Friday, 3 September 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 3,2021




Share:

Thursday, 2 September 2021

WAZIRI CHAMURIHO AFUNGUA MAADHIMISHO YA 18 YA SIKU YA WAHANDISI NCHINI DODOMA


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho,akizungumza wakati akifungua maadhimisho ya 18 ya siku ya wahandisi nchini yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Malongo, akisisitiza jambo kwa wahandisi (hawap pichani), wakati wa maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi, yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Prof. Ninatubu Lema, akizungumza na wahandisi (hawapo pichani), katika maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi, yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Msajili wa Bodi ya Wahandisi Patric Barozi,akizungumza katika maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi, yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka ,akizungumza katika maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi, yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Sehemu ya wahandisi wakifatilia hotuba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho,(hayupo pichani) wakati akifungua maadhimisho ya 18 ya siku ya wahandisi nchini yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Wahandisi 632 wakila kiapo cha utii katika maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi,yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akimkabidhi leseni ya uhandisi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Eng. Robert Gabriel, mara baada ya kula kiapo cha utii katika maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi, yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuriho, akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Usajili ya Wahandisi (ERB) mara baada ya kufungua maadhimisho ya 18 ya Siku ya Wahandisi,yaliyofanyika leo September 2,2021 jijini Dodoma.

........................................................................................

Na.Alex Sonna,Dodoma

WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi,Mhandisi Dk.Leonard Chamuriho amewataka wahandisi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuweza kukamilisha miradi yote nchini kwa muda uliopangwa.

Hayo ameyasema leo September 2,2021 jijini Dodoma wakati akifungua maadhimisho ya 18 ya siku ya wahandisi nchini ambapo jumla ya Wahandisi 3500 wamehudhiria huku Wahandisi 630 wakila kiapo.

Dkt.Chimuriho amesema katika mwaka huu wa fedha serikali imetenga kiasi cha Sh. Trilioni 13.3 kwa ajili ya kukamilisha miradi mikubwa mbalimbali ya Ujenzi inayoendelea na ambayo haijaanza hapa nchini.

''Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Samia Suluhu Hassan ameelekeza fedha zitengwa ili kuwezesha miradi mikubwa yote iliyoanza kutekelezwa kukamilika na ambayo ilikuwa haijanza ikamilike''amesema Dkt.Chimuriho

Hata hivyo amesema kuwa kipengele chenye takwa la kisheria la kuwajengea uwezo wahandisi wazawa hususani vijana kiwekwe katika mikataba yote ya ujenzi itakayoingiwa na Serikali kuanzia sasa.

"Ujuzi wakiupata utabaki nchini na utawawezesha wahandisi wetu kuwa na uwezo wa kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo hapa nchini, hivyo nawaagiza mhakikishe zabuni zote mpya mtakazo ingia na kuzitoa kwa wakandarasi kigezo cha Kujenga uwezo kiwe cha kisheria''ameongeza

Katika utekelezaji wa miradi kwa 'Force Account' ambao umekuwa ukisababisha wakandarasi binafsi kukosa kazi, amesema kuwa serikali imeiona na tayari imeanza kulifanyia kazi changamoto hiyo kama alivyoelekeza na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kuanzia mradi wa Ujenzi wa mji wa serikali utajengwa kwa ubia na sekta binafsi.

Kwa upande wake Msajili wa Bodi ya Wahandisi Patric Barozi, amesema kuwa mpaka sasa bodi hiyo imesajili jumla ya Wahandisi 31,729 wanawake wakiwa ni 544 sawa na asilimia 32, na kuendeleza Wahandisi 9,441 kati yao wanawake 756, kupitia mpango wao wa kuendeleza wahandisi nchini ambao wamesajiliwa kwenye bodi hiyo kwa mwaka 2020.

Awali Mwenyekiti wa Bodi ya wahandisi, Prof. Ninatubu Lema, aliwataka Wahandisi kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia na kujiandaa kukabiliana nayo katika utendaji kazi zao.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka ameeleza kuwa bado kuna shida katika utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofanywa na wakandarasi wazawa akiwataka wakandarasi wazawa wanaoshinda zabuni kujenga uaminifu ili waweze kuaminika zaidi na kupewa kazi.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Malongo, ameitaka ERB kufanya tathimini ya maazimio yaliyofikiwa mwaka jana kuona kama yametekelezwa na hivyo kujipima katika yale matarajio yaliyofikiwa.

''Umuhimu wa kufuatilia wahandisi wahitimu wanaofanya vizuri katika masomo yao ili kuona kama wanafanya vizuri katika utendaji wa kazi zao kama ambavyo maadili ya taaluma yao yanavyowataka''amesema Mhandisi Malongo
Share:

NHIF YAKUTANISHA WADAU KUFANYA TATHIMINI YA MIAKA 20



Mwenyekiti wa bodi wa NHIF Juma Muhimba akizungumza kuhusiana na na ushauri wa bodi unavyofanya kuweza kufanya vizuri katika utendaji ili kutoa huduma bora kwa wanachama, jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa umoja wa watoa huduma za afya Binafsi (AFTA) Dkt. Egina Makwabe akizungumza kuhusiana na mchango wao katika mfuko wa NHIF

Katibu Tawala wa mkoa wa Dar es Salaam Hassan Rwaga akizungumza katika mkutano wa wadau wa watoa huduma za afya na NHIF kwa ajili ya kufanya tathimini ya miaka 20 uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bernad Konga akizungumza kuhusiana na mfuko huo tangu ulipoanzishwa na hatimaye kufika miaka 20 katika mkutano wa wadau wa Afya na NHIF uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Picha mbalimbali za washiriki wa mkutano kati NHIF na wadau wa watoa huduma za afya

*************************

*Katibu tawala Mkoa Dar es Salaam aipongeza NHIF kwa kuimarisha huduma



SERIKALI ya Mkoa wa Dar es Salaam imesema kuwa itaendelea kutoa ushuirikiano kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) katika kuimarisha mfuko huo uendelee kufanya vizuri kwa kuongeza idadi wanachama la kufikia asilimia 50 ya dhamira Rais Samia Hassan Suluhu.

Hayo ameyasema Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Hassan Rwagwa wakati akifungua mkutano wa Watoa Huduma za afya na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)uliofanyika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutathimini mfuko huo kwa mafanikio miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mfuko na kuangalia masuala mengine ya kufanya kufanya vizuri zaidi.

Rugwa amesema kuwa licha ya kufanya vizuri kwa mfuko watoa huduma wa afya wa serikali wanatakiwa kuwa tofauti katika utoaji wa huduma ili kufanya wananchi kuwa na imani na huduma za afya na kuachana mambo yasiyo mpendeza mteja.

''Miaka 20 ya NHIF kielelezo kuwa mmepita kwenye changamoto ambazo mliweza kuhmili na kusimamia mfuko katika kuweza kuwahudumia watanzania ambapo sasa bado mnaendelea katika maboresho mbalimbali ya kuujenga mfuko''amesema Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Sslaam Rugwa.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)Bernad Konga amesema kuwa lengo la mkutanoni kuwashukuru Watoa Huduma za matibau kwa wanachama wa Mfuko huu kwa mchango mkubwa kwa taasisi hii kwa miaka hii 20 ya uhai wake.

''Hatuwezi kuhesabu mafanikio ya Mfuko huu bila kuhusisha kundi hili muhimu kwa Mfuko maana sisi ni kiungo tu kati ya Wanachama na Watoa huduma hawa na kuadhimisha miaka 20 ya NHIF kwa pamoja na Watoa Huduma za Afya kwa kuangalia kwa pamoja tulipotoka, tulipo na tunapoelekea huku tukiimarisha mahusiano baina yetu na kujenga dhana ya uwazi katika utendaji kazi wetu sisi kama Mfuko na Watoa Huduma'' amesema Konga.

Amesema mwendelezo wa kushirikisha kundi hili mara kwa mara umesaidia katika kuharakisha mafanikio ya kihuduma kwa wanachama na Mfuko umekuwa ukikitania na Watoa Huduma mara kwa mara kwa umoja wao, kupitia umoja wao na hata kimikoa kupitia ofisi zetu mikoani na kuendelea kupeana mrejesho ya yaliyofanyika katika kipindi chote hiki na kujadili kwa pamoja mambo mbalimbali yanayotuhusu katika kuhudumia wanachama wa Mfuko.

Amesema tumekuwa na mikutano ya mara kwa mara na hata mawasilsiano ya maandishi hasa panapotokea maboresho, changamoto na miongozo mbalimbali. Mathalani tunapofanya maboresho ya kitita cha mafao, huwa unawashirikisha Watoa huduma kama wadau muhimu katika hili.

Lengo kubwa la kuwashirikisha wadau wetu ni kuhakikisha wote kwa pamoja tunatembea tukizungumza lugha moja kwa nia ya kuwahudumia vizuri wanachama ambao wamechangia kabla ya kuugua.

Aidha amesema NHIF umewezesha vituo mbalimbali kuimarisha huduma za matibabu na miundombinu kupitia mikopo nafuu inayotulewa na NHIF. Vituo kama MNH, MOI, KCMS, BMH na vingine ni wanufaika.

Malipo kwa Watoa huduma kwa sasa yanalipwa ndani ya muda mfupi zaidi wa kati ya siku 30 hadi 45 ikilinganishwa na awali ambapo ilikuwa ni siku 60 na wakati mwingine kuzidi na kufikia 100. Aidha malipo hayo yamewezesha vituo kuwa na mapato ya uhakika ambayo yanawezesha vituo kuimarisha huduma.

Amesema NHIF imeboresha kitita cha mafao kwa wanachama wetu ambapo kwa sasa wanapata huduma nyingi zaidi zikiwemo za kitalaam na ambazo awali hazikupatikana hapa nchini ikiwemo huduma za figo.

Konga amesema wameimarisha utendaji kupitia TEHAMA, na kwa sasa ipo mifumo ya uchakataji na ulipaji madai, usajili wa wanachama, mifumo ya mawasiliano pamoja na kutanua uwigo wa upatikanaji wa huduma kwa wanachama kwa kusaijili zaidi ya vituo 8000 katika mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar na vituo hivi ni pamoja na vya serikali, binafsi, madhehebu ya dini na maduka ya dawa.

Hata hivyo amesema katika safari ya NHIF na Watoa huduma kwa miaka hii 20 zipo changamoto nzuri zinazoleta mafanikio ambapo kati ya hayo ni malalamiko ya watoa huduma kucheleweshewa malipo ya madai ao hali iliyofanya kuanzisha mfumo wa uwasilishaji, uchakataji na ulipaji wa madai kwa njia ya mtandao.

changamoto ya udanganyifu kwenye huduma na madai ya malipo kwa kuimarisha mifumo ya huduma kupitia TEHEMA mfano sasa hivi mwanachama anapata taarifa ya huduma alizopata kupitia simu zao mara baada ya huduma, pia tumeanzisha kitengo cha kushughulikia udanganyifu na tumeendelea kufanya support supervision.

Amesema Kuwepo kwa malalamiko kwa baadhi ya wanachama kukosa huduma katika vituo ambazo zinalipiwa na Mfuko – Tumeendelea kutoa elimu kwa watoa huduma lakini pia kuchukua hatua kwa wanaofanya kinyume na makubaliano pia kuendelea kuimarisha mawasilisno na wanachama ili kupata taarifa kwa wakati.

Mfuko huo sasa umetimiza miaka 20 tarehe 1 Julai 2021. Tukiangalia tulipotoka ni mbali na tunayo mikakati ya tunapoelekea kama taasisi kwa kufikia wananchi wote na mpango wa bima ya afya (Bima ya Afya kwa Wote)kuendelea kuboresha huduma za matibabu kwakushirikiana na wadau ikiwemo Watoa huduma kuendelea kushiriki uimarishaji wa huduma za matibabu kwa kuwezesha vituo kupitia mikopo ya vifaa tiba na miundombinu.

kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Juma Muhimbi amesema kazi ya bodi ilitembelea na kuzungumza na watoa huduma wenu wa nchi nzima huku mkoa wa Dera es Salaam ukiwa na wa vituo vingi vya huduma kuliko mikoa yote, unawapa nafasi ya kufahamu na pia kuona hali halisi ya matibabu katika vituo vyetu vya kutolea huduma, hatua inayowapa mwanga zaidi katika utoaji wa maamuzi hususan mnapojadili namna ya uboreshaji wa huduma katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

Muhimbi amesema uwepo wa vituo hivi ni ishara nzuri ya upatikanaji wa huduma kwa wanachama kiurahisi, lakini pamoja na uwepo wa vituo hivi bado naamini kuwa zipo changamoto za hapa na pale hivyo kupitia kikao hiki changamoto hizi zitajadiliwa na kufikia maamuzi ya pamoja ya namna ya kukabiliana nazo.

Amesema kwa upande wa Serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam tutaendelea kuwapa ushirikiano mkubwa ili kuhakikisha ndoto ya Serikali yetu ya upatikanaji wa huduma za matibabu kwa wote inafikiwa. Tunaamini kwamba unapokuwa na wananchi wenye afya njema na uhakika wa matibabu unakuwa na uhakika wa kuzalisha zaidi na kufikia malengo ya Taifa huku azma ya serikali hii kufikia watanzania wote na huduma bora za matibabu kupitia bima ya afya kwa wote.
Share:

MCHUNGAJI ACHOMA MOTO MAWIGI YA MUUMINI


Picha ya Mchungaji Cyril Utomi

Mchungaji Cyril Utomi kutoka Nigeria ameyachoma mawigi na vipodozi vya muumini wa kike kwa madai asingeweza kukutana na Yesu akiwa na nywele na vitu vingine vya bandia ikiwa ni pamoja na viatu virefu.

Utomi alichoma vitu hivyo katika mkutano wa mahubiri ulioandaliwa na Holiness Revival Movement Worldwide mwishoni mwa mwezi Agosti na baada ya tukio hilo aliamua ku-post picha zinazoonesha vitu hivyo vikiteketea kwa moto katika mtandao wa facebook.
Share:

CHARAHANI ATOBOA KURA ZA MAONI UBUNGE CCM JIMBO LA USHETU, AWABWAGA WENZAKE 18

Emmanuel Charahani

Na Salvatory Ntandu - Kahama
Emmanuel Charahani ameibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kura za maoni katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano mkuu wa jimbo la Ushetu wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa kupata kura 442 na kuwashinda wenzake 18.

Akitangaza matokeo ya kura za maoni za jimbo hilo, msimamizi mkuu wa uchaguzi huo, James Kusekwa amesema kuwa uchaguzi huo ulikuwa huru na haki ambapo wagombea wote waliridhika na kusaini matokeo ya jimbo hilo lenye wajumbe 880.

Kusekwa aliwataja watia nia wengine walioshiriki uchaguzi huo kuwa ni pamoja na Makoye Mayenga aliyepata kura 143,Alhad Mlyansi kura 125,J ames Lembeli kura 56, Dk. Lamek Makoye kura 16 na Samson Lutonja kura 11.

Wengine ni pamoja na Ernest Nila kura 8 ,Bundala Shija kura 11 Dk Mathew Masele kura tano, Merry Lema kura tano Bether Juma kura tatu,Ahmed Haroun kura tatu,Michael Paschal kura mbili, Balindo Jordani kura moja, na Martine Mwakatundu kura 0.

Wakizungumza baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo baadhi ya watia nia wa jimbo hilo akiwemo Betha Juma amewataka wagombea wenzake kuvunja makundi yaliyokuwepo wakati wa kura za maoni na badala yake wamuunge mkono mgombea yeyote atakayeteuliwa na tume.

“Tuvunje makundi kuanzia leo,sisi ni wamoja na wajumbe wametupanga kwa uwezo wetu, jina lolote litakalorudishwa na chama sisi tutakuwa mstari wa mbele kumtafutia kura ili chama chetu kiweze kushinda katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Oktoba tisa mwaka huu”, amesema Juma.

Dk Yohana Masonda amesema wataendelea kuheshimu maamuzi ya wajumbe wa mkutano huo mkuu wa jimbo kwa kumchagua Charahani kuongoza katika kura za maoni na kuwataka wagombea wenzake kuwa na ummoja na mshikamano na kuachana na makundi yasiyokuwa na tija.

Awali akiwashukuru wajumbe wa mkutano huo, Emmanuel Charahani amesema kuwa atahakikisha anashirikiana na wagombea wengine katika kutafuta kura za CCM kwa atakayepitishwa na chama kupeperusha bendera katika uchaguzi mdogo ujao.

“Niwahakikishie mimi nitaendelea kushirikiana nanyi katika kutafuta maendeleo ya wakazi wa jimbo la Ushetu,bado tunachangomoto nyingi tunapaswa kuzitatua ili wananchi wetu waweze kupata maendeleo hususani katika sekta za afya,maji,umeme na miundombinu ya barabara,”amesema Charahani.
Share:

DED SHINYANGA NICE MUNISSY ATAKA WAENDESHA BODABODA KUPEWA ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Nice Munissy 
Mkurugenzi wa Shirika la TVMC Bw. Musa Ngangala

Na Josephine Charles - Shinyanga
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Nice Munissy amezitaka Asasi za Kiraia kuwashirikisha Vijana wanaendesha Pikipiki za biashara maarufu kama Bodaboda kwa kuhusishwa zaidi kwenye maeneo yao kupewa elimu za kupinga Ukatili wa Kijinsia dhidi ya watoto na Wanawake kwa kuwa moja kati ya vyanzo vya ukatili kwa watoto ni waendesha bodaboda. 
Munissy ametoa rai hiyo leo Mjini Shinyanga katika Kikao kazi kwa ajili ya Mradi wa Kupinga Ukatili wa Kijinsia unaotekelezwa na Shirika la The Voice of Marginalized Community(TVMC) chini ya Ufadhili wa Shirika la Foundation for Civil Society (FCS) kwenye kata Saba ambazo Samuye,Usanda,Didia,Masengwa,Tinde,Nsalala na Ilola za Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Kikao hichho kimehusisha Watendaji kata,Maafisa elimu, Maafisa Maendeleo ya Jamii,Wakuu wa Vituo vya Polisi,Bodaboda,Mahakimu,Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka kata husika na Maafisa kutoka Dawati la jinsia Polisi Wilaya ya Shinyanga. 

Akizungumza katika Kikao hicho Mkurugenzi wa Shirika la TVMC Bw. Musa Ngangala amesema lengo la kukutana na Wawakilishi kutoka katika kata hizo ni kuangalia namna gani zinafanya kazi hizo Sheria ndogondogo ambazo ziliundwa 2017 na mpaka kufikia sasa na kuangalia namna gani watazimbaza kwa Jamii iweze kujua kwamba kuna Sheria hizo pamoja na kutengeneza Mpango kazi wa pamoja katika maeneo hayo ili kupinga Ukatili kwa wanawake na watoto kwa kutumia Kamati za Ulinzi na Usalama wa Mtoto.

Kwa Upande wao Washiriki wa Kikao hicho wamesema vitendo vya Ukatili wa Kijinsia kuisha ni ngumu kutokana na changamoto mbalimbali zilizopo katika jamii ikiwemo elimu ndogo kwa Wazazi,Malezi hafifu yasiyo na msingi mzuri kwa watoto hususani mila potofu na kandamizi.

Aidha Mkutano huo umefunguliwa leo Septemba 2, 2021 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Bi. Nice Munissy na unatarajiwa kufungwa hapo kesho Septemba 3, 2021 na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Bi. Jasinta Mboneko.


Share:

HESLB Yaongeza Siku 15 Kwa Waombaji Mikopo Elimu Ya Juu.


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa uombaji mikopo kwa siku 15 zaidi kuanzia Septemba 1 hadi 15 mwaka huu ili kuwapa fursa kwa waombaji mikopo ambao wamejisajili katika mfumo kukamilisha maombi yao.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru ametangaza uamuzi huo  (Jumatano, Septemba 1, 2021) jijini Dar es salaam na kufafanua kuwa uamuzi huo umetokana na maombi na ushauri walioupokea kutoka kwa wadau.

Idadi ya waombaji
“Tulianza kupokea maombi kwa njia ya mtandao Julai 9, mwaka huu na hadi jana ambayo ilikua siku ya mwisho ya kuomba tulikua na waombaji 91,445 waliowasilisha maombi, na kati ya hayo, maombi 12,252 yalikua hayajakamilika na wateja wetu wameomba muda wa kukamilisha,” amesema Badru.

Mkurugenzi Mtendaji alikua akiongea katika mkutano na wanahabari uliofanyika katika ofisi za HESLB jijini Dar es salaam ambao pia ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) na Shirika la Posta Tanzania (TPC) ambao pia wanawahudumia waombaji mkopo.

Hatua inayofuata
Kwa mujibu wa Badru, hatua inayofuata ni uhakiki wa nyaraka na taarifa zilizowasilisha na waombaji 79,193 ambao maombi yao yamekamilika kama yanavyoonekana kwenye mfumo.

“Kuna makundi mawili, wale 12,252 ambao maombi hayana viambatisho na hivyo hayajakamilika … na kuna maombi 79,193 yenye nyaraka, sasa tunaanza kuhakiki usahihi wake na baadae tutaangalia kama wamepata udahili na wale wenye sifa ndiyo watapangiwa mkopo,” amesema Badru.

Fursa ya kuomba mkopo vijana waliopo JKT
Kuhusu wanafunzi wahitaji wanaoendelea na mafunzo katika Kambi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Badru amesema vijana hao waliopo katika kambi 19 nchini watapata fursa ya kuomba mkopo kwa siku 10 kuanzia Septemba 20 hadi 30 mwaka huu.

“Tumekuwa tukiwasiliana na Makao Makuu ya JKT, na tumekwenda na kukutana na vijana hao katika kambi zote na tuliwaahidi kuwa watapata fursa … ambayo ni kuanzia Septemba 20 hadi 30 mwaka huu, hivyo wasiwe na wasiwasi,” amesema Badru.

RITA na TPC kuendelea kuwahudumia waombaji
Katika mkutano huo, Badru pia ameeleza kuwa HESLB imekubaliana na RITA na TPC kuendelea kuwahudumia waombaji mkopo katika kipindi chote kilichoongezwa.

“Wenzetu wa RITA wanaendelea kuhakiki vyeti vya vifo na kuzaliwa wanavyopokea na wamekuwa wakifanya hivyo hata kabla ya kufunguliwa kwa dirisha la maombi … na Posta (TPC) wameahidi kuendelea kupokea nyaraka kupitia huduma ya EMS katika muda ulioongezwa, tunawashukuru sana” amesema Badru.

Bajeti ya mikopo kwa 2021/2022

Katika mwaka wa masomo 2021/2022, Serikali imetenga kiasi cha TZS 570 Bilioni kwa ajili ya kugharamia mikopo ya wanafunzi 160,000 wa taasisi za elimu ya juu. Kati ya hao, wanafunzi 62,000 wanatarajiwa kuwa ni wa mwaka wa kwanza na wanafunzi 98,000 wanaoendelea na masomo. Bajeti kwa mwaka 2020/2021 ilikua TZS 464 bilioni na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 149,398.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu


Share:

RAIS SAMIA : TOZO ZA MIAMALA YA SIMU ZITAENDELEA KUWEPO KAMA KAWAIDA


Rais Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa tozo za miamala ya simu zitaendelea kuwepo kama kawaida ili kupata fedha za kuendeleza miradi ya maendeleo na kujiepusha kuwa kwenye mikono ya wafadhili.

Kauli hiyo ameitoa leo Septemba 2, 2021, wakati akiwasalimia wananchi wa Tegeta akiwa njiani kuelekea Bagamoyo kwa ajili ya kurekodi vipande vya filamu vitakavyotangaza utalii wa Tanzania kimataifa, filamu ambayo itazinduliwa nchini Marekani.

"Nataka niwaambie kwamba tozo zitaendelea kuwepo na sitaki kuwaficha, kwa sababu tozo zile miezi miwili tuliyoanza nayo tumekusanya zaidi ya shilingi bilioni 60 na zimepelekwa kujenga vituo vya afya 220 hivyo tunajenga wenyewe ili wafadhili wanaokuja na masharti wasituingilie mambo yetu," amesema Rais Samia.

CHANZO - EATV
Share:

Assistant Lecturer (Insurance and Risk Management) at Institute of Accountancy Arusha IAA

POST ASSISTANT LECTURER (INSURANCE AND RISK MANAGEMENT) – 1 POST   POST CATEGORY(S) ENVIRONMENTAL SCIENCES AND GEOGRAPHY TAXATION AND SOCIAL PROTECTION EMPLOYER Institute of Accountancy Arusha (IAA) APPLICATION TIMELINE: 2021-08-31 2021-09-13 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA Level 8 (Bachelor Degree); ii. To prepare learning resources for tutorial exercises; […]

This post Assistant Lecturer (Insurance and Risk Management) at Institute of Accountancy Arusha IAA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lecturer (Banking) at Institute of Accountancy Arusha (IAA)

POST LECTURER (BANKING) – 1 POST   POST CATEGORY(S) BANKING, ECONOMICS AND FINANCIAL SERVICES EMPLOYER Institute of Accountancy Arusha (IAA) APPLICATION TIMELINE: 2021-08-31 2021-09-13 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA Level 8 for Master’s Degree holders and up to NTA Level 9 for PhD holders; ii. To guide and […]

This post Lecturer (Banking) at Institute of Accountancy Arusha (IAA) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Relationship Manager, Local & Mid Corporates at Standard Chartered Bank

About Standard Chartered    We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit.  It’s about showing how you embody our valued behaviours – do the right thing, better together and never settle […]

This post Relationship Manager, Local & Mid Corporates at Standard Chartered Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MEJIMENTI MPYA YAANZA KAZI MAKAO MAKUU YA PAPU


Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika, (PAPU) anayemaliza muda wake Ndugu Younouss Djibrine ( kushoto) akikabidhi Ofisi kwa Katibu Mkuu Mtendaji Mpya Ndugu Sifundo Chief Moyo kwenye Ofisi za PAPU Jijini Arusha, leo Tarehe 1 Septemba 2021. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Dkt. Faustine Ndugulile (wa tatu kutoka kulia), Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta Zimbabwe na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania( TCRA) Dkt. Emmanuel Manasseh (wa kwanza kushoto). PICHA NA: TCRA


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (Mb) akitoa hotuba kwa washiriki wa Mkutano wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) uliofanyika jijini Arusha mapema juma hili. Washiriki wa Mkutano huo wameshuhudia makabidhiano ya ofisi baina ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja huo aliemaliza muda wake Younouss Djibrine Katibu Mkuu Mtendaji mpya Ndugu Sifundo Chief Moyo. PICHA NA: TCRA


Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta nchini Zimbabwe Mhe. Supa Mandiwanzira akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) jijini Arusha, Tanzania kushuhudia makabidhiano ya ofisi ya Katibu Mtendaji Mkuu wa umoja huo ; anaeshuhudia ni Katibu Mkuu Mtendaji wa umoja huo aliemaliza muda wake Ndugu Younouss Djibrine. PICHA NA: TCRA


Kutoka kulia ni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (Mb) akiwa sambamba na Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta nchini Zimbabwe Mhe. Supa Mandiwanzira wakifuatilia shughuli za mkutano wa makabidhiano ya Ofisi ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) jijini Arusha mapema wiki hii. Aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa umoja huo Ndugu Younouss Djibrine (Cameron) amekabidhi ofisi kwa Ndugu Sifundo Chief Moyo(Zimbabwe). PICHA NA: TCRA


Washiriki wa Mkutano wa Makabidhiano ya ofisi ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) wakiongozwa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania Mhe. Dkt Faustine Ndugulile. Katika Mkutano huo uliofanyika makao makuu ya PAPU jijini Arusha, Tanzania; Ndugu Younouss Djibrine (Cameron) (wa pili mstari wa pili kulia) amekabidhi ofisi kwa Ndugu Sifundo Chief Moyo(Zimbabwe) wa kwanza mstari wa pili kulia). PICHA NA: TCRA

****************************


Menejimenti mpya ya chombo cha sekta ya posta barani Afrika, Umoja wa Posta Afrika (PAPU) imeanza kazi leo, tarehe 1 Septemba 2021 kufuatia sherehe iliyofana iliyofanyika kwenye jengo la uwekezai PAPU, makao makuu Arusha mjini mkoani Arusha.

Katibu Mkuu WA PAPU aliyemaliza muhula wake, Bwana Younouss Djibrine; alikabidhi uongozi kwa Katibu Mkuu mpya wa Umoja huo, Bwana Sifundo Chief Moyo kwenye shughuli ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Dr. Faustin Ndugulile (Mb.).

Kma sehemu ya mabadiliko ya uongozi katika chombo hicho cha bara la Afrika, Katibu Mkuu Msaidizi aliyemaliza muhula wake kwenye Umoja huo, Bwana Kolawole Aduloju pia alikabidhi ofisi kwa Bi. Jessica Hope Uwera Sengooba.

PAPU inaendele kutekeleza majumumu yake muhimu ya kujenga ENEO MOJA LA SHUGHULI ZA POSTA wakati wote na katika mazingira yote, kama mchango wake kwenye kufikia azma ya pamoja na ya muda mrefu ya watu wa Afrika ya kuleta maendeleo shirikishi na endelevu kwa jamii.

Mabadiliko ya menejimenti ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) yameainishwa kwenye utaratibu rasmi wa kukabidhiana madaraka kwa mpangilio baada ya kumalizika kwa muhula wa uongozi wenye mafanikio makubwa.

Menejimenti mpya inaingia ofisini kipindi cha janga la UVIKO-19 ambalo limevuruga shughuli za mifumo ya shughuli za kibiashara na ambalo linahofiwa kuleta athari za muda mrefu kwenye maendeleo ya kawaida ya biashara na kwa hivyo kuibua changamoto kwa umma kwa ujumla kutathmini upya njia bora za kukabili athari hizo.

Mikakati ya kutathmini upya na kukabili hali hii inahitajika ili kuweza kugeuza changamoto zilizojitoketa kuwa fursa kwa ama kubadilimifumo ya utoaji huduma au kubadili bidhaa na huduma zinazotolewa ili kuendelea kuwa na wateja na hivyo kuendeleza biashara. Hii itachangia katika kulinda sekta ya posta na kuimarisha uwezo wake wa kugundua mapema na kukabiliana na majanga mengine kama haya mbeleni.
Share:

JINSI DAKTARI WANGU WA KIENYEJI ALIVYOKOMESHA MARADHI HAYA



Niite Anita, mimi ni mama ambaye nimekuwa mgonjwa kwa muda mrefu mno na tumetumia kiasi kukubwa cha hela kwa matibabu yangu bila mafanikio. 

Madaktari bandia wamekula hela zetu wakidanganya kuwa wana uwezo wa kunitibu lakini wote ni matapeli tu.

 Nilizaliwa nikiwa mzima kabisa na hata utotoni mwanangu sikuwahi kuwa mgonjwa kiholela holela lakini nilipofika kidato cha tatu, ndipo hali yangu ya kiafya ilianza kudhoofika. 

Miguu ikaanza kuvimba kidogokidogo. Sikuwahi kudhani ugonjwa huo ungelikuwa mkubwa hadi pale ukalipoathiri miguu yangu yote.

 Wazazi wangu walianza juhudi za kuhakikisha kuwa nimepata matibabu maalum kwa kunipeleka hospitali mbalimbali kote nchini lakini hali ilibakia hivyo hivyo.

 Kwa kweli babangu alifika mahali akaamua kuuza kipande kidogo cha ardhi ili kunilipia matibabu lakini la kushangaza hela hizo zote kima cha shilingi elfu mia sita zilipotelea kwa madaktari bandia.

 Ilikuwa mwaka jana ndipo shangazi wangu mmoja alitutembela na aliponiangalia na kuona hali niliokuwemo, alibubujikwa na machozi kisha akatuibia siri ya Doctor Kiwanga. 

Kiwanga ni daktari aliye na uwezo wa kuyatibu maradhi mbalimbali akitumia miti za kiasili. Shangazi alitusihi atupeleke kwa Kiwanga Doctors na la kushangaza tulipofika tu hivi Daktari alishika mguu wangu wa kwanza akauangalia kisha akainua mguu nwingine na kupaka mafuta fulani baridi. 

Alipomaliza shughuli alituambia turudi nyumbani. Leo hii ninapoongea nanyi mimi ni mzima wa afya. 

Ahsante Kiwanga Doctors; laiti ningelijua mapema hatungekuwa tumearibu pesa zetu kwa madaktari wengine bandia.

 Vile vile, kama unajuwa una matatizo na mambo ya mapenzi kwa nyumba yako tafadhali nakusihi upate matibabu wa Kiwanga. Kiwanga Doctors ni shujaa wa mambo yote. 

Ninatoa wito kwa wenye shida za magonjwa, mapenzi, ndoa, biashara, kikazi na afya kuharakisha kuwatembelea madaktari was Kiwanga. Tovuti au Website yao ni: www.kiwangadoctors.com; Simu: +254 769404965 au wasiliana kwa barua pepe yaani Email: kiwangadoctors@gmail.com.

Sio lazima usafiri hadi ofisi zao. Ongea nao kwa njia ya simu na utasaidika kwa haraka kama vile watu wengine wanavyopata usaidizi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger