Thursday, 6 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 6,2023

 







             

        




Share:

Wednesday, 5 April 2023

ONGEZA USHINDI X1000 YA DAU LAKO KUPITIA VENI VIDI VICI




 Aprili ya Kishua unaambiwaje jisajili Meridianbet upate mizunguko 50 ya bure kucheza sloti ya kasino ya mtandaoni. Kujisajili bonyeza hapa: https://a.meridianbet.co.tz/c/GLd6O8

 

Furahia sloti mpya kutoka Kasino ya Mtandaoni ikielezea Roma ya Kale! Cheza kipekee katika sloti ya Meridianbet Veni Vidi Vici!

 

Mambo ya kale yafuza na kushangaza pia, bila shaka ulishawahi kuisoma historia ya Warumi/Roman kuna mwamba mmoja anaitwa Julius Caesar alikua ni moja ya viongozi wenye nguvu kubwa sana kisiasa na kijeshi. Ili kukurudisha nyuma huku ukipiga hela Meridianbet pamoja na Expanse Studios inakuletea sloti yenye kuelezea mambo ya Roman Empire ni Vedi Vidi Vici.

Ushawishi wa hadithi za Kirumi pia unatambuliwa kwa jina la sloti, lakini mcehzo huu una kitu gani kipya?

Sloti ya Veni Vidi Vici ina Kolamu ambayo inakupa taji la mvinyo, ngao na upanga, mikokoteni, askari wachache, wakati alama ya msingi ya mchezo ni Caesar mwenyewe.

Kadi mbili za porini (Wild) zinakuongoza kwenye mzunguko wa bonasi kutoka Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet, wakati kadi tatu au zaidi za porini (Wild) zinaamsha Bonasi ya Sloti ya Veni Vidi Vidi.

 

Kuna msemo mmoja mkubwa wa Gaius Julius Caesar husema ’kete imetupwa’ na katika kasino ya mtandaoni mchezo wa Veni Vidi Vici, Caesar huzungusha kete! Aina hii ya bonasi inakuja katika ngazi tatu, na ya tatu inaweza kukuletea ushindi mpaka mara 1,000 zaidi!

Sloti hii ina bonasi ya ubashiri ambayo inaweza kuongeza kila ushindi mara mbili, pamoja na jackpots tatu zinazoendelea: Mini, Midi na Mega.

 

Sifa kuu ya sloti hii ni chaguo la BONUS NUNUA (Bonus Buy option), ambalo unaweza kuwezesha Bonasi ya Veni Vidi Vici, na RTP nzuri ya 96.28%!

Dhibiti Ufalme/ Kasri ya Roma na upate mafanikio makubwa!


Share:

NEMC YAKIPA SIKU SABA KIWANDA BUBU KUJIBU TUHUMA ZA TAKA HATARISHI

Mmoja wa Maafisa kutoka NEMC akikagua baadhi ya taka za hospitalini zikiwa zimekusanywa katika kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maafisa kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wakitazama baadhi ya taka za hospitalini zikiwa zimekusanywa katika kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa Maafisa kutoka NEMC akikagua baadhi ya taka za hospitalini zikiwa zimekusanywa katika kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya taka za hospitalini ambazo zimekutwa katika kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria NEMC, Bw.Thobias Mwesiga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ukaguzi kwenye kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki katika eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.
Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki Kusini Bw.Hamadi Taimuru akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufanya ukaguzi kwenye kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki katika eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam.


**********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limempatia siku saba (7) mmiliki wa kiwanda bubu cha kukusanya na kusaga chupa za plastiki katika eneo la Kisarawe II wilayani Kigamboni kufika katika ofisi za NEMC kujibu tuhuma za kukutwa na taka hatarishi za hospitali katika eneo lake la kiwanda.

Agizo hilo limetolewa leo Aprili 5,2023 Jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sheria NEMC, Bw.Thobias Mwesiga mara baada ya kufanya ukaguzi wa kimazingira na kutembelea na kushuhudia shughuli mbalimbali zinafanyikakwenye kiwanda hicho kinyume na sheria.

Amesema kwa kuwa wamebaini pia kiwanda hicho hakina vibali muhusika huyo atachukuliwa hatua za kisheria kwa kutozwa faini kwa kukiuka taratibu na ataelekezwa utaratibu wa kwenda kusajili kiwanda chake ambacho kinapaswa kusajiliwa kwa mujibu wa sheria.

"Faini itakayotozwa kwa mwenye kiwanda haitakuwa pungufu ya Milioni 5, na faini hiyo ni ya fedha ambayo anailipa kwa serikali". Amesema Bw. Mwesiga.

Aidha NEMC imetoa rai kwa hospitali zote nchini kufuata utaratibu wa namna ya kuteketeza taka zinazotokana na shughuli zao za mahospitalini.

"Sheria za Mazingira na kanuni zake inazitaka hospitali zote nchini kuwa na mfumo na utaratibu mzuri ndani ya hizo hospitali kuteketeza taka zao wenyewe, kuwa na vifaa ambavyo zile taka zinazozalishwa katika hospitali hazitaweza kurudi kwenye mazingira". Amesema

Kwa upande wake Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki Kusini Bw.Hamadi Taimuru amesema watampa maelekezo kwenye kiwanda pindi atakapofika kwenye ofisi za NEMC ndani ya siku saba, na kuanzia sasa wamesimamisha rasmi shughuli zote ambazo zimekuwa zikifanywa kwenye kiwanda hicho mpaka taratibu zote zitakapofuatwa.

"Hii haiwezi kukubarika kwaani hata hawa wanaofanya kazi kwenye kiwanda hiki wanafanya kazi pasipokuwa na vifaa maalumu hivvyo wanaweza kupata na wao madhara kwenye taka hizo za hospitali, madhara kwasasa ni mengi". Amesema Bw.Taimuru.

Pamoja na hayo amesema watahakikisha wanatembelea katika hospitali kuona takataka zao wanazihifadhi na kuzipeleka wapi na kuonesha uthibitisho unaoonesha sehemu ambayo wanazipeleka takataka hizo.


Nae Mmiliki wa Kiwanda hicho, Bw. Salumu Madongo amekiri kuwa kiwanda chake hakina kibali kutoka NEMC lakini vibali vya kiwanda anavyo hivyo basi atafika katika ofisi za NEMC ili aweze kupewa utaratibu na kuweza kupata kibali cha Mazingira.

Kuhusu taka za hospitali kukutwa katika kiwanda chake amesema ni kutokana na wale ambao wanakusanya chupa za plastiki na kuzipeleka pale ndo walikuja na taka hizo zikiwa ndani ya mfuko wa kubebea chupa za plastiki
Share:

FAMILIA YA GULAM HAFEEZ MUKADAM YATOA SADAKA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI KWA WATOTO BUHANGIJA

Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam (kulia) ikikabidhi sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katika Muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam imetoa sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum (Wasioona, Viziwi na wenye ulemavu wa ngozi) cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.


Akizungumza wakati wa kukabidhi vyakula hivyo, leo Jumatano Aprili 5,2023, Diwani wa kata ya Mjini Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam amesema familia yake imefika katika kituo hicho cha Buhangija kwa ajili ya kupeleka sadaka kwa watoto hao wenye mahitaji maalum.


“Tupo kwenye mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, tumekuja hapa kwa niaba ya wafadhili wetu waliopo Marekani kwa ajili ya kuleta chakula kwa watoto hawa”,ameeleza Mukadam.


Amevitaja vyakula hivyo kuwa ni Mchele kilo 50, unga wa sembe kilo 30, sukari kilo 25, unga wa ngano kilo 25,mafuta ya kupikia lita 10,maharage kilo 25, chumvi pakti 1, sabuni ya unga kilo 25, sabuni za vipande boksi 1,nyama kilo 10,viazi kilo 10, tambi boksi moja vyote vikiwa na thamani ya shilingi 700,000/=.

“Tunawashukuru wadau walioungana na familia yetu kutupatia msaada kwa ajili ya watoto hawa ambao nimekuwa mdau wa muda mrefu nikiwa miongoni mwa waanzilishi wa kituo hiki. Wito wangu ni kwa wadau mbalimbali tuwe mfano wa kuwambuka watoto hawa kwani ni watoto wote sote”,amesema Mukadam.

Gulam pia ametoa wito kwa Taasisi mbalimbali na jamii kwa ujumla kujenga utamaduni wa kuwasaidia mara kwa mara watoto hao ambao kwa sehemu kubwa wanatoka katika familia duni na wengine ni yatima hasa ikizingatiwa kuwa mahitaji yao ya kila siku ni makubwa.

Kwa upande wake, Mke wa Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru amewataja wafadhili waliofanikisha kupatikana kwa vyakula kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum Buhangija kuwa ni ndugu Nisha Kumar, Sumairah Toor,Zehra Toor, Anjum Toor, Nabeel Siddiqui na Farjana Chilwan.


Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Buhangija Jumuishi, Bi. Rose Daudi amewashukuru wadau hao kwa kusaidia watoto hao huku akimpongeza na kumshukuru Mhe. Gulam Hafeez Mukadam kwa kuendelea kuwa karibu na kituo cha Buhangija na kufanikisha kupatikana kwa mahitaji mbalimbali katika kituo hicho ambacho sasa kina jumla ya watoto 201 wenye ulemavu wa ngozi, viziwi na wasiosikia.


Nao watoto hao wameishukuru familia ya Mzee Gulam Hafeez Mukadam kwa kuwapatia msaada huo na kuomba wadau wengine kuendelea kufika katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum.


Katika hatua nyingine Diwani huyo wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam amekabidhi msaada wa mifuko mitatu ya saruji kwa Mjasiriamali Alafat Ntemanya mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum (Wasioona, Viziwi na wenye ulemavu wa ngozi) cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum (Wasioona, Viziwi na wenye ulemavu wa ngozi) cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Mke wa Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Mke wa Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Mke wa Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru akizungumza katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru na wageni mbalimbali wakiwa katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Vyakula mbalimbali vilivyotolewa na familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam kwa ajili ya watoto wanaolelewa kwenye kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam Bi. Mehrunnissa Allimia Chilwan maarufu Anti Meru na wageni mbalimbali wakiwa katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam (kulia) ikikabidhi sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam (kulia) ikikabidhi sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam (kulia) ikikabidhi sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam (kulia) ikikabidhi sadaka ya vyakula katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Buhangija Jumuishi, Bi. Rose Daudi akitoa neno la shukrani
Mwanafunzi akitoa neno la shukrani
Familia ya Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam wakipiga picha ya pamoja na sehemu ya watoto katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza na watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza na watoto wenye mahitaji maalum cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Diwani huyo wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumzma wakati akikabidhi msaada wa mifuko mitatu ya saruji kwa Mjasiriamali Alafat Ntemanya mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Mjasiriamali Alafat Ntemanya mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga akizungumza wakati akipokea mifuko ya saruji kutoka kwa Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam  (wa pili kulia) akikabidhi msaada wa mifuko mitatu ya saruji kwa Mjasiriamali Alafat Ntemanya  (wa pili kushoto) mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam  (wa pili kulia) akikabidhi msaada wa mifuko mitatu ya saruji kwa Mjasiriamali Alafat Ntemanya  (wa pili kushoto) mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Mifuko mitatu ya saruji iliyotolewa na Diwani wa kata ya Mjini Manispaa ya Shinyanga Mhe. Gulam Hafeez Mukadam kwa Mjasiriamali Alafat Ntemanya  mkazi wa Mtaa wa Viwandani Mjini Shinyanga kwa ajili ya kuboresha kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya kibanda cha kuoneshea michezo kinachojulikana kwa jina la Home and Away Sports Arena kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger