Friday, 31 March 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 31,2023



























Share:

Thursday, 30 March 2023

NAMIBIA YAVUTIWA NA TANZANIA INAVYOKABILIANA NA TATIZO LA AJIRA



Na Mwandishi Wetu, DODOMA

UJUMBE wa Bunge la Namibia umeimwagia sifa Serikali ya Tanzania namna ilivyojipanga kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana kupitia programu zinazotekelezwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu.

Kiongozi wa ujumbe huo na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge hilo ya Rasilimali watu na Maendeleo ya Jamii ambaye pia ni Mbunge, Mhe. Nono Katjingisua, ametoa pongezi hizo leo Machi 30, 2023 baada ya kukutana na Mofisa wa Ofisi hiyo wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii, Festo Fute.

Mhe.Katjingisua amesema Serikali ya Namibia mwaka 2022 ilikumbwa na tatizo la ajira kwa vijana hivyo hali hiyo imewasukuma kuja Tanzania kujifunza namna inavyokabiliana na tatizo hilo.

“Tumepata maelezo ambayo na sisi tutakaporejea bungeni tutazingatia kama vile kuwa na program ya taifa ya kukuzaji ujuzi ili kuwajengea uwezo vijana kupata ujuzi utakaowasaidia kujiajiri au kuajiriwa kulingana na mahitaji ya soko la ajira,tumeona wenzetu wana mfuko wa maendeleo ya vijana ambao unatoa mitaji kwa vijana, tumejifunza mengi,”amesema.

Naye, Mjumbe wa Kamati hiyo ya Bunge, Tjiveze, Herlinde, amevutiwa na Tanzania inavyofanya jitihada mbalimbali za kuwakwamua vijana ikiwamo kutunga sheria ya manunuzi ya umma inayoelekeza asilimia fulani ya zabuni iwe ya vijana na namna inavyowajumuisha vijana wenye ulemavu kwenye fursa zilizopo za ajira.

Awali, akiwaongoza Maofisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu kueleza namna inavyotekeleza program za vijana na uratibu wa ajira, Mkurugenzi wa Idara ya Hifadhi ya Jamii, Festo Fute, amesema ofisi hiyo ni mratibu mkuu wa masuala ya vijana na kuna sera ya vijana ambayo kwasasa inafanyiwa mapitio ili iendane na wakati.

Share:

PIGA PESA KASINO YA MTANDAONI NA SLOTI YA PUMPKIN PATCH


Jisajili Meridianbet upate mizunguko 50 bure ya kucheza moja ya mchezo wa kasino ya mtandaoni utakaopenda! Kujisajili bonyeza hapa https://a.meridianbet.co.tz/c/RGCCr7


Sloti ya Pumpkin Patch

Hawajawahi kukosea hata kidogo  Meridianbet kutoa bonasi kubwa, Odds kubwa na Promosheni za kumwaga. Wiki hii kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuletea mchezo wa kukata na shoka na utakao kutengenezea faida uitwao Pumpkin Patch.

Pumpkin Patch ni mchezo wenye maudhui ya siku ya Halloween uliotengenezwa na watengenezaji maarufu wa michezo ya kasino Habanero. Licha ya mchezo huu wenye maudhui ya siku maruhani (Halloween), Sloti ya Pumpkin Patch imekuwa ni moja ya mchezo unaopendwa zaidi kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.

Mchezo huu wa kusisimua una kolamu 5 na mistari 25 ya malipo na kubwa Zaidi unakujia na jakipoti kubwa mbili. Unasubiri nini? Jiunge na familia ya mabingwa ya Meridianbet ili uweze kuwa mshindi.

Namna ya Kucheza Sloti ya Pumpkin Patch

Jinsi ya kucheza mchezo huu wa kasino ya mtandaoni ni rahisi sana. Unachotakiwa kuwafanya ni kubofya kitufe chenye neno *Spin kuanzisha mzunguko ambapo Sloti ya Pumpkin Patch ina alama kuu mbili.

 

Alama ya Boga linalo cheza likiwa kwenye kifukuzia kunguru na alama ya Wild. Ikiwa alama ya Kunguru ikaangukia pembeni ya Boga, itasababisha boga hilo kusambaa kwenye kolamu ya sloti na kutengeneza alama ya ushindi yenye kukuletea malipo ya kiwango kikubwa iitwayo Complex Wild.

 

Kama Kindi (Squirrel) akiangukia pembeni ya Boga, basi Boga hilo litabadilika na kuwa alama ya ushindi ambayo itakutea malipo mara mbili ya mwanzo iitwayo Wild.

 

Ndio! Ni Meridianbet pekee ndio inayo kuhakishia ushindi kwa kukupa Bonasi, Odds kubwa na Promosheni za kipekee. Sio hivyo tu, Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet ya sloti ya Pumpkin Patch inakupa nafasi ya kushinda mizunguko kibao ya bure. Jiunge sasa kupitia  https://www.meridianbet.co.tz na upate bonasi ya bure ya kuanzia.

 


Share:

WATSWANA WAVUTIWA NA MATUMIZI YA TEHAMA KATIKA TAASISI YA OSHA

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka ya Botswana, Bw.Gopolang Maakwe akizungumza na viongozi wa Menejimenti ya OSHA wakati wa ziara yake ya kutembelea Ofisi za OSHA Dar es salaam akiambatana na baadhi ya watumishi wa Ofisi yake kwa lengo la kuijifunza jinsi taasisi ya OSHA inavyotumia mifumo ya TEHAMA katika usimamizi wa masula ya usalama na afya mahali pa kazi.



Meneja wa Afya wa OSHA, Dkt. Jerome Materu akikabidhi zawadi kwa Kaimu, Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka ya Botswana, Bw.Gopolang Maakwe mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea ofisi za OSHA Dar es salaam.



Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka ya Botswana, Bw.Gopolang Maakwe pamoja na watumishi wa Ofisi yake (waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi katika Menejimenti ya OSHA katika Ofisi za Dar es salaam.

*************************





Na Mwandishi Wetu

Wataalam kutoka Ofisi ya Kumbukumbu na Nyaraka ya Botswana wamefanya ziara katika Ofisi za Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kujifunza jinsi Taasisi hiyo inavyotumia mifumo ya TEHAMA katika usimamizi wa masuala ya Afya na Usalama mahali pa kazi.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Serikali wa Botswana, Bw. Gopolang Maakwe, Nchi yake ipo katika mchakato wa kutengeneza mfumo wake wa ofisi mtandao kwa ajili ya kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi.

Akizungumza alipotembelea Ofisi za OSHA na kufanya kikao na menejimenti hivi karibuni, amesema wameona ni muhimu kujifunza kwa nchi ambazo zimepiga hatua katika matumizi ya mifumo hiyo.

“Tumekuja hapa kujifunza namna ambavyo Tanzania imefanikiwa kujenga na kutumia mfumo wa ofisi mtandao katika Taasisi zake zaidi ya 200. Tuliposikia kwamba Tanzania wamefanikiwa katika eneo hili tukaona ni vyema akawa mshirika wetu katika zoezi lililopo mbele yetu la kuhakikisha kwamba Serikali nzima ya Botswana inaingia katika matumizi ya ofisi mtandao kuanzia mwaka 2024/2025,” amesema Bw. Maakwe.

Ameongeza kuwa: “Katika ziara yao wamefurahi kusikia kwamba mfumo unaotumika Tanzania umeandaliwa kwa kutumia wataalam wa ndani hivyo hata uangalizi na matengenezo yake hayatakuwa na gharama kubwa kwani mara nyingi uundaji wa mifumo ya TEHEMA umekuwa ukitegemea watoa huduma wa nje ya serikali jambo ambalo limekuwa likiongeza gharama za uendeshaji.”

Aidha, ameishukuru OSHA na serikali ya Tanzania kwa ujumla kwa ukarimu wao na ameahidi kwamba wataendelea kuja kujifunza zaidi hadi hapo watakapokamilisha mfumo wa nchi yao.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa OSHA, Dkt. Jerome Materu, amemshukuru Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Taasisi ya OSHA kutumia mfumo wa ofisi mtandao na mifumo mingine ya serikali ambayo imesaidia kuongeza ufanisi katika utendaji wa OSHA.

“Mfumo wa ofisi mtandao pamoja na mifumo mingine iliyoandaliwa na serikali yetu imesaidia sana kupunguza urasimu na kutuongezea kasi ya kuwahudumia Watanzania. Sisi kama OSHA tunao mfumo wetu wa ndani wa Usimamizi wa Taarifa za maeneo ya kazi nchini ujulikanao kama WIMS ambao tunautumia sambamba na mfumo wa ofisi mtandao na mifumo mingine ya serikali katika kuwahudumia wadau wetu,” alieleza Dkt. Materu.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa Huduma za Usalama na Afya, kabla ya kuanza kutumia mifumo hiyo kulikuwa na changamoto katika upatikanaji wa huduma za OSHA ambapo cheti cha usajili wa eneo la kazi kilikuwa kinapatikana baada ya siku saba huku cheti cha kukidhi viwango vya usalama na afya kikiandaliwa kwa mwezi mzima.

“Kwasasa mdau anaweza kusajili eneo lake la kazi ndani ya masaa machache na kupata cheti cha kukidhi viwango vya usalama na afya ndani ya siku tatu,” amefafanua Mkurugenzi Materu.

OSHA ni Taasisi chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) ambayo inasimamia utekelezaji wa Sheria Na. 5 ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi ya mwaka 2003. Usimamizi wa Sheria hii unahusisha kuyatambua maeneo ya kazi kwa kuyapa usajili na kisha kuyafikia kwa ajili ya ukaguzi na ushauri wa kitaalam juu ya uboreshaji wa mazingira ya kazi kwa minajili ya kuwakinga wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vya ajali na magonjwa mahali pa kazi.
Share:

WAJIBU YAZIPIKA AZAKI, WAANDISHI WA HABARI USIMAMIZI WA FEDHA ZA UMMA



TAASISI ya WAJIBU imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari na Asasi za Kiraia (AZAKI) namna ya kufanya uchambuzi wa masuala ya uwajibikaji na usimamizi wa fedha za umma.Akizungumza mbele ya wadau hao wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo ya siku mbili jana Machi 29, 2023,jijini Dodoma Meneja wa Fedha na Utawala wa Taasisi ya WAJIBU, Jackson Mmary ameeleza hatua kwa hatua umuhimu wa kuwa na wadau kutoka maeneo mbalimbali ili kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.

Amefafanua kuwa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu (CAG) ambayo inahusu masuala ya fedha ni nyenzo muhimu ya kufuatilia mipango ya Serikali Kuu ama Serikali za Mitaa na taasisi za kiraia.

“Tumekuwa tukifanya uchambuzi wa ripoti ya CAG peke yetu kwa kipindi cha miaka sita iliyopita, sasa tumeona kuna umuhimu wa kuwashirikisha wadau. Kwa muelekeo wa WAJIBU tukasema ukitaka kwenda haraka nenda peke yako lakini ukitaka kwenda mbali nenda na wenzako, kwa hiyo tukaona ni muda muafaka kuanza kwenda na wenzako,” amesema Mmary na kuongeza:

“Miaka iliyopita tulikuwa tunafanya uchambuzi halafu tunawaletea, sasa hivi tunataka kuwaongeza ili sisi na ninyi tufanye uchambuzi kwa pamoja halafu tukitoka hapa twende mbele. Kwa kufanya hivyo tutawezesha kujenga kwa pamoja yale tuliyokuwa tunayachambua na kuwaletea.

Kwa hiyo hivi sasa nanyi mtakuwa na uwezo wa kuchambua, kwa hiyo tutakuwa na nguvu zaidi kwa sababu ya kuhusika sote kwa pamoja. Kingine kitatuongezea mawanda ya uchambuzi kwani tumekuwa tukifanya uchambuzi kama sisi na kama tulikuwa watu 20 hapa leo wapo zaidi ya 40.”

Kutokana na uwezeshaji uliofanywa, kwa sasa amesema kutakuwa na macho mengine 80 zaidi yale yaliyokuwa yanafanya uchambuzi mwanzoni.

“Sisi WAJIBU na ninyi kuanzia leo tukitembea kwa pamoja tutakuwa tumejijengea uwezo, ninyi mtakuwa mmetujengea uwezo na sisi tunawajengea uwezo, kwa hiyo tutaongeza uzoefu na hasa ninyi mnaofanya kazi mikoani katika halmashauri.

Pia kuna mambo ambayo inawezekana tusiyaone namna ambavyo yanaathiri jamii na kila mtu anahoji ndio maana hapa kuna redio za jamii, magazeti ya kitaifa pamoja na kuna asasi za kiraia. Kwa hiyo tukiweka huo mchanganyiko tutaongeza mawanda, uzoefu zaidi katika kufanya uchambuzi wa mambo yanayoathiri jamii,” amesema Mmary.
Meneja wa Fedha na Utawala wa Taasisi ya WAJIBU, Jackson Mmary akizungumza mbele ya Wanahabari na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini wakati wa ufunguzi wa Mafunzo siku mbili yanayoendelea jijini Dodoma yaliyohusu namna ya kufanya uchambuzi wa masuala ya uwajibikaji na usimamizi wa fedha za umma,lengo mojawapo ikiwa ni kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.
Baadhi ya Wanahabari na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo wakati mafunzo yakiendelea.
Mmoja wa Wandishi wa habari akichangia jambo katika suala zima la kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.

Ofisa Utafiti na Uchambuzi wa Fedha kutoka Taasisi ya WAJIBU Maureen Mboka akieleza jambo mbele ya Wanahabari na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini wakati wa ufunguzi wa Mafunzo siku mbili yanayoendelea jijini Dodoma yaliyohusu namna ya kufanya uchambuzi wa masuala ya uwajibikaji na usimamizi wa fedha za umma,lengo mojawapo ikiwa ni kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.

Wakifuatilia baadhi ya vitabu vinavyohusu Ripoti ya uwajibikaji vinavyoandaliwa na Taasisi ya WAJIBU ikiwa ni sehemu ya kujengeana uwezo wa kuchambua ripoti zinazohusu uwajibikaji wa fedha za umma.
Picha mbalimbali wakati wa Majadiliano wa mafunzo hayo yakiendelea
Ofisa Mawasiliano wa Taasisi ya WAJIBU Hassan Kissena akitoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiibuliwa wakati wa majadiliano kwenye mafunzo hayo yaliyowakutanisha Waandishi wa habari pamoja na Wadau wa Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka maeneo mbalimbali nchini
Share:

Wimbo Mpya : NTEMI OMABALA - OBHUKWINGWA

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MACHI 30,2023





















Share:

Wednesday, 29 March 2023

MERIDIANBET INARUDISHA DAU LAKO MPAKA X100 UKICHANA MKEKA


Sub-Heading: Pata mizunguko 50 ya bure kucheza sloti na michezo ya kasino ya mtandaoni ukijisajili na Meridianbet. Jisajili kupitia link hii.

Waswahili waliwahi kusema ukiona moshi ujue kuna shughuli na shughuli ni wat una watu wenyewe ni wewe, usemi huu una maana kubwa sana Meridianbet nyumba ya Odds kubwa, wamekuja na OFA Kabambe kwaajili yako unayechana mkeka/tiketi kila kukicha.

Habari njema zikufikie popote ulipo mdau wa kubashiri na Meridianbet kwakuwa unapata odds kubwa, machaguo Zaidi ya 1000+ na Ofa za kumwanga, kuna hii nyingine ya kijanja Zaidi unaambiwaje usijali endapo mkeka wako utachanika kwa timu moja, kwao Meridianbet mkeka bado umeshinda kwa sababu wanakurudishia mara 100 ya dau lako uliloweka.

Nifanyeje Nirudishiwe Hela Zangu?

Kitu unachopaswa kufanya ni kuhakikisha umebashiri tiketi yenye odds kubwa kuanzia 25+ hadi 950+ utarejeshewa mara 100 ya dau lako endapo ikatokea timu moja imechana mkeka wako.


Mchanganuo Uko hivi!



Zingatia:



Ø Tiketi haitakiwi kuwa na bashiri ya mechi moja tu

Ø Unatakiwa uwe na angalau bashiri moja kutoka bashiri za kabla ya mechi.

Ø Haitakiwa kuweka machaguo mengi (Mult-bet) kutoka mechi moja

Ø Hii ni maalumu kwa tiketi zilizopoteza mechi moja na dau la bonasi halihusiki kwenye promosheni hii.

Ø Kupata jumla ya ushindi zidisha jumlaya odds zilizoshinda pekee (Odds za bonasi hazihesabiwi) kisha zidisha kwa namba zilizoainishwa kwenye jedwali hapo kulingana na idadi ya mechi kwenye tiketi yako.

Ø Hesabu za Odds kubwa zilizoshinda hazihusishi ongezeko la odds za bonasi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger