Monday, 20 March 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 20,2023


 

Share:

Sunday, 19 March 2023

SERIKALI YASAINI MKATABA WA UJENZI WA BARABARA YA UTETE-NYAMWAGE NA DARAJA LA MBAMBE WILAYANI RUFIJI

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mohammed Mchengerwa wakishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani.Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya akiwa pamoja na Mbunge wa Jimbo la Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mohammed Mchengerwa wakishuhudia utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani. Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani.Mbunge wa Jimbo la Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mohammed Mchengerwa akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe.Aboubakar Kunenge akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani. Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) Mhandisi Rogatus Matavila akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani.Viongozi wa Ulinzi na Usalama wakiwa katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani. Watumishi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) wakiwa katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani. Baadhi ya wahandisi wakiwa katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami uliofanyika leo Machi 19, 2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

***************************

NA EMMANUEL MBATILO NA MWAMVUA MWINYI, PWANI

Wakati leo Rais wa Jamhuri ya Muungano anapongezwa na Wanawake wote kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) historia inaandikwa kwa Serikali yake kutia saini mikataba ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage (33.7km) na daraja la Mbambe (81m) ikihusisha barabara unganishi (3km) kwa kiwango cha lami.

Ambapo Serikali kupitia Wakala wa barabara Tanzania (TANROADS) wameingia mkataba na Kampuni ya China Railways Seventh Group Limited kutekeleza ujenzi wa barabara ya Utete -Nyamwage km.33.7 pamoja na Kampuni ya Nyanza Roads Works katika ujenzi wa daraja la Mbambe.

Zoezi hilo limefanyika leo Machi 19,2023 katika Viwanja vya Azimio Utete Rufiji mkoani Pwani huku Mbunge wa Jimbo la Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Mohammed Mchengerwa kushuhudia zoezi hilo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Mhe. Mchengerwa ameipongeza Serikali kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage na amewaomba wakandarasi waanze ujenzi kwa kuanzia Utete hadi Nyamwage badala ya kuanzia Nyamwage kwenda Utete.

Mchengerwa amesema wanaRufiji walisubiri kwa kipindi chote ,na Sasa wanaishukuru Serikali kwa maendeleo yanayofanyika na kwenda Kuwa kitovu Cha maendeleo kupitia ujenzi wa miundombinu.

"Walipita viongozi mbalimbali kwa nyakati tofauti,na kila mmoja kuipigania Rufiji kadri ya uwezo wake na leo tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya miaka miwili kutuletea Neema hii ya barabara ya Utete -Nyamwage kwa zaidi ya Bilioni 67" Amesema Mhe.Mchengerwa.

Nae Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema gharama za ujenzi wa barabara ya Utete-Nyamwage na Daraja la Mbambe zitagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100 wakati miradi yote itagharimu zaidi ya sh.Bilioni 67 hadi kukamilika kwake.

Aidha Mhandisi Kasekenya ameiagiza TANROADS kusimamia ujenzi huo na kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kuzingatia thamani ya fedha.

Amesema ujenzi wa miundombinu inaendelea kujengwa na kutanua mtandao wa barabara nchini ambapo hadi sasa zimeshajengwa km. 11,000 huku km.24,000 zikiwa bado zinahitaji lami.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROAD) Mhandisi Rogatus Matavila amesema upembuzi yakinifu wa barabara hiyo ulianza 2014 ambapo kutokana na muda kupita 2019 usanifu ulipitiwa upya .

Ameeleza kuwa zabuni ilitangazwa Sept mwaka 2022 na kufunguliwa November 2022 na baada ya tathmini kukamilika ilishinda Kampuni ya China Bil 43.4 bila VAT na itajengwa kwa muda wa miaka miwili.

Akielezea kuhusu ujenzi wa Daraja la Mbambe Mhandisi Matavila amesema kuwa Daraja la sasa limejengwa kwa mbao ni jembemba lenye njia moja ya kupita magari na halina uwezo wa kubeba magari yasiyozidi tani tano na Lina miaka 30.

Pamoja na hayo amesema Daraja litakalojengwa litakuwa na njia mbili na upana wa mita 7.5 na upana wa Jumla mita 10.5 ,nguzo mbili za pembeni mwanzo na mwisho wa Daraja kukutana na barabara zote ili kuwezesha kupanda juu ili lisiathirike na maji.

"Ujenzi huo utaenda Sambamba uwekaji wa alama za barabarani na kuweka taa za barabarani solar lights 18 ambazo zitasaidia kulinda usalama wa watumiaji nyakati za usiku." Amesema Mhandisi Matavila.
Share:

CPB YATEKELEZA KWA VITENDO JUHUDI ZA RAIS SAMIA KUKUZA SEKTA YA KILIMO

Meneja wa Nyanda za Juu Kusini Dkt. Samweli Jasper akionesha shehena ya unga unaosagwa katika kiwanda chao na kuhifadhiwa vizuri.


Na Mwandishi wetu,IRINGA.

BODI ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) imetekeleza kwa vitendo juhudi za Rais Samia Suluhu Hassani katika kukuza sekta ya Kilimo nchini, kwa kuwahudumia wananchi na kuwapa ahueni kwa kuwauzuia bidhaa zao kwa bei nafuu na zenye ubora.

Aidha CPB imelenga kukuza Uchumi wa Nchi na Mwananchi mmoja moja kwa kuuza bidhaa zao nje ya nchi na ndani ya nchi lakini katika ubora unaozingatia Afya kwa maana ya kuhakikisha virutubisho vyote vilivyomo katika Nafaka vinakuepo katika bidhaa zao.

Meneja wa Nyanda za Juu  Kusini wa CPB Dkt Jasper Samweli amesema hayo mkoani hapa wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu bodi hiyo inavyosimamia sekta ya kilimo na kueleza kuwa  ipo kwa ajili ya Wananchi kwa kuwapa bidhaa iliyo na kuwauzia kwa bei nafuu kwani hilo ndio lengo la Serikali ya Rais Samia.

‘’CPB inamuunga mkono Rais Samia kwa vitendo kwa kutoa huduma iliyo bora kwa Wananchi kuhakikisha wanakula vyakula vilivyopimwa na kuchakatwa kwa usahihi bila kupoteza virutubisho vilivopo katika mazao’’, alisema Dkt. jasper amesema.
8
Aidha Meneja huyo amesema Rais Samia Suluhu ametoa zaidi ya Billioni 200 katika sekta ya Kilimo hivyo CPB haina budi kufanya kazi kwa uhakika na umakini ukilenga kuwasaidia wananchi katika kupata chakula bora.

Meneja huyo amesema  kuwa CPB Nyanda za Juu Kusini wamekuwa wakihudumia katika Mikoa ya Mbeya, Ruvuma, Songwe, Njombe na Iringa yenyewe hivyo wananchi wa ukanda huo wamekuwa wakipata huduma ya kuuziwa bidhaa zao na kunufàika kupitia sekta hiyo.

"Lengo la CPB ni kuinua Uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini na wa Nchi pia, hivyo tunanunua mazao kutoka kwa wakulima wa ukanda huu na kuyachakata, kusindika na kusaga alafu tunawauzia bidhaa zetu kwa bei nafuu ukilinganisha bei za sehemu nyingine’’, amesema Meneja huyo.

Amesema katika kukuza Uchumi wa Nchi CPB imekuwa ikiuza bidhaa zake nje ya nchi kama vile Rwanda,  Kenya na Malawi na kwamba  bidhaa zao zipo katika kila ujazo kwani wanauza rejereja na jumla hivyo wamekuwa wakiuzia wafanyabiashara wakubwa,wakati na wadogo pamoja na wananchi wa kawaida.

‘’Tuna mtambo ambao una uwezo wa kuzalisha tani 50 hadi 55 za mahindi  kwa siku ambao ukisagwa zinatoka tani 45 za unga,ni juhudi kubwa ambayo imetokana na Serikali, ili kuwafikia wananchi wote CPB inatarajia kuweka Mawakala wa bidhaa zao kila Mkoa ambao watakuwa wakisambaza bidhaa hizo,"anafafanua Meneja huyo.
Share:

JISHINDIE TZS 800,000/= KASINO YA MTANDAONI


Ajira imekuwa ni kilio kwa watu wengi sana, kuna waliosoma na kufika elimu kubwa tu lakini wanahangaika bila kazi, leo nakwambiajee unaweza ukaondokana kwenye janga la kutokuwa na ajira kwa kuichagua Meridianbet, kwa sababu kutoka kasino ya mtandaoni inatoa TZS 800,000/= kwa washindi wa michezo ya Expanse.

 

Meridianbet wakali wa Kasino ya mtandaoni wenye sloti rahisi kushinda kama Aviator, Poker na Roullete wanagawa mpunga wa kutosha mwezi huu, usipange kukosa. Michezo ya sloti inayohusika kutoa mtonyo huu ni Book of Egypt, Bounty hunters, Capital City Derby, Forest Rock, Pirates Power, Spinning Buddha, The Book of Eskimo, Wild icy fruits.

 

Jinsi ya Kushiriki kwenye Promosheni hii

 

Ni rahisi sana wala huhitaji kutumia nguvu kubwa, ni kama kumsukuma mlevi vile hata kwa kutumia kidole anasogea tu. Cha kufanya zingatia yafuatayo ili kuwa moja ya wachezaji wazuri wa Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet:

 

• Promosheni ya mashindano ya Expanse - itafanyika katika kipindi cha kuanzia Machi 17 mpaka Machi 22-2023.

 

•Promosheni hii itahusisha wachezaji waliosajiliwa kwenye APP ya simu na tovuti ya  www.meridianbet.co.tz

 

•Wakati wa ofa, wachezaji hushindana kulingana na idadi ya mizunguko inayochezwa kwenye michezo ya watoa huduma ya Expanse kutoka kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Michezo ambayo inahusika wakati wa mashindano ni: Book of Egypt, Bounty hunters, Capital City Derby, Forest Rock, Pirates Power, Spinning Buddha, The Book of Eskimo, Wild icy fruits.

 

•Orodha ya nafasi iko ndani ya mchezo na itaonekana saa 24 baada ya mwisho wa mashindano.

 

• Kulingana na orodha ya mwisho ya nafasi, wachezaji 5 walioshika nafasi za juu watatunukiwa bonasi za kasino ya mtandaoni katika viwango vifuatavyo:

 

       •1. Nafasi ya Kwanza       250,000 TZS

       •2. Nafasi ya Pili               200,000 TZS

       •3. Nafasi ya Tatu            150,000 TZS

       •4. Nafasi ya nne              100,000 TZS

       •5. Nafasi ya Tano            100,000 TZS

 

• Ili bonasi ya kasino ya mtandaoni iliyokabidhiwa ihamishwe kwa akaunti ya pesa ya mchezaji, ni muhimu kuiwekeza mara 30 kwenye mchezo wowote wa yanayopangwa wa mtoa huduma wa Expanse. Ushindi wa juu unaoweza kutolewa ni 500,000TZS.

 

•Ofa hii ni halali kwa kila mtumiaji, anwani ya IP na kaya.

 


Share:

WASHIRIKI KONGAMANO LA GESI WAPONGEZA UWEKEZAJI ORYX GAS


Matukio mbalimbali katika picha baada ya washiriki wa Kongamano la Kimataifa la Gesi 2023 kutembelea Kampuni ya Oryx Gas iliyoko Kigamboni jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuona shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo katika kuendeleza sekta ya gesi . 


********** 


Na Mwandishi Wetu 


WASHIRIKI kongamano la kimataifa la wadau wa gesi Afrika Mashariki ambalo pia limehusisha mataifa mengine wamefanya ziara ya kutembelea Kampuni ya Oryx Gas huku wakieleza kuvutiwa na uwekezaji uliofanywa na kampuni hiyo. 


Wakizungumza baada ya ziara hiyo iliyofanyika katika kiwanda cha kampuni hiyo siku mbili baada ya kumalizika kwa kongamano hilo, baadhi ya washiriki hao wamesema wamevutiwa na teknolojia ya kisasa inayotumika katika ujazaji wa gesi, matengenezo ya mitungi na usafirishaji. 


Akizungumzia ziara ya washiriki hao, Meneja Operesheni wa Oryx Gas Lukas Banzi, amesema wadau hao wamefika kiwandani hapo na kuona shughuli mbalimbali zinazofanyika. 


“Wameona mitambo yetu ya kisasa kabisa, jinsi tunavyojaza gesi kwa kuzingatia ubora, tunajaza gesi kwa mitambo iliyothibitishwa kwa ubora na tunawahakikishia wateja bidhaa ambazo wanazipata kutoka kwetu zinakwenda sambamba na thamani ya fedha wanayotoa. 


“Kwa hiyo wageni wetu wameona na kufurahia jinsi tunavyofanya kazi, wameona jinsi tunavyohifadhi gesi, tunavyofanyia matengenezo mitungi yetu na usalama uliopo eneo la kiwanda. Tunajivunia kwani mbali ya kusambaza gesi, pia tumetoa ajira kwenye maeneo mbalimbali,” amesema. 


Ameongeza kuwa, wanajivunia kusambaza gesi ya matumizi ya nyumbani, hivyo kuwa sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika kuepusha wananchi kuendelea kutumia nishati chafu ya kupikia hususani kuni, mkaa na badala yake wanatumia gesi kuhifadhi mazingira. 


Kwa upande wake Mratibu wa ziara hiyo ambaye pia ni mratibu wa kongamano hilo la gesi kimataifa 2023, Catherine Ho, amesema washiriki wa mkutano huo wamepata nafasi ya kuona jinsi Tanzania inavyoendelea kujiimarisha katika uwekezaji wa gesi na kutoa fursa kwa wawekezaji kuwekeza katika sekta hiyo. 


“Umefika wakati kwa wadau wa sekta ya gesi Afrika Mashariki, Afrika na dunia kwa ujuma kuunganisha nguvu kwa pamoja kuhakikisha matumizi ya gesi yanapewa nafasi kubwa, yanatumiwa na kila mmoja wetu na kwa usalama,” amesema Ho. 


Wakati huo huo Mkurugenzi wa Kampuni ya Top Masai inayojuhusisha na usambazaji wa gesi, Winner Lukumay, ambaye ni miongoni mwa washiriki waliotembelea Oryx Gas amesema amevutiwa na uwekezaji unaondelea katika sekta hiyo. 


“Uwepo wa nishati ya gesi unaongeza fursa za kibiashara kwa Mtanzania yeyote na kiwango chochote, usambazaji hauishii tu kwa msambazaji mkubwa bali unakwenda hadi kwa msambazaji mdogo, kwa hiyo sekta ya gesi inafungua nchi kiuchumi, imefungua mipaka ya nchi yetu,” amesema. 


Mdau wa sekta ya gesi Mhandisi Isaac Maguhwa ameipongeza Oryx Gas kwa uwekezaji mkubwa ambao umefanyika kwenye kampuni hiyo kwani wameshuhudia mitambo ya kisasa inayotumika kutkeleza shughuli mbalimbali zinazohusiana na gesi. “Tumekuja kwenye ziara hii kuona Oryx Gas nini wanafanya , wamefanya uwekezaji mkubwa lakini mwito wetu Tanzania tumebahatika kuwa na gesi nyingi , hivyo kama nchi tuendelee kuitangaza na kuhamasisha matumizi ya gesi majumbani kufika kwa watu wengi.”
Share:

NEC YATWAA KOMBE LA KAMBA BONANZA LA UKAGUZI


Nahodha wa timu ya Kamba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Robert Keboya akipokea kombe la mahindi wa Kamba kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kicherebaada ya kukamilika kwa Bonanza la watumishi lililoamdaliwa na Ofisi ya CAG na kufanyika viwanja vya Kilimani Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Club ya Michezo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC SPORTS CLUB) Juvenile Kaiza akiwa na kombe hilo.
Bingwa wa Netbal timu ya Ukaguzi ikikabidhiwa Kombe lake.

Bingwa wa Mpira wa Miguu, timu ya Makao Makuu Jogging Club wakikabidhiwa kombe lao.

Mazoezi ya viungo na kukimbia Jogging vilifanyika kabla ya kuanza bonanza hilo.

Watumishi waliokuja na watoto wao wakipiga picha na CAG, Charles Kichere.

Wafukuza upepo nao walikuwepo
Mbio za magunia
Kukimbia na yao kwenye kijiko
Kufukuza kuku mahindi alikua timu ya NEC.
Timu Kamba ya NEC ikiwavuta Ukaguzi.
Mchezo wa Netbal nao ulikuwepo na Ukaguzi kutwaa ubingwa.

TIMU ya Kamba ya Tume ya Aifa ya Uchaguzi (NEC) imefanikiwa kutwaa kombe katika Bonanza la Ukaguzi lililofanyika Jijini Dodoma na kushirikisha timu zaidi ya sita.


NEC ilitwaa ushindi huo baada ya kuwavu ta kwa mivuto miwili Timu ya Ukaguzi.


Katika Mpira wa Miguu NEC hawakufurukuta mbele ya Makao Makuu Jogging baada ya kuwatupa nje kwa mikwaju ya penati ambao badae katika fainali walikutana Ugakuzi na Makao Makuu na Makao Makuu kutwaa ubingwa wa Soka.


Katika mchezo wa Mpira wa Netball timu ya Ukaguzi iliibuka kidedea baada ya kuwatndika bila huruma timu za Wizara ya Afya na Madini.


Mapema akizungumza wakati wa ufunguzi wa bonanza hilo, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere ametoa rai kwa watumishi wa umma wakiwemo wa Ofisi yake kushiri kwenye michezo kwani ni tiba isiyo na gharama.


Taasisi zilizoshiriki mbali na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), Mfuko wa Bima ya Afya ya Uchaguzi(NHIF), Wakala wa Barabara(Tanroads) Ofisi ya Rais Ikulu na Wizara ya Afya.


Alisema ili kuwa na afya njema ni vyema watumishi wakashiriki mazoezi na kusisitiza kuwa mazoezi ni tiba isiyo na gharama kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza na pia kuipunguzia Serikali mzigo wa kuhudumia magonjwa hayo.


"Kazi zetu sisi Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali tunatumia muda mwingi kuandika taarifa hivyo tumekuwa tukiweka utaratibu wa kutoka nje kufanya mazoezi na ni utaratibu mzuri katika kulinda afya za watumishi."


Kichere pia alisema wanatumia bonanza hilo kujiandaa tayari na bonazan lingine litakalokutanisha na wabunge.


" Wabunge ni watu ambao tunafanya kazi nao kwa karibu, hivyo mwezi ujao tutakuwa na bonanza la kushirikiana na wabunge kwa hiyo hii ni sehemu ya mazoezi yetu."


Kichere alisema katika bonanza Hilo pia watalitumia kuchagia damu benki ya Taifa ya damu Ili kusaidia kutoka maisha ya watu wanaohitaji damu.


Naye Mkurugenzi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu kutoka Ofisi ya CAG, Novat Mfalamagoha kutokana na mtindo wa maisha ya mwanadamu mazoezi ni mabadala mzuri wa dawa za hospitali.


Pia alishauri wazazi kujenga tabia ya kuwashirikisha watoto kwenye mazoezi ambayo itawafanya kujenga moyo wa kupenda mazoezi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger