Saturday, 29 March 2025

UJENZI WA STENDI YA MABASI MADABA KUANZA RASMI APRILI

Mbunge wa Jimbo la Madaba Mhe. Joseph Kizito Mhagama akizungumza na wananchi katika eneo la stendi inayotarajiwa kuanza ujenzi wake wiki ijayo
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba Abdul Manga akizungumza na wananchi kuhusu mradi huo wa ujenzi wa stendi Lituta kitongoji cha kifaguro Madaba


Mhandisi Jeremiah Chambai akionesha Mchoro wa ramani ya stendi itakayojengwa Lituta Madaba
Wananchi na Wanachama waliojitokeza kumpokea Mbunge Joseph Kizito Mhagama Katika kata ya Lituta kitongoji cha kifaguro Madaba Mkoani Ruvuma
 Mbunge wa Madaba Joseph Kizito Mhagama alipowasili katika eneo la kitongoji cha kifaguro ambapo mradi wa ujenzi wa stendi hiyo unaotarajiwa kufanyika


Na Regina Ndumbaro-Madaba.

Ujenzi wa stendi ya mabasi katika Halmashauri ya  Madaba, mkoani Ruvuma, unatarajiwa kuanza rasmi mwezi Aprili 2025. 

Stendi hiyo itakayojengwa katika kitongoji cha Kifaguro kata ya Lituta, ina gharimu kiasi cha shilingi bilioni 5.

 Mbunge wa Madaba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Joseph Kizito Mhagama, amethibitisha taarifa hiyo katika kikao cha utekelezaji wa miradi mbalimbali katika jimbo lake. 

Amesema kuwa mradi huu ni moja ya hatua kubwa za maendeleo zinazotekelezwa kwa manufaa ya wananchi wa Madaba.

Mhagama amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kipaumbele kikubwa alichotoa kwa wananchi wa Madaba kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Ameeleza kuwa, pamoja na mradi wa ujenzi wa stendi, mradi mwingine mkubwa unaoendelea ni wa maji katika Kata ya Mtyangimbole, wenye thamani ya shilingi bilioni 5.500.

 Ameongeza kuwa miradi hii inaashiria uwekezaji mkubwa wa serikali katika kuimarisha huduma za kijamii kwa wananchi wa Madaba.

Aidha, Mhagama amewashukuru viongozi wa Halmashauri ya Madaba na wananchi wa Kata ya Lituta kwa kushirikiana kikamilifu katika kuhakikisha mradi huu unafanikiwa. 

Amesisitiza kuwa, wakazi wa maeneo jirani kama Mahanje, Matetereka, na Wino pia watanufaika na mradi huu. 

Pia ameipongeza kamati ya mradi iliyoundwa kutoka vijiji hivyo kwa mshikamano wao katika kuhakikisha utekelezaji wa ujenzi wa stendi unafanikiwa.

Kwa upande wake, Mhandisi Jeremiah Chambai, ambaye amepewa jukumu la kusimamia mradi huo, amethibitisha kuwa stendi hiyo itajengwa katika eneo lenye ukubwa wa takriban hekari tatu. 

Ameeleza kuwa mchoro wa ramani ya stendi hiyo tayari umeandaliwa na wananchi wameonyeshwa jinsi itakavyokuwa. 

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Madaba, Abdul Manga, amesema kuwa ujenzi wa stendi hii utafanyika kwa viwango vya juu, ikiendana na hadhi ya stendi kubwa za miji mingine kama Njombe na Tanga na Iringa.

Manga ameongeza kuwa stendi hii italeta manufaa makubwa kwa wakazi wa Madaba, ikiwemo kuboresha biashara na kuondoa kero za usafiri kwa abiria. 

Amesema kuwa ujenzi utaanza na awamu ya kwanza kwa gharama ya shilingi milioni 205.

 Pia amewataka wafanyabiashara waliopo katika maeneo ya stendi kushiriki katika majadiliano kuhusu mpangilio wa majengo mapya ili kuhakikisha hakuna anayepata hasara na mji wa Madaba unakuwa na taswira inayolingana na hadhi mpya ya stendi hiyo.

 viongozi wa Madaba wameeleza matumaini yao kuwa mradi huu utachochea maendeleo makubwa katika eneo hilo. 

Wananchi wa Kata ya Kifaguro wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kusikiliza kilio chao na kuwapatia fedha za mradi huu.

Pia wamempongeza Mbunge wao Joseph Kizito Mhagama kwa kazi kubwa anayoifanya. 

Ujenzi wa stendi hii unatarajiwa kubadilisha mazingira ya usafiri na biashara, huku ukiimarisha uchumi wa Madaba na maeneo jirani.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MACHI 29,2025


Magazeti
 
Share:

Friday, 28 March 2025

THE RUNNERS TANZANIA YAZINDUA MSIMU WA TANO WA ABSA DARCITY MARATHONI 2025

 

*********
Na Mwandishi wetu....
The Runners Tanzania wamezindua rasmi Absa Dar City Marathon 2025, ikiwa ni msimu wa tano wa mbio hizo, zitakazofanyika Mei 4, 2025, katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. Lengo kuu la mbio hizi ni kusaidia mahitaji ya Hospitali ya Mnazi Mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Godfrey Mwangungulu, Makamu Mwenyekiti wa Runners Club, amesema wanatarajia washiriki wasiopungua 3,000 msimu huu na amewasihi watu kuendelea kujisajili kwa ada ya shilingi 40,000.

“Tunakwenda kufanya msimu wa tano wa Dar City Marathon, mbio ambazo zimekuwa zikifanyika kwa mafanikio na kuendelea kukua mwaka hadi mwaka. Mwaka huu tunatarajia washiriki zaidi ya 3,000,” alisema Mwangungulu.

Aliendelea kusisitiza kuwa mbio hizi si za mashindano tu, bali pia ni fursa ya kujenga mshikamano na kusherehekea pamoja.

Kwa upande wake, Aron Luhanga, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Absa Bank, amesema benki hiyo kama mdhamini mkuu imejipanga vyema kuunga mkono mbio hizo.


“Kaulimbiu yetu ni ‘Tunathamini Story Yako,’ na tunaamini hakuna mtu anayeweza kuandika hadithi nzuri bila kuwa na afya njema. Afya bora ndiyo msingi wa mafanikio,” alisema Luhanga.

Naye Juma Patrice, Mkuu wa Kitengo cha Bima kupitia Taasisi za Fedha, Alliance Life Assurance Limited, amesema wamekuwa wadau wa mbio hizi tangu zilipoanzishwa na wafanyakazi wa kampuni hiyo hushiriki kila mwaka. Amewahimiza wakazi wa Dar es Salaam kujisajili na kushiriki mbio hizo kwa manufaa ya afya na jamii.

“Mbio hizi si tu za kusaidia Hospitali ya Mnazi Mmoja, bali pia zinahamasisha watu kufanya mazoezi, kujenga afya bora, na hata kuutambua mji wetu wa Dar es Salaam kwa mtazamo wa utalii wa ndani,” alisema Patrice.

Felix Donald, Kiongozi wa Kamati Tendaji wa Shirikisho la Urais Tanzania, amepongeza The Runners kwa kushirikiana na Absa Bank kuandaa mbio hizi kwa mara ya tano.

“Mbio hizi zinachangia maendeleo ya afya, utalii, na kusaidia jamii. Ni muhimu kuendelea kuziboresha kila mwaka,” alisema Donald.

Naye Epson Elias kutoka Kilimanjaro Fresh ameushukuru uongozi wa Dar City Marathon kwa kuwawezesha kuwa sehemu ya mbio hizo na kuwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki, kama njia ya kurudisha shukrani kwa jamii.






Share:

Video Mpya : MAYIKU SAYI - NA ENJOY

Share:

JE, UMEWAHI KUDHULUMIWA?, PATA HAKI YAKO SASA!

Naitwa Amani kutokea Babati, unajua hakuna kitu kibaya maishani kama kudhulumu mali ambayo sio yako, kuna watu mikosi haiondoki katika maisha yao kutokana na dhuluma walizozifanya huko nyuma.

Nasema hivyo kwa sababu Baba yetu aliamua kununua magari mawili kwa ajili ya watoto wake ili hapo baadaye tusije kuteseka katika maisha, haya magari ni mabasi kwa ajili ya usafiri na kila mmoja alipewa lake.

Basi niliamua kukodisha bus langu wakati naendelea na masomo na fedha niliyopata nilikuwa nalipa nayo ada ya chuo na matumizi mengine, dereva niliyempa gari langu alikuwa mwaminifu, kila mwisho wa wiki alinitumia fedha yangu kama tulivyokubaliana.

Sasa baada ya kumaliza chuo nilitaka kuchukua bus langu, hivyo nilimpaa taarifa hiyo, cha kusikitisha ni kwamba alikataa na kudai bus lile ni lake na kwamba nilimkodisha kwa makubaliano ya kumuuzia akifikisha kiwango fulani cha fedha.

Kubwa zaidi nilishangaa sana pale alipoamua kutoa nyaraka kuwa anamiliki bus lile, ugomvi ulikuwa mkubwa hadi Baba yangu alikuja lakini bado aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa gari ni mali yake.

Binafsi nilitaka kwenda mahakamni kufungua kesi, lakini rafiki yangu mmoja Leornad aliniambia kuna mtu mmoja anaitwa Kiwanga Doctors anaweza kunisaidia na kupata mali yangu bila kusumbuka sana.

Leornad alinipa mawasiliano ya Kiwanga Doctors kutokea Migori nchini Kenya na kuniambia niwasiliane naye mara moja, nilimpigia na kueleza shida yangu hiyo iliyokuwa inanisumbua, aliniambia nisijali kwani ndani ya siku chache mwenyewe atarudisha gari langu maana ameshafanya dawa, find lost items spell.

Baada ya siku chache yule dereva alinipigia simu akiwa hoi kitandani hata kuzungumza kwake ilikuwa kwa shida sana, aliniomba msamaha sana na kuniambia nikachuke gari langu. Nami nilienda nikachukua gari na kuweza kuendelea na biashara zangu na sasa nimepiga hatua kubwa kimaendeleo.

Tukio hilo ni la miaka mitano iliyopita, nimelikumbuka na kuandika stori yake hapa kwa sababu yule dereva hivi karibuni kanipigia simu na kusema tangu wakati ule kila akipata gari aendesha kwa ajili ya biashara anapata ajali, anaona kama imekuwa ni mkosi kwake.

Aliomba msamaha kwa mara ya pili na kuniambia nimuondolee mkosi huo, mimi nilichofanya ni kumpatia namba ya Kiwanga Doctors na kumtaka awasiliane naye na kumueleza changamoto yake.

Ni watu wengi hadi sasa wamepata mafanikio na furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +254 116469840 au tembelea tovuti yao kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zao ambazo zimewasaidia wengi. 

Share:

KAMATI YA BUNGE YAPITISHA MPANGO NA BAJETI YA OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA TAASISI ZAKE KWA MWAKA WA FEDHA 2025/26

 



Na. Veronica Mwafisi-Dodoma


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imepitisha Mpango na Bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa fedha 2025/26 baada ya kupitia mafungu yote yaliyo chini ya ofisi hiyo na kujiridhisha.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Florent Kyombo amezungumza hayo tarehe 27 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Bunge jijini Dodoma alipokuwa akikaimu nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo mara baada ya Wajumbe wa Kamati kujadili na kuridhia taarifa ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2025/26 ya Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora.

“Kamati imejadili na kuridhia kupitisha Mpango na Bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa fedha 2025/26, niwapongeze kwa maandalizi mazuri yenye uwazi, Kamati inawaasa kuwa na matumizi mazuri ya fedha pale zitakapopitishwa katika vikao vya Bunge la Bajeti ambapo tunaamini mtafikia malengo ya kuwatumikia watanzania kwa maendeleo ya nchi. Mhe. Kyombo amesema.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kwa kuwa na majadiliano mazuri na ofisi anayoiongoza ambayo wanaamini yatawasaidia kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji wa majukumu yao kupitia bajeti hiyo.

Mhe. Mwenyekiti, nitoe shukrani za dhati kwa niaba ya ofisi ninayoiongoza mara zote tumepokea maoni, ushauri na michango mbalimbali kutoka katika Kamati yako inayolenga kuboresha Utumishi wa Umma nchini kwa lengo la kutimiza azma ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwa na Utumishi wa Umma uliotukuka.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya ofisi hiyo, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI, Bw. Juma Mkomi amesema Kamati hiyo imekuwa msaada mkubwa wa kuiongoza Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora kwa kuwapatia maarifa mengi kutoka kwa Wajumbe wote wa Kamati hiyo yenye kuboresha utendajikazi.

Mpango na Bajeti ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na taasisi zake kwa Mwaka wa fedha 2025/26 umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025, Maelekezo ya Ilani ya CCM kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 na Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2021/22-2025/26).







Share:

Thursday, 27 March 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 28,2025


Magazeti ya leo
Share:

PAC YAISHAURI TEMESA KUONGEZA KASI YA USIMAMIZI MRADI WA KIVUKO KIPYA MAFIA NYAMISATI



Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeishauri TEMESA kuhakikisha inaongeza kasi ya kusimamia mkandarasi anaetekeleza mradi wa ujenzi wa kivuko kipya cha Mafia Nyamisati ili umalizike haraka na wananchi waweze kupata huduma ya kivuko.

Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya mradi huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Naghenjwa Kaboyoka amesema wananchi wa maeneo ya Mafia na Nyamisati wanahitaji huduma ya kivuko na Serikali ipo inatazama kwa ukaribu kuona mradi huo unakamilika kwa wakati.

"Kwa hiyo tunasema kwamba hili jambo litupiwe macho tuone kwamba huu ujenzi wa kivuko hiki kipya cha Mafia na Nyamisati unafanywa kwa ukamilifu ili wananchi wapate ile huduma iliyotakiwa, hivyo tunawashauri na tunawataka mjiongeze, mjiongeze kwa kiasi kikubwa kukamilisha mradi huo.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Japhet Hasunga ameiomba Serikali kuhakikisha fedha zinatolewa kwa wakati ili mradi huo uweze kukamilika kwa wakati huku akiitaka TEMESA kuhakikisha inasimamia maendeleo ya mradi huo kila siku kwa kuwepo katika eneo la ujenzi.

"TEMESA mnatakiwa kuwepo eneo la mradi kila siku kusimamia utekelezaji wa huu mradi, mnatakiwa kuusimamia kuwa sehemu ya huu mradi, muiunde timu haraka iwezekanavyo iweze kuunusuru huu mradi, iwepo pale na itoe taarifa kila siku kwamba tumefikia hapa tumenasa wapi nini kimefanyika, vifaa hivi vimekuja hii imefungwa hii haijafungwa. Amesisitiza Mhe. Hasunga.

Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa kivuko hiko kipya, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Lazaro Kilahala amesema kivuko kipya kinachojengwa kitakuwa na uwezo wa kubeba tani 120, abiria 300 na magari madogo 10.

Ameongeza kuwa kivuko hicho kitakuwa na uwezo zaidi kulinganisha na kinachoendelea kutoa huduma hivi sasa cha MV. KILINDONI ambacho kinao uwezo wa kubeba abiria 200 pekee.

Kilahala amesema kuwa ujenzi wa kivuko hicho kipya kitakachokuwa kinatoa huduma kati ya Mafia na Nyamisati unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Agosti mwaka huu.




Share:

UKATILI WA KIJINSIA NA MAAMBUKIZI YA VVU: CHANGAMOTO ZINAZOKUMBA WANANDOA NA JAMII YA KALENGA


*Wanawake Wanyima Waume zao Tendo la Ndoa "Bila kunipa 20,000 Sikupi'

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Katika kijiji kidogo cha Kalenga kilichozungukwa na milima ya Iringa, hali ya kiuchumi imekuwa ikileta changamoto kubwa katika ndoa na familia. Miongoni mwa matatizo yanayojitokeza ni vitendo vya ukatili wa kijinsia na maambukizi ya virusi vya UKIMWI vinavyofanywa kwa maksudi. 

Hii ni kutokana na wanawake ambao wamekuwa wakinyima waume zao haki ya tendo la ndoa kutokana na changamoto za kifedha, hali inayosababisha migogoro ya familia na jamii kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Rose Wasiko, Mwenyekiti wa Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kalenga, kumekuwepo na ongezeko la mashindano kati ya wanandoa, ambapo kila mmoja anashutumu mwingine kwa kutembea nje ya ndoa. 

Wakati mwingine, kwa lengo la kulipiza kisasi, wanandoa hutafuta wenzi wengine, baadhi yao wakiwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI. Hii ni hali inayosababisha madhara makubwa kwa afya ya jamii.
Rose Wasiko, Mwenyekiti Kituo cha Taarifa na Maarifa Kata ya Kalenga Wilaya ya Iringa


"Ni jambo la kushangaza na la kutisha kuona jinsi wanandoa wanavyoshindana kushitakiana kwa kutembea nje ya ndoa, huku wengine wakitafuta wenzi wengine wenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa makusudi, kana kwamba ni njia ya kulipiza kisasi," alisema Rose.

Wakati hali hii inashika kasi, wanawake wengi katika Kata ya Kalenga wameshtumiwa kwa kunyima waume zao haki ya tendo la ndoa kwa kigezo cha kukosa fedha. Hali hii inatokea hasa wanapoingia katika matatizo ya kifedha, ambapo wanawake wanapinga kutoa unyumba hadi wapate kiasi fulani cha fedha.

 "Mwanamke anaweza kumwambia mumewe, bila kiasi cha shilingi 20,000, basi sikupi tendo la ndoa, anavaa suruali na kujifunga mfuko wa sandarusi ili mumewe asimshike" alieleza Rose.

Hii ni changamoto kubwa kwa wanandoa katika Kata ya Kalenga, ambapo hali ya kiuchumi inavyozorota, ndivyo vitendo vya ukatili vinavyozidi kukithiri. 

Wanandoa wanapokosa kushughulikia migogoro yao kwa njia za kiraia au za kiutu, wanageukia mikakati hatari ya kulipiza kisasi, jambo ambalo lina madhara makubwa kwa afya na ustawi wa familia zao.

Elimu na Huduma kwa Jamii: Njia ya Kupambana na Ukatili

Kituo cha Taarifa na Maarifa, kilichoanzishwa miezi sita iliyopita, kimekuwa na jukumu kubwa la kutoa msaada kwa wanandoa na familia zinazokumbwa na changamoto za kiuchumi na ukatili wa kijinsia.

 Hadi sasa, kituo kimepokea kesi sita zinazohusiana na migogoro ya ndoa, vipigo, ulawiti, na kunyimana tendo la ndoa, pamoja na matatizo mengine yanayohusiana na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Rose Wisiko alieleza kwamba, licha ya changamoto nyingi, wananchi wamekuwa na muitikio mkubwa katika kutoa taarifa za vitendo vya ukatili kutokana na elimu waliyoipata. 

"Wananchi wamejua haki zao, na sasa wanajua ni wapi pa kwenda pindi wanapojikuta katika hali ya ukatili," alisema Rose, akisisitiza kuwa kituo hicho kinatoa huduma kwa usiri ili kuhakikisha kwamba waathirika wanapata msaada bila aibu.

Kwa upande mwingine, katika Kata ya Mabogini mkoani Kilimanjaro, Hatangimana Justine, Makamu Mwenyekiti wa Kituo cha Taarifa na Maarifa, alisema kuwa elimu kuhusu ukatili wa kijinsia inatolewa katika vijiji vyote vya kata hiyo. 

Mikutano ya vijiji, klabu za watoto, na shule za msingi na sekondari ni sehemu muhimu ya kufikisha ujumbe huu kwa jamii.

Hatangimana Justine, Makamu Mwenyekiti Kituo cha Taarifa na Maarifa Kata ya Mabogini Mkoa wa Kilimanjaro

Hatangimana alisisitiza kwamba lengo la elimu hii ni kuhakikisha jamii inakuwa na uelewa wa kuchukua hatua stahiki wakati wanapokutana na vitendo vya ukatili. 

"Tunataka jamii iwe na uwezo wa kuchukua hatua mara moja, na hivyo kuzuia madhara makubwa yanayotokana na ukatili wa kijinsia," alisema.

Changamoto za Kimasai: Dhana za Kijadi na Elimu

Hata hivyo, changamoto kubwa katika baadhi ya maeneo ni dhana za kijadi zinazohusisha jamii za Kimasai, ambazo mara nyingi haziruhusu watoto wa kiume, hasa wa kwanza, kupata elimu.

 Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Mgagao, mkoani Kilimanjaro, kimekuwa kikipambana na dhana hii, kuhakikisha watoto wote wanapata haki ya elimu bila kujali jinsia au umri.

Beatrice Msofe, Mwenyekiti wa Kituo hicho, alisema kuwa jamii ya Kimasai bado inakutana na changamoto kubwa katika kumfundisha mtoto wa kike au wa kiume. 

"Tunajitahidi kubadilisha mtindo huu wa kijadi ili kuhakikisha kwamba kila mtoto anapata haki ya elimu," alisema Beatrice.

Kuhamasisha Jamii: Msingi wa Maendeleo na Ustawi wa Familia

Kama ilivyo katika maeneo mengine ya nchi, elimu kuhusu ukatili wa kijinsia ni muhimu kwa jamii. Katika maeneo kama Kalenga na Mabogini, kutoa elimu ya haki za binadamu na jinsi ya kushughulikia changamoto za kifedha ni hatua muhimu katika kupambana na ukatili wa kijinsia.

 Hii si tu inasaidia kupunguza matukio ya vurugu na maambukizi ya virusi vya Ukimwi, bali pia inachochea maendeleo ya familia na jamii kwa ujumla.

Kwa kuwa jamii inaendelea kukabiliana na changamoto hizi, ni dhahiri kuwa elimu na ushirikiano wa viongozi wa kijiji na serikali utakuwa msingi wa kufanikisha mabadiliko chanya. 

Majukumu ya kila mmoja katika kulinda haki za binadamu na kuhakikisha usalama na afya ya familia ni muhimu katika kujenga jamii imara na yenye ustawi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger