Tuesday, 1 July 2025

MIRADI SABA YA BILIONI 2.4 YAZINDULIWA TANGA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO YA AJIRA KWA VIJANA NA WATOTO


Na Hadija Bagasha Tanga, 

Changamoto ya kukithiri kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ulawiti na ajira kwa vijana Mkoani Tanga inakwenda kupatiwa ufumbuzi baada ya ujio wa miradi mikubwa saba yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.4.

Shirika la Botner Foundation la Nchini Uswis limetoa zaidi ya shilingi bilioni 2.4 kwajili ya ufadhili wa miradi saba ikiwemo mradi wa kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana na mradi wa  malezi na makuzi ya watoto ukilenga kumaliza vitendo vya ulawiti kwenye kundi hilo

Akizunguza wakati wa uzinduzi wa miradi hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tanga Dadi Kolimba ametaka fedha zilizotolewa na wafadhili kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa kuwafikia walengwa. 

"Tunafanya uzinduzi wa miradi saba ambayo imakwenda kusaidia vijana na watoto kama mnavyofajamu nchi yetu kwa upande wa vijana kumekuwa na shida kubwa ya ajira soko la ajira katika nchi yetu ni changamoto na hivyo kupitia miradi hii ya Tanga yetu ambayo inapata ufadhili kutoka kwa Botnar foundation na wenzetu tumezindua leo miradi hii saba, "alisema Kolimba. 

"Miradi hii inakwenda kusaidia vijana katika upande wa miradi ya afya lakini pia na elimu na tumeona fedha zinazokwenda kutekeleza miradi hii  ni karibu bilioni 2.4 na sisi tutahakikisha kwamba tunasimamia vizuri miradi hii ili iweze kuwakomboa vijana katika jiji letu la Tanga waweze kujikwamua na kusimamia miradi yao na kuhakikisha wanaiendesha vizuri, "alisisitiza Kolimba. 

Mwenyekiti wa Kamati ya uendeshaji mradi wa Tanga Yetu Juma Rashid ametaka vijana kushiriki kwenye miradi hiyo ili iweze kuwanufaisha na kuleta mabadiliko kwenye maisha ya watoto na kulifanya jiji la Tanga kuwa mahali pazuri pa kuishi. 

"Awamu hii tuna miradi 7 na kati ya hii mitatu  ipo kwenye sekta ya afya na mmoja eneo la ujasiriamalli,  michezo ambayo sasa no ajira rasmi kwa vijana lakini linawaahughulisha vijana pamoja na watu wazima, "

"Eneo jingine ni la elimu , malezi na makuzi ya watoto ambapo miradi yote itakapotekelezwa vizuri na  kazi yetu kubwa kama kamati ya uendeshaji  ni kusimamia utekelezaji wa uendeshaji wa miradii hii iteekelezwevile imepangwa na itoe matokeo ambayo tunayafikiria yataleta mabadilikp katika maisha ya watoto na vijana, 

Kwa upande wake mratibu wa asasi ya kiraia ya Gift of hope Said Bandawe amesema mtadi huo utakuwa na manufaa makubwa kwa waraibu wa dawa za kulevya huku Mkurugenzi wa Taasisi ya Tayota George Bwire akisema mradi huo utasaidia kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vimekuwa vikiongezeka mara kwa mara. 

Miradi hiyo ambayo inalenga maeneo mbalimbali ikiwemo afya,  ujasiriamali,  michezo,  elimu na makuzi ya watoto ikotekelezwa ipasavyo inatarajiwa kuwa na matokeo chanya katika jiji la Tanga. 
Share:

BALOZI CHANA AONGOZA UVISHAJI VYEO NCAA, ATAKA UADILIFU NA WELEDI








Na Woinde Shizza , Arusha

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Dk. Pindi Chana, amewavisha vyeo Manaibu Kamishna wawili wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) huku pia akishuhudia zoezi la uvishaji wa vyeo kwa Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Uhifadhi watano, waliovishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NCAA, Jenerali mstaafu Venance Mabeyo.

Waliopewa vyeo na Waziri Chana ni Joas John Makwati, aliyepandishwa kutoka Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi na kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Uhifadhi, Utalii na Maendeleo ya Jamii, pamoja na Aidan Paul Makalla, aliyepandishwa kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Shirika NCAA.

Kwa upande mwingine, makamishna waliovishwa vyeo na Jenerali Mabeyo ni Gasper Stanley Lyimo (Mipango na Uwekezaji), Paul Geofrey Shaidi (Huduma za Sheria), Charles Marwa Wangwe (Idara ya Uhasibu na Fedha), Godwin Felician Kashaga (Ukaguzi wa Ndani) pamoja na Mariam Kobelo, aliyepandishwa kutoka Afisa Uhifadhi Mkuu Daraja la Kwanza na kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia Huduma za Utalii na Masoko.

Akizungumza baada ya hafla hiyo, Balozi Dk. Chana aliwataka maafisa hao waliopandishwa vyeo kuwajibika kwa bidii na kuonyesha uadilifu katika utendaji wao, akisisitiza kuwa cheo ni dhamana inayokuja na wajibu mkubwa.

“Nina imani kuwa viongozi mliovishwa vyeo leo mtakuwa chachu ya utendaji bora, mtatoa mfano kwa maafisa na askari mnaowaongoza. Juhudi zenu zitachangia kwa kiasi kikubwa kuhifadhi na kulinda eneo la Ngorongoro pamoja na kulitangaza kama kivutio cha utalii,” alisema Dk. Chana.

Naye Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA, Abdul-Razak Badru, alisema watumishi wote wa mamlaka hiyo wamekamilisha mafunzo ya kijeshi, hatua iliyochukuliwa kutoka mfumo wa awali wa kiraia, na kwamba sasa rasilimali watu iliyopo itatumika kwa ufanisi zaidi kulinda rasilimali za taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya NCAA, Jenerali mstaafu Mabeyo, aliwataka viongozi hao kutumia nafasi walizopewa kwa uadilifu mkubwa, akisisitiza kuwa mafanikio ya hifadhi hiyo yanatokana na uwajibikaji wa viongozi wake.
“Natumaini kuwa viongozi waliovishwa vyeo watabeba matumaini mapya ya kuboresha sekta ya uhifadhi, utalii na maendeleo ya jamii. Nawapongeza pia wadau wote waliounga mkono juhudi za kuendeleza Ngorongoro hadi kutangazwa kuwa Kivutio Bora cha Utalii Barani Afrika kwa mwaka 2025,” alisema Mabeyo.
Share:

Monday, 30 June 2025

VIONGOZI WA DINI NA TGNP WAJIPANGA KUKUZA USAWA WA KIJINSIA KONDOA NA CHEMBA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Katika harakati za kuendeleza juhudi za kuleta usawa wa kijinsia na kuondoa vikwazo vinavyowakwamisha wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Aga Khan Foundation (AKF) umeandaa kikao kazi muhimu na viongozi wa dini kutoka BAKWATA Mkoa wa Dodoma.

Kikao kazi hicho, kilichofanyika katika ofisi za BAKWATA Mkoa wa Dodoma, kiliwakutanisha wadau mbalimbali wa mradi wa TUINUKE PAMOJA, wakiwemo Meneja wa Mradi Mkoa wa Dodoma, Nestory Muhando, Mtaalam wa Jinsia kutoka AKF, Bi. Zainab Mmary, na Mwezeshaji wa Mradi, Deogratius Temba, pamoja na Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaban, Katibu wa BAKWATA Mkoa, Sheikh Husein Kazungu, na Sheikh wa Wilaya ya Kondoa, Sheikh Hamis Nchao.

Mradi wa TUINUKE PAMOJA, unaotekelezwa na TGNP kwa ushirikiano na Aga Khan Foundation, unalenga kukuza usawa wa kijinsia na kuondoa vikwazo vya kijamii na kiutamaduni vinavyowakwamisha wanawake kushiriki kikamilifu katika nafasi za uongozi na maendeleo, kwa njia inayoheshimu misingi ya jamii na mafundisho ya dini.

Akizungumza katika kikao hicho, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaban, alisisitiza umuhimu wa kushirikiana kwa pamoja katika kujenga jamii yenye misingi ya haki, heshima, na ushirikiano:

"Dini inafundisha haki, usawa na heshima kwa binadamu wote. BAKWATA tumejipanga kushirikiana na wadau kuhakikisha elimu ya haki za binadamu na madhara ya ukatili wa kijinsia inawafikia waumini wetu, ili jamii ijitokeze kwa wingi kushiriki kwenye shughuli za maendeleo bila ubaguzi," alisema.

Kwa upande wake, Bi. Zainab Mmary kutoka AKF, alibainisha kuwa viongozi wa dini ni nyenzo muhimu ya kufanikisha mabadiliko ya kijamii:

"Tunahitaji viongozi wa dini kuwa mabalozi wa mabadiliko ya mtazamo kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii. Tunajenga jamii inayotambua na kuthamini mchango wa wanawake katika maendeleo ya familia na taifa."

Nestory Muhando, Meneja wa Mradi wa TUINUKE PMOJA Mkoa, alieleza kuwa ushirikiano kati ya taasisi za dini na mashirika ya maendeleo ni muhimu kwa uendelevu wa matokeo ya mradi:
"Mradi wa TUINUKE PAMOJA unahitaji umiliki wa jamii nzima. Kwa kushirikiana na taasisi za dini, tunajenga msingi wa mabadiliko ya kweli kwa jamii ya Kondoa na Chemba."

Akichangia mjadala, Deogratius Temba, Mwezeshaji wa Mradi, alifafanua kuwa dhana ya usawa wa kijinsia inayoelezwa katika mradi huu haipingani na mila, desturi au mafundisho ya dini, bali inajikita katika misingi ya heshima, utu, maadili na haki kama inavyofundishwa na dini zote:

"Usawa wa kijinsia tunaouzungumzia hauwalengi wananchi kwenda kinyume na misingi ya imani au mafundisho ya dini zao. Badala yake, tunahamasisha jamii kuishi kwa heshima, kulinda utu na haki za kila mmoja – jambo ambalo pia ni agizo la Mwenyezi Mungu kwa wanadamu wote," alisema Temba.

Kikao hiki kimejikita kuimarisha mshikamano wa kiimani na kijamii katika utekelezaji wa mradi wa TUINUKE PAMOJA, huku kikilenga kujenga jamii jumuishi, yenye amani, haki na maendeleo endelevu kwa wote. Mradi huu unatekelezwa katika wilaya za Kondoa na Chemba, ukihusisha wanajamii, viongozi wa dini, na serikali za mitaa kwa pamoja ili kufanikisha mabadiliko ya kijamii kwa kuzingatia usawa wa kijinsia na haki za binadamu.

Share:

NGATALE ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE SHINYANGA MJINI



Na Mwandishi wetu Malunde 1 Blog.

Aliyekuwa Mkurugenzi Msaidizi idara ya sheria katika ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mzalendo harisi Mwanashinyanga Ndugu. Eustad Ngatale ameonyesha dhamira yake ya kuwania nafasi ya Ubunge katika jimbo la Shinyanga Mjini kwa kuchukua fomu katika ofisi za Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.

Ngatale amechukua fomu mapema leo Juni 30, 2025 katika ofisi za CCM Shinyanga Mjini na kukabidhiwa na katibu wa CCM Bi. Hamisa Chacha.


Share:

FADHILI SALMON NAFUTARI ACHUKUA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA ITWANGI, SHINYANGA VIJIJINI

 

Fadhili Salmon Nafutari, Mtanzania mzalendo na kijana mwenye maono ya kweli ya maendeleo, ametangaza rasmi nia yake ya kugombea nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Itwangi, Wilaya ya Shinyanga. akiwa na msukumo wa kulijenga jimbo hilo kupitia rasilimali zake za asili na nguvu kazi ya wananchi wake, Fadhili anakuja na dira mpya ya maendeleo yenye kugusa maisha ya kila mwananchi.

Fadhili Salmon Nafutari amechukua fomu mapema leo Juni 30, 2025 katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Vijijini. 

Kwa miaka kadhaa, Fadhili amekuwa mstari wa mbele katika masuala ya maendeleo ya wananchi, akiwa amewahi kushika nafasi mbalimbali za uongozi zikiwemo:

· Kiongozi wa Chama cha Wachimbaji Wadogo – akishughulika moja kwa moja na masuala ya rasilimali madini na haki za wachimbaji,

· Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Tawi, akishiriki kupanga na kusimamia ajenda za maendeleo kwa msingi wa kisera na kimkakati,

· Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Wazazi Wilaya ya Shinyanga DC, nafasi ambayo bado anaendelea kuitumikia kwa bidii na uaminifu.

· Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Shinyanga Vijijini, nafasi ambayo bado anaendelea kuitumiakia kwa bidii hadi sasa katika kutekeleza sera za cahama cha Mapinduzi CCM.

· Mkurugenzi kampuni ya Fadson General Company Limited.

·Mpaka sasa ni mkulima na mchimbaji wa madini ya dhahabu, mwekezaji wa sekta ya madini ya dhahabu Shinyanga vijijini.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 30,2025


Magazeti ya leo

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger