Monday, 25 January 2021

Waziri Bashungwa: Sekta za Wizara ya Habari ni mihimili Muhimu Nchini.


Na Shamimu Nyaki - WHUSM
Sekta za Wizara ya Habari ni sekta muhimu  zenye  mchango mkubwa katika kuchangia uchumi wa nchi na kuleta  maendeleo.

 Hayo yamesemwa  leo Jijini Dodoma na Waziri  wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa wakati akiwasilisha Muundo pamoja na Majukumu ya Wizara hiyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii.

Mhe. Bashungwa amesema kwamba Sekta ya Sanaa na Michezo zimechangia katika Ongezeko la pato la Taifa ambapo kwa mwaka 2018, shughuli za burudani zimechangia pato la Taifa kwa asilimia 13.7 na kushika nafasi ya kwanza  na  mwaka 2019 shughuli hizo zilichangia asilimia 11.2 na kushika nafasi ya tatu.

"Tunashukuru Kamati kwa kutupa mawazo chanya ambayo yatasaidia kuboresha na kuendeleza sekta hizi, naahidi mimi pamoja na timu yangu tutayafanyia kazi mawazo mliyotupa na tayari tumeanza kufanya hivyo katika sekta zote" alisema Mhe. Bashungwa.

Akiendelea kuzungumza Mhe. Bashungwa ameeleza kuwa Wizara tayari imeanza kutengeneza Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Michezo pamoja na ujenzi wa Ukumbi wa Michezo na Sanaa (Sports and Arts Arena) ambayo itaanza kujengwa Jijini Dodoma.

Aidha, Mhe. Bashungwa ameeleza kuwa TCRA pamoja na TRA wameanza kushirikiana namna ya  kukusanya mapato ya kazi za Sanaa kupitia njia za Kidijiti (Digital Taxation).

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Stasilaus Nyongo Mbunge wa  Jimbo la Maswa Mashariki ameipongeza Wizara hiyo kwa Mikakati mizuri ya kusaidia Sekta inazozisimia, huku akishauri Wizara hiyo kuongeza ubunifu katika kukusanya mapato ya Serikali kupitia Sanaa na Michezo.   

"Nashauri Wizara hii, Wizara ya Elimu pamoja na TAMISEMI  kuwa na utaratibu unaotambulika wa kuendesha na kusimamia shughuli za michezo shuleni" Mhe. Nyongo.

Naye Mhe. Jumanne  Sagini Mbunge wa Jimbo la Butiama ambaye ni Mjumbe wa Kamati hiyo amepongeza juhudi za Wizara hiyo katika kutekeleza majukumu yake ambapo ameeleza kuwa ipo haja ya kufanya mapitio ya Sera zote zilizochini ya Wizara hiyo ili kama kuna ambazo zinahitaji marekebisho zifanyiwe maboresho ili kuendana na mahitaji ya wakati huu.

Kamati hiyo imepokea taarifa ya Muundo na Majukumu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambapo kesho Januari 26, 2021 itapokea Taarifa ya Majukumu ya Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo.

Mwishoo....


Share:

KAIMU AFISA VIJANA MKOA WA SINGIDA FREDERICK NDAHANI AISHAURI SERIKALI KUFUFUA SHULE ZA UFUNDI

 

Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (wa pili kushoto) akizungumza na Walimu wa Ufundi  wa Shule ya Msingi Makiungua iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida alipoitembelea juzi kwa lengo la kukagua uwezeshwaji mafunzo na ujuzi kwa vijana.

Madawati yakitengenezwa. na Shule ya Msingi Makiungu iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Madawati yaliyotengenezwa.
Kaimu Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (kulia) akikagua utengenezaji wa madawati.
Madawati yaliyotengenezwa.

Na Dotto Mwaibale, Singida.

KAIMU Afisa Vijana mkoani hapa,  Frederick Ndahani ameishauri Serikali kufufua Shule za Msingi za ufundi Nchini. 

Ndahani alitoa ushauri huo juzi alipotembelea  Shule ya Msingi Makiungu iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida kwa lengo la kukagua uwezeshwaji mafunzo na ujuzi kwa vijana.

Ndahani alisema Shule ya Msingi Makiungu ni moja ya shule zilizofanya  vizuri katika mradi waliopewa wa kutengeneza madawati 1000  ya shule za msingi zilizopo wilayani humo.

Ndahani alisema shule hiyo ya mchepuo wa ufundi   ni moja ya shule inayoifanya vizuri na kusababisha ofisi ya mkurugenzi wa wilaya ya  Ikungi kuwapa kazi ya kutengeneza madawati hayo.

" Shule hizi za mchepuo wa ufundi hapa nchini zikiboreshwa zinaweza kusawaidia vijana wa kitanzania kupata ujuzi wa ufundi mbalimbali." alisema Ndahani.

Alisema  wanafunzi wanaojiunga katika shule hiyo hapa ni wale ambao wamekosa nafasi ya kuendelea na elimu ya sekondari na vyuo na kuwa faida wanayoipata ni kupata mafunzo hayo ya ufundi bure  kama ilivyo elimu ya msingi.

Alisema  kuboreshwa kwa shule  hizo kutasaidia kupata mafundi ambao watatumika kukarabati samani mbalimbali zilizopo mashuleni badala ya kuwapa mafundi kutoka nje ambao watahitaji kulipwa fedha nyingi.

Kwa upande wao  Walimu wa Ufundi katika shule hiyo Cosmas Uhiku na  Haji Kidabu Wameiomba Serikali kuwapatia vifaa vya kutosha kwani wanao uwezo wa kuwapatia vijana mafunzo ya kisasa  sanjari na vyeti baada ya kumaliza mafunzo kwa muda wa miaka miwili.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo  Hashimu Ntandu amemshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi kwa kuwapatia mradi huo mkubwa wa kutengeneza madawati ambapo wanatengeneza kwa gharama nafuu.


Share:

NAIBU WAZIRI SILINDE AAGIZA TSC IPEWE OFISI ZENYE HADHI


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), mjini Morogoro, Januari 25, 2021. Wengine kutoka kulia ni Mwenyekiti wa TSC Profesa Willy Komba, Kaimu Katibu wa TSC Moses Chitama na Katibu wa Baraza husika,Lawrence Chankani.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde (kushoto), akisalimiana na Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Profesa Willy Komba, muda mfupi baada ya Naibu Waziri kufungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa TSC, mjini Morogoro, Januari 25, 2021. Katikati ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama. 
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Profesa Willy Komba (kulia), akitoa hotuba ya ukaribisho wa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde (katikati), wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo, Januari 25, 2021 mjini Morogoro. Kushoto ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama. 
Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Moses Chitama akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo, uliofanyika Jaunuari 25, 2021 mjini Morogoro. Katikati ni Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde na kulia ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Profesa Willy Komba. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde (wa tatu - kulia), akiungana na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kuimba wimbo maarufu wa ‘Solidarity Forever’. Naibu Waziri alifungua Mkutano huo mjini Morogoro, Januari 25, 2021. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa TSC, Profesa Willy Komba na kulia kwake ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama. 
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano huo mjini Morogoro, Januari 25, 2021. 
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Abihudi Hemba akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Baraza hilo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde (hayupo pichani) baada ya kufungua Mkutano huo mjini Morogoro, Januari 25, 2021. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde (katikati-waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), muda mfupi baada ya kufungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakzi wa Tume hiyo Januari 25, 2021 mjini Morogoro. Kushoto kwa Naibu Waziri ni Mwenyekiti wa TSC, Profesa Willy Komba na kushoto kwake ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama.

*************************

Na Veronica Simba - TSC

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde amewaagiza Wakurugenzi wa Wilaya kote nchini, kuhakikisha wanawapatia ofisi zenye hadhi, watumishi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) katika maeneo yao.

Ametoa maagizo hayo leo, Januari 25, 2021 mjini Morogoro wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume.

Naibu Waziri ametoa maagizo hayo baada ya kuelezwa changamoto mbalimbali zinazoikabili Tume husika, ambapo mojawapo ni ya ukosefu wa ofisi zenye hadhi kwa watumishi wa TSC hususani zilizoko katika baadhi ya Wilaya nchini.

“Nitumie fursa hii kuagiza Wakurugenzi wote nchini kuhakikisha wanawapatia Makatibu Wasaidizi wa Tume, ofisi ambazo zinaendana na hadhi ya utumishi wa umma.”

Aidha, ameitaka Tume kuhakikisha inawawezesha Walimu kujitambua na kuelewa sheria, kanuni, taratibu, haki na wajibu wao.

Vilevile, ameipongeza Tume kwa kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kwa moyo wa uzalendo, pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili. Pamoja na kutoa pongezi, ameitaka Tume kuendelea kutoa huduma bora kwa Walimu.

"Sote tunafahamu kuwa tunapotoa huduma bora kwa Mwalimu inamwezesha kutekeleza majukumu yake shuleni kwa ufanisi hatimaye kuinua kiwango cha elimu nchini.”

Naibu Waziri ameihakikishia Tume kuwa ushirikiano uliopo katika utendaji kazi kati ya Tume na Ofisi ya Rais – TAMISEMI ni endelevu. Aidha, ameongeza kuwa Ofisi yake itaendelea kusisitiza kila Wilaya kuhakikisha kazi za kushughulikia masuala ya kiutumishi ya Walimu zinatekelezwa kwa ushirikiano ili kuleta tija na ufanisi katika suala zima la kuwahudumia walimu.

Awali, akiwasilisha hotuba ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mwenyekiti wa Tume, Profesa Willy Komba alibainisha changamoto kadhaa zinazoikabili, ikiwa ni pamoja na kutokuwa na jengo la Ofisi za Tume Makao Makuu na Wilaya.

Alisema changamoto nyingine ni baadhi ya waajiri kutokuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika kushughulikia masuala ya kinidhamu ya Walimu.

“Mfano kuchelewa kuwasilisha mashtaka kwa Mamlaka ya Nidhamu, kuchukua jukumu la kutoa adhabu kinyume cha utaratibu na kuwaondoa Walimu kwenye mfumo wa malipo kabla ya mchakato wa mashauri kuanza na kukamilika,” amefafanua Profesa Komba.

Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa pia na Kaimu Katibu wa Tume, Moses Chitama, Menejimenti ya Tume pamoja na wawakilishi mbalimbali kutoka wilaya zote nchini.

Tume ya Utumishi wa Walimu ni Mamlaka ya Ajira na Nidhamu kwa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari za Serikali, Tanzania Bara. Naibu Waziri David Silinde ndiye amepewa wajibu wa kusimamia Taasisi hii pamoja na nyingine zilizo chini ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

Share:

Database Administrator at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Database Administrator   Background CRDB Bank Plc is an African bank and a leading Financial Services Provider in Tanzania with current presence in Tanzania and Burundi, East Africa. The Bank was established in 1996 and was listed on The Dar Es Salaam Stock exchange (DSE) in June 2009. Over the years, CRDB Bank has grown […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Digital Channels Systems at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior Specialist, Digital Channels Systems     CRDB Bank PLC is looking for a suitable candidate to fill 2 vacant positions of Senior Specialist, Digital Channels Systems existing in the Department of Information & Communication Technology (ICT) at Head Office, Dar es Salaam. Job Purpose: To effectively lead a team of ICT Specialist, Systems administrators, responsible […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Manager ICT Strategy & Governance at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior Manager ICT Strategy & Governance     CRDB Bank PLC is looking for a suitable candidate to fill 1 vacant position of Senior Manager ICT Strategy & Governance existing in the Department of Information & Communication Technology (ICT) at Head Office, Dar es Salaam. Job Purpose: The Senior Manager ICT Strategy & Governance is responsible […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

ICT Risk & Compliance specialist at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ICT Risk & Compliance specialists    CRDB Bank PLC is looking for a suitable candidate to fill 2 vacant position of ICT Risk & Compliance specialist existing in the Department of Information & Communication Technology (ICT) at Head Office, Dar es Salaam Job Purpose:   Responsible for managing and maintaining the IT risk assurance program […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Specialist ICT Security solutions at CRDB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Specialist ICT Security solutions     CRDB Bank PLC is looking for a suitable candidate to fill 2 vacant positions of Specialist ICT Security solution existing in the Department of Information & Communication Technology (ICT) at Head Office, Dar es Salaam. Job Purpose Daily monitoring of the IT Infrastructure using security technical expertise and looking for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Coordinator at Aga Khan Education Service

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

PYP Coordinator     AGA KHAN EDUCATION SERVICE TANZANIA CAREER OPPORTUNITY Aga Khan Education Service, Tanzania (AKESJ), is a private, not for profit, service company registered under the Companies Act and operates three schools in Tanzania. The vision of AKESJ is to provide accessible, world-class education, which prepares students to become self-confident, open-minded articulate and ethical […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Head of Creative Arts at Aga Khan Education Service

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Head of Creative Arts     AGA KHAN EDUCATION SERVICE TANZANIA CAREER OPPORTUNITY Aga Khan Education Service, Tanzania (AKESJ), is a private, not for profit, service company registered under the Companies Act and operates three schools in Tanzania. The vision of AKESJ is to provide accessible, world-class education, which prepares students to become self-confident, open-minded articulate […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Account Manager at Standard Chartered

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Account Manager, Group Special Assets Management – (2000020304)   Job: Risk Primary Location: Africa & Middle East-Tanzania-Dar es Salaam Schedule: Full-time Employee Status: Permanent Posting Date: 22/Jan/2021, 12:07:57 PM Unposting Date: 06/Feb/2021, 2:59:00 AM About Standard Chartered  We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Market Development Executives at Mwananchi Communications

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Market Development Executives     Job Summary To increase copy sales and develop relationships with partners in the distribution channel and to ensure that you meet you’re set sales targets while maintaining an optimal return level. Full Job Description   Promotes and coordinates sale and distribution of newspapers in areas served by franchised wholesale distributors: Surveys […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Relationship Managers at NMB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Relationship Manager, SME (2 positions)   Reporting Line: Senior Coverage Manager, SME Location: Lake Zone (1 position) – to be based in Mwanza & Southern Zone (1 position) – to be based in Mtwara Application Deadline: 6th February 2021 Job Purpose Responsible for growing both Liabilities (Deposits) and Assets from Small and Medium Enterprises (SMEs) for […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MWAMBA ALIYEONDOKA NYUMBANI KWENDA KUTAFUTA AJIRA MIAKA 46 ILIYOPITA AREJEA


Mzee mwenye miaka 75, amerejea nyumbani kwao katika kijiji cha Kolait, Teso Kaskazini, kaunti ya Busia nchini Kenya baada ya kutoweka kwa miaka 46 kutafuta ajira.

Francis Indek Arachabon anaripotiwa kuondoka nyumbani kwao mwaka 1975, akiwa na miaka 29 akielekea Kimilili kumtembelea mjomba wake lakini aliamua kurefusha safari yake hadi Soy kutafuta ajira ambapo alipoteza mawasiliano na familia yake. 

Kwa mujibu wa Nation, familia yake ilimtafuta kwa jamaa zake, vituo vya polisi na hata katika hifadhi ya maiti. 

Lakini baada ya miaka 46, Arachabon alirejea nyumbani mnamo Jumapili, Januari 17,2021 na alipokelewa na kaka yake mwenye miaka 71, Erneo Okadapao. 

Okadapao aliongezea kuwa mchungaji mmoja kutoka nchini Uganda alimuahidi kuwa kaka yake atarejea na kweli unabii huo umetimia. 

Arachabon alisema kwa miaka ambayo alitoweka, alimuoa Susan Tabolei na wamejaliwa watoto watatu na ni kutokana na familia yake mpya ndio ilimchochea kufuta mawazo ya kurejea nyumbani.

 Mzee huyo aliongezea kuwa alikuwa akilima mashamba ya watu na kufanya vibarua vingine vidogo ili kujichumia riziki. 

Katika taarifa tofauti, wakazi wa kijiji cha Nabisiongo, eneo bunge la Matayos katika kaunti ya Busia walishtuka baada ya mwanamume aliyedhaniwa kufariki na kuzikwa kujitokeza miezi minne baadaye.

 Familia ya Steven Ogolla ilikuwa imeandaa mazishi yake baada ya kutoweka kwa miezi minne. Kaka yake Ogolla, Steven Ouma alichana mbuga akidhania kuwa ameona zimwi kwani walikuwa wamemzika.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 25, 2021


Magazetini leo Jumatatu January 25,2021



















Share:

MAABARA YA TMDA KANDA YA ZIWA YAJIIMARISHA ILI KUWA KITOVU CHA UCHUNGUZI WA VIPUKUSI



Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Kanda ya Ziwa (TMDA) Kanda ya Ziwa, Sophia Mziray.
Kaimu Mkurugenzi wa Maabara ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA -Kanda ya Ziwa) Bugusu Nyamweri.
Mchunguzi wa Maabara ya TMDA – Kanda ya Ziwa, Maximilian Rwezaula.
Muonekano wa jengo la Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) kanda ya Ziwa. 

.................................................

Kaimu Mkurugenzi wa Maabara  ya Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA -Kanda ya Ziwa) Bugusu Nyamweri amesema TMDA inataka  maabara hiyo ibobee kwenye uchunguzi wa vipukusi, ‘Hand Sanitizers’.

Mamlaka ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA – Dar es Salaam) imeona ni vema maabara hii (TMDA – Kanda ya Ziwa) ipewe kazi hiyo kwa sababu ina vifaa vya kisasa pamoja na wachunguzi ambao wana ujuzi katika kuchunguza vipukusi Amesema Nyamweri.

Amesema maabara hiyo  itachunguza pia vipukusi vingine kwa mfano dettol, vidonge vya Chroline ambavyo huyeyushwa kwa kiwango kinachoelekezwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ajili ya matumizi kwenye maeneo ya hospitalini.

Anaongeza kuwa hii ni sehemu ya vipukusi, ndiyo maana katika  mlolongo wa kuwa na vifaa vya kisasa  vya uchunguzi wa vipukusi, tumeleta mashine ya ‘Steam Distillation Unit’ ambayo ni miongoni mwa mashine zilizopo hapa maalum kwa uchunguzi wa Vipukusi.

Nyamweri anasema hii ni maalum kwa uchunguzi wa vipukusi aina ya vitakasa mikono ‘Hand Wash Sanitizers’.Vitakasa mikono ni aina mojawapo ya vipukusi (Antiseptic) ambavyo vipo katika kundi la kuua vimelea vya bakteria au vimelea vinavyosababishwa na virusi.

Akifafanua zaidi Kaimu Mkurugenzi wa Maabara hiyo Bw. Bugusu Nyamweri  anasema tulifanya uchunguzi kwa kutumia kifaa kingine lakini mashine hii ya sasa ni nzuri kwa sababu inarahisisha kazi, katika utumiaji ni nzuri katika  kutoa (kuchuja) kiwango cha pombe kinachohitajika katika sampuli ili kukamilisha uchunguzi,” anasema Nyamweri.

Anasema pamoja na uchunguzi wa kiwango cha pombe pia wanachunguza kiwango cha ‘PH’ ndani ya vipukusi hususan vitakasa mikono kwani kisipokuwa cha kutosha huweza kuathiri ngozi ya binadamu.

Anasema haimaanishi mashine ya awali haikuwa na ufanisi, ilikuwa nao, ila kutokana na  (uhitaji wa sasa), mashine hii ya sasa ni nzuri zaidi na inarahisisha kazi.

Bugusu Nyamweri anasema mashine hiyo hufanya kazi kwa dakika nne kuchuja kiwango cha ‘Alcohol’ wanachohitaji kukichunguza na kwamba ndani ya dakika sita tayari mtaalamu anakuwa ameweza kupata majibu ya sampuli yake.

“Ingawa mashine tulizokuwa tunazitumia awali zenyewe zinatumia muda mrefu katika uchunguzi, hii ya hapa Mwanza, ni ya kisasa zaidi inatoa majibu ndani ya dakika nne,” anabainisha.

Nyamweri anasema wateja wengi wanaowapokea wanaohitaji kufanyiwa uchunguzi wa vitakasa mikono wanavyotengeneza ni wajasiriamali, vituo vya afya na hospitali mbalimbali ikiwamo ile ya Kanda (Bugando) na hata vyuo vya mafunzo ya afya.

“Hii ni bidhaa muhimu ndiyo maana tunaendelea kuboresha uchunguzi wa vipukusi, kwa sababu  vinatumika mno hospitalini hivyo lazima tufuatilie kujua ubora wake, ili kuendelea kulinda afya ya jamii,” anasema.

Anasema uchunguzi wa vipukusi haukuwa katika viwango vinavyohitajika, kuna vingine ubora wake au utumiaji wake haufuatiliwi vizuri, kwa mfano kuna vile ambavyo  inabidi ‘wazimue’ na maji ili kuvitumia kwa mfano kusafisha viti meza mabenchi ya kukalia, vidonda, kuta na vifaa tiba vinginevyo.

Nyamweri anasisitiza kuwa “Tayari mipango mikakati imeshaandaliwa ikiwamo ya kuwajengea uwezo wataalamu katika matumizi ya teknolojia mpya pamoja na kuendelea kuongeza vifaa vya kisasa kwa ajili ya uchunguzi wa vipukusi.

Anasema kwa upande wa mashine ya ‘Steam Distllation Unit’ iliyonunuliwa miezi minane iliyopita wamefanikiwa kufanya uchunguzi wa sampuli za vitakasa mikono zaidi ya 90.

“Tumeona ufanisi wa utendaji kazi wa mashine upo vizuri kwa sababu tunapima kwa kutumia  (Viwango) vya Kimataifa, inafanya kazi vizuri.

Akiielezea mashine hiyo Mchunguzi wa Maabara ya TMDA – Kanda ya Ziwa, Maximilian Rwezaula anasema mashine hii ya ‘Steam Distillation Unit’ ina uwezo wa kutathmini na kuangalia ubora wa kiwango cha pombe (Alcohol) kilichomo kwenye kitakasa mikono.

Anaongeza kuwa Inafanya kazi kwa kutumia njia ya joto ili kuondoa kiwango cha pombe kinachohitajika kwa uchunguzi kwa mvuke, ambacho hukusanywa katika kifaa maalum kisha hatua za upimaji hufanyika kwa kutumia ‘Alcohol Meter’.

Maximilian  anasema ‘Alcohol’ iliyomo ndani ya kitakasa mikono ndicho kiambata muhimu kinachotumika kuua vidudu.

Unatakiwa kuangalia uuaji wa wadudu pamoja na muda ambao wadudu hao watakufa, tunaweka wadudu hao kitaalamu kwa muda maalum, tukikuta wamekufa, tunajua kitakasa mikono hicho kinaweza kufanya kazi,” anasema.

Anasema Kiwango cha pombe kisipofika asilimia 60 inakuwa haina uwezo wa kuua vidudu, hivyo tunapima kuhakikisha kimefikia, kabla hata ya kuruhusu bidhaa kuingia sokoni, pia kuna vipimo vingine vya Micro-Biology ambavyo tunaita Challenge Test.

Naye Meneja wa TMDA Kanda ya Ziwa, Sophia Mziray, anasema Mamlaka hiyo imedhamiria kwa dhati kuifanya maabara hiyo ya Kanda kuwa bora na maalumu kwa uchunguzi vipukusi.

“Hivi sasa maabara hiyo ya kanda ya ziwa ndiyo pekee kwa Nchi wanachama wa Ukanda wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) yenye uwezo wa kupima vipukusi na kutoa majibu yasiyo na shaka. Anaongeza Sophia Mziray.

“Na kwa kuwa ni maabara pekee katika Kanda ya Ziwa, hivyo tunaendelea pia kuchunguza dawa kutoka kanda nyingine, kutoa elimu kwa umma, na kuhakikisha Watanzania wanapata bidhaa bora, salama na zenye ufanisi.

“Mpango huu tunaotarajia utakamilika ndani ya miaka mitatu kuanza sasa, maabara hii ipo kwenye taratibu kuwa kubwa, ya kisasa, bora na bobezi katika uchunguzi wa vipukusi katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na hata Bara zima la Afrika,” amesema.

Anaongeza kuwa  Maabara hii ina mifumo ambayo imethibitishwa. Mamlaka inaandaa nyaraka, upembuzi yakinifu kujiridhisha kama rasilimali zinatosheleza ili kutimiza nia ya kuwa na maabara bora zaidi.

Share:

WADAU WA TIBA ASILI WATAKIWA KUJIPANGA KUUSHIKA UCHUMI WA MAUZO YA DAWA ASILI NA MIMEA DAWA KIMATAIFA


Mkurugenzi msaidizi wa tiba asili na tiba mbadala kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dkt. Paul Mhame akitoa hotuba ya uzinduzi wa jukwaa hili. 
Naibu Mkamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA upande wa utawala na fedha Prof. Amandus Mhairwa akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua rasmi jukwaa. 
Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko akitia neno kwa wagana hao wa tiba asili na wadau wengine wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo. 
Mkuu wa mradi huo wa GRILI Dkt. Faitha Mabiki akieleza kwa kifupia majukumua na malengo ya mradi huo wa GRILI na yale ambayo yamefanyika toka mradi uanzishwe. 
Wadau wa tiba sili na tiba mbadala kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania wakifuatilia hotuba na maneno ya uzunduzi wa Jukwaa lao kutoka kwa viongozi.

*****************************

NA: Calvin Gwabara - Morogoro.

Wataalamu wa chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA wametakiwa kushirikiana na wataalamu wa tiba asili na taasisi zingine katika kufanya tafiti za dawa ambazo zitasaidia dunia katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa COVID 19 na magonjwa mengine hatari kwa afya ya binadamu,Wanyama na hata mimea kwani takwimu nchini Tanzania zinaonyesha tiba asili inatoa mchango wa zaidi ya asilimia 45 katika unga wa matibabu.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi msaidizi wa tiba asili na tiba mbadala kutoka wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dkt. Paul Mhame kwa niaba ya Katibu mkuu wa wizara hiyo wakati wa ufunguzi wa jukwaa la ubunifu la wadau wa tiba asili Tanzania uliofanyika SUA mkoani Morogoro.

Dkt.Mhame amesema kuwa Tiba asili inayo nafasi kubwa katika kukabiliana na magonjwa hayo ikiwa ni pamoja na kutafuta namna ya kuzuaia na kutibu na ndio maana kuna sheria ya tiba asili na tiba mbadala Na.23 2002.

“Upatikanaji a tiba asili na tiba mbadala inayotokana na mimea dawa itasaidia sana kufikia wananchi wengi hasa wanaoishi vijijini hivyo nimefurahishwa na malengo ya jukwaa hili kwani yanaendana na malengo ya serikali kupitia wizara yetu hii ya afya ya kuhakikisha tunaboresha afya za wananchi wetu kupitia za kisasa na tiba asili” Alisema Dkt. Mhame.

Amefafanua kuwa biashara ya tiba asili duniani inakuwa kwa kasi sana kwani kwa takwimu za shirika la fya duniani WHO zinasema mwaka 2000 mauzo yake yalikuwa dola za kimarekani bilioni 20,mwaka 2012 ilipanda na kufikia dola za kimarekani bilioni 60,Mwaka 2018 ikafikia dola bilioni 80 na sasa inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050 mauzo ya tiba asili yatafikia dola za kimarekani trilioni 3.

“Kwahiyo niwaombe sana ndugu zangu watafiti wa SUA na waganga wa tiba asili nchini kushirikiana ili kusaidia kujipanga vizuri ili Tanzania nayo inufaike kama China na nchi zingine duniani kwenye mauzo ya dawa za tiba asili wakati yakielekea kufikia Trilioni 3” Alisistiza Dkt. Mhame.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi huyo kuzindua jukwaa hilo Naibu Mkamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA upande wa utawala na fedha Prof. Amandus Mhairwa kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda amesema lengo la jukwaa hilo ni kuibua ubunifu nna kutatua changamoto zilizoko kwenye mnyaroro wa thamani wa biashara ya bidhaa za miti mimea dawa Tanzania ili iweze kuwa endelevu na kutoa mchango mkubwa kwenye kipato cha Wananchi na Tanzania kwa ujumla.

“Malengo ya Chuo chetu pia yanahusisha uendelezaji wa maarifa na ujuzi,bunifu,busaraza kitaalamu na uelewa kupitia mafunzo,matokeo ya tafiti,huduma za ugani na ushauri wa kitaalamu na katika uzalishajiu hivyo tunaamini kuwa uratibu wetu wa kuanzisha jukwaa hili uko kwenye mojawapo ya majukumu yetu na malengo ya uanzishwaji wa chuo chetu” Alifafanua Prof. Mhaurwa.

Aliongeza kuwa SUA kupitia watafiti wake kwenye mradi huu wamefanya tafiti nyingi ambazo zimeonesha kuwa kuna changamoto nyingi kwenye mnyororo mzima wa thamani wa biashara ya tiba asili na mimea dawa hasa ubunifu mchache unaoibuliwa kwenye biashara hii,SUA imeona ni vyema kutumia uzoefu wake wa ndani kwa kushirikiana na wadau wengine kuratibu uanzishwaji wa jukwaa hili.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko amewataka waganga hao wa tiba asili kuendelea kushirikiana na ofisi yake katika kupima viambata mbalimbali vinavyopatikana kwenye dawa zao ili kusaidia kuepusha madhara yoyote yanayoweza kutokea kwa wateja wao endapo dawa itakuwa na viambata ambavyo sio salama.

“Kazi ya ofisi yangu sio kuzuaia nyinyi kupata usajili wa dawa zenu bali tunataka kuona kila dawa mnayoitoa kwa wagonjwa iwe na viambata sahihi ili iweze kutibu vizuri na isilete madhara kwa wateja wenu lakini pia upimaji wetu ndio wa mwisho ili muweze kupata usajili wadawa tukiweka sahihi yetu kuwa dawa iko salama hakuna wa kupinga hivyo msiogope tushirikiane” Alisema Dkt. Mafumiko.

Mkemia mkuu huyo wa serikali alisema kuwa malengo ya waganga wa tiba asili na malengo ya ofisi yake ni moja tuu kuhakikisha usalama wa wananchi na watumiaji wa dawa hizo na ofisi yake inavyo vifaa na wataalamu wa kutosha kubaini kila kilicho kwenye dawa hivyo wale wachache wanaofanya udanganyifu waache maana watabainika.

Pia Dkt. Mafumiko ameipongeza SUA na watalaamu wake kwa jitihada kuwa wanazozichukua katika kuwasaidia waganga hao wa tiba asili kuweza kuboresha huduma ya tiba wanayoitoa kwa Jamii ili iweze kuwa bora na yenye viwango vinavyohitajika.

Mkemia mkuu huyo wa Serikali iliahidi kushirkiana na SUA kwenye mpango huo ili uweze kuleta tija inayokusudiwa kwa jamii na taifa kupitia wataalamu wa ofisi yake muda wowote watakapohitajika.

Kwa upande wake Mkuu wa mradi huo wa GRILI Dkt. Faitha Mabiki alisema kuwa toka mradi huo uanze mwaka 2018 umekuwa na mafanikio makubwa kwa wadau wa tiba asili Tanzania nab ado unaendelea kushirikiana nao kuhakikisha biashara ya tiba asili na mimea dawa inachangia uchumi wa wadau hao na taifa.

“ Wakati tunaanza mradi huu mwaka 2018 waganga wengi hapa wa tiba asili walikuwa wanauza dawa zao kwenye mkifuko ya Rambo,magunia na vifungashio vingine visovyo na ubora lakini tunafurahi leo wakati tunazindua jukwaa hili tunaona wote wameweka dawa kwenye vifungashio bora na vye viwango vinavyokubalika kitaalamu.”Alisema Alifafanua Dkt. Mabiki.

Aliongeza “Lengo letu ni kutaka kuona biashara ya mimea dawa na uuzaji wa dawa za asili haufanyiki tuu hapa nchini bali wataalamu hawa wa tiba asili waweze kufungasha vizuri na kuuza hadi nje ya nchi na kupata mapato wao wenyewe lakini pia na taifa kama ambavyo ilivyo kwa nchi nyingine duniani kama China na India”.

Dkt. Mabiki alisema ili hilo lifanikiwe pia lazima kuwe na uendelevu wa upatikanaji wa mimea dawa hiyo ili pale inapohitajika kwa wingi iweze kupatikana na ndio maana mradi unawafundisha namna ya kuanzisha mashamba ya mimea dawa ili waweze kulima na kuipata kwa wingi na kirahisi pale inapohitajika.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger