Tuesday, 12 July 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 12,2022


Magazetini leo jumanne July 12 2022

Share:

MWENYE NYUMBA AEZUA PAA KWENYE VYUMBA VYA WAPANGAJI WAKE NGOKOLO SHINYANGA


Na Mapuli Misalaba Shinyanga

Wapangaji watatu wa nyumba ya mzee Mkama aliyefariki dunia, mtaa wa Mwinamila kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga wameiomba serikali kuingilia kati mgogoro unaowakabili kati yao na mtoto wa mwenye nyumba ili kulinda usalama wao.

Wapangaji hao ambao ni Hidaya Gimbi, Faustine Longino pamoja na Felista Charles wamesema nyumba waliyokuwa wamepanga kwa muda mrefu ametokea mmoja wa watoto wa mzee Mkama aitwaye Neema Mkama na kuezua mabati ya nyumba waliyokuwa wamepanga bila sababu za msingi na kwamba wapangaji hao wamesema hawadaiwi kodi ya nyumba.

Waandishi wetu wamefika kwenye tukio hilo na kuzungumza na Mwenyekiti wa mtaa wa Mwinamila Rukia Athuman ambaye ameeleza kuwa taarifa za tukio hilo amezipokea leo majira ya jioni baada ya wapangaji hao kuezuliwa Mabati takribani 10 kwenye sehemu ya vyumba vyao.

“Majira ya saa kumi na moja nilipigiwa simu na mjumbe kuwa baada ya wapangaji wameezuliwa mabati kwenye vyumba vyao lakini baada ya muda mfipi wakaja hao wapangaji wakanieleza nikawauliza shida ni nini wakasema hatujui ila mwenye nyumba ameleta fundi kuezua mabati kwenye sehemu yetu ila kwenye chumba chake maana tunaishi naye kwake hajaezua” . amesema Mwenyekiti Rukia

Waandishi wa habari wamempata mama mwenye nyumba hakutaka kuzungumza
Share:

Monday, 11 July 2022

FURAHA YAGEUKA KARAHA KWENYE NDOA

Share:

JITIBU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME KWA KUTUMIA FULL POWER

Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;


1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama


Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 au 0754568767  utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

KATIBU MKUU (OWM) PROFESA JAMAL KATUNDU ATEMBELEA PSSSF NA NSSF KWENYE MAONESHO YA SABASABA YANAYOENDELEA JIJINI

Share:

MAJAMBAZI YAVAMIA BAA NA KUUA WATU 15

 





Watu 15 wameuawa kwa kupigwa risasi huku wengine 11 wakijeruhiwa baada ya kuvamiwa na majambazi katika baa moja iliyopo kitongoji cha Soweto nchini Afrika Kusini.

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo ya habari nchini humo, tukio hilo lilijiri usiku wa kuamkia Jumapili, Julai 10, muda mfupi baada ya saa sita usiku.

Watu wengine 11 walijeruhiwa katika kisa hicho ambapo walikimbizwa hospitali huku nane kati yao wakiwa mahututi.

“Ndio, ninaweza kuthibitisha kuwa kisa hicho kilitokea mwendo was aa sita na nusu asubuhi hii,” Kamishna wa Polisi wa Gauteng Elias Mawela amenukuliwa na eNCA, ambalo ni shirika la habari la nchini humo.

Kamishna huyo wa polisi vilevile alisema kuwa waathiriwa ni wa kati ya umri wa miaka 19 na 35. Washukiwa wanaripotiwa kutoroka punde tu baada ya kutekeleza kisa hicho.

“Mwanzo wa upepelezi unaonyesha kuwa watu walikuwa wanaburudika katika eneo moja la burudani. Waliingia na kuwamiminia risasi kiholela,” Mawela alisema.
Share:

Sunday, 10 July 2022

ELIMU MATUMIZI SAHIHI UTUMIAJI CHANDARUA CHA MBU YATOLEWA KWA WAKAZI WAPYA MSOMERA


WANANCHI wa kaya 104 waliohamia Kijiji cha Msomera wilayani Handeni wakitokea Hifadhi ya Ngorongoro wamepatiwa vyandarua vitatu kwa kila nyumba sambamba na elimu sahihi ya matumizi ya chandarua ili kujikinga na malaria pamoja na magonjwa mengine yanayotokana na mabaadiliko ya hali ya hewa.

Akizungumza wakati wa kugawa vyandarua hivyo kwa wananchi hao walioamua kuhama kwa hiari yao kwenye hifadhi hiyo na kuhamia Kijiji cha Msomera ,Tabibu Mwandamizi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Grace Vincent amesema eneo la afya ni muhimu , hivyo wameamua kugawa neti hizo kwa wenzao waliotoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro waliohama kwa hiari yao wenyewe.

“Eneo la afya huwa tunajali sana afya za wakazi hao na hivyo tumenunua vyandarua kujikinga na mbu. Kwasababu Wilaya ya Handeni ni Wilaya mojawapo yenye maralia nyingi , sasa na wao wametoka maeneo yenye muinuko wa juu ambako mbu huwa hawakai.

“Kutokana na hali hiyo tutakuwa nao sambamba na wananchi kwa kuhakikisha wanapata elimu ya vyandarua na tutaitoa nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha wanaenda kuzifunga ndani ya usimamizi na tunahakikisha wanakuwa ndani ya neti hizo ili wasipate malaria kwani kubadilisha hali ya hewa inaweza kuathiri afya zao na sasa tunasema kinga ni bora kuliko tiba.”

Tabibu huyo ameongeza na sio kutumia chandarua tu bali kutumia kwa usahihi maana unaweza kuweka kichwani na ukaacha kufunika miguu wakati miguu nayo ni sehemu ya mwili ambao unaweza kung’atwa na mbu.Unaweza ukawa hujaweka vizuri chandarua , hivyo mbu naye anapata nafasi, hivyo unatakiwa kuhakikisha unaweka neti vizuri ili mbu asipate nafasi,”amesema.

Amefafanua kuwa utaratibu wao wanagawa vyandarua vitatu kwa kila nyumba na wanatoa idadi hiyo kwasababu kila nyumba inavyumba vitatu na lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha wenyeji wao waliotoka Hifadhi ya Ngorongoro wanapata kinga au wanapata tahadhari , kule Ngongoro walikotoka hakuna majani, maana yake mazingira ya kule yako kwenye maeneo ya muinuko hivyo mbu hawezi kuishi vizuri lakini unapobadilisha hali ya hewa ni lazima tuhakikishe unapata huduma nzuri za afya ili miili yao iimarike ili wasije kupata maradhi yatokanayo na mabadiliko ya hali ya hewa.

Aidha amesema iwapo kuna mtu anatumia dawa zake kwa muda mrefu wakifika wataungana na wenzao ili kuhakikisha anaendelea kupata wakati kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupata chanjo kwa usahihi na kwa mama mjamzito watahakikisha anaendelea kwenda kliniki yake ili kujifungua salama.

“Kwa hiyo sisi idara yetu ya afya na kitengo chetu cha zana cha Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro itahakikisha kwanza ni afya ambayo iko sahihi na kwamba wanashauri uangaliaji afya za wakazi hao unatakiwa kufanyika kwa miezi sita.

Kwa upande wake Masiaya Laizer ambaye ni miongoni mwa wakazi walionufaika na elimu hiyo ameishukuru Serikali kupitia NCAA kwa kutuma wataalam wake kuwapa elimu hiyo na kuongeza uelewa wa namna wa kujilinda na kujikinga dhidi ya maambukizi ya malaria katika mazingira hayo mapya.

“Mimi nilitoka Kijiji cha Esere Ngorongoro, kule ni mazingira ya baridi na hakuna mbu. Msomera ni mazingira tofauti na baridi ni ya kawaida na wakati mwingine joto hivyo elimu hii ni muhimu sana kwetu ili tujikinge pamoja na Watoto wetu” aliongeza Laizer.”


Tabibu Mwandamizi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Grace Vincent akeieleza jambo wakati akitoa elimu kwa WANANCHI wa kaya 104 waliohamia Kijiji cha Msomera wilayani Handeni wakitokea Hifadhi ya Ngorongoro namna ya kutumia vyandarua kwa usahihi ili kujikinga na malaria pamoja na magonjwa mengine yanayotokanayo na mabaadiliko ya hali ya hewa.Chini ni picha mbalimbali zikionesha namna gani ya kutumia vyndarua hivyo kutoka kwa Wataalamu wa NCAA.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR-MSOMERA-HANDENI
Share:

ANAYETAKA KUNUNUA MTANDAO WA TWITTER AANZA KUZINGUA


Billionea Elon Musk (Anayetaka kuachana na mpango wa kuinunua twitter)

Elon Musk anataka kuacha azma yake ya kununua mtandao wa kijamii wa Twitter kwa dola 44 (£36bn), akidai kuwa kumekuwa na uvunjaji wa mara nyingi wa makubaliano.


Tangazo hilo ni mabadiliko ya hivi karibuni katika sakata inayoendeelea baada ya mtu huyu tajiri zaidi duniani kuamua kununua Twitter mwezi Aprili.


Bw Musk amesema ameamua kujiondoa kwasababu Twitter ilishindwa kutoa taarifa za kutosha kuhusu idadi ya akaunti gushi na ambazo hazitumiwi.


Twitter inasema inapanga kuchukua hatua ya kisheria kutekeleza makubaliano.


"Bodi ya Twitter Board imejitolea kuzuwia uhamishaji wa fedha kuhusu bei na masharti yaliyofikiwa kati yake na Bw Musk,"Mwenyekiti wa Twitter Bret Taylor aliandika kwenye ujumbe wake wa Twitter, hatua inayoashiria uwezekano wa makabiliano ya muda mrefu ya kisheria baina ya pande hizo mbili.


Makubaliano ya makubwa ya awali yalijumuisha dola bilioni 1 (£830m) bila kuvunjwa.


Mzozo kuhusu akaunti gushi


Mwezi Mei, Bw Musk alisema mkataba ulikuwa "umezuiwa kwa muda" kwasababu alikuwa anasubiri data kuhusu akaunti feki na zisizotumiwa za Twitter.


Mfanyabiashara huyo bilionea alikuwa ameomba ushahidi wa kuthibitisha maelezo ya kampuni kwamba akaunti gushi na zile zisizotumiwa ni sawa na 5% ya watumiaji wa mtandao huo kwa ujumla.


Katika barua iliyowasilishwa na taasisi za usalama za Marekani na tume ya ubadilishaji wa pesa, wakili wa Bw Musk alisema kuwa Twitter ilishindwa au ilikataa kutoa taarifa hizi.
Share:

KAGAME KUWANIA TENA URAIS RWANDA

Rais wa Rwanda, Paul Kagame,amesema atagombea tena urais katika uchaguzi wa mwaka 2024.

Katika mahojiano na televisheni ya Ufaransa, Bwana Kagame mwenye umri wa miaka 64 amesema kuwa "anaangalia uwezekano wa kugombea kwa miaka mingine 20".

"Uchaguzi ni kuhusu watu kuchagua," aliongeza.

Katika mwaka 2015 Bw Kagame alibadilisha katiba na hivyo kumruhusu kubakia mamlakani hadi mwaka 2034.

Katika uchaguzi wa mwishii miaka mitano iliyopita, takwimu rasmi zilionyesha kuwa alishinda kwa 99%ya kura – jambo ambalo wengi nje ya nchi hiyo walilipinga kuwa lisilowezekana.

Rais Kagame alitetea vikali rekodi ya haki za binadamuya Rwanda katika Mkutano wa Jumuiya ya Madola uliofanyika mwezi Juni mjini Kigali.
Share:

CHUMA YA UVCCM 'CHIEF MAKWAIYA' AJITOSA KUGOMBEA UENYEKITI SHINYANGA MJINI


CHIEF Fravian Patrick Makwaiya (kushoto) akikabidhi Fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga, (kulia) ni Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini Naibu Katalambula akipokea Fomu hiyo.
 CHIEF Fravian Patrick Makwaiya (kushoto) akikabidhi Fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga, (kulia) ni Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini Naibu Katalambula akipokea Fomu hiyo.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

CHIEF Fravian Patrick Makwaiya aliyekuwa Afisa Masoko wa Kampuni ya Jambo Food Products ya mkoani Shinyanga, amechukua na kuirejesha kwa wakati fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti ya Umoja wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini.

Amechukua Fomu hiyo leo Julai 10 ,2022 katika Ofisi za (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini na kuirejesha.

Akizungumza wakati wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu hiyo, amesema Umoja huo wa Vijana wa CCM (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini, unahitaji kijana makini, mwenye ushawishi ndani ya Chama na Serikali, na mwenye kuziishi changamoto za vijana na kuzitatua kwa wakati, sifa ambazo yeye anazo.

Makwaiya almaarufu kwa jina la Chuma cha UVCCM, ameongeza sifa zingine ni kusimamia ajenda za vijana kwenye vikao na nje ya vikao, ili aweze kuleta maendeleo ndani ya umoja wa vijana.

"Umoja wa Vijana (UVCCM) wilaya ya Shinyanga mjini, unahitaji kuwa na Mwenyekiti Mchapakazi na Mwaminifu kama mimi Makwaiya na siyo kijana asiyeweza kutatua shida za vijana," amesema Chief Makwaiya.

Aidha, amesema kutokana uzoefu wake wa uongozi alionao ndani ya Chama na Serikali, na amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi ndiyo sababu iliyomsukuma kugombea nafasi hiyo ya Uenyekiti UVCCM wilaya ya Shinyanga, ili kuleta maendeleo ndani ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Kwa upande wake Katibu wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Naibu Katalambula, amesema mpaka sasa waliochukua Fomu kugombea nafasi ya Uenyekiti (UVCCM) wilayani humo wamefika 10.

 CHIEF; Fravian Patrick Makwaiya (kushoto) akikabidhi Fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga, (kulia) ni Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini Naibu Katalambula akipokea Fomu hiyo.
Share:

WAZIRI MAKAMBA KUFANYA ZIARA YA SIKU 21 KUKAGUA MIRADI KATIKA MIKOA 14 NCHINI

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 10,2022 katika Ofisi za Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.

**********************

Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba anatarajia kufanya ziara ya siku 21 kuanzia kesho Julai 11, 2022, katika mikoa 14 na Wilaya 38 kwa lengo la kukagua na kusimamia miradi inayotekelezwa na Wizara hiyo kwa lengo la kuinua uchumi wa Watanzania.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Waziri Makamba amesema kuwa katika ziara yake hiyo atapokea kero na maoni kutoka kwa wananchi kuhusu utekelezaji na changamoto za upatikanaji wa umeme ili Serikali iweze kuzitatua na kuweka sekta hiyo imara Zaidi kwa maendeleo ya Taifa.

“Nitapita katika maeneo niliyoyataja katika mikoa ya Mara, Mwanza, Geita, Simiyu, Kagera, Shinyanga, Tabora, Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe, Ruvuma, na mwisho ni mkoa wa Mtwara lakini mikoa mingine itahusika katika awamu ijayo, na katika maeneo haya nitazungumza na wananchi na kupokea kero na maoni ili kuimarisha utendaji wa sekta ya nishati nchini”, Alisema Waziri Makamba.

Waziri Makamba alisema Kipaumbele katika ziara hiyo itakuwa ni kuelimisha wananchi kuhusu upatikanaji wa matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia, usambaaji wa umeme vijijini na Vitongoji pamoja na upatikanaji wa umeme wa uhakika katika maeneo tajwa.

Maeneo mengine ya kipaumbele katika ziara hiyo ni uboreshaji wa huduma zinazotolewa na Wizara na Taasisi zake na usambazaji wa mafuta salama na ya bei nafuu kwa wananchi ili kuzuia matumizi ya mafuta machafu ambayo yanasababisha uharibifu wa vyombo vyao vya moyo .

Aidha, Waziri Makamba alisema lengo la jumla la ziara hiyo ni kusogeza huduma za Wizara kwa wananchi hasa wale wa maeneo ya vijijini na pia kuongeza uelewa kwa Watanzania kuhusu sekta ya nishati na mageuzi makubwa yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita Chini ya Uongozi wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan yenye lengo la kuhakikisha kwamba sekta ya nishati inachangia katika ukuaji wa uchumi na kuboresha Maisha ya Watanzania
Share:

SIMBA GAS YAJIWEKA TAYARI KWA UCHIMBAJI WA GESI YA UKAA BAADA YA KUPOKEA RIPOTI YA UTAFITI KUTOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye (wa pili kushoto) akimkabidhi Ripoti ya Utafiti wa Gesi Ukaa, Mkurugenzi Mtendaji wa Simbagas, David Ndelwa (wa pili kulia) kwa ajili ya kampuni hiyo kuanza uchimbaji wa gesi hiyo mkoani Mbeya, hafla ya makabidhiano ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa kitivo cha Jiolojia na Madini wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Elisante Mshiu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera.
**


Kampuni ya Kitanzania ya Simba Gas, inajiandaa na uchimbaji wa gesi ya ukaa (Carbon dioxide) huku ikilenga kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya bidhaa hiyo katika soko la ndani na nje.

Uchimbaji utaanza baada ya kupata vibali vyote vya udhibiti kutoka katika taasisi zote zinazohusika.

Haya yanajiri wakati kampuni hiyo ikipata uhakika wa upatikanaji wa gesi ya ukaa katika eneo la Kata ya Suma lililopo Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya baada ya zoezi la utafiti wa miezi miwili lililofanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Simba Gas - ambayo ilisajiliwa mwaka 2021 kama sehemu ya kundi la makampuni ya Simba ikijikita katika kuchimba na kuuza gesi ya ukaa imepokea matokeo ya utafiti kutoka kitivo cha jiologia na Madini cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya Nishati na Madini ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mh. Juma Zuberi Homera.

Gesi ya Ukaa hutumika katika utengenezaji wa vinywaji vyenye gesi, Pia hutumiwa kama kipoozo katika vizima moto kwa kuingizwa katika vifaa vya uokoaji, uchomelea vyuma katika miradi mikubwa, utengenezaji wa barafu kavu (dry ice) zinazotumika kupozea vinjwaji , ulipuaji wa makaa ya mawe, utengenezaji wa vifaa vya mpira na plastiki, ukuzaji wa mimea katika vitalu nyumba na pia kupunguza nguvu za wanyama kabla ya kuchinjwa.

Akiongea wakati wa hafla ya kupokea ripoti ya utafiti, Mkurugenzi wa kampuni Simba Gas ndugu David Ndelwa, alisema soko la gesi ya ukaa linakua kwa kasi kubwa ndani na nje ya nchi. "Kwa sasa, mahitaji ya gesi ukaa katika soko la ndani yanafikia tani 1,060 kwa wiki na tunao upungufu wa tani 360 kwa wiki,” alisema.

Vile vile, mahitaji ya soko la mauzo ya nje la gesi ya ukaa kwa sasa ni takribani tani 2,000 ambapo upungufu ni tani 1,460.

"Inakadiriwa kuwa hadi sasa, soko la kimataifa la gesi ukaa linafikia thamani ya dola bilioni 10.36. Kampuni yetu imejiandaa vya kutosha na itawekeza kwa kiasi kikubwa ili kuhakikisha kuwa tunatumia rasilimali tulizo nazo ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi,” alisema David Ndelwa

David Ndelwa alisema Simba Gas, imefanya utafiti na kuona soko kubwa la gesi ukaa katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Congo, Malawi, Msumbiji, Afrika Kusini, Botswana, Angola, Sudan Kusini, Rwanda na Namibia pamoja na nchi nyinginezo.

“tunatambua kwa kusafirisha gesi yetu nje ya nchi, tutaleta fedha za kigeni nchini. Pia tutazalisha nafasi za ajira za moja kwa moja 150 na zingine 300 za muda maalum” alisema.

Hata hivyo alibainisha kuwa tafiti zaidi zitalazimika kufanyika ili kukidhi matakwa ya kimataifa ya uvunaji wa bidhaa hiyo na ameiomba Serikali kuendelea kuweka mazingira mazuri yatakayovutia ufadhili zaidi wa shughuli hizo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mh. Juma Zuberi Homera, alisema Serikali, inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, inajitahidi kuboresha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji katika sekta ya nishati na viwanda miongoni mwa mambo mengine.

Aliipongeza Simba Gas kwa kuwekeza Mbeya, na kubainisha kuwa kwa kufanya hivyo, kampuni hiyo itakuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha azma ya serikali ya kukuza sekta ya uwekezaji na kuisaidia nchi kukuza uchumi wake.

"Mradi huu utakapoanza rasmi, utazalisha ajira, kuongeza mapato ya serikali za mitaa na kusaidia jamii kupitia mipango ya uwajibikaji kwa jamii," alisema, akibainisha kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono uwekezaji huo.

Naye Mkuu wa kitivo cha Jiolojia na Madini wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Elisante Mshiu alisema anawashukuru kampuni ya Simba Gas kwa kuwaamini wataalamu wa ndani ambao wamejikita kuleta ukombozi na mageuzi makubwa ya kufanya tafiti za kimkakati na kuhakikisha taifa linanufaika na rasilimali zake.

Simba gesi wamedhubutu kufanya tafiti katika uchimbaji wa gesi ukaa, tunaamini watafungua fursa nyingi pia kwa vijana wetu ambao tunawazalisha wakiwa wamebobea katika kuendesha mitambo ya gesi na itafungua milango ya ajira kwa vijana wetu.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa William Anangisye (wa pili kushoto) akimkabidhi Ripoti ya Utafiti wa Gesi Ukaa, Mkurugenzi Mtendaji wa Simbagas, David Ndelwa (wa pili kulia) kwa ajili ya kampuni hiyo kuanza uchimbaji wa gesi hiyo mkoani Mbeya, hafla ya makabidhiano ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam . Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera na kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Simba, Farid Nahdi(kushoto) ni (Kushoto) ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Angelina Ngalula .
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Simbagas, David Ndelwa, akizungumza wakati wa hafla
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya viongozi wa Serikali kutoka mkoani Mbeya wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo.
Share:

Tanzia : BI HINDU AFARIKI DUNIA


Picha ya Bi Hindu enzi za uhai wake

Mmoja wa waasisi wa Kaole Sanaa Bi Chuma Suleiman maarufu kama 'Bi Hindu' amefariki dunia leo nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger