Sunday, 9 March 2025
KATAMBI ATOA KIBUNDA KINGINE MASHINDANO U-17 CUP, VIPAJI VYAANZA KUONEKANA!
RAIS SAMIA : TANZANIA NI MSIMAMIZI MPANGO WA NISHATI SAFI AFRIKA








WAFANYAKAZI WANAWAKE BARRICK WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUSAIDIA JAMII
Wafanyakazi wanawake wa kampuni ya Barrick nchini na wakandarasi wake wameshiriki maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa kujikita kutoa msaada kwenye jamii sambamba na kujitolea muda wao kusaidia shughuli za kijamii ambapo baadhi yao wameshiriki maadhimisho ya kitaifa yaliyofanyika katika jiji la Arusha.Saturday, 8 March 2025
MENEJIMENTI VETA, YATEMBELEA EMIRATE ALLUMINIUM PROFILE KUPATA UZOEFU WA UFUNDI WA ALUMINIAMU

Menejimenti ya VETA ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA. Anthony Kasore, leo, tarehe 7 Machi 2025 imetembelea kiwanda cha Emirate Alluminium Profile kilichopo Tegeta jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujifunza na kupata uzoefu kuhusu namna ufundi wa Aluminiamu unavyofundishwa sehemu ya kazi.
Ziara ililenga pia kuona namna ya kuanzisha ushirikiano kati ya VETA na Emirate Alluminium Profile ili kuwezesha wanafunzi wanaosoma katika vyuo vya VETA kupata ujuzi zaidi kuhusiana na ufundi wa Aluminiamu kupitia mafunzo ya mahala pa kazi. Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA. Anthony Kasore, amesema wamebaini shughuli za ufundi zinazofanywa katika kampuni hiyo zinaakisi Mitaala ya VETA, ambapo wanafunzi wa fani ya Useremala wanafundishwa masuala ya utengenezaji wa Aluminiamu.
CPA Kasore amesema kiwanda hicho kina mafundi waliobobea wenye uzoefu ambao VETA itawatumia kutufundisha na kufundisha katika vyuo vyake.
"Sisi VETA kwa kukutana na Emirates Alluminium Profile tunaenda kuwa na ushirikiano ambao utawezesha kutoa huduma na kuwezesha watu kwenda kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri na kuajiriwa katika viwanda mbalimbali nchini," amesema CPA Kasore.
Aidha, CPA Kasore amesema kupitia ziara hiyo wameona kuna haja ya kutenganisha ufundi wa Aluminiamu na Useremala, ili kila moja iweze kujitegemea, hivyo kuzalisha vijana waliobobea kwenye ufundi wa Aluminiamu ambao una fursa nyingi kwa sasa.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Emirate Alluminium Profile, Ndugu Deogratius Marandu amewataka vijana kuwekeza katika kufanya kazi kwa kutumia mikono na sio kutumia ujanja ujanja ili kufanikiwa na hivyo kuiomba VETA kuendelea na kazi ya kuwaanda vijana ili waweze kuajirika na kujiajiri na kuchangia katika maendeleo ya jamii zao na Taifa. "Mimi nina imani sana na VETA hasa katika kuwanoa vijana naamini tunaenda kushuhudia mabadiliko mbalimbali katika masuala ya Ufundi stadi na tunaenda kuwapata wataalamu watakaoenda kufanya kazi kwa ufanisi," amesema. Kiwanda cha Emirate Alluminium Profile kinajihusisha na uagizaji na uuzaji wa Aluminiamu, vioo, pamoja na mipira kwa ajili ya kutengenezea madirisha na milango ya Aluminiamu.
VIJANA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MAKUNDI HATARISHI
Mchungaji Peter Mayengo wa Kanisa la Moravian Jimbo la Ziwa Tanganyika Manispaa ya Bukoba Mkoani KageraNa Lydia Lugakila-Bukoba
Vijana Katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wametakiwa kuachana na makundi mbali mbali yasiyofaa ikiwemo ikiwemo kujiingiza katika tamaa za kujipatia fedha za mkato bila kuwajibika, kukaa vijiweni, kujihusisha na madawa ya kulevya.
Kauli hiyo imetolewa na Mchungaji Peter Mayengo wa Kanisa la Moravian Jimbo la Ziwa Tanganyika muda mfupi kabla ya semina ya ujasiliamali iliyolenga kuwanoa watu wa rika zote hasa vijana iliyofanyika kanisani hapo.
Mchungaji Mayengo amesema vijana wanatakiwa wajifunze neno la Mungu na kufanya kazi huku akikili kuwepo kwa vijana wavivu ambao wamejikuta kutamani vitu vingi kwa wakati ambapo sio sahihi kwa namna yake.
"Vijana pia wamejikuta wakitoa lugha za matusi, wapo pia wanaoingia kwenye madawa ya kulevya na wana makundi ya ajabu yasiyoleta mafanikio katika Taifa"amesema mchungaji Mayengo.
Mtumishi huyo wa Mungu ameongeza kuwa inaumiza kuona vijana wengi wa Bukoba wanakaa katika vijiwe vya Kahawa na Wazazi hawawakemei jambo linalosababisha kutengeneza vijana na Taifa ambalo linaenda kuharibika.
Amesema ni wakati sasa Wazazi na Watumishi wa Mungu kusimama vizuri katika kurekebisha vijana hao ki maadili ili kuwa naTaifa bora.
Aidha amesema malalamiko juu ya Vijana kukengeuka ki maadili ni mengi huku jamii ikishindwa kuelewa chanzo ni nini.
"Wazazi wanatakiwa kuwatengeneza vijana katika maadili pia Watumishi wa Mungu kuchukua nafasi ya pekee katika kutoa mafunzo ya neno la Mungu ili hofu iwe ndani yao"amesema Mayengo.
Hata hivyo amewahimiza vijana kujikita katika masuala ya ujasiriamali ili wapate ujuzi utakao wasaidia kwa maisha ya baadae huku akiiomba Serikali pia kuona namna ya kuwasaidia vijana wenye ujuzi ili kuwa na Taifa lenye wataalam wengi.


























