Wednesday, 15 January 2025

ZIARA YA DC MTATIRO KIJIJI KWA KIJIJI YAZIDI KUFICHUA MAZITO... AKERWA PESA ZA WANANCHI KUCHEZEWA UPAUAJI JENGO LA ZAHANATI

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

MKUU wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro,ameonyesha kukasirishwa na kitendo cha wananchi wa kijiji cha Mwang'halanga kuchangishwa fedha za kupaua jengo la Zahanati ya kijiji hicho sh.milioni 11.7 lakini fedha hizo zimeshindwa kutekeleza ujenzi huo.
Mtatiro amesikitishwa na kitendo hilo leo Januari 15,2025 wakati akisikiliza kero za wananchi wa kijiji cha Mwang'halanga na kuzitatua,ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake kufikia kila kijiji kusikiliza kero za wananchi,ambapo amefika pia kijiji cha Singita na Manyada.


Amesema kwa changamoto ya wananchi wa kijiji cha Mwang'halanga kushindwa kupauliwa Zahanati yao, na wakati wamechangishwa fedha kila Kaya Sh.28,000, na kuna Kaya 418 sawa na sh.milioni 11.7, lakini fedha hizo hadi leo hazijapaua jengo hilo la Zahanati,na kwamba huko ni kucheza na pesa za wananchi.
"Acheni mchezo na pesa za wananchi,dunia gani utapata wananchi wanachangishana fedha hadi Sh.milioni 11 utawapata wapi,leo mnakuja kuniambia zimekwama kwenye mfumo wa NeST hili hapana," amesema Mtatiro.


"Haiwezekani Mtendaji wa Kijijji amechangisha pesa wananchi, na pesa hizo akaziweka kwenye Akaunti ya kijiji kwa uaminifu kabisa pamoja na fedha za mfuko wa jimbo Sh.milioni 3 jumla milioni 14,na hadi sasa jengo hilo halijapauliwa,na kunieleza sababu ni mfumo wa NesT huku ni kucheza na pesa za wananchi,"ameongeza Mtatiro.
Aidha,ameagiza Menejimenti ya Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga,kwamba ifikapo tarehe 27/1/2025 kuwa siku hiyo ni siku ya kwenda kupaua jengo la Zahanati hiyo, na yeye atafika hapo pamoja na Kamati yake ya ulinzi na usalama kupaua pamoja na wananchi.


Mtendaji wa kijiji cha Mwang'halanga Helena Kayagila,amesema wananchi wa kijiji hicho walichangishwa fedha hizo Agosti 30 mwaka jana,pamoja kutolewa sh.milioni 3 fedha za mfuko wa jimbo,na yeye akaziweka kwenye akaunti ya kijiji jumla sh.milioni 14.


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Edward Maduhu,akitoa majibu amesema kwamba upauaji wa jengo la Zahanati hiyo, limekwamishwa na tatizo la
mfumo mpya wa kielektroniki wa manunuzi ya umma NeST.
Diwani wa Samuye John Ngengeshi,naye akizungumza kwenye mkutano huo, alikazia kwamba ukwamishaji wa fedha hizo za wananchi kupauwa zahanati ya kijiji hicho, linatokana na kukwama kwa mfumo wa NeST, sababu ambayo mkuu wa wilaya hakukubaliana nayo.


Nao baadhi ya wanakijiji cha Mwang'halanga akiwamo Manase Elias,awali walisema kama pesa zao walizochanga zimeshindwa kupaua Zahanati yao, ni vyema wakarudishiwa pesa hizo, na kwamba wao walilidhia kuchangishana ili wapate huduma za matibabu karibu na makazi yao lakini wanaona hakuna kinachoendelea.
Katika ziara hiyo ya Mkuu wa wilaya amesikiliza kero za wananchi ikiwamo changamoto ya ukosefu wa maji,ubovu wa miundombinu ya barabara,kutokamilika maboma ya zahanati,umeme,pamoja na migogoro ya ardhi,huku akiagiza wazazi kupeleka watoto wao shule, na kwamba mwisho itakuwa ijumaa na baada ya hapo zoezi la ukamataji lita anza.


TAZAMA PICHA 👇👇
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akisikiliza kero za wananchi na kuzitatua.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Usanda Edson Jisena akizungumza kwenye mkutano huo.
Diwani wa Usanda Forest Nkole akizungumza kwenye mkutano huo.
Diwani wa Samuye John Ngengeshi akizungumza kwenye mkutano huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Edward Maduhu akitoa majibu kwenye mkutano.

Share:

WIZARA YA NISHATI YAWASILISHA UTEKELEZAJI WA BAJETI 2024/2025 KATIKA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI

📌 Maeneo ya kipaumbele yaliyotekelezwa kwa mwaka 2024/2025 yaelezwa

📌 Ni pamoja na hali ya uzalishaji na upatikanaji wa Nishati ya Umeme nchini

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga (Mb) ameongoza Menejimenti ya Wizara ya Nishati kuwasilisha taarifa utekelezaji wa bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2024/2025 katika Kipindi Cha Julai hadi Desemba 2024 katika Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini.

Taarifa hiyo imewasilishwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Nishati Petro Lyatu ambaye ameeleza kuwa Wizara ya Nishati  imetekeleza bajeti katika maeneo mbalimbali  ikiwa ni yale ya kipaumbele na kimkakati pamoja na kuendelea kutekeleza miradi ya uzalishaji ,usafirishaji na usambazaji wa Umeme Ili kuufikisha gridi ya Taifa katika mikoa iliyosalia.

Amesema Wizara imeendelea kupeleka nishati Vijijini ikiwemo kusambaza umeme katika vitongoji Tanzania Bara pamoja na kutekeleza miradi ya kielelezo na kimkakati ya mafuta na gesi asilia ikiwa ni sambamba na mradi wa kuchakata na kusindika gesi asilia kuwa kimiminika.

Amesema Wizara ya Nishati inaendelea kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika na unaokidhi mahitaji ya kiuchumi na kijamii, ikiwa ni pamoja  na kuongeza uwezo wa mitambo ya kufua umeme iliyounganishwa katika mfumo wa Gridi ya Taifa na kuongezeka kufikia Megawati 3,091.71 mwezi Desemba,2024.

Amesema ongezeko hilo limetokana na kukamilika kwa miradi mbalimbali hususani Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Maji wa Julius Nyerere ambapo hadi Desemba 2024 mitambo mitano (5) kati ya tisa ilikuwa imekamilika na inazalisha umeme na kuingizwa katika Gridi ya Taifa.

Vile vile, Lyatu amebainisha kuwa Wizara imekamilisha Mkakati wa Matumizi Bora ya Nishati (2024/2025) mwezi Novemba 2024 ambao ulizinduliwa Desemba 3, 2024 wakati wa Kongamano la Kikanda katika Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) la Matumizi Bora ya Nishati, Mkakati ambao  pamoja na masuala mengine unalenga kuendelea kuhakikisha Watanzania kutumia Nishati kwa ufanisi Ili kupunguza gharama za Matumizi pamoja na kuendelea kuimarisha upatikanaji na Matumizi ya Nishati safi ya Kupikia. 

Mwenyekiti wa Kamati  ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini  Dk. David Mathayo David baada ya kupokea taarifa amesema kuwa  "Wizara Haina budi kuendelea  kuunga mkono Sera ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan juu ya Matumizi ya Nishati safi ya Kupikia kwa Watanzania,kwa kuendelea kufanya tafiti, kuhamasisha watumiaji, kutoa elimu na kuanzisha sheria ya kulinda miundombinu mbalimbali ya nishati ya kupikia na kuhakikisha gesi kwa watumiaji inapatikana kila Kona ya Tanzania".

Share:

MAANDALIZI YA MKUTANO WA NISHATI WA WAKUU WA NCHI AFRIKA (MISSION 300) YAMEFIKIA ASILIMIA 95- DKT. BITEKO


Dkt. Doto Biteko

📌 Watanzania milioni 13.5 kusambaziwa umeme ifikapo 2030 kutoka milioni 5.2 ya sasa

📌 Asema Mkutano wa Mission 300 umekuwa kivutio duniani; Taasisi za Kimataifa zaonesha nia ya kushiriki

📌 Ataja sababu za mkutano wa M300 kufanyika Tanzania


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.Dkt.Doto Biteko amesema kuwa maandalizi ya Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika wenye lengo la kuharakisha upatikanaji umeme kwa Waafrika milioni 300 ifikapo 2030 (Mission 300) utakaofanyika tarehe 27 na 28 Januari jijini Dar es Salaam yamefikia asilimia 95.



Dkt.Biteko amesema hayo tarehe 15 Januari 2025 mara baada ya kukagua maandalizi ya Mkutano huo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila.


Amesema Wakuu wa Nchi 54 kutoka Bara la Afrika wanatarajiwa kushiriki pamoja na viongozi wengine ambao ni Mawaziri wa Fedha na Nishati kutoka barani Afrika, Marais wa Benki ya Dunia (WB) na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), pamoja viongozi kutoka Jumuiya ya Ulaya na Jumuiya ya Umoja wa Afrika ambapo kazi zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na kukamilisha ukarabati wa ukumbi wa JNICC.


“Kazi nyingine zinazoendelea ni pamoja na usajili na uthibitisho wa wageni ambao watakuja kwa ajili ya ushiriki na ukarabati wa maeneo mengine yatakayotumika kwenye mkutano huu, nichukue nafasi hii kuupongeza uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa hatua iliyofikiwa na kuliweka jiji kwenye mandhari ya kuvutia.” Amesema Dkt.Biteko


Ameongeza kuwa, Mkutano wa M300 umekuwa kivutio ambacho kimewashawishi Wakuu wa Taasisi nyingi za Kimataifa kuonesha nia ya kushiriki mkutano huo mkubwa katika Sekta ya Nishati.


Ameeleza kuwa, Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo kumetokana na Diplomasia nzuri ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambayo imezidi kuimarisha uhusiano wa Tanzania kimataifa na kupelekea WB na AfDB kuichagua Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano.


Ametaja sababu nyingine ya Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo muhimu ni mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya Nishati huku akitoa mfano wa mafanikio katika usambazaji wa nishati vijijini.


Amesema vijiji vyote nchini 12,318 vimesambaziwa umeme na Vitongoji 34,000 kati ya 64,274 vilivyopo nchini, tayari vimesambaziwa umeme.


Ametaja baadhi ya faida za mkutano huo kuwa ni pamoja na kuongezeka idadi ya Watanzania watakaounganishwa na umeme ifikapo mwaka 2030 hadi kufikia milioni 13.5 kutoka milioni 5.2 ya sasa.


Ameongeza kuwa, katika mkutano huo nchi zitasaini mikakati ya kuharakisha kusambaza umeme kwa wananchi ambayo itaeleza kwa kina hatua gani zitachukuliwa chini ya mwavuli wa WB na AfDB.


Ameongeza kuwa, faida nyingine zitakazotokana na mkutano wa M300 ni kuongezeka kwa fursa za uwekezaji, kuimarisha biashara na kuongeza heshima ya nchi katika Duru za kimataifa na Tanzania kuwa Taifa linalopigiwa mfano kwenye nyanja mbalimbali.


Dkt. Biteko ametoa wito kwa Watanzania kuupokea kwa mikono miwili mkutano huo ambao kwa kiasi kikubwa unazidi kumheshimisha Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Watanzania kwa ujumla.


Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuendelea na hali ya amani na utulivu kuelekea katika mkutano huo wa kihistoria kutoka nchi ipige hatua kwenye Sekta ya Nishati kwani ni Mkutano Mkubwa wa kwanza kufanyika.


Vilevile ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuutangaza Mkutano huo kwa Watanzania ili waufahamu kwa kina na kufahamu fursa zilizopo.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema maandalizi ya kupokea ugeni huo yako katika hatua za mwisho.


Amesema ili kufanikisha mkutano huo, baadhi ya mitaa itafungwa ili kuwezesha maonesho na utalii wa ndani ikiwa ni pamoja na utalii wa tiba.


Share:

ZIARA YA DC MTATIRO KIJIJI KWA KIJIJI MOTO! YAMNG'OA MTENDAJI CHA POMBE, ATOA MAAGIZO MAZITO

Share:

Tuesday, 14 January 2025

Tanzia : MKUU WA WILAYA YA MBOZI ESTER MAHAWE AFARIKI DUNIA



Mkuu wa wilaya ya Mbozi mkoani Songwe Mhe. Ester Mahawe amefariki dunia leo Januari 14, 2024 kwenye hospitaki ya KCMC mkoani Kilimanjaro alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kupitia mitandao ya kijamii , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika ujumbe ufuatao:

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe, Bi. Esther Alexander Mahawe, kilichotokea leo tarehe 14 Januari, 2025 katika hospitali ya KCMC, mkoani Kilimanjaro. 

Nawapa pole familia ya marehemu, Mkuu wa Mkoa wa Songwe, ndugu, jamaa na wote walioguswa na msiba huu. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha ya Bi. Esther na utumishi wake kwa umma ambao uliongozwa na uchapakazi hodari, ukweli na msimamo thabiti katika utendaji. 

Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi. 

Amina."

Share:

Video Mpya : MITINJE KAYUNGILO - MALUHO

Share:

AJALI YA LORI YAUA WATU 11 WAKISHUHUDIA AJALI NYINGINE, 13 WAJERUHIWA TANGA

 

Watu 11 wamefariki dunia na wengine 13 kujeruhiwa baada ya lori lililokuwa limebeba saruji kufeli breki na kugonga watu mashuhuda wa ajali ya gari dogo aina ya Coaster Tata katika kijiji cha Changombe, kata ya Segera, wilayani Handeni, mkoa wa Tanga.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Burian, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo akisema kuwa tukio hilo ni la kusikitisha kwa sababu waliofariki walikuwa wakijaribu kuwasaidia majeruhi wa ajali ya awali.

Kwa mujibu wa taarifa, lori hilo lenye namba za usajili T 680 BQW, likiwa linatokea Tanga, lilishindwa breki na kuwakumba watu waliokuwa pembezoni mwa barabara, kusababisha vifo vya watu 11 papo hapo na kujeruhi wengine 13.

Mkuu wa Mkoa ametoa pole kwa familia za marehemu na kuwatakia nafuu ya haraka majeruhi wote. Aidha, ametoa wito kwa madereva na wamiliki wa vyombo vya moto kuhakikisha magari yao yanakuwa katika hali nzuri ya kiufundi ili kuepusha ajali za namna hii.




Share:

Monday, 13 January 2025

HUYU NDIYE SAID LUGUMI, HISTORIA YAKE YA KWELI

 

Bilionea Saidi Lugumi sio jina geni Nchini, huyu sio mtoto wa mjini, sio Kiongozi na huenda kwenye familia yake hakuna historia ya mwanasiasa zaidi ya marehemu baba yake ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Magu.

Ni kijana kutoka Jijini Mwanza, Wilaya ya Magu mwenye Elimu ya darasa la Saba pekee, hana Elimu ya kutisha lakini usishangae ukisikia Lugumi ni Daktari (PhD) udaktari wa heshima kwakuwa anastahili hilo kwa kiwango kikubwa kutokana na namna anavyojitoa kwa jamii.

Tofauti na Wafanyabiashara wengine, ukisikia habari zao mitandaoni ni mambo tofauti lakini kwa Lugumi imekuwa tofauti sana ambapo mwishoni mwa mwaka 2024 mwezi Disemba aliibua mjadala katika mitandao ya kijamii baada ya kuonesha sehemu ya nyumba anazojenga kwaajili ya watoto Yatima anao walea katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Bilionea Saidi Lugumi anaeleza kwa sasa kuna watoto yatima zaidi ya 800 kutoka maeneo tofauti ya jiji la Dar es Salaam ambao anawahudumia kwa kila kitu ikiwemo chakula, mavazi, malazi, elimu, afya l, na hiyo inatokana na wito alionao kutoka kwa Mwenyezi Mungu na si vinginevyo.

Desemba 25, 2024 katika kusherekea sikukuu ya Krismasi alijumuika na watoto wake mtaa wa Msufini, wilaya ya Kinondoni kwa ajili ya kushirikinao dua na kisomo maalum sambamba na kushirikinao chakula cha pamoja alichokiandaa kwa ajili yao

Sambamba na hilo, katika kuboresha makazi yao Lugumi alisema kwa sasa anajenga majengo sita (6) ya ghorofa huku malengo yakiwa ni kujenga ghorofa nane (8) kwa ajili ya watoto hao, kwenye maeneo tofauti ya jiji hilo, ambapo jengo moja kati ya hayo linajengwa eneo hilo la Msufini.

"Hii ni nyumba yao (jengo la ghorofa), nyumba kama hizi ziko sita (6) lakini tumeanzia hapa kwa sababu nyumba hii iko mbioni kumalizika, chakula tutakula na wao hapa, na wenyewe wameweza kuwa na furaha kuona sehemu yao, kila kituo kinatarajiwa hakitazidi kukaa watoto 100, unaona nyumba kama hii ni watoto 100 tu na kwa namna Mungu anavyonijaalia nitazidi kuongeza, kwa sasa tumepanga nyumba kama tatu na nyingine tumenunua lakini bado hazitoshi", alisema Lugumi.

Lugumi anaeleza kuwa alianza kulea watoto hao na alipata maono hayo mnamo mwaka 2013 ambapo ni takribani miaka 12 sasa na amesisitiza kuwa yuko tayari apoteze kitu chochote lakini sio kuwapoteza watoto hao.

Kila Kituo kuna madaktari na maafisa Ustawi wa Jamii ambao wapo kwaajili ya kuwahudumia watoto hao ukiachana na suala la mavazi na malazi watoto hao wanasomeshwa mpaka ngazi za juu za Elimu na kuendelea na maisha yao na wengine hupatiwa mitaji ya Biashara huku wengine wakianza ajira zao.

Lugumi anasimulia kuwa sio kwamba siku zote wanapitia raha na wanae, kuna vipindi hali inakuwa sio nzuri na wanalazika kula wanachokipata.

Viongozi wa Dini wamepongeza juhudi za Lugumi, akiwemo Mtume Boniface Mwamposa 'Buldoza' wa Kanisa la Inuka Uangaze amempongeza mfanyabiashara Lugumi kwa kujenga maghorofa matano kwa ajili ya watoto yatima.

“Ninampongeza Lugumi, ni jambo jema lenye roho ya kumcha Mungu,” alisema Mwamposa.

Majengo hayo, yanayotarajiwa kukamilika Machi mwaka huu, yatanufaisha zaidi ya watoto 800 wenye mahitaji maalum jijini Dar es Salaam.

Saidi Lugumi ni mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania, anayejulikana zaidi kama Mkurugenzi Mtendaji wa Lugumi Enterprises Limited.

Lakini pia kupitia kampuni ya Tactical Defencs (T) Limited ni wakala wa makampuni makubwa ya silaha duniani.

Lakini pia, kampuni yake inajihusisha na huduma za uchapishaji wa vifaa vya ki-ofisi, teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT) na hajawahi kuwa na Biashara nyingine tofauti na ilivyodaiwa kuwa anajihusisha na uuzaji wa madawa ya kulevya.

Maisha yake binafsi Lugumi amekuwa sio Mtu wa kuweka wazi sana familia yake, lakini amewahi kukiri kuwa na watoto Saba (7) ambao ni wa kwake wa kuwazaa na wapo sehemu tofauti tofauti, huku akikanusha taarifa za kuwahi kumuoa binti aliyedaiwa kuwa ni familia ya aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, Saidi Mwema.

Share:

Video Mpya : SAYI KAPEMBE - MPOGOMI

Share:

SERENGETI BYTES YATOA ORODHA YA WATANZANIA 100 WALIOCHOCHEA MABADILIKO KATIKA MWAKA 2024

 
Kampuni ya Serengeti Bytes imetangaza rasmi toleo la pili la jarida la Watanzania 100 Wanaochochea Mabadiliko (100 Tanzanian Changemakers 2024), ambalo linahusisha taarifa za watanzania wanaoleta mabadiliko chanya katika sekta mbalimbali nchini.

 Jarida hili linaangazia juhudi za viongozi, wavumbuzi, wabunifu, wajasiriamali, na wanaharakati wanaochangia maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kiteknolojia nchini Tanzania.

Toleo hili la pili linajumuisha wasifu wa watu 100 walioleta mchango mkubwa katika nyanja tofauti. Wakurugenzi wa Serengeti Bytes wanasema jarida hili si tu njia ya kuwaenzi bali pia jukwaa la kuhamasisha Watanzania kuungana katika kujenga taifa lenye ustawi.

“Orodha ya mwaka huu inaonyesha utofauti wa vipaji na kazi za kipekee zinazofanywa na Watanzania kutoka sehemu mbalimbali,” amesema Kennedy Mmari, Mkurugenzi Mtendaji wa Serengeti Bytes. “Hawa ni watu wanaoonesha kwa vitendo kuwa mabadiliko yanawezekana kupitia bidii, ubunifu, na kujituma.”

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Serengeti Bytes, Michael Mallya, ameongeza kwa kusema: “Kila aliyeingia katika orodha hii ni ushuhuda wa nguvu ya maono na kushirikiana. Kupitia hadithi zao, tunalenga si tu kusherehekea mafanikio yao bali pia kuhamasisha ushirikiano wa kitaifa katika kuchochea maendeleo.”

Jarida hili limeandaliwa kwa umakini kupitia mchakato ulioshirikisha mapendekezo ya umma, tathmini za wadau, na utafiti wa kina. Kila hadithi inaelezea mchango wa wahusika katika kuboresha maisha ya watu na kujenga jamii zenye ustawi endelevu.

Kwa mujibu wa Serengeti Bytes, mpango huu unalenga zaidi ya kusherehekea mafanikio ya mtu mmoja mmoja, bali pia kuhamasisha mshikamano wa kitaifa. “Jarida hili ni njia mojawapo ya kuleta pamoja fikra na maono ya mabadiliko. Tunataka kila Mtanzania atambue kuwa anaweza kuchangia kujenga taifa lenye nguvu na fursa kwa wote,” ameongeza Mmari.

Orodha hii imegawanywa katika makundi tisa ikigusa sekta mbalimbali ikiwemo Serikali na Uongozi wa Umma, Biashara na Ujasiriamali, Teknolojia na Uvumbuzi, Sekta ya Azaki na Maendeleo, Sekta ya Tafiti na Taaluma, Vyombo vya Habari, Michezo, Sanaa na Burudani, Afya na Ustawi pamoja na Wadau wa Maendeleo wa Kimataifa. 

Katika tolea la mwaka 2024 tumeongeza kipengele cha Wadau/Marafiki wa Maendeleo ya Tanzania kwa lengo la kutambua mchango mkubwa wa watu ambao si raia wa Tanzania lakini wamekuwa na mchango unaostahili kutambuliwa kwa upekee.” ,amehitimisha Mallya. 

Jarida linapatikana kwa njia ya kielektoniki. Kwa maelezo zaidi au kupata nakala yako, tembelea https://changemakers.co.tz/ au wasiliana na Serengeti Bytes kupitia hello@serengetibytes.com.

Share:

Sunday, 12 January 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 13, 2025

Share:

BALOZI NCHIMBI NA MONGELLA WAMTEMBELEA MZEE MANGULA


KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiambatana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Ndugu John Mongella, amemtembelea kwa ajili ya kumsabahi na kumjulia hali Mzee Philip Japhet Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM Mstaafu (Bara), nyumbani kwake Msalato, Dodoma, leo Jumapili tarehe 12 Januari 2025.

Baada ya mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye maktaba ya Mzee Mangula, Balozi Nchimbi pia alipata wasaa wa kuchukua picha yeye mwenyewe kwa njia ya 'selfie', kama inavyoonekana pichani.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger