Thursday, 1 May 2025

EFG YATOA MAFUNZO YA USAWA WA KIJINSIA, UONGOZI NA HAKI ZA KIRAIA KWA WANAWAKE WAFANYABIASHARA SOKONI MANISPAA YA SHINYANGA


Na Kadama Malunde – Malunde 1 Blog

Shirika lisilo la kiserikali la Equality for Growth (EfG) limeendesha mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.

Mafunzo hayo ya siku mbili (Mei 1-2, 2025) yanafanyika katika ukumbi wa Liga Hotel mjini Shinyanga, yakiwaleta pamoja wanawake wafanyabiashara kutoka masoko sita ya Manispaa ya Shinyanga ( Soko Kuu, Ibinzamata, Ngokolo, Kambarage, Nguzo Nane na Majengo Mapya).

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Ford Foundation, Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta, amesema lengo kuu ni kuwajengea uwezo wanawake wafanyabiashara kushiriki kikamilifu katika nafasi za uongozi, kufanya maamuzi na kusimamia shughuli za kibiashara katika mazingira ya soko.
 Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta

“Tunataka kuona wanawake wakiongoza, wakielewa haki zao na wakihusika moja kwa moja katika kupanga na kusimamia ajenda zinazowagusa. Mafunzo haya ni sehemu ya mchakato wa kuwawezesha,” amesema Bi. Suzan.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya Sauti ya Mwanamke Sokoni, iliyoanzishwa Oktoba 2011, na ambayo hadi sasa imetekelezwa katika zaidi ya masoko 47 katika mikoa 10 nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Shinyanga, Lindi, Mtwara, Mbeya, Iringa, Tanga (Lushoto), Musoma na Dodoma.
Kwa upande wake, Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo, amewatia moyo wanawake hao kuendeleza ushirikiano wao kwa kujiunga kwenye vikundi ili waweze kunufaika na fursa za mikopo kutoka halmashauri, na hivyo kuimarisha biashara zao na kujenga uongozi thabiti ndani ya jamii ya wafanyabiashara.

“Kupitia ushirikiano na vikundi, wanawake wanaweza kupata mikopo, kushirikishana maarifa na kusimama imara kama viongozi katika maeneo yao ya biashara,” amesema Bi. Evah.

EfG ni shirika lisilo la kiserikali lililosajiliwa rasmi tarehe 6 Agosti 2008, likiwa na dhamira ya kuinua sekta isiyo rasmi, hasa kwa wanawake, kwa kutoa mafunzo ya sheria na haki za binadamu, msaada wa kisheria, kuwezesha usawa wa kijinsia katika fursa za kibiashara, na kushawishi sera zinazolenga maendeleo jumuishi.
 
Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta akizungumza wakati wa
mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde
 Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta akizungumza wakati wa
mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
 Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta akizungumza wakati wa
mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
 Afisa Miradi wa EfG, Bi. Susan Sitta akizungumza wakati wa
mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.

Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo akitoa mada kuhusu Uongozi na Haki za Kiraia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo akitoa mada kuhusu Uongozi na Haki za Kiraia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo akitoa mada kuhusu Uongozi na Haki za Kiraia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo akitoa mada kuhusu Uongozi na Haki za Kiraia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Utawala wa EfG, Bi. Evah Buhembo akitoa mada kuhusu Uongozi na Haki za Kiraia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
 Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mshiriki wa mafunzo akichangia hoja wakati Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia kwenye mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Program wa EfG, Nandipa Shadrack akitoa mada kuhusu Usawa wa Kijinsia wakati wa mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia kwa wanawake wafanyabiashara wa masoko mbalimbali katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Wanawake wafanyabiashara sokoni wakifuatilia mafunzo kuhusu Usawa wa Kijinsia, Uongozi na Haki za Kiraia
Share:

Wednesday, 30 April 2025

BARRICK YASHINDA TUZO 6 ZA KIMKAKATI ZA OSHA


Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Bi Zuhura Yunus akitoa moja ya tuzo kwa wafanyakazi wa kampuni ya Barrick kwenye hafla hiyo
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Bi. Mary Maganga akikabidhi tuzo kwa Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Zonnastraal Mumbi kwenye hafla hiyo
Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu , (Ajira, Kazi na watu wenye ulemavu) Ridhiwani Kikwete akikabidhi tuzo kwa Mrakibu wa Usalama Mgodi wa Barrick North Mara , Meshack Issack
Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu , (Ajira, Kazi na watu wenye ulemavu) Ridhiwani Kikwete akikabidhi tuzo kwa Mrakibu wa Usalama Mgodi wa Barrick North Mara , Meshack Issack
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahia ushindi katika hafla hiyo
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahia ushindi katika hafla hiyo
Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu , (Ajira, Kazi na watu wenye ulemavu) Ridhiwani Kikwete akikabidhi tuzo kwa Mrakibu wa Usalama Mgodi wa Barrick North Mara , Meshack Issack
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahia tuzo hizo
Wafanyakazi wa Barrick kwenye picha ya pamoja baada ya kupokea tuzo mbalimbali kwenye hafla hiyo
Barrick Tanzania yenye ubia na serikali kupitia kampuni ya Twiga imenyakua tuzo tano za kimkakati katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) ya 2025 iliyofanyika mjini Singida ambapo Mgodi wa Barrick Bulyanhulu umeshinda tuzo kubwa ya mshindi wa juu wa jumla katika kipengele cha Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) na Mgodi wa North Mara kuwa mshiriki bora wa maonesho ya mwaka huu (Overall Best OHS Exhibitor- North Mara).

Mbali na ushindi huo mkubwa migodi ya Barrick nchini ya Bulyanhulu, North Mara na Buzwagi ambao upo kwenye mchakato wa kufungwa imeshinda tuzo za Ujumuishaji katika maonesho (Exhibitor and Inclusion North Mara), Shughuli za mifumo ya Uchimbaji (Mining and Quarrying North Mara), ubunifu katika maonesho (Exhibitor and Innovation -Barrick Bulyanhulu), utaalamu wa ufundi wa kisayansi (Professional and Technical Scientific Buzwagi), na tuzo ya uwezeshaji wa maonesho.

Katika Hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi na Watu Wenye Ulemavu) Mhe, Ridhiwani Kikwete ambaye amesisitiza umuhimu wa waajiri na wafanyakazi kuzingati sheria, kanuni na miongozo inayotolewa na serikali kupitia Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) ili kumlinda mfanyakazi na uwekezaji na biashara kwa ujumla.

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa kazi (OSHA), Bi Khadija Mwenda ametumia nafasi hiyo kuwashukuru washiriki wote, waajiri na wafanyakazi kwa kuendelea kuzingatia kanuni na sheria za afya na usalama mahali pa kazi kama injini ya kuongeza uzalishaji kwenye maeneo yao ya kazi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchini kwa ujumla.

Mwakilishi wa Barrick katika hafla hiyo ambaye ni Mrakibu wa Usalama , Mgodi wa North Mara Bw. Meshack Issack amesema Barrick -Twiga itaendelea kushirikiana na serikali katika kulinda afya za wafanyakazi wake pamoja na kudumisha usalama kama nyenzo ya kuchochea uzalishaji , ufanisi na matumizi ya akili mnemba katika sekta ya madini hapa nchini.

Ushindi wa mwaka huu ni mwendelezo wa ushindi katika maonyesho ya OSHA yaliyofanyika katika miaka ya karibuni ambapo mwaka jana pia kampuni ilishinda tuzo tano ikiwemo tuzo ya mshindi wa jumla.

Suala la Afya na Usalama ni DNA ya kampuni ya Barrick na imeendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa za kidigitali na akili mnemba kuhakikisha inaimarisha zaidi usalama kwenye maeneo yake ya kazi na inatekeleza program za usalama ya Journey to Zero na kufanikisha kutokomeza matukio ya ajali kazini na nje ya kazi kwa wafanyakazi wake.

Mbali na kuwekeza katika usalama, Barrick imeendelea kuchangia pato la Serikali kupitia kodi na tozo mbalimbali, Kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii kupitia fedha za CSR zinazotolewa na migodi yake hususani katika mikoa ya Mara ulipo mgodi wa North Mara na Shinyanga na Geita ulipo mgodi wa Barrick Bulyanhulu hususani katika sekta za afya, elimu na miundombinu ambayo imebadilisha maisha ya Wananchi kuwa bora zaidi.

Pia kampuni imekuwa kinara wa kutekeleza sera ya Maudhui ya ndani (Local content) ambayo inaendelea kuwanufaisha wazawa kwa kufanya kazi na migodi yake.

Share:

TIJA KWA NCHI NDIYO KIPAUMBELE CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI ASILIA (LNG)- DKT. BITEKO


📌 Asema kiu ya Serikali ni kuona mradi unatekelezwa ila maslahi ya Taifa ndiyo kipaumbele

📌 Alieleza Bunge hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhamasisha ujenzi wa vituo vya gesi (CNG) na matumizi

📌 Aeleza kuhusu kuundwa kwa Timu kuangalia unafuu wa gharama za umeme kwa Wananchi

📌 Kapinga azungumzia kazi za kupeleka umeme wa Gridi Rukwa, Kagera, Katavi, Lindi na Mtwara

📌 Shilingi Bilioni 9.89 kupeleka umeme jua kwenye visiwa 118

📌 Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati 2025/2026 kwa asilimia 100

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko amesema dhamira ya Serikali ni kutekeleza mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) kutokana na faida zake kiuchumi ila kwa sasa kuna maeneo ambayo Serikali inayafanyia kazi kwa kina kupitia majadiliano na Wawekezaji ili mradi husika uwe na tija kwa nchi na wananchi.

Ameyasema hayo tarehe 29 Aprili 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na Wabunge kuhusu Hotuba ya Bajeti ya  Wizara ya Nishati ya shilingi Trilioni 2.2 kwa mwaka 2025/2026 kabla ya kupitishwa kwa kishindo na Bunge hilo kwa asilimia 100.

“ Mradi wa LNG umeanza kusemwa kwa muda mrefu na kila mmoja angetamani mradi huu ukamilike jana lakini lazima tukubaliane kuwa lazima tujadiliane kwa kina na wawekezaji ili kupata kilicho bora na kuleta tija, ninachotaka kuwahakikishia ni kuwa timu ya majadiliano ya Serikali na Wawekezaji wanaendelea na majadiliano na tunatarajia kuwa ndani ya mwaka huu 2025 kama tutakuwa tumemaliza masuala matatu yaliyosalia kujadiliwa, mkataba huo utasainiwa ili mradi uanze mara moja.” Amesema Dkt.Biteko

Ameongeza kuwa, Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan ana kiu ya kuona mradi huo  unaanza na alishatoa maagizo kwa Wizara ya kuhakikisha kuwa mradi unaanza kutekelezwa.

Akijibu hoja kuhusu vituo vya mafuta vinavyoongezeka na kujengwa kwa kukaribiana,
Dkt.Biteko amesema kuwa Wizara ya Nishati imeanza mazungumzo na Wizara ya Ardhi ili kuongeza umbali kati ya kituo kimoja na kingine kutoka mita 200 za sasa kwa lengo la kuleta usalama wa watu, mazingira na shughuli za kijamii.

Kuhusu msamaha wa kodi mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa gesi inayotumika kwenye vyombo vya moto kama vile magari (CNG), Dkt. Biteko amesema kuwa Serikali ilishatoa msamaha wa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa vifaa na mashine mbalimbali zinazotumika katika mnyororo wa thamani kwa miradi ya CNG kama vile mitungi ya CNG pamoja na vifaa vya kuwezesha kufunga mfumo kuwezesha magari kutumia gesi hiyo.

Ameongeza kuwa, katika mwaka 2024/2025 Wizara ya Nishati imewasilisha Wizara ya Fedha mapendekezo ya maboresho ya kodi katika gesi asilia inayotumika kwenye magari ili kuzidi kuhamasisha matumizi ya CNG na wawekezaji wanaowekeza kwenye miradi hiyo wapate faida na kurudisha gharama wanazowekeza kwa haraka.

Akijibu  hoja za Wabunge kuhusu gharama za kuunganisha umeme vijijini na mijini, Dkt.Biteko amesema kuwa imeundwa timu kwa ajili ya kuangalia namna gani gharama hizo zitapunguzwa lengo likiwa ni kuleta unafuu kwa wananchi.

Kuhusu usambazaji wa umeme Vijijini, Dkt.Biteko amesema kuwa, Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan anapaswa kupongezwa kwa kufikisha umeme katika Vijiji vyote 12,318 kama ilivyoelekezwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 huku kazi ya kupeleka umeme vitongojini ikiendelea kwa kasi.

Akizungumzia ujenzi wa vituo vya kupoza umeme katika wilaya zote nchini kupitia mradi wa gridi imara, Dkt. Biteko amesema kuwa tayari Serikali imeshanunua viwanja kwa ajili kujenga vituo hivyo na katika awamu ya kwanza vitajengwa vituo 14 huku utekelezaji ukiendelea na katika laini za umeme ambazo ni ndefu sana Serikali itaweka switching stations.

Aidha, kuhusu suala la kukatika kwa umeme nchini, Dkt.Biteko amesema kuwa  limepungua kwa asilimia 48 huku dakika za kukatika umeme zikipungua kwa asilimia 64 na kwa sasa umeme ukikatika ni kwa sababu tu ya matengenezo ya miundombinu. Hata hivyo amesema Serikali inaendelea kuimarisha kituo cha huduma kwa  Wateja TANESCO ili taarifa ziwafikie wananchi kwa wakati pale umeme unapokatika ikiwemo kila wilaya kuwa na kundi sogozi.

Awali, wakati wa kuhitimisha Hotuba hiyo ya Wizara ya Nishati, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga alimpongeza Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayofanya katika Taifa hususan kwenye Sekta ya Nishati akieleza kuwa moja ya misingi ya ukuaji wa kiuchumi na maendeleo katika Taifa lolote ni uwekezaji katika Sekta ya Nishati.

Akizungumzia mikoa ambayo bado haijaunganishwa katika gridi ya Taifa ya umeme, Kapinga alisema kuwa kuna miradi mbalimbali inayoendelea ambapo katika Mkoa wa Rukwa kuna mradi mkubwa wa kusafirisha umeme unaoendelea wa kutoka Iringa-Tunduma hadi Rukwa na kipande kingine cha mradi kitakachounganisha gridi ya Tanzania na Zambia.

“Mhe.Spika  katika Mkoa wa Mtwara na Lindi tayari mkandarasi yupo eneo la kazi, mradi umeanza kwa kujenga njia ya umeme kutokea Songea-Tunduru-Masasi hadi Mahumbika na tumeshaanza kulipa fidia katika eneo la Tunduru hadi Masasi takriban shilingi bilioni 4.6 na eneo lililobakia la Songea kuelekea Namtumbo na Tunduru tutaendelea kulipa fidia ya takriban shilingi bilioni 2.7.” Alisema Kapinga

Kuhusu kupeleka gridi ya Taifa katika Mkoa wa Kagera alisema kuwa kazi inaendelea kupitia ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya Benaco-Kyaka na katika Mkoa wa Katavi mradi wa kupeleka umeme wa gridi mkoani humo uko katika hatua za mwisho.

Akizungumzia kazi ya kupeleka umeme kwenye visiwa mbalimbali nchini, Kapinga alisema kuwa, Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 9.89 ili kupeleka mifumo ya umeme jua katika visiwa 118 ambavyo vipo katika mikoa zaidi ya mitano hususan Wilaya ya Ukerewe.

Kuhusu maboresho miundombinu ya umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Kapinga alieleza kuwa kuna kazi zinaendelea kwa lengo la kuwawezesha wananchi kupata umeme wa uhakika ikiwemo uboreshaji wa kituo cha Mbagala ambacho kilikuwa na transfoma yenye uwezo wa MVA 50 lakini sasa inawekwa transfoma mpya yenye uwezo wa MVA 120 ili kukiongezea uwezo kituo hicho ili wananchi wa Mbagala, Temeke, Yombo, Mkuranga na baadhi ya maeneo ya Kigamboni waendelee kupata umeme wa uhakika.

Alieleza kuwa kazi hiyo imefikia mwishoni na muda wowote transfoma hiyo itaanza kufanya kazi. Kwa eneo la Kigamboni amesema maboresho pia yanaendelea kufanyika na kwamba wananchi tayari wameshaanza kuona mabadiliko ya upatikanaji umeme kupitia maboresho hayo.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 30, 2025


 

Magazeti ya leo


















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger