Monday, 16 August 2021

FHI 360 YATOA BAISKELI 242 KWA WAWEZESHAJI UCHUMI KUPAMBANA NA VVU SHINYANGA


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati (wa pili kushoto) akikabidhi baiskeli kwa Mwezeshaji Uchumi, Yasinta Moses (kulia). Kushoto ni  Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka, Wa pili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Shirika la Family Health International (FHI 360) limetoa msaada wa Baiskeli 242 kwa Wawezeshaji uchumi (Empowerment Workers) ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.

Hafla fupi ya makabidhiano ya Baiskeli hizo imefanyika leo Jumatatu Agosti 16,2021 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati.

Akipokea baiskeli hizo, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati amelipongeza Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia mradi wa EPIC, wafadhili wa mradi USAID na PEPFAR pamoja na asasi za kiraia kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuchangia na kusaidiana na serikali katika mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwa makundi yaliyoko kwenye athari za kupata maambukizi ya VVU hasa mabinti.

“Wawezeshaji kiuchumi nendeni mkafanye kazi kwa niaba ya serikali. Kafanyeni kazi ya kuwafikia mabinti ili tupunguze maambukizi ya VVU katika jamii yetu,toeni elimu ya miundo na uchumi ili wasichana wafanye kazi na kupata mitaji na kupunguza tabia hatarishi za kupata maambukizi ya VVU”,amesema Dkt. Sengati.

Amesema kwa mujibu wa Tanzania HIV Impact Survey ,2016-17, takwimu zinaonesha hali ya maambukizi ya VVU kwa wasichana balehe na wamama vijana ni asilimia 15.3% ukilinganisha na umri wao huo ambao ni asilimia 6.6%.

“Pia kwa mujibu wa Utafiti wa Idadi ya Watu na Afya Tanzania na Utafiti wa Kiashiria cha Malaria, 2015 - 16 takwimu zinaonesha asilimia 27 ya wasichana balehe wenye umri wa miaka kati ya 15-19 wamepata mtoto au ujauzito”,ameeleza.

“Kutokana na takwimu hizo inaonesha ni jinsi gani wasichana balehe na wamama vijana wako katika athari kubwa na wanapaswa kulindwa na kuhakikisha tunapunguza maambukizi ya VVU/UKIMWI miongoni mwao”,ameongeza Dkt. Sengati.

Mkuu huyo wa mkoa ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha yanaifikia jamii na kutoa eleimu ya kutosha ili kupunguza changamoto zinazowakumba wasichana zikiwemo mimba za utotoni,ukatili wa kijinsia na maambukizi ya VVU na kwamba serikali itaendelea kushirikiana nao ili kuwa na jamii inayomthamini mtoto wa kike na kumpa ulinzi wa kutosha.

“Serikai tunatambua na kuthamini mchango wa wadau na hatuwezi kufanya kila kitu ndiyo maana nyinyi kama wadau mko mstari wa mbele kuisaidia serikali kutekeleza agenda ya maendeleo ya 2030 na kuhakikisha kwamba 95-95-95 (95 % ya watu wanaoishi na VVU wanajua hali yao ya maambukizi, 95% ya waliopima wameanza kutumia dawa na 95% ya walioanza dawa wamepunguza makali ya VVU”, amesema Dkt. Sengati.

Akikabidhi baiskeli 24 kati ya 242 Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka amesema Shirika la Family Health International (FHI 360) limetoa baiskeli hizo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kimataifa wa EPIC kwa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).

“Kupitia mradi huu tumetoa jumla ya baiskeli 242 kwa mkoa wa Shinyanga ambazo zinagawiwa kwa walengwa katika halmashauri 5 za wilaya ambazo ni Shinyanga, Manispaa ya Shinyanga na Kahama, Ushetu na Msalala. Leo tumekusanyika hapa kwa dhumuni la kugawa baiskeli kwa wawezeshaji uchumi 24 wa Manispaa ya Shinyanga”,amesema Dkt. Msuka.

Ameeleza kuwa baiskeli hizo zitasaidia Wawezeshaji Kiuchumi kuwafikia wa wasichana balehe na wamama vijana na kuchangia jitihada za serikali katika kuhakikisha maambukizi ya VVU/UKIMWI yanapunguzwa na kufikia malengo ya 95-95-95.

“Baiskeli hizi ni sehemu ya vitendea kazi kwa wawezeshaji uchumi,tunaamini zitapunguza changamoto ya usafiri na kuwawezesha kuwafikia wasichana wengi zaidi katika kata, vijiji,vitongoji na hata ngazi ya kaya”,amesema Dkt. Msuka.

“Baiskeli hizi zinapaswa kutumika kwa matumizi ya mradi tu na si vinginevyo ili kuboresha hali ya mabinti na kutokomeza janga la UKIMWI. Tanzania bila UKIMWI inawezekana, tuendelee kutoa elimu kwa kila mtu asimame katika nafasi yake kufikia na kuendeleza udhibiti wa janga la VVU/UKIMWI nchini Tanzani”,ameongeza Dkt. Msuka.

Dkt. Msuka amesema Mradi wa EPIC unatekeleza afua za utoaji wa huduma zinazohusiana na VVU zikiwalenga makundi maalumu na yanayohitaji kupewa kipaumbele ikiwemo wasichana wa rika balehe na wamama vijana, wanaume na wanawake walio katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Amefafanua kuwa Mpango wa DREAMS ni kati ya afua zinazotekelezwa na mradi wa EPIC wenye lengo la kupunguza maambukizi ya VVU kwa wasichana balehe na wanawake vijana wenye umri wa miaka 9 hadi 24, wanaoishi katika mazingira hatarishi na wanafanya ngono katika umri mdogo ili waweze kumudu gharama za maisha.

Mradi wa EPIC unatekeleza mpango wa DREAMS katika halmashauri 6 za mkoa wa Shinyanga tangu mwezi Februari 2020 kupitia mashirika manne ya kijamii ambayo ni Rafiki SDO, TADEPA, HUHESO Foundation na SHIDEPHA. Tayari jumla ya wasichana 100,000 wamefikiwa.

“Wasichana 20,000 wamefikiwa na huduma za kitabibu kama upimaji wa VVU kwa hiari,uchunguzi wa ukatili wa kijinsia,huduma za uzazi wa mpango,uchunguzi wa magonjwa ya zinaa na huduma za dawa kinga (PREP), 38,000 wamefikiwa na huduma za miundo ambako wanaweka akiba na kukopa, 13,000 wameweza kuanzisha biashara zao wenyewe na 100,000 wamefikiwa na huduma za mabadiliko ya tabia”,ameongeza.

Akizungumza kwa niaba ya Wawezeshaji Uchumi,Sophia Chamba amelishukuru Shirika la FHI 360 na Mradi wa EPIC kwa kuwapatia baiskeli hizo ambazo watazitumia kuifikia jamii kutekeleza majukumu yao ambayo ni pamoja na kuwafundisha mabinti balehe na wanawake vijana masomo ya uchumi na yanayosaidia kujikinga na maambukizi mapya ya VVU.

Ameyataja majukumu mengine kuwa ni kutoa elimua ya mabadiliko ya tabia na upimaji wa VVU kwa kushirikiana na waelimisha rika,kufundisha masuala ya ujasiriamali na kuandikisha mabinti balehe na wanawake vijana katika vikundi kulinga na umri wao.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza leo Jumatatu Agosti 16,2021 wakati akipokea baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi (Empowerment Workers) ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza wakati akipokea baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi (Empowerment Workers) ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
 Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka akizungumza leo Jumatatu Agosti 16,2021 wakati akikabidhi baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
 Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka akizungumza leo Jumatatu Agosti 16,2021 wakati akikabidhi baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Mwezeshaji Uchumi,Sophia Chamba akilishukuru Shirika la FHI 360 na Mradi wa EPIC kwa kuwapatia baiskeli hizo ambazo watazitumia kuifikia jamii kutekeleza majukumu yao.
Mratibu wa TACAIDS mkoa wa Shinyanga Geofrey Mambo akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi ngazi ya kata mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akikagua baiskeli moja kati ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akiendesha baiskeli ambayo kati ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akiendesha baiskeli ambayo kati ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata ili kuwafikia wasichana balehe na wamama vijana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati (wa pili kushoto) akikabidhi baiskeli kwa Mwezeshaji Uchumi, Rachel Manga (kulia). Kushoto ni  Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka, Wa pili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary. Hizi ni sehemu ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati (wa pili kushoto) akikabidhi baiskeli kwa Mwezeshaji Uchumi, Amina Bundala (kulia). Kushoto ni  Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka, Wa pili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary. Hizi ni sehemu ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati (wa pili kushoto) akikabidhi baiskeli kwa Mwezeshaji Uchumi, Elizabeth Sollo (kulia). Kushoto ni  Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka, Wa pili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary. Hizi ni sehemu ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati (wa pili kushoto) akikabidhi baiskeli kwa Mwezeshaji Uchumi, Mary Ford (kulia). Kushoto ni  Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka, Wa pili kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary. Hizi ni sehemu ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wawezeshaji Uchumi wakiendesha baiskeli zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wawezeshaji Uchumi wakiendesha baiskeli zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya baiskeli zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Muonekano wa sehemu ya baiskeli zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wawezeshaji Uchumi wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya kukabidhiwa baiskeli zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Meneja wa Mradi wa EPIC Mkoa wa Shinyanga Dkt. Shinje Msuka (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.
Wadau wa VVU/UKIMWI na Wawezeshaji Uchumi wakiwa ukumbini wakati wa hafla ya makabidhiano ya baiskeli 242 zilizotolewa na Shirika la Family Health International (FHI 360) kupitia Mradi wa EPIC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR kwa Wawezeshaji uchumi  ngazi ya kata mkoani Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

MGOMBEA WA UPINZANI ASHINDA URAIS ZAMBIA


Rais mteule wa Zambia kupitia Chama cha UPND Hakainde Hichilema na Makamu wake wa Rais Mutale Nalumango
***
Mgombea wa kiti cha urais nchini Zambia kupitia chama cha upinzani cha UPND Hakainde Hichilema, ameshinda katika kinyang'anyiro hicho kwa kupata kura milioni 2.8 na kumshinda aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Edgar Lungu aliyepata kura milioni 1.8.

Hichilema amepata ushindi huo baada ya kushindwa mara tano katika chaguzi kama hizo na amemshinda mpinzani wake wa siku nyingi Edgar Lungu, ambaye amedai kwamba uchaguzi huo haukuwa huru na wa haki kwa madai ya kuwa maafisa wa chama chake waliokuwa wakisimamia uchaguzi walifukuzwa kwenye vituo vya kupigia kura.

Uongozi wa miaka sita chini ya Rais Edgar Lungu ulikosolewa kwa madai ya kukiuka haki za binadamu, ufisadi na uchumi uliodorora pamoja na ukosefu wa ajira, ambapo Rais mteule wa sasa pamoja na Makamu wake Mutale Nalumango, watakabiliwa na changamoto ya kubadilisha uchumi wa taifa hilo.

Rais mteule wa taifa hilo Hakainde Hichilema, ana umri wa miaka 59.

Uchaguzi huo umefanyika Agosti 12, mwaka huu
Share:

MWALIMU NA MWENZAKE MBARONI WAKITUHUMIWA KUMUUA MTOTO WA MIAKA MITANO KWA KIPIGO SINGIDA

Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi wa Polisi (  ACP) Stella Mutabihirwa.
 


Na Dotto Mwaibale, Singia


JESHI la Polisi Mkoa wa Singida linawashikilia Mwalimu   Regina Laurent, (28) wa Shule ya Msingi Mang'onyi na  Mathias Marmo  (30) kwa tuhuma za kumuua kwa kipigo mtoto mwenye umri wa miaka 5 aitwaye Joyce John, mkazi wa Kijiji na Kata ya Mang’onyi,  wilayani Ikungi mkoani hapa.

Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi wa Polisi (  ACP) Stella Mutabihirwa  amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa watuhumiwa hao walikuwa ni walezi wa mtoto huyo na kuwa uchunguzi zaidi ukikamilika wote wawiliwatafikishwa mahakamani kujibu shitaka linalowakabili.

Mutabihirwa akizungumza na waandishi wa habari mwishoni mwa wiki kuhusu tukio hilo alisema Agosti 11/2021 majira ya saa 1:30 usiku katika Hospitali ya Malkia wa Ulimwengu iliyopo maeneo ya Puma, Wilayani Ikungi, Mkoa wa Singida mtoto huyo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu hospitalini hapo ambapo wauguzi wa hospitali hiyo walitilia mashaka kifo hicho kutokana na majeraha aliyokuwa nayo marehemu na ndipo waliamua kutoa tarifa kwa Jeshi la Polisi.

Alisema Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida lilipata taarifa hizo siku hiyo majira ya saa 2:00 usiku ambapo lilifanya uchunguzi wa awali na kubaini kuwa majeraha aliyoyapata marehemu yalitokana na kupigwa na vitu vinavyodhaniwa  kuwa ni fimbo na kitu butu sehemu mbalimbali za mwili wake na wazazi wake walezi ambao ni Mathias Marmo, (30), Mwalimu wa Shule ya Msingi Mang'onyi na Regina Laurent, (28), wote wairaq na wakazi wa mang'onyi.

Aidha Mutabihirwa alisema uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtoto huyo alikuwa akipigwa na kufanyiwa ukatili mara kwa mara na walezi wake hao na kuwa mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi wa kitabibu na kukabidhiwa kwa ndugu kwa hatua za mazishi. 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kukemea vitendo vya kikatili vinavyofanywa na baadhi wazazi na walezi na linawaomba wananchi kuachana na vitendo hivyo vikiwemo kutoa adhabu zisizokuwa na mipaka kwa watoto na kusababisha unyanyasaji wa kijinsia na wazazi wameaswa kuwalea watoto wao katika maadili mema.

Share:

NAIBU WAZIRI DK.MABULA AKUTANA NA WADAIWA SUGU WA KODI ZA ARDHI MKOA WA SINGIDA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula, akizungumza katikati ya wiki na watumishi wa idara za ardhi na wadau mbalimbali wa Mkoa wa Singida katika ziara yake ya siku moja ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi. Kutoka kulia ni Mwakilishi wa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida Mjini, Eva Jeremia na Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Singida, Shamim Hozza.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (kulia) akingalia namna upimaji ardhi unavyofanyika kwa kutumia teknolojia ya kisasa katika Kijiji cha Mnang’ana wilayani Ikungi mkoani Singida alipokwenda katikati ya wiki kukagua mradi wa upimaji ardhi unaotekelezwa kwa pamoja na UN WOMEN, UNFPA na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa ufadhili wa KOICA. Kutoka kushoto ni Mpima Ardhi Arafat  Rajab, Kaimu Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ambrose Ngonyani na Mpima Ardhi Aisha Juma.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, akizungumza na wananchi na Wapima Ardhi wa Kijiji cha cha Mnang’ana.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, akizungumza na watoto mapacha Hussein Yusuf (kushoto) na Hassan Yusuf ambao walikuwa katika zoezi la kupimiwa ardhi zao waliopatiwa na wazazi wao. Kulia ni Baba wa watoto hao Yusuf Misanga Diwani mstaafu wa Kata ya Sepuka.
Kaimu Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ambrose Ngonyani (kushoto),akielezea zoezi la upimaji wa maeneo hayo. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Singida Shamim Hozza na Diwani wa Kata ya Sepuka, Halima Athuman Nyimba.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, akikabidhi hati za kiwanja.
Hati za viwanja zikikabidhiwa.
Father Manoel Tsing akizungumza kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Father Justine Boniface akizungumza kwenye kikao hicho.


Na Dotto Mwaibale, Singida.


NAIBU Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula amekutana na wadaiwa sugu wa kodi ya pango la Ardhi Mkoa wa Singida ili kutafuta njia bora za kulipa madeni hayo.

Mabula alikutana na wadaiwa hao katikati ya wiki hii baada ya kukutanishwa nao kwenye kikao chake na watumishi wa idara za ardhi na wadau mbalimbali wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi mkoani hapa.

Alisema kwenye Sheria ya ardhi kifungu cha (33) kifungu kidogo cha (3),kinasema mtu yeyote ambaye anamiliki ardhi anatakiwa kulipa kodi ya pango la ardhi kama sheria inavyoelekeza.

Alisema lakini kuna baadhi ya watu baada ya kupimiwa maeneo yao hujificha na  hawaendi kuomba kumilikishwa ili waanze kulipa kodi.

Alisema kutokana na hali hiyo Serikali iliona iweke utaratibu kwa  mtu yeyote ambaye amepimiwa eneo lake apewa siku 90 za kuomba kumilikishwa na asipofanya hivyo baada ya siku hizo atatakiwa kulipa kodi, ambapo pia ilitoa msamaha kwa waliopimiwa kipindi cha nyuma wataanza kulipa kuanzia mwaka jana sheria ilipoanzishwa.

Mabula alisema wizara imeamua kutoa nafasi hiyo kwa wadaiwa hao kabla ya kuanza utekelezaji wa sheria ili waweze kujua wajibu wao kama raia, taasisi na watu binafsi wa kulipa kodi ambapo wizara itatoa nafasi ya mwaka mmoja waweze kulipa madeni yao.

"Niwatake watumishi wa wizara hii mkaanze kusimamia sheria, kwasababu hamsimamii sheria vizuri ndio maana mchakato huu wa kulipa kodi unakuwa mgumu,nniwaombe walipa kodi lipeni kodi zenu kila mwaka mkivusha zoezi la kulipa litakuwa zito kwasababu kiwango kitaongezeka kutokana na kulimbikiza." alisema Mabula.

 Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Singida Shamim Hozza akisoma taarifa ya utekelezaji wa wizara hiyo mkoani hapa alisema mkoa ulipangiwa kukusanya maduhuri yatokanayo na ardhi Sh. Bilioni moja na milioni mia tisa lakini walikusanya Sh. Bilioni moja na milioni mia mbili sawa na 66%.

 Alisema moja ya changamoto zilizosababisha ofisi yake kushindwa kufikia lengo ni madeni makubwa ya Serikali na baadhi ya taasisi za dini ambazo zimekuwa na ukakasi wa kulipa madeni hayo.

Hozza  alisema ili kukabiliana na changamoto hizo ofisi yake inaendelea kufanya jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhamasisha na kufanya mikutano ya wananchi pamoja na kutoa matangazo kwa njia mbalimbali, kutoa nyaraka za umilikishaji na madeni na kwa wale ambao walikaidi kulipa madeni walifikishwa kwenye mabaraza ya ardhi kwa hatua zaidi.

Dkt.Mabula kabla ya kufanya kikao hicho alishiriki katika zoezi la mradi wa upimaji mipaka ya vijiji na makazi katika Kijiji cha Mnang'ana wilayani Ikungi ambao unatekelezwa kwa pamoja na mashirika ya UN WOMEN, UNFPA na Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa ufadhili wa KOICA.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 16, 2021


















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger