Friday, 21 October 2022

KANISA LA IEAGT LA MTUNUKU CHETI CHA PONGEZI MKURUGENZI WA MANISPAA YA SHINYANGA KUUBADILISHA MJI KIMAENDELEO

Mchungaji wa Kanisa la IEAGT David Mabushi (kushoto) akimkabidhi cheti cha Pongezi Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura.

Mchungaji wa Kanisa la IEAGT David Mabushi (kushoto) akimkabidhi cheti cha Pongezi Afisa Utumishi wa Manispaa ya Shinyanga Getruda Gisema.

 

Picha ya pamoja ikipigwa mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kukabidhi vyeti vya pongezi.

 Na Marco Maduhu, SHINYANGA

KANISA la International Evangelical Assemblies Of God (IEAGT) Mjini Shinyanga, limemtunuku cheti cha Pongezi Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, pamoja na watumishi kutokana na kazi kubwa ambayo wameifanya ya kuubadilisha mji huo kimaendeleo.



Mchungaji wa Kanisa hilo la IEAGT David Mabushi, amesema kwa kazi kubwa ambayo ameifanya Mkurugenzi huyo ya kuubadilisha mji wa Shinyanga kimaendeleo ndani ya muda mfupi, wameona siyo vyema kukaa kimya, bali wampatie pongezi ili kuendelea kumtia moyo na kuchapa kazi kwa bidii.

“Tangu Mkurugenzi umefika hapa Shinyanga tumeona umeubadilisha mji wetu kimaendeleo, hivyo tumeona sisi kama Kanisa tufike hapa Ofisini kwako ili tukupatie cheti chako cha Pongezi, na Cheti kingine kwa ajili ya watumishi sababu mmefanya kazi kubwa,”amesema Mabushi.

“Nawaombeni watumishi muendelee na moyo huo huo wa kufanya kazi kwa ushirikiano na Mkurugenzi wenu ili kuletea maendeleo wananchi, tumefurahi sana kuona mji wetu unabadilika, na sisi viongozi wa dini tutaendelea kuwaombea,”ameongeza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, amesema cheti hicho cha pongezi ni deni kubwa kwake, katika kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo, huku akihidi kuendelea kuchapa kazi kwa bidii kwa kushirikiana na watumishi, na kuubadilisha mji huo kuwa na hadhi ya Makao Makuu ya Mkoa na kitovu cha kibiashara.

Amesema alipohamishiwa hapa Shinyanga Agost Mwaka jana na Rais Samia Suluh Hassan akitokea Lindi, walikaa na watumishi na kuainisha vipaumbele vyao vya kuubadilisha mji huo, na kuanza na uboreshaji wa utoaji wa huduma za kijamii ili kubadilisha ustawi wa maisha ya wananchi.

Amesema kitu kingine ni kuboresha miundombinu na kuweka mazingira mazuri ya wananchi kufanya biashara, sababu huo ndiyo wajibu wa Serikali katika kuandaa mazingira shawishi ya kibiashara.

“Nawashukuru viongozi wa dini kwa cheti hiki cha Pongezi pamoja na Cheti kingine kwa ajili ya watumishi, ni wahakikishie tu halmashauri ipo kwenye mikono salama, na huu ni mwanzo tu bali tuna mipango mingi ya kuubadilisha mji huu kimaendeleo,”amesema Satura.

Aidha, amewaomba watumishi wa halmashauri hiyo waendelee kuchapa kazi kwa bidii pamoja na ushirikiano, sababu hizo ndiyo nguzo kuu ya kusonga mbele kimaendeleo.
Share:

Thursday, 20 October 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 21,2022
















Share:

TAASISI YA AFRIKA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YA NELSON MANDELA KUINGIZA SOKONI MFUMO WA KUBAINI MACHAPISHO YA WIZI

 
Makamu Mkuu wa Chuo, Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Emmanuel Luoga akizungumza na waandishi wa habari ( hawapo pichani) leo Oktoba 20,2022 jijini Dodoma kuhusu shughuli za taasisi hiyo na mwelekeo wa utekelezaji kwa Mwaka wa Fedha 2022/23


Na Dotto Kwilasa, DODOMA.

MAKAMU Mkuu wa Chuo, Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Emmanuel Luoga
amesema wapo katika hatua za mwisho kuingiza sokoni mfumo wa kubaini machapisho ya wizi ambapo mfumo uliokuwa ukitumika katika vyuo vingi ni wa kutoka nje na wa gharama kubwa.

Hayo yamesemwa leo Oktoba 22,2022 jijini Dodoma na Makamu Mkuu wa Taasisi hiyo, Prof.Emmanuel Luoga,wakati akitoa taarifa  kuhusu Utekelezaji wa Shughuli mbalimbali za taasisi hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Prof. Luoga amesema kuwa Taasisi hiyo imejikita katika matumizi ya TEHAMA ambapo itapata Dola za Marekani milioni 10 mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia, fedha hiyo itatumika kuimarisha mifumo ya TEHAMA na kuhakikisha inapata ithibati ya maabara ya viwango vya kimataifa.

“Taasisi imejikita katika kuboresha ufundishaji kwa kutumia teknolojia ya masafa (e-learning) kwa waadhiri na kupanua wigo kwa wanafunzi walio mbali na kampasi kupata elimu ya masafa,”amesema Prof.Luoga

Amesema kuwa mpaka sasa taasisi imefanya bunifu 73 ambazo ni matokeo ya ushirikiano wa hali ya juu kati ya wahadhiri na wanafunzi pamoja na Serikali na wadau wa maendeleo kutoka nje ya nchi. 

“Katika masuala ya utafiti na ubunifu, mpaka sasa taasisi yetu imefanikiwa kufanya bunifu 73 ambazo ni matokeo ya ushirikiano wa hali ya juu kati ya wahadhiri na wanafunzi pamoja na Serikali na wadau wa maendeleo kutoka nje ya nchi,”Amesema Prof.Luoga

Prof.Luaga amesema kuwa taasisi hiyo kwa kushirikiana na taasisi zingine mbili wanaanzisha Kituo cha Umahiri cha Ndizi ambacho kitahusika na masuala ya utafiti wa mbegu, namna ya kuongeza tija katika upandaji na usimamizi wa zao la ndizi na matumizi bora. 

Aidha amesema Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23, Serikali imeidhinisha bajeti ya takriban Shilingi bilioni 43 kwa ajili ya taasisi hiyo ambapo  kipaumbele kikubwa ni ujenzi wa bweni maalum kwa ajili ya wanachuo wanawake wenye mahitaji maalum na wenye watoto wadogo ambao mradi huo  tayari umeshaanza tangu Oktoba, 2021 na kiasi cha Shilingi bilioni 1.7 kimeshatumika.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-Maelezo  na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema kuwa serikali inafanya kazi kubwa kuandaa wanasayansi kutoka shule za msingi mpaka shahada za kwanza ambapo kwa sasa inajenga shule moja ya sekondari ya masomo ya sayansi kwa kila mkoa kwa ajili ya wasichana. 


"Nitoe wito kwa vyuo mbalimbali nchini kuweka kozi za umahiri kwa Waandishi wa Habari ili wakafanye tafiti za kutosha, hivyo kuondokana na kutoa habari za uongo na zisizokuwa na tija kwa umma,"amesema




Share:

NAIBU WAZIRI KIPANGA AFURAHISHWA NA WANUFAIKA WA SDF


Mgeni rasmi wa kilele cha maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima nchini, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Juma Kipanga amefurahia kuona wanufaika wa Mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi yanayofadhiliwa na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF) na kusimamiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wanaweza kutumia mafunzo hayo katika kujipatia kipato.

Mhe. Kipanga amesema hayo alipotembelea banda la maonesho la TEA katika kilele cha maadhimisho na maonesho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima yanayoendelea kwenye viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Jijini Dar es Salaam. Juma hilo lilianza tarehe 17-21 Oktoba 2022.

Akiwa bandani hapo Mhe. Kipanga alizungumza na wanufaika wa mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi (SDF), Esther Shebe ambaye ni mkulima wa Uyoga jijini Dar es Salaam pamoja na Azalia Madege ambaye alipata mafunzo ya kuendesha na kutengeneza pikipiki za miguu miwili na mitatu na kwasasa ameajiriwa katika kampuni ya kuagiza na kuuza pikipiki ya Fekon kama fundi.

Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF) ni sehemu ya Programu ya Kuendeleza Elimu ya Ujuzi na Mafunzo ya Stadi za Kazi zenye kuleta Tija katika Ajira (ESPJ) na Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Kukuza na Kuendeleza ujuzi nchini (NSDS) ambayo inasimamiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) na inafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Benki ya Dunia (WB)

Zaidi ya wananchi 36,870 wamenufaika na ruzuku ya Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi ili kuwawezesha kuajiriwa au kujiajiri wenyewe. Awamu ya kwanza ya SDF ilianza kutekelezwa mwaka wa fedha 2018/2019 ambapo Taasisi 15 zilifadhiliwa kwa jumla ya Shilingi Bilioni 3.1 wakati katika awamu ya pili Taasisi 81 zimenufaika kwa ufadhili wa kiasi cha Shilingi Bilioni 9.7 zikitumika kuendesha programu za mafunzo ya ujuzi.
Share:

KATAMBI AZINDUA MPANGO WA MAJUKWAA YA WANAWAKE NA WASICHANA WENYE ULEMAVU

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobass Katambi amezindua Mpango wa Majukwaa ya Wanawake na wasichana wenye ulemavu, Katika Hafla iliyofanyika Jijini Dar es Salaam Leo Oktoba 20, 2022.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger