Sunday, 12 September 2021

Serikali Yatoa Sh. bilioni 49.5 kuimarisha Shirika la Posta

Na Jonas Kamaleki, Dodoma
Serikali imetoa shilingi bilioni 49.5 kuimarisha Shirika la Posta na hadi sasa  vituo viwili vinavyotoa huduma za pamoja vimeshaanzishwa Dar es Salaam na Dodoma, kwa awamu hii ya kwanza mikoa 10 itafikiwa ikiwemo vituo 2 Pemba na Unguja, Awamu ya pili itafikia vituo (Mikoa) 17 na lengo ni kuwa ifikapo mwaka 2025 mikoa na wilaya zote za Tanzania ziwe na vituo hivi.

Wiki hii Serikali imefanya uzinduzi wa vituo vya huduma za pamoja katika Shirika la Posta. Uzinduzi huu umefanyika Jijini Dar es Salaam na umefanywa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.

Hayo yamesemwa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson msigwa alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari.

“Ningependa kufafanua kidogo kuhusu hizi huduma za pamoja, ni kwamba Serikali imeamua kulifanyia mageuzi makubwa ya kimfumo, kiundeshaji na kiteknolojia Shirika letu Posta ambalo katika miaka ya karibuni lilikuwa hoi biin taabani”, alisema Msigwa.

Moja ya mageuzi hayo makubwa ni kuanzishwa kwa vituo vya huduma pamoja kumwezesha mwananchi kupata huduma mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali katika kituo kimoja. Serikali inataka kupitia vituo hivyo vya huduma pamoja mwananchi akienda pale apate huduma za vitambulisho vya Taifa (NIDA), Huduma za Bima ya Afya, Huduma za Usajili wa Vizazi na Vifo, usajili wa biashara, huduma za kibenki, Huduma za TRA, hifadhi ya jamii na huduma za kusafirisha vifurushi katika kituo kimoja.

Serikali imefanya utafiti na kubaini kuwa kutokana na huduma hizo kutolewa na kila taasisi pekee kivyake, ilikuwa inasababisha usumbufu mkubwa, upotevu mkubwa wa muda na gharama kubwa za watu kufuata huduma. Utafiti umeonesha watu walitumia hadi wiki 4 kupata huduma ambazo sasa zitapatikana katika kituo kimoja kwa muda kati ya dakika chache hadi siku 3.

Aidha, Msigwa amesema kuwa sambamba na hili Serikali inataka Posta iwe shirika linaloendeshwa kisasa. Ukienda kwenye hivi vituo utaona huduma zinatolewa katika madirisha mengi, yaani kila taasisi ina dirisha lake na inatumia mifumo yake. Malengo ya baadaye ni kuwa huduma zile zote zipatikane katika dirisha moja na hiyo itawezekana baada ya mifumo ya kidigitali kuunganishwa.

Lakini huduma zenyewe za Posta zinaboreshwa zaidi ili kwenda kisasa na kidigitali zaidi. Posta hii inakwenda kuwa chombo cha usafirishaji cha kitaifa na kimataifa kama ilivyo vyombo vya mataifa mengine kama DHL, TNT, Royal Cargo n.k, Shirika la Posta linakwenda kuwa Wakala wa mabenki, Bima na taasisi nyingine zinazotoa huduma kwa wananchi, Shirika la Posta tayari limeanzisha Duka Mtandao (www.postashoptz.post) kama ilivyo maduka mtandao ya Alibaba, Amazon, E-bay n.k, na pia Posta inapelekwa kiganjani kwamba sasa Mtanzania na mtu yeyote duniani anaweza kupata huduma za posta kupitia simu ya mkononi. Na Posta ipo kwenye mfumo wa Posta wa Kimataifa na ipo kwa lugha zaidi ya 20.

Ndio Maana unamuona Kaimu Postamasta Mkuu Bw. Macrice Mbodo anatamba kuwa Posta hii sasa sio Posta ya barua tu, bali ni Posta ya Kidigitali. Tayari Serikali imeshatoa shilingi bilioni 3.9 kwa ajili ya kuiwezesha Posta kuimarisha huduma zake za usafirishaji wa vifurushi vya wananchi, aliongeza Msigwa.

“Fursa za kufanikisha jambo hili zipo, Shirika letu la Posta lina ofisi zaidi ya 300 nchi nzima, ni mwanachama wa Umoja wa Posta Afrika na Duniani. Makao Makuu ya Posta Afrika yapo hapa Tanzania pale jijini Arusha. Lakini pia ni washiriki wa Mkutano wa Mawaziri wa Mawasiliano Duniani (hawa ndio Katibu Mkuu wa Posta Duniani na wanatunga sera za Posta), ni wajumbe wa Baraza la Utawala la Posta Duniani ambalo lina wajumbe 40 (hawa ndio wanasimamia utekelezaji wa Sera na Mikakati kutoka kwa Mawaziri) na ni wajumbe wa Baraza la uendeshaji la Posta Duniani (hili ndilo linaendesha shughuli za kila siku za Posta duniani, na zaidi tunaongoza kamati ya biashara mtandao {e-commerce} ya baraza la uendeshaji)”, alifafanua Msigwa.

Mwisho



Share:

RAIS SAMIA KUZINDUA MKAKATI WA UELIMISHAJI, UHAMASISHAJI MASUALA YA SENSA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka 

Na Dotto Kwilasa, Dodoma
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu inatarajia kuzindua Kitabu cha Mkakati wa uelimishaji na uhamasishaji wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 jijini Dodoma huku Rais Samia Suluhu Hassan akitarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka amethibitisha hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu ujio wa tukio hilo ambapo alisema linalenga kuandaa umma na wadau kwa ujumla kwa ujio wa sensa ya watu na makazi ya mwaka ujao.

Mtaka amesema pamoja na Rais Samia,uzinduzi huo pia utahudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,Mwenyekiti wa kamati ya Kuu ya sensa Tanzania bara na visiwani na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdallah.

Viongozi wengine ni "Kamisaa wa sensa Tanzania Bara ,Anne Makinda,Kamisaa wa sensa Zanzibar ,Balozi Mohamed Haji Hamza ,pamoja na Mawaziri,Manaibu Waziri ,Makatibu wakuu ,Manaibu katibu wakuu na viongozi wa serikali kutoka Mikoa minne,"amesema na kuongeza;

"Viongozi wa serikali kutoka Mikoa minne watashiriki,Mkoa wa Singida,Iringa, Morogoro na Manyara hivyo hata wananchi wa wadodoma wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono Rais wetu kwasababu sensa ni jambo letu wote,"amesema.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi,Ofisi ya Taifa ya Takwimu ,Daniel Masolwa amesema kutokana jukumu iliyopewa ofisi hiyo,itawajibika kwa ukaribu kuratibu masuala ya sensa kwa kuhusisha madodoso manne.

"Tumeandaa dodoso kuu,dodoso la nyumba,watu pamoja na anuani za makazi, tayari tumeshaandaa sensa ya majaribio ambayo inafanyika katika Mikoa 13,lengo la majaribio hayo ni kupima na kuhakiki vitendea kazi vyetu na ikiwa vitakuwa na changamoto yoyote virekebishwe,"amesema.
Share:

WATU 50 WANAODHANIWA KULA CHAKULA CHENYE SUMU SINGIDA WARUHUSIWA KURUDI NYUMBANI

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akimjulia hali jana Mwanahamisi Shabani ambaye ni mjamzito mmoja wa wananchi ambaye amelazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida akipatiwa matibabu akidhaniwa kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akimjulia hali na kuzungumza na Sheikh wa Kata ya Unyambwa, Ramadhani Yusuf  (kulia) ambaye amelazwa  katika Hospitali hiyo akipatiwa matibabu akidhaniwa kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu. Katikati ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akiwajulia hali  wahanga wa tukio hilo alipo watembelea jana kabla ya kuruhusiwa..
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge akiwajulia hali  wahanga wa tukio hilo alipo watembelea jana kabla ya kuruhusiwa..
Wahanga wa tukio hilo wakiwa hospitalini hapo kabla ya kuruhusiwa.
Wahanga wa tukio hilo wakiwa hospitalini hapo kabla ya kuruhusiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa, akizungumza na madaktari wa Hospitali wakati mkuu wa mkoa alipo watembelea wahanga wa tukio hilo. 


Na Dotto Mwaibale, Singida 


WATU 50 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Mkoa wa Singida wakipatiwa matibabu baada ya kunusurika kufa baada ya kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu wameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya afya zao kuhimarika.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge alipowatembelea wananchi hao jana Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Banuba Deogratius alisema juzi walipokea juzi jumla ya wagonjwa 50, Wanawake 34 na Wanaume 16 ambapo hali hadi jana hali zao zilikuwa zikiendelea vizuri na baadhi yao wameanza kuwaruhusu kurudi nyumbani kuendelea na majukumu yao ya ujenzi wa Taifa.

Banuba alisema wakazi hao wa Kata ya Unyambwa Kijiji cha Kisasida katika Manispaa ya Singida mkoani hapa walifikishwa hospitalini hapo  baada ya hali zao kuwa mbaya kutokana na kula chakula kilichoandaliwa katika shughuli za ufunguzi wa Madrasa moja Katika kijiji hicho.

Akipokea taarifa hiyo  Mkuu wa Mkoa Singida Dkt Bilinith Mahenge aliwapongeza madaktari wa Hospitali hiyo kwa jitihada walizozifanya za kuhakikisha wananusuru maisha ya wananchi hao ambapo kwa sasa hali zao zinaendelea vizuri na kuipongeza Serikali kwa kuweka miundombinu mizuri ya huduma katika sekta ya afya.

Alitoa wito kwa viongozi wa Serikali na Dini kuwajibika kikamilifu katika kutoa elimu ya namna ya kuandaa chakula pamoja na kusimamia inapotokea sherehe mbalimbali kwenye maeneo yao ili kuepuka madhara ya namna hiyo yasije kutokea tena.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ASP) Stella Mutabihirwa alisema wanawashikilia watu saba kuhusika na tukio hilo.

" Tuna walishiriki watu saba ambao waliandaa chakula hicho na  uchunguzi ukikamilika tutatoa taarifa kamili kwa sasa tayari tumechukua mabaki ya chakula hicho kwa ajili ya kuyachunguza," alisema Mutabihirwa.

Alisema katika tukio hilo  mtoto mmoja mwenye umri wa miaka (7) aliye mtaja kwa jina la Fahad Masoud alifariki dunia kabla ya kufikishwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Share:

Watumishi Wa TRA , Wadau Wa Kodi Waelimishwa Mabadiliko Ya Sheria Za Kodi

Na Mwandishi wetu, Simiyu
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaendelea kutoa elimu ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 kwa watumishi wa mamlaka hiyo, wadau na walipakodi katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Akizungumza na watumishi, wadau na walipakodi hao katika mikoa ya Simiyu na Mara, Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka TRA Makao Makuu Dar es Salaam Bw. Zakeo Kowero alisema kwamba, lengo la kutoa elimu hiyo ni kuwa na uelewa mmoja kwa watumishi wa TRA na kwa upande wa walipakodi na wadau ni kuwafahamisha mabadiliko yaliyotokea ili kuongeza uhiari wa ulipaji kodi.

“Tumeamua kuzunguka kutoa elimu hii ya mabadiliko ya sheria za kodi yaliyofanywa na Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22 ili kuhakikisha watumishi tunakuwa na lugha moja wakati tunapowahudumia wateja wetu na kwa upande wa wadau na walipakodi ni kuwafahamisha kuhusu mabadiliko yaliyotokea,” alisema Kowero.

Kati ya mabadiliko yaliyotokea ni pamoja na kuongeza idadi ya waajiriwa kwenye Kodi ya Kuendeleza Mafunzo ya Ufundi Stadi (SDL) kutoka wafanyakazi wanne hadi kumi lakini uwasilishaji wa ritani utaendelea kama kawaida bila kujali idadi ya watumishi.

Eneo lingine lililofanyiwa mabadiliko katika kodi hii ya uendelezaji mafunzo ya ufundi stadi ni la taasisi za kidini ambapo zimesamehewa kulipa kodi kwenye huduma za afya ya umma.      

“Lengo la kuongeza idadi ya waajiriwa ni kuwapunguzia mzigo waajiri wadogo ili kukuza mitaji yao na dhumuni la kutoa msamaha kwenye taasisi za dini ni kuzipa unafuu katika kutoa huduma kwa jamii,” alibainisha Kowero.

Akizungumzia mabadiliko yaliyofanyika katika Kodi ya Majengo alisema kwamba, viwango vimeongezeka kwenye nyumba za kawaida katika Majiji, Manispaa na Halmashauri za Miji kutoka shilingi 10,000 hadi shilingi 12,000 kwa mwaka.

Kwa upande wa kila sakafu ya nyumba za ghorofa katika majiji, manispaa, halmashauri za miji, kodi imeongezeka kutoka shilingi 50,000 hadi shilingi 60,000 kwa mwaka na kwa nyumba za ghorofa zilizoko katika halmashauri za wilaya, kodi imeongezeka kutoka shilingi 20,000 hadi shilingi 60,000 kwa jengo zima kwa mwaka.

“Hata hivyo, Serikali imebadilisha njia ya utozaji kodi hii ambapo kwa sasa kodi ya majengo inalipwa kupitia njia ya ununuzi wa umeme wa LUKU kwa kukata shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba za kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa nyumba za ghorofa,” alieleza Kowero.

Kwenye Sheria ya Usajili wa Vyombo vya Moto, Serikali imepunguza kodi ya usajili wa namba binafsi kutoka shilingi 10,000,000 hadi shilingi 5,000,000 na usajili huo utadumu kwa miaka mitatu. Lengo la mabadiliko hayo ni kuwavutia watu kusajili vyombo vyao vya moto na hivyo kuongeza mapato ya serikali.

Mabadiliko mengine yamefanyika kwenye sheria ya Ushuru wa Stempu kwa mfano, ushuru wa stempu katika nyaraka mbalimbali umeongezeka kutoka shilingi 500 hadi shilingi 2000.

Naye, Danieli Singiri mmoja wa viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wa mkoani Simiyu waliohuduria semina ya mabadiliko ya sheria mkoani humo, alisema amefurahishwa na elimu hiyo na ameiomba serikali kuangalia kifungu kipya cha kodi ya zuio ya asilimia mbili iliyowekwa kwenye mazao ya kilimo kwani kitawaumiza wakulima.

“Tumefurahi kwa kutupatia elimu hii muhimu lakini tunaiomba serikali iangalie kodi ya zuio ya asilimia mbili kwenye mazao ya kilimo kwani itawadidimiza wakulima kwasababu watapokea fedha pungufu japokuwa lengo la kodi hii ni zuri na imelenga kuongeza mapato ya serikali hata hivyo nashauri itafutwe njia nyingine tofauti na hii,” alisema Singiri.   

Elimu ya mabadiliko ya sheria za kodi imekwishatolewa katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga. Kwa sasa elimu hiyo inaendelea kutolewa katika mikoa ya Simiyu, Mara, Mwanza, Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi.
Mwisho.



Share:

MGEJA AWAPONGEZA MACHIFU KUMSIMIKA RAIS SAMIA 'KUWA CHIFU MKUU WA MACHIFU TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Mkuki na Ngao kutoka kwa Chifu Fundi Kira Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania mara baada ya kusimikwa kuwa Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika Septemba ,08,2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza
Khamis Mgeja

Na Baltazar Mashaka - Kahama
MWENYEKITI wa Tanzania Mzalendo Foundation, Khamis Mgeja ameupongeza Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) kwa kumpa heshima iliyotukuka Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kumsimika kuwa Chifu Mkuu wa Machifu nchini Tanzania.

Alitoa pongezi mjini Kahama, jana alipoombwa na waandishi wa habari kutoa maoni yake kuhusu Rais Samia kusimikwa kuwa Chifu Mkuu wa Watemi nchini na kupewa jina la Hangaya lenye maana ya Nyota Njema.

Mgeja alisema, Machifu kumpa Rais Samia heshima hiyo adhimu iliyotukuka kwenye mila,desturi na utamaduni wa Kiafrika,wanastahili pongezi.

“Nitumie fursa hii pia kumpongeza Rais Samia au Chifu Hangaya kuwa Chifu Mkuu wa Watemi na nina imani atatuongoza vizuri Watanzania ili tuendelee kudumisha na kuenzi utamaduni wetu,mila na desturi,”alisema.

Mgeja ambaye ni mmoja wa wanafamilia ya wanangwa (wasaidizi) wa Chifu Kapela wa eneo la Kijiji cha Nhumbili, Tinde, Wilaya ya Shinyanga , alisema jina alilopewa la Hangaya (Nyota njema/Nyota inayong'aa) ni la heri kubwa kwa Watanzania likiwa na falsafa pana ya heri na mafanikio.

“Majina yote mawili yana heri kubwa ya uongozi katika nchi yetu,ukiunganisha jina la Hangaya na Suluhu, moja linabeba heshima na mafanikio kama nchi na Watanzania wote, la pili la Suluhu linabeba suluhisho la changamoto zinazoikabili nchi na zinazogusa maisha ya Watanzania,”alifafanua zaidi.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini na Mwenyekiti wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, pia aliyewahi kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), alisema majina mazuri ya viongozi yana manufaa na heri nyingi, hata viongozi wa dini wamekuwa wakisistiza jamii kuwapa watoto majina mazuri.

Alisema duniani kote nchi zinazoheshimu,kudumisha kuenzi,kurithisisha utamaduni,mila na desturi zao zimepiga hatua kubwa kimaendeleo,kiutamaduni na kimaadili,akatolea mfano China,Japan,Korea,India,Ujerumani na nyingine.

Mwenyekiti huyo wa Mzalendo Tanzania Foundation aliwaomba Watanzania kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Sita kwa pamoja kuendeleza na kudumisha utamaduni wetu, ni muhimu sana na lazima lipewe kipaumbele kwa kiwango cha juu na jamii.

Mgeja akimnukuu Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alisema 'Taifa lolote lisilokuwa na utamaduni wake limekufa.

“Hivi sasa Tanzania tulikuwa tukielekea huko na bahati nzuri tumempata Rais msikivu na naamini hatutafika huko na hatutakuwa taifa mfu chini ya Chifu Hangaya,” alisema Mgeja na kuongeza;

“Kama nchi tukitaka kuwa na viongozi wazalendo na waadilifu ni muhimu wakatokana na malezi yanayozingatia mila,desturi na maadili yakiwemo ya dini na wala tusidanganyane, hatuwezi kupata viongozi waadilifu, wazalendo wasipoandaliwa kwenye misingi ya malezi na makuzi yao.”

Aidha kuhusu maombi yaliyotolewa na machifu kwenye hafla ya kumsimika Rais Samia iliyofanyika kwenye Uwanja wa Red Cross Kisesa na kupewa jina la Chifu Hangaya, Mgeja alieleza kuwa, ana imani serikali ya awamu ya sita itafanyia kazi.

Pia alisistiza serikali iendelee kushirikiana kwa karibu na machifu kwani ni watu muhimu na waoaheshimika sana kwenye jamii, wana sauti na ushawishi mkubwa.

Aliongeza kuwa serikali kuwa karibu na machifu ni mwanzo mzuri,hatua hiyo inastahili pongezi na mengine yatafuata ya kudusmisha ushirikiano kwani Tanzania kudumisha ushirikiano na machifu kuwa na utamaduni imara inawezekana,hivyo twende pamoja kulijenga taifa letu.ssss
Share:

BETWAY YAZINDUA KITUO CHA KUSHUHUDIA MICHEZO TANZANIA

 

Kampuni ya kimataifa ya michezo ya kubashiri, Betway imechukua hatua kubwa katika kuongeza thamani kwenye sekta ya michezo nchini Tanzania.  Betway imezindua kituo cha kisasa cha kushuhudia michezo na kubashiri kistaarabu ‘Betway Sports Experience Center.’

Kituo hicho cha kipekee na cha aina yake ni sehemu itakayowakutanisha wapenzi wa michezo kushuhudia michezo mbalimbali na kufanya ubashiri katika mazingira ya kuvutia.

Kituo hiki ambacho kimepewa jina la Dimba la Betway kitakuwa pia ni kituo cha elimu kuhusu michezo na namna ya kubashiri kistaarabu. Kituo hicho kipo ndani ya ofisi za Betway zilizopo Mbezi Beach, Dar es salaam.

Eneo hili la Betway limewekewa vifaa vya kisasa ikiwemo simu janja na kompyuta maalumu kwa ajili ya wateja kujisajili na kufanya ubashiri wa michezo inayoendelea mubashara. 

Kituo hicho kimefungwa skrini maalumu za runinga zinazoonesha michezo mubashara inayochezwa kwa wakati huo na kutoa nafasi kwa wateja kufuatilia matokeo ya mechi hizo. Pia, kituo hicho kinatoa nafasi kwa wateja kucheza michezo ya kasino na michezo mingine ya ubashiri.

Ndani ya dimba la Betway mashabiki wa michezo watapata nafasi ya kukutana na kuwasiliana moja kwa moja na timu ya Betway kwa uhuru na katika mazingira mazuri zaidi.

 Pia, kituo hiki kinatoa nafasi ya wateja kuuliza maswali, kusajili akaunti mpya, na kufanya ubashiri kwa kutumia simu na kompyuta zilizopo ndani ya kituo.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi, Meneja Uendeshaji wa Betway Tanzania, Jimmy Masaoe alisema kuwa uzinduzi wa kituo hicho cha ni sehemu ya juhudi za kampuni hiyo kuongeza thamani katika sekta ya michezo nchini.

"Sisi (Betway) tuna furaha kubwa kuzindua kituo hiki cha kipekee na muhimu kwa mashabiki wa michezo nchini Tanzania kuweza kukutana na kufurahia kwa pamoja na kwenye mazingira ya kuvutia.

 Hii ni sehemu ya ahadi yetu - kuongeza thamani katika michezo ya kubashiri na sekta ya michezo kwa ujumla kwa sababu kituo hiki kitakuwa kama kitovu cha michezo ambapo mashabiki wataweza kukutana, kutazama michezo, na kufanya ubashiri wao kwa njia bora ambayo haijawahi kutokea hapo awali," alisema.

Akizungumza na wadau wa michezo pamoja na wanahabari waliohudhuria tukio la uzinduzi, Jimmy alisema kuwa Betway inafanya kazi kutimiza ahadi zake za kukuza maendeleo ya michezo nchini Tanzania kama ilivyoahidi wakati ikiingia nchini na kuwahakikishia wote kuwa Kampuni hiyo itaweza kuwaongoza wateja wake katika kuiishi na kuitimiza kauli mbiu ya "Bashiri Kistaarabu" kwa kuwaonyesha wateja wake kwa vitendo.

"Sisi Betway tunajivunia kuhamasisha wateja wetu wote kubashiri kistaarabu. Tutatumia kituo hiki kama kituo cha kuelimisha mashabiki wa michezo nchini Tanzania kuhakikisha wanaielewa na kuikubali dhana ya kubashiri kistaarabu. Tunawakaribisha mashabiki wa michezo kufika katika kituo hiki kujionea na kufurahia maana halisi ya michezo,'' aliongeza.

Kama sehemu ya hafla ya uzinduzi, wahudhuriaji walifurahia uchambuzi wa moja kwa moja wa michezo ya Ligi Kuu ya Uingereza iliyochezwa siku ya Jumamosi. 

Uchambuzi kutoka kwa wachambuzi maarufu wa michezo nchini Tanzania, Maulid Kitenge, na Edo Kumwembe uliwavutia mashabiki wadau waliohudhuria hafla hiyo. 

Wahudhuriaji pia walishiriki katika mashindano ya michezo kama vile utabiri wa matokeo na wafungaji wa mabao, na kuweza kujipatia zawadi mbalimbali kutoka Betway.

Michael Valentine, aliyejitambulisha kuwa ni shabiki wa timu ya Manchester United alikuwa ni moja ya waliohudhuria katika hafla hii na kueleza kuwa alijionea utofauti mkubwa katika kituo hicho cha Betway. Michael pia ameunga mkono hatua ya kampuni ya Betway kuwekeza nchini Tanzania na kuitaka iendelee kutoa huduma za kipekee. 

“Mimi ni shabiki mkubwa wa michezo, kwa muda mwingi nimekuwa nikiwaona Betway kwenye vyombo vya habari kupitia timu za ligi kuu ya Uingereza zinazofadhiliwa na Betway, na furaha kuona wamekuja nyumbani Tanzania,” alisema.

Pia, aliongeza kwa kusema “sijawahi kuona kituo kama hiki nchini, kituo hiki ni cha kwanza hapa Tanzania na natumaini kitachochea uwekezaji mkubwa zaidi kwenye sekta ya michezo, na mashabiki watafurahia sana Betway kuanzisha shughuli zake nchini”.

Kituo hiki cha Betway kitakuwa kikifunguliwa katika siku zote 7 za wiki kuanzia asubuhi saa 3:00 hadi 5:00 usiku.


Share:

JAMAA ADAIWA KUWAUA WATOTO WAKE BAADA YA KUGOMBANA NA MKEWE


Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 44 kutoka kijiji cha Bochura kaunti ya Kisii amedaiwa kuwauwa watoto wake wawili na kisha kujitoa uhai.

Kisa hicho kilithibitishwa na chifu wa kijiji hicho Lawrence Omar ambaye alisema Daniel Mosota aliwaua watoto wake wa miaka 5 na mwingine wa miaka saba kwa kuwakata kwa panga. 

Omar alisema  Mosota anadaiwa alikuwa amegombana na mkewe Naomi Nyaboke kabla ya kutekeleza kitendo hicho.

 Chifu huyo aliongezea kwamba Nyaboke alifanikiwa kukimbilia usalama wake Mosoto alipoanza kuwavamia ndani ya nyumba yao. 

Maafisa wa polisi walifika eneo la tukio na kuchukua miili ya watatu hayo, imehifadhiwa katika mochwari ya hospitali ya rufaa ya Kisii ikisubiri kufanyiwa uchunguzi wa maiti.

Aidha, chifu huyo aliwarai wanandoa ambao wana mazoea ya kuzozana kila mara watafute ushauri kutoka kwa wataalam au viongozi wa kanisa badala ya kuuana kiholela.

CHANZO-  TUKO NEWS
Share:

TAMBUA DALILI ZA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME NA TIBA YAKE


Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;


1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama


Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO


Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

WATUMISHI WA TRA, WADAU WA KODI WAELIMISHWA MABADILIKO YA SHERIA ZA KODI


Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu Dar es Salaam Bw. Zakeo Kowero akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 kwa viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika pamoja na wanunuzi wa zao la pamba wa mkoani Simiyu wakati wa semina iliyoandaliwa na TRA mjini Bariadi mkoani humo.

Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Simiyu Bw. Michael Nsobi akifafanua jambo wakati wa semina ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 iliyofanyika mjini Bariadi mkoani humo.

Afisa Msimamizi Mwandamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara Bw. Zake Wilbard akifafanua jambo wakati wa semina ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 iliyofanyika mjini Bariadi mkoani Simiyu.

Mmoja wa viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wa mkoani Simiyu akichangia hoja wakati wa semina ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mjini Bariadi mkoani humo.
Baadhi ya viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika pamoja na wanunuzi wa zao la pamba wa mkoani Simiyu wakiwa katika semina ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mjini Bariadi mkoani Simiyu.
(PICHA ZOTE NA TRA).

***************************

Na Mwandishi wetu

Simiyu

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inaendelea kutoa elimu ya mabadiliko ya sheria za kodi ya mwaka 2021 kwa watumishi wa mamlaka hiyo, wadau na walipakodi katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Akizungumza na watumishi, wadau na walipakodi hao katika mikoa ya Simiyu na Mara, Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka TRA Makao Makuu Dar es Salaam Bw. Zakeo Kowero alisema kwamba, lengo la kutoa elimu hiyo ni kuwa na uelewa mmoja kwa watumishi wa TRA na kwa upande wa walipakodi na wadau ni kuwafahamisha mabadiliko yaliyotokea ili kuongeza uhiari wa ulipaji kodi.

“Tumeamua kuzunguka kutoa elimu hii ya mabadiliko ya sheria za kodi yaliyofanywa na Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22 ili kuhakikisha watumishi tunakuwa na lugha moja wakati tunapowahudumia wateja wetu na kwa upande wa wadau na walipakodi ni kuwafahamisha kuhusu mabadiliko yaliyotokea,” alisema Kowero.

Kati ya mabadiliko yaliyotokea ni pamoja na kuongeza idadi ya waajiriwa kwenye Kodi ya Kuendeleza Mafunzo ya Ufundi Stadi (SDL) kutoka wafanyakazi wanne hadi kumi lakini uwasilishaji wa ritani utaendelea kama kawaida bila kujali idadi ya watumishi.

Eneo lingine lililofanyiwa mabadiliko katika kodi hii ya uendelezaji mafunzo ya ufundi stadi ni la taasisi za kidini ambapo zimesamehewa kulipa kodi kwenye huduma za afya ya umma.

“Lengo la kuongeza idadi ya waajiriwa ni kuwapunguzia mzigo waajiri wadogo ili kukuza mitaji yao na dhumuni la kutoa msamaha kwenye taasisi za dini ni kuzipa unafuu katika kutoa huduma kwa jamii,” alibainisha Kowero.

Akizungumzia mabadiliko yaliyofanyika katika Kodi ya Majengo alisema kwamba, viwango vimeongezeka kwenye nyumba za kawaida katika Majiji, Manispaa na Halmashauri za Miji kutoka shilingi 10,000 hadi shilingi 12,000 kwa mwaka.

Kwa upande wa kila sakafu ya nyumba za ghorofa katika majiji, manispaa, halmashauri za miji, kodi imeongezeka kutoka shilingi 50,000 hadi shilingi 60,000 kwa mwaka na kwa nyumba za ghorofa zilizoko katika halmashauri za wilaya, kodi imeongezeka kutoka shilingi 20,000 hadi shilingi 60,000 kwa jengo zima kwa mwaka.

“Hata hivyo, Serikali imebadilisha njia ya utozaji kodi hii ambapo kwa sasa kodi ya majengo inalipwa kupitia njia ya ununuzi wa umeme wa LUKU kwa kukata shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba za kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa nyumba za ghorofa,” alieleza Kowero.

Kwenye Sheria ya Usajili wa Vyombo vya Moto, Serikali imepunguza kodi ya usajili wa namba binafsi kutoka shilingi 10,000,000 hadi shilingi 5,000,000 na usajili huo utadumu kwa miaka mitatu. Lengo la mabadiliko hayo ni kuwavutia watu kusajili vyombo vyao vya moto na hivyo kuongeza mapato ya serikali.

Mabadiliko mengine yamefanyika kwenye sheria ya Ushuru wa Stempu kwa mfano, ushuru wa stempu katika nyaraka mbalimbali umeongezeka kutoka shilingi 500 hadi shilingi 2000.

Naye, Danieli Singiri mmoja wa viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wa mkoani Simiyu waliohuduria semina ya mabadiliko ya sheria mkoani humo, alisema amefurahishwa na elimu hiyo na ameiomba serikali kuangalia kifungu kipya cha kodi ya zuio ya asilimia mbili iliyowekwa kwenye mazao ya kilimo kwani kitawaumiza wakulima.

“Tumefurahi kwa kutupatia elimu hii muhimu lakini tunaiomba serikali iangalie kodi ya zuio ya asilimia mbili kwenye mazao ya kilimo kwani itawadidimiza wakulima kwasababu watapokea fedha pungufu japokuwa lengo la kodi hii ni zuri na imelenga kuongeza mapato ya serikali hata hivyo nashauri itafutwe njia nyingine tofauti na hii,” alisema Singiri.

Elimu ya mabadiliko ya sheria za kodi imekwishatolewa katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga. Kwa sasa elimu hiyo inaendelea kutolewa katika mikoa ya Simiyu, Mara, Mwanza, Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi.
Share:

WAZIRI BITEKO: MICHEZO NI AFYA TUSHIRIKIANE KWA PAMOJA

 

Mshindi wa kwanza timu ya wanaume kukimbia mita 100 kutoka Wizara ya Madini David Ibrahim akipewa medali ya dhahabu na Waziri wa Madini, Doto Biteko katika Bonanza yaliyofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Doto Biteko (kushoto), Mwenyekiti wa Tume ya  Madini Prof. Idris Kikula (kulia) wakiwa kwenye mazoezi ya kuzunguka uwanja katika Bonanza la Wizara na Tume ya Madini lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani, jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Doto Biteko akitoa medali ya dhahabu kwa Mshindi wa kwanza timu ya wanawake kukimbia mita 100 kutoka Wizara ya Madini Bi. Hilda Masanche katika Bonanza la Wizara na Tume ya Madini lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani, jijini Dodoma.
Katibu Mtendaji Tume ya Madini Mhandisi Yahya Samamba akipewa medali ya fedha ya kuwa mshindi wa pili wa kukimbia na yai katika Bonanza la Wizara na Tume ya Madini lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani jijini Dodoma.
Waziri wa Madini Doto Biteko akitoa kikombe kwa mchezaji bora wa mpira wa miguu kutoka timu ya Wizara ya Madini Bw. Casmiri Daudi katika Bonanza la Wizara na Tume ya Madini lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani jijini Dodoma.
Washindi wa kuvuta kamba timu ya wanawake kutoka Tume ya Madini wakishangilia baada ya kupewa kikombe cha ushindi na Waziri wa Madini, Doto Biteko katika Bonanza la Wizara na Tume ya Madini lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani jijini Dodoma.

 Waziri Biteko akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Bonanza kutoka Wizara na Tume ya Madini katika Bonanza hilo  lililofanyika Septemba 11, 2021 katika viwanja vya Kilimani jijini Dodoma.



IMEELEZWA  kuwa, michezo inaleta afya, akili , urafiki na kuwaweka pamoja Wafanyakazi wa Wizara pamoja  na Taasisi zake.

Hayo yamebainisha leo Septemba 11, 2021 na Waziri wa Madini, Doto Biteko wakati wa ufunguzi wa Bonanza ya Wizara ya Madini na Tume ya Madini lililofanyika katika Viwanja vya Kilimani, Jijini Dodoma.

“Nawapongeza Wafanyakazi wote kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika michezo mbalimbali , tuendelee kufanya mazoezi ili tuweze kupata nguvu ya kuendelea kufanya kazi ya kulinda rasilimali zetu na kukuza Uchumi wa Nchi,” amesema Waziri Biteko.

“Nimechezesha vizuri mechi ya mpira wa miguu kama refa bila upendeleo wowote , niendele kuwapongeza wachezaji kwa kuwa mahiri na kucheza vizuri,” ameongeza Waziri Biteko.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula amewapongeza washiriki wa Bonanza na kuwataka waendelee kufanya mazoezi mara kwa mara maana michezo ni furaha.

Naye, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amesema Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan, anawasisitiza watu wafanyemazoezi  kwa kuwa ni moja kati ya kinga ya kuufanya mwili kuwa imara ili kukabiliana na magonjwa mbalimbali.

“Msisitizo kutoka kwa Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ni kwamba Wizara na Taasisi  zote za Serikali zifanye mazoezi kwa pamoja, na mazoezi hayo ni maandalizi ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) ambayo yamerudishwa na Serikali,”amesema Mhandisi Samamba ”.

Kwa upande wake, Kamishna wa Tume ya Madini, Janet Ruben amesema kuwa watu wapo ofisini lakin ukija kwenye mazoezi wapo, rai yangu tusiache mazoezi tushirikiane na kuwa pamoja Wizara na Tume ya Madini.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 12,2021

Magazetini leo Jumapili September 12 2021














Share:

RAIS MWINYI ATUMA SALAMU ZA POLE KUFUATIA KIFO CHA JAJI WA MAHAKAMA KUU ZANZIBARI HAJI OMARI HAJI


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi
**
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Jaji Haji Omar Haji, Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Kifo cha Jaji Haji Omar Haji kimetokea leo katika Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mnazi Mmoja Jijini Zanzibar na anatarajiwa kuzikwa kesho Shakani, Wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja mnamo saa saba za mchana.

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa amepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa ya kifo cha Jaji Haji Omar Haji.

Aidha, kupitia salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi alimuomba Mwenyezi Mungu kuwapa moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hichi kigumu cha msiba, familia, marafiki, ndugu pamoja na wafanyakazi na viongozi wote wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.

Salamu hizo ziliendelea kumuomba Mwenyezi Mungu kumpa rehma na kumjaalia makaazi mema peponi. Amin.


Marehemu Jaji Haji Omar Haji aliteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar mnamo Februari 01, 2021 na kuapishwa mnamo Februari 08, 2021.


Sambamba na hayo, mnamo Agosti 16, 2021 marehemu Jaji Haji Omar Haji aliteuliwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar Jaji Omar Othman Makungu kuwa Jaji Mkaazi Pemba.
Share:

Saturday, 11 September 2021

WAPENZI WAKUTWA WAMEFARIKI WAKIDAIWA KUNYWA JUISI YA SUMU




Watu wawili wanaodhaniwa kuwa ni wapenzi wamekutwa wamefariki huku chanzo kikidaiwa kuwa walikunywa sumu katika Kitongoji cha Mlandizi kata ya Mlandizi Tarafa ya Mlandizi Wilaya ya Kipolisi Mlandizi, mkoani Pwani.

Akizungumzia tukio hilo la kustaajabisha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amesema; “Mnamo Tarehe 5 Septemba, 2021 asubuhi huko Mlandizi, watu wawili wanaodaiwa kuwa ni wapenzi walikutwa wamefariki katika makazi yao baada ya kunywa kitu kinachodhaniwa ni sumu.

“Watu hao ni Godfrey Pius Mandai (48) ambaye alikuwa ni Dereva wa Kampuni na Veronica Gerald (42), mfanyabiashara na mkazi wa Mtwara ambaye alisafiri kutoka Mtwara na kumfuata mpenzi wake huyo Mlandizi.

“Imedaiwa kuwa mwanaume yule alitengengeza juisi ambayo ndani yake ilikuwa na sumu akampa Veronica akanywa na kufariki dunia, mwanaume hutyo alipoona mpenzi wake amefariki na yeye akanywa ile juisi yenye sumu na akafariki dunia.

“Inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa mapenzi ambapo mwanaume alikuwa akimtuhumu Veronica kuwa anafanya usaliti.

“Kwenye eneo la tukio tumekuta chupa yenye masalia ya sumu na tumekuta pia karatasi ambayo inadhaniwa imeandikwa na mmoja wao ikiwa na maneno yanayosomeka ‘HUU NI USALITI TU.’

 Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi kutokana na tukio hilo,” amesema Kamanda Nyigesa.
Share:

MO DEWJI: HANS POPE ALIKUWA NA WEMA WA KIPEKEE



Na Emmanuel Mbatilo - Dar es salaam
Wanamichezo nchini wamepokea kwa masikitiko kwa kifo cha Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Zacharia HansPope ambaye amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Aghakhan Jijini Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu.

Viongozi mbalimbali wa michezo wameshindwa kujizuia na kutamka ya moyoni kuhusu umuhimu wa kiongozi huyo katika tasnia ya michezo hapa nchini.

Licha ya kuwa kiongozi wa klabu ya Simba alikuwa mtu wa hamasa katika kuitangaza tasnia ya michezo kwa taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mohammed Dewji amesema Hans Pope alikuwa ni mtu wa kipekee alihakikisha klabu ya Simba kusonga mbele na alijali maslahi ya klabu.

“Nimefanya kazi na wewe kwa miaka mingi, na kila siku uliweka maslahi ya Simba mbele. Kaka yangu ulikua na wema wa kipekee, na ulikua wa kwanza na ulinyooka linapokuja suala la kuilinda Simba, hukuwa na maslahi binafsi. Ulikua rafiki wa marafiki wa Simba, na ulikua tofauti na wasioitakia mema Simba.” Amesema Mo Dewji

Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu amesema Hans Pope alikuwa anapenda umoja na mshikamano kwa wanasimba wote kwani alikuwa anapenda mafanikio kwa ujumla ndani ya klabu.

“Ninamfahamu kwa miaka mingi akiwa ni Mwana Simba mahiri , mwenye msimamo na ukweli. Ni mtu aliependa umoja na kupata mafanikio kwa jumla. Siku zote alikubali kutumikia klabu kwa moyo wake wote , bila kujali muda wake, mali au hasara”. Amesema Mangungu
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger