Monday, 27 March 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 27,2023






























































Share:

Sunday, 26 March 2023

SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI YAAGIZWA KUCHUNGUZWA BAADHI YA VIONGOZI WANAOJIHUSISHA NA VITENDO VYA MGONGANO WA MASLAHI


WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Jenista Mhagama,akizungumza wakati akifungua Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililofanyika leo Machi 24,2023 jijini Dodoma.


KAMISHNA wa Maadili Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi ,akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililofanyika leo Machi 24,2023 jijini Dodoma.



WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Jenista Mhagama,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma lililofanyika leo Machi 24,2023 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA



WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Jenista Mhagama,ameiagiza Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuwachunguza baadhi ya viongozi wanaojihusisha na vitendo vya rushwa na mgongano wa maslahi nchini.

Agizo hilo amelitoa leo Machi 24,2023 jijini Dodoma wakati akifungua Baraza la wafanyakazi wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Waziri Mhagama amesema kuwa wapo baadhi ya viongozi wa umma wanaojihusisha na vitendo vya mgongano wa maslahi wanapotimiza majukumu yao na wengine kukinza hasa katika halmashauri ambako serikali imeelekeza fedha nyingi za miradi.

“Kwa kutumia mbinu za uchunguzi mlizonazo, fuatilieni kwa ukaribu viongozi wanaojihusisha na vitendo vya ukiukwaji wa maadili ikiwemo rushwa na mgongano wa maslahi ili haki iweze kutendeka ikiwemno kuchukua hatua za kisheria kwa watakaobainika.

”kiongozi wa umma anapotoa kauli inayokinzana na kiongozi mwenzake au na mamlaka iliyomteua ni ukiukwaji wa maadili na tabia hiyo sio nzuri katika kuwaletea wananchi maendeleo.''amesema Mhagama

Hata hivyo amewataka kutumia baraza hilo kukumbushana kuwa wanapotoa elimu kwa viongozi wa umma wakumbushe matumizi sahihi ya madaraka kwa kutunza siri.

“Zingatieni viapo vyenu vya usiri wa taarifa mnazozipata ili na nyie mthaminiwe na muaminike na wadau wenu wa nje na ndani. Kumbukeni kuwa kila taarifa ya kiongozi inayokujia ni siri, isipotunzwa vizuri inaweza kuharibu taswira nzuri ya kiongozi na Serikali kwa ujumla,”amesisitiza

Kwa upande wake Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi amesema watajadili mapitio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23 na pia kujadili mipango na mikakati kwa ajili ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha ujao wa 2023/24.

“Tunaahidi tutaendelea kutekeleza majukumu yetu tuliyokabidhiwa kisheria bila kupoteza uelekeo ili kufikia dira ya kuwa taasisi yenye ufanisi na kuaminika katika kukuza na kusimamia misingi ya maadili ya viongozi wa umm.'amesema Jaji Mstaafu Mwangesi

Share:

MWANAMKE AFARIKI AKIHONDOMOLA URODA NA MPENZI WAKE KICHAKANI


Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 37, yuko taabani kufuatia kifo cha mpenzi wake ambaye alifariki dunia wakirusha roho kichakani katika eneo la Mbita, Kaunti ya Homa Bay nchini Kenya.

Marehemu aliyetambulika kwa jina la Milca mwenye umri wa miaka 48, aliangamia jioni ya Jumapili ya Machi 19, 2023 baada ya kuamua kuingia kwenye kichaka eneo la Got Rateng na mpenzi wake kumumunya uroda wakirejea nyumbani wakitokea kunywa pombe.


 Akithibitisha kisa hicho, chifu wa eneo hilo Bernard Ouma alisema kuwa wapenzi hao awali walikuwa wameonywa dhidi ya kushiriki tendo la ndoa wakiwa wamelewa lakini walipuuza.

Kulingana na Ouma, mshukiwa alijaribu kuuzikwa mwili wa Milca na hivyo kupelekea kukamatwa kwake.

"Kuna wakati niliwaita na kuwaonya kuhusu kufanya mapenzi sehemu zisizo na staha hasa baada ya kunywa pombe, waliendelea na ninafikiri hilo linaweza kuwa chanzo cha maafa haya," alisema chifu Ouma. 

Inaripotiwa kwamba mwanaume huyo alimrithi Milca baada ya kifo cha mume wake kama ilivyo utamadumi wa jamii ya Waluo ambapo mwanamke anaruhusiwa kurithiwa mumewe anapofariki dunia. 

Kwa sasa mwanaume huyo anazuiliwa na polisi wa Homa Bay baada ya kukiri chanzo cha kifo hicho huku mwili wa Milca ukipelekwa katika hifadhi ya maiti ya Hospitali ya Rufaa ya Homa Bay, uchunguzi zaidi ukiendelea.

Chanzo - Tuko news
Share:

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUWAHIMIZA WAUMINI KUHESHIMU IMANI ZA WENGINE

Na Mwandishi wetu,Dar Es Salaam.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana amesema ni jukumu la viongozi wa dini kuwaunganisha Watanzania, kudumisha amani, umoja na mshikamano.

Pia, ametaka Viongozi hao kuendeleza utamaduni wa kuheshimu imani ya kila mmoja kwa kutazama mambo mazuri na sio changamoto chache zinazojitokeza.

Kinana ameyasema hayo leo Machi 26, 2023 wakati akizungumza katika hafla ya mashindano ya kuhifadhi na kusoma Kuraani tukufu yaliyoandaliwa na Taasisi ya Aswhabu al-Kahfi Islamic Centre, yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

“Hivi sasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameweka mkazo kwenye maridhiano na tuna taasisi ya maridhiano na amani mbayo imeunganisha dini na madhehebu mbalimbali nchini, lengo ni kudumisha umoja, mshikamano na amani katika taifa letu.

“Mimi ningependa kuwasihi viongozi wa dini, kila madhehebu, kila dini ni muhimu tushikame,msitafute mapungufu ya kila mmoja, mtafute mema ya kila mmoja ili tuweze kushikamana,” amesema.

Kinana pia amewasihi  Watanzania kuzingatia na kutanguliza mambo mazuri ya kila mmoja Ili kuondoa uwezekano wa kuibua migogoro isiyo na tija kwa ustawi wa taifa.

Awali akimkaribisha Kinana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo, amesema amani na maadili yanasisitizwa mahali popoote kwani hata Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 imetaja ajenda ya amani na maadili.

"Kila mtanzania ana nafasi ya kukemea tabia zisizofaa kwenye jamii,tuishi Kwa kuzingatia miiko yetu na hii itasaidia kuishi kwenye hali ya utulivu na amani,"amesisitiza Waziri Jafo.

Share:

WIZARA YA AFYA YAWATOA HOFU WANANCHI MAAMBUKIZI MAPYA YA MARBURG





Na. WAF - Ziara Mkoani Kagera, Bukoba.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amefanya ziara ya kutembelea katika Kijiji cha Ntoma Wilaya ya Bukoba Mkoani Kagera kwa lengo la kujionea hali inavyoendelea baada ya kutangazwa kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg Mkoani humo. 

Katika Ziara hiyo, Waziri Ummy ameambatana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Zabron Yoti pamoja na Mwakilishi wa Shirika la UNICEF Bi. Shalini Bahuguna.

Aidha, Waziri Ummy amesema kwa sasa hali ni salama na kuwataka Wananchi wa kijiji hicho na watanzania kwa ujumla kuondoa hofu kwa kuwa Serikali inawajali Wananchi wake. 

“Niwatoe hofu Watanzania tuendelee kufanya kazi zetu lakini tuzingatie maelekezo ya Serikali ya kujikinga na ugonjwa huu kwa kuepuka kushikana mikono hususan kipindi hiki lakini pia tujitahidi kunawa mikono mara kwa mara kwa maji tiririka na sabuni.” amesema Waziri Ummy

Hata hivyo, Waziri Ummy amesema kuwa Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea na juhudi za kuhakikisha ugonjwa huo unamalizika na hautatokea tena katika maeneo hayo. 

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kanyangele Bw. Hamim Hassan ameishukuru Serikali kwa kufanya juhudi kubwa ambapo hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyeongezeka kwa kuthibitika kuwa na ugonjwa huo. 

“Hatua za Serikali kupitia Wizara ya Afya zilizochukuliwa za kuwaweka sehemu maalumu waliokuwa karibu na wagonjwa imesaidia sana kutoendeleza maambukizi kwingine na hali ni shwari kwa sasa.” amesema Bw. Hassan

Share:

MERIDIANBET KASINO YA MTANDAONI YAJA NA SLOTI YA WANYAMA

Sloti ya Forest Rock             

Je, unajua kuwa wanyama pori wanaweza kukuletea ushindi? Ndio! Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet yote hayo yanawezekana. Meridianbet inakuletea sloti mpya yenye maudhui ya Rock ‘n’ Roll iliyotengenezwa na watengenezaji maarufu wa sloti Expanse Studio iitwayo Forest Rock.

 

Sloti ya Forest Rock ina muundo wa kizamani wenye kolamu 5 na mistari 15 ya ushindi. Kama kawaida ukiichagua kasino ya mtandaoni ya Meridianbet basi umechagua ushindi.

 

Sloti hii pendwa ya Forest Rock ina alama mbalimbali za wanyama pori wenye kukuletea faida kama vile Sungura alievaa headphone, Paka mwitu mpiga gitaa na Dubu ambaye anasimama kama meneja, Simba ni bonge la msanii na Tembo akiwa kama mpiga ngoma mkubwa. Sio hivyo tu, alama za Karata nazo zipo. Unasubiri nini kujiunga na familia ya washindi ya MeridianbetJiunge leo na ushinde.

Jinsi ya Kucheza Sloti ya Forest Rock

 

Ni rahisi sana kucheza sloti ya Forest Rock, unachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha unapata alama tatu zenye kufanana ili ushinde. Kubwa zaidi ya yote ni pale utakapo pata alama tatu zenye nembo ya mchezo wa Forest Rock ambayo itakulipa hadi mara 20 ya dau uliloliweka. Sio hayo tu, Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet inakupa fursa ya kupata hadi mizunguko 20 ya bure.

 

Ukipata Jokeri tatu kwenye sloti hii utapewa mizunguko mingine zaidi. Sloti hii ya Forest Rock ina chaguo la kubashiri (Gambling option) ambalo linakupa fursa ya kuchagua kati ya kadi mbili ambazo ni Nyekundu na Nyeusi, uchague ipi itaanguka mezani na itakupa mara mbili ya faida uliyoipata. Cheza Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet upate bonasi kibao.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MACHI 26,2023











Share:

Saturday, 25 March 2023

MERIDIANBET YAZINDUA DUKA JIPYA FIRE

Mabingwa wa michezo ya kubahatisha Meridianbet baada ya kusubiri kwa hamu duka jipya hatimaye leo hii mtaa wa Fire jijini Dar es salaam kunameremeta kwani limezinduliwa duka kwa ajili ya kubashiri michezo mbalimbali huku ODDS KUBWA kama mvua zikimwagika kila siku kazi inabaki kwako tu kuweka dau na kubashiri. 


Duka hili litawawezesha wakazi wa Fire na wengine wapita njia kubashiri wakichagua machaguo zaidi ya 1000 wanayotaka.

 

Hii si mara  ya kwanza Meridianbet wanazindua duka ni kawaida yao kwani mpaka sasa wana maduka mengi sana kwaajili ya kubetia katika maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam kila mtaa ni wao tu rangi nyekundu ipo kila mahali na sasa wana Jackpot kubwa kabisa.

 

Beti na Meridianbet mechi za ligi zote, odds ni kubwa sana, usikose pia Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet yenye michezo rahisi ya sloti kama Poker, Aviator, Roulette.

 

 Baada ya uzinduzi wa duka hilo mitaa ya Fire, Bwana Twaha Ibrahim ambaye ni mkuu wa kitengo cha Maudhui Meridianbet kwanza alisema kuwa; “Duka hili ambalo tumezindua ni la nne kwa mwezi huu, na hakika natumaini mmefurahi sisi kuwaletea duka hili kwaajili ya kuwarahisishia kwenye shughuli zenu za kubetia”

 

Twaha hakuishia hapo aliwashukuru watu wote ambao walihudhuria kwenye uzinduzi huo na kuwaambia kuwa hawajakosea kuchagua Meridianbet kwenye kubashiri kwani Meridianbet hutoa kile ambacho wanakitaka na pia ODDS KUBWA zipo hapa.

Pia tembelea tovuti ya Meridianbet meridianbet.co.tz kuona ongezeko la odds kubwa na machaguo kibao.

 

Meridianbet pia wana kile ambacho unakipenda ambapo michezo ya kasino ya matandaoni hapa ndipo mahali pake kuna sloti za kijanja na michezo rahisi kushinda kama Aviator, Poker na Roulette, jiunge Meridianbet uwe moja ya washindi wa kila siku. Pia unaweza kubashiri  mubashara mechi hizo.

Share:

FALSAFA YA MONTESSORI YATUMIKA KUWANOA WALIMU KAGERA


Baadhi ya Walimu kazini waliohitimu kozi maalumu ya mafunzo mbinu yaliyofanyika kwa miezi sita katika Chuo cha Partage Montessori cha Bukoba
Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Erasto Yohana Sima akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila wakati wa mahafali ya mafunzo mbinu kwa walimu ishirini wa shule za msingi Mkoani Kagera yaliyoendeshwa kwa miezi sita katika Chuo cha Partage Montessori.
Baadhi ya wahitimu wa kozi ya miezi sita kwa walimu kazini kupitia Chuo cha Ualimu Partage Montessori wakipokea vyeti wakati wa mahafali ambayo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Erasto Yohana Sima kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila
Mkurugenzi wa Shirika la Partage Philippe Krynen(kulia) na Mkuu wa Chuo cha Ualimu cha Partage Montessori cha Bukoba Mkoani Kagera Jacqueline Mwombeki, wakifuatilia matukio wakati wa mahafali ya mafunzo mbinu ya Walimu kazini awamu ya kwanza.
Baadhi ya watoto wanaosoma katika shule ya awali ya Partage ambapo mafunzo yake hufanyika kwa vitendo zaidi kwa kutumia mbinu za Mwanafalsafa Maria Montessori
Mdhibiti Ubora wa Shule kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Agusta Lupokela akitoa salamu wakati wa mahafali ya wahitimu ishirini kutoka shule za msingi za Serikali Mkoani Kagera yaliyoendeshwa kwa miezi sita katika Chuo cha Ualimu cha Partage Montessori Bukoba.

Na Mwandishi wetu

Walimu ishirini walio kazini kutoka shule za msingi za Serikali Mkoani Kagera wamenolewa kutumia Falsafa ya Maria Montessori ambayo watoto wadogo hufundishwa zaidi kwa vitendo huku wakijengwa Kisaikolojia ili wapende kujifunza.


Akifunga mafunzo hayo ya miezi sita yaliyoendeshwa na Chuo cha Ualimu cha Partage Montessori cha mjini Bukoba, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila,amewataka wahitimu kutumia mbinu walizopata kuwasaidia wanafunzi kubadili tabia ili kujenga jamii bora.


Mkuu huyo wa Mkoa ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba,Erasto Yohana Sima,alisema wanatakiwa kuonesha matokeo chanya huku wakitumia lugha rafiki kwa wanafunzi,na kutaka ufuatiliaji uwe unafanyika.


"Elimu mliyoipata isaidie kutatua changamoto za kielimu likiwemo suala la malezi ya watoto wadogo katika jamii yetu,tumieni lugha rafiki na ifikapo mwaka 2025 Halmashauri zitatoa walimu wengi zaidi wa kunufaika na mafunzo haya",alisema Sima.


Naye Mdhibiti Ubora kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia,Agusta Lupokela alisema Serikali kwa kushirikiana na Wadau wengine wataendelea kusimamia elimu inayotolewa katika ngazi zote na kuwa Shirika la Partage limefanikiwa kutekeleza makubaliano ya mradi.


Aliwaasa wahitimu kujenga taswira njema na kuwa msaada kwa wengine ambao hawajanufaika na mafunzo hayo na kuwa suala hilo linatakiwa kuwa endelevu huku akipongeza Mkoa wa Kagera kwa kuhakikisha hatua hiyo inafanikiwa.


Mkuu wa Chuo cha Ualimu Partage Montessori, Jacqueline Mwombeki,alisema mafunzo mbinu ya Walimu kazini yanajenga hamasa kwa watoto na kuwafanya waongeze bidii katika masomo yao ili waweze kufikia ndoto zao.

Alisema walimu watabadili tabia za watoto bila kutumia nguvu ikiwa ni pamoja na kutowapa adhhabu kali huku wakitumia mbinu walizojifunza kurekebisha tabia za watoto kwa kutumia lugha rafiki itakayowavuta wapende kujifunza.


Maria Montessori ni Mwanafalsafa wa Kitaliano aliyezaliwa mwaka 1870. Alianzisha mbinu za kuwafundisha watoto kwa vitendo zaidi na alitumia muda wake mwingi kutoa elimu kwa watoto waliotoka kwenye familia zenye kipato duni.


Katika risala yao wahitimu hao waliomba Serikali iboreshe miundombinu ya vyumba vya madarasa hasa kuaznia awali hadi darasa la tatu ili waweze kuutumia zana wezeshi watakazopewa kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwa na kabati imara za kutunzi zana hizo.


Pia walisema idadi ya walimu waliopata mafunzo hayo ni ndogo ikilinganishwa na ukubwa wa mahitaji,huku wakihaidi kuonyesha matokeo chanya baada ya mafunzo kwamba pia wamefundishwa kutambua mahitaji ya kundi hilo kwa kuzingatia umri wao.

Share:

TGNP YAWAKUTANISHA WANAUME KUJADILI MASUALA YA NAFASI YA WANAUME KATIKA KUENDELEZA USAWA WA KIJINSIA

Meneja wa Fedha TGNP Bw.Altho Mwangoa akizungumza katika Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia kilichofanyika leo Machi 25,2023 kwenye ukumbi wa Lost Beach Jijini Dar es Salaam.

********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Lengo la usawa wa kijinsia katika Nyanja zote ni kwaajili ya kuboresha hali za kiuchumi, kuhimiza ustahimilivu, kuleta haki kwa kila mmoja (hasa haki ya kuishi) mwisho wa siku kujenga taifa lililo bora.

Ameyasema hayo leo Machi 25,2023 Jijini Dar es Salaam, Meneja wa Fedha TGNP Bw.Altho Mwangoa wakati akifungua Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia .

Amesema kuwa dhana ya wanaume kufunguka kulingana na mila na desturi kunamaanisha udhaifu na fedheha lakini, unapowaweka wanaume pamoja katika kundi, wanajiamini zaidi, wanazungumza akili zao, na wanapatikana kihisia.

"Jamii imewafundisha wanaume ''man up'' na kukabiliana na mapambano yao. Hata hivyo, wakati kuna nafasi salama ambapo wanaweza kuzungumza juu ya siri zao za giza, matamanio ya kujificha, au mawazo yao juu ya uanaume (masculinity), hubadilisha maoni yao juu ya hisia na ufanyaji maamuzi". Amesema.

Pamoja na hayo amesema takwimu mbalimbali zinaonesha kuwa bado kuna pengo kubwa la wanawake katika sekta ya teknolojia nchini, na kulingana na takwimu za GSMA Intelligence, Tanzania inapengo la kijinsia kwa asilimia 11 ambapo wanawake (asilimia 77) na wanaume (asilimia 86).

Kwa upande wa washiriki wameipongeza TGNP kwa kuwapa nafasi kushiriki kongamano hilo kwani wameweza kupata uelewa kuhusu sheria za kutumia mitandao ya kijamii pamoja na madhara yatakayojitokeza pindi udhalilishaji kwa wanawake utakapojitokeza.

Bw.Benard Mwakyembe ambaye ni mmoja wa washiriki amesema amejifunza jinsi ya kupambana na ukatili wa kijinsia mitandaoni hivyo ameshauri makongamano kama haya yafanyike kuanzia ngazi ya vijiji, mitaa, kata, pamoja na wilaya ili kutoa mafunzo zaidi kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia na jamii ipate uelewa mkubwa na kutokomeza vitendo hivyo.

"Tuwe huru kwenye mahisiano yetu kuhusu hizi simu za smartphones kwani tukiwa wazi hatutaweza kuweka contents za kuwadhalilisha wamama na mabinti zetu mitandaoni". Amesema mmoja wa washiriki wa Kongamano hilo.

Meneja wa Fedha TGNP Bw.Altho Mwangoa akifungua Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia kilichofanyika leo Machi 25,2023 kwenye ukumbi wa Lost Beach Jijini Dar es Salaam. Mwezeshaji Adv.Pasiense Mlowe akizungumza katika Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia kilichofanyika leo Machi 25,2023 kwenye ukumbi wa Lost Beach Jijini Dar es Salaam. Mwezeshaji Dkt.Kitanta Simwanza akizungumza katika Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia kilichofanyika leo Machi 25,2023 kwenye ukumbi wa Lost Beach Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya washiriki wanaume wakifuatilia Kilinge salama maalumu cha wanaume kugusia masuala ya Nafasi ya wanaume katika kuendeleza usawa wa kijinsia kilichofanyika leo Machi 25,2023 kwenye ukumbi wa Lost Beach Jijini Dar es Salaam.
Share:

BABA MWENYE NYUMBA ACHARAZWA VIBOKO HADHARANI BAADA YA KUNASWA AKIPAKUA ASALI YA MPANGAJI WAKE


Wakazi wa kijiji cha Kibwera wilayani Geita mkoani Geita nchini Tanzania wamemuadhibu mwanamume mmoja kwa kuvuka mipaka ya maadili.


Mwanaume huyo aliyetambulika kwa jina la Katayo Bote alinaswa na mke wa mtu mwingine wakirushana roho hali iliyowakasirisha wakazi wa eneo hilo.


Katayo alipigwa viboko hadharani na kutozwa faini ya shilingi Laki mbili kufuatia kisa hicho kilichowaudhi wenyeji. Emmanuel Ndalawa aliyeumia moyoni alisema alimfumania Katayo akimtafuna mke wake mdogo chumbani kwake.

Ndalawa alisema kwa siku nyingi, aligundua mpenzi wake alikuwa akionesha upendo usio wa kawaida kwake Katayo tangu walipohamia eneo hilo.


Ndalawa ambaye ana wake wawili, alisema alimkuta mke wake wa pili na mdogo akijivinjari na Katayo, baba mwenye nyumba waliyopangisha.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger