Saturday, 18 September 2021

MBUNGE NEEMA LUGANGIRA :USHIRIKI WA RAIS SAMIA MKUTANO MKUU WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA NI FURSA KWA WATANZANIA

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Mhe Neema Lugangira 
 

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Mhe Neema Lugangira amesema hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, New York nchini Marekani na kulihutubia Baraza hilo itasaidia kufungua fursa nyingi na kuwaweka Watanzania katika nafasi nzuri ya kunufaika 


Mkutano huo unatarajiwa kufanyika Septemba 23 mwaka huu Newe York nchini Marekani

Mbunge Neema Lugangira aliyasema hayo leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ambapo alisema kwa sababu Rais Samia Suluhu anapokwenda kuhudhuria Mkutano huo mkubwa wa Umoja wa Mataifa anakutana na fursa nyingi na mahitaji duniani yapo mengi na ushindani ni mkubwa sana baina ya nchi na nchi hivyo kitendo cha kushiriki kwenye mkutano huo kitafungua milango kwa Tanzania na kuiweka Tanzania katika nafasi ya kupata kipaumbele kwenye fursa mbalimbali.

Alisema kwa sababu Rais Samia amepanga kuwa na mikutano mengine mingi ikiwemo kukutana na wakuu wa Taasisi za Kimataifa na Marais wa Nchi nyengine na kushiriki katika kilele cha mikutano mengine inayohusu Usalama wa Chakula, Mabadiliko ya Tabia Nchi,  na Utekelezaji waMalengo ya maendeleo Endelevu (SDGs)...."Hivyo nikiwa kama Mbunge na Mwenyekiti wa Wabunge Vinara wa Usalama wa Chakula nimefarijika kuona Mhe Rais ameibaba agenda yetu ya Usalama waChakula hivyo tunasubiri kwa hamu kusikiliza hotuba yake na kutekeleza aliyokubaliana na Umoja wa Mataifa na Wadau wengine.

Aidha, Mbunge Lugangira aliwataka Watanzania wakae tayari na kuchangamkia fursa zitakazotokana na ziara hiyo ya Mhe Rais Samia ambayo itakuwa chachu kwa chachu Maendeleo ya Taifa.

“Kwa kweli nimefurahi sana kwa kwa sababu Mhe Rais Samia Suluhu Hassan anakwenda kuhudhuria
Mkutano Mkuu wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na atahutubia kwenye baraza hilo. Ni jambo kubwa sana na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan anastahili pongezi kubwa kwa uamuzi wa kushiriki maana mara ya mwisho Rais wa Tanzania kushiriki mkutano wa Mwaka wa  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ilikuwa ni 2015". 

Mbunge Lugangira alitoa areja mwaka 2019 Tanzania ilifanya tathimini ya utekelezaji wake wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (Sustainable Development Goals- SDGs) na katika tathimini hiyo ilionyesha Tanzania haifanyi vizuri katika lengo la namba 17 (SDG 17) ambayo inalenga mashirikiano na mahusiano baina ya nchi moja na nchi
nyengine na wadau wengine kama Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia na Wadau wa maendeleo. Alisema hivyo ilishauriwa Tanzania iweke jitihada kubwa kuhakikisha inaimarisha mahusiano yake na ushirikino wake ili iweze kutekeza lengonamba 17 (SDG 17).

“Watanzania mtakubaliana nani kwamba tokea Mhe Rais Samia ameingia Madarakani hiyo agenda ya SDG 17 kuhakikisha Tanzania inaimarisha mahusiano na ushirikiano  wake na Mataifa mengine,  Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia, na Wadau wa Maendeleo ameibeba na imekuwa ni moja ya agenda zake kuu.

Mbunge huyo alisema hivyo Mhe Rais Samia amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha Tanzania inaimarisha mahusiano na mashirikiano na tayari Mhe Rais Samia anatekeleza yale yaliyo shauriwa kwenye tathmini ya mwaka 2019.
Share:

AWESO AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI, AWAPA KAZI YA KUKAMILISHA MIRADI YA MAJI YA PEMBEZONI YA DAR


Waziri wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma wakizindua Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) akimkabidhi vitendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira , Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange mara baada ya kuzindua Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso(kulia) akikabidhi vitendea kazi Katibu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam Mhandisi Cyprian Luhemeja mara baada ya kuzindua Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam
Share:

ZILE NDOO ZA KUCHUJIA MAJI YA KUNYWA SASA ZIPO MTAANI KWAKO....PIGA 0753392805

 BS- Africa Water Filters imekusogezea karibu ndoo maalumu za kuchujia maji ya kunywa majumbani ambapo kulazimika kuchemsha maji.

 Ndoo (filters) hizi hazitumii umeme, hazitumii kemikali wala dawa, zinachuja maji na yanakuwa safi na salama. Ndoo hizi ni rahisi kuzitumia na ni rafiki kwa mazingira. 

Punguza gharama za kununua maji lakini pia kuchemsha maji kwa kutumia Filters hizi.

Tunapatikana Majengo Mapya Mjini Shinyanga. Kwa waliopo nje ya Shinyanga utatumiwa mzigo wako kwa wakati na usalama kabisa. 

Mawasiliano piga simu namba 0753392805

Chaguo sahihi kwa ajili ya familia yako, ishi kisasa
Share:

IGP SIMON SIRRO APANGUA MAKAMANDA WA POLISI




Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro amefanya mabadiliko madogo ya makamanda wa Polisi wa mikoa kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa polisi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa jeshi hilo, David Misime imeeleza kuwa, Kamishna msaidizi wa Polisi, ACP Revocatus Malimi amehamishwa kutoka mkoa wa Kagera kwenda makao Makuu ya Polisi Dodoma.

Aidha,nafasi yake imechukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Kamishna Msaidizi waPolisi, ACP Awadhi Juma Haji.

Wakati huo huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Omary Said Nassiri amehamishwa kutoka Makao Makuu ya Polisi Zanzibar na kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi.
Share:

WIZARA YA MIFUGO YAANZA KUBAINI WAFUGAJI WALIOSHINDA KESI MAHAKAMANI

Waziri wa Mifugo Mashimba Ndaki akizungumza na wafugaji.
**
Na Costantine Mathias Meatu
WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imeanza kutekeleza agizo la Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa la kuitaka kuwatambua wafugaji wote walioshinda kesi zao mahakamani  za mifugo lakini hadi sasa hawajaweza kurejeshewa mifugo yao.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Mifugo Mashimba Ndaki kwa nyakati tofauti mkoani Simiyu  katika kijiji cha  Longalambogo wilaya ya Itilima na kijiji cha Mwalilo wilaya ya Meatu wakati akizungumza na wafugaji wa maeneo hayo.

Amesema kuwa wanachokifanya kwa sasa ni kupita katika maeneo yote ambayo wafugaji walikuwa na migogoro na maeneo ya hifadhi za wanyama na mifugo yao kutaifishwa lakini wakawa wameshinda kesi mahakamani ila mifugo yao hawajarejeshewa hadi sasa.

Amesema kuwa kitendo cha kuwadhulumu wafugaji mifugo yao wakati wamepewa haki na vyombo vya sheria hakikubaliki hata kidogo.

Hivyo amewaagiza Wakuu wa wilaya za Itilima na Meatu kuhakikisha wanapeleka orodha ya wafugaji hao pamoja na vielelezo vyao vya kushinda kesi ili aweze kuiwasilisha kwa Waziri Mkuu ambaye naye ataipeleka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maamuzi.

Aidha ameshangazwa na baadhi ya maafisa mifugo katika wilaya kuwageuza wafugaji vitega uchumi vyao kwa kushiriki vitendo vya kuwadhulumu kwa kisingizio kuwa mifugo iliyotakiwa kurejeshwa kwa wafugaji wa wilaya ya Itilima ipatayo 280 imekwisha kufa.
Share:

DKT. TAX : MASUALA YA ULINZI NA SUALA HAYAWEZI KUTENGANISHWA NA MASUALA YA KIDIPLOMASIA


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax

 Na Magrethy Katengu -Dar es salaam

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax amesema serikali itahakikisha inatoa fursa ya mafunzo  ya diplomasia ya mara kwa mara kwa Kamati ya Bunge ya Kudumu  ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama ili kuimarisha maarifa ya wajumbe juu ya masuala mbalimbali ikiwemo uchumi.

Dkt. Tax ameyasema hayo jana wakati akifunga mafunzo ya siku tano ya Wajumbe wa Kamati Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama ambapo amesema Ulinzi na Usalama hayawezi kutenganishwa na masuala ya kidiplomasia kwa kuwa ndiyo maslahi ya taifa.

Ameongeza kuwa Kamati inalo jukumu la kuhimiza matumizi mazuri ya mitandao na nyenzo nyingine za teknolojia kwa kuwa teknolojia isipotumika vyema itahatarisha usalama wa wa taifa. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine amesema mafunzo hayo yamelenga kusaidia kuwajengea uzoefu katika masuala ya kidiplomasia ya uchumi, maslai ya Taifa, uchumi wa blue, na uhifadhi wa nyaraka za kibalozi. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Musa Hassan Zungu amesema taifa haliwezi kukwepa kushirikiana na wawekezaji wa nje kwani kuna miradi mikubwa inayohitaji utekelezaji wa baraka kwa kushirikiana nao itasaidia kupata teknolojia mpya na ubunifu. 

"Uchumi imara unahitaji mabadiliko ya kidiplomasia  hivyo watanzania tusiogope miradi mikubwa ambayo ndiyo chachu ya mabadiliko ya Taifa letu",amesema.

Aidha ameishukuru Wizara hiyo  kwa kuwapatia mafunzo hayo kwani itasaidia wawapo katika majukumu yao kutetea maslahi  mapana  ya taifa
Share:

AMUUA MKE, WATOTO WAKE WAWILI KWA MCHI WA KUTWANGIA


Jeshi la Polisi mkoani Tabora linamshikilia mwanaume mmoja kwa tuhuma za mauaji ya mkewe na watoto wawili wanaodaiwa kuuawa kwa kupigwa kichwani na mchi wa kutwangia kisha miili yao kutelekezwa ndani ya nyumba waliokuwa wakiishi huko katika Kijiji cha Mkolye Wilayani Sikonge mkoani Tabora.

Kamanda wa Polisi mkoa waTabora, ACP Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo majira ya saa moja usiku ikiwa ni mfululizo wa mauaji ya raia wasiokuwa na hatia ambayo yameendelea kutokea wiki hii huko mkoani Tabora.
Share:

RAIS WA ZAMANI WA ALGERIA AFARIKI DUNIA


Rais wa zamani wa Algeria, Abdelaziz Bouteflika, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 84 baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Bouteflika aliongoza nchi hiyo kwa karibu miongo miwili na kuachia madaraka mwaka 2019 baada ya jaribio lake la kugombea muhula wa tano kusababisha maandamano makubwa.

Alikuwa kiungo muhimu katika vita vya kupigania uhuru wa Algeria miaka ya 1950 na 60.

Mwaka 1999, baada ya Algeria kujikwamua kutoka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilisababisha vifo vya karibu watu 200,000, alikuwa raia baada ya kuombwa na jeshi la nchi hiyo.

Bouteflika hajaonekana hadharani tangu mwaka 2013, baada ya kuugua kiharusi ambacho kiliathiri uwezo wake wa kuzungumza na kutembea.

Chanzo - BBC SWAHILI

Share:

Mzumbe University MU second round selected applicants 2021/2022

Mzumbe University MU second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Mzumbe University (MU) for the 2021/2022 academic year second round application window. The Mzumbe University MU second round applications and MU second selection 2021/2022 […]

This post Mzumbe University MU second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

University second round selection 2021/2022

If you have applied for the second-round admission at various universities and colleges , the second-round selection process will be finalized by 06th September 2021 and second selection results will be out by 18th September 2021. Once the selection results are out, All the candidates who have applied for second round admission can visit the […]

This post University second round selection 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Majaliwa: Rais Samia Ametoa Fedha Nyingi Uendelezaji Wa Miradi Ya Maendeleo

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya uendelezaji na ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya maji, elimu na barabara.

Amesema lengo la utekelezaji wa miradi hiyo ni kuboresha maisha ya Watanzania, hivyo amewasihi wananchi wafanye kazi kwa bidii kila mmoja kwenye eneo lake na waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Septemba 17, 2021) wakati akiongea na wananchi wa wilaya za Kasulu na Kibondo mkoani Kigoma baada ya kuzindua ghala la kuhifadhia mazao katika kijiji cha Mvugwe na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji Kifura.

“Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amedhamiria kupeleka huduma mbalimbali za jamii kwa wananchi wote nchini. Huduma hizo ni pamoja na  upatikanaji wa maji safi na salama kwa sababu anajua namna akinamama na vijana wanavyohangaika kutafuta maji.”

Naye, Meneja wa RUWASA mkoa wa Kigoma Mathius Mwenda alisema mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 2.4 mkataba wake ulisainiwa Agosti mwaka huu na unatarajiwa kukamilika Februari mwakani. Mradi huo utakapokamilika utakuwa na vituo 50 vya kuchotea maji.

Meneja huyo alisema kuwa kukamilika kwa mradi huo kunakwenda kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa kijiji cha Kifura, hivyo watahakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyostahiki.

Akizungumza kuhusu ujenzi wa mradi wa ghala la kuhifadhia mazao, Mheshimiwa Majaliwa aliwapongeza kwa kubuni mradi huo na alisisitiza kuwa wananchi hao waendeleze ushirika wao na watumie ghala hilo kwa ajili ya kuuza mazao yao.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Joseph Rwiza alisema mradi huo uliogharimu shilingi milioni 464 unalenga kupunguza upotevu wa mazao, kutunza na kuongeza ubora wa mazao pamoja na kuwepo kwa soko la uhakika na bei yenye tija kwa wakulima.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU



Share:

Serikali Kujenga Vyuo Vya Veta Kwenye Kila Halmashauri

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imedhamiria kujenga vyuo vya Ufundi Stadi (VETA) katika kila halmashauri nchini.

Amesema kuwa lengo la ujenzi wa vyuo hivyo ni kuhakikisha vinatoa elimu ya ujuzi maalum kwa vijana wa Kitanzania katika maeneo mbalimbali ikiwemo utaalam wa TEHAMA, Ufundi Umeme, makenika na maeneo mengine.

Amesema hayo jana Ijumaa (Septemba 17, 2021) wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya Buhingwe ambacho kitagharimu shilingi bilioni 2.4 mpaka kukamilika kwake, ambapo mpaka sasa kiasi cha shilingi bilioni 1.6 zimeshatumika.

“Tulianza na ujezi wa vyuo vya VETA kimoja kimoja kila mkoa, sasa tunashuka chini kwenye kila halmashauri, chuo hichi nimeweka jiwe la msingi leo, maana yake hakitasimama, kitajengwa mpaka kikamilike kwa ajili ya vijana wetu kupata eneo la kujiongezea ujuzi”

Aidha, Waziri Mkuu amepongeza VETA kwa kusimamia maelekezo ya Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya ujenzi wa chuo hicho ambacho kitakuwa mkombozi kwa vijana “Endeleeni kuwa na imani ya Serikali yenu”

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Omary Kipanga amesema kuwa katika awamu ya kwanza wanajenga vyuo vya VETA  29 na zitatumika zaidi ya shilingi bilioni 48.6. “Tutasimamia ujenzi wa vyuo hivi kwa weledi na umakini mkubwa ili kuhakikisha maono ya Rais Samia yanatimia”

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa VETA Dkt. Pacras Bujulu amesema kuwa chuo hicho ambacho kinajengwa kwa gharama za Serikali, kinatarajiwa kuanza kutoa mafunzo ifikapo mwezi Januari, 2022 na mpaka sasa majengo 15 kati ya 17 yameshaezekwa.

Akiongea na wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu baada ya kukagua shamba za chikichi linalomilikwa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Msalaba Mwekundu amewataka wakazi hao kulima zao la chikichi kwa kuwa linafaida kubwa na kwa muda mrefu “chikichi hii unaweza kuivuan kwa miaka 30

Aliongeza kuwa mwaka 2018 Serikali iliamua kuanzisha mbegu yake ya Chikichi  ambayo ni bora zitakazolimwa lengo ni kuhakikisha nchi inajiongezea uchumi kupitia zao la chikichi.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU



Share:

TPSD second round selected applicants 2021/2022

The Tanzania Public Service College Dar es Salaam Campus TPSD second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Tanzania Public Service College Dar es Salaam Campus (TPSD) for the 2021/2022 academic year second round application […]

This post TPSD second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MARUCO second round selected applicants 2021/2022

The Marian University College MARUCO second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Marian University College (MARUCO) for the 2021/2022 academic year second round application window. The Marian University College MARUCO second round applications and […]

This post MARUCO second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

UDSM second round selected applicants 2021/2022

University of Dar es Salaam UDSM second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at University of Dar es Salaam (UDSM) for the 2021/2022 academic year second round application window. The University of Dar es Salaam […]

This post UDSM second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

SUA second round selected applicants 2021/2022

Sokoine University of Agriculture SUA second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Sokoine University of Agriculture (SUA) for the 2021/2022 academic year second round application window. The Sokoine University of Agriculture SUA second round […]

This post SUA second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

UDOM second round selected applicants 2021/2022

University of Dodoma UDOM second round selected applicants 2021/2022 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at University of Dodoma (UDOM) for the 2021/2022 academic year second round application window. The University of Dodoma UDOM second round applications and UDOM […]

This post UDOM second round selected applicants 2021/2022 has been posted by Udahiliportal

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger