopo kati ya sekta binafsi na wadau wa sekta ya michezo katika kufanikisha ajenda ya Serikali ya kukuza vipaji na kuendeleza michezo nchini.

Naye Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastraal Mumbi, amesema kutengwa kwa eneo la kujengwa kituo cha michezo katika eneo hilo la mgodi uliofungwa kumezingatia dhamira ya kampuni ya kusaidia jamii sambamba na kuunga mkono jitihada za serikali za kukuza vipaji na kuchochea maendeleo ya michezo nchini.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger