Thursday, 20 May 2021

Serikali Yawaonya Wakuu Wa Taasisi Wanaoanzisha Mifumo Bila Kuzingatia Sheria

Na Faustin Gimu-Dodoma

SERIKALI imewaonya wakuu wote wa Taasisi za Serikali ambao wamekuwa wakianzisha mifumo ya kimtandao bila kuzingatia kanuni,Sheria na taratibu zinazoongozwa kwa misingi ya sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019 na kanuni zake za mwaka 2020'

Hayo   yameelezwa na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Mohamed Mchengerwa jijini Dar es Salaama wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea ofisi hiyo na kuzungumza na watumishi wa Mamlaka hiyo ya Serikali Mtandao ambapo pia amewaonya wakuu wa Taasisi za umma nchini wenye lengo la kujitoa katika matumizi ya mifumo iliyotengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) na kusema kuwa kufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa Sheria

''Ninafahamu kuna baadhi ya Taasisi za Serikali kushirikiana na wadau wao wanaotaka kujitoa katika matumizi ya mifumo inayotengenezwa na eGA,kujitoa katika mifumo ambayo tayari tumeirasimisha kwa misingi ya sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019 na kanuni zake za mwaka 2020 ni kinyume cha Sheria''Alisema Waziri wa Mchengerwa

''Nitoe rai na onyo kwa wakuu wote wa Taasisi za Serikali kuwa hakuna Taasisi wala Ofisi yoyote ya Serikali ambayo inaruhusiwa kujitoa kwenye mifumoinayosimamiwa na eGA''Aliongeza Waziri Mchengerwa

Aidha pia ameiagiza eGA kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuhakikisha wanadhibiti  uvujaji wa siri lakini pia utolewaji wa taarifa ambazo hazistahili kwenda moja kwa moja kwa watumiaji wa kawaida

Vile vile ameipongeza eGA kwa  jitihada kubwa wanazofanya za kuendelea kubuni mifumo ambayo ina rahisisha utendaji kazi Serikalini ambapo pia amewasihi kuendelea kutekeleza jukumu hilo kwa kuzingatia kasi ya Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) Mhandisi Benedict Ndomba yeye ametaja baadhi ya athari zinazoweza kujitokeza endapo Taasisi za umma hazitopeleka taarifa za mifumo inayoanzisha kuwa ni pamoja na kutokufata viwango na miongozo jambo linalopelekea mifumo kutowasiliana



Share:

Prof. Mkumbo Aongoza Kikao Cha 32 Cha Bodi Ya Wakurugenzi Wa EPZA


Waziri wa Viwanda na Biashara na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa EPZA, Prof. Kitila Mkumbo ameongoza kikao cha kawaida cha 32 cha bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maeneo Maalum ya Uzalishaji kwa Mauzo ya nje (Export Processing Zones Authorty -EPZA).

Kikao kimefanyika  Mei 19, 2021 Jijini Dodoma katika ukumbi wa Mkutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Jengo la Mkapa na  kimeudhuliwa na viongozi mbalimbali; Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Dotto James, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil Abdallah, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EPZA, Mathew Mnali na wajumbe wengine wa bodi ya wakurugenzi wa EPZA.

Kikao hicho kimekuwa na lengo la kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ripoti ya Mkurugenzi wa EPZA kwa kipindi cha Januari – Machi 2021, Makadirio ya mapato na matumizi ya Mamlaka ya (EPZA) kwa mwaka 2021/2022, utaratibu wa kuendeleza Mradi wa kurasini SEZ, mradi wa kubangua korosho kwa kushirikiana na wajasiriamali (SMEs) na mengineyo


Share:

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kufanya ziara ya kikazi ya siku moja Hapa Nchini


Rais wa Uganda, Mhe. Museveni leo Mei 20, 2021 atafanya ziara ya kikazi ya siku 1 hapa nchini.

Akiwa nchini Mhe. Rais Museveni na Mhe. Rais Samia watashuhudia utiaji saini wa mikataba ya bomba la mafuta la Hoima - Tanga kati ya Tanzania na kampuni za uwekezaji katika mradi huo.


Share:

Rais Samia amteua Brigedia Generali Nduku Mabele kuwa Mkuu wa JKT, na Kanali Lyanga Shausi kuwa Mkurugenzi wa SUMA - JKT


Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Rajabu Mabele

**

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan  tarehe 19 Mei 2021 amemteua Brigedia Jenerali Rajabu Nduku Mabele kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa. Hatua hiyo inafuatia kuteuliwa kwa aliyekuwa Mkuu wa Jeshi hilo, Meja Jenerali Charles Mbugekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera hivi karibuni.

Brigedia Jenerali Mabele alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tarehe 25 Novemba 1993 na kutunukiwa Kamisheni kuwa Afisa tarehe 25 Machi 1995. Pamoja na taaluma nyingine za Kijeshi, Jenerali Mabele ana Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Biashara (Master of Business Administration), alijikita katika Usimamizi wa Mashirika (Corporate Management).

Katika utumishi wake Brigedia Jenerali Mabele amewahi kushika nyadhifa mbalimbali zikiwemo Afisa Usalama na Utambuzi katika Vikosi kadhaa; Afisa Mnadhimu Malipo na Afisa Malipo wa Kikosi Makao Makuu ya Jeshi; Mkurugenzi wa Fedha za Umma na Uhasibu (Director for Public Finance and Accounting) na baadae alihamishiwa Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA-JKT), nafasi aliyohudumu hadi kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Sambamba na uteuzi huo, Mhe. Rais amemteua pia Kanali Absolomon Lyanga Shausi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA-JKT. Kabla ya uteuzi huo Kanali Shausi alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Shirika hilo.

Kwa niaba ya Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo anawapongeza Brigedia Jenerali Mabele na Kanali Shausi kwa kuaminiwa katika nyaadhifa hizo na kuwatakia heri na fanaka katika utendaji wao.



Share:

Pakistan, Iran Zaahidi Kuimarisha Diplomasia Ya Uchumi


Na Mwandishi wetu
Pakistan na Iran zimeahidi kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi mapana ya pande zote.

Ahadi hizo zimetolewa kwa nyakati tofauti wakati Mabalozi wa Pakistan na Iran walipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mabalozi waliokutana na Waziri Mulamula ni Balozi wa Pakistani hapa nchini Mhe. Mohammad Saleem pamoja na Kaimu Balozi wa Irani hapa nchini Mhe. Hossein Alvandi Behineh ambapo viongozi hao wamejadili masuala ya kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Nchi zao lakini pia kuimarisha na kuboresha diplomasia ya uchumi kwa maslahi mapana ya nchi zote.

Pamoja na mambo mengine, Balozi wa Pakistan Mhe. Saleem ameelezea kufurahishwa na uhusiano mzuri uliopo baina ya Iran na Tanzania na amepongeza hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Tanzania imeendelea kuzichukua katika kuimarisha diplomasia ya uchumi.

Nae Kaimu Balozi wa Iran amesisitiza juu ya uwekezaji na biashara ambapo amesema kuwa Serikali yake ipo tayari kufanya biashara na Tanzania na kuinua uchumi wa wananchi wan chi zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Liberata Mulamula (Mb) amewahakikishia mazingira salama ya biashara na uwekezaji na kuwaahidi ushirikiano wa kutosha kutoka Tanzania.

Kadhalika, Waziri Mulamula amesema ushirikiano wa diplomasia ya uchumi kati ya Tanzania na Pakistan unatoa fursa nyingi ikiwemo kukuza biashara hasa katika sekta ya kilimo ikiwemo chai, pamba, korosho, mbegu za mafuta, Madini ya Tanzanite, pamoja na uwekezaji.


Share:

HUDUMA YA KUNUNUA UMEME 'LUKU' KUPITIA MITANDAO YA SIMU NA BENKI YAREJEA

 


Share:

Program Support Specialist at Compassion International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The role of Program Health Support Specialist will provide subject matter expertise regarding the health of all program beneficiaries (pregnancy through youth). This role will collaborate with other Support Specialists, Program Trainers and Partnership Facilitators to ensure staff and Frontline Church Partners (FCP) are adequately informed and equipped to ensure preventative and curative care for all beneficiaries. […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Fieldworker (2 posts) at Ifakara Health Institute 2021

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Position:                    Fieldworker (2 posts) Reports To:               Project Leader/Supervisor Work Station:           Mtwara   Institute Overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, training and services, the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Research Scientist at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Position:               Research Scientist  (1 post) Reports To:            Principal Investigator Work Station:              Rufiji/Kibiti  Institute Overview Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, training and services, the Institute’s […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Field Supervisor at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Summary Position:                    Field Supervisor (1 post) Reports To:               Project Leader Work Station:           Mtwara   Institute Overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, training and services, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 20 2021
















Share:

Wednesday, 19 May 2021

MHANDISI MALONGO AWATAKA WAHANDISI KUTEMBELEA MIRADI MIKUBWA....AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU TATU

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Malongo,akifungua mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Malongo,akisisitiza jambo kwa washiriki wa mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Malongo,akizungumza na washiriki (hawapo pichani) wakati wa mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021 jijini Dodoma.

Baadhi ya Wahandisi wakifatilia hotuba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Malongo,(hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021 jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wahandisi,Mhandisi Ninatubu Lema,akizungumza wakati wa mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021.

Msajili wa Bodi ya Wahandisi,Mhandisi Patrick Barozi,akielezea lengo la mafunzo hayo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021.

Msajili wa Bodi ya Wahandisi,Mhandisi Patrick Barozi,akionyesha kitabu chenye mwongozo wakati wa mafunzo ya Wahandisi yanayofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma kuanzia leo Mei 19 hadi 21,2021.


Na.Alex Sonna,Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Malongo,amefungua mafunzo ya siku tatu ya Wahandishi wenye lengo la kujadili miradi ya kimkakati ili iweze kusaidia Taifa katika utekelezaji na usimamizi wa miradi hiyo huku akiwataka kutembelea miradi mikubwa nchini ili kujionea changamoto zilizopo.

Akizungumza leo Mei 19,2021 wakati akifungua mafunzo hayo kuhusu uendeshaji wa maswala ya miradi ya kimkakati kwa wahandisi itakayosaidia kukidhi mahitaji ya watanzania yalioandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi nchini (ERB) yanayofanyika kwa siku tatu jijini Dodoma.

Mhandisi Malongo amesema kuwa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa kwenye sekta ya ujenzi hivyo wahandisi wanatakiwa kupata elimu ili kukabiliana na malalamiko kwa Wahandisi kwenye utekelezaji wa miardi yao.

Amewataka kuanzisha mafunzo yajayo yasihusishe wahandisi pekee bali ihusishe wote wanaofanya miradi kutimia.

“Ni vizuri tukianzisha mafunzo mengine tuhakikishe kuwa wahandisi, watunza fedha na wanasiasa watakuwepo ili kuwe na mchanganuo mzuri wa mawazo” amesema Mhandisi Malongo

Hata hivyo ameipoongeza bodi ya usajili wa wahandisi (ERB) kwa kuanzisha mafunzo hayo badala ya kuitegemea serikali kujiendeleza kitaaluma kwani ilikuwa inawarudisha nyuma wahandisi.

Aidha amewaomba wahandisi kuanza kutembelea miradi mikubwa inayoendelea nchini ili kujifunza changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wahandisi Ninatubu Lema amesema kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo wahandisi kuhusu nini kifanyike katika kuendana na kasi ya teknolojia huku kuwaongezea elimu kuibua, kusimamia miradi ya kimkakati itakayoleta tija kwa Taifa.

Awali Msajili wa Wahandisi, Mhandisi Patrick Barozi, amesema kuwa mafunzo ya usimamizi wa miradi yataendelea kutolewa ili kuimarisha uwezo wa wahandisi nchini na kuwataka wahandisi wenye sifa kujisajili na Bodi hiyo.

Share:

Picha : MAMIA WAMIMINIKA KUSAKA UMEME 'LUKU' TANESCO SHINYANGA

Mamia ya wakazi wa Shinyanga wamemiminika katika ofisi za Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) mkoa wa Shinyanga na Wakala wa Luku Mfoy kwa ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki.

Malunde 1 blog imeshuhudia wakazi wa Shinyanga wakiwa wamepanga foleni katika ofisi za TANESCO na Wakala Mfoy aliyepo katika eneo la Stendi ya Mabasi Mjini Shinyanga ili kupata huduma ya umeme huku wengine wakionekana kukata tamaa kutokana na foleni ndefu kufikia huduma hiyo. 

Tayari Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani ameagiza kusimamishwa kazi kwa siku 10 watumishi watatu wa TANESCO akiwemo Meneja wa mfumo wa LUKU kwa kushindwa kutatua tatizo la LUKU lililojitokeza kwa siku tatu na kuleta usumbufu kwa wananchi.

Waliosimamishwa kazi ni Meneja wa TEHAMA na huduma za biashara wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Lonus Feruzi na Wasaidizi wake Frank Mushi na Idda Njau ili watoe maelezo kufuatia kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki na kusema endapo maelezo yao hayatojitosheleza wataondolewa kazini.

Kwa muda wa siku tatu, Wateja wa TANESCO wameshindwa kununua umeme wa LUKU kwa njia ya Kielekroniki hivyo kulilazimu Shirika hilo kuwaelekeza Wateja wake kununua umeme kwenye ofisi zake za Mikoa na Wilaya katika maeneo mbalimbali nchini.
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi za Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi za Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi za Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi za Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi ya Wakala wa LUKU Mfoy kwa ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi ya Wakala wa LUKU Mfoy kwa ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi ya Wakala wa LUKU Mfoy kwa ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki
Wakazi wa Shinyanga wakiwa katika ofisi ya Wakala wa LUKU Mfoy kwa ajili ya kupata huduma ya umeme kutokana na kuwepo kwa tatizo katika huduma ya manunuzi ya LUKU kupitia njia za kielektroniki.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Tyre Fitter at dangote

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Description Key Duties and Responsibilities · Inspect tire casing for defects such as holes and tears. · Rotate tires to different positions on vehicles, using hand tools · Prepare rims and wheel drums for reassembly. · Reassemble tires onto wheels. · Tire scrap analysis · Tire retreading · Tire care and tire management · Seal […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Public Health Administrative Management Assistant (Finance) at U.S. Embassy Dar es Salaam

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and qualified applicants for the position below. Position Title: Public Health Administrative Management Assistant (Finance) Vacancy Number: DaresSalaam-2021 -021 Duties Extramural Budget Execution/Analysis/Management 35% Provides expert technical advice to implementing partners in the development of long and short term financial strategies and plans to achieve […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

JAMAA AJICHIMBIA KABURI NA KUJENGA MNARA, ANUNULIWA JENEZA ANALOPENDA



Katika kile wengi wanaweza kuelezea kama jambo lisilokuwa la kawaida, mwanaume Mnigeria akiwa bado hai na buheri wa siha, Chifu Clement Usoro amejiandaa kwa kifo chake baada ya kujijengea kaburi na hata kusherehekea hafla hiyo kabla ya kuondoka kwake akisema hataki watoto wake kuandaa hafla ya mazishi baada ya kifo chake.

Mzee huyo mwenye umri wa miaka 73, katika mahojiano na BBC Pidgin, alisema alifanya maandalizi muhimu ya mazishi yake miaka mitatu iliyopita wakati alitimiza umri wa miaka 70.

 Kulingana naye, tayari ameandika wosia. Hata hivyo, Usoro, alisema anaendelea kuusahihisha kila wakati.

"Nimeandika wosia wangu na nitaendelea kuusahihisha kulingana na muda.Nimejenga kaburi langu. Ni kaburi lenye futi 9 kwa 9. Pia nimejenga mnara kando yake. "Rafiki yangu alikwenda nami katika duka la jeneza kuona lenye nitapenda.Aliamua kuninunulia. Kama chifu, kuna mambo unatakiwa kufanya kabla ya kufa ama wafanye baada yako," alisema Usoro.

Chifu Usoro pia alifichua kuwa amelipia vitu muhimu vya ibada kwa machifu wake wasaidizi akitoa ng'ombe ili kuwazuia wanawe kuwa na wasiwasi baada ya kifo chake.

 Aliongezea kuwa hataki familia yake kuandaa hafla ya mazishi baada ya kifo chake akidai kuwa kusherehekea kifo chake ni kupoteza muda na pesa.

 Mzee huyo pia alisema aliwaagiza watoto wake kumzika siku tatu baada ya kifo chake. 
Share:

SHUHUDIA MAAJABU YA NG'OMBE WANAOOGELEA KAMA BINADAMU


Ng'ombe wakiogelea na binadamu
Jamii ya Njemps au Ilchamus

Mwandishi ni Kevin Anindo, Kaunti ya Nairobi.

Hii ni Afrika na Afrika kuna mengi ya kuvutia. Leo nakuangushia makala kuhusu mila ya zamani ya kabila la eneo la Ziwa Baringo linalohusishwa na biashara na maisha ya kabila lililo katika hatari ya kuangamia inakuwa kivutio halisi cha watalii, hasa kipindi hiki Kenya inapoendelea kushuhudia kuimarika zaidi kwa utalii wa ndani na kupungua kwa wageni au kusafiri nje kwa matajiri.

 Hili ni tukio la "ajabu" lisicho la kawaida la ng'ombe wanaoogelea wa Kisiwa cha Kokwa. Jamii ya wafugaji ya Njemps, kabila la dogo la Wamaasai ambalo idadi ya watu wake ni zaidi ya 30,000, hawana njia nyingine ya kuuza ng'ombe wao zaidi ya kusafirisha kila wiki kwenda sokoni katika mji wa Marigat.

Njemps ni moja ya jamii zinazotajwa kuwa maskini sana na wana mitumbwi ya miti ya asili ambayo hawawezi kuitumia kusafirishia ng'ombe wao hadi okoni, kwa hivyo kwa miaka mingi wamefundisha ng'ombe wao kuogelea kwenye maji ya ziwa kufikia ufukweni kutoka kisiwa hicho.

 Kwa muda baada ya hamu ya kushuhudia ng'ombe hao wakiogelea, tukio hilo sasa ni moja katika vivutio vya utalii huko Baringo na eneo jirani na mara nyingi ng'ombe hao husindikizwa na boti zilizobeba watalii na wao hufurahia kupiga picha na video hata kwa kutumia simu zao za rununu. 

Wakati mwingine, boti zile zile ambazo, kwa upande mwingine, labda zinamilikiwa na hoteli ambazo hutumika kushuhudia "kivutio hicho cha kabila hili" hutumiwa kuwabeba ng'ombe hao. 

Lakini ni vipi ng’ombe wanaojulikana kuwa waoga wa maji ya kina kirefu hufaulu kuogelea?

 Ingawa ng'ombe kwa kawaida ni mwogeleaji mzuri lakini inategemea mazingira, anaweza kuogelea vizuri-kama sio bora-kushinda mwanadamu. Maeneo mengine mfano hili tunalozungumzia, ng'ombe huogelea kwenye maji ya vina tofauti na ni sehemu ya maisha yao.

Mmoja wa wafugaji wa eneo hilo aliyezungumza na TUKO.co.ke alisema, "Walishaji mifugo wa Njemps hupeleka mifugo wao hadi kwenye ufukwe wa kisiwa hicho, kisha huwatupa majini ndama lakini wakiwa makini wasije wakazama au kusombwa.

"Kwa kuhofia kumpoteza ndama ng'ombe hufuata ili kuwaokoa na polepole watajifunza kuogelea.Wao huwarejesha ndama wao ufukweni na kisha tukio hilo hurejelewa mara kadha kwa kipindi fulani, mpaka watakapozoea kuogelea peke yao, bila kujali sana kuokoa watoto wao". 

Mazoea huwafanya ng'ombe kuwa tayari muda wote kuvuka mito peke yao kwa msaada mdogo. Lakini ni bora kufahamu kuwa, haimaanishi ng'ombe wanaoogolea wanaweza kuogelea tu bila kikomo.

 Ng'ombe wakianguka kwenye maji, wanahitaji njia ya kuwawezesha kutoka nje kabla ya kuchoka na labda kuzama. Nyakati nyingi, mito na maziwa huwa na maeneo yanayoteremkia fukweni ambayo huwasaidia ng,ombe walioingia kwenye maji hayo kutoka nje salama.

CHANZO - TUKO NEWS
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger