Sunday, 23 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 24, 2023



=


Share:

Video Mpya : BHUDAGALA & GUDE GUDE - NG'WANA MPOGOMI

Magwiji wa nyimbo za asili Bhudagala Ng'wana Malonja na Gudegude wanakualika kutazama video yao Mpya inaitwa Ng'wana Mpogomi

 
Share:

Video Mpya Kali Balaa!! NELEMI MBASANDO - NALUGALE


Msaniii Nelemi Mbasando ameachia ngoma mpya inaitwa Nalugale


Share:

YANGA SC YACHUNGULIA NUSU FAINALI CAFCC, YAITANDIKA RIVERS UNITED 2-0

 

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya YAnga imefanikiwa kuondoka na ushindi mnono wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya timu ya Rivers United ya nchini Nigeria katika mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali Kombe la Shirikisho barani Afrika.

Kipindi cha kwanza Yanga iliingia ikicheza mfumo wa mabeki watano ambapo upande wa beki wa kushoto alicheza Lomalisa ambaye alikuwa anapanda na kushuka vilevile kwa upande wake Djuma Shabaan.

Kipindi cha pili Yanga ilifanya mabadiliko kuanzia kwenye mfumo kutoka 3-5-2 na kuwa 4-4-2 na kuwapumzisha baadhi ya wachezaji ambapo mabadiliko hayo yalizaa matunda kwani yalisaidia kupata matokeo hayo.

Pongezi za pekee ziende kwa Nahodha Bakari Mwamnyeto ambaye alitoa pasi za mabao yote mawili ambayo yalifungwa na Mshambuliaji Fiston Mayele.
Share:

KARIBU TOFIKI TRADERS SHINYANGA UJIPATIE BIDHAA KWA BEI NAFUU

 
Share:

Saturday, 22 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 23,2023















Share:

USHOGA,USAGAJI NA ULAWITI VYAPINGWA KILA KONA

 
sheikhe wa Mkoa wa Dodoma Mustapha Rajab.

Na Dotto Kwilasa,DODOMA.

SHEKHE wa mkoa wa Dodoma Mustapha Rajabu amewataka watanzania kukemea na kupinga vitendo vya ushoga, ndoa za jinsia moja, ulawiti pamoja na usagaji.

Amesema ni  jukumu la kila Mtanzania kukemea mambo mabaya na kuhamasisha matendo mema na kwamba jamii inapaswa kusimama pamoja kama taifa kuhakikisha kuwa mambo haya ya hovyo yanatoweka.

Ameyasema hayo mapema leo jijini hapa kwenye ibada ya swala ya Eid el Fitri, iliyofanyika katika msikiti wa Gadafi ambapo amesema vita hiyo ni ya wote na si viongozi wa dini na Serikali pekee.

Shekhe Mustapha pia amesema "Jamii iachane na woga wa kutokemea mambo haya ya hovyo ambayo mataiafa ya nje wanataka kutuletea tunayapinga kwakuwa ni kinyume na mila na desturi zetu”amesema 

Amesisitiza kuwa pamoja na kuwa mambo hayo ni kunyume na mila za kitanzania pia ni kinyume na maagizo ya Mungu kwa mwanaume kumuoa mwanaume mwenzake au mwanamke kuwa na mahusiano hayo na mwanamke mwingine.

Ametumia nafasi hiyo pia kuwataka Watanzania kuacha tabia ya kupokea kila kitu kinachoingizwa nchini na mataifa mengine kwakuwa hali hiyo inaweza kusababisha kuongozeka kwa vitendo vya mmomonyoko wa maadili.

“Mmomonyoko wa maadili hivi sasa umekithiri nchini kutokana na kuiga mambo ambayo siyo mila zetu hali hiyo inasababisha kuongezeka kwa vitendo vya maasi ikiwemo baba kurawiti watoto wao wa kuwazaa,wanandoa kuuana pamoja na mauaji katika jamii zetu”amesema

Sheikh huyo pia amepongeza hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan, makamu wa Rais Dk. Philp Mpango na waziri mkuu Kassim Majaliwa kwa kusimama imara kueleza hisia zao waziwazi za kupinga vitendo hivyo vya ushoga na ndoa za jinsia moja nchini.


Share:

AUAWA KWA KUCHOMWA KISU TUMBONI


Charles Elias (18) Mkazi wa Mtaa wa Kigoma, mkoani Katavi amefariki dunia baada ya kuchomwa kisu tumboni na watu wasiojulikana majira ya usiku katika eneo la Mtaa wa Kawajense Manispaa ya Mpanda.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Ali Makame amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema kuwa uchunguzi unaendelea.

Naye Mama wa kijana huyo aliyepoteza maisha Easter Helman ameeleza kusikitishwa na tukio hilo ambalo limesababisha kifo cha mtoto wake na kuliomba jeshi la polisi kuwachukulia hatua za kisheria wale wote waliohusika.

Tukio hilo linajiri ikiwa ni wiki moja imepita baada ya kutokea tukio lingine la kuuawa kwa kijana Michael Chapa mkazi wa Shanwe, kwa kile kilichodaiwa kujihusisha na vikundi vya uhalifu maarufu kama Damu Chafu.

Chanzo - EATV
Share:

Tazama Picha : SWALA YA EID -EL -FITR SHINYANGA....SHEIKH MAKUSANYA ATOA KAULI NZITO CCM NA VYAMA VYA UPINZANI

Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya amewataka Watanzania kupendana (Waislamu na wasiokuwa Waislamu, Wenye dini na wasiokuwa na dini) huku akitaka vyama vya upinzani na chama tawala (CCM) vipendane, visogezane, visaidiane kwa ajili ya kuitengeneza nchi ya Tanzania akisisitiza kuwa kama hakuna vyama pinzani basi harakati ya maendeleo itakuwa ni ndogo.

Sheikh Makusanya ameyasema hayo leo Jumamosi Aprili 22,2023 wakati akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga.

“Tunamuombea Rais Samia Suluhu Hassan pamoja serikali yake pamoja na chama chake lakini pia tunaviombea na vyama pinzani kwa sababu kama hakuna vyama pinzani basi harakati ya maendeleo itakuwa ni ndogo na wao tunawaombea Mwenyezi Mungu awape kila la heri. Hawa vyama vya upinzani hawa na chama tawala vipendane, visogezane,visaidiane kwa ajili ya kuitengeneza nchi ya Tanzania”,amesema Sheikh Makusanya.

Ibada ya Eid El Fitr ikiendelea katika uwanja wa Sabasaba Mjini Shinyanga

“Tunamuomba Mwenyezi Mungu kwa kufunga kwetu siku 30, kwa kusimama kwetu, misimamo mbalimbali ya ibada mbalimbali, Mwenyezi Mungu atuletee amani na utulivu katika nchi yetu ya Tanzania. Mwenyezi Mungu atuletee kupendana Waislamu na wasiokuwa Waislamu, Wenye dini na wasiokuwa na dini. Tunamuomba Mwenyezi Mungu kwa visimamo hivi na swaumu hizi, Mwenyezi amkurubie muda wa uongozi wake, Rais wetu kipenzi cha watu, mwenye huruma na watu asiyetaka makuu, kila mwananchi ni wa kwake, habagui, Mwenyezi Mungu ampe kila la heri.

Na kila yeyote aliyepewa dhamana ama na Mwenyezi Mungu, ama na Rais wetu akafanye hiyana katika dhamana yake aliyopewa, Tunamuomba Mwenyezi Mungu mtu huyu amfichue, afichuke ili watu wamuelewe kwamba anafanya hiyana, anawafanyia hiyana Watanzania na yeyote yule atakayeonesha dhuluma ya kuidhulumu Tanzania, ya kumdhulumu Rais wetu tunakukabidhi kwako wewe Mwenyezi Mungu”,amesema Sheikh Makusanya.


Akitoa hotuba wakati wa Swala ya Eid Elf Fitri, Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategire amesema baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani matendo mema yaendelee kufanywa na waumini wa dini ya kiislamu badala ya kurudi kwenye uovu.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Habib Makusanya akitoa Ujumbe wa Sikukuu ya Eid El Fitr baada ya Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategire akitoa hotuba wakati wa Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategire akitoa hotuba wakati wa Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanga Soud Kategire akitoa hotuba wakati wa Ibada ya Eid El Fitri katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga 
Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga
Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga
Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga

Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga
Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika uwanja wa Saba Saba Mjini Shinyanga
Sheikh Salum Khamis akiongoza Ibada ya Eid El Fitri katika Msikiti wa Safina Ndembezi Mjini Shinyanga
Sheikh Salum Khamis akiongoza Ibada ya Eid El Fitri katika Msikiti wa Safina Ndembezi Mjini Shinyanga
Sheikh Salum Khamis akiongoza Ibada ya Eid El Fitri katika Msikiti wa Safina Ndembezi Mjini Shinyanga
Ibada ya Eid El Fitri ikiendelea katika Msikiti wa Safina Ndembezi Mjini Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde  - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger