Friday, 17 March 2023

BUNGE LA AFRIKA LAHAMASISHA MATUMIZI YA DAWA ZA ASILI


Makamu wa Rais wa Pili wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament - PAP) Mhe. Dkt. Ashebiri Gayo kutoka Ethiopia akizungumza leo Jumatano Machi 15,2023 wakati anafungua
Warsha ya Pamoja juu ya nafasi ya dawa za asili (Traditional medicine) katika mifumo ya afya ya Afrika iliyoshirikisha Wabunge wa Bunge la Afrika na Wadau mbalimbali wa afya katika Ukumbi wa Bunge la Afrika, Mdrand Afrika Kusini.
Dkt. Gayo amesema suala la dawa za asili linagusa uchumi hivyo kuna uhitaji mkubwa wa kukuza dawa za asili ili kuwezesha kuunganishwa kwake katika mifumo ya afya barani Afrika huku akiliomba Shirika la Afya Duniani (WHO) kushirikiana na Afrika pindi wanapogundua dawa  kwa matumizi mbalimbali badala ya kuweka vikwazo.


"Tunataka kukuza tiba asilia katika nchi zetu za Afrika ili kuchangia katika kuboresha huduma ya afya ya watu wetu lakini pia kuhakikisha nafasi ya dawa za asili katika mifumo ya afya inatambuliwa. Tunataka pia kuhakikisha dawa za asili zinaboreshwa kisasa lakini pia Sheria zinaimarishwa ili kudhibiti utafiti katika dawa za asili",amesema Dkt. Gayo.


Nao washiriki wa warsha hiyo wamesema WaAfrika wanatakiwa kuzipa kipaumbele dawa za asili na kuondokana na mitazamo hasi kwamba kutumia dawa za asili ni ushamba/uchawi/zimepitwa na wakati wakibainisha kuwa hata wakati wa janga na Covid - 19 dawa za asili zimesaidia sana kutibu afya za watu lakini pia dawa hizo zimekuwa zikitumiwa na mababu zetu hivyo ni vyema utamaduni ukaenziwa kwa kuwekewa nguvu zaidi pia kwenye Idara za Afya/Wizara za Afya katika nchi.

Aidha wameshauri Serikali za nchi za Afrika kuongeza Bajeti kwenye eneo la Tiba Asili kwani tiba asilia ni nzuri na ina gharama nafuu.
Makamu wa Rais wa Pili wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament - PAP) Mhe. Dkt. Ashebiri Gayo kutoka Ethiopia akizungumza leo Jumatano Machi 15,2023 wakati anafungua
Warsha ya Pamoja juu ya nafasi ya dawa za asili (Traditional medicine) katika mifumo ya afya ya Afrika. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
 
Makamu wa Rais wa Pili wa Bunge la Afrika (Pan African Parliament - PAP) Mhe. Dkt. Ashebiri Gayo kutoka Ethiopia akizungumza leo Jumatano Machi 15,2023 wakati anafungua
Warsha ya Pamoja juu ya nafasi ya dawa za asili (Traditional medicine) katika mifumo ya afya ya Afrika
Dkt. Georges Ki Zerbo kutoka WHO akiwasilisha mada wakati wa warsha hiyo
Mtaalamu wa Tiba Asili  Rene Munya kutoka Afya Health Products (M- Power & Moringa) akiwasilisha mada wakati wa warsha hiyo

The Pan-African Parliament (PAP) is stepping up parliamentary campaigns on traditional medicine to facilitate its integration into health systems in Africa.

This came out during the PAP Committees’ Joint Workshop on the Place of Traditional Medicine in Africa’s Health Systems, held during the sitting of the Permanent Committees of the sixth Parliament of PAP currently happening in Midrand, South Africa under the AU theme for 2023, “Accelerating the implementation of African Continental Free Trade Area (AfCFTA)”

In attendance were Committee on Health, Labour and Social Affairs, Committee on Gender, Family, Youth and People with Disabilities, Committee on Rural Economy, Agriculture, Natural Resources and Environment, and Committee on Education, Culture, Tourism and Human Resources.

The main objective of the workshop was to sensitise participants on the need to develop traditional medicine to facilitate its integration into health systems in Africa.

“We need to intensify parliamentary advocacy on traditional medicine to establish a comprehensive legal framework for continental herbal trade, and to promote the establishment or strengthening of national and regional research centres to support the development of traditional medicine towards its integration in African Health Systems,” said the 2nd Vice President Hon. Dr Ashebiri Gayo while giving an opening speech of the workshop.

He also acknowledged the importance of traditional medicine and believes that its high time it is accorded its rightful status in the world.

“Traditional medicine, according to academics, is the primary source of healthcare for almost 80% of the population in poor countries. However, unlike Chinese medicine, African Traditional Medicine does not have the same status of being allowed and accepted in the world, which is the challenge we face. Nevertheless, this should be a thing of the past, as it is time for traditional medicine to reclaim its rightful place in the medical fraternity,” said Hon. Dr Gayo.

Hon Jean Patrice France Quirin, Chairperson of the Committee on Health, Labour, and Social Affairs, feels that developing Model Law surrounding traditional medicine will go a long way toward supporting the integration of traditional medicine into Health Systems.

“We need to initiate the development of a Model Law on the integration of Traditional Medicine into Health Systems that will harmonize the strategies of AU Member States through the PAP Committee on Health, Labour and Social Affairs,” he said.

He also discussed how Climate Change is threatening the development of traditional medicine by threatening biodiversity.

“We need to support the development of a Model Law on Climate Change by the PAP Committee on Rural Economy to guide AU Member States to build a collective climate resilience to ensure climate change mitigation and adaptation, and to deliver on Nationally Determined Contributions to achieve greater greenhouse gas emission reductions and ensure an effective planning, implementation, and financing of climate change efforts both at the national and regional levels,” said Hon. Quirin.

-Ends-

Share:

BENKI YA CRDB YATOA ELIMU YA BIMA MAISHA NA FURSA MBALIMBALI ZA KIBENKI KWA VIONGOZI WA VICOBA SHINYANGA

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wambura Wagana akizungumza wakati wa akifungua semina kwa viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga

Na Halima Khoya - Malunde 1 blog

Benki ya CRDB imetoa elimu ya Bima Maisha , huduma mbalimbali za kibenki pamoja na uwezeshwaji Kibiashara kwa viongozi wa VICOBA (wanawake na vijana) Manispaa ya Shinyanga ili kujikwamua kiuchumi na kujiletea maendeleo.


Mafunzo hayo kwa viongozi wa VICOBA yamefanyika leo Jumatano Machi 15, 2023 katika ukumbi wa Empire hotel Mjini Shinyanga.


Akifungua mafunzo hayo, Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wambura Wagana amewataka wana kikundi hao kukata bima ya maisha kwa ajili ya kuwasaidia kipindi cha majanga kama vile kifo kwa mwanakikundi , mwenza wake , mtoto au kupata ulemavu wa kudumu kwa mwanachama mwenyewe akitolea mfano wa Fao la Amani ambalo mteja huchangia 4000/= kwa mwezi na pindi mwanakikundi akifarikidunia benki inatoa pole ya shilingi milioni 10, mwenza milioni 5 , mtoto milioni 3, akipata ulemavu wa kudumu shilingi milioni 10.


Pia amesema benki ya CRDB inatoa bima zingine kwa ajili ya kukinga majanga kama moto, kwenye biashara, nyumba, magari, pikipiki hivyo kuwasihi viongozi hao wa VICOBA kuwa mabalozi kwa wanachama wenzao na wananchi kwa ujumla.



Kwa upande wake Meneja Biashara wa benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddy amewashauri wanakikundi hao kufungua akaunti ambazo hazina riba wala makato ambazo zitasaidia kuwainua kiuchumi wanavikundi na wananchi katika sekta mbalimbali.


Mwanahamisi amezitaja miongoni mwa akaunti zilizopo katika Benki ya CRDB ni pamoja na Junior Jumbo, Fixed Deposit, Malkia account, Dhahabu account , Fahari Kilimo, Hodari account, Nia Moja account na Islamic account ambazo zinatoa huduma bora na zenye kuaminika katika jamii.


Afisa Mahusiano Biashara za Bima Benki ya CRDB tawi la Shinyanga ,Jacob Elias amesema kuwa umuhimu wa bima kwa wanavikundi ni kupata mafao wanapopata changamoto yeyote kulingana na ukubwa wa bima aliyoikata ambapo kwenye bima kuna bima ya magari,nyumba na pikipiki sambamba na bima kwa wanakikundi inayosaidia kutatua tatizo na kutoa msaada wa haraka zaidi.


Kwa upande wake Mchambuzi wa Biashara Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Samson Ngwaltu, ametumia fursa hiyo kutambulisha rasmi Programu ya iMBEJU ambayo inalenga kutoa mafunzo, ushauri, na mitaji wezeshi kwa vijana na wanawake.


“Kwa vijana ambao ni wabunifu siyo lazima awe na akaunti ndiyo apewe mtaji wezeshi bali ni ubunifu wake ndiyo utamfanya afaidike na benki yetu, vijana ni lazima wapitie katika ofisi ya TEHAMA wilayani ili apewe cheti kitakachomuwezesha kupata huduma za kibenki lakini kwa wanawake wanaenda moja kwa moja benki na kueleza ubunifu wao”, amesema Ngwaltu.


Naye Meneja Mahusiano Kilimo Biashara, Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Anselm Mwenda amesema upatikanaji wa mikopo kwa wakulima hulingana na hali halisi ya maisha ya mwanakikundi ambapo dhamana yake ni mali zisizohamishika huku wanavikundi wakiahidi kuyafanyia kazi maelekezo waliyopatiwa na watoa elimu benki ya CRDB ili kuongeza kasi ya maendeleo.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Jumanne Wambura Wagana akizungumza wakati wa akifungua semina kwa viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga
Mchambuzi wa Biashara Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Samson Ngwaltu akitoa elimu kwa viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga
Mchambuzi wa Biashara Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Samson Ngwaltu akitoa elimu kwa viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga
Meneja Mahusiano Kilimo Biashara, Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Anselm Mwenda akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
Meneja Mahusiano Kilimo Biashara, Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Anselm Mwenda akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
Meneja Mahusiano Biashara za Serikali Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Yohana Bunzali akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
 Meneja Mahusiano Biashara za Serikali Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi, Yohana Bunzali akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
Meneja wa CRDB tawi la Shinyanga,Luther Mneney akizungumza kwenye Semina kwa viongzi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa CRDB tawi la Shinyanga,Luther Mneney akizungumza kwenye Semina kwa viongzi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga.
Meneja Biashara wa benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddy akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
Meneja Biashara wa benki ya CRDB Tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddy akizungumza kwenye semina ya utoaji elimu kwa viongozi wa VICOBA Shinyanga.
Viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga wakiendelea na semina.

Viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga wakiendelea na semina.
Viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga wakiendelea na semina.
Viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga wakiendelea na semina.
Viongozi wa VICOBA Manispaa ya Shinyanga wakiendelea na semina.
Share:

KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA NA KUKAGUA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA MKOA WA SHINYANGA

Share:

Thursday, 16 March 2023

NAIBU KATIBU MKUU FEDHA AZIPONGEZA TIRA NA BENKI YA CRDB UANZISHWAJI WA AKAUNTI YA DHAMANA YA BIMA

Dar es Salaam 16 Machi 2023 – Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Bima (TIRA), pamoja na Benki ya CRDB kwa kutekeleza mchakato wa uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima (Trust Account).

Mafuru ametoa pongezi hizo wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya utekelezaji wa akaunti hiyo kwa Wakurugenzi Watendaji na Maafisa Wakuu wa Fedha wa makampuni ya bima nchini yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.

Mafuru amesema uanzishwaji wa Akaunti hiyo ya Dhamana ya Bima ni hatua nzuri ambayo itasaidia kuimarisha usimamizi wa sekta ya bima kuendana na matakwa ya kisheria na udhibiti yaliyowekwa na TIRA.

Akielezea changamoto za hapo awali, Mafuru amesema utaratibu uliokuwa ukitumika mwanzoni katika usimamizi wa dhamana ya bima haukuwa mzuri jambo ambalo lilipelekea TIRA kushindwa kusimamia vizuri amana hizo pindi ziliporejeshwa kwa makampuni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kuiva.

Amesema kuwa kampuni nyingi za bima zilikuwa zikitumia fedha za amana ya Akiba katika matumizi mengine, pasipo kupata idhini ya TIRA hivyo kupelekea kuingia katika changamoto ya ukwasi, na wakati mwengine kushindwa kulipa fidia kwa wateja kutokana na fedha kuwekezwa katika miradi mingine.

Mafuru alibainisha kuwa uamuzi wa kufungua Akaunti ya Dhamana ya Bima katika benki za biashara ni mwarobaini wa changamoto hiyo, kwani sasa TIRA itaweza kusimamia moja kwa moja fedha hizo za amana za akiba, jambo ambalo si tu litaimarisha usimamizi, bali pia kuboresha maendeleo ya sekta ya fedha.
“Niwapongeze Benki ya CRDB kwa kuwa benki ya kwanza kuungana na TIRA katika uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Akiba. Lakini nimevutiwa na namna ambavyo mmeona kuna umuhimu wa kuandaa mafunzo haya ambayo yanalenga kuwajengea uelewa makampuni ya bima juu ya uendeshaji wa akaunti hiyo,” amesema Mafuru.

Aidha, Mafuru alimtaka Kamishina wa TIRA kuhakikisha kampuni zote za bima zinafuata sheria kwa kuweka dhamana ya amana. Alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia kuchochea mafanikio ya sekta ndogo ya bima kama ilivyoanishwa katika Mpango wa Taifa wa miaka 10 wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Nchini ‘Financial Sector Development Master Plan’.

Akizungumza katika warsha hiyo, Kamishina wa Mamlaka ya Bima, Dkt. Baghayo Saqware amesema chimbuko la Akaunti hiyo ya Dhamana ya Bima ni Kanuni ya Bima ya mwaka 2009 inayozitaka Kampuni za Bima kuweka Amana za Usalama angalau asilimia 50 ya kiwango cha chini cha mtaji halisi wa kampuni husika ya bima.

Dkt. Saqware amesema mwaka jana Mamlaka kwa kushirikiana Chama cha Watoa Huduma za Bima (ATI), walikubaliana kuandaa Mwongozo wa Uwekazaji wa Usimamizi wa Ukwasi ambao pia ulielekeza uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Akiba kupitia benki za biashara ili kuondokana na tatizo la changamoto ya kimtaji au kushindwa kulipa fidia za madai ya wateja wake.
“Mfumo unaokwenda kutumika katika akaunti hii mbali na kuboresha usimamizi, lakini pia ni rafiki na unaleta uwazi zaidi kwa wadau kwa maana ya kampuni za bima. Makampuni yataweza kupata taarifa ya dhamana kwa wakati, na kufanya uwekezaji kulingana na makubaliano na Mamlaka,” aliongezea Dkt. Saqware.

Akitoa taarifa za utendaji wa sekta ya bima, Dkt. Saqware alimjulisha Naibu Katibu Mkuu kuwa sekta hiyo imeendelea kukua kulinganisha na miaka iliyopita. Amesema mwaka jana mauzo ya bima yaliongezeka kwa asilimia 25 kufikia Shilingi Trilioni 1.146 kulinganisha na mauzo ya 2021. Aidha, alibainisha kuwa malengo ya mwaka huu ni kufikia Shilingi Trilioni 1.5.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid ameishukuru TIRA kwa kuipa fursa ya kushiriki katika uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima. Nsekela alipongeza uamuzi wa uanzishwaji wa akaunti hiyo na kusisitiza kuwa inachukua jukumu muhimu katika kukuza uwazi zaidi na uwajibikaji katika sekta ya bima, na kuwa itakwenda kusaidia pia kujenga imani kwa wadau wa sekta hiyo.

Nsekela Akaunti ya Dhamana ya Bima iliyofunguliwa Benki ya CRDB imezingatia kwa asilimia mia moja mapendekezo ya TIRA na wadau wa sekta ya bima, huku akibainisha kuwa akaunti hiyo imeunganishwa na mifumo ya kidijitali itakayosaidia katika usimamizi na utoaji wa taarifa kwa Mamlaka na kampuni za bima.

“Kwa kuzingatia kuwa fedha hizi pia zimekuwa zikitumika kwa uwekezaji wa makampuni, Benki yetu imejipanga kikamilifu katika kutoa ushauri na usaidizi wa uwekezaji kupitia Idara yetu ya Hazina na Masoko ya Mitaji,” amesema Nsekela.

Nsekela alimuhakikishia Naibu Katibu Mkuu kuwa Benki ya CRDB itaendelea kushirikiana na TIRA na wadau wa sekta ya bima kusaidia Kuboresha sekta hiyo. Nsekela alisema Benki hiyo imekuwa kinara katika utoaji wa huduma za bima kupitia mfumo wa BancAssuarance, huku akibainisha kuwa imekuwa ikitoa huduma hizo katika matawi yake, CRDB Wakala, na kidijitali kupitia SimBanking.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru (katikati), Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware (kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB na TIRA walioshirika katika mchakato wa uanzishaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima wakati wa hafla ya mafunzo ya uendeshaji wa akaunti hiyo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB na TIRA.
Dar es Salaam 16 Machi 2023 – Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Bima (TIRA), pamoja na Benki ya CRDB kwa kutekeleza mchakato wa uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima (Trust Account).

Mafuru ametoa pongezi hizo wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya utekelezaji wa akaunti hiyo kwa Wakurugenzi Watendaji na Maafisa Wakuu wa Fedha wa makampuni ya bima nchini yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.

Mafuru amesema uanzishwaji wa Akaunti hiyo ya Dhamana ya Bima ni hatua nzuri ambayo itasaidia kuimarisha usimamizi wa sekta ya bima kuendana na matakwa ya kisheria na udhibiti yaliyowekwa na TIRA.

Akielezea changamoto za hapo awali, Mafuru amesema utaratibu uliokuwa ukitumika mwanzoni katika usimamizi wa dhamana ya bima haukuwa mzuri jambo ambalo lilipelekea TIRA kushindwa kusimamia vizuri amana hizo pindi ziliporejeshwa kwa makampuni kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) baada ya kuiva.

Amesema kuwa kampuni nyingi za bima zilikuwa zikitumia fedha za amana ya Akiba katika matumizi mengine, pasipo kupata idhini ya TIRA hivyo kupelekea kuingia katika changamoto ya ukwasi, na wakati mwengine kushindwa kulipa fidia kwa wateja kutokana na fedha kuwekezwa katika miradi mingine.

Mafuru alibainisha kuwa uamuzi wa kufungua Akaunti ya Dhamana ya Bima katika benki za biashara ni mwarobaini wa changamoto hiyo, kwani sasa TIRA itaweza kusimamia moja kwa moja fedha hizo za amana za akiba, jambo ambalo si tu litaimarisha usimamizi, bali pia kuboresha maendeleo ya sekta ya fedha.
“Niwapongeze Benki ya CRDB kwa kuwa benki ya kwanza kuungana na TIRA katika uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Akiba. Lakini nimevutiwa na namna ambavyo mmeona kuna umuhimu wa kuandaa mafunzo haya ambayo yanalenga kuwajengea uelewa makampuni ya bima juu ya uendeshaji wa akaunti hiyo,” amesema Mafuru.

Aidha, Mafuru alimtaka Kamishina wa TIRA kuhakikisha kampuni zote za bima zinafuata sheria kwa kuweka dhamana ya amana. Alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia kuchochea mafanikio ya sekta ndogo ya bima kama ilivyoanishwa katika Mpango wa Taifa wa miaka 10 wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Nchini ‘Financial Sector Development Master Plan’.

Akizungumza katika warsha hiyo, Kamishina wa Mamlaka ya Bima, Dkt. Baghayo Saqware amesema chimbuko la Akaunti hiyo ya Dhamana ya Bima ni Kanuni ya Bima ya mwaka 2009 inayozitaka Kampuni za Bima kuweka Amana za Usalama angalau asilimia 50 ya kiwango cha chini cha mtaji halisi wa kampuni husika ya bima.

Dkt. Saqware amesema mwaka jana Mamlaka kwa kushirikiana Chama cha Watoa Huduma za Bima (ATI), walikubaliana kuandaa Mwongozo wa Uwekazaji wa Usimamizi wa Ukwasi ambao pia ulielekeza uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Akiba kupitia benki za biashara ili kuondokana na tatizo la changamoto ya kimtaji au kushindwa kulipa fidia za madai ya wateja wake.
“Mfumo unaokwenda kutumika katika akaunti hii mbali na kuboresha usimamizi, lakini pia ni rafiki na unaleta uwazi zaidi kwa wadau kwa maana ya kampuni za bima. Makampuni yataweza kupata taarifa ya dhamana kwa wakati, na kufanya uwekezaji kulingana na makubaliano na Mamlaka,” aliongezea Dkt. Saqware.

Akitoa taarifa za utendaji wa sekta ya bima, Dkt. Saqware alimjulisha Naibu Katibu Mkuu kuwa sekta hiyo imeendelea kukua kulinganisha na miaka iliyopita. Amesema mwaka jana mauzo ya bima yaliongezeka kwa asilimia 25 kufikia Shilingi Trilioni 1.146 kulinganisha na mauzo ya 2021. Aidha, alibainisha kuwa malengo ya mwaka huu ni kufikia Shilingi Trilioni 1.5.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid ameishukuru TIRA kwa kuipa fursa ya kushiriki katika uanzishwaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima. Nsekela alipongeza uamuzi wa uanzishwaji wa akaunti hiyo na kusisitiza kuwa inachukua jukumu muhimu katika kukuza uwazi zaidi na uwajibikaji katika sekta ya bima, na kuwa itakwenda kusaidia pia kujenga imani kwa wadau wa sekta hiyo.

Nsekela Akaunti ya Dhamana ya Bima iliyofunguliwa Benki ya CRDB imezingatia kwa asilimia mia moja mapendekezo ya TIRA na wadau wa sekta ya bima, huku akibainisha kuwa akaunti hiyo imeunganishwa na mifumo ya kidijitali itakayosaidia katika usimamizi na utoaji wa taarifa kwa Mamlaka na kampuni za bima.
“Kwa kuzingatia kuwa fedha hizi pia zimekuwa zikitumika kwa uwekezaji wa makampuni, Benki yetu imejipanga kikamilifu katika kutoa ushauri na usaidizi wa uwekezaji kupitia Idara yetu ya Hazina na Masoko ya Mitaji,” amesema Nsekela.

Nsekela alimuhakikishia Naibu Katibu Mkuu kuwa Benki ya CRDB itaendelea kushirikiana na TIRA na wadau wa sekta ya bima kusaidia Kuboresha sekta hiyo. Nsekela alisema Benki hiyo imekuwa kinara katika utoaji wa huduma za bima kupitia mfumo wa BancAssuarance, huku akibainisha kuwa imekuwa ikitoa huduma hizo katika matawi yake, CRDB Wakala, na kidijitali kupitia SimBanking.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru (katikati), Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware (kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB na TIRA walioshirika katika mchakato wa uanzishaji wa Akaunti ya Dhamana ya Bima wakati wa hafla ya mafunzo ya uendeshaji wa akaunti hiyo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB na TIRA.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger