Wednesday, 18 December 2024

BILIONEA MULOKOZI ANUNUA NDEGE BINAFSI, ATUA MANYARA



Na Ferdinand Shayo ,Manyara .


Mkurugenzi wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited David Mulokozi amenunua ndege binafsi aina ya Helkopta ambapo ametua kwa mara ya kwanza katika Uwanja wa Tanzanite Kwaraa Stedium akiwa ameambatana na familia yake.

Mulokozi anaingia miongoni mwa Watanzania wachache wanaomiliki ndege binafsi ambapo amesema kuwa kampuni yake imekua ikikua siku hadi siku na kuonyesha vitu vya tofauti .

“Hakuna Mtu alitegemea kuwa Manyara kunaweza kuwa na helkopta ni mambo mengi yanaanza ,Wafanyabiashara wengi wanajifunza, kila mtu anaruhusiwa kumiliki chombo hichi inawezekana” Anaeleza David Mulokozi.

Amesema kuwa ndege hiyo itasaidia katika utoaji wa huduma katika kampuni yake inayojihusisha na uzalishaji wa vinywaji changamshi.

Mulokozi ameiomba serikali ijenge kiwanja cha ndege ili ndege nyingi zaidi ziweze kutua mkoani Manyara .

Kwa upande wao wakazi wa mkoa wa Manyara waliofika na kushuhudia helkopta hiyo ikitua akiwemo Melkiori Enyasi anaelezea furaha yake baada ya kuona ndege binafsi ya kwanza ya mkazi wa mkoa wa Manyara ikitua katika ardhi nyumbani.

Enyasi amempongeza Mulokozi kwa kununua ndege binafsi itakayochochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi .




Share:

REA YATENGA FEDHA KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI TANGA

Na Hadija Bagasha Tanga,

WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) imetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa wa miradi ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ikiwemo gesi katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji lengo likiwa ni kuwezesha huduma ya nishati safi ya kupikia na hatimaye kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa inayosababisha mabadiliko ya tabia Nchi.

Hivyo kupitia mpango huo itatoa mitungi ya gesi 26,040 kwa wilaya nane za mkoa wa Tanga zitakazokuwa na thamani ya shilingi milioni 455.7 ambazo zitagawiwa wananchi kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya uharibifu wa mazingira unaotokana na watu kutumia nishati ya mkaa.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa uuzwaji mitungi ya gesi ya LPG ya uzito wa kilo sita kwa bei ya ruzuku katika mkoa wa Tanga Mkurugenzi wa Teklonojia za Nishati Jadidifu na Mbadala, wa REA Mhandisi Advera Mwijage katika hafla fupi ya kumkabidhi mradi huo Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian, alisema kila wilaya za mkoa huo utapatiwa mitungi 3,255.

Alisema mitungi hiyo ambayo wananchi watalazimika kununua kwa kiasi cha sh, 17,500 na serikali itaongeza sh. 17,500 na msambazi katika mkoa wa Tanga itakuwa kampuni ya Manjis ambao wataisambaza kwa wakala watakaowachagua hasa katika maeneo ya vijijini.

Alisema Tanzania ina uwezo wa kuhakikisha upatikanaji wa nisahati safi, bora na rafiki wa mazingira katika maeneo ya vijijini, lakini pia idadi kubwa ya watu wanatumia mazao yanayotokana na misitu kupikia hivyo kuleta uharibifu mkubwa wa mazingira.

Mhandisi Mwijage alisema utafiti uliofanywa mwaka 2016 unakadiriwa kuwa watu 33,024 hufariki dunia kabla ya wakati kila mwaka ambayo ni sawa na asilimia 8.49 ya vifo vyote nchini kutokana na magonjwa ambayo yanachangiwa na uchafuzi wa hewa ndani ya nyumba wakati wa upikaji kwa kutumia nishati isiyo safi na salama.

“Hivyo serikali kupitia wakala wa nishati vijiji REA umetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ikiwemo gesi LPG katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji kupitia mradi wa ufadhili unaotegemea matokeo (RBF) lengo ni kukukuza, kuchochea, kuwezesha na kuboresdha upatikanaji wa nishati safi na salama.

Mhandisi Mwijage alisema utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na malengo ya makakati wa Kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia ya mwaka 2024-2034 uliozinduliwa Mei 2024 na Rais Dkt Samia Sukuhu Hassan  ambao unalenga kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia kufikia asilimia 80 ya Watanzania wote wanaotumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.

Akipokea mradi huo Mkuu wa mkoa wa Tanga, Balozi Burian wa unaendelea kumpongeza Rais Dkt Samia kwa kuendelea kuwa kinara wa maono baada ya kuzindua mpango huo ambao utasaidia wananchi kutunza mazingira kwa ajili ya nchi. 

Alisema mkoa huo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wametoa elimu kwa wananchi ili waweze kuachana na matumizi ya nishati za kuni na mkaa badala yake waweze kutumia nishati safi na salama na wameweka mpango kuhakikisha ziara ya rais hivi karibuni mkoani hapa watagawa mitungi hiyo kuendelea kuwahamasisha wananchi matumizi ya nishati hiyo.

Hata hivyo, Mkuu wa mkoa huyo alitoa rai kwa REA kuhakikisha wanatoa elimu kwa vijana ili waweze kutengeneza majiko makubwa ya gesi ambayo yatatumika na wananchi hasa mamantilie ambao mitungi ya gesi inayosambazwa haiwezi kukidhi mahitaji yao ya kupika chakula na mboga.

“REA kaeni na taasisi hizi,  vijana wetu hawana ajira wabuni na watengeneze majiko yatakayowasaidia mamantilie kuweza kupika chakula na mboga kwa wakati mmoja, lakini pia hakikisheni mnatengeneza mitungi ya gesi ya lita tatu ili wananchi wetu vijijini waweze kumudu kununua,” alisema Balozi Burian.



Share:

Tuesday, 17 December 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 18, 2024

Share:

WANANCHI WACHOSHWA NA AHADI, WAAMUA KUCHONGA BARABARA WENYEWE KWA SOFI MHONGOLO

 

Wananchi wa mtaa wa Sofi kata ya Mhongolo wakichimba mtaro ili kupunguza maji yanayotuama katika eneo hilo yanayosababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya kata ya Mhongolo na kata ya Busoka Manispaa ya Kahama.


NA NEEMA NKUMBI -KAHAMA


Wakazi wa mtaa wa Sofi, Kata ya Mhongolo, Manispaa ya Kahama, wamechukua hatua ya kujitolea kufanya marekebisho ya barabara inayounganisha Sofi, Mhongolo na Busoka baada ya kukumbwa na changamoto ya mafuriko na ukosefu wa mawasiliano wakati wa masika.


Wananchi hao wameamua kuchangishana michango ya fedha na wengine kujitolea nguvu zao ili kuchimba mtaro na kununua mawe kwa lengo la kuepuka adha za mafuriko yanayozuia mawasiliano katika eneo hilo.


Mkazi wa Sofi, Neema Toyi, amesema kuwa barabara hiyo imekuwa kikwazo kikubwa kwao kila mwaka, hasa wakati wa masika, ambapo watoto wanashindwa kwenda shule na akina mama wajawazito wanapata ugumu wa kufika hospitali.

"Hii barabara inatutesa sana wakati wa mvua hata kama mvua haitanyesha katika mtaa wetu maji hutoka huko mjini na kutuvamia huku, tunapata shida sana watoto wanashindwa kuvuka kwenda shule, na ukinitazama mimi hapa na hali yangu(mjamzito) ninapata wasiwasi kama nikipata uchungu nitavukaje kwenda hospitali serikali na itutazame itujengee daraja hali ni mbaya sana", amesema Neema.

Beatus Mswati, mkazi mwingine, amekiri kwamba juhudi zao za kutengeneza barabara hiyo ni muhimu kwa ajili ya usalama wa familia zao na kuendelea na shughuli za kiuchumi.

Beatus amesema," Tumeamua kujitoa wenyewe kutengeneza barabara hii ili kuokoa maisha yetu na watoto wetu, tunapata shida wakati wa mvua tunashindwa kupitisha biashara zetu tutawezaje kulipa kodi? Maisha yetu ni magumu sana tunashindwa kukaa kwa amani kwa sababu ya maji yanayojaa hapa".

Mathias Mwita amesema kuwa licha ya juhudi za viongozi wakiwemo Diwani na Mbunge kutembelea eneo hilo, tatizo la barabara halijapata ufumbuzi wa kudumu hivyo, wananchi wameamua kujitolea kuungana na kuchangishana fedha ili kurekebisha barabara hiyo muhimu kwa maisha yao.


Mwenyekiti wa Mtaa wa Mhongolo, Emanuel Nangale, amepongeza juhudi za wananchi na kuongeza kuwa wamekuwa wakishirikiana na TARURA kuhakikisha barabara hiyo inapata bajeti.


"Sisi kama serikali ya mtaa tunatambua tatizo hilo eneo hilo ni korofi sana na tumepambana kuhakikisha barabara inapata bajeti na ikapata bajeti ya serikali kupitia TARURA, TARURA walikuja wakakwangua barabara ila hawajaweka changarawe na daraja ila tumewasiliana na Diwani wa Kata ya Mhongolo amesema analifuatilia kwa karibu", amesema Nangale.


Meneja wa TARURA Kahama, Joseph Mkwizu, amesema kuwa barabara hiyo ilikuwa na bajeti katika mwaka wa fedha 2023/2024 na kwamba Diwani ametoa maombi ya kipaumbele kwa eneo la Sofi katika bajeti ya mwaka 2025/2026 ili kutatua changamoto hiyo.

Mkwizu amefafanua, "Barabara hiyo inayounganisha Mhongolo Sofi na Busoka ilikuwa na bajeti katika mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo tulijenga kalavati mbili, kuchoronga barabara km 4.7 na kuweka changarawe (moramu) km 1.3 katika eneo la Busoka iliyo gharimu shilingi milion 63.

Barabara inayounganisha Sofi na Mhongolo ni muhimu kwa usafiri wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Bomani na Sekondari ya Nyashimbi, pamoja na wakazi wa eneo hilo katika shughuli zao za kilimo na biashara, Kukosekana kwa barabara hiyo kunaleta hasara kubwa kwao, na hivyo ni jambo la dharura kwa serikali kushughulikia tatizo hili kwa haraka.
Neema akielezea hali ngumu wanayokutana nayo wananchi wa mtaa wa Sofi kutokana na mvua, ambapo barabara inafurika maji kutoka mjini na Watoto wanashindwa kuvuka kwenda shule na hata wagonjwa, wakiwemo wajawazito kama Neema, wanapata shida kubwa kufika hospitali, huku akisisitiza kuwa serikali inapaswa kuchukua hatua ya dharura kuwajengea daraja ili kupunguza madhila haya.
Neema akielezea hali ngumu wanayokutana nayo wananchi wa mtaa wa Sofi kutokana na mvua, ambapo barabara inafurika maji kutoka mjini na Watoto wanashindwa kuvuka kwenda shule na hata wagonjwa, wakiwemo wajawazito kama Neema, wanapata shida kubwa kufika hospitali, huku akisisitiza kuwa serikali inapaswa kuchukua hatua ya dharura kuwajengea daraja ili kupunguza madhila haya.
Meneja wa TARURA Kahama, Joseph Mkwizu, akielezea juhudi za kuboresha barabara inayounganisha Mhongolo Sofi na Busoka. 


Mathias Mwita akielezea juhudi za viongozi kama Diwani na Mbunge kutembelea eneo hili, lakini tatizo la barabara halijapata ufumbuzi wa kudumu.

Wananchi wa mtaa wa Sofi wakichimba mtaro ili kupunguza maji yanayotuama katika eneo hilo yanayosababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya kata ya Mhongolo na kata ya Busoka
Wananchi wa mtaa wa Sofi wakichimba mtaro ili kupunguza maji yanayotuama katika eneo hilo yanayosababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya kata ya Mhongolo na kata ya Busoka
Wananchi wa mtaa wa Sofi wakichimba mtaro ili kupunguza maji yanayotuama katika eneo hilo yanayosababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya kata ya Mhongolo na kata ya Busoka
Wananchi wa mtaa wa Sofi wakichimba mtaro ili kupunguza maji yanayotuama katika eneo hilo yanayosababisha kukatika kwa mawasiliano kati ya kata ya Mhongolo na kata ya Busoka

Share:

ZIARA YA SEKTA YA MAJI KOREA KUSINI YAFANIKISHA MRADI WA MAJITAKA DAR ES SALAAM

 


Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amesema ziara iliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan nchini Korea Kusini imetengeneza mahusiano mazuri na kuchangia kupatikana kwa fedha kwa ajili ya mradi mikubwa wa majisafi na usafi wa mazingira.

Akizungumza baada ya kushuhudia utiaji saini wa Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa Mfumo wa Kutibu Majitaka Katika Jiji la Dar Es Salaam kati ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam ( DAWASA) na Mkandarasi kampuni ya Kolon Global Corporation kutoka inchini Korea Kusini kwa ufadhili wa Korea Exim Bank ikiwa ni siku chache baada ya Ziara ya Waziri Aweso na timu nzima ya sekta ya Maji Nchini Korea Kusini.

"Baada ya kupata nafasi ya kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan alifanya ziara inchini Korea Kusini baadae na mimi nikapata nafasi safari hizo zimepelekea tumepata zaidi ya Dola za kimarekani zaidi ya milioni 240 kwa ajili ya uwekezaji kwenye miradi ya usafi wa Mazingira" amesema Waziri Aweso

Ameongeza kuwa hiyo inathibitisha mahusiano mazuri na urafiki wa thamani uliopo baina ya nchi hizi mbili.

Katika hatua nyingine Waziri Aweso amemshukuru Balozi wa Korea Kusini nchini Mhe. Eunju Ahn kwa kuwa sehemu kubwa ya kusaidia kupatikana kwa ufadhili wa miradi hiyo.

Zoezi hilo la utiaji saini limeshuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kwenye kikao kazi cha mafunzo kwa wenyeviti wa Serikali za mitaa ambapo alisisitiza ushirikishwaji wa viongozi kuanzia ngazi za mitaa kwani ni muhimu kwa wao kuwa na taarifa sahihi ili kurahisisha uwasilishaji kwa wananchi.

Naye, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Mkama Bwire akitoa maelezo wa mradi amesema mradi utahusisha ujenzi wa mtambo mkubwa wa kisasa wa kuchakata majitaka eneo la Buguruni, Ujenzi wa vituo viwili vikubwa vya kusukuma majitaka eneo la Gymkana na Jangwani, 

Ameongeza kuwa utahusisha pia kazi ya ulazaji wa bomba kubwa kwa umbali wa zaidi ya kilomita 52 na ukarabati wa mfumo uliopo wa majitaka, Mradi unategemea kunufaisha wakazi 733,865 katika Wilaya za Ilala na Kinondoni.

Mradi huo utagharimu zaidi ya dola milioni 90 sawa na bilioni 170 fedha za kitanzania mpaka utakapokamilika ambapo Waziri Aweso amesema itakuwa suluhisho kubwa kwa changamoto za maji katika hilo kukamilika kwake kutaongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za usafi wa mazingira kwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam kutoka asilimia 45 ya sasa hadi asilimia 65"
Share:

HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUINGIA KIDATO CHA KWANZA, 2025, SHULE WALIZOPANGIWA

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger