Wednesday, 4 October 2023

SHIRIKA LA ELIMU KIBAHA LAANZA KUTOA MAFUNZO KWA VYUO VINGINE MKOANI PWANI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko akifungua rasmi mafunzo ya kozi za muda mfupi kwa wanafunzi wa Chuo cha Biashara Kibaha. Mafunzo hayo yanatolewa katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha– FDC). Kutoka kulia ni mmiliki wa Chuo cha Biashara Kibaha, Prof. Lemayon Melyok akifuatiwa na Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha-FDC), Bw. Joseph Nchimbi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Biashara Kibaha Bi. Nembris Lucas Kimbele akifuatiwa na Mratibu wa Mpango wa AHADI kutoka World Vision, Bi. Eveline Sanga.


*******************

Shirika la Elimu Kibaha (KEC) limepokea wanafunzi wapya 46 kutoka katika Chuo cha Biashara Kibaha (KIB) kwa ajili ya kuwapatia mafunzo ya kozi za muda mfupi wa miezi miwili.

Katika kipindi cha miezi miwili Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha- FDC) kitatoa mafunzo ya urembo na ususi, hotelia, ufundi magari, mapambo, ushonaji na ubunifu wa mitindo kwa wanafunzi wa Chuo cha Kibaha Institute of Business.

Akifungua mafunzo hayo, mgeni rasmi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko amekishukuru Chuo cha biashara Kibaha (KIB) kwa kuchagua Shirika la Elimu Kibaha kupitia Kibaha-FDC, kwa kuwapeleka wanafunzi wa KIB kupata mafunzo Kibaha-FDC.

Bw. Nnko aliwashauri wanafunzi wa KIB kufanya mafunzo kwa vitendo ili kujiimarisha wakati wakipatiwa mafunzo hayo lakini pia waweze kujiajiri na kuajiri watu wengine baada ya kumaliza mafunzo hayo.

“Nidhamu ni sehemu ya mafanikio, nidhamu itawasaidia kokote mtakapokuwa, sisi tumejipanga kutoa mafunzo bora,” amesema Bw. Nnko.

Mmiliki wa Chuo cha Biashara Kibaha (KIB), Prof. Lemayon Melyok amekishukuru Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha kwa kukubali kuwapokea wanafunzi wa chuo chake.

“Sisi tuliona kuwa wanafunzi wetu wakija kusoma hapa Kibaha watakuwa salama kwani watapata elimu ya nadharia na vitendo,” amesema Prof. Melyok.

Mratibu wa Mradi wa AHADI wa World Vision, Bi. Eveline Sanga amewataka wanafunzi hao kuwa makini darasani kwani mafunzo hayo yatawasaidia kupata kipato ambacho kitawasaidia kuboresha maisha yao.

Mwanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha, Asha Njoroka aliwakaribisha wanafunzi wa KIB na kuwataka kuwa na ushirikiano wakati wa mafunzo hayo.

Naye, mwanafunzi wa KIB, Rosemary Emily aliahidi kutoa ushirikiano kwa walimu na wanafunzi wa Kibaha- FDC.

Shirika la Elimu Kibaha kupitia Kibaha-FDC limewapokea wanafunzi 46, wakiwemo wanawake 30 na wanaume 16 ambao wanafadhiliwa na mradi wa AHADI wa World Vision wenye lengo la kuwakomboa kifikra na kiuchumi watoto wa umri wa miaka 13 mpaka 19.

Wanafunzi wakisikiliza maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha-FDC), Bw. Joseph Nchimbi (pichani hayupo) katika ufunguzi wa mafunzo ya muda mfupi yanayofanyika Kibaha-FDC.
Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha-FDC), Bw. Joseph Nchimbi akitoa maelekezo kwa wanafunzi wapya wa Chuo cha Biashara Kibaha (KIB). Kulia ni mmiliki wa Chuo cha Biashara Kibaha, Prof. Lemayon Melyok. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Biashara Kibaha, Bi. Nembris Lucas Kimbele, Mratibu wa Mpango wa AHADI kutoka World Vision, Bi. Eveline Sanga akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko.
Mmiliki wa Chuo Cha Biashara Kibaha, Prof. Lemayon Melyok akitoa shukurani kwa uongozi wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC) kwa mapokezi mazuri kwao na wanafunzi kwa ujumla. Kulia ni Mratibu wa Mafunzo katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha-FDC), Bw. Fidelis Maziku. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko akifuatiwa na Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha-FDC), Bw. Joseph Nchimbi.
Mratibu wa Mpango wa AHADI kutoka World Vision, Bi. Eveline Sanga akiwasisitiza wanafunzi kuwa nafasi waliopata ni Neema hivyo waitumie vizuri. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko na kushoto ni Mkuu wa Chuo cha Biashara Kibaha, Bi. Nembris Lucas Kimbele.
Wanafunzi wapya kutoka Chuo cha Biashara Kibaha (KIB) wakitambulishwa kwa wanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (Kibaha- FDC).
Walimu wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha na Walimu wa Chuo cha Biashara Kibaha wakitambulishwa kwa wanafunzi.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha (KEC), Bw. Anathe Nnko (alievaa kaunda suti ya bluu) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo cha Biashara Kibaha.

Share:

PROF. OREKU: TAFITI BORA, CHANZO CHA MAPATO


Tafiti na machapisho yenye kukidhi ubora wa ushindani yanaweza kukisaidia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) katika kupata ufadhili na miradi itakayosaidia kuongeza mapato ya ndani ya chuo.

Hayo yamesemwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania anayesimamia Mipango, Fedha na Utawala, Prof. George Oreku, alipokuwa akifungua mafunzo ya siku tano ya uandishi wa mapendekezo ya utafiti yenye viwango vya juu vya ubora na shindani, Oktoba 03, 2023 katika shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha, mkoani Pwani.

“Kurugenzi yetu ya Utafiti, Machapisho na Ubunifu imeundwa kwa lengo kuitumikia taasisi yetu kuhakikisha tafiti, machapisho na bunifu zinazotoka zinakuwa na ubora unaokidhi viwango vya hali ya juu. Hapa tunawajengea uwezo wahadhiri kuweza kuandika mapendekezo ya utafiti yenye viwango vya kiushindani ili maandiko yao yaweze kushinda na hili ni muhimu sana kwa kuongeza mapato ya chuo na kusaidia shughuli nyingine za kimaendeleo za chuo.” Amesema Prof. Oreku.

Aidha, aliendelea kueleza kuwa mapendekezo ya utafiti yakiandikwa vizuri Kitaalamu na kibobezi yatashinda na kuwa pia ni sehemu ya kukitangaza chuo na kukaribisha wafadhili na wadau wa maendeleo ambao watawekeza kwa kuanzisha miradi mbalimbali kwa kushirikiana na chuo.

Naye Mkurugenzi wa Utafiti, Machapisho na Ubunifu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Dkt. Harrieth Mtae, amesema mafunzo haya yanalega kuongeza ujuzi wa uandishi wa kiushindani kwa wanataaluma wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania katika kuandika mapendekezo ya utafiti na miradi itakayoshinda kutokana na ubora wake.

“Mafunzo haya ni ya awali, tunataraji kuyafanya mafunzo mengi zaidi kama haya ili washiriki wawe na uwezo wa kuandika maandiko hasa mapendekezo ya utafiti yenye ubora wa viwango vya juu na kushinda ili kupata fedha za kuanzisha na miradi mbalimbali. Pia, mafunzo haya ni utekelezaji wa mpango mkakati wa chuo pamoja na ajenda ya utafiti ya chuo, ambazo zote zinachagiza uwepo wa machapisho na tafiti nyingi zenye kutatua matatizo ya jamii nchini." Amesema Dkt. Mtae.

Akizungumza katika Mafunzo hayo, Mratibu Mwandamizi wa Tafiti kutoka COSTECH, Bi. Bestina Daniel, amewakumbusha watafiti kusajili tafiti zao na kupata kibali kabla ya kuanza kufanya utafiti ili kuhakikisha zinafuata sheria, maadili na taratibu za nchi.

“Wakati mwingine tafiti hasa za kimataifa zinazohusisha watafti kutoka nje ya nchi zinaweza kuwa ni tafiti ambazo kwao ni sahihi lakini nchini kwetu zikawa haziendani na sheria, tamaduni au miiko yetu, hivyo usajili wa tafiti ili kupata kibali ni muhimu sana kwa watafiti wote.” Amesema Bi. Bestina.

Mafunzo haya ya siku tano ya uandishi wa mapendekezo ya utafiti yenye ubora yanayoendelea katika shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha, mkoani Pwani. Mafunzo haya yanasimamiwa na kurugenzi ya Utafiti, Mchapisho na Ubunifu ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania. yameanza Oktoba 2 na yanatarajiwa kumalizika Oktoba 6, 2023. Watumishi mbalimbali wa chuo hiki wanashiriki katika mafunzo hayo ambayo yanalenga kuongeza wingi wa tafiti lakini pia ubora wa tafiti na machapisho chuoni. Dkt. Edefonce Nfuka amepata heshima ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa majadiliano katika mafunzo hayo kwa siku zote tano za mafunzo hayo. Dkt. Nfuka ni Mkurugenzi wa huduma za ushauri wa kitaalamu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Share:

CHONGOLO AHUDHURIA KIKAO CHA BALOZI WA SHINA NAMBA 5 LA CCM WILAYANI TANGANYIKA MKOANI KATAVI,ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI.


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndugu Daniel Godfrey Chongolo leo Jumanne Oktoba 3,2023 amehudhuria na kushiriki kikao cha Balozi wa Shina namba 5, Ndugu Mikael Ndayambue Migelelo katika Tawi la Kapalamsenga, Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi.

Ndugu Chongolo pia alitumia nafasi hiyo kusikiliza kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi katika maeneo hayo, kuzitolea maelekezo ya kuzitatua pamoja na kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 4,2023







Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger