Thursday, 6 April 2023

SHEIKH WALID KAWAMBWA AIPONGEZA PUMA ENERGY TANZANIA KWA KUWAUNGANISHA WATANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah, akiwashukuru wageni waalikwa mbalimbali baada ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo, Dar es Salaam, Miongoni mwa wageni waaalikwa kwenye futari hiyo ni Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa.
*******************

Na Mwandishi Wetu

KAIMU Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa ameipongeza Kampuni ya Puma Energy Tanzania kwa kuwaunganisha Watanzania kupitia programu zake mbalimbali za kibiashara.

Amesema kampuni hiyo inajali kazi zake, kwa sababu ni chombo cha kibiashara na moja ya utaratibu wa biashara ni kuvuta soko ambalo halipatikani bila kutanguliza mapenzi ya dhati ya shughuli zake.

Sheikh Walid ametoa pongezi hizo, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wageni wadau mbalimbali huku kwa upande wa Puma wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wake Fatma Abdallah na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk. Suleiman Majige.

Amesema walichokifa Puma Energy Tanzania, kimeonesha wameelewa maagizo ya Mwenyezi Mungu ya kutaka watu kuishi pamoja, huku akisisitiza kampuni hiyo inajali kazi zake.

“Niwapongeze Puma Energy Tanzania, kwa wakati huu tuliokuwepo wa Mwezi wa Ramadhan, ambao Mwenyezi Mungu anatuagiza tufanye mengi ya kheri yanayomridhisha yeye,” amesema.

Amesisitiza kwamba kampuni hiyo inajali kazi zake kwa sababu ni chombo cha kibiashara na moja ya utaratibu wa kibiashara ni kuvuta soko ambalo halipatikani bila kutanguliza mapenzi ya dhati kwa shughuli zake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania, Dk. Suleiman Majige, alisema wanaendelea kuiombea kampuni hiyo kwani ni mali ya Watanzania, iendelee kufanya kaza vizuri.

Pia, Dk. Majige ameishukuru Menejimenti ya Puma Energy Tanzania kwa kazi walioifanya ya kuwaunganisha na kuwakaribisha katika hafla hiyo, pamoja na kuwatakia mfungo mwema wa Ramadhani inayoendelea.

Aidha amewataka kuwa karibu na Mungu katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao ni muhimu kumuomba Mungu kila wakati aendelee kuleta neema na mapenzi mema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah(wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk . Suleiman Majige ( wa pili kulia) wakibadilishana mawazo na Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa( kushoto) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam

Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa akitoa salamu kwa wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania .Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam wakiongozwa
Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa (katikati) waliokaa mbele akiwa katika picha ya pamoja na maofisa mbalimbali wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Fatma Abdallah ( wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk Suleiman Majige ( wa pili kulia)


Share:

WAZIRI JAFO ATAKA UHIFADHI WA MAZINGIRA MLIMA KILIMANJARO KUENDELEZWA

waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Dkt.Seleman Jafo akizungumza Leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Dkt.Selemani Jafo akizungúmza na Naibu waziriwa wa Wizara hiyo Hamza Hamis Chillo leo April 6,2023 Bungeni Dodoma.


Na Dotto Kwilasa, DODOMA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt.Selemani Jafo ametoa wito kwa Watanzania kuhifadhi na kuutunza Mlima Kilimanjaro ili uendelee kuinufaisha nchi.


Ametoa wito huo leo Aprili 04, 2023 Bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malecela aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali katika kukabiliana na matukio ya uchomaji moto Mlima Kiliamanjro.


Mhe. Jafo amesema kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii ina dhamira ya dhati katika kuhakikisha matukio hayo yanakoma.


Amesema pamoja na Serikali kuunda timu ya kufanya utafiti wa matukio ya moto wananchi wana wajibu wa kuacha vitendo vya ukataji miti na uchomaji moto eneo la hifadhi ya Mlima Kilimanjaro. 


Awali akijibu swali la msingi la Mbunge wa Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis amesema Serikali kupitia Taasisi mbalimbali za ndani ya nchi zikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine, na Chuo Kikuu cha Nelson Mandela vinaendelea kufanya tafiti kuhusu suala hili. 


Hata hivyo amebainisha kuwa baadhi ya sababu zilizobainishwa kuchangia hali hiyo ni pamoja na kuongezeka kwa wastani wa joto duniani, shughuli za binadamu zisizoendelevu,ukataji wa miti na uchomaji moto misitu.


“Napenda kuchukua fursa hii kuhimiza uongozi na wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro kuongeza jitihada za kutunza Mazingira ya Mlima huo kwa kudhibiti uchomaji moto ovyo na kuongeza jitihada za kuhifadhi na kupanda miti,” amesema.


Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Khamis amesema Serikali inahakikisha Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR) unaotekelezwa kwenye Wilaya ya Kaskazini A, Unguja na Mradi wa Kurejesha Ardhi iliyoharibika Kuongeza Usalama wa Chakula katika Maeneo kame nchini (LDFS) unaotekelezwa katika Wilaya ya Micheweni, Pemba inakamilika kwa wakati.


Hivyo, amesema tayari Serikali imechukua hatua za kiutendaji kwa kuwataka waratibu wa miradi kitaifa kuhakikisha miradi inakamilika kikamilifu na kwa ubora.


Aidha, naibu waziri amesema Ofisi ya Makamu wa Rais (SJMT) imeendelea kuwasilina na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais (SMZ) ili Kusimamamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa upande wa Zanzibar ili Miradi hii ikamilike kwa wakati. 


Mhe. Khamis ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Chaani Mhe. Hamad Juma Usonge aliyeuliza

 Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Miradi ya muda mrefu ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayotekelezwa Zanzibar.

Share:

MCHANGO WA SEKTA YA MADINI KWENYE PATO LA TAIFA WAZIDI KUONGEZEKA





Na Mwandishi wetu,TABORA.

IMEELEZWA kuwa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita mchango wa Sekta ya Madini umeendelea kukua  hadi kufikia asilimia tisa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wachimbaji wadogo  wanaojishughulisha na shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu Wilayani  Nzega mkoani Tabora kupitia mahojiano maalum wamesema kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa Serikali kupitia Tume ya Madini  wa Sekta ya Madini hali iliyopelekea  kuongezeka kwa uzalishaji wa madini unaofanywa na wachimbaji wadogo kwa kutumia  teknolojia za kisasa.

Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji wadogo wa eneo hilo, Peter Mashiri, kutoka Kikundi cha  Msilale kilichopo katika eneo hilo  amesema kuwa kuongezeka kwa mapato yatokanayo na Sekta ya Madini kumetokana na matumizi ya teknolojia za kisasa na jitihada za Serikali za kuhakikisha makundi yote yanashiriki katika sekta hiyo.

Akizungumzia manufaa ya kikundi hicho kwa jamii inayouzunguka mgodi wake Mashiri amesema kuwa kikundi cha Msilale kimesaidia kutoa ajira kwa vijana wanaozunguka mgodi ambapo hadi sasa watu zaidi ya 48 wameajiriwa.

“Tunaipongeza Serikali kwa namna inavyowajali wachimbaji wadogo kwa kutoa leseni  kwa makundi hayo ambayo imesaidia kuongeza wigo wa ajira kwa wananchi na kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla, tunaiomba Serikali iendelee kuwagawia maeneo ambayo bado yanamilikiwa na wachimbaji wakubwa bila kuendelezwa.

Kwa upande wa Katibu wa kikundi hicho, Magreth Emmanuel amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Sekta ya Madini kwa kuwa Serikali imeweka mazingira wezeshi.

Ameongeza kuwa uwepo wa Sekta ya Madini umefungua fursa na hamasa kwa wanawake wengi ambao kwa sasa wameanza kujihusisha na shughuli za uchimbaji, uchenjuaji, na biashara ya madini sambamba na kutoa huduma kwenye migodi ya madini na kujipatia fedha kwa ajili ya kujikimu na kuhudumia familia zao.

Naye Msimamizi wa Mazingira wa kikundi hicho amesitiza kuwa mgodi huo umeendelea kuboresha mazingira yake kwa kuweka mitambo ya kisasa ambayo inawasaidia kuingia na kutoka ndani ya migodi, tofauti na awali ambapo walikuwa wanatumia kamba kushuka chini jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa usalama wao.

Share:

Picha : MATUKIO YANAYOENDELEA MSIBA WA MFANYABIASHARA MAARUFU MUSOMA FOOD..MAZISHI YANAFANYIKA LEO KAMBARAGE

Maelfu ya waombolezaji wamejitokeza kuaga mwili wa Mfanyabiashara wa nafaka mkoa wa Shinyanga Said Makilagi maarufu Musoma Food aliyefariki dunia ghafla jijini Mwanza Jumatatu Aprili 3,2023 akiwa Hotelini.

Mazishi ya marehemu Said Kate Makilagi yanafanyika leo Alhamisi Aprili 6,2023 nyumbani kwake Kambarage Mjini Shinyanga.

Tazama Picha matukio yanayoendelea muda huu...Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

BENKI YA CRDB YAFUTURISHA WATEJA NA WADAU NA KUTOA CHAKULA KWA WATOTO YATIMA TABORA….RC BATILDA APONGEZA HUDUMA YA AL BARAKAH BANKING

Kaimu Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Ndg. Jumanne Wambura Wagana akizungumza wakati Benki ya CRDB ikiwafuturisha Wateja na Wadau wa Benki ya CRDB Mkoa wa Tabora

Na Mwandishi Wetu – Malunde 1 blog Tabora

Benki ya CRDB imewafuturisha Wateja na Wadau wa Benki ya CRDB Mkoa wa Tabora ikiwa ni mwendelezo wa utamaduni wa Benki hiyo kuungana na Waumini wa Dini ya Kiislamu wanaoishiriki Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.


Hafla ya Futari iliyoandaliwa na Benki ya CRDB imefanyika Jumatano Aprili 5,2023 katika Hoteli Ya Ristalemi na kuhudhuriwa na viongozi wa dini, Viongozi wa Serikali, Taasisi za Umma na Binafsi, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa,Viongozi na Wafanyakazi kutoka Benki ya CRDB, Watoto yatima na wateja na wadau wa Benki ya CRDB ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani.

Akizungumza wakati wa Futari hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani ameipongeza Menejimenti ya Benki ya CRDB kwa kuanzisha na kuendeleza utaratibu huo wa kufutari na wateja, wadau na wenye uhitaji katika jamii katika kipindi cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

“Nimefurahishwa na jambo mlilolifanya leo la kutoa msaada wa fulana na kofia kwa Watoto wenye uhitaji maalum katika Shule ya Furaha, hakika lile ni jambo la kuigwa. Nimekuwa nikiwafuatilia kwa muda na kuona namna gani ambavyo mmekua mkitekeleza jambo hili na niliona mwaka huu mlianza jambo hili kwa kufuturu na wateja wa Dar es Salaam mkiongozwa na Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally, Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania. Hongereni sana”, amesema Dkt. Batilda.


“Ushiriki wenu katika kuandaa futari hizi katika mwezi Ramadhani inaonesha ni kwa jinsi gani Benki ya CRDB inatambua kuwa pamoja na kufanya biashara lakini ni sehemu ya jamii na inapaswa kushiriki katika masuala mbalimbali ya kijamii. Hakika hili ni jambo jema linalopaswa kuigwa na taasisi nyingine ambazo ni sehemu ya jamii yetu”,amesema.


Aidha pamoja na mazuri hayo ambayo Benki ya CRDB wamefanya kwa kushiriki na wateja na wadau wao katika futari, Mkuu huyo wa mkoa ameeleza kufurahishwa na uamuzi wa Benki hiyo kuanzisha huduma makhususi za Al Barakah Banking ambazo zinafuata misingi ya dini ya Kiislamu.


“Hakika hii inadhihirisha kuwa CRDB ni Benki inayomsikiliza Mteja kwani mmeweza kutambua mahitaji ya kundi lenye uhitaji wa huduma zinazofata misingi ya dini ya Kiislamu na kuweza kubuni huduma zinazoendana na mahitaji yao.Mafanikio ya huduma ya Al Barakah yatanufaisha sio tu Benki ya CRDB kwani kwa kuanzisha huduma hii mmeweza kuwajumuisha watu ambao mwanzo wasingeweza kujumuishwa katika huduma rasmi za kibenki kwa kuwa huduma zilizokuwepo zilikua haziendani na misingi ya imani yao”,amesema Dkt. Batilda.


“Hivyo kwa kuwajumuisha watu hawa mana yake mmeongeza wigo wenu wa kupokea amana na kwa sababu hiyo mtaweza kutoa mikopo zaidi kwa wafanyabiashara nchini na hivyo kutoa ajira zaidi, kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa pamoja na uwekezaji kwa ujumla wake.

Hivyo kama Mkuu wa Mkoa, nafurahishwa na jambo hili kwani kwa namna moja au nyingine mmtakuwa na mchango katika kutimiza majukumu yangu ya kumsaidia Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa kuyafikia makundi yote yaliyopo katika jamii”, ameongeza Mkuu huyo wa Mkoa wa Tabora.

Akitoa salamu za benki ya CRDB, Kaimu Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Ndg. Jumanne Wambura Wagana amesema benki hiyo imekuwa na utaratibu huo kila mwaka wakati wa Ramadhan kushiriki Futari na wateja wake na kutoa Sadaka ya vyakula kwa watoto yatima.


Wagana amesema mwaka 2021 benki ya CRDB ilianzisha dirisha la huduma za kibenki ambazo zimefuata misingi ya dini ya kiislamu maarufu kama Al Barakah Banking ambapo mpaka mwaka 2022 benki hiyo imeweza kupata wateja zaidi ya 30,000 na kutoa mikopo isiyo na riba kwa wateja wake kwa kiasi zaidi ya Shilingi Bilioni 73.


Amesema kwa Kanda ya Magharibi yaani Shinyanga, Geita, Kigoma na Tabora amesema mkoa wa Tabora umepokea huduma hiyo mpya ya Al Barakah kwa kasi zaidi hivyo kuwaomba watanzania ambao hawajajiunga wachangamkie fursa kwani ukiweka amana kwa akaunti ya Al Barakah haitengenezi riba na pia ukipewa mkopo hauna riba.

Wagana amewapa uhakika wa huduma wateja wote ambapo amesema benki hiyo kinara nchini yenye kauli mbiu ya benki inayomsikiliza mteja kwa sasa imeendelea kuzifanya huduma zake zipatikane kidigitali zaidi ikiwemo kupitia Mawakala, ATM, Simbanking, Vituo vya malipo n.k huku ikiendelea kupanua mtandao wake nje ya Tanzania ambapo kwa sasa CRDB inafanya vizuri nchini Burundi kama benki namba 2 na hivi karibuni wanatarajia kuanza kutoa huduma nchini Congo.


Mkurugenzi wa NBS na MNEC Tabora Mhe. Mohamed Nasson naye ameguswa na kitendo cha CRDB kutoa sadaka ya vyakula kwa watoto yatima akatoa Tsh 250,000/= huku mkuu wa Mkoa Dkt. Batilda Buriani naye akiguswa na kuongezea Tsh 250,000/= na kufanya iwe 500,000/= ambapo fedha hizo zitakabidhiwa kwa viongozi wa kituo cha kulelea watoto yatima ili wanunue mahitaji kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Balozi Dkt. Batilda Buriani akizungumza wakati Benki ya CRDB ikiwafuturisha Wateja na Wadau wa Benki ya CRDB Mkoa wa Tabora
Kaimu Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Ndg. Jumanne Wambura Wagana akizungumza wakati Benki ya CRDB ikiwafuturisha Wateja na Wadau wa Benki ya CRDB Mkoa wa Tabora
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger