Tuesday, 7 January 2025

MBIVU MBICHI NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM KUJULIKANA JANUARI 18 AU 19




Na Selina Kusenha, Dodoma

BAADA ya kimya cha muda mrefu kuhusu nani anachukua nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM) jibu limepatikana ambapo anatarajiwa kupatikana kati ya January 18 au 19 mwaka huu.

Hatua hii ni mara baada ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Abdulrahman Kinaana kutangaza kustaafu kwenye nafasi hiyo tangu Julai mwaka jana kwa madai ya kutaka kupumzika ambapo Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan aliliridhia ombi lake.

Akizungumza leo Januari 7,2025 Jijini Dodoma, Katibu wa NEC,Itikadi , Uenezi na Mafunzo wa Chama hicho Amos Makala ameeleza kuwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti huwa haigombewi wala kujazwa fomu bali hutokana na mapendekezo ya Mkutano Mkuu na halmashauri kuu ya CCM.

"Niwaombe wanachama watu kuachana na taharuki zinazoendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mrithi wa Makumu Mwenyekiti wa chama Abdulahman Kinana, nafasi hii haigombewi ila inapendekezwa, " ameeleza Makala.
Makala amewaambia waandishi wa habari kuwa kwa sasa hakuna mchakato wowote wa mrithi wa nafasi hiyo ambaye atapatikana baada ya mapendekezo ya jina katika kikao cha Kamati kuu na Halmashauri kuu Taifa.

" Wale waliokuwa wakibashiri mrithi wa Kinana muda huo haupo badala yake mrithi tutampata kwa jina kupendekezwa kwenye vikao na tayari maandailizi yote yanaendelea kufanyika kupitia Katibu mkuu wa Chama chetu Emmanuel Nchimbi, hivyo tuache taharuki CCM kinaendeshwa kwa Katiba na utaratibu,"amesema

Wakati huo huo Katibu Mwenezi huyo ametoa taarifa juu ya uwepo wa Mkutano Mkuu CCM January 18 hadi 19 2025 ambapo ameeleza kuwa Mkutano huo utaendana na vikao vya Kamati kuu na Halmashauri kuu Taifa.





Share:

Ngoma Mpya : NELEMI MBASANDO - WAWEKEZAJI

 

Share:

Monday, 6 January 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 7,2025

 

Magazeti ya leo
 
       
Share:

DUH! MREMBO ATOA KALI YA MWAKA MTANDAONI

Kuna siku mrembo mmoja aliwashangaza marafiki zake wengi kwenye mitandao ya kijamii baada ya kusema kuwa tangu aolewe na mumewe, hajawahi kumuita jina lolote tamu kwa ajili ya kunogesha mapenzi yao. 

Anasema walikuwa wanaishi tu kwenye ndoa lakini alikuwa na wasiwasi kutokana mumewe amekuwa akimtenga kutokana na ukweli kwamba wawili hao walikuwa wakiishi kwenye ndoa ya sogea tuishi ambayo haifuati taratibu za kidini na kimila. 

Kama alivyosema, siku zote alitamani kwamba mume wake siku moja angemwita majina kama "asali wa moyo" lakini kwa jinsi mambo yalivyokuwa yakienda, aliona angesubiri kwa miaka mingi kuona jambo hilo likitokea. 

"Tulikuwa kwenye ndoa kwa takribani miaka sita na hakuwahi kuniita jina lolote tamu. Nilikuwa nikijitahidi kadri niwezavyo lakini mume wangu alionekana kuwa mtu asiye na akili ya kujiongeza. Alikuwa akiniita kwa majina yangu kama yanavyoonekana kwenye kitambulisho changu." alisema. 

Anasema hali hii ilifanya ndoa yao kuwa ya kuchosha sana lakini kupitia mtandao wa kijamii, alifahamu kuhusu huduma za Dr Bokko ambaye ni mtaalam wa tiba asilia katika eneo zima la Afrika Mashariki na Kati. 

Mrembo huyo alipitia baadhi ya shuhuda kwenye tovuti yake na kugundua kuwa Dr Bokko ameokoa ndoa nyingine zenye hali mbaya kama yake, ndipo akaamua kuwasiliana naye kwa ajili ya huduma yake.  

Huko kwa Dr Bokko alipewa maneno ya mapenzi yenye nguvu ambayo yalikusudiwa kuamsha mapenzi katika ndoa yake. Baada ya muda anasema aliona mabadiliko makubwa kwa mume wake. Aligeuka kuwa mtu wa kimapenzi tofauti na hapo awali. 

Sasa anamwita majina matamu na pia akabadilika na kuwa mtu wa kimapenzi, jambo ambalo anasema liliifanya ndoa yao kuwa tamu ajabu. Wasiliana na Dr Bokko kwa namba +255618536050 ili nawe upate utatizo wa changamoto yako katika mapenzi. 

Mwisho.

Share:

VYANDARUA 1,542,836 VYENYE DAWA KUSAMBAZWA KATIKA MKOA WA SHINYANGA

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Jumla ya vyandarua 1,542,836 vyenye dawa vinatarajiwa kusambazwa katika mkoa wa Shinyanga mwezi huu, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali na wadau wake kupambana na ugonjwa wa malaria. 

Taarifa hiyo imetolewa leo Januari 6,2025 wakati wa kikao kazi cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga juu ya kampeni ya ugawaji wa vyandarua vyenye dawa Mkoani Shinyanga.

Katika kikao hicho waandishi wa habari wamepitishwa katika mada mbalimbali ikiwemo hali ya malaria nchini Tanzania na mkakati wa kinga dhidi ya malaria, kampeni ya ugawaji wa vyandarua mkoani Shinyanga, mbinu bora za kuwasilisha taarifa za malaria, taarifa muhimu kwa jamii juu ya kampeni ya ugawaji vyandarua na mchango wa vyombo vya habari katika utoaji wa taarifa za kampeni ya ugawaji vyandarua.

Vyandarua hivi vitasambazwa kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo, huku lengo likiwa ni kupunguza maambukizi ya malaria.

Usambazaji huu utakuwa sehemu ya mpango wa kitaifa wa kupunguza vifo vinavyosababishwa na ugonjwa wa Malari, ambao bado ni changamoto kubwa katika baadhi ya mikoa ya Tanzania.

Vyandarua vyenye dawa vimekuwa moja ya njia bora za kudhibiti maambukizi ya malaria. 

Serikali ya Tanzania inatarajia usambazaji huu utafikia kaya nyingi zaidi na hivyo kuokoa maisha ya wananchi. Usambazaji huu utafanyika kwa ushirikiano wa karibu na Serikali za Mitaa, na kwamba vyandarua vitasambazwa kwa usawa na kwa kasi ili watu wa maeneo ya vijijini wasiachwe nyuma.

Kwa sasa, wananchi wanahimizwa kutumia vyandarua vyenye dawa, na pia kuendelea kuchukua tahadhari nyingine kama vile kupiga dawa za kuua mbu katika makazi yao na kujiepusha na maeneo yenye maambukizi makubwa.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger